Saturday, March 27, 2021

 KKKKK

Sunday, November 27, 2016

Rais Fidel Castro hatupo naye tena

Rais wa kwanza wa Kuba aaga dunia.


Havana, Kuba - 26/11/2016. Fidel Castro 90 rais wa kwanza wa Kuba na mwana mapinduzi amaefariki dunia.
Akitangaza kupitia luninga ya nchi hiyo, rais was sasa wa Kuba Raul Castro, alisema kuwa "rais wetu wa kwanza na kiongozi na mwanamapinduzi Komrade Fidel Castro amefariki leo 25/11/2016."
Kufuatia kifo cha rais Castro, Kuba itakuwa katika maombelezo ya siku tisa. Mazishi ya rais huyo wa Kuba yanatarajiwa kuudhuliwa na viongozi mbalimbali wa dunia.
Fidel Castro alikuwa mpinzani wa siasa za kibepari na alikuwa akipenda kusema "Uwanamapinduzi ni ni mapambano mpaka kufa ya wakati uliyo pita na wakati ujao."
"Wanaongea kushindwa kwa ujamaaa, lakini yapo wapi mafanikio ya siasa za kibepari katika bara la Afrika Asia na Latin Amerika?
" Sikubaliani na ubepari, ni mbaya auvutii na unatenganisha unaleta vita vitna na mashindano yasiyo na tija katika jamii."
Marehemu rais mstaafu wa Kuba Fidel Castro alizaliwa mwaka 31/08/1926 mjini Biran Kuba.

Wednesday, November 9, 2016

Donald John Trump ashangaza ulimwengu wa Siasa, Achaguliwa kuwa rais wa Marekani

Donaldo John Trump achaguliwa kuwa rais wa 45 wa Marekani

New York, Marekani - 09/10/2016.  Donald John Trump, amechaguliwa kuwa rais wa 45 Marekani baada ya kupata vit vya kura 289 zidi ya mpinzani wake Hillary Clinton aliyepata viti vya kura 218.

Donald Trump akiongea mbele ya wapenzi na washabiki wake walikuwa katika hotel yake inayo julikana kama The Trump alisema. " Hillary Clinton amenipigia simu na kutupongeza na ninampongeza kwa jitihada zake wakati wa harakati wa uchaguzi huu."

"Ushindi wa leo, ni harakati na hazikuwa kampeni za uchaguzi, hivyo hizi harakati ndio sasa zimeanza kazi."

Vilevile rais mteule Donald Trup, aliwaomba watu wote kuwa wamoja na kwa kusema kuwa wale waliomchagua na wasionipigia kura wote wawe kitu kimoja na kuwa atakuwa rais wa Wamarekani wote.  "Nawaomba wote walio umia kutokana na uchaguzi tuwe wamoja ili kujenga Marekani mpya."

Rais mteule, Donald Trump, alikumbana na vikwazo vya kila namna katika kampeni za kuwania urais wa Marekani, kwa kudaiwa kuwa mbaguzi, msemaji wa vitu na mambo ambayo si yakiutu an pia kudaiwa kuwa alikuwa anadhalilisha wanawake.

Ushindi wa Donald Trup unatafsiliwa kuwa ni jibu kwa wanasiasa kwamba wabadirike kwa kuwa wa watu wamechoka na siasa zisizo eleweka na haadi wazizotimiza.

Friday, October 28, 2016

Tony Blair ateta lake juu ya Brexit



London Uingereza - 28/10/2016. Waziri wa zamaniwa Uingereza Tony Blair, ameongelea wasiwasi wake kuhusu madhara ambayo huenda yakatokea baada ya Uingereza kuanza rasmi mazungumzo ya kujitoa katika jumuiya ya muungano wa nchi za umoja wa Ulaya.

Akiongea na BBC 4 radio, Blair alisema "Ikiwa tutatoka katika jumuiya ya Ulaya, basi madhara yake yatakuwa makubwa kijamii na kiuchumi."
Blair aliyasema hayo kwa kusisitiza kuwa watu 48% ya wakipiga kura walipiga kura ya kubaki ndani ya Umoja wa Ulaya na kwani walijua umuhimu wake.

"Wananchi wanatakiwa wapewe nafasi ya kuliangalia hili suala kwa undani, ikibidi kuwepo na kura ya nyingine kuhusu Uingereza kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya."

Hata hivyo Maria Caulfield, mbunge wa chama tawala cha Conservative na mmoja wa viongozi wanao shughulikia Uingereza kujitoa katika muungano wa umoja wa Ulaya amesema " Blair anatakiwa  kutoa mawazo ya kuijenga Uingereza iliyo amua kuwa nje ya jumuiya ya nchi za Ulaya na siyo vinginevyo"

"Blair anapinga demaokrasi, wanachi walishaamua na matakwa yao lazima sisi kama viongozi tuyatekeleze." Alisisitiza  Caulfield.

Maoni hayo ya Tony Blair yamekuja kufuatatia maswali mengi yanayo ulizwa kuhusu nafasi ya Uingereza baada ya kujitoa rasmi katika muungano wa jumuiya ya nchi za Ulaya na kushuka kwa thamani ya fedha ya Uingereza tangu Waingereza kupiga kura ya kukataa kuwa jumuiya ya Ulaya.

 

Sunday, March 20, 2016

Rais Jakaya Kikwete


Mwandishi wa Habari na Mtangazaji, Rukundo L Kibatala, anakuletea makala fupi ya historia ya Uongozi wa Rais Mstaafu wa Tanzania ndugu Jakaya M Kikwete.

Wednesday, March 9, 2016

Iran yarusha makombora.


Tehran, Iran 09/03/2016. Jeshi la Iran limefanikiwa kurusha makombora mawili  (Ballist missiles)  Urushaji wa makombora hayo yaliyo pewa majina ya Qadr -H na Qadr F ulifanyika kaskazini mwa nchi hiyo katika eneo lijulikanao Alborz Mashariki. Makombora hayo yanauwezo wa kushambulia umbali wa kilomita 1500 hadi 2000.

Kamanda wa kitengo cha usalama wa anga wa Iran, Brigedia, Amirali Hajizadeh amesema kuwa. "Kombora aina ya Qadr H linuwezo wa kushambulia umbali wa kilomita 1700 na jingine Qadr F linaweza haribu na kuchakaza kabisa kitu chochote kilichopo umbali wa kilomita 2000."

Tamko la Iran kuhusu kurusha makombora yake, limekuja baada ya msemaji  wa serikala ya Marekani Mark Toner kukosoa kitendo hicho nakusema " Kufuatia kitendo hicho cha Iran, Marekani italifikisha suala hilo katika balaza la usalama la umoja wa mataifa."

Hata hivyo waziri wa mambo ya nje wa Iran Javad Zarif, amesema kuwa " Iran haitaji ruhusa yoyote katika masuala yake ya kiulinzi wa nchi, na tulisha sema kuwa hatuta ulizia wala  omba ruhusa katika kushughulikia masuala yetu ya kiulinzi."

Iran nchi ambayo ilikuwa imewekewa  vikwazo vya kiuchumi kwa muda mrefu na Marekani na washiriki wake, imekuwa kwa miaka mingi ikijitengenezea mitambo ya kiulinzi ya kijeshi na pia kuhakikishia jumuia ya kimataifa kuwa utengenezaji wa zana za kiulinzi  ni harakati za kujiimarisha katika suala la ulinzi wa nchi.




Wednesday, March 2, 2016

Osama bin Laden alitaka mirathi yake itumike kundeleza mapambano. 


Aliyekuwa kiongozi wa kundi la Al Qaeda, Osama bin Laden, alikuwa ameandika kuwa mirathi yake  ya kifedha zipatazo $29 millioni, kwa kiasi kikubwa zitumike takika kusaidia kuendeleza "Jihad" mapambano,  na kiasi kidogo kigawiwe kwa ndugu wa familia, ijapokuwa mpaka hazijulikani hizo fedha zipo wapi.

Zikiwa zimeandikwa kwa mkono wa Osama bin Laden, habari hizi, zimetolewa na serikali ya Marekani wiki hii, baada ya kuruhusu mafaili yaliyo kamatwa na kikosi maalumu cha kijeshi cha Marekani wakati walipo kuvamia makazi na  maficho  ya Osama bin Laden yaliyo kuwepo kwenye mji wa Abbottabad  Pakistan siku ya 1. Mai 2011 na kufanikiwa kumua.

"Nivyema kwa jamii kufahamu nini kiongozi wa Al Qaeda alipanga"  Alisema Brian Hale Mkurugenzi wa mambo ya jamii kutoka idara ya upelelezi ya taifa ya Marekani huku akiwa anaonyesha makaratasi yaliyo chukuliwa kutoka katika makazi wa Osama bin Laden

Karatasi hiyo ambayo inaonyesha nini kiongozi wa Al Qaeda alitaka kifanyike katika mirathi yake, ni moja ya makatasi 100 ambayo yameruhusiwa kuwekwa hadharani, baada ya kamati ya ulinzi na usalama kuyapitia kwa uangalifu.



Sunday, February 28, 2016

Urusi yazidi kujiimarisha kijeshi.


Urusi yazidi kujiimarisha kijeshi.

Urusi imeonyesha rasmi gari mpya  aina ya Batmobile ambayo itatumika katika mapambano ya kivita na vurugu za aina yoyote. Gari hiyo ambayo hapo awali ilijulikana kama  Punisher, inasemekana ni jibu kwa gari la kijeshi la Kimarekani Humvee.


Akiongea wakati wa kukagua gari hii mpya ya kijeshi, rais wa Urusi, Vladmir Putin alisema "nawashukuru kwa jitihada  na hii inahakikishia kuwa Urusi ipo tiyari kujibu mashambulizi ya aina yoyote pindipo tutakapo shambuliwa."

Kwa mujibu wa shirikala la habari la Urusi RT, gari hii mpya ya Kirusi, inauwezo wa kuchua watu kumi na ndani gari hii ina muundo wa V ambao inatoa kinga kubwa kwa watumiaji wa gari hii pindipo wakishambuliwa au gari kushambuliwa na bomu na vilevile hili gari lina mitambo ya kurushia mizinga.

Uzinduzi wa gari hili, unatarajiwa kuleta vichwa kuuma kwa Marekani na washiriki wake, kwani Urusi tangu iingilie vita vya Syria, nguvu zake za kijeshi zimefanya kuwepo na mabadiriko makubwa ya kivita kati ya serikali ya Syria inayo ungwa mkono na Urusi na wapinzani wa serikali wanao ungwa mkono na nchi za magharibi.

Thursday, February 4, 2016

Shirika la utangazaji la RT la Urusi lawa tishio.

Shirika la utangazaji la RT la Urusi lawa tishio.


Shirika la utafiti wa masuala ya kiusalama la Marekani CEPA, limemlaumu George Galloway mtangazaji na mwanasiasa mkongwe wa Uingereza ya kuwa kipindi chake  Sputnik kinacho tangazwa katika luninga ya Kirusi - RT kuwa kinahatarisha na kuzidharaulisha serikali za nchi za Magaharibi na NATO.

CEPA Center for European Policy Analysis yenye makao ya ke makuu jijini Washington, limesema kutokana na kuwepo na RT  inayo tangaza kiingereza, kipindi cha Sputnik, kimekuwa kikitumika kama sehemu ya kukuza na kundesha  juhudi za Urusi dunia kwa kuponda mipango na mikakati ya Marekani na washirika wake.

Ripoti ya hiyo ambayo ilitolewa January 2016, iliandaliwa ili kufanya utafiti ni kwa jinsi gani amshirika ya habari yanavyo fanya kazi na shirika la utangazaji wa luninga RT likanonekana kuwa linazidi kukua na kuwa tishio kwa mashirika ta utangazaji ya nchi za Ulaya Mgharibi na Marekani.




Tuesday, November 10, 2015

Rais Putin asema njama za Marekani zipo wazi.

Rais Putin asema njama za Marekani zipo wazi.

Moscow, Urusi - 10/11/2015. Rais wa Urusi Vladmir Putin amesema kuwa Marekani na washirika wake wanampango wa kupunguza nguvu za kinyuklia za Urusi kwa kutaka kuweka mitambo ya siraha za kinyuklia barani Ulaya.

Akiongea na katika mkutano wa Sochi, rais Putin alisema " Iran na Korea ya Kaskazini zinatumiwa na Marekani kama kigezo cha kuwekwa mitambo ya kijeshi barani Ulaya. Lakini nia yake ni kujaribu kupunguza dhamira ya Urusi ya kuwekeza nguvu zake za kijeshi.

" Hivyo napenda kuwahakikishia kuwa Urusi haitakubaliana na kitendo hicho, na kwa sasa tunatengeneza siraha ambazo zitaweza kukabiriana na siraha hizo za Kimarekani." Alisisitiza raia Putin.

Mvutano wa kijeshi kati ya Urusi na Marekani, umekuwa wa muda sasa, tangu Marekani ilipo pendekeza kuweka mitambo yake ta Kijeshi barani Ulaya kwa madai kuwa ni kwa ajili ya ulinzi wa NATO jambo ambalo Urusi inalipinga.

Tuesday, June 16, 2015

Urusi kuandaa kuwekeza siraha za kinyukia kiulinzi.

Mkuu namba 2 wa Al-Qaeda auawa.

Sanaa, Yemen - 16/06/2013. Kiongozi wa pili kwa uongozi katika kundi la Al-Qaeda, Nasir Wahishi, ameuawa kufuatia mashambulizi ya kutoka angani yaliyofanywa na ndege za kijeshi za Marekani.

Kuuawa huko kwa Nasir al- Wahishi, kunasadikiwa ni pigo la pili kubwa kwa kundi la Al-Qaeda,  kufuatia pigo la kwanza la kuuawa kwa kiongozi mkuu wa Al-Qaeda Osama bin Laden mwaka 2011.

Kutokana na kuuawa kwa kiongozi huyo namba mbili wa Al-Qaeda, Qassim al Raim, huenda akachukua kiti cha uongozi wa kundi hilo katika maeneo ya Peninsula.


Rais aliyepinduliwa nchini Misri ahukumiwa kifo.


Kairo, Misri - 16/06/2015. Mahakama kuu nchini Misri, imemuhukumu adhabu ya kifo rais aliye pinduliwa Mohamed Mosri.

Mahakama imemkuta na hatia bwana Musri kwa kuhusika katika makosa ya mauaji na makosa mengine ya ukiukwaji wa haki za binadamu. Pia hukumu kama hiyo ilitolewa kwa  wanachama  80 wa chama  cha Undugu wa Kislaam (Muslim Brotherhood), japokuwa hawakuwepo mahakamani.

Rais Mohamed Mosri,alipinduliwa kijeshi kutoka madarakani mnamo mwaka 2013 July, na toka hapo amekuwa chini ya ulinzi, nahuku mlolongo wa kesi zikimfuta, kutokana naaliyoyafanya wakati alipo kuwa madarakani.

Urusi kuandaa kuwekeza siraha za kinyukia kiulinzi.



Moscow, Urusi - 16/06/2015. Rais wa Urusi Vladmir Putin, amesema  Urusi itaweka mitambo yake ya kinyuklia 40, ikiwa ni njia ya  kuujiami kiulinzi.

Akiongea katika  sherehe za kuazimisha maonyesho ya kijeshi, rais Putin alisema "Mizinga 40  yenye uwezo wa kubeba siraha za nyuklia zitakuwa zimekwisha wekezwa ifikapo mwisho wa mwaka wa 2015."

   Matamshi hayo ya rais Putin, yamekuja baada ya Marekani kutamka hivi karibuni, itaongeza ulinzi wa kisiraha katika bara la Ulaya ikiwa nji ya kujihami kutokana na vitisho vinavyo wekwa na Urusi.

Sunday, February 1, 2015

Mmoja wa waandishi wa habari wa Aljazeera aachiwa.

Rais Robert Mugabe mwenyekiti wa AU.


Adis Ababa, Ethiopia - 01/02/2015. Rais Robert Mugabe , amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa jumuiya ya muungano wa nchi za Afrika  AU, baada ya mwenyekiti wa sasa rais wa Mauritania Mohamed Ould Abdel Aziz kumaliza muda wake.

Akiongea mara baada ya kuchaguliwa kwake kuwa mwenyekiti, rais Mugabe alisema " kazi yangu ni kuhakikisha yote yaliyo azimiwa yanatimizwa, hivyo kama nchi za Ulaya na washiriki wake watasema kuhusu kuchaguliwa kwangu, hilo haliniusu."

"Lengo ni kuhakikisha tunatumikia wananchi wa Afrika, na hasa kuinua hali ya wanawake, japo tupo tofauti kimaumbile, wanawake wanaweza fanya kazi fulani na kuna kazi nyingine wanaume hawawezi kufanya kama kubeba motto tumboni, hivyo tunaangalia ni njinsi gani wanawake wasaidiwe katika jamii ili kuchangia ujenzi wa bara hili kiuchumi."

"Zimbawe leo tuna majaji na marubani wanawake, hivyo tunajua umuhimu wa wanawake katika jamii nzima ya kiaafrika."

Rais Robert Mugabe, ndiye rais mkubwa kiumri, na ambaye amekuwa akisifiwa na kupendwa sana katika bara la Afrika kama mginaji halisi wa Wafrika, na hasa kwa kupinga na kufokea hadharani  tabia za baadhi ya nchi zinazo taka kuleta muvurugo na kuiba mali zilizopo katika bara la Afrika kiujanja ujanja.

Mmoja wa waandishi wa habari wa Aljazeera aachiwa.
 
Kairo, Misri - 01/02/2015. Peter Greste, mwandishi wa habari wa shirika la habari la Aljazeera, ameachiwa huru na kusafirishwa kwao nchini Australia, wakati waandishi wenzake Baher Mohamed, na Mohamed Fanny wakiwa bado jela.

Greste Muaustralia na wenzake Baher na Fanny, wamekaa jela siku 400, tangu mahakama jijini Kairo kuwahukumu vifungo, baada ya kushatakiwa kukisaidia kihabari chama kilicho tolewa madarakani cha Muslim Brotherhood  kwa nguvu na rais wake Mohammed Mosri kukamatwa.

Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema kuwa " Greste alipakizwa kwenye ndege ya shirika la ndege la Misri leo hasubuhi, akiwa na kaka yake.

Mostefa Soug, mkuurugenzi mkuu wa  Aljazeera akiongea kuachiwa kwa Peter Grste alisema "tunafurahi kuwachiwa kwa Peter Greste, lakini hata hivyo bado tunasisitiza Baher na Fanny lazima waachiwe huru, na hatuta pumzika mpaka waachiwe."

Kuachiwa huko kwa Greste kumekuja kutokana na msukomo wa kimataifa unao isukuma serikali ya Misri ya kutaka kuachiwa kwa waandishi wa habari wa Aljazeera waliopo ambo mmoja wao Peter Greste kuachiwa  huru na wenzake Beher Mohammed na Mohamed Fanny bado wapo jela.

Wakwepa kodi nchini Ugiriki walikuwa kitisho kwa serikali.

Athens, Ugiriki - 01/02/2015. Mkuu wa umiliki na ukusanyaji wa kodi nchini Ugiriki Nikos Karavitis Theoharis, alilazimika kujiudhuru, baada ya kupokea vitisho kutoka kwa wakwepa kodi.

Akiongea, mara baada ya kuchaguliwa kwa serikali mpya ya Siryiza,  Theoharis alisema " Nilikuwa napokea  simu za vitisho ofisini kwangu na ujumbe kupitia mitandao yakuwa ni Euro 5,000 zitatumika kuvunja miguu yangu."

"Vitisho nilivyo kuwa nikipokea, vinaonyesha ni kwa kiasi gani wakwepa kodi walivyo kuwa wanaibia nchi bila uwoga, na hivyo baada ya kuona nipo imara ndipo walipo nitisha na kwa usalama ikabidi  nijiudhuru."
"
 
"Lakini naamini serikali iliyo ingingia madarakani, itakuwa shubiri kwa wakwepa kodi. kwani vitisho walivyo kuwa wakivitumia havita saidia"

Theohari,s aliyaongea haya baada ya kushinda kuwa kama mbuge, na ambaye anaunga mkono serikali mpya iliyo chaguliwa nchini Ugiriki, inayo pinga mbinyo na makato ya serikali kwa wananchi ili kulipa madeni ya nchi. Hatua ambayo inadhaniwa huenda ikaleta mtafaruku katika jumuiya ya umoja wa Ulaya.




Thursday, January 1, 2015

Mamilioni washerekea kuanza kwa mwaka mpya.

Mamilioni washerekea kuanza kwa mwaka mpya.

 Mungu Baba tunakushukuru, utubariki, utulinde, utuzidishie kwa kila jambo tulifanyalo na utufanye tuzidi kukuomba na kukutegemea wewe Muumba kwa kila jambo. Amina.


 Wapalestina wajiunga na Mahamakama ya Kimataifa.
Ramalhah, Palestina - 01/01/2015. Rais wa Palestina Mahamoud Abbas, ametia siani mkataba wa makubaliano wa kujiunga rasmi kuwa mwanachama wa mahakama ya kimataifa inayo shughulikia  makosa ya jina na ukiukwaji wa haki za binadamu ICC, masaa machache baada ya kamati ya usalama ya umoja wa mataifa kushindwa kupitisha ombi la uhuru wa Wapalestina.

Akiongea baada ya kumaliza kusaini kujiunga na ICC, rais Mahmoud Abbas alisema " wanatushambulia kila siku, angani, majini na kila sehemu, wapi tutapeleka malalamiko yatu? Ikiwa kakati ya usalama ya umoja wa mataifa imetukataa."

Akiunga mkoni kitendo cha rais Abbas kusaini kujiunga na ICC, Hanan Ashrawi, ambaye  ni mwanadiplomasia alisema " tumekuwa watu wapole katika majadiliano tangu 1991, wakati mpango wa kuwa na mataifa mawili ya Kipalestina na la Kizrael kuzikwa, hivyo hiki kitendo cha leo ni muhimu kwa Wapalestina."

Kufuatia kujiunga kwa Wapalestina na ICC, kumetoa uwezo kwa mahakama ya kimataifa kuweza kuchunguza mauaji na ukiukwaji wa haki za binadamu ambayo yamefanyika katika maeneo ya Wapalestina.

Kufuatia kujiunga kwa Wapalestina kwenye koti ya ICC, waziri mkuu wa Izrael, Benjamin Netanyahu amesema " Kitendo cha Abbas, kutawafanya Wapalestina kushitakiwa, kutokana na vitendo vyao vya kigaidi na hasa kwa kuunga mkono kundi la Hamas.
"Sisi kwa upande wa Izrael hatukubaliani na uamuzi wa Wapalestina, na tutalinda haki za Waizrael."

Uamuzi huu wa Wapalestina kujiunga na ICC, kumekuja baada ya kamati ya Usalama ya umoja wa mataifa kushindwa kupitisha muswaada ulioletwa na Wapalestina, baada ya Marekani na Australia kupinga muswaada huo, ambao ulikuwa unadai Izrael kusimamisha kitendo cha kuchukua ardhi ya Wapalestina kwa nguvu na kurudisha wanazo kalia kwa kufuata mipaka ya makubaliano ya mwaka 1967.







Tuesday, December 30, 2014

Marekani yataka nguvu za kijeshi kutumika nchini JD Kongo.
 

Kinshasa, JD ya Kongo - 30/12/2014. Wanajeshi wa umoja wa mataifa waliopo nchini JD Kongo, wametakiwa kutumia nguvu za kijeshi, ikiwa kundi la apiganaji wa DFLR ( Democratic Force for the Liberation of Rwanda) litashidwa kusalimisha siraha walizo nazo itakapofikia January 2.

Russ Feingold, ambaye ni mwakilishi wa Marekani katika ukanda wa Maziwa makuu amesema "
"Ikiwa kutatokea ucheleweshaji wa kukabidhisha siraha, kundi la DFLR ndilo litakalo faidika, huenda wakazitumia siraha hizo katika ukiukaji wa haki za binadamu. 

"Hivyo  jeshi la umonja wa mataifa - MUNUSCO, lipo tayari pindipo hili nilisemalo litatokea ili kukabiliana na kundi hilo, na napenda hili lieleweke kuwa nguvu za kijeshi zitatumika."

 Kundi la DFLR ambalo ni la Wahutu wenye mlengo mkali na wanaopingana na serikali ya Kigali, wamekuwa wakishutumiwa kwa kuhusika na ukiukwaji wa haki za binadamu na inaaminika bado kuna wapiganaji 1400  ambo bado wanashirikiria siraha zao.

 Iran yadai haita buruzwa katika mazungumzo ya kinyulia.
Tehran, Iran - 30/12/2014. Waziri wa mambo ya nje wa Iran, Mohammad Javad Zalif, amesemakuwa Iran itasimama imara katika majadiliano yake kinyuklia  yatakayo anza 15/01/2015.

Akiongea Javad Zalif alisema " bado kuna upana ambao unatakiwa kipunguzwa katika mazungumzo hayo. Hatupo tayari kusukumwa sukumwa.

"Tutakuwa Imara kama mwanzo na la muhimu ni kuhakikisha vikwazo vyote vinaondolewa kama tulivyo sema hapo awali. Nakama hakutakuwa na makubaliano, Iran ipo tayari kwa hali na mali kukabiliana na lolote litakalotokeo."

Mazungumzo hayo ya Iran na mpango wake wa kuendelea na muzalisha nyuklia yanangojewa, kwani matokeo ya katika mkutano huo yanaweza badirisha sura ya dunia katika ulimwengu wa kinyuklia.
 
Mazungumzo ya kinyuklia ya Iran  yanajulikana kamaya nchi 5+1 ambayo yanajumuisha Urusi, Marekani, China, Unigereza na Ufaransa. 

Uingereza kupingwa muswaada wa Wapelestina UN.
New York, Marekani - 30/12.2014. Uingereza imetamka kuwa itapinga muswaada wa Wapalestina  walio uwakilisha umoja wa mataifa, ambao unaitaka Izrael kusimamisha chukuaji wake wa ardhi ya Wapelestina kinguu, na kurudisha maeneo yote wanayo miliki Waizrael.

Mark Lyall, ambaye ni balozi wa Uingereza wa Umoja wa mataifa ameseama kuwa " jibu la Uingereza ni hapana kwa muswaada huo.

"Kwani lugha ambayo imetumika inaleta walakini, hasa kuongezeka kwa lugha ya wakimbizi, na hivyo kunaugumu katika sualazima la hali hiyo."

Matamshi hayo ya Uingereza, yamekuja baada ya hapo awali Marekani kutamka kuwa inapinga muswaada huo wa Wapalestina kwa kuwa haukuelezakuhusu usalama wa Izrael

Muswaada wa Wapalestina umekuwa ukipigiwa chepuo na Jordan, ambapo  inataka kura ya kupitisha muswaada huo ipigwe siku ya Alhamis, jambo ambalo kwa sasa linaelekea kuwa na ugumu. Kwani Uingereza na Marekani zaweza tumia kura zao za vito kupinga muswaada huu.
 


Talibani waikejeli NATO.

Wapalestina wawakilisha muswaada wao uhuru umoja wa Mataifa

New York, Marekani - 29/12/2014. Jumuiya ya nchi za muungano wa Kiarabu, zimekubaliana kwa pamoja muswaada uliyo letwa na serikali ya Wapelestina kwenye umoja wa mataifa, ambao unataka Izrael kusitisha vitendo vyake vya kuchukua ardhi ya Wapalestina kinguvu, na kutoka katika maeneno yoye iliyo yachukua kinguvu ifikapo 2017, jambo ambalo Marekani na Izrael zimepinga.

"Ni suala la kuwaunga mkono Wapalestina ni muhimu, na ndio maana nchi za muungano wa nchi za Kiarabu zimeunga mkono muswaadahuo.
Alisema balozi wa Dina Kawar, ambaye ni balozi wa Jordani wa Umoja wa Mataifa.

"Kutakuwa na mazungumzo na wajumbe wa Palestina, nini kifanyike na lini kura zipigwe, ili kupitisha muswaada huo." aliongezea Kawar

Muswaada huo wa Wapalestina, ulipingwa na Marekani na Izrael, kwa madai kuwa hauelezei kuhusu hali ya Amani ya Izrael.

Hata hivyo wajumbe wa Palestina wamesema kuwa katika muswaada huo, lipo suala la majadiliano ya miji ya West Bank, Mashariki ya Jerusalem na Ukanda wa Gaza, miji ambayo michoro yake ya kiramani ilibadirika baada ya vita vya Mashariki ya Kati vya 1967.

Hatung'oi buti nchini Sudani ya Kusini, asema raia Museven.

Kampala, Uganda - 29/12.2014. Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Mseven, amesema kuwa jeshi la Uganda litaondoka nchini Sudani ya Kusini pindipo Amani ya kudumu itakapo patikana.

Akiongea kuhusu hali ya Amani ya Sudani ya Kusini, rais Museven alimeam, "tatizo si la  Uganda, tatizo ni Amani ya kudumu inayo takiwa nchini Sudani ya Kusini.

Kunatakiwa hali ya utulivu na Amani iwepo, kwani jeshi la Uganda haliwezi ondoka na kuachia mwanya wa vurugu kurudia.

Serikali ya Uganda iliamua kupeleka jeshi lake nchini Sudan ya Kusini, baada ya kutokea mvutano wa madaraka kati ya rais Salva Kiir na makamu wake Riek Machar, jambo ambalo lilileta kuvurugika kwa Amani.

Hata hivyo Riek Machar, amekuwa akidai kuwa jeshi la Uganda linatakiwa kuondoka nchini Sudani ya Kusini,kwa kuhisi kuwa lina unga mkono utawala wa SPLM uliopo chini ya raia Salva Kiir.

Talibani waikejeli NATO.

 
Kabul, Afghanistani - 29/12.2014. Kundi la Taliban la Afghanistan limekejeli  kuondoka kwa NATO ni dalili ya kushindwa kwao, na kwamba kundi hilo ndilo lililo ibuka na ushndi, baada ya kampeni ya kivita iliyochukua miaka 13.

"NATO na washiriki wake wamekunja bendera katika mazingira ya kushindwa, na kukabidhi madaraka ya kiulinzi kwa serikali ya Afghanistan, ni jibu kuwa Taliban wameshinda, kwani mpaka leo sisi bado tupo. Alisema msemaji wa Taliban Zabihulla Mujahid.

"Na Kuanzia sasa Taliban itashika usukani, na wale waliofikiliwa kuachiwa madaraka watashughulikiwa kama tulivyo lishughulikia jeshi la NATO na washirikia wake na sasa wanakimbia." Aliongezea  Mujahid.

Vita zidi ya kundi la Taliban vilianza mwaka 2001, vikiwa na madhumuni ya kuungamiza utawala wa Taliban, na kusababisha vifo wanajeshi karibu 3,500, na pia kuleta hasara kijamii nchini Afghanistan na watu wengi kupoteza maisha yao.

 

Monday, December 22, 2014

Muhammad Ali alazwa hospitalin.


Obama alaani mauaji ya Polisi.



New York, Marekani - 21/12/2014. Rais wa Marekani Barack Obama amelaani mauaji ya polisi wawili katika jiji la New York, ambao walikuwa wakishika doria ndani ya gari lao. 

Kamishna wa polisi wa New York Bill Bratton, amesema "Ismaaiyl Brinsley, mwenye umri wa miaka 28, aliwapiga risasi kichwani polisi hao bila kuwepo onyo lolote. Na kabla ya hapo Brinsley ambaye anaasili ya kiafrika, alimpiga risasi mchumba wake wazami kabla ya kuwauwa  polisi hayo wa mji wa Brookyl."

Mauaji ya polisi hao wawili, yametoke,  wiki chache baada ya  maandamano ya watu wenye hasira, kupinga vitendo vya polisi kuhusika na matukio ya polisi kuwauwa watu weusi ambao hawakuwa na silaha. 

Ismail Brinsley alijiua mwenyewe kwa risasi baada ya kukimbilia kwenye kituo cha treni zinazopita chini ya ardhi. 

Polisi imesema alikuwa ameweka ujumbe kwenye mtandao wa wake kuwa alipanga kuwauwa "nguruwe" wawili kama hatua ya kulipiza kisasi kifo cha Eric Garner, Mmarekani mweusi aliyeuawa kwa kukabwa koo na polisi.

 Rais wa Misri amfuta kazi Mkuu wa ujasusi

Kairo Misri - 21/12/2014. Rais wa Misri Abdel Fattah al-Sisi leo amemfukuza kazi mkuu wa upelelezi  Jenerali Mohamed Farid el- Tohamy aliyeteuliwa siku chache tu baada ya kuondolewa madarakani rais wa zamani Mohamed Mursi mwezi Julai mwaka jana. 

Jenerali Khaled Mahmoud Fuad Fawzy ambaye alikuwa msaidizi wa Farid el Tohany ndiye aliyeteuliwa kuchukua nafasi yake. 

Hata hivyo hakuna sababu zozote zilizo elezwa za kufukuzwa kazi kwa Jenera Farid el 
Tohan.

Wakati huo huo, Misri leo imekifungua  mpaka wa Rafah, ambao utawawezesha  wakazi wa Ukanda wa Gaza, kwa mara ya kwanza katika kipindi cha karibu miwezi miwili kuweza kuingia na  kutoka Misri. 

Misri ilifunga mpaka wa kuingia Gaza, Oktoba 25 baada ya wanamgambo wenye itikadi kali za Kiislamu katika eneo la Sinai kuwauwa wanajeshi wake 33.




Marekani  kuchunguza uvamizi wa mtandao wa Sony.


Marekani ,Washington -21/12/2014 Rais wa Marekani Mabaka Obama, amesema kuwa Marekani inachunguza ili kuweza kujua kama Korea ya Kaskazini inahusika na ushambuliaji wa mtandao wa Sony, na kama ikigundulika ilihusika, basi hatua za kisheria zitachukuliwa.

Obama alisema, "tunalianagalia hili  suala la kushambuliwa kwa Kampuni ya Sony kwa makini, nakuwa kila sheria ya kukabiliana na jambo hili zipo tiyari.

"Kwani hatufanyi maamuzi kwa kupitia vyombo vya habari, bali ukweli utakapo patikana basi sheria zitafuata."

Mazungumzo hayo ya rais Obama yamekuja  baada ya Korea ya Kaskazini kukanusha kuhusika na mashambulizi ya kimtandao kwa kampuni ya Sony, na kuitaka  Marekani  kuonyesha ushirikino ili kulitafutia ukweli suala la uvamiaji wa mtandao wa kampuni ya Sony.  


Muhammad Ali alazwa hospitalini.

 

Kentaki, Marekani - 21/12/2014. Aliyekuwa bingwa  ndondi kwa uzito wa juu duniani Muhammad Ali  mwenye miaka 72, amelazwa katika hospitali ya mji wa Loiseville ili kutibiwa  homa ya mapafu. 

Bob Gunnell, ambaye ni msemaji wa Ali, alisema " Ali anatibiwa na kundi la madaktari wake na yuko anaendelea vyema.

Mohammed Ali, ameshakuwa hospitali kwa siku moja na anatarajiwa kuruhusuhusiwa kutoka hopitalini baada ya Madaktari kulidhika na mwenendo wa afya yake .



 


 


 

Saturday, December 20, 2014

Liberia yasifiwa na Ban Ki-moon zidi vita vya Ebola.


Nchi za Africa zatakiwa kushirikiana na mahakama ya ICC.



Mahakama kimataifa inayo shugulikia makosa ya jina (ICC)  imeanza mkutano wake wa siku tatu, jiji New York,Marekani,  ambapo umeghubikwa na mfukuto wa kwanini mahakama hiyo imekuwa ikiiandama bara la Afrika tangu kuanzishwa kwa mahakama hiyo mwaka 2002.

Akiongea katika ufunguzi huo rais mpya wa Baraza la mataifa wanachama wa ICC, Sidiki Kaba, ambaye ni Waziri wa sheria wa Senegal,Alisema " Naomba kuwepo na ushirikiano barani  Afrika, ili kubadili mawazo potofu yanayo haribu mahakama hiyo ya ICC.

"Nana penda  kusisitiza kwamba malalamiko ya nchi wanachama  yanapaswa kusikilizwa, na kutafutiwa ufumbuzi." Aliongeza Kaba.


Mkutano huo ambao unajumuisha nchi wanachama 122, Pia uliudhuliwa na wajumbe kutoka Palestina ambapo walikubaliwa rasmi kuwa waangalizi katika mkutano.

 Na kwa mujibu wa Mahakamaya ICC  uamuzi huo wa kuruhusu kuwepo kwa Wapalestina ni hatua moja muhimu ambayo inafungua njia kwa Wapalestina  kujiunga kama mwanachama kamili wa mahaka hiyo ya uhalifu ya kimataifa.



Liberia yasifiwa na Ban Ki-moon zidi vita vya Ebola.


Serikali ya Liberia, imepongezwa kwa juhudi zake katika kupambana na ugonjwa wa Ebola, Pongezi hizo zilitolewa na katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban KI-moon, ambaye yupo nchini humo ili kuona ni hatua gani zimefikiwa katika kupambana ugonjwa wa Ebola.


Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Ban Ki-moon kutembelea Liberia, tangu ugonjwa wa Ebola ulipozuka ambao hadi sasa umeshaua watu zaidi ya 7000 katika eneo zima la Afrika ya Magharibi.

Mkuu wa masuala ya kigeni wa Umoja wa Ulaya kuiuzuru Irak. 

Mkuu wa  kitengo kinacho  shughuli masuala ya  kigeni ya Umoja wa Ulaya  Federica Mogherini anatazamiwa kuizuru  Iraq  wiki ijayo  kwaajili ya kufanya  mazungumzo na  viongozi wa serikali na pia kukutana na viongozi wa  serikali ya Kikurdi.

Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema  kuwa Mogherini  atakutana na kufanya mazungumzo na Waziri mkuu Haider Al-Abadi,  na baadaye  siku ya Jumanne atakuwa na mazungumzo na rais wa jimbo la Kurdi, Masoud Barzani katika mji wa Irbil.

Ziara hiyo za Mogherini itakuwa na madhumuni ya kuona ni kwa jinsi gani  Umoja wa Ulaya, utasaidia katika kupambana na kundi na dola la Kiislaam ,  ambapo hadi sasa Umoja wa Ulaya  umeshatoa  euro milioni 20 kusaidia kutatua matatizo ya kiutu ambayo yamesababishwa na kundi hilo wapiganaji wa IS wanaoshikiria maeneo kadhaa nchini  Iraq.


Waziri Frank Walter Steinmeier aonya kuhusu Urusi.


Waziri wa mambo ya nje ya nchi  wa  Ujerumani Frank Walter Steinmeier,ameleezea wasiwasi wake kuhusu msukumo uliyopo wa  vikwazo kutoka kwa nchi wanachama wa nchi za umoja wa Ulaya kuwa  hutahatarisha na kuiyumbisha Urusi, ambapo wimbi lake litaleta mtikiso katika bara la Ulaya.

Walter Steinmeier alisema kuwa, kushuka kwa tahamni ya Lubo, fedha inayo tumika Urusi, hakutakuwa na faida kwa nchi za Ulaya, hivyo ni bora kuwepo na uangalizi katika sheria za kuweka vikwazo kwa Urusi.

Mazungumzo hayo ya Steinmeier, yamekuja baada kikao cha wakuu wanchi za jumuiya ya Ulaya, kuionya Urusi kuwa kama haitabadiri msimamo wake dhidi ya Ukraine, nchi za Umoja wa Ulaya hazita sita kuongeza  vikwazo zidi ya Urusi.