Sunday, February 17, 2008

Hatimaye serikali yaomba msamaha

Dhahabu ya muziki wa pop,waadhimisha miaka 25 ya albumu iliyo vunja rekodi ya mauzo.

New York, Amerika - Kinara na nyota wa muziki wa pop na kuruka majoka, Michael Jackson ameadhimisha miaka 25 ya muziki uliotikisa dunia ujulikanao kama Thriller's.
Mwanamuziki huyu,ambaye albamu yake ya Thriller's ilimwingizia faranga(pesa) nyingi na kuvunja rekodi ya mauzo.
Akiongea na kuwashukuru wapenzi wake, kwakutumia mtandao, Michael Jackson, alisema ya kua ni vigumu kuamini ya kuwa tangu siku ile yeye pamoja na msanii na mtunzi bwana Quincy Jones walikaa na kutua albamu ijulikanayo kama Thriller's, na hivi sasa inatimiza miaka 25.
Albamu ya Thriller's, ilitolewa November 1982.
Michael Jackson, amehaidi ya kuwa wapenzi wasife moyo kwani hivi karibuni atatoa muziki, kwa kushirikiana na Kanye West, Akon. Fergie .
Pichani hapo juu anaonekana, Michael Jackson,akiwa amepozi mbele ya jalada la albamu ya Thriller's.
Picha ya pili zinaonekana picha za Michael Jackson, ya kwanza kushoto ni enzi zake baada ya kutoa albamu ya Thrillr's na picha ya upande wa kulia anaonekana Michael Jackson wa sasa.
Picha ya mwisho anaonekana mfalme wa muziki wa pop akiwatumbwiza washabiki wake, miaka ya hivi karibuni.
Baba wa taifa la Kuba, atangaza kujiuzulu uongozi"Ameongoza nchi nusu karne"
Havana, Kuba - Rais wa Kuba bwana Fidel Castro, ametangaza rasmi kuwa hatagombania tena urais wa Kuba, kutokana na afya yake.
Rais Castro ambaye ametawala Kuba kwa muda wa nusu karne, amesema yakuwa hataweza tena kuwa kiongozi wa Kuba kwa kuzingatia umri wake na afya yake kwa ujumla.
Rais Fidel Castro, ambaye amefanyiwa upasuaji wa tumbo, amekuwa hajishuhurishi na kazi za kiserikali tangu afanyiwe upasuaji huu, na alimwachia kiti mdogo wake bwana Raul Castro.
Rais Fidel Castro, ambaye amekoswa ku uwawa mara nyingi, na majasusi wa kila aina zaidi ya mara miasita, kutokana na maelezo ya habari za usalama wa taifa wa Kuba.
Picha hapo juu, wanaoneka Fidel Castro na Che Guevara wakati wa harakati wa kuikomboa Kuba kutoka kwenye utawala wa kizalimu na rushwa wa rais Batista.
Viongozi wa Kuba, ambao wametawala zaidi ya nusu karne, ambao ni ndugu,rais Fidel Castro na mdogo wake Raul Castro.
Hapo anaonekana rais Fidel Castro akihurubia mamia ya wa Kuba enzi hizo kabla ya kufanyiwa upasuaji.
Picha ya mwisho anaonekana rais Fidel Castro, akishangilia kwa kutumia bendera ya Kuba.
Matunda ya uongozi bora, yaaanza kuonekana,Tanzania yapata kitita kutoka kwa US.
Dar es Salam, Tanzania - Serikali ya Amerika imeipatia serikali ya Tanzania kiasi cha 700 million dola, baada ya kumaliza kutiliana mkataba.
Pesa hizo ambazo zitapatikana katika kipindi cha miaka mitano ni moja ya jitihada za serikali ya Amerika, kusaidia bara la Afrika kupambana na umasikini, magonjwa na kuinua uchumi.
Pesa hizi zimetolewa kwa serikali ya Tanzania, wakati rais George Bush alipo tembelea Tanzania hivi karibuni wakati wa kutembelea baadhi ya mataifa ya Afrika.
Pichani hapo juu wanaonekana rais George Bush akipena mkono na rais wa Tanzania, bwana Jakaya Kikwete baada ya kumaliza kutiliana mkataba kati ya serikali hizi mbili.
Picha chini wanaonekana wakina mama, wakicheza ngoma huku wakiwa wamevalia kanga zenye picha ya rais George Bush.
Ndoto ya kumtumbwiza mwanahaki za binadamu ni za kila mtu.
Pretoria, Afrika ya Kusini - Kundi la musiki lijulikanalo kama Spice Girls, wamesema wangependelea kumtubwiza shujaa na mpigania haki za binadamu, mwanamapinduzi, na kiongozi aliyeongoza kupinga ubaguzi wa rangi nchini Afrika ya Kusini, rais wa zamani wa Afrika ya Kusini bwana Nelson Mandela.
Pendekezo hilo lilitolewa na wanamuziki hawa yakuwa itakuwa kama ndoto kwao ya kuwa kutwimbiza siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa bwana Nelson Mandela, atakapo adhimisha miaka 90 ya kuzaliwa siku ya tarehe, 27/ june, mjini London kwenye uwanja wa Hyde Park.
Picha hapo juu anaonekana babu, Mandela akiwa amekula pozi baada ya kazi ngumu wakati wa urais wake.
Chini ni picha ya kundi Spice Girls ambao wanaota usiku na mchana kumtumbwiza baba, babu Nelson Mandela.
Tunaomba msamahaa, hatimayake serikali ya Australia yakubali ya kuwa ilifanya mabaya kwa wazawa.
Sidney,Australia - Serikali ya Australia imeomba msamahaa kwa mara ya kwanza kwa Wakazi wa Asili wa Bara la Australia.
Wakazi hao ambao wanajulikana kama Aboligini, waliobwa msamaha huu na waziri mkuu mpya wa Australia bwana Kevi Rudd.
Waziri mkuu,bwana Kevin Rudd, kwa kuonyesha masikitiko na hudhuni,kwa kitendo hicho, alisema tunaomba msamahaa na tunakili ya kuwa tulikosa.
Waaboligini hawa, waliombwa msamaha huu, baada ya serikali ya Australia kukubali na kuelewa baadhi maafa ambayo waliyaleta tangu wazungu wa kwanza walipo ingia katika bara hili la Australia.
Moja ya maafa yale yaliyo sababishwa na Australia, ni wakati serikali ya Australia, ilipo wateka nyara na kuwachukua kwa nguvu baadhi ya watoto wa jamii ya Akiabolijini na kuwa ingiza katika jamii ya Wazungu.
Kwa kitendo hicho cha serikali ya Australia, kutambua na kukubali maafa ambayo waliyatenda, kimepokelwa kwa furaha na wananchi wa jamii ya Aboligini kwa hisia tofauti.
Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Australia, bwana Kevin Rudd, alipo kuwa bungeni hivi karibuni kuomba msamahaa kwa wana nchi wa jamii ya Aboligini.
Picha ya kati anaonekana mmoja ya wananchi wa jamii ya abolijini, akitambika kukubali msamahaa kuktoka kwa serikali.
Chini ni picha ya baadhi ya wananchi wa jamii ya Aboligini, wakiwa wamefungwa minyororo kwenye shingo tayari kuelekea sehemu ambayo hawaijui kutumikia kifungo.
Urusi ya toa onyo"Siraha za kulinda Urusi zitaelekezwa nchi Ukraini.
Moscow, Urusi -Rais wa Vladamil Putin wa Urusi, amesemaya kuwa upo uwezekano wa nchi yake kuelekeza mitambo na siraha za nyuklia nchini Ukraini,ikiwa Ukraini itajiunga NATO, (Jumuia ya ushirikiano wa kiulinzi ,kijeshi na usalama wa Ulaya ya Mgharibi na Amerika).
Akiongea haya baada ya kumaliza kuongea na kutiliana mkataba wa kujenga mitambo ya mafuta na gas hivi karibuni, na rais wa Ukraini bwana, Yushchenko.
Akiongezea alisisitizia ya kuwa Urusi, Ukraini, Amerika na Ulaya Magharibi zinawajibika kwa ujumla kuangalia usalama na ulinzi.
Putin amabye anamaliza muda wake wa kumaliza wa kuwa rais wa Urusi mwezi wa Mei,amezilaumu NATO na Amerika kuwa zinaleta utata wa usalama na amani kwa upande wa Urusi.
Wakati huu rais Vladamil Putin, amealikwa kwenye mkutano wa jumuia ya NATO, utakao fanyika mwezi wa nne .Kwa mara ya mwisho rais Putin, aliuzuria mkutano huu mwaka 2002. Pichani anaonekana rais wa Ukraini bwana, Viktor Yushchenko na rais Putini walipo kutana hivi karibuni.

Monday, February 11, 2008

Rais avamiwa Ikulu, waasi wa Mashariki wa Timor wataka kuleta machafuko.

Kosa la kaptain wetu, humtokea kila mchezaji, kwani mpira unazunguka"Wachezaji wa Kamerooni"

Younde, Kameroon - Wachezaji watimu ya taifa ya Kameroon, wamesema yakuwa kushindwa kwao kubeba kombe la maifa ya Afrika nchini Ghana, sikwasababu ya kosa la kaptain wao Rigobert Song,bali haikuwa siku yao ya kushinda kombe hilo.
Wakiongea kwa wakati tofauti, wachezaji wa timu ya taifa ya Kameroon, walisema kosa ambalo amefanya Song , humtokea mchezaji yoyote, na kwa wale wanao jua au wamesha wahi kucheza mpira wanajua yakuwa mpira huwa wakati mwingine unafanya mchezaji asifanye alivyo tarajiwa na mpira unazunguka, hivyo ulimzunguka kaptaini wao mara moja na hapo mchezaji wa Misri timu ya taifa ya Misri Zidan, akaupata mpira na kumpasia Boutrika aliyefunga goli lililo wapa ushindi Wamisri.
Hivyo sisi wachezaji wote tupo pamoja nae, bado tutazidi kuichezea Kamerooon mpaka hapo miguu ikikataa, aliongea haya Geremi Ndjitap, huku akipewa sapoti na Samuel Eto'o.Kwani tuna kombe la Afrika nchini Angola ,na badye kombe la dunia nchini Afrika ya Kusini, hivyo kwa sasa tutaanza panga mikakati ya kuweza kucheza vizuri ili tuweze kushindana kwenye mashindano haya ya 2010 nchini Angola na Afrika ya kusini.
Picha hapo juu anaonekana kaptain wa timu ya taifa ya Kamerooni Rigobert Song, akiwa ndani ya jezi ya timu yake ya taifa ya Kameroon, na huku mguu wake wa kushoto ukiwa umefungwa bandaji,hivyo maumivu ya mwili wake yapo ndani ya mapenzi ya nchi yake.
Picha ya pili anaonekana Rigobert Song, akiwa kazini kutetea nchi yake siku ya mwisho ya mishindano ya kombe la Afrika,wakati Kamerooni ilipo cheza na Misri na kufungwa goli moja kwa nungu.
Picha ya chini ni picha ambayo wapenzi wasoka wa Kamerooni hawataisahau, kwani anaonekana kaptain wa timu ya taifa ya Kamerooni Rigobert Song,akigombea mpira na Mohammed Zidan, baada ya mpira kumzunguka Song, na hatimayake Zidan, aliupata mpira na kutoa pasi mwanana kwa Boutrika aliye wanyima ushindi wa kombe la Afrika Wakamerooni kwa kufunga bao la pekee.
Eddy Murphy King of Zamunda, aowa nakuacha kwa kipindi kifupi.
Los Angeles, USA - Mcheza sinema na mwana vitimbwi, Eddy Murphy, ameachana na mkewe ,bi Tracey Edmond, baada ya kufunga ndoa kwa kipindi cha wiki mbili.
Eddy Murphy mwenye umri wa miaka 46 na bi Tracey Edmond mwenye miaka 40, walifunga ndoa kwenye kisiwa cha Bora Bora.
Eddy Murphy mwenye watoto sita, kutoka kwa ndoa ya zamani, amecheza sinema nyingi, na moja ya sinema ambazo zimempa umaharufu ni ile ijulikanayo Coming to America.
Picha juu anaonekana bwana Eddy Murphy akiwa kazini kataika harakati za kucheza sinema, amabzo huwa kivutio kwa wapenzi wa sinema.
Picha ya pili anaonekana bwana Eddy Murphy, akiwa amekula kodo,mbela ya wapenzi wake baaday ya kumaliza kufanya mavitu yakeya sinema.
Picha ya mwisho anaonekana Eddy Murphy, akiwa na aliyekuwa mkewe, bi Tracey Edmond siku zakaribuni kabla ya kufunga ndoa yao iliyodumu wiki mbili tu.
Misri yawa bingwa wa kombe la Afrika,Kamerooni yakosa kombe kwa kosa la beki.
Accra, Ghana - Timu ya taifa ya Misri imeibuka na ubingwa kwa mara ya sita, baada ya kuzaba bao moja kwa nunge timu ya taifa ya Kamerooni.
Bao hilo la ushindi lilifunngwa na mshambuliaji hatari Mohammed Aboutrika, baada ya kupata pasi kutoka kwa Zidan, ambaye aliweza kufaidika kutokana na makosa ya beki mzoefu wa Kamerooni rigobert Song.
Ushindi huu wa the FARAOS, unakuja kwa kujumisha wachezaji wanao cheza ligi ya Misri,na wachezaji wawili wanao cheza nje ya ligi ya Misri ndiyo walioitwa kujiunga na timu hiyo ya taifa.Hii ni mara ya pili kwa the Farao, kuwafunga Simba wa Kamerooni, kwani katika mzunguko wa kwanza wakati wakigombania kuingia awamu ya pili Misri iliifunga Kamerooni goli 4-2.
Pichani anaonekana timu kamptain wa Misri, Ahamed Hassan akinyanyua kombe la ubingwa la mataifa ya Afrika. Misri imeshinda kome hili kwa mara ya sita.
Picha ya chini anaonekana Mohammed Zidan, akishangilia huku amebebwa na mchezaji mwenzake baaday ya kumzidi maarifa beki wa Kamerooni, Rigobert Song na kumpasia Mohammed Aboutrika, ambaye bila makosa alifanya vitu vyake kwa kuona nyavu za mlinda mlango wa Kamerooni Idriss Kameni, nakuwa bao la ushindi.
Chini ni picha ya wachezaji wa Misri wakishangilia baada ya kukabidhiwa Kombe lao.
Mgombea mwenza wa ZANU-PF afutwa uanachama"Huyu ni kibaraka ZANU -PF ya dai"
Harare, Zimbabwe - Chama tawala cha ZANU - PF, kimemfukuza uanachama bwana, Simba Makoni, baada ya kuamua kugombania kiti cha urais kama mgombea wa kujitegemea.
Bwana Makoni. alitangaza hivi karibuni ya kuwa atagombania kiti cha urais wakati wa uchaguzi wa rais mapema mwishoni mwa mwezi wa tatu, na bwana Makoni alishwa wahi kuwa waziri wa faranga wa Zimbabwe, lakini alitolewa kwenye wizara hiyo .
Akiongea na waandishi wa habari,makamu wa chama tawala ZANU-PF, bwana, Joseph Chinotimba, aliseama ya kuwa bwana Makoni,amekuwa kibaraka wa serikali za magharibi, Amerika na Uingereza, nakuwa hataweza kuigawa ZANU-PF,hivyo atashindwa na kuumbuka, baada ya uchaguzi, hivyo nasikitika sana, kwani alikuwa mmoja wa wapiganaji wenzetu wakati wa kumpiga mkoloni, lakini sasa kawa kibaraka wao.
Pichani anaonekana bwana Simba Makoni,enzi zake akiwa kama waziri wa faranga wa Zimbabwe akielekea bungeni kutoa miswada.
Hapo chini ni picha ya bwana Simba Makoni,akiongea na waandishi wa habari baada ya kutangaza kugombea urais kama mgombea wa kujitegemea.
Mahaka ya Hague yapata mshitakiwa mwingine,ashutumiwa na mauaji ya Ituri.
Hague, Holland - Aliyekuwa kiongozi wa jeshi la waasi lijulikanalo kama(DRC)Democratic Republican of Congo bwana Mathieu Ngdjolo amekamatwa na mjini Kinshasa na kuletwa nchini Holland, kujibu mashitaka ya mauaji ya mamia ya watu.Alisema wakili mmoja wa mahakama ya mjini Hague, ICC (International Criminal Court), bwana Luis Moreno Ocampo.
Bwana, Mathieu Ngdjolo anashitakiwa kwa kutoa amri ya kutekateza zaidi ya wana vijiji wapatao 200 mwaka 2003 wakatia aliipo kuwa mkuu wa usalama wa taifa.
Tuhuma hizo ambazo zinamkabili ni mauaji yaliyo tokea maeneo ya Ituri na kijiji cha Bogoro.
Kutokana na watetezi wa haki zabinadamu na kuhudumia watu waliopata matatizo, wanadai zaidi ya watu wapatao 600,000 wamakimbia makazi yao tangu machafuko ya Ituri yaanze mapema kwenye mwaka ya 1999. Pichani kulia ni picha ya bwana Mathieu Ngdjolo,alipo kuwa kazini enzi zake kama afisa usalama wa taifa, miaka ya 2003.
Waasi wadai wageni wasaidia serikali, wasiwasi waongezeka "roho zipo nyengema"
Ndjamena, Chad - Wakimbizi amabo walikimbilia nchni Kameroni, wakati wa majaribu ya kiipindua serikali ya rais Idriss Deby, wamaeanza kurudishwa nyumbani kwao.
Hii ionakuja baada ya wapinzani wa serikali kushindwa kumuondoa madarakani rais Idriss Deby.
Kutokana wa msemaji mmoja wa kuhudunia watu waliokumbwa na maafa, alisema yakuwa, hali bado ya mashaka mjini Ndjamena, ijapokuwa watu wamekuwa wakiambiwa ya kuwa waasi hawatarudi tena kushambulia jiji la Ndjamena.
Japokuwa kunahabari ya kuwa waasi hawa wanajijenga tayari kwa mashambulizi mengine, na wamedai yakuwa wanashikiria miji ya n Momgo na Bitkine iliyopo katikati ya nchi ya Chad.
Hata hivyo waasi wa serikali wamezidi ilaumu serikali ya Ufaransa kwa kuisidia serikali ya rais Idriss Deby.
Pichani wanaonekana wanajeshi wa serikali wakila doria mjini Ndjamena, baada ya kuyarudisha majeshi ya waasi nyuma ya jiji na vitongoji vyake.
Chini wanaonekana wanajeshi wa Ufaransa wakiwa wanalinda maeneo muhimu ya kusaidi huduma za binadamu jijini Ndjamena.
Chni nim picha ya kina mama wakiwa wamekaa bila kujua ni nini kinafuata kataiaka kambi moja ya wakimbizi.
Mtuhumiwa wa septemba 11/2001, afunguliwa mashitaka, akabiliwa na kinyongo.
Washington,USA - Serikali ya Amerika imetangaza na kumfungulia mashitaka, aliye kuwa kiongozi wa ugaidi wa sempemba 11/2001 bwana Khalid Sheikh Mohammed.
Akiongea haya Brigedia,General Thomas Hartmann, alisema ya kuwa bwana, Khalid Sheikh Mohammed, anatuhumiwa kwa kuhusika kutumia ujuzi wa hali juu, kwa kusaidiana wa magaidi wengine wa Alqaeda walitumia ndege kashambulia ,kulipua na kuharibu majengo yajulikanayo kama World Trade Centle mjini New York na majengo mengini njini Washington, ambapo zidi ya
watu wapatao 3000 walipoteza maisha yao.
Hata hivyo inasadikiwa bwana Khalid Sheikh Mohammed, alikiri makosa baada ya kuteswa kwa kutumia mbinu ijulikanayo kama " Water Boarding" ambayo watetezi wa haki za binadamu wanasema ni kinyume na sheria za haki za binadamu na sheria za nchi.
Inaamini ka ikiwa bwana Khalid Sheikh Mohammed akikutwa na hatia, anaweza kuhukumiwa kifo Hapo juu ni njia tofauti au mojawapo ambayo watetezi wa haki za binadamu wanadai yakuwa ni kunyume cha haki zabinadamu kutumia njia hii kupata ushahidi au ukweli kutoka kwa mtuhumiwa. Picha ya chini ni picha ya Khalid Sheikh Mohammed, ambaye anashutumiwa kwa kuhusika na uigaidi na mauaji ya semptemba 2001
Rais avamiwa Ikulu ,Waasi wa Mashariki wa Timor wataka kuleta machafuko.
Dili, Mashariki ya Timor - Rais wa Mashariki ya Tomor, bwana Jose Ramos Horta, amenusurika kuuwawa na risasi, baada ya waasi wa Mashariki ya Tomor kuvamia nyumbani kwakwe siku ya jumatatu 11/02/08 na kumpiga risasi za tumbo.
Mapambano hayo yaliongozwa na mmoja wa wanajeshi waasi wa Mashariki ya Timor, bwana Afredo Reinado ambaye waliuwawa wakati wa kutupiana risasi na walinzi wa rais.
Rais Jose Ramos Horta, alikimbizwa hospitali ya jeshi iliyopo mjini Dili, nabaadaye kupelekwa Australia kwa matibabu zaidi.
Picha juu ni kiongozi wa waasi wa Mashariki ya Timor, bwana Afredo Reinado, ambaye aliyeongoza kujaribu kuleta mapinduzi ya kijeshi.
Picha ya pili anaonekana rais Jose Horta, akiwa katika hali mbaya kukimbiziwa hospitali kwa matibabu.
Hapo juu ni picha ya rais Jose Ramos Horta, akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.

Sunday, February 3, 2008

Rais wa Tanzania achaguliwa kuwa mwenyekiti wa AU - Afrikani Union.

Mashindano ya Magari ya Paris Dakar yasimamishwa'Manazi wa kigaidi wawakikwazo"

Paris, Ufaransa - Shirikisho la mbio za magari ya Paris kueleka Dakar Senegel, yamesimamishwa baadaya kutokea tishio la kutekwa na kutokuwa na huakika wa usalama wa washiriki wa mbio hizo.
Uamuzi huo umetolewa na serikali ya Ufaransa, baada ya watu wenye urai wa Ufaransa kuuwawa na watu wanaodaiwa kuwa wanazi wa ugadi na utekaji nyara, katika nchi ya Mauritania. Kwenye nchi ya Mauritania,mbio hizi huwa na vituo visivyo pungua vinane kati ya kumi natano.
Hata hivyo msemaji mmoja wa serikali amesema ya kuwa, hali ya usalama kwa washirki wa mbio hizo ilikuwa katika hali nzuri,na hivyo uamuzi wa kusimamisha mashindano hayo ni pigo kwa wana nchi wa Mauritania kiutalii na kibiashara kwa kuzingatia raia wengi huza vitu vyao kwa wingi wakatio wa mbio hizo.
Picha hapo juu ni picha za pikipiki gari ndogo na roli ambazo hushiriki kwenye mashindano haya, na kwa kiasi kikubwa hupitaia maeneo ya jangani.
Chad yawa kidonda kingine cha vita kwa nchi za Afrika.
Ndjamena, Chad - Wapiganaji wa jeshi la upinzani nchini Chad, wamesimamisha mapambano kwa muda ili kuwapa wananchi kutoka ndani ya jiji la ndjamena, kabla ya kuanza kushambulia jiji hilo upya.
Hatua hii imekuja baadaya mapambano makubwana na makali ambayo wapinzani waliweza kuingia hadi ikiru.
Wapinzani hawa wanapingana na rais wa Idriss Deby ambaye alichuwa madaraka ya urais 1990 .
Kufuatia tukio hilo, serikali ya Ufaransa inasaidia kuwapeleka nje ya nchi raia wote amabo si wa Chad wapatao 600.
Picha hapo juu ni gari iliyo lipuliwa kwa bomu jiji Ndjamena wakati wamapambano, kati ya majeshi ya serikali na wapinzani.
Chini ni picha ya raia wasio wa Chad wakikimbia mapambano, kwa kusaidiwa na wanajeshi wa Ufaransa.
Tetemeko la ardhi la sababisha maafa makubwa nchini zilizo zungukwa na maziwa makuu.
Kigali, Rwanda - Tetemeko kubwa la ardhi limelikumba maeneo ya maziwa makuu.
Maafafa ya tetemeko hilo yameleta mstuko mkubwa kwa wananchi wa Kongo DRC na Rwanda .
Tetemeko hilo, ambalo kimetokea nchini Rwanda na kuua zaidi ya watu wapatao 33 na mamia kujeruhiwa limekuja baada ya kusababisha maafa makubwa nchini Kongo DRC, ambapo tetemeko lilitokea mapema kabla ya tetemoko lililo tokea nchni Rwanda, hata hivyo msemaji wa serikali ya Rwanda Mary Gahonzire, amesema ya kuwa serikali inatoa kilamsaada ili kuwaokoa wananchi kutoka maeneo yaliyo kumbwa na maafa ya tetemeko hilo.
Tete meko hilo lilitokea muda wa saa saaba mchana na wakati nchini Kongo DRC, tetemeko lilitokea saa nne hasubuhi.
Pichani hapo juu ni maafa yaliyo sababishwa na tetemeko la ardhi nchini Kongo DRC.
Picha nyingine inaonyesha ramani ya maeneo yaliyo kumbwa na tetemeko la ardhi hivi karibuni.
Rais wa Tanzania, achaguliwa kuwa mwenyekiti wa AU- African Union.
Addis Ababa, Etheopia- Umoja wa Afrika (AU- Afrikani Union) umemchagua rais wa Tanzania bwana Jakaya M Kikwete kuwa mwenyekiti wa uongozi huo kuchukua nafasi iliyo achwa wazi na rais wa Ghana bwana John Kufuor.
Katika kikao chake cha 53, AU imekuwa na migongano ya kichwa jinsi gani wanaweza kutatua migogo ya kivita na kisiasa ambayo inazikumba nchi za Afrika tangu vugu vugu la mageuzi ya kisiasa kuingia Afrika.
Pichani anaonekana rais Jakaya Kikwete, akisoma baadhi ya mambo muhimu wakati alipo hudhulia mkutanao wa kujenga dunia kiuchumi nchini Uswisi hivi karibuni.
Picha ya chini aanaonekana rais Kikwete, akiongea na wakatia wa mkutano wa kujenga dunia kiuchumi, nchini Uswisi
Mbwa asaidia kukamata faranga zilizo potea bila kujulikana.
Soweto, Afrika ya Kusini - Watu wapatao wanne wamekamatwa na polisi nchini Afrika ya Kusini, kwa kosa la kukutwa na pesa zipatazo R2,8 milion.
Ukamatwaji wa pesa hizo ulifanya na mbwa wa pilisi,ambaye amefunzwa kunusa pesa.
Polisi walianza uchunguzi wao baada ya gari la kubebe pesa kupotea katika mazingira ya utata, na hadi walipo pata pesa hizo ndani ya mmoja wa wakazi wa mji wa Soweto.
Watu hao waliokamatwa na kushukiwa na wizi huu watafikishwa mahakamani hivi karibuni.
Picha hapo juu ni picha ya polisi akiwa na mbwa, ambao husaidia kufuatilia makosa na kukumata wahalifu.
Hapo chini ni picha ya mbwa wa polisi akiwa mfunzoni.
Wizi wachangia mgongano wa kisiasa, mapambo ya kumwenzi kiongozi wa UNITA ya ibiwa.
Luanda, Angola - Kaburi la marehemu kiongozi wa zamani wa UNITA Jonas Savimbi limebomolewa na kuibiwa wa baadhi ya mapambo ambayo yalikuwa yamepambwa ili kumuenzi.
Jonas Savimbi, ambaye alikuwa kiongozi aliye kuwa akiongoza UNITA, kupamabana na serikali ya Angola chini ya chama MPLA kwa kipindi kisicho pungua robo karne..
Hata hivyo viongozi wa NITA wamekuwa wakidai ya kuwa wizi huu umefanya na wanachama wa MPLA.
Pichani hapo juu ni picha ya Jonas Savimbi enzi hizo za uhahi wake, huku akiwa ndani ya magwanda ya kiafande.
Jitiada za Kofi Annan, bado kuzaa matunda, watu wazidi poteza maisha yao nchini Kenya.
Nairobi, Kenya - Mazungumzo kati ya viongozi wa Kenya Bwana Mwai Kibaki na Laila Odinga, bado yapo mashakani.
Vijana wakiwa mitaani na mapanga na malungu na vyombo vya dola vikiwa na siraha kali kama bunduki na mabomu ya kutoa machozi, ndiyo hali ambayo wanchi wa Kenya kwa sasa wanavyo ishi katika maisha yao ya kila siku.
Kiongozi mmoja wa vijana wanao andamana aliseamaya kuwa wacha waongee na Kofi Annan, lakini "sisi bado tuna tete haki zetu "
Kufuatia wachunguzi wa mambo ya kisiasa nchini Kenya, wanasema ya kuwa hali yakufikia makubaliano bado ipo tata, hii inakuja baada ya baadhi ya makubaliano kuwa ya kusimamisha malumbano ya kisiasa amabyo yanasababisha umwagaji wa damu.
Akiongea mmoja wa wazee wa jadi mjini Nivasha alisema, hadi viongozi hawa bwana Laila na Kibaki, watakapo jua ya kuwa hali hii itakuwa ni moja ya historia ambayo itakuwa inawafuata kila wananapo kwenda, hivyo ni vizuri wakae wakubaliane, ili kuleta amani nchini mwetu (Kenya) Hadi sasa maisha ya wananchi walio wengi nchini Kenya wanapoteza maisha kwa kilile wasicho kijua,bali wanakumbwa na mauaji ya kikabila au chuki za umaskini zilizo kuwa zikiwaleme, na sasa wanaona ni njia pekee ya kutoa hasira zao ni kulipa kwa kupitia njia ya kufanya ualifu au mauaji, alimalizia mzee huyu wa jadi ambaye anaisha mjini Naivasha.
Pichani hapo juu ni picha ya wananchi wa Kenya wakiama maeneo ambayo hawatakiwi kuishi kutokana na kutokuwa kabila la wakazi.
Picha nyingine anaonekana mtoto akiwa amekaa kenya taruma la reli, hajui la kufanya baada ya wazazi wake,kupoteana na mtoto wa kati wa machafuko ya kikabila nchini Kenya