Wednesday, July 16, 2008

Hezbollah na Israel zatimiziana ahadi" Wabadilishana wafungwa na miili ya wapiganaji wao".

Brad na Angelina wawa baba na mama mapacha au (mapasa) "Picha za watoto kughalimu mamillioni".

Nice, Ufaransa - Mcheza sinema , balozi wa umoja wa mataifa kwa upande wa UNICEF na nyota maarufu duniani bi Angelina Jolie amejifungua watoto mapasa(Mapacha) wakiki na wakiume katika Hospitali ya French Riviera.
Watoto hao mapacha ambao walipishana dakika moja walizaliwa siku ya jumamosi 12/07/2008, jioni walikuwa na paundi 5 kila mmoja.
Watoto hao walioitwa Knox Leon na Vivienne Maecheline
Inatarajiwa picha zao za kwanza huenda zikauzwa kwa bei ya juu zaidi kufika kiasi cha $ 20 million,alisema mmoja wa mpiga picha bwana, Darryn Lyons, anayemiliki gazeti la Big Pictures la London.
Akiongea hay mganga aliyesaidia kuzaliwa kwa watoto hawa mapacha,alisema Brad Pitt alikuwa pembeni wakati Angelina anajifungua.
Pichani wanaonekana Brad na Angelina wakati walipo kuwa katika moja ya sherehe, kwa sasa wanitwa baba na mama MAPASA.
Picha ya pili wanaonekana Brad na Angelina, walipo udhulia pamoja katika maonyesho ya manyota wa dunia kabla ya Angela kujifungua.
Picha ya tatu, anaonekana Angelina akiwa amesimama wakati alipo kuwa mja mzito wa watotomapasa.
Hezbollah na Israel zatimiziana ahadi"Wabadilishana wafungwa na miili ya wapiganaji wao".
Beiruti,Labanoni - Wafungwa watano ambao walikuwa wanashikiliwa na serikali ya Israel kama wauwaji na magaidi leo 16/07/2008, wameachiwa huru na kurudishwa nchini Lebanon na miili ya wanajeshi wa jeshi la Israel kurudishwa nchini Israel, ikiwa ni moja ya makubaliano kati ya serikali ya Israel na kundi la Hezbollah.
Kwa upande wa Labanon ilikuwa ni sherehe na nderemo kwa kuachiwa kwa wapiganaji wao na kwa upande wa Israel ilikuwa ni masikitiko makubwa alisikika msemaji mmoja wa serikali akisema haya.
Miili ya wanajeshi, Ehud Goldwasser na Eldad Regev ambao waliuwawa wakati wa mapambano na Hezbolah.
Hata hivyo kuachiwa kwa wafungwa hao watano,kuliambatana na kutolewa kwa miili ya wapiganaji wa Hezbollah na Palestina ambao waliuwawa wakati wamapigano kwa kipindi tofauti na jeshi la Israel.
Pichani hapo juu anaonekana viongozi wa Hezbollah wakiwa na wanachama wao wakishangilia kuachiwa kwa wapiganaji wao.
Picha ya pili ni moja ya jeneza lililo beba mwili wa mmoja wa wapiganaji wa Hezbollh akitolewa ili kukabidhiwa kwa uongozi wa Hezbollah.
Picha ya tatu, wanaonekana badhi ya ndugu wa wanajeshi wa Israel wakilia kwa uchungu, mara baada ya kukabidhiwa miili ya wapiganaji wao.
Wazambia na chama cha upinzani wataka kujua kiundani kuhusu afya ya rais"Wapinzani"
Lusaka, Zambia - Chama kikuu cha upinzani nchini Zambia Patriotic Front(PF) kimetaka uwepo uwazi wa maelezo ya afya ya rais Levy Mwanawaswa kama bado kama anauwezo wa kuongoza nchi.
Akiongea haya, kiongozi wa wa chama hicho bwana, Michel Sata,amesema hawaamini taarifa ya serikali inayo sema hali ya afya inaendelea vizuri.
Rais, Levy Mwanawaswa mwenye miaka 59,amelazwa katika hospitali mjini Paris baada ya kupata ugonjwa wa kiarusi wakati alipo udhulia mkutano wa umoja wa Afrika nchini Misri. Picha ya hapo juu ni anaonekana rais Levy Mwanawasa, alipokuwa akihutubia balaza kuu la umoja wa mataifa.
Picha ya chini anaonekana rais,Levy Mwanawaswa, akikagua mradi wa maji safi hivi karibuni kabla ya kwenda kwenye mkutano nchini Misri.
Kampuni na serikali bado kuvutana" Waadhulika walitakakupewa malipo madogo".
Kano,Nigeria - Kampuni ya madawa ijulikanayo kama Pfizer imetangaza yakuwa mazungumzo kati ya srikali ya Nigeria umevunjika hivi karibuni.
Akiongea haya, wakili wa kampuni hii ya madawa Pfizer, alisema mkutano huu ulioudhuliwa na waziri wa sheria wa Nigeria na wakili mkuu bwana, Michel Andoakaa ,na mwakilishi wa wadhulika bwana, Alhaji Maisikeli.
Mwakilishi wa wadhulika alisema, mkutano huu haukufikia makubaliano,kwani kampuni ya Pfizer likuwa imetoa malipo ya kiasi cha $21million kwa maswala ya sheria na waathirika 200 kupata jumla ya $10million, na ni jambo ambalo haliwezekani, kwani watu waliotumia dawa hii aina ya "Trovan" kama majaribio mwaka 1996,walidhulika na wengine kupoteza maisha.
Picha ya picha ya bendera ya Nigeria.
Picha ya pili ni picha ya baadhi ya na dawa amabyo hutumiwa na binadamu karibu kila siku.
Afrika yawa na njia mbili kuhusu kukamatwa kwa rais wa Sudani.
Addis Ababa - Ethiopia - Umoja wa Afrika umeonya vikali yakuwa kitendo cha kumshitaki rais wa Sudan bwana, Omar Al-Bashir, kunaweza kuatarisha hali halisi ya usalama nchini Sudan hasa kwenye eneo la Darfur.
Na Umoja huu wa Afrika, umesema pia kushitakiwa huku kwa rais, Omar Bashir kunaweza kuwa ni njia moja ya kuanza kuwatishia viongozi wa Afrika kwa kutimika nguvu za mahakama pasipo kihalali hasa panapo kuwepo na swala la kisiasa.
Kushitakiwa kwa rais Bashir,kulitamkwa rasmi na wakili wa mahakama ya Hague bwana, Luis Moremo Ocampo, (ICC) wakati alipo kuwa akieleza mashitaka yanayo mkabili rais, Omar Al Bashir.
Mashitaka hayo yanayo muhusu rais Omar Al Bashir, ni kukiuka kwa haki za kibinadamu kwa serikali yake na vita vilivyo leta mauaji mauaji katika eneo la Darfur.
Hata hivyo Umoja huu wa Afrika , unapinga kukika kwa haki za binadamu katika nchi wanachama wake.
Juu ni picha ya alama ya mahakama, ambayo hutumika kutafutia haki kwa wale wanao onewa.
Picha ya pili anaonekana rais, Omar Al-Bashir akiwapungia mikono baadhi ya watu waliokuja kumuunga mkono kwa kupinga kushitakiwa kwake na mahakama ya mjini Hague.
Picha ya tatu wanaonekana baadhi ya watu wapatao maelfu ambao wanaathirika na kupata taabu kutokana na mgogoro unao kabiri eneo la Darfur.

Uchunguzi wa kifo cha bi,Benazir Bhutto kuanza "Umoja wa matifa"

Wachezaji lazima watimize makubaliano na timu zao "Pele"

London,Uingereza - Mfalme wa soka duniani Pele,amesema hivi karibuni yakuwa ni lazima wachezaji watimize na kutekeleza mikataba ambayo wamekubaliana na timu zao.
Pele,aliongezea kwa kusema yakuwa kauli ya kiongozi wa shirikisho la soka bwana, Sepp Blatter ya kuwa wachezaji wanakuwa kama watumwa ni kauli isiyo kuwa ya makini.
Picha hapo juu anaonekana mfalme Pele, akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.
Chini anaonekana Pele, akiwa ameshikilia moja ya nishani ambazo amekuwa akitunikiwa kutokana na umaili wake kwenye soka miaka ya nyuma.
Picha ya pili anaonekana, mfalme wa soka duniani, Pele akishangilia baada ya kufunga moja ya magoli ambalo liliifanya Brazil kuwa bingwa wa soka duniani mara ya tatu wakati wa enzi zake.
Chavez na Uribe wakutana mjini Caracas"Uhusiano utaimarika tena wasema marais hawa".
Caracas, Venazuela - Rais wa Venezuela bwana Hugo Chavez amekutana na rais wa Kolombia bwana, Alvaro Uribe.
Katika mkutano huu viongozi hawa walizungumzia ni jinsi gani wataweza kujenga na kudumisha uhusiano wao upya ambao ulikuwa si mzuri kwa kipindi kilefu.
Kwa upande wake rais Uribe , alisema yakuwa mkutano huu na rais Chavez,umefungua upya uhusiano wa nchi hizi mbili.
Hapo juu wanaonekana rais wa Kolombia bwana,Uribe akipunga mkono na rais Charvez akiwa amesima karibu, wakati rais,Uribe alipo wasili nchini Venezuela.
Chini wanaonekana rais Chavez , akiongea kitu fulani kwa rais wa Kolombia Alvaro Uribe.
Uchunguzi wa kifo cha bi,Benazir Bhutto kuanza"Umoja wa mataifa".
Islamabad, Pakistan - Umaoja wa mataifa umesema ya kuwa uchunguzi wa mauaji ya waziri mkuu wa zamani wa Pakistani, bi Benazir Bhutto.
Kukubalika kwa uchunguzi huo, kumekuja baada ya katibu mkuu wa umoja wa Mataifa bwana Ban Ki - Moon kukutana na waziri wa mabao ya nchi za nje wa Pakistan bwana ,Shah Mahamood Qureshi.
Kwa kusisitiza swala hili , bwana Shah Qureshi , alisema ya kuwa serikali ya Pakistani itatoa kila msaada katika kukamilisha uchunguzi huu wa mauaji ya bi Benazir Bhutto.
Picha ya kwanza , anaonekana bi Benazir Bhutto akiwa kwenye gari wakati wa kampeni ya kuimarisha chama chake, siku chache kabla ya mauaji yake. Picha ya pili, anaonekana bi,Benazir Bhutto na mumewe,wakati walipo kutana na rais wa zamani wa Palestina,hayati Yasir Arafat.
Picha ya tatu anaonekana waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, akiandika rambi rambi za serikali ya Amerika baada ya kifo cha bi Benazir Bhutto.
Chini picha ya mwisho, wanaonekana baadhi ya wapenzi na ndugu wa hayati bi Benazir Bhutto, wakiomboleza baada ya kifo cha bi Benazir Bhutto.
Amani ya Mashariki ya Kati ipo karibu "Asema waziri mkuu"
Paris, Ufaransa - Rais wa Ufaransa bwana, Nicholas Sarkozy amezungumza na viongozi wa Izrael na Palestina wakati wa kufunguliwa kwa mikutano ushirikiano wa nchi za ukanda wa Mediteranian uliofanyika katika jiji la Parisi.
Katika mkutano huo, viongozi hawa aliongea kwa pamoja ni amani tu, itakayo leta uelewano na ujirani mwema kati ya Israel na Palestina.
Akisisitiza hayo waziri mkuu wa Izrael kwa kusema ya kuwa hii inaonyesha yakuwa amani ya mashariki ya kati ipo karibu, na hasa kati ya Waizrael na Wapalestina.
Pichani hapo juu ni wanaonekana viongozi wa Israel kulia bwana Ehud Olmert , kati ni rais wa Ufaransa Nicholas Sarkozy na rais wa Parestina bwana Mohmoud Abbas, wakati walipo kuwa wakiongea na waandishi wa habari.
Picha ya pili anaonekana rais Nicholas Sarkozy, akipita na gari wakati wa sherehe ya kitaifa iliyo hudhuliwa na viongozi wa jumuia ya mwakanda wa Mediteraniani.
Kanisa Katoliki kuomba radhi tena kwa matukio yaliyofanywa kutumia jina la kanisa.
Sydeney, Australia - Askofu mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Baba Mtakatifu Benedict, amewasili nchini Australia siku ya tarehe 13/07/2008 tayari kunza ziara yake ya kidini.
Katika ziara hiyo Baba Mtakatifu, amesema yakuwa atawaomba radhi wale wote waliotendewa vibaya na baadhi ya wafanyaka au naviongozi wa dini wa dhehebu la katoliki.
Akiongea hayo , Baba Mtakatifu, alisema ni muhimu kwa Kanisa kukubali na yakuwa kuna mambo mabaya yalitendeka kwa kutumia jina la Kanisa Katoliki na hivyo ni lazima kanisa lifanye kila njia kuweka sawa na kuendelea kutangaza na kufanya kazi yake kama kanisa na kutangaza neno la Mungu.
Pichani hapo juu anaonekana, Baba Mtakatifu,anaonekana akiwabariki waumini waliokuja kuhudhulia misa.
Picha ya pili anaonekana , Baba Mtakatifu akifunga mikono kukubali kukaribishwa kwake katika ziara yake nchi Australia.
China na Urusi zakataa na kuonyesha misuri yake ndani ya Umoja wa Mataifa.
New York, Amerika - China na Urusi zimepinga hatua yoyote ya kuiwekea vikwazo serikali ya Zimbabwe inayo ongozwa na rais Robert Mugabe.
Akiongea haya waziri wa mambo ya nchi za njee wa Urusi, alisema itakuwa ni wahatari na kitendo cha kamati ya ulinzi ya umoja wa mataifa kuingilia maswala ya nchi hasa hasa katika maswala ya kisiasa.
Hata hivyo,waziri wa mambo ya njee wa Urusi aliongezea kwa kusema ya kuwa serikali ya Urusi, inapinga kitendo chochote cha kukandamiza haki za binadamu popote duniani na kulaani matukio yote yaliyotokea nchini Zimbabwe.
Picha hapo juu ni picha ya bendera ya Urusi na bendera ya China, nchi ambazo zimepinga kuwekewa vikwazo kwa serikali ya Zimbabwe.

Tuesday, July 8, 2008

Rais, Paul Kagame aionya Ufaransa"Rwanda sasa ni miaka 13 imepita.

Uwanja wa Nelson Mandela hautakuwa tayari kwa mashindano ya mabingwa wa soka wa mabara sita"Yasema kamati"

Port Elizabeth, Afrika ya Kusini - Uwezekano wa kuwa tayari moja ya uwanja utakao tumika kutimula daruga na gozi la ngombe lililo la mviringo ili kutafuta bingwa wa mabara yote sita ya dunia kwa upandea wasoka upo mashakani.
Mashindano haya yalianzishwa mwaka 1992 hadi 1995, kama mashindano ya kugombea kikombe cha Mfalme Fahd,ambapo zilialikwatimu kutoka nchi tofauti kupambana timu ya taifa ya Saudi Arabia.
Ndipo mwaka 1997, ndipo FIFA, shirikisho la soka duniani kulitambua rasmi na kuanza kugombaniwa na mataifa mabingwa wa mabara yote sitakabla ya kuanza kwa fainali za kugombea kombe la dunia..
Kwamujibu wa mwenyeki bwana, Ivin Khoza, na kamati inayo simamia ubora wa viwanja hivi nchini Afrika ya Kusini, amesema huenda uwanja wa Nelson Mandela ulipo mjini Port Elizabeth hautatayari kwa kuchezea mashindano hayo.
Hata hivyo huwanja huo utakuwa umekamilika ifikapo 2010, tayari kwa mashindano ya kugombea bingwa wa soka wa Dunia.
Picha hapo juu anaonekana bwana Danny Jordan, ambaye alipigania kwa kila hali hadi Afrika na Afrika ya Kusini kuweza kupewa nafasi ya kuwa mwenyeji wa kombe la dunia kwa mara ya kwanza.
Picha ya pili inaonyesha pilika za ujenzi wa kiwanja vinaendelea, hapo nimoja ya kiwanja kikiwa kinajengwa tayari kwa soka la dunia.
Chini ni picha ya bwana Ivin Khoza, ambaye ni mmoja ya wajumbe na viongozi wanao simamia ujenzi na maandalizi ya viwanja vitakavyo cheze wa soka ili kupata bingwa wa soka 2010 nchini Afrika ya Kusini.
Rais, Paul Kagame aionya Ufaransa" Rwanda sasa ni miaka 13 imepita".
Kigali, Rwanda - Rais wa Rwanda Paul Kagame, amesema yakuwa huenda ikaishitaki serikali ya Ufaransa kwa kuhusika kwake katika mauaji ya yaliyo tokea nchini Rwanda mwaka 1994.
Rais Kagame alisema yakuwa, ikiwa serikali ya Ufaransa aitafutilia mbali madai ya kuwashitaki baadhi ya viongozi wa serikali ya Rwanda katika mahakama za Ulaya.
Rais, Kagame alisisitiza kwa kusema yakuwa , uchunguzi uliofanywa umeonyesha ya kuwa Ufaransa ilihusika katika vita vilivyotokea nchini Rwanda vya wenyewe kwa wenyewe kati ya jamii ya watu wa kihutu na wakitutsi, na kusababisha maisha ya watu wasiopungua 800,000 kupoteza maisha yao wengi wao wakiwa watu kutoka jamii ya Kitusti.
Picha hapo juu anaonekana rais, Paul Kagame wa kwanza kushoto,akielekea kwenye mnara wa kumbukumbu ya mauaji ya mwaka 1994 ulipopo Murambi, huu ni mwaka wa kumi natatu tangu mauaji haya kutokea.
Picha ya pili wanaonekana rais, Paul Kagame na mke wake mama Jannette Kagame wakiweka shada la maua kwenye mnara wa kumbukumbu ya mauaji ya yaliyo tokea nchini Rwanda mwaka 1994.
Picha ya tatu anaonekan rais, Paul Kagame, akihutubia wananchi waliokuja kuadhimisha siku hiyo ya kumbukumbu ya mauaji ya watu wasiopungua 800,000, wananchi wa Rwanda.
Mugabe bado hawa shubiri kwa jumuia ya kimataifa"Afrika haya nia ya Wazimbabwe wenyewe."
Hakaido Toyako, Japan - Kundi la nchi tajiri zijulikanazo kama, G8 zimekubaliana kwa pamoja kwa kulaani hali ya kisiasa nchini Zimbabwe, na kuhaidi kuweka vikwazo kwa viongozi na wale watu wote walio usika katika kuleta mgogoro wa kisiasa nchini Zimbabwe.
Hata hivyo viongozi wa Afrika walio udhulia mkutano huu, walipinga na kusema swala la kuiwekea vikwazo Zimbabwe hakutasaidia kubadilisha matokea ya uongozi nchini Zimbabwe.
Viongozi hao wa Afrika, wakiongozwa na na mwenyekiti wa Muungano wa nchi za Afrika (AU), rais wa Tanzania bwana Jakaya Kikwete, walisema yakuwa swala la Zimbabwe waachiwe Wazimbwe wenyewe.
Hata hivyo,msemaji wa serikali ya serikali ya Zimbabwe,alisema ya kuwa kuwa uamuzi wa (G8) nchi tajiri duniani ni wakibaguzi, kwani serikali ya Zimbabwe imefanya ilichokuwa ikipigania tangu hapo mwanzo kurudisha ardhi kwa wananchi Wazimbabwe.
Picha hapo juu ni picha ya rais wa Zimbabwe bwana Robert Mugabe, ambaye amekuwa shubiri katika jumia ya kimataifa hasa bara la Ulaya na Amerika.
Chini ni picha ya viongozi wa nchi tajiri duniani walioudhulia kikao kilicho fanyika nchini Japan 2008.
Haini afungwa miaka 34,"Adhabu kali ndiyo mfano kwa wale wenye mawazo kama haya".
Malabo, Guinea Ikweta - Mtuhumiwa ambaye anahusika katika njama za kutaka kupindua serikali ya Guinea Ikweta bwana Simon Mann, amehukumiwa kwenda jela miaka 34 na miezi minne, baada ya kukutwa na hatia.
Hukumu hiyo ilitolewa siku ya tarehe 7/july/2007, bwana Simon Mann, alisema yakuwa yeye mwenyewe alikuwa siyo muhusika mkuu, bali kulikuwa na wakubwa wake , hata hivyo mahakama ya mjini Malabo haikujali malalamiko yake na kumpa adhabu kali kuwa mfano kwa wengine wenye mawazo hayo, alisikika akisema mmoja wa wasemaji wa serikali.
Guinea Ikweta, ni nchi moja wapo katika bara la Afrika, ambayo ni nchi iliyo na utajiri wa mali ya asili kama mafuta na gasi ambazo huuzwa katika nchi za Ulaya na Amerika.
Picha hapo juu ni picha ya rais wa, Guinea Ikweta bwana Teodoro Obiang Nguemo,amabye serikali yake ilitaka kupinduliwa na kundi la bwan Simon Mann.
Chini wanaonekana bwana, Simon Mann kushoto akiwa na mwenzake ambao walihusika katika jaribio la kutaka kupindua serikali, siya kwanza walipo kuwa wanaenda mahakamani kusikiliza kesi yao ya uhaini.
Jean Piera Bemba, asikiliza kesi yake kwa mara ya kwanza" Hati ya kukamatwa kwake ilikuwa siri".
Hague, Uhollanzi - Mahakama kuu inayo shughulikia makosa ya nayotokana na kukiuka haki za binadamu na makosa ya jamii iliyopo nchi Huollanzi hivi karibuni ilianza kusikiliza kesi ya bwana, Jeans Piere Bemba ambaye pia ni makamu wa rais wa Jamuhuri ya Kongo.
Kukamatwa kwa bwana, Jean Piere Bemba, kumekuja mara baada ya kuingia nchini Ubeligiji kutembelea ndugu zake, na hapo alikamatwa na polisi na kupelekwa nchini Uholanzi kujibu mashitaka dhidi yake.
Kwa mujibu wa msemaji mmoja wa mahakama ICC ya Hague, waraka wa kukamatwa kwa bwana, Jean Piere Bemba ilikuwepo toka zamani na ilikuwa imefanywa siri tangu kupitishwa kwake.
Juu ni picha ya bendera ya Umoja wa Mataifa ambayo ndiyo mama wa kila nchi.
Picha ya kati anaonekana bwana, Jean Piere Bemba aalipo kuwa mahakamani kusikiliza kesi dhidi yake.
Picha ya tatu ni moja ya alama inayo onyesha jinsi gani mahama ya Hague, ilivyo zingirwa na kazi kubwa ya kutafuta haki kwa wale waasilika na matukio ya tofauti ya dunia.
Uturuki ni nchi muhimu kwa ulinzi na usalama wa Ulaya"Mkurugenzi wa NATO"
Brussels,Ubeligiji - Mkurugenzi mkuu wa Shirikisho la Ulinzi la nchi za Ulaya NATO, bwana Jaap Hoop Scheffer,amesema hipo haja ya umoja huo kufanya kila njia kushirikaiana na serikali ya Uturuki ili kuimarisha ushirikiano zaidi.
Bwana, Jaap Hoop Scheffer, alisema yakuwa ipo haj kubwa sana ya kuialika Uturuki katikajumuia ya ulinzi na usalama wa Ulaya.
Na mkurugenzi wa NATO alisema hii itaimarisha kuimarika kwa jumuia hiyo.
Picha hapo juu ni picha ya bendera ya Uturuki nchi ambayo ina itajika kwa kila hali katika swala la ulinzi wa Ulaya.
Kati ni alama ya NATO.
Chini anaonekana mkurugenzi mkuu wa NATO bwana Jaap Hoop Scheffer akiongea hivi karibuni kataika moja ya mikutano ya NATO.
Amerika yatiliana mkataba na Cezch kujenga mitambo ya ulinzi.
Prague, Czech - Serikali ya Amerika na Serikali ya Czech zimetiliana mkataba wa kujenga rada kwa ajili ya matumizi ya kijeshi na ulinzi.
Makubaliano haya ni moj ya mipango ya serikali ya Amerika kuweza kujenga mitambo ya kulinda ulinzi katika maeneo ya Ulaya na maeneo mengine.
Hata hivyo serikali ya Amerika imekuwa ikisisitiza ya kuwa kuwekwa kwa mitambo hii kutasaidia kulinda pindipo nchi za Ulaya zikishambuliwa na nchi kama Iran, ikiwa nchi ya Iran itaweza kutengeneza mizinga/siraha ifikapo mwaka 2015.
Picha hapo juu anaonekana bi, Condeleeze Rice anaye shughulikia maswaya ya mambo ya nje ya nchi akitia saini mkataba wa kuwekwa kwa mitambo ya kijeshi nchini Cezch.
Picha chini wanaonekan bi Condeleeze Rice na waziri mkuu wa Cezch bwana, Mirek Topolanek wakionyesha vitabu ambavyo wamaetilana ambavyo mkataba wa kujengwa kwa mitambo ya kijeshi nchini Cezch.

Sunday, July 6, 2008

Venus atetea ubingwa wake,Williams wawanyota ya Wimbledon 2008.

Venus ateta ubingwa wake, Williams wawanyota ya Wimbledon 2008.

London, Uingereza - Bingwa mtetezi wa mchezo wa tenis kwa upande wa wanawake, Venus Williams ameweza kutetea ubingwa wake kwa kuweza kushinda tena kombe la mashindano ya Wembledon kwa mara ya nne, baada ya kumshinda mdogo wake Serena Williams, katika mchezo wa kutafuta bingwa wa tenis kwenye mashindayo hayo yaliyo fanyika nchini Uingereza.
Fainali hiyo iliyo udhuliwa na watu wasio pungua elfu kumi, wakiwemo aliyekuwa waziri mkuu wa zamani wa Uingereza bi Barones Thatcher, pamoja na wageni wengine waalikwa.
Picha hapo juu anaonekana, Venus Williams akiwa ameshikilia dishi/kombe la ubingwa wa tenis la Wimbledon kwa upande wa wanawake mara baada ya kumshinda mdogo wake Serena kwa seti 7-5,6-4.
Picha ya pili wanaonekana Venus na Serena Williams, wakiwa wameshikia vikombe mara baada ya kushinda tena mchezo wa tenis kwa upande wa wanawake , ambapo hushindanisha wapinzani wawili kwa wawili.
Picha ya tatu wanaonekana Venus na Serena, wakiwa wameshikilia madishi yao mara baada ya kumaliza kupambana, mshindi alikuwa Venus.
Picha ya nne , ni ya baba ya Serena na Venus, mzee Williams, akiangalia kwa makini nini la kufanya ili watoto wake waweze kushinda, hata hivyo wakati Venus na Serena walipo kutana, mzee Williams akuangalia mechi hii na aliamua kueleka nyumbani USA, kwani alisema ya kuwa kazi yake alisha maliza nani kazi ya watoto wake kujijua nani ni mshidi kati yao.
Picha ya tano wanaonekana Venus na Serena wakimenyana kutafuta nani bingwa wa Wimbledon 2008.
Picha ya mwisho wanaonekana Serena na Venus wakiiongi uwanjani tayari kwa mpmbano wakutafuta bingwa kwa upande wa wanawake 2008 kwenye mashindano ya Wimbledon.
Maombi ya wengi yasikika, Bi, Ingrid Betancourt,yupo huru baada ya miaaka sita.
Paris, Ufaransa - Bi, Ingrid Betancourt aliwasili hivi karibuni nchi Ufaransa, baaada ya kuachiliwa huru na kundi la FARC lilipo nchini Kolombia tarehe 2/07/2008.
Bi, Ingrid Betancourt, alikuwa ameshikiliwa na kundi la moja linalo pinga ns kupigana na serikali ya Kolombia kwa kipindi kisicho pungua miaka sita.
Hata hivyo bi, Ingrid Betancourt, aliachiwa huru pamoja na mateka wengine watatu, ambao ni raia wa Amerika na wengine kumi na moja raia wa Kolombia.
Picha hapo juu wanaoneka bi, Ingrid Betancourt, akimkumbatia kwa hamu toto wake wakike wakati walipo walipo kwenda kumpokea.
Picha ya pili anaonekana, bi, Ingrid Betancourt, akiwa analia kwa furaha,baada ya kutangaziwa yakuwa hawapo tena chini ya mikono ya kundi la FARC, na wapo huru kuelekea nyimbani.
Picha ya tatu, bi, Ingrid Betancourt anaonekana akimshika mtoto wake wa kike, Merania kwa upendo, wakati walipo kuwa wakijiaandaa kutoa shukurani za dhati kwa watu wote walio shirikaana katika sara hadi alipo achiwa huru. Picha ya nne anaonekana ,bi Ingrid Betancourt, akiwa anaangalia juu na kumshukuru Mungu kwa maajabu na uwezo wake alioufanya hadi sasa yupo huru.
Picha ya mwisho chini anaonekana bi. Ingri Betancourt, akiwa pamoja na rais wa Ufaransa, bwana Nicolas Sarkozy wakati walipo kutana mara baada ya kuwasiri nchini Ufarannsa.
Hatutachanganya siasa na misaada au biashara katika bara la Afrika.
Beijing,China - Serikali ya China imesema yakuwa kuziwekea vikwazo nchi ni kinyume na haki za binadamu.
Msemaji huyo wa wa serikali, bwana Liu Guijin, ambaye ni kiongozi anayeshughulika maswala ya Afrika, alisema yakuwa China, aitachanganya siasa na uchumi katika kufanya biashara au utoaji wa misaada kwa bara la Afrika.
Hapo juu ni picha ya ramani ya bara la Afrika, ambalo limekuwa katika hali ya utata kila kunapo kucha.
Nchi tajiri duniani kukutana tena kujadili hali ya duniani.
Tokoyo, Japan - Viongozi wa nchi tajiri na zenye viwanda duniani wanakutana nchini Japan, ilikujadili hali halisi ya dunia, hasa kupanda kwa bei ya mafuta na upandaji wa bei ya vyakula na nyezo zakufanyia kazi.
Mkutano huu ambao utachukua siku tatu, vilevile utajadili hali ya ilivyo bara la Afrika na mabadiliko ya hali hewa duniani.
Nchi hizo,tajiri duniani ni, Canada, France,Germany, Itali, Russia,na Japan, Amerika na Uingereza.
Hapo juu wanaonekana polisi walikijiandaa tayari kulinda usalama wa mkutano wa nchi tajiri duniani
Irak yafutiwa madeni na nchi za jumuia ya nchi za Kiarabu.
Bagdad,Irak - Muungano wa jumuia ya nchi za Kiarabu, (UAE) , zimetangaza rasmi kufuta madeni yote ambayo yalikuwa yanaidai nchi ya Irak, ambayo yanathamani ya dola - $7billion.
Haya yametamkwa na ujumbe wa shirilikisho hilo la nchi za kiarabu, zilizo ongozwa na Sheikh Khalif bin Zayed al Nahayan.
Nawakati huu, muungano huu wa nchi za Kiarabu zimemteua bwana, Abdalah Ibrahim al Sheihhi, kuwa balozi wa jumuhia hio nchini Irak.
Shirikisho hili lilifunga ofisi zake za kibalozi nchini Iraq, baada ya aliyekuwa balozi wa nchi ya Misri kutekwa nyara na kuuwawa.
Picha hapo juu ni wanaonekana waziri mkuu wa Irak bwana Nouri Al Malik aliyea kaa kushoto, akiongea na Sheikh Khalifa aliyekaa kulia wakati walipo kutana hivi karibuni.