Makundi ya kivita ya Somalia ya ungana kuipinga serikali.
Gedo,Somalia - 24/08/09. Kundi la Hizbu lililopo kusini mwa Somalia,limesema ya kuwa limeungana na kundi la Al-Shabaab.
Kujiunga kwa kundi la Hizbu, kulitangazwa na , Sheikh Ahmed Mohamud, ambaye ni makamu wa wa kundi hilo alitangaza hayo wakati alipo kutana na waandishi wa habari hivi karibuni.
Kiongozi huyo wa Hizbu, alisema wanaungana na wenzao ili kupambana na wapinga Wasomalia na tutawashinda alimalizia kwa kusema kiongozi huyo wa kundi la Hizbu lililopo mjini Gedo kusini mwa nchi ya Somalia.Picha hapo juu, ni wapiganaji wa kundi la Hizbu,kundi ambali limeungana na kundi la Al- Shabaab kupambana na serikali.
Shirika la ujasusi la Amerika na mkuu wake wasimama njia panda.
Washingiton, Amerika - 24/08/09.Shirika la kijasusi la Amerika, huenda lakawa na wakati mgumu kufuatia habari ya kuwa huenda kesi zinazo husiana na mateso ya watu walio daiwa ni magaidi, zikafunguliwa na kuanza kuchunguzwa tena.
Kesi hizo zilifutwa wakati wa uongozi wa rais wa zamani wa Amerika, George Bush, lakini tandu uongozi mpya wa rais , Baraka Obama, chini ya mwanasheria mkuu ,Erik H. Holder umekuwa na mtazamo upya katika swala zima la ugaidi.
Picha hapo juu, ni alama ya shirika la kijasusi la Amerika, ambalo ndicho kiini cha ulinzi wa serikali ya Amerika.
Picha ya pili, ni ya mwanasheria mkuu, wa Amerika, Erik H.Holder, ambaye tangu achukue ofisi, amekuwa na wakati mgumu kujaribu kuweza kurudisha hadhi ya shirika la kijasusi la Amerika.
Bargam, Afghanistan - 24/08/09.Wakuu wa majeshi ya Amerika na NATO wamesema ya kuwa hawana majeshi ya kutosha kuweza kupambana na kundi la Taliban hadi kuliangamiza.
















































