Friday, April 29, 2011

William na Catherine wafunga pingu za maisha.

Mamia washuhudia William na Catherine walipokuwa wana wafunga pingu za maisha.
London, Uingereza 29/04/2011. Mamia ya wakazi wa jiji la London na dunia nzima wameshuhudia mjuukuu wa malkia Elizabeth, William akifunga ndoa na mchumba wake Catherine.
Harusi hiyo iliyo fungwa kanisani, na kuhudhuliwa na Malkia na familia yake, wazazi wa bibi harusi na familia yao, viongozi wa dini ,serikali na wageni wengine waalikwa.
Harusi hii ilitangazwa katika runinga kwenye nchi zaidi ya 108 dunia.
Bwana na bibi harusi William na Catherine wakipeana kisss, kuchuuum mbele za mamia kuashiria ya kuwa wao niwapendanao.
Bwana na bibi harusi William na Catherine wakionekana kwa mara ya kwanza mbele za mamia kama mke na mume mbele ya baraza katika makazi yao.
Mania walikuwepo kushuhudia kuchumooo kisss wa kukata na shoka.
Ishara ya yote kukamilika, bwana na bibi harusi walivalishana pete ikiwa ni haadi ya kuwa wamekuwa kama mke na mume
Picha hapo juu wanaonekana bwana hariusi William na bibi harusi Catherine wakiwa katika mkokoteni wa asili ambao unavyutwa na farasi njiani kueekea nyumbani kwa mapumziko , huku bwana harusi akikitoa tabasamukisi, baada ya kukabidhiwa mke wake na wazazi wa binti.
Hapa wanaonekana bwana harusi William na bi harusi Catherine wakila kiapo kwa pamoja mbele ya kasisi.
Baada ya harusi, bwana na bibi harusi wanatoka kanisani wakiwa kama mume na mke, na huku wakiwa wanatizamana kwa tabasamu la mahaba.
Picha hapo juu wanaonekana mke na mume wakiangaliana kwa furaha baada ya kumaliza kuimba nyimbo ya kumshukuru Mungu. hapa inaelekea Willy akimwambia mkewe, kumbe unajua kuimba hata nyimbo za dini.
Picha hapo juu anaonekana, William akimvalisha pete mke wake Catherine mbele ya kasisi, huku mkewe akitabasamu kwa furaha.
Picha hapo juu, baba wa Catherine, Middleton akimwakilisha mwanae mbele ya Kasisi tayari kula kiapo kumtwaa William kama mme wake, na huku kulia kwao mume wake Willy na mdogo wake Hurry wakimakini tayari kusikia habari njema toka kwa Catherine.
Picha hapo juu, wanaonekana bibi Malkia Elizabeth na kulia babu Philips wakiwa wamekaa tayari kungojea mjukuu wao kula kiapo mbele ya Mungu na kasisi ya kuwa anamchukua Catherine kama mke wake. mmm sasa mme wangu Willy anachukuliwa hivi hivi namwona , yaaa na mimi napata mke mwingine , hapo inaelekea bibi na babu wakiwa wanawaza.
Picha hapo juu anaonekana Catherine akielekea kuingia kanisani tayari kula kiapo cha kumpenda mume wake Willy.
Picha, hapa inaonekana mdogo wa Willy, Hurry akimwambia kaka yeke sasa unakwenda kuwa mme wa mtu, na kaka yake Willy akisema yaaa naenda kuanza maisha mapya mdogo wangu, hata hivyo wewe ni mgodo wangu na ndugu yangu milele.

Monday, April 25, 2011

Taliban wavunja jela na kutoroka.

Gaidi akamatwa nchi Venezuela.
Caracas, Venezuela - 25/04/2011. Maafisa wa usalama serikali ya Venezuela wamemkamata gaidi ambaye ameshukiwa kutaka kuhusika na kitendo cha kigaidi.
Kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya Venezuela zinasema "gaidi huyo Joaquin Perez Becerra alikamatwa siku jumamosi baada serikali ya Kolombia kuwasiliana na serikali ya kuwa gidi huyo atapitia nchini"
Kukamatwa huko kwa Perez kuna kumekuja baada ya Interpol kutoa hati ya kukumatwa kwake wakati akitokea nchini German.
Huusiano wa serikali ya Venezuela na Kolombia umekuja baaada ya nchi hizo kukubaliana kushirikiana kiusalama baada ya rais mpya wa Kolombia Juan Manuel Santos kukutana na rais wa Venezuela Hugo Chavez na kuongea kumaliza uhasama kati ya nchi hizo mbili.
Taliban wavunja jela na kutoroka.
Kandahar, Afghanistan 25/04/2011. Zaidi ya wafungwa mianne wametoroka kutoka katika jela moja ambayo wengi wa wafungwa hao walikuwa wapiganaji wa kundi la Taliban.
Wafungwa hao ambao wametoroka kupitia shimo walio lichimba kwa urefu chini ya ardhi hadi kutoke nje gereza bila watu wausalama kutambua.
Msemaji wa Zabuillah Mujahed alisema " shimo hilo lilichimbwa kwa muda wa miezi mitano na walichukua masaa manne na nusu kutoka ndani ya jela hiyo.
NATO, alitibitisha habari hizi kwa kusema " tuna habari ya kuwa wametoraka kupitia shimo ambalo walilichimba kwa umbali wa zaidi ya mita 320.
Naye msemaji wa serikali ya Afghanistan, Waheed Omer kutoroka kwa wafungwa hao siyo picha nzuri kwa serikali , na tutahakikisha tunawakama wote waliotoroka."
Hii itakuwa ni mara ya pili wa wafungwa kutoka toka jela, baaada ya tukio kama hili mwaka 2008 ambapo wafungwa wapatao 1,000 walitoroka.
Makazi ya Muammar Gaddafi yashambuliwa.
Tripoli, Libya 25/04/2011.Ndege za jeshi la NATO limeshambulia makazi ya rais wa Libya ambaye majeshi yake yanapambana na majeshi ya upinzani yanayo ungwa mkono na Ufaransa, Uingereza na jumuia ya NATO.
Msemaji wa serikali Mussa Ibrahim amesema " ndege za jeshi la NATO lilishambulia makazi hayo kwa nia ya kutaka kumua rais wa sasa Muammar Gaddafi, ambaye nchi wanachama wa NATO zinataka atoke madaraka kwa kutumia nguvu za kijeshi jambo ambalo linaonyesha nini nia ya NATO."
Katika mashambulizi hayo, baadhi ya raia na wanajeshi waliokuwepo kwenye eneo hilo wanjeruhiwa vibaya na kuharibu kwa kiasi kikubwa majengo ya eneo hilo lililopo Ba el Azizia.

Friday, April 22, 2011

Ndege aina ya Drone kuanza kutumika nchini Libya.

Umoja wa Afrika waondolea vikwazo Ivory Coast.
Adis Abeba, Ethiopia -22/04/2011. Umoja wa Afrika umeondoa vikwazo amba
yo vilikuwa vimewekwa zidi ya nchi ya Ivory Coast.
Akiongea kuondolewa kwa vikwazo hivyo, mwenyekiti wa kamati ya amani ya Umoja wa Afrika alisema " tunapenda serikali iliyo chukua madaraka ihakikishe yakuwa ina imarisha usalama, haki na amani kwa watu wote katika misingi ya kidemokrasia na kuanzisha mpango mzima wa watu kusameheana."
Uamuzi huo umekuja baada ya aliye kuwa rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, kutolewa madarakani kwa nguvu na jeshi la Alassane Ouattara kwa kusaidiwa na jeshi la Ufaransa.
Wapinzani hao katika kiti kugombea kiti cha urais Laurent Gbagbo na Alassane Ouattara walianza kuvutana kisiasa baada ya matokeo ya uchaguzi kutolewa n a huku kila mmoja kudai ndiye aliye ibuka mshindi.
Ndege aina ya Drone kuanza kutumiwa nchi Libya.
Benghazi, Libya 22/04/2011. Aliyekuwa mgombea wa kiti cha urais na ambaye pia ni mbuge wa chama cha Republikan cha Amerika amewasili nchini Libya.
John McCain, amewasili nchini Libya ili kuongea na viongozi wa upinzani ambao wanapingana na serikali ya Libya inayo ongozwa na Kanali Muammar Gaddafi.
Akijibu swali nini nia ya madhumuni ya ziara yake nchini humo, McCain alisema " nimekuja ili kuangalia hali halisi kutokana na matukio yanayo endelea."
Kuwasili huko kwa McCain kumekuja baada ya rais wa Amerika Baraka Obama kuruhusu matumizi ya ndege Drones ambazo zinatumia nguvu za mtandao katika kufanya mashambulizi zitumike katika vita zidi ya serikali ya Libya.

Sunday, April 17, 2011

Serikali ya Kuba kufanya mabadiliko ya kisiasa.

Serikali ya Kuba kufanya mabadiliko ya kisiasa. Havana, Cuba -17/04/2011. Rais wa Kuba ametangaza mabadiliko ya kisiasa ambayo yatakayo fanyika nchini humo.

Rais wa Kuba Raul Castro akiwahutubia viongozi na wanachama tawala wapatao 1000 katika mkutano mkuu wa chama tawala alisema "tumefikia wakati wa kukubaliana na hali halisi ya mabadiliko ya kisiasa , kwa minajili hiyo tumekubaliana ya kuwa kiongozi wa nchi atakuwa anakaa madarakani kwa kipindi cha miaka hadi kumi tu.
rais Raul Castro alimekuwa mtawala wa nchi hiyo tangu alipo achiwa madaraka na kaka yake Fidel Castro
Iran yazindua gari mpya ya kifahari.
Tehran, Iran 17/04/2011.Serikali ya Iran imetangaza yakuwa inampango wa kujenga meli kebu ambayo itatumika katika kukagua na kulinda mipaka yake katika pwani ya kusini mwa nchi hiyo.
Mkuu wa jeshi la Iran, Admiral Amir Farhadi, alisema "meli kebu hiyo ambayo itakuwa na uzito wa tani 500 na itakuwa tayari kuanza kazi mwaka 2012 Julai."
Irani imekuwa ikipiga hatua za kisayansi na teknolojia na kuwa nauwezo wa kutengeneza mitambo na siraha za kijeshi.
Wakati huo huo kampuni ya kutengeneza magari ya Iran, imezindua gari mpya ya aina ya Dena ambayo inatarajiwa kuwa katika barabara hivi karibui, na wanunuzi wa magari kutoka Iran,nchi za Rusia,Syria, Turkey, iraq,Ukraine na Misri, wataaanza kuyatumia magari mwaka 2011.

Friday, April 15, 2011

Obama,Sarkoz na Kameron tutahakikisha Gaddafi anang'oka.

Obama, Sarkoz na Kameron tutahakikisha Gaddafi anang'oka.

London, Uingereza 15/04/2011. Viongozi wa Uingereza, Ufaransa na Amerika wamekubaliana kwa pamoja kuundeleza mapambano dhidi ya kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Nikolas Sarkozi rais wa Ufaransa, waziri mkuu wa Uingereza David Kameon na rais wa Amerika Baraka Obama, kwa pamoja wamekubaliana kuhakikisha kiongozi wa Muammar Gaddafi anatoka madarakani.
Viongozi hao walitoa waraka wao wa pamoja na kusisitiza "sheria ya muswada ya kamati ya usalama ya umoja wa mataifa ya 1973, inataka jumuia ya kimataifa kulinda usalama wa raia na razima waitekeleze."
Waraka huo uliongezea " NATO na washiriki wake wataendelea na jukumu lao la kulinda raia na kuhakikisha Kanali Muammar Gaddafi anatoka na kuwapa uhuru wa na nchi wa Libya kujitawala wenyewe.
Hata hivyo baada ya waraka huo kutoka, kiongozi wa Libya alionoekana katika mitaa ya Tripoli akiwaslimia wanchi na wadau wanao muunga mkono, na huku mwanae wa kike Aisha Gaddafi aliwahutubia watu waliokuja Bab al Azizyah kuadhimisha miaka 25 tangu Amerika ilipo vamia Libya na kusema baba yake hataachia madaraka kwa kulazimishwa wala vitisho vya nchi za Magharibi na washirika wake.

Wednesday, April 13, 2011

Viongozi wakutana Katar kutathmin hali ya Walibya.

Nchi zinazo ongoza kukua kwa uchumi dunia zakutana nchini China. Hainan, China 13/04/2011. Viongozi wa serikali na mabenk wamekutana nchi China ili kuangalia kiundani njia bora ya kuimarisha sekta ya bishara ya kifedha na uchumi.

Li Wuwei, makamu wa mwenyekiti na mshauri wa mambo ya kisiasa alisema, " nchi wanachama zimejitahidi na kushirikiana katika kuinua hali ya kiuchumi baada ya ya myumbo wa kiuchumi kutokea na zitaendele kufanya hivyo hasa katia nchi zinazohitaji kuinuka kiuchumi ili ziweze kukidhi mahitaji ya jamii zao."
Mkutano huo unaojulikana kama BRICS unajumuisha nchi za Brazil, Urussi, China na Afrika ya kusini nchi ambazo zinaongoza katika kukua kwa uchumi kwa haraka zaidi.
Rais wa zamani wa Misri na watoto wake wawekwa chini ya ulinzi wa polisi.
Kairo, Misri 13/04/2011. Rais wa zamani wa Misri amewekwa kizuizini pamoja ya watoto wake wawili wa kiume, ilikuwezesha uchunguzi zidi ya kesi inayo wakabili ya rushwa na unyanyasaji.
Kwa mujibi wa wakili wa serikali alisema " Hosni Mubaraka na watoto zake Gamal na Alaa watakuwa kuzuizini kwa muda wa siku15 wakati uchunguzi unaendelea zidi yao."
Hosni Mubaraka 82, ambaye ametawala Misri kwa miaka zaidi ya miongo mitatu alitolewa madarakani na maandamano ya watu waliotaka aachie madaraka mapema mwanzoni mwa mwaka huu..
Habaria zinasema rais Hosni Mubaraka anamatatizo ya moyo na hivi sasa yupo hspitali amelazwa kwa uchunguzi zaidi wakati watoto wake wako chini ya ulinzi wa polisi.
Viongozi wakutana Katar kutathmini hali ya Walibya.
Doha,Katar - 13/04/2011. Viongozi wa kundi la upinzani linalo pingana na serikali ya Libya wamekutana na viongoziwa nchi tofauti nchi Katar ili kujadili hali halisi ya mapambano yanayo endelea ili kung'oa madarakani kiongozi wa Libya MuammarGaddafi.
Akiongea mbele ya viongozi walioudhuria mkutano huo waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza William Hague amesema, "nilazima tuhakikishe tunafanya kila njia ili tunasaidia kundi la upinzani ili kuliwezesha kuimarisha demokrasi nakuhakikisha Muammara Gaddafi anakubaliana na matwakwa ya wanchi wa Libya."
Msemaji wa kundi la upinzani linalo mpinga serikaliya Mahmud Shamman alisema, " tungependa tutambulike kama wawakilishi wa serikali mpya ya Libya ambao tupo kwa ajili ya kuijenga Libya kwa kila Mlibya."
Mkutano wa huu umefanyika ili kuangalia ni kwa kiasigani jumuiya ya kimataifa itaweza kuisaidia Libya.

Monday, April 11, 2011

Jeshi la Alassane Ouattara la mkamata Laurent Gbagbo.

Jeshi la Alassane Ouattara la mkamata Laurent Gbagbo. Abidjan, Ivory Coast -11/04/2011.Jeshi la upinzani linalo ongozwa na Alassane Ouattara, kwa kushirikiana na jeshi la Ufaransa limefanikiwa kumkamata aliyekuwa rais wa Ivory Coast baada ya kuvamia makazi yake.

Rais huyo wa Ivory Coast Laurent Gbagbo,alikamatwa baada ya mashambulizi kati ja jeshi lake na jeshi la Ouattara kwa msaada wa Ufaransa na vifaru huku helkopta zikisaidia kuhakisha ya kuwa Gbagbo na jeshi lake hawawezi kuendeleza mashambulizi.
Msemaji wa Alassane Ouattara, Affaoussy Bamba alisema, " Laurent Gbagbo amekamatwa na sasa yupo mokononi mwa jeshi letu.
Hata hivyo , msemaji wa Laurent GbagboToussaint Alain , alisema jeshi la Ufaransa limemkamata Gbagbo baada ya kuvamia makazi yake.
Kufuatia madai hayo, waziri wa ulinzi wa Ufaransa alikanusha madai hayo na kusema ,"Gbagbo alikamatwa na jeshi la Alassane Ouattara."
Kukamatwa huko kwa Laurent Gbagbo, kumekuja baada ya rais huyo kudai yakuwa yeye ndiye mshindi wa matokeo ya uchaguzi, na huku mpinzani wake Alassane Ouattara akidai yeye pia ameshinda uchaguzi na umoja wa mataifa kuunga mkono.
Kundi la upinzani la kataa mpango wa kuleta amani nchini Libya.
Benghazi, Libya - 11/04/2011. Kundi la upinzani linalopigana na serikali ya Libya limepinga mpango uliopitishwa na umoja wa Africa ili kusimamisha mapigano.
Msemaji wa kundo hilo lili na makao yake makuu Benghazi, Mustafa Jabiri alisema " hatuwezi kushirikiana na uongozi wa Muammar Gaddafi, na lazima uachie madaraka yeye na familia zao, na tutakufa nao au tuchukue ushindi kwa mtutu wa bunduki."
Uamuzi wa kundi hilo kukataa mpango wa umoja wa Africa ili kuleta amani kati ya serikali ya Libya na wapinzani wake ulikuja baada ya viongozi wa jumuia hiyo chini ya rais wa Afrika ya Kusini Jacob Zuma kukutana na Muammar Gaddafi ili kujadili mpango wa kuleta amani.

Iceland yasumbua vichwa vya wafadhili wake.

Iceland yasumbua vichwa vya wafadhili wake.

Hague, Netherland - 11/04/2011. Serikali ya Uingereza na serikali ya Netherland zimeishitaki serikali ya Iceland baada ya kutoke mgogoro wa kulipa deni.
Uamuzi huo wa serikali hizo kuishitaki Iceland limekuja baada ya wanchi wa Iceland kupinga kitendo cha serikali yao kulipa deni la pesa ambazo ziliazimwa kwa Iceland ili kusaidi serikali ya nchi hiyo baada ya myumbo wa Mabenki nchini humo.
Hata hivyo msemaji wa serikali ya Iceland alisema " serikali ya Iceland haina wasiwasi n aitalipa dei hilo, hata kama wanachi hawapendelei kitendo hicho."
Serikali ya Iceland ilipewa pesa na serikali za Uingereza na Netherland ili kuimarisha mabenki yake baada ya kutokea kwa myumbo wa kipesa na kutishia uchumi wa Iceland.

Thursday, April 7, 2011

Mahakama ya Hague yaanza kesi za machafuko ya Kenya.

Mahakama ya Hague yaanza kusikiliza kesi za machafuko ya Kenya.

Hague, Netherland -07/04/2011. Viongozi wa siasa kutoka nchini Kenya wamefikishwa mahakamani kufuatia machafuko yaliyo tokea wakati na kabla uchaguzi.
William Ruto,Henry Kosges ambao walikuwa mawaziri na mtangazaji Joshua Arao Sang wanashita kwa kuchochea machafuko ya kikabila yaliyopo nchini Kenya.
Hata hivyo bado kuna watuhuniwa wengine wanatarajiwa kufikishwa mahakani kujibu mashitaka kama haya.
Uchaguzi wa urais wa mwaka 2007 nchini Kenya ulileta machafuko ya kisiasa na hata kupelekea kumwagika kwa damu na watu kupoteza maisha yao.
Japan yakumbwa na tetemeko la ardhi jingine.
Tokyo, Japan -07/04/2011. Tetemeo kubwa la ardhi limeikumba tena Japan baada ya tetemeko la kwanza ambalo limeleta maafa makubwa.
Tetemeko hili lililo tokea kaskazini mwa Japan, limepelekea jamii nzima ya maeneo imetakiwa kuondoka kwani kunawasiwasi tsunami kutokea.
Wataalamu wa mambo ya kiyasansi ya ardhi na hali ya hewa wamesema "tete hilo limekuwa na nguvu za uwezo wa 7.1 magnitude."
Hata hivyo mpaka sasa hakuna habari zaidi kimaafa na watu kupoteza maisha.

Wednesday, April 6, 2011

Uingereza ya kubali baadhi makosa.

Uingereza ya kubali baadhi ya makosa.

Islamabad, Pakistani - 06/04/2011. Waziri mkuu wa Uingereza amewahutubia waandishi wa habari wanafunzi na viongozi wa serikali wa Pakistan na kukubali yakuwa Uingereza inatakiwa ibebe lawama kutokana na machafuko katika eneo hilo.
David Cameron alisema " Uingereza imekuwa ni chanzo cha matatizo katika eneo hilo na tumekuwa tukihusika katika sehemu tofauti hapo mwanzo.
"Ukiangalia kiundani utaona historia ina husisha Uingereza kwa njia moja au nyingine."
Waziri mkuu wa Uingereza yupo ziarani nchini Pakistani ili kukuza uhusiano na nchi hiyo ambayo ni mshiriki mkubwa katika vita zidi ya ugaidi.

Tuesday, April 5, 2011

Mke wa Ratko Maladic aiambia mahakama mume wake huenda amefariki.

Mke wa Ratko Mladic aiambia mahakama mume wake huenda amefariki. Belgrade,Serbia - 05/04/2011. Mke wa aliyekuwa kiongozi kivita vilivyo tokea nchi za Balkan amefikishwa mahakani ili kujibu mashitaka ya kukutwa na siraha. Bosijlika Mladik, ambaye alifikishwa mahakamani, aliiambia mahakama ya kuwa siraha hizo ziliwekwa na mumewe na aliwazuia kugusa kabati hilo.

Akiongelea kuhusu swala la mume wake Bosijlika Mladik alisema " mume wangu aliondoka nyumbani mwaka 2001 siku ambayo Slobadan Milosoevik alikamatwa na tangu siku hiyo hatujamwona na huenda amesha fariki kwani alikuwa anatumia vidonge kwa ajili ya matibabu na nivigumu kuishi bila kutumia vidonge hivyo."
Ratko Mladic ambaye alikukuwa mkuu wa majeshi wakati wa vita hivyo vilivyo tolekea katika nchi za Balkani
Haiti ya mchagua aliyekuwa msanii wa muziki kuwa rais wao.
Port-au-Price, Haiti 05/04/2011.Matokeo ya uchaguzi nchi Haiti yametangazwa na aliyekuwa mwanamusiki maharufu nchini humo kushinda katika kiti cha kugombania uchaguzi wa rais.
Michel Martelly au Sweet Micky, ameshinda uchaguzi huo baada ya wadau na wapenzi wa mwanamziki Wyclies Jean kumpigia kura kwa wingi .Wyclif Jean ambaye hapo mwanzoni aligombea kiti hicho lakini kujitoa kutokana na sababu za kiufundi.
Akiongea baada ya matokeo hayo Michel Martel, alisema" nitajitaidi kuijenga upya Haiti na kuzidisha mshikamano na ushirikiano katika jamii ya Wahaiti."
Uchaguzi huo wa Haiti utawezesha nchi hiyo kujengwa upya baada ya kukutwa na janga la tetemeko la Ardhi ambalo lilisababisha uharibufu mkubwa karibu nchi nzima.

Sunday, April 3, 2011

Mahaka ya kimataifa yakataa kesi iliyofunguliwa na Georgia.

Mahakama ya kimataifa yakataa kesi iliyo funguliwa na Georgia. Hague, Uhollanzi - 03/04/2011. Mahakama ya kimataifa ya umoja wa mataifa imekataa kesi iliyo letwa na serikali ya Georgia zidi ya Russia.

Habari kutoka mahakama hiyo zinasema " mahakama haiwezi kuendelea na kesi kutokana na baadhi ya mazungumzo haya kufanyika na kuchunguzwa."

Kesi hiyo ulifunguliwa na serikali ya Georgia baada ya jeshi la Urussi kuivamia Georgia ili kuzuia mauaji dhidi ya wakazi wa Abkhazia na Kusini Ossetia.

Jeshi la Ufaransa la zuia kiwanja cha ndege.
Abidjan, Ivory Coast -03/04/2011.Jeshi la Ufaransa limeshikilia kiwanja cha ndege cha jiji la Abidjan.
Jeshi hilo la Ufaransa ambalo lipo chini ya Umoja wa Mataifa huku majeshi ya rais wa sasa wa Ivory Coast Laurent Gbagbo na mpinzani wake Alassane Ouattara ya kiendelea kupigana.
Machafuko ya kisiasa nchini Ivory Coast yalianza baada ya uchaguzi mkuu wa kumchagua rais kuingia mgogoro dhidi ya Gbagbo na Ouattara kufuatia matokeo yaliyo tangazwa.

Friday, April 1, 2011

Wafanyakazi wa Umoja wa mataifa wavamiwa.

Wafanyakazi wa Umoja wa mataifa wavamiwa. Mazar-el-Sharif, Afghanistan -01/04/2011. Ofisi za umoja wa mataifa nchini Afghanistan zimevamiwa na waandamanaji ambao walikuwa wanapinaga kitendo cha mchungaji mmoja kuchoma Kuraan.

Waandamanaji hao walivunja jengo la umoja wamataifa na kuwavamia wafanyakazi waliokuwemo katika eneo hilo na kusababisha vifo vya wafanyakazi wanane wa umoja wa mataifa.
Masemaji wa polisi alisema " baadhi ya waandamanaji walivamia majengo ya umoja wa mataifa kwa nguvu na kupanda juu ya ofisi hizo na kuleta madhara makubwa."
Maandamano hayo yalifanyika baada ya swala ya ijumaa ili kupinga kitendo cha mchungaji mmoja kuchoma kitabu cha dini.

Wednesday, March 30, 2011

Rais wa Syria ahutubia wananchi baada ya maandamano.

Rais wa Syria ahutubia na wanachi baada ya maandamano. Syria, Damascus - 30/03/2011. Rais wa Syria amelihutubia taifa siku kadhaa baada maandamano yaliyo fanyika nchini humo kutaka mageuzi.

Akiongea kupitia runinga na mbele ya bunge rais Bashar al Asad alianza kwa kusemasema " mimi ni Msyria na yoyote ambaye ni Msyria atakuwa anajidai kwa kutembea kifua mbela."
Najua Wasyria walikuwa wanasubiri maoni yangu, lakini ulinibidi nisubiri ili nipate picha kamili na huhakika wa hali halisi ili kuto wapa maadui wa Syria kutokana na hali iliyokuwawakati huo."
Naomba niwaeleze Wasyria wenzangu lazima tuwe na umoja na tutatue tofauti zetu bila magomvi na tuta shinda mbinu zinazo tumiwa na vyombo vya habari ambavyo vinatumika kudanganya dunia kuhusu hali ya nchi yetu."
Rais Al-Asad alikuwa akihutubia ili kuelezea ni kwa jinsi gani uongozi wake unavyo kabiriana na mageuzi yanato likumba bara la Waarabu.

Tuesday, March 29, 2011

Viongozi wakutana kujadili hali halisi ya Libya.

Viongozi wakutana kujadili hali halisi ya Libya.

London, Uingereza - 29/03/2011. Viongozi wa nchi za jumuia ya NATO na washiriki wake wanakutana jijini London ili kujadili hali halisi nchini Libya.
Akifungua mkutano huo, waziri mkuu wa Uingereza David Cameroon alisema " tumekutana hapa ili kusaidia nia ya watu wa Libya na ambao wanataka kujenga nchi yao bila vitisho na kuhakikisha lengo lao linafanikiwa."
Mkutano huo ambao utakuwa na lengo la kupanga na tutathmini hali ya kisiasa nchini humo pindipo mageuzi ya takapo fanikiwa nchini Libya.

Friday, March 25, 2011

NATO kuongoza mapambano zidi ya Libya.

NATO kuongoza mapambano zidi ya Libya.

Brussels,Ubeligiji - 25/03/2011. Jumuia ya ulinzi na shirikisho la kijeshi la nchi wanachama wa
NATO zimekubaliana kuchukua majukumu na kuongoza vita zidi ya kiongozi wa Libya.
Katibu mkuu wa NATO Anders Fogh Rasmussen aliongea na waandishi wa habari baada ya kikao cha viongozi hao kuamua kuchukua jukumu hilo kutoka kwa serikali ya Amerika.
Anders Fogh Rasmussen alisema " NATO itachukuwa majukumu yote ya kuhakikisha ya kuwa amri iliyo wekwa na umoja wa mataifa ya kumzuia kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi kutumia jeshi la anga katika mashabulizi zidi ya wapinzani wake."
NATO ilianza mashabulizi nchi Libya baada ya kamati ya usalama ya umoja wa mataifa kupiga kura kumzuai kiongozi wa Libya kutumia jeshi la anga.
Wimbi la mageuzi ya kisiasa la aanza nchini Syria.
Daraa, Syria - 25/03/2011. Maafias wa usalama nchini Syria wamewashambulia waandamanaji ambao wanataka serikali ifanya mageuzi ya kisiasa.
Waandamanaji hao ambao waliandamana katika mji wa Daraa, walikutana na police na maafisa usalama wakati wakiwa njiani kuelekea kwenye ofosi za serikali.
Rais wa Syria Bashar al Assad ametangaza kuachiwa kwa wale wote walio kamatwa.
Maandamano yanayofanyikannchini Syria ni moja ya wimbi la mageuzi ambayo yana vuma katika bara la Kiarabu na nchi za Kiarabu pia.

Wednesday, March 23, 2011

Jerusalem ya kutwa na mlipuko wa bomu.

Jerusalemu ya kutwa na mlipuko wa bomu.

Jerusalem, Izrael 23/03/2011. Mlipuko wa bomu umetokea katika jiji la Jerusalem kwenye maeneo ya al Quads.
Msemaji wa polisi alisema " mlipuko huo ulisababishwa na bomu lenye uzito wa kati ya kili 1-2 na ulipakiwa katika sanduku dogo."
Mlipuko huo umesababisha watu wapatao 30 kujeruhiwa na mtu mmoja kupoteza maisha.
Waziri mkuu wa Benyamin Netanyahu amelaani kitendo hicho na kukatiza safari yake ya kiserikali nchini Urussi.

Monday, March 21, 2011

Vladmil Putin alaani mashambulizi zidi ya LIbya.

Vladmil Putin alaani mashambulizi zidi ya Libya. Moscow, Urussi 21/03/2011. Waziri mkuu wa Urussi amezilaumu nchi za magharibi kwa kitendo chake cha kuishambulia Libya.

Vladamil Putin alisema " mashambulizi yanayo endelea nchini Libya ni ya kishetani na Amerika na washiriki wake wanafanya mashambulizi bila hata kufikilia mbele."
Na hii inaashiria ya kuwa lazima tuongeze uwezo wetu wa kijeshi ili kuendana na hali ahalisi."
Wakati huo huo, mtoto wa kiongozi wa Libya Saif al Gaddafi amesema "rais wa Ufaransa Nikolas Sarkozy anatakiwa kurudisha pesa zote ambazo serikali ya Libya ilimsaidia wakati wa kampeni zake za Urais, kwani malipo yake ni kuongoza na kuwa kinara wa kutushambulia kivita na kusahahu misaada yote na tunao ushahidi."
Hata hivyo msemaji wa rais Nikolas Sarkozy amekanusha maelezo hayo yaliyo tolewa na mtoto wa Muammar Gaddafi.

Sunday, March 20, 2011

Mashambulizi nchini Libya ya zidi kupamba moto.

Mashambulizi nchini Libya ya zidi kupamba moto.

Paris, Ufaransa - 20/03/20. Jeshi la Ufaransa kwa kushirikiana na washiriki wake wanaenedelea na mashambulizi kwa kutumia jeshi la anga ilikuzuia jeshi la Muammar Gaddafi.
Mashambulizi hayo ambayo yameshachukua siku mbili yameanza kuchukupicha tofauti baada ya maafa kutokea na kuleta hisia tofauti.
Akiongea kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi alisema " vita vilivyo anzishwa na nchi za Magharibi na washirika wake vitakuwa na maafa makubwa kwa jamii nzima ya kimataifa na itachukua muda mrefu kuliko walivyo dhania."
Mmoja wa mkuu wa jeshi la Amerika Admiral Mike Mullen amesema "mashambulizi nchini Libya hayana maana ya kumtoa madarakani kiongozi wa nchi hiyo."
Wakati huo huo jumuia ya nchi za Kiarabu imelaumu mashambulizi yaliyo fanywa na Ufaransa na washiriki wake, akiongea katibu mkuu wa jumuia hiyo Amr Mussa alisema "majeshi ya Ufaransa na washiriki wake yanafanya kinyume na makubaliano ambayo ni kulizuia jeshi la Libya lisitumie jeshi la anga, lakini sasa mashambulizi yanaelekea kuleta maafa kwa raia."
Mashambulizi nchini Libya yameanza baada ya Umoja wa matifa kupigakura na kukubali kuingilia kati matatizo ya wenyewe kwa wenye kati ya watu wanaomuunga mkono Muammar Gaddafi na ya wapinzani wake.

Monday, March 14, 2011

Saudu na washirki wake wavamia Bahrain.

Saudia na washiriki wake wavamia Bahrain.

Manama, Bahrain - 14/03/2011. Mamia ya wanajeshi na askari wa nchi jumuia Gulfu wameingia nchini Bahrain ilikusaidia serikali ya nchi hiyo.
Uamuzi huo wa jumuia ya nchi za Gulfu ulikuja baada ya serikali ya Bahrain kuomba msaada ili kupambana na waandamanaji ambao wanataka mageuzi ya kisiasa.
Uamuzi huo wa kuvamia Bahrain umelaumiwa na wanasiasa na shirika la kutetea haki za binandamu na kutaka umoja wa matifa uingilie kati.
Japan yakumbwa na tetemeko la ardhi na tsunami.
Tokyo, Japan 14/03/2011. Wanachi wa Japan wapo katika hali mshtuko baada ya tetemeko la ardhi kutokea na kusababisha tsunami.
Tsunami hiyo ilisababisha maafa makubwa na inasadikiwa watu wapatao elfu kumi na tano wamepoteza maisha yao kwa kuzingatia huaribifu uliofanywa na tsunami kuvamia na kuaribu makazi ya watu na kuleta hasara ya zidi ya mabilion ya pesa.
Kufuatia tsunami hiyo ambayo ilisababisha milipuko katika visima vya mitambo ya nyuklia.

Thursday, March 10, 2011

Dalai Lama kuachia madaraka hivi karibuni.

Dalai Lama kuachia madaraka hivi karibuni. Dharamshala,India - 10/03/2011.Kiongozi wa kiimani ambaye ni mzaliwa wa himaya za Tibeti ametangaza atajiudhulu maswala yote ya kisiasa.

Dalai Lama, ambaye amekuwa kiongozi wa wananchi wa Himaya za Tibeti alitangaza habari hizo kwa kusema" nafikili umefika wakati wa kumchagua kiongozi mwingine atakaye waongoza wana Tibeti na umefika wakati wa kutoa nafasi hiyo."
Dalai Lama ambaye anaishi ugenini nchini India baada ya kukumbi kutoka himaya za Tibet baada ya mapinduzi kushindwa zidi ya serikali ya China mnamo miaka ya mwisho ya hamsini.
Ufansa yaitambua serikali ya wapinzani wa Muammar Gaddafi.
Paris, Ufaransa - 10/03/2011. Serikali ya Ufaransa imekuwa nchi ya kwanza kuitambua serikali ya upinzani inayo mpinga kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Akiongea mbele ya ujumbe na viongozi wa upinzani rais wa Ufaransa Nicolas Sozy alisema " tunaelewa umuhimu wa kuwaunga mkono watu wa Libya."
Uamuzi huo wa Ufaansa umekuja baada ya Amerika, na washiriki wake kutaka kuwepo na uzuizi wa anga ili kumdhibiti kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi kutumia anga katika mashambulizi zidi ya wapinzani wa serikali.

Saturday, March 5, 2011

Waganda waombeleza kutokwa na kiongozi wao.

Waganda waombeleza kutokwa na kiongozi wao

Kampala Uganda - 05/03/2011. Aliye kuwa rais wa Uganda kwa muda wa siku tatu amefariki dunia baada ya kuungua kwa muda mfupi.
Walter Ochora Odoch ambaye alikuwa mmoja wa wamajeshi walio ongoza mapinduzi ya kumng'oa madarakani hayati rais wa Uganda Milton Obote.
Akiwa na cheo cha Kanal, Walter Ochora alikuwa kiongozi wa mstari wa mbele kuleta amani katika maeneo ya kaskazini mwa Uganda na hasa aliopo ongozi katika mazungumzo na mpinzani wa serikali ya Uganda Joseph Kony
Marehemu Walter Ochora ameshe wahi kushika nyazifa mbalimbali za serikali enzi za uhai wake.
Jeshi la serikali la Libya kuanza mashambulizi zidi ya wapinzani.
Tripol, Libya - 05/03/2011. Jeshi la serikali ya Libya limeanza mashambulizi zidi ya makundi ya wapinzani ambayo yanapinga serikali.
Mapigano ya kuipinga serikali ya Libya inayo ongozwa na Muammar Gaddafi yalianza mara baada ya kiongozi huyo kukutaa kutoka madarakani.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema " jeshi linalo muunga mkono Muammar Gaddafi limefanikiwa kukamata baadhi ya maaeneo ambayo yalikuwa mikononi mwa makundi ya upinzani.
Chamzo cha kutaka mapinduzi dhizi ya serikali ya Libya yalianzia katika mji wa Benghazi na kuenea sehemu tofauti nchini LIbya.

Monday, February 28, 2011

Brussels, Ubeligiji - Jumuia ya Ulaya imekubaliana kwa pamoja kumwekea vikwazo kiongozi wa Libya kufuatia matukio ya nayo endelea kutokana na maandamano ya kupinga uongozi wa serikali.
Vikwazo hivyo vilivyo pitishwa ni pamoja na ununuzi wa siraha, kuzuiliwa kusafiri, na pesa zote ambazo zilikuwa zimewekwezwa na familia yake.
Serikali ya Misri ya mzuai Hosni Mubaraka na familia yake kusafiri.
Kairo, Misri - 28/02/2011. Serikali ya Misri imezua familia ya rais wa zamani wa Misri kusafiri nje ya nchi kufuatia uchunguzi unaoendelea.
Akiongea mbele ya waandishi wa habari msemaji wa mwanasheria mkuu wa serikali Abel el Saeed alisema " serikali imeamua kumzuia Hosni Mubaraka kutoka nje ya nchi yeye na familia yake kufuatia uchunguzi dhidi ya yake.
Rais Hosni Mubaraka, alitolewa madarakani baada ya wanachi wa Misri kuandamana kumtaka atoke madarakani kutokana na kutoridhishwa na uongozi wake wa miaka 32.
BMW na Citreon kuunangana kibiashara.
Geneva, Uswiss - 28/02/2011. Makampuni ya magari ya BMW na Peugeot Cirtoen yamekubaliana kuungana kibiashara ili kutengeneza aina mpya ya gari itakayo endana na teknolojia mpya.
Akongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa PSA Peugeot Citreon Phillipe Varin alisema " huu ni mwanzo na muungano huu utaiwezesha jumuia ya Ulaya kutengeneza magari ya kisasa ambayo yataendana na teknologiajia mpya."
Utengenezaji wa magari hayo ambayo yatajulikana kama magari ya Hybrid yata leta ajira kwa watu wapatao 400.

Saturday, February 26, 2011

Umoja wa mataifa kuwekea vikwazo serikali ya Libya.

Umoja wa mataifa kuwekea vikwazo serikali ya Libya. New York, Marekani - Kamati ya usalama ya umoja wa Mataifa imekutana ili kujadili muswada wa kuiwekea vikwazo serikali ya Libya.

Uamuzi huo wa umoja wa mataifa umekuja baada ya serikali ya Libya chini ya kiongozi wa nchi hiyo Muammar Gaddafi kutumia nguvu kuvunja maandamano ambayo yanapinga serikali yake.
Kwa mujibu wa habari kutoka katika kamati hiyo ya umoja wa mataifa zinasema " serikali ya Libya inatumia nguvu zake za dola kimyume na kusababisha vifo na maafa katika jamii nzima ya Walibya."
Hali ya kiusalama nchini Libya imebadilika na kuwa uwanja wa vita mara baada ya maandamano ya kumtaka kiongozi wa nchi hiyo Muammar Gaddafi kutika madarakani jambo ambalo kiongozi huyo amekataa.
Picha hapo juu anaonekana kiongoziwa Libya Muammar Gaddafi akiwahutubiwa wananchi kwa mara ya tatu tangu kuanza maandamano ya kumtaka aachie madaraka.
Hali ya kuzuka vita vya wenyewe kwa wenyewe huenda ikatokea.
Abidjani, Ivory Coast-26/02/2011. Milio ya risasi imesikika katikati ya jijila Abidjani na kuwafanya wakazi wake kukimbia kwenye maficho huku katibu mkuu wa umoja wa mataifa akionya kuibuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Mapigano hayo ambayo yalikuwa kati ya kundi la rais wa sasa wa nchi hiyo Laurence Gbagbo na Alassane Ouattara.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zimasema " halisiyo shwali katika jiji hilo."
Hali ya machafuko ilianza mara baada ya uchaguzi mkuu kufanyika na Gbagbo kudai yeye ndiye aliye shinda uchaguzi na huku mpinzani wake Ouattara kudai yeye ndiye mshindi wa uchaguzi huo.
Picha hapo juu ni viongozi wa makundi yanayo pigana nchini Ivory Coast, Watara kushoto na Gbagbo kulia

Thursday, February 24, 2011

Rufaa ya mwanzilishi wa WikiLeaks yakataliwa.

Rufaa ya mwanzilishi wa WikiLeaks yakataliwa.

London, Uingereza - 24/02/2011. Mahakama jijini London imetupilia mbali rufaa ya mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks ambayo inapinga kupelekwa kwake nchini Sweden ili kujibu mashitaka.
Jaji Howard Riddle alisema " tumuma zidi ya mshitakiwa ni za kisheria na zinatakiwa zijibiwe kisheria hivyo inatakiwa mshitakiwa akajibu mashitaka."
Akiongea baada ya hukumu mwanasheria wa mshitakiwa Julian Assange alisema " tutakata rufaa dhizi ya uamuzi huu."
Juliana Assange ambaye amekuwa shubiri katika jamii ya kidipromasia baada ya mtandao wake WikiLeaks kutoa siri za viongozi na mabalozi wanapo kutana kila mara.
Mahakama ya kimataifa ya muhukumu miaka 27 jela mkuu wa zamani wa Polisi wa Serbi.
Hague, Holland 24/02/2011. Mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi za Yugoslavia imemuhukumu aliyekuwa mkuu wa polisi Serb kwa miaka zaidi ya miongo miwili.
Vlastimir Djordjevic alihukumiwa na baada ya mahakama kumkuta na hatia ya kushiriki machafuko na mauaji ya Kosovo Albania.
Akitoa hukumu jaji Kevin Parker alisema " unahukumiwa kifungo cha miaka 27 jela kwa kukutwa na makosa ya kuhusika na mauaji ya watu 724 wa Kosovo Albania na kuleta mgawanyiko wa jamii katika eneo hilo."
Vlastimir Djordjevic alikamatwa mwaka 2007 huko Montenegro maada ya kukimbia na mafichoni kwa muda wa miaka minne.

Tuesday, February 22, 2011

Muhammar Gaddafi asema hatoki madarakani

Muhammar Gaddafi asema hatoki madarakani. Tripol, Libya - 22/02/2011. Rais wa Libya melihutubia taifa la Libya na kusema hataondoka nchi na yupo tayari kufa kwa ajili ya nchi yake.

Kanal Muhammaar Gaddafi alisema, " mimi ni shujaa na mpiganaji kutoka kwenya turubai, nipo tayari kufa na nitapigana hadi mwisho, mimi siyo rais uacha madaraka, mimi ni mpiganaji."
Akiongea kwa hasira aliongezea " wale wote wananifata naawagiza wawakamate watu wote wanlioleta machafuko na wafikishwe kwenyw sheria."
"Nitahakikisha tunasafisha kila nyumba kama wasipo jisalimisha."
"Kama Libya ita yumba itakuwa makao ya Al-Qaeda."
Maandamano siyo kuaribu na siyo waasi wa nchi.
Rais wa Libya aliyasema hayo baada ya Walibya kuandamana kumtaka aachie madaraka na kuruhusu mabadiliko ya kisiasa.
Manoari za Kiiran zapita Suez Kanal kwa mara ya kwanza.
Suez Kanal, Misri - 22/02/2011. Manoari mbili za kijeshi za Iran zimepita kwa mara ya kwanza kwenye mfereji wa Suezi Kanal. Meli hizo zimepita muda wa saa tisa na dakika arobaini na tano kwenye mfereji huo na zinategemewa kurudi mwezi Tatu mwaka 2011.
Meli za Iran zimepita kwenye mfereji huo kwa mara ya kwanza tangu kuanguka kwa serikali ya Hosni Mubaraka.
Kufuatia kupita kwa meli hizo serikali ya serikali ya Izrael imesema " tunatizama kwa uangalifu mwenendo huo wa Iran."
Uongozi wa Suez Kanal uliripoti ya kuwa Meli za Iran zimepita kwenye eneo hilo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1974.
Rais wa Urussi aonya kuhusu mapinduzi katika nchi za Kiarabu.
Moscow, Urussi - 22/02/2011.Rais wa Urusi ameonya ya kuwa mabadiliko ya kisiasa yanatotokea katika nchi za kiarabu yanaweza kuleta athali kubwa.
Rais Dmitry Medveded alisema " siafiki na jinsi viongozi wa nchi za magharibi ambao wamekuwa wana unga mkono mapinduzi ya kisiasa yanayo tokea katika nchi za Kiarabu, kwani yanaweza kuleta machafuko na kugawa nchi hizo ambapo matokeo yake yatakuwa mabaya kwa muda mrefu."
Akiongezaa " Inawezekana nchi hizi zikaja kutawaliwa na viongozi ambao wataleta maafa katika jamii. alisema rais Medved.
Maoni ya rais wa Urussi yamekuja kufuatia machafuko na mabadiliko ya yanayoendelea katika nchi za Kiarabu ambayo yameishitua dunia.