Wednesday, June 1, 2011

Kaptain Sepp Blatter kuongoza Shirikisho la Soka FIFA tena.

Zuriki, Uswizi - 01/06/2011. Wajumbe wa shirikisho la soka duniani FIFA,wamemchagua tena rais wa shirikisho hilo kushikiria kiti hicho kwa kipindi kingine cha miaka minne.
Wajumbe hao waliweza kumchagua Sepp Blatter kwa wingi wa kura zipatazo 186 kati ya kura 203 zilizo pigwa.
Sepp Blatter, ambaye alikuwa mgombea pekee katika kiti hicho, baada ya mpinzani wake Mohamed bin Hammam kujitoa kutokana na kashfa za rushwa.
Hata hivyo, uchaguzi huo ulifanyika baada ya Uingereza kushindwa kuwashawishi nchi wanachama wa shirikisho hilo kupiga kura ya kutaka uchaguzi huo usimamishwe kwa muda, ili achaguliwe mpinzani dhidi ya Sepp Blatter, lakini matokea ya kura hizo yalipinga maombi ya Uingereza kwa 172 kutaka uchaguzi ufanyike na 17 kuunga mkono Uingereza.
Kuchaguliwa kwa Sepp Blatter, kumeaandamana na misukosuko mingi iliyo ikuta shirikosho hilo baada ya kashfa za rushwa kuandama uongozi mzima wa shirikisho hilo FIFA.
Akiongea baada ya matokeo ya uchaguzi, rais huyo wa FIFA Sepp Blatter alisema "Mimi ni kaptain ambaye naongoza jahazi lililo kumbwa na mawimbi na tuta hakikisha shirikisho la soka litakuwa mairi na kulinda heshima ya mchezo huu, kuweka wazi kila jambo na kuhakikisha matatizo yaliyo tokea hayatotokea tena, na nahaidi kwa baraka za Muumba na uzima atakao nipa basi tuta fanikiwa kuhakikisha shirikisho hili lina kuwa swafi na imara."
Mtuhumiwa wa mauaji ya Bosnia Serbi Ratko Mladik awasilishwa Hague kujibu mashitaka.
Hague, Uhollanzi -01/06/2011.Aliyekuwa mkuu wa majeshi wa Bosnia Serbia ambaye anashutumiwa kwa kuhusika na mauaji yaliyo tokea wakati wa vita 1992-95 nchini humo amewasilishwa kwenye mahakama ya kutetea haki za binadamu ili kujibu mashitaka yanayo mkabili.
Ratko Maladik, atafikishwa mahakamani siku ya Ijumaa tayari kuanza kusikiliza kesi yake itakayo endeshwa jaji kutoka Uhollanzi.
Kwa mujibu wa habari kutoka mahamani zinasema "Mladik anakabiliwa kujibu mshitaka yaziyo pungua 11."
Ratko Mladik, alikamatwa baada ya kukumbia mafichano kwa muda usiyo pungua miaka 16 iliyo pita.
Hussein Mubaraka na watoto wake wawili kufikishwa mahakamani.
Kairo, Misri 01/06/2011. Serikali ya Misri imetangaza ya kuwa aliyekuwa rais wa zamani wa nchi hiyo atafikishwa mahakamani yeye na watoto wake kujibu mashitaka ya kusababisha maafa yaliyo tokea wakati wa maandamano ya kutaka ang'olewe madarakani kwa rais huyo.
Kwa mujibu wa habari kutoka serikali zinasema " Hussein Mubaraka na watoto wake wawili wa kiume watafikishwa mahakamani kuanzia tarehe 13, mwezi wa nane."
Habari hizo pia zilisisitiza yakuwa ikiwa "Hussein Mubaraka atakutwa na hatia ya kuhusika na machafuko yaliyo sababisha mauaji wakati wa kutaka atolewe madarakani baada ya kutawala Misri kwa muda wa miaka 30, basi huenda akaukumiwa adhabu ya kifo."
Rais Hussein Mubaraka alitolewa madarakani baada ya maandamano yaliyo chukua siku 18 ya kutaka atoke madarakani.

Tuesday, May 31, 2011

Mshukiwa wa mauaji ya Serbia,Meja Ratko Mladik kupelekwa Uhollanzi.

Mshukiwa wa mauaji ya Serbia, meja Ratko Mladik kupelekwa Uhollanzi.
Belgrade, Serbia - 31/05/2011.Mahakama kuu nchini Serbia imekataaa na kuitupilia mbali rufaa ya mshukiwa na muhusika mkuu wa mauaji ya liyo tokea wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyo tokea miaka ya 1991-95.
Mtuhumiwa huyo Ratko Mladik, ambaye alikuwa mkuu wa majeshi anakabiliwa na mashitaka ya dhidi yake kwa kuhusika na mauaji ambayo yalisababishwa na vita hivyo, wakati yeye akiwa kama mkuu wa majeshi.
Kufuatia kukataliwa rufaa hiyo, mkuu wa majeshi huyo Ratko Mladik, anatarajiwa kupelekwa kwenye mahakama kuu ya kutetea haki za binandamu iliyopo nchini Hollanzi ili kujibu mashitaka yanayo mkabili.
Hata hivyo kabla ya kupelekwa nchini Uhollanzi, Ratko Mladik, aliruhusiwa kutembela kaburi la mwanaye wa kike ambaye alijiua baada ya baba yake kushutumiwa ya kuwa anamehusika katika mauaji.

Monday, May 30, 2011

Rais wa Soka asema hakuna shaka ni matatizo ya muda.

Zurich, Switzaland - 30/05/2011 Rais wa shirikisho la mchezo wa mpira wa miguu duniani FIFA, amekataa ya kuwa shirikisho hilo lipo na mvutano ndani ya uongozi wake.
Sepp Blatter, alisema "shirikisho hilo halina mvutano na matatizo yalito tokea ni kutokana na mlolongo wa shutuma ya kuwa ndani ya shirikisho hilo kuana milungura na rushwa ambazo zimefanyika na matatizo yaho ni ya muda yatatafutiwa uvunbuzi."
Rais huyo wa FIFA anatarajiwa kuwa mgombea pekee wa kiti cha urais baada ya mpinzani wake Mohamed bin Hammam kujitoa kutokana na shutuma hizo za rushwa.
Rais wa Afrika ya Kusini kutafuta suruhisho kati ya Walibya.
Tripol,
Libya 30/05/2011. Rais wa Afrika ya Kusini amewasili nchini Libya kutafuta njia mbadala za kuweza kuleta amni na kusimaisha vita vinavyo endelea kati ya kundi linalo pinga serikali ya Libya na ambalo lina ungwa mkono na serikali za Ulaya Mgharibi.
Kwa mujibu wa habari kutoka ofoce ya rais zinasema, "rais Jokob Zuma atakuwa nchini Libya ili kuongea na kujadiliana na kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi ili kusimamisha mapigano.
hata hivyo kundi la upinzani lenye makao yake makuu Benghazi limesma" inaelekea kuwasili kwa rais wa Afrika ya Kusini kunaleta utata, kwani mpaka sasa hakuna dalili za au amelezo ya kuwa Muammar Gaddafi atatoka madarakani na kuondoka.".
Kuwasili kwa rais wa Afriaka ya Kusini nchi Libya kunatazamiwa kuleta maono tofauti ambayo huenda ya leta mabadiliko katika kampeni nzima ya kidemokrasi nchini Libya

Thursday, May 26, 2011

Viongozi wa nchi za G8 wakutana nchini Ufaransa.

Deauville, Ufransa - 26/05/2011. Viongozi na wakuu wa serikali wa kundi lijulikanalo kama G8 wamekutana nchi Ufaransa ili kujadili hali halisi ya mwenendo wa kiuchumi na kidemokrasia duniani. Wakihutubia nini la kufanya ili kuimarisha uchumi dunia na kuunga mkono mageuzi ya kisiasa duniani, viongozi na wakuu hao wamehaidi kutoa misaada tofauti kwa nchi tofauti kwa kuzingatia hali halisi za nchi hizo na kuhaidi kushirikiana kiuchumi kwa karibu. Vile vile viongozi hao walijadiliana kuhusu machafuko na vita vinavyoendela Libya jambo ambalo linapingwa na baadhi ya viongozi wanao udhuria mkutano huo wa G8 na mageuzi ya nayo endelea katika nchi za Kiarabu.

Hatimaye Ratko Mladic akamatwa.

Belgradi, Serbia- 26/05/2011. Serikali ya Serbia imetangaza kukumatwa kwa aliyekuwa mkuu wa jeshi Bosnia Serbi ambaye anakabiliwa na mashitaka ya mauaji wakati wa vita vilivyo tokea mwaka 1992-95. Generali Ratko Mladic ambaye alikuwa natafutwa ili ajibu amshitaka dhidi yake, alipotea mara baada ya kesi dhidi yake kufunguliwa na mahakama ya kimataifa. Akitangaza kuhusu kukumatwa huko, rais wa Serbia Boris Tadic alisema "kwaniaba ya wanchi wa Serbia napenda kuwatangazia ya kuwa Ratko Mladic amekamatwa, na kuanzia sasa tunafungua kitabu kipya ambacho kitatuwezesha kusamehena na kukubaliana kuishi pamoja." "Na tunahaidi wale wote wafanyao mabaya lazima watajibu mashitaka"alimalizia kwa kusema haya rais wa Serbia Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema "Ratko Mladic hakuwa na matata au kuleta kipingamizi wakati wakukamatwa kwake na inasemekana anamatatizo katika moja ya mkono wake."

Serikali ya Libya kuitaka Uhispania katafuta njia ya luleta amani.

Madrid, Uhispania - 26/05/2011.Serikali ya Uhispania imepokea maombi kutoka serikali ya Libya ya kutaka kuwepo na mazungumzo ya kusimamisha vita vinavyo endelea nchini Libya. Habari kutoka ofosi ya waziri mkuu wa Uhispania, zinasema " tumepokea mswaada kutoka serikali ya Libya ambao unaomba kuwa na mazungumzo ya kuleta amani nchini Libya." Akiongea mbele ya waandishi wa habari, waziri mkuu wa Libya Al-Baghdadi al Mahmoud "alisema serikali ya ke ingependelea kuanza mazungumzo ya kuleta amani na kusimamisha mashambulizi nchini Libya yanayofanywa na NATO." "Na Muammar Gaddafi bado na atakuwa kiongozi wa LIbya, na kama Gaddafi akiondolewa kwa kutumia nguvu, basi hakutakuwepo na Libya watu wanayo tarajia." Hata hivyo, kundi la upinzani linalo pinga serikali ya Gaddafi, linadai lazima kiongozi huo ataoke madarakani na ndipo amani ipataikane.

Wednesday, May 25, 2011

Obama na Cameron kupambana na Gaddafi hadi mwisho.

Obama na Cameron kupambana na Gaddafi hadi mwisho.
London, Uingereza - 25/05/2011. Waziri mkuu wa Uingereza na rais wa Amerika wakubaliana kwa pamoja yakuwa wataendelea kusisitiza kwa kila hali ili kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi kutoka madarakani.
Wakiongea pamoja, wakati walipo wakiongea na waandishi wa habari, rais wa AAmerika Baraka Obama na David Cameron, walisema, tunaamini zipo nguvu za kutosha za kuhakisha Muammar Gaddafi anaachia madaraka.
Wakati huo huo serikali ya Afrika ya kusini, imesema inafanya mmpango wa kutaka kuleta amani nchi Libya na kuandaa njia ya kutoka madarakani kwa kiongozi wa nchi hiyo Muammar Gaddafi.
Rais Baraka Obama yupo ziarani katika nchi za Ulaya kwa muda wa siku sita.
Kwa mujibu habari kutoka serikali ya Afrika ya Kusini, zinasema, rais wa Jacob Zuma atatembelea Libya ili kutafuta suruhisho katika nchi hivyo ambao, imekuwa na mapigano kati ya serikali ya Libya na wale wanaoipinga.
Libya imekuwa ikishambuliwa na ndege za majeshi ya NATO, ili kupunguza mashambulizi yanayofanywa na serikali ya Gaddafi zidi ya wapinzani wanaopinga serikali.
Serikali ya India kuimarisha uhusiano na bara la Afrika.
Adis Abeba
, Ethiopia - 25/05/2011. Waziri mkuu wa India amehaidi yakuwa serikali yake itakuwa karibu na Afrika, ili kusaidia kujenga uchumi wa bara zima.
Akiwahutubia katika mkutano ulio wakutanisha viongozi wa Afrika na India, waziri mkuu Manmohan Singh alisema, " kuna mafanikio ya kiuchumi ambayo yanaendelea barakani Afrika, na India itashirikiana kikamilifu na bara la Afrika, kwa kuzingatia India na Afrika kunauhusiano mkubwa kihistoria.
Serikali ya India, imekuwa mbioni kuimarisha uhusiano wake na bara la Afrika kwa kuwekeza zaidi ya $5billion, na hii inaonekana ni katika kukabiliana na mataifa kama China, na Umoja wa nchi za Ulaya ambazo zimekuwa zijaribu kushirikiana na serikali za Afrika.

Tuesday, May 17, 2011

Luis Moreno Ocampo ataka Muammar Gaddafi afikishwe mahakamani.

Den Haag, Uhollanzi , 16/05. 2011. Wakili wa mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi zidi ya kukiukwa haki za binadamu, amewaomba majaji wa mahakama hiyo watoe rukhsa ya kukumatwa kwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi, mtoto wake wa pili Saif al Islam na mkuu wa usalama wa taifa Abdullah Senussi. Luis Moreno Ocampo, aliyasema haya mbele ya waandishi wa habari, kwa kusema " upo ushaidi wa kutosha ya kuwa haki za binadamu zimekiukwa na serikali ya kiongozi huyo tangu kuanza kwa mvumo wa kutaka aaondoke madarakani." Akiwakilisha na kuonyesha kurasa zipatazo 74 ambazo ameziwakilisha katika mahakama jijini Den haag (Hague), na zimeelezea ushaidi wa kutosha wa kukiukwa kwa haki za binadamu nchi libya na uongozi wa Muammar Gaddafi. Muamar Gaddafi ambaye ametawala Libya zaidi ya miaka 40, amekumbwa na wimbi lililotokea kwemye maoenao ya Afrika ya Kaskazini baada wanachi kutaka demokrasi na mageuzi ya kisiasa. Mkurugenzi mkuu wa IMF akataliwa dhamana na mahakama. New York, Marekani - 16/05/2011. Halimu wa mahakama jijini New York amemkatalia kumpa dhamana mkurungenzi mkuu wa shirika la fedha duniani (IMF) Internaltional Monetary Fund. Mkurugenzi hyo kwa IFM, Dominik Strauss-Kahn, amekataliwa dhamana hiyo na jaji kwa madai huenda akaondoka nchini humo kwa kutumia ndege. Dominik Strauss anakabiliwa na shitaka la kutaka kumbaka mmoja wa mfanyakazi wa hotel aliyo kuwa amelala na anatarajiwa kurudi mahakamani Mei 20.

Sunday, May 15, 2011

Serikali ya Amerika kuchunguza shirika la ulinzi la raia wa Amerika. Abudhabi, UAE - 15/02/2011. Serikali ya Amerika imeanza uchunguzi zidi ya mwanzilishi wa shikika la ulinzi lililo julikana kama Blackwater na sasa kama Xe, baada ya ya habari kuenea yakuwa amekodishwa ilikutoa ushauri wa kiulinzi na kuunda majeshi katika nchi tofauti. Erick Prince, ambaye ndiye mwanzilishi wa shirika la ulinzi la Blackwater, anesemekana amtiliana sahii mkataba na nchi za Kolombia na nchi nyingine ili kampuni yake ijulikanayo kwa sasa Xe kusaidia kupambana na wale wote wanaopinga serikali hizo. Kwa mujibu habari kutoka serikali ya Amerika zinasema " inaangalia sheria ipi iliyo vyunjwa kwa raia wa Amerika kutoa mafunzo ya kijeshi nje ya Amerika." Vile vile kunahabri nyingine ambazo zinasema "shirika hilo aliwaajili watu wenye imani ya Kiislaam kwa kuofia ya kuwa watu waimani hiyo hawatakuwa tayari kushambuliana waislaam wenzao." Shirika hilo ambalo limekuwa linato ajira kwa walinzi na wapiganaji walio acha kazi za kijeshi na ulinzi lili wahi kukumbwa na kashfa ya kuuhusika katika mauaji yaliyo tokea nchi Irak mwaka 2007.

Mkurugenzi wa IMF akabiliwa na shitaka la ubakaji.

Umoja wa mataifa waagiza kutotupa vyakula ovyo. Hong Kong, China - 15/05/2011. Shirika la umoja wa mataifa linalo shughulikia maswala ya kilimo na chakula duniani limeagiza tabia ya kutupoteza au kuharibu vyakula usimamishwe mara moja. Kwa mijibu wa shirika hilo limesema, "nchi tajiri na watu matajiri ndiyo huwa wanatupa au kuharibu vyakula kwa wingi kuliko wale watu masikini na nchi masikini." Kwa kuongea habari hizo zimesisitiza zaidi ya asilimia thelathini, huwa kuharibiwa karibu kila mwaka duniani kutokana na kutokuwa makini. Mkurugenzi wa IMF akabiliwa na shitaka la ubakaji. New York, Amerika - 15/05/2011. Mkurugenzi mkuu wa shirika la kimataifa la kutathmini maswala ya fedha namisaada ya kifedha -Internaltional Monetary Fund(IFM) amefunguliwa mashitaka. Dominik Strauss Kahn, alikamatwa na polisi baada ya muhudumu mmoja katika hotel aliyo kuwa amefikia kudai yakuwa alisumbiliwa kijinsia na mkurugenzi huyo. Msemaji wa polisi, Ryan Sesa alisema, Dominik Strauss Kahn, amekamatwa na polisi wakati akiwa njiano kuelekea uwanja wandege. Hata hivyo mwansheria wa Dominik Strauss, amesema "mteja wake atakana shitaka hilo." Domink Strauss, ambaye inasemekana alikuwa mmoja ya wale viongozi waliokuwa wamepanga kugombe akiti cha urais wa Ufaransa mwaka 2012 ili kuchuana na rais wa sasa. Marekani ya sema Walibya ndiyo wataamua uongozo wao Washington, Marekani - 15/05/2011. Viongozi wa serikali ya upinzani wa Libya wameondoka kwa shingo upande baada ya selikali ya Amerika kushindwa kuikubali kimsaada wa hali na mali. Kwa mujibu wa habari kutoka ikulu ya Marekani zinasema, "serikali ya Amerika haiwezi kuitambua au kuuutambua uongozi huo, kwani uamuzi huo upo mikononi mwa wanachi wa Libya kuwachagua viongozi wao." Hata hivyo serikali ya Amerika, imesisitiza msimamo wake wake wakuunga mkono wanchi wa Libya katika harakati za kuleta mabadiliko ya kisiasa na demeokrasia. Wakati huo huo wataalamu wa mabo ya kisiasa, kidiplomasia na uchumi, wanasema "vita vinavyo endelea nchini Libya, vinasababishwa na nchi zenye hisa nchini humo, nahasa nia kubwa ni kuhakikisha Urussi na China zisitawale maeneo hayo kiuchumi."

Sunday, May 1, 2011

Papa John Paul afanywa kuwa mteule.

Vatican City,Vatican - 01/05/2011. Kanisa Katoliki limetangaza rasmi yakuwa aliye kuwa Papa John Paul wa Pili amekuwa mteule rasmi. Kufanywa huko kuwa mteule kumekuja baada ya ushahidi kutolewa ya kuwa alikuwa ni mtu wa aina ya pekee. Mmoja ya watu waliotoa ushahidi huo, ni sista wa Marie Simon Pierre ambaye alisema yakuwa "alitibiwa na Papa John Paul kupitia maombi." Sherehe hiyo iliudhuliwa na viongozi wa serikali na wakidini akiwemo rais wa Zimbabwe Robert Mugabe na mkewe.

Mashambulizi ya jeshi la NATO laua mtoto wa Gaddafi.

Tripol, Libya- 01/05/2011. Ndege za jeshi la NATO zimeshambulia makazi ya rais wa Libya na maisha ya watu waliokuwepo katika jengo hilo. Kwa mujibu wa msemaji wa serikali Moussa Ibrahim, amesema " Mashambulizi yaliyo fanywa na NATO yameuwa mtot wa mwisho wa kiume Saif al Arab Gaddafi wa Kanali Muammar Gaddafi na wajukuu zake watatu." "Kijana aliye uwawa alikuwa anasoma nchini Ujerumani na hakuwa anahusika na mambo ya kisiasa na hii inaonyesha yakuwa NATO na washiriki wake wanataka kumwua kiongozi wetu. Lakini hata hivyo Koingozi Kanali Muammar Gaddafi yeye na mke wake ni wazima." Mashambulizi dhidi ya serikali ya Libya yalinza li kusinikisha kiongozi wa nchi hiyo kuacha kuwashambulia raia wa Bhengazi na kuachia madaraka ambayo amekuwa akiyashikiria zaidi ya miaka arobaini.

Friday, April 29, 2011

William na Catherine wafunga pingu za maisha.

Mamia washuhudia William na Catherine walipokuwa wana wafunga pingu za maisha.
London, Uingereza 29/04/2011. Mamia ya wakazi wa jiji la London na dunia nzima wameshuhudia mjuukuu wa malkia Elizabeth, William akifunga ndoa na mchumba wake Catherine.
Harusi hiyo iliyo fungwa kanisani, na kuhudhuliwa na Malkia na familia yake, wazazi wa bibi harusi na familia yao, viongozi wa dini ,serikali na wageni wengine waalikwa.
Harusi hii ilitangazwa katika runinga kwenye nchi zaidi ya 108 dunia.
Bwana na bibi harusi William na Catherine wakipeana kisss, kuchuuum mbele za mamia kuashiria ya kuwa wao niwapendanao.
Bwana na bibi harusi William na Catherine wakionekana kwa mara ya kwanza mbele za mamia kama mke na mume mbele ya baraza katika makazi yao.
Mania walikuwepo kushuhudia kuchumooo kisss wa kukata na shoka.
Ishara ya yote kukamilika, bwana na bibi harusi walivalishana pete ikiwa ni haadi ya kuwa wamekuwa kama mke na mume
Picha hapo juu wanaonekana bwana hariusi William na bibi harusi Catherine wakiwa katika mkokoteni wa asili ambao unavyutwa na farasi njiani kueekea nyumbani kwa mapumziko , huku bwana harusi akikitoa tabasamukisi, baada ya kukabidhiwa mke wake na wazazi wa binti.
Hapa wanaonekana bwana harusi William na bi harusi Catherine wakila kiapo kwa pamoja mbele ya kasisi.
Baada ya harusi, bwana na bibi harusi wanatoka kanisani wakiwa kama mume na mke, na huku wakiwa wanatizamana kwa tabasamu la mahaba.
Picha hapo juu wanaonekana mke na mume wakiangaliana kwa furaha baada ya kumaliza kuimba nyimbo ya kumshukuru Mungu. hapa inaelekea Willy akimwambia mkewe, kumbe unajua kuimba hata nyimbo za dini.
Picha hapo juu anaonekana, William akimvalisha pete mke wake Catherine mbele ya kasisi, huku mkewe akitabasamu kwa furaha.
Picha hapo juu, baba wa Catherine, Middleton akimwakilisha mwanae mbele ya Kasisi tayari kula kiapo kumtwaa William kama mme wake, na huku kulia kwao mume wake Willy na mdogo wake Hurry wakimakini tayari kusikia habari njema toka kwa Catherine.
Picha hapo juu, wanaonekana bibi Malkia Elizabeth na kulia babu Philips wakiwa wamekaa tayari kungojea mjukuu wao kula kiapo mbele ya Mungu na kasisi ya kuwa anamchukua Catherine kama mke wake. mmm sasa mme wangu Willy anachukuliwa hivi hivi namwona , yaaa na mimi napata mke mwingine , hapo inaelekea bibi na babu wakiwa wanawaza.
Picha hapo juu anaonekana Catherine akielekea kuingia kanisani tayari kula kiapo cha kumpenda mume wake Willy.
Picha, hapa inaonekana mdogo wa Willy, Hurry akimwambia kaka yeke sasa unakwenda kuwa mme wa mtu, na kaka yake Willy akisema yaaa naenda kuanza maisha mapya mdogo wangu, hata hivyo wewe ni mgodo wangu na ndugu yangu milele.

Monday, April 25, 2011

Taliban wavunja jela na kutoroka.

Gaidi akamatwa nchi Venezuela.
Caracas, Venezuela - 25/04/2011. Maafisa wa usalama serikali ya Venezuela wamemkamata gaidi ambaye ameshukiwa kutaka kuhusika na kitendo cha kigaidi.
Kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya Venezuela zinasema "gaidi huyo Joaquin Perez Becerra alikamatwa siku jumamosi baada serikali ya Kolombia kuwasiliana na serikali ya kuwa gidi huyo atapitia nchini"
Kukamatwa huko kwa Perez kuna kumekuja baada ya Interpol kutoa hati ya kukumatwa kwake wakati akitokea nchini German.
Huusiano wa serikali ya Venezuela na Kolombia umekuja baaada ya nchi hizo kukubaliana kushirikiana kiusalama baada ya rais mpya wa Kolombia Juan Manuel Santos kukutana na rais wa Venezuela Hugo Chavez na kuongea kumaliza uhasama kati ya nchi hizo mbili.
Taliban wavunja jela na kutoroka.
Kandahar, Afghanistan 25/04/2011. Zaidi ya wafungwa mianne wametoroka kutoka katika jela moja ambayo wengi wa wafungwa hao walikuwa wapiganaji wa kundi la Taliban.
Wafungwa hao ambao wametoroka kupitia shimo walio lichimba kwa urefu chini ya ardhi hadi kutoke nje gereza bila watu wausalama kutambua.
Msemaji wa Zabuillah Mujahed alisema " shimo hilo lilichimbwa kwa muda wa miezi mitano na walichukua masaa manne na nusu kutoka ndani ya jela hiyo.
NATO, alitibitisha habari hizi kwa kusema " tuna habari ya kuwa wametoraka kupitia shimo ambalo walilichimba kwa umbali wa zaidi ya mita 320.
Naye msemaji wa serikali ya Afghanistan, Waheed Omer kutoroka kwa wafungwa hao siyo picha nzuri kwa serikali , na tutahakikisha tunawakama wote waliotoroka."
Hii itakuwa ni mara ya pili wa wafungwa kutoka toka jela, baaada ya tukio kama hili mwaka 2008 ambapo wafungwa wapatao 1,000 walitoroka.
Makazi ya Muammar Gaddafi yashambuliwa.
Tripoli, Libya 25/04/2011.Ndege za jeshi la NATO limeshambulia makazi ya rais wa Libya ambaye majeshi yake yanapambana na majeshi ya upinzani yanayo ungwa mkono na Ufaransa, Uingereza na jumuia ya NATO.
Msemaji wa serikali Mussa Ibrahim amesema " ndege za jeshi la NATO lilishambulia makazi hayo kwa nia ya kutaka kumua rais wa sasa Muammar Gaddafi, ambaye nchi wanachama wa NATO zinataka atoke madaraka kwa kutumia nguvu za kijeshi jambo ambalo linaonyesha nini nia ya NATO."
Katika mashambulizi hayo, baadhi ya raia na wanajeshi waliokuwepo kwenye eneo hilo wanjeruhiwa vibaya na kuharibu kwa kiasi kikubwa majengo ya eneo hilo lililopo Ba el Azizia.

Friday, April 22, 2011

Ndege aina ya Drone kuanza kutumika nchini Libya.

Umoja wa Afrika waondolea vikwazo Ivory Coast.
Adis Abeba, Ethiopia -22/04/2011. Umoja wa Afrika umeondoa vikwazo amba
yo vilikuwa vimewekwa zidi ya nchi ya Ivory Coast.
Akiongea kuondolewa kwa vikwazo hivyo, mwenyekiti wa kamati ya amani ya Umoja wa Afrika alisema " tunapenda serikali iliyo chukua madaraka ihakikishe yakuwa ina imarisha usalama, haki na amani kwa watu wote katika misingi ya kidemokrasia na kuanzisha mpango mzima wa watu kusameheana."
Uamuzi huo umekuja baada ya aliye kuwa rais wa nchi hiyo Laurent Gbagbo, kutolewa madarakani kwa nguvu na jeshi la Alassane Ouattara kwa kusaidiwa na jeshi la Ufaransa.
Wapinzani hao katika kiti kugombea kiti cha urais Laurent Gbagbo na Alassane Ouattara walianza kuvutana kisiasa baada ya matokeo ya uchaguzi kutolewa n a huku kila mmoja kudai ndiye aliye ibuka mshindi.
Ndege aina ya Drone kuanza kutumiwa nchi Libya.
Benghazi, Libya 22/04/2011. Aliyekuwa mgombea wa kiti cha urais na ambaye pia ni mbuge wa chama cha Republikan cha Amerika amewasili nchini Libya.
John McCain, amewasili nchini Libya ili kuongea na viongozi wa upinzani ambao wanapingana na serikali ya Libya inayo ongozwa na Kanali Muammar Gaddafi.
Akijibu swali nini nia ya madhumuni ya ziara yake nchini humo, McCain alisema " nimekuja ili kuangalia hali halisi kutokana na matukio yanayo endelea."
Kuwasili huko kwa McCain kumekuja baada ya rais wa Amerika Baraka Obama kuruhusu matumizi ya ndege Drones ambazo zinatumia nguvu za mtandao katika kufanya mashambulizi zitumike katika vita zidi ya serikali ya Libya.

Sunday, April 17, 2011

Serikali ya Kuba kufanya mabadiliko ya kisiasa.

Serikali ya Kuba kufanya mabadiliko ya kisiasa. Havana, Cuba -17/04/2011. Rais wa Kuba ametangaza mabadiliko ya kisiasa ambayo yatakayo fanyika nchini humo.

Rais wa Kuba Raul Castro akiwahutubia viongozi na wanachama tawala wapatao 1000 katika mkutano mkuu wa chama tawala alisema "tumefikia wakati wa kukubaliana na hali halisi ya mabadiliko ya kisiasa , kwa minajili hiyo tumekubaliana ya kuwa kiongozi wa nchi atakuwa anakaa madarakani kwa kipindi cha miaka hadi kumi tu.
rais Raul Castro alimekuwa mtawala wa nchi hiyo tangu alipo achiwa madaraka na kaka yake Fidel Castro
Iran yazindua gari mpya ya kifahari.
Tehran, Iran 17/04/2011.Serikali ya Iran imetangaza yakuwa inampango wa kujenga meli kebu ambayo itatumika katika kukagua na kulinda mipaka yake katika pwani ya kusini mwa nchi hiyo.
Mkuu wa jeshi la Iran, Admiral Amir Farhadi, alisema "meli kebu hiyo ambayo itakuwa na uzito wa tani 500 na itakuwa tayari kuanza kazi mwaka 2012 Julai."
Irani imekuwa ikipiga hatua za kisayansi na teknolojia na kuwa nauwezo wa kutengeneza mitambo na siraha za kijeshi.
Wakati huo huo kampuni ya kutengeneza magari ya Iran, imezindua gari mpya ya aina ya Dena ambayo inatarajiwa kuwa katika barabara hivi karibui, na wanunuzi wa magari kutoka Iran,nchi za Rusia,Syria, Turkey, iraq,Ukraine na Misri, wataaanza kuyatumia magari mwaka 2011.

Friday, April 15, 2011

Obama,Sarkoz na Kameron tutahakikisha Gaddafi anang'oka.

Obama, Sarkoz na Kameron tutahakikisha Gaddafi anang'oka.

London, Uingereza 15/04/2011. Viongozi wa Uingereza, Ufaransa na Amerika wamekubaliana kwa pamoja kuundeleza mapambano dhidi ya kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Nikolas Sarkozi rais wa Ufaransa, waziri mkuu wa Uingereza David Kameon na rais wa Amerika Baraka Obama, kwa pamoja wamekubaliana kuhakikisha kiongozi wa Muammar Gaddafi anatoka madarakani.
Viongozi hao walitoa waraka wao wa pamoja na kusisitiza "sheria ya muswada ya kamati ya usalama ya umoja wa mataifa ya 1973, inataka jumuia ya kimataifa kulinda usalama wa raia na razima waitekeleze."
Waraka huo uliongezea " NATO na washiriki wake wataendelea na jukumu lao la kulinda raia na kuhakikisha Kanali Muammar Gaddafi anatoka na kuwapa uhuru wa na nchi wa Libya kujitawala wenyewe.
Hata hivyo baada ya waraka huo kutoka, kiongozi wa Libya alionoekana katika mitaa ya Tripoli akiwaslimia wanchi na wadau wanao muunga mkono, na huku mwanae wa kike Aisha Gaddafi aliwahutubia watu waliokuja Bab al Azizyah kuadhimisha miaka 25 tangu Amerika ilipo vamia Libya na kusema baba yake hataachia madaraka kwa kulazimishwa wala vitisho vya nchi za Magharibi na washirika wake.

Wednesday, April 13, 2011

Viongozi wakutana Katar kutathmin hali ya Walibya.

Nchi zinazo ongoza kukua kwa uchumi dunia zakutana nchini China. Hainan, China 13/04/2011. Viongozi wa serikali na mabenk wamekutana nchi China ili kuangalia kiundani njia bora ya kuimarisha sekta ya bishara ya kifedha na uchumi.

Li Wuwei, makamu wa mwenyekiti na mshauri wa mambo ya kisiasa alisema, " nchi wanachama zimejitahidi na kushirikiana katika kuinua hali ya kiuchumi baada ya ya myumbo wa kiuchumi kutokea na zitaendele kufanya hivyo hasa katia nchi zinazohitaji kuinuka kiuchumi ili ziweze kukidhi mahitaji ya jamii zao."
Mkutano huo unaojulikana kama BRICS unajumuisha nchi za Brazil, Urussi, China na Afrika ya kusini nchi ambazo zinaongoza katika kukua kwa uchumi kwa haraka zaidi.
Rais wa zamani wa Misri na watoto wake wawekwa chini ya ulinzi wa polisi.
Kairo, Misri 13/04/2011. Rais wa zamani wa Misri amewekwa kizuizini pamoja ya watoto wake wawili wa kiume, ilikuwezesha uchunguzi zidi ya kesi inayo wakabili ya rushwa na unyanyasaji.
Kwa mujibi wa wakili wa serikali alisema " Hosni Mubaraka na watoto zake Gamal na Alaa watakuwa kuzuizini kwa muda wa siku15 wakati uchunguzi unaendelea zidi yao."
Hosni Mubaraka 82, ambaye ametawala Misri kwa miaka zaidi ya miongo mitatu alitolewa madarakani na maandamano ya watu waliotaka aachie madaraka mapema mwanzoni mwa mwaka huu..
Habaria zinasema rais Hosni Mubaraka anamatatizo ya moyo na hivi sasa yupo hspitali amelazwa kwa uchunguzi zaidi wakati watoto wake wako chini ya ulinzi wa polisi.
Viongozi wakutana Katar kutathmini hali ya Walibya.
Doha,Katar - 13/04/2011. Viongozi wa kundi la upinzani linalo pingana na serikali ya Libya wamekutana na viongoziwa nchi tofauti nchi Katar ili kujadili hali halisi ya mapambano yanayo endelea ili kung'oa madarakani kiongozi wa Libya MuammarGaddafi.
Akiongea mbele ya viongozi walioudhuria mkutano huo waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza William Hague amesema, "nilazima tuhakikishe tunafanya kila njia ili tunasaidia kundi la upinzani ili kuliwezesha kuimarisha demokrasi nakuhakikisha Muammara Gaddafi anakubaliana na matwakwa ya wanchi wa Libya."
Msemaji wa kundi la upinzani linalo mpinga serikaliya Mahmud Shamman alisema, " tungependa tutambulike kama wawakilishi wa serikali mpya ya Libya ambao tupo kwa ajili ya kuijenga Libya kwa kila Mlibya."
Mkutano wa huu umefanyika ili kuangalia ni kwa kiasigani jumuiya ya kimataifa itaweza kuisaidia Libya.

Monday, April 11, 2011

Jeshi la Alassane Ouattara la mkamata Laurent Gbagbo.

Jeshi la Alassane Ouattara la mkamata Laurent Gbagbo. Abidjan, Ivory Coast -11/04/2011.Jeshi la upinzani linalo ongozwa na Alassane Ouattara, kwa kushirikiana na jeshi la Ufaransa limefanikiwa kumkamata aliyekuwa rais wa Ivory Coast baada ya kuvamia makazi yake.

Rais huyo wa Ivory Coast Laurent Gbagbo,alikamatwa baada ya mashambulizi kati ja jeshi lake na jeshi la Ouattara kwa msaada wa Ufaransa na vifaru huku helkopta zikisaidia kuhakisha ya kuwa Gbagbo na jeshi lake hawawezi kuendeleza mashambulizi.
Msemaji wa Alassane Ouattara, Affaoussy Bamba alisema, " Laurent Gbagbo amekamatwa na sasa yupo mokononi mwa jeshi letu.
Hata hivyo , msemaji wa Laurent GbagboToussaint Alain , alisema jeshi la Ufaransa limemkamata Gbagbo baada ya kuvamia makazi yake.
Kufuatia madai hayo, waziri wa ulinzi wa Ufaransa alikanusha madai hayo na kusema ,"Gbagbo alikamatwa na jeshi la Alassane Ouattara."
Kukamatwa huko kwa Laurent Gbagbo, kumekuja baada ya rais huyo kudai yakuwa yeye ndiye mshindi wa matokeo ya uchaguzi, na huku mpinzani wake Alassane Ouattara akidai yeye pia ameshinda uchaguzi na umoja wa mataifa kuunga mkono.
Kundi la upinzani la kataa mpango wa kuleta amani nchini Libya.
Benghazi, Libya - 11/04/2011. Kundi la upinzani linalopigana na serikali ya Libya limepinga mpango uliopitishwa na umoja wa Africa ili kusimamisha mapigano.
Msemaji wa kundo hilo lili na makao yake makuu Benghazi, Mustafa Jabiri alisema " hatuwezi kushirikiana na uongozi wa Muammar Gaddafi, na lazima uachie madaraka yeye na familia zao, na tutakufa nao au tuchukue ushindi kwa mtutu wa bunduki."
Uamuzi wa kundi hilo kukataa mpango wa umoja wa Africa ili kuleta amani kati ya serikali ya Libya na wapinzani wake ulikuja baada ya viongozi wa jumuia hiyo chini ya rais wa Afrika ya Kusini Jacob Zuma kukutana na Muammar Gaddafi ili kujadili mpango wa kuleta amani.