Sunday, May 11, 2008

Morgan Tsvangarai kupigania kiti cha urais tena,"Hii ni kwaajili ya watu wa Zimbabwe"Tsvangarai.

Harare,Zimbabwe - Kiongozi mpinzani wa chama MDC nchini Zimbabwe, kinacho ongozwa na bwana Morgan Tsvangarai, kimetangaza ya kuwa kitashiriki katika uchaguzi mwingine wa kuchagua rais atakaye ongoza Zimbabwe katika kipindi cha miaka mitano itakayo fuata.
Akiongea na waandishi wa habari mjini Pretoria, bwana, Morgan Tsvangarai, alisema yakuwa
marudio ya uchaguzi huu ni kwa ajili ya wananchi, wananchi walisha zungumza kutumia kura zao na sasa watasema tena kutumia kura zao.
Hata hivyo alipo ulizwa kuhusu ,mpatanishi wa sakata hilo la kisiasa nchi Zimbabwe, ambaye ni rais wa Afrika ya Kusini bwana Thabo Mbeki,bwana Tsvangarai, alisema ya kuwa hana imani na mpatanishi huyo ,a kuiomba jumuia ya kimataifa iliangalie kwa undani swala hilo.
Picha ya hapo ju, anaonekana bwana Morgan Tsvangari akiongea na waandishi wa habari mjini Pretoria siki ya jumamosi
Picha nyingine ni picha ya marais wa Zimbabwe bwana Robert Mugabe Kulia, na bwana Thabo Mbeki alipokutani siku ya ijumaa kwa ajili ya mazunfumzo.

Friday, May 9, 2008

Taifa teule latimiza miaka 60 tangu kuundwa, na wakati huo huo waziri mkuu kiti moto.

Barc'a wasema sasa basi kwa Frank Rijkaard, wataka bahati mpya, "Rais wa timu".

Barcelona, Uispania - Kocha maili wa mchezo wa soka Frank Rijkaard, ameachishwa kazi ya ukocha na timu yake ya FC Barcelona.
Rijkaard, ambaye alikuwa kucha wa timu hii ya FC Barcelona tangu mwaka 2003, nakuweza kurudisha jina la timu ya Barcelona duniani, kwa kuchuku ubingwa wa mashindano ya ligi ya Uispania (La Liga) na timu ya FC barcelona Kuwa bingwa wa mashindano ya vilabu vya Ulaya mwaka 2006.
Akisema haya, rais wa timu ya Barcelona , bwana Joan Laporta, alisema ya kuwa Rijkaard, ameiletea sifa timu yetu, lakini matokeo ya mwaka huu haya kuridhisha, hivyo uongozi wa FC Barcelona, unamshukuru sana na niwakati wake wakwenda kupumzika, tumpe nafasi kocha mwingine.
Kocha aliye teuliwa kuiongoza FC Barcelona ni aliye kua timu kaptain wa zamani wa timu hiyo,Pep Guardiola.
Frank Rijkaard alikuwa na mkataba wa kuwa kocha wa timu ya FC Barcelona hadi 2009.
Picha hapo juu anaonekan Frank akiwa anafanya mavitus enzi zake alipo kuwa akichezea timu ya AC Milan ya Itali.
Picha nyingine anaonekana Rijkaard, akiwa ana mpoza mchezaji nyota wa dunia Ronadinho, baada ya hali kuwa mbaya wakati walipo cheza moja ya mechi zao na kushindwa kushinda.
Frnk Rijkaard, anaonekana akitoka uwanjani kwa hasira baada ya timu ya kuendelea kutofanya vizuri katika moja ya mashindano ya la liga.
Hapo chini ni picha ya mwisho anaonekana, Rijkaard akiwa anajaribu kumyang'anya mpira Denis Bergkamp, wakati wa mchezo walipo cheza pamoja kwa ajili ya kuchangisha fedha.
Taifa teule latimiza miaka 60 tangu kuundwa, na wakati huo huo waziri mkuu kiti moto.
Tel Aviv. Israel - Wananchi wa Israel, wameadhimisha hivi karibuni miaka 60 tangu kuanzishwa kwa taifa la Kiisrael.
Kuanzishwa kwataifa la Kiizrael 1948, kulitokea baada ya Umoja wa Mataifa, kupiga kura mnamo mwaka 1947/29/11, li kuundwa taifa la hili, na matokeo ya kura ni kwamba kura zili pita kwa 33 kwa 13 na 10 hazikupigwa. Nakutokana na kura hii . ndipo kulipitishwa hazimio la kuanzishwa taifa la Waisrael,ambao kwa miaka mingi walikutwa na matatizo mbali mbali, na hasa lile la mauaji ya kutisha yaliyo tolea nchini, Ujerumani, Austria na Polandi,ambapo zaidi ya Waizrael millioni 6, waliuwawa, wakati wa utawala wa Aldoph Hitler, ambaye alikuwa kiongozi wa Ujerumani wakati huo.
Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Izrael, bwana Ehud Olmet, akisalimiana na watu walio kuja kusherekea siku ya kuanzishwa kwa taifa la Izrael mjini Jerusalem.
Picha ya pili wanaonekana, rais wa Israel bwana, Shimon Perez na waziri mkuu wa Izrael, bwana Ehud Olmet wakiingi kwenye ukumbi tayari kusherekea miaka 60 ya taifa la Izrael.
Picha ya mwisho anaonekana waziri mkuu wa Izrael, bwana Ehud Olmet. akiongea na waamdi shi wa habari, kujibu kashfa inayo mkabili yakupokea pesa kinyume cha sheria kutoka kwa mfanya biashara mmoja, ili aweze kushinda na kuwa waziri mkuu. Hataa hivyo waziri mkuu bwana Ehud Olmet, alikanusha madai haya na kudai hakufanya makosa, ijapo kuwa, kuwan wito unatolewa wa kudai ajiudhulu toka madarakani.
Pesa na mali zilizo potea kwa ubadhilifu zapatikana" Serikali ya Zambia".
Lusaka, Zambia - Serikali ya Zambia imesema ya kuwa , imezipata baadhi ya fedha na mali zenye thamani yaUs Dolla , $ 60 million za aliye kuwa rais wa zamani wa Zambia, bwana Fredrick Chiluba.
Akisema hayo, waziri wa habari wa Zambia, bwana Mike Mulongoti, baadhi ya vitu vilivyo taifishwa ni nyumba ya bwana Chiluba iliyopo nchini Ubeligiji, ambayo itauzwa na fedha zake zitatumiwa kuwasaidia wanachi kukarabati hospitali,na zahanati.
Bwana Chiluba, anakabiliwa na kesi ya kutumia vibaya fedha za umma na ubadhilifu (rushwa), wakati alipo kuwa madarakani kama rais wa Zambi.
Picha hapo juu anaonekana bwana Fredrick Chiluba,akiwa mahakamani kwa mara ya kwanza kusikiliza kesi yake ya ubadhilifu wa mali ya umma.
Picha ya chini anaonekana bwana, Chiluba akitoka nje ya mahakama kusikiliza kesi inayomkabili.
Chini anaonekana bwana Fredrick Chiluba enzi hizo akiwa kama rais wa Zambia, akitembea kuelekea nyumbani baada ya kazi ngumu.
Amani bado kitendawili, jeshi ladai kuua waasi wanaopinga serikali"Kanali".
Bujumbura, Burundi - Jeshi la Burundi limedai yakuwa limewaua waasi wapatao 50 hivi karibuni wakati wamapigano yalizuka siku zpatazo kadhaa.
Msemaji wa jeshi,Kanali Aldophe Manilakiza, alisema ya kuwa mapigano na waaasi hawa yalitokea wakati wanajeshi walipo kuwa wakiwasaka waasi, ambao wamekuwa wanapingana na serikali ya Burundi inayo ongozwa na rais Pierre Nkurunzinza.
Pichani ni picha ya rais Pierre Nkurunzinza, siku ya kwanza alipo apishwa kuwa rais, kuhaidi kuleta amani na maelewano nchini Burundi.
Picha ya kati wanaonekana wanajeshi wakimpa kisago jamaa mmoja, ambaye anashukiwa ni mwasi anaye saidia kuleta vurugu.
Picha ya chini wanaonekana baadhi ya watu walio kimbia mapigano wakiwa wanaongea matatizo yao mbele ya viongozi wa swerikali na pembeni ni mmoja ya maasisa wa kijeshi, wakiwasikiliza kwa makini.
Urusi yapata rais mpya , nguvu mpya za kijeshi zaonekana mbele ya dunia.
Moscow, Urusi - Rais mpya wa Urusi leo amepokea gwaride la heshima kwenye eneo linalo julikana kama (Red Square) Uwanja mwekundu, karibu na makao makuu ya serikali ya Urusi, lililo andaliwa kushangila siku ya Ushindi wa Urusi baada ya vita vya pili vya dunia.
Zaidi ya wanajeshi wapatao 8000 wakiongozwa na zana za kivita zenye nguvu za nyuklia na zakawaida, walipita mbele ya rais mpya wa wa Rusia, bwana Medvedev na waziri mkuu mpya wa Urusi bwana Vladamil Putin. Maonyesho haya ni ya kwanza tangu kuvunjika kwa muungano wa jumuia ya Urusi.
Hata vivyo, rais Medvedev alionya ya kuwa watu ndio wanaosababisha vita , hivyo alisema nilazima watu wajitahidi kuepuka hali ya vita kutokea. Na alimalizia kwa kusema ya kuwa kuwa na nguvu za kijeshi ni kwa ajili ya kulinda nchi.
Juu kabisa katika picha, anaonekana amiri jeshi mkuu wa Urusi rais, Medvedev akisalimiana na wanajeshi wakati wa kukagua graride hilo.
Chini ni picha ya rais Medvedev, akiwa kwenye ofisi yake ya urais kwa mara ya kwanza tangu kuapishwa kuwa rais wa Urusi.
Picha ya mwisho, anaonekana waziri mkuu mpya wa Urusi, bwana Vladamil Putin , akiongea baada ya kupitishwa kuwa waziri mkuu hivi karibuni.
Lebanon yawa kidonda kingine kisicho pona, hali ya kuzuka vita vya wenyewe kwa wenyewe yazuka na kuleta wasiwasi.
Beiruti,Labanon - Hali ya wasiwasi imezuka tena nchini Lebanon, baada ya vikundi tofauti ya kisiasa na vya kijamii kuanza kupigana katika mitaa tofauti ya jiji la Beirut.
Mmoja wa wachunguzi wa kisisa za mashariki ya kati alisema haya.
"Kutokana na kutokuwa na amani na serikali kamili, imesemekana ni chanzo cha vurugu hizo na kusababisha kuvipa nguvu vikundi kama Hezbollah vinavyao pinga serikali, kuweza kujiamulia nini la kufanya na hatimayake kwa kutumia nguvu zake za kijeshi kukamata sehemu ya magharibi ya ya jiji la Beiruti".
Hadi kufikia sasa serikali iliyopo ambayo inasaidiwa na nchi za magharibi, imekuwa haina la kufanya na kuiacha nchi kuwa katika hali mbaya,na hali hii itasababisha kuzuka vita vya wenyewe kw wenyewe, alimalizia kwa kusema.
Hadi habari hizi zipo hewani, kundi la Hezbollah ndilo linalo shikilia sehemu kubwa ya jiji la Beiruti baada ya mapigano yaliyo chukuwa siku tatu hadi sasa.
Pichani hapo juu, linaonekana moja ya jengo linaungua kwa moto , baaada ya mapigano kati ya kundi la Sunni na Washia yaliyo tokea hivi karibuni.
Hapo chini ni picha ya baadhi ya wapiganaji wanao pigania vikundi vyao, wakiwa na ana angalia moja ya siraha ambazo ndizo zinazo tumika katika mapigano yanayo endelea.

Tuesday, May 6, 2008

China na Watibet wakubaliana kimsingi, wasema wasemaji wa Dali Lama.

Pete ya ndoa ya harusi yaghalimu madola, penzi limefika palipo.

Nassaua City, Bahama - Mwana mziki maarufu duniani wa mtindo wa R&B, bi Miarah Kerry, amefunga pingu za maisha na mwanamziki, mcheza sinema na T show,bwana Nick Cannon.
Harusi hii imefanyika hivi karibuni Bahama, baada ya hwa wapendanao kuchumbiana kwa kipindi cha mwezi mmoja.
Pete ya harusi ya bi Mariah Kerry, aliyo vaa wakati wa sherehe hizo bi Mariah ilighalimu kiasi cha dola 2,5 million .
Sherehe hiyo iliudhuliwa na watu wakaribi saana wa bi Mariah na bwana Cannon, ni pamoja na mwanamuziki Da Brat
Picha hapo juu,anaonekana bi,Mariah Kerry akiwa kazini kimuziki kutumbwiza wapenzi wa muziki wake.
Picha ya chini anaonekana bwana, Nick Cannon akiwa anaonyesha misuli ambayo imemchanganya bi, Mariah.
Hapo juu ni picha ya bi Maria, akiwa ame pozi huku uzuri wake ukuionekana.
Chini picha ya mwisho wanaonekana Mariah na Nick wakiashilia ya kuwa huo ulikuwa mwanzo wao tu sasa wamethibitisha ya kuwa roho zimeridhiana.
China na Watibet wakubaliana kimsingi,wasema wasemaji wa Dalai Lama.
Beijing, China - Mazungumzo kati ya serikali ya China na Wawakilishi wa Jimbo la Tibet, linalo ongozwa na Kiongozi wa Kidini Dalai Lama, yameisha katika hawamu ya kwanza.
Akisema hayo walipo wasili kwenye kiwanja cha ndege cha Hong Kong, msemaji wana mwakilishi wa Dalai Lama, kuwa mazumngumzo hayo yalikuwa ndio mwanzo wakutafuta ufumbuzi wa mgoggr wa Tibet, na hivyo kutakuwa namazungumzo mingine hapo baadaye, ijapo kuwa akueleza yatafanyika lini.
Mazungumzo haya yamekuja baada ya purukushani, maandamano na hata baadhi ya watu kupoteza maisha yao wakati wakupinga sera zote za China katika jimbo la Tibet.
China mwenyeji wa mashindano ya Olimpiki ya 2008, hivyo mazungumzo haya yatasaidia kupunguza baadhi ya maoni yaliyo tolewa kuhusu serikali ya China dhidi ya jimbo la Tibet.
Juu ni bendera ya China, na serikali ya China inasema Tibet ni sehemu ya China.
Picha mbili tofauti hapo juu, anaonekana kiongozi wa Kidini, Dalai Lama, akiwa anaongoza maombi ya swala.
Rais wa Misri, atimiza miaka 80, makubaliono ya siasa bado mvutano.
Cairo, Misri - Rais wa Misri, Hussein Mubarak, ametimiza miaka 80, hivi karibuni huku hali ya kisiasa nchini humo ikiwa katika hali ya mvutano.
Rais Mubarak,ambaye aliingia madarakani baada ya kifo cha rais, Anwar Sadat, amekuwa madarakani tangu 1981, na kwa kipindi kisicho pungua miaka 27 amekuwa rais wanchi hiyo ya Misri hadi hivi sasa.
Na wakati huo hu polisi wa kulinda mpaka kati Misri na Israel, wamefyatua risasi na kuwauwa watu kadhaa, akiwepo kijana mmoja wa Kinageria, wakati walipo jaribu kuvuka mpaka na kuingia nchini Israel.
Picha hapo juu ni picha ya rais Hussein Mubaraka, ambaye ametawala kwa kipindi kisicho pungua miaka 27 nchini Misri.
Chini pi picha ya rais, Mubaraka akiongea na rais George Bush, mapema mwaka huu wakati rais Bush alipo tembelea Misri.
Chini wanaonekana polisi wa kuzuia fujo wakiwatimua waandamanaji kwa kutumi hewa ya kutoa machozi, na hapo anaonekana mwana mama anakimbia kwa nguvu zake zote kujiepusha na janga hili.
Hawakuweza kunishawishi kukiuka madaili yangu ya kazi, ili niwatumikie.
Khartumu, Sudani - Shirika la Utangazaji la Al Jazeera, ndugu pamoja na marafiki walishangilia baada ya kumwona mmoja ya wafanyakazi mwenzao bwana Sami Al Hajj, ambaye ameachiwa hivi karibuni kutoka jela ya Guantanamo Bay.
Akielezea , bwana Sami Al Hajj, alisema ya kuwa aliojiwa zaidi ya mara 130, kati ya haya 95 ni kuhusu kazi yangu, "Na walitaka mimi niwe shushu wao Amerika"Hivyo baadaye waliamua kumkamata mwandishi yoyote, ambaye atataka kuonye ukweli kuhusuhali halisi wakati vita Afganistani vilipoanza.
Hata hivyo msemaji, wa Jeshi la Amerika, alisema ya kuwa yote yaliyo ongelewa na bwana Sami al Hajj ni ya uongo na alijifanya mgojwa saana alipo wasili mjini Kartumu.
Picha hapo juu ni picha ya bwana Sami Al Hajj, alipo kutana na ndugu, jamaa na marafiki wakati alipo wasili mjini Kartumu nchni Sudani.
Bwana Sami al Hajj alieama"Na walizidi kunitaka niwatumikie nikiwa kama mwandishi wa habari, hata hivyo hawakuweza kunishwishi kukiuka maadili ya kazi yangu ya uandishi wa habari".
Kuwepo kwa mitambo yetu ni moja njia ya kukua kwa kundi letu "Hezbollah".
Beirut, Lebanoni - Serikali ya Lebanoni, imesema yakuwa itachukuwa hatua za kisheria dhidi ya kundi la Hezbollah,ambacho kinaongozwa na viongozi wa Kishia.
Akisema haya msemaji wa serikali ya Lebanoni, bwana Ghazi al Aridi, alisema haya karibuni ya kuwa kikundi cha Hezbollah, linakwenda kinyume, kwa kutumia kutumia mawasiliano amabyo yanamilikiwa na kundi hili la Hezbollah. Akiongezaa , alisema ya kuwa imefikia hadi kundi hili limeweka kamera katika kiwanja ndege, ambazo zimekuwa zikitumiwa na kundi hili kuangalia na kuchunguza nani anaingia na nani anatoka.
Hata hivyo msemaji wa Hezbollah, alisema ya kuwa wanavyombo ya mawasiliano na alikataa ya kuwa Hezbollah, hawatakubali kusikia serikili ya Lebanoni inasema nini. Hapo juu ni picha ya bwana Qassem(Kassim), ambaye alisema mitambo hii ni njia mija wapo ya kukua kwa kundi hili.
Picha chini ni ya bendera la kundi la Hezbollah ikipepea huku pembeni zinaonekana bendera za nchi ya Lebanoni zikipepea, wakati wanachama na wapenzi wa Hezbollah walipoandamana hivi karibuni.

Mpambano nchini Afghanistani bado, na rais anusurika na mashambuliza.
Washington, USA - Rais George Bush, amesema hivi karibuni ya kuwa hali ya Afghanistani bado haijafikia kiwango kizuri cha kimaendeleo.Lakini hata hivyo alisisitiza ya kuwa jumuia za kimataifa na majeshi yake yanafanya kila njia na hali itakua nzuri hapo baadaye.
Rais, George Bush, alisema haya baada ya wapiganaji wa Taliban, walipo shambulia gwaride ambalo liliudhuliwa na rais Hamid Karzai, na kusababisha vifo vya watu wasio pungua sita akiwemo mmoja wa wabunge wa serikali.
Picha hapo juu ni wanaonekana baadhi ya wakazi wa sehemu fulani nchini Afghanistani, wakiwa wamelizunguka gari la jeshi la kimataifa linalo ongozwa na Amerika.
Chini ni picha ya wanajeshi wa Afghanistani wakiwa wanakula kwata, tayari kuwa imara kulinda nchi.
Hapo juu anaonekana rais, Hamid Karzai, akiongea baada ya chambuli lililo fanywa wapiganaji wa Talibani
Moscow yazidi kuimarisha ngome zake mipakani.
Moscow,Urusi - Serikali ya mjini Moscow, imeongeza majeshi yake hivi karibuni karibu na mpaka wa nchi ya Georgia.
Kutokana na msemaji wa serikali ya Moscow,alisema ya kuwa kuwepo kwa jeshi hili ni kukamilisha na kuendeleza ile kazi ya kudumisha amani kufuatia mkataba ulipitishwa mwaka 1994.
Hata hivyo, msemaji wa serikali ya Georgia alisema ya kuwa, kitendo hiki cha serikali ya Moscow, ni kinyume cha sheria za kimataifa, na inahataisha usalama wa eneo zima.
Picha hapo juu wanaonekana wanajeshi wa Urusi wakiwa mbioni, kujiandaa na safari ya kuelekea mpakani na nchi ya Georgia.
Picha ya chini, inaonekana na ramani ya ianayo onyesha mpaka kati ya Georgia na Abkhazia .

Thursday, May 1, 2008

Msanii apigwa marufuku kwa kupiga nyimbo za kupinga ushoga.

Nadal awa moto wa kuotea mbali, Roger Feder,hakuamini macho yake.

Monaco, Monte, Monaco - Mchezaji maarufu wa mchezo wa tenis na anaye shuikila numbea mbili duniani katika mchezo hu kwa upande wa wanaume, Rafael Nadal, amejiongezea tena donge nono na kikombe kinginem baada ya kumshinda mchezaji namba moja wa machezo huo duniani Roger Feder kwa point 7-5, 7 -5, katika fainali iliyochezwqa hivi karibuni mjini Monte Carlo.
Kocha wa mchezaji Rafael Nadal, alisema ya kuwa ushindi huu ni changamoto kwa mchezaji wake, kwa kujiandaa na mashindano ya Wimbleydon yatakayo anza hivi karibuni.
Wakati huo huo, waandalizi wa mchezo wa tenis, nchini Uingereza, wa mashindano ya Wimbleydon wametangaza rasmi ya kuwa bingwa wa mashindano haya watapata donge nono zaidi, kwani wameongeza ongezeko la asilimia 4.7%.
Hivyo washindi wa mashindayo hayo, ambayo yapo katika maandalizi watapata kiasi cha paundi 750,00, sawa na Euro 1.49 mil.
Msanii apigwa marufuku kwa kupiga nyimbo za kupinga ushoga.
Guyana, Georgetown - Serikali ya Guyana imempiga marufuku mwanamuziki wa maadhi ya miziki wa regge kutoka Jamaika, Bounty Killer kupiga musiki wake nchini humo hivi karibuni.
Akitangaza uamuzi huo, waziri wa mambo ya ndani ya Guyana, bwana Clement Rohee, alisema yakuwa, serikali imemkatalia msani huyo, kwani itikadi yake ya kupinga ushoga ni kinyume na haki za binadamu na uamuzi wakuwatenga watu kijinsia kwa kutumia nyimbo zake ni kinyume na sheria na anahatarisha usalama wa badhazi ya watu.
Na hii siyo mara ya kwanza kwa serikali ya Guyana kupiga marufuku kuingia baadhi ya wasanii kutoka Jamaika, kwani hata sikun zanyuma ilimpiga marufuku masanii ajulikanaye kwa jina Mavado.
Pichani hapo juu anaonekan msanii,Bounty Killer akiwa anawaangali wapenzi wa muziki wake kwa macho, kama ujumbe wameu pata.
Picha nyingine anaonekana akilfanya vitu vyake jukwaani hivi karibuni katika moja ya maonyesho yake.
Karata nyingine, Tarika Aziz afikishwa kizimbani kujibu mashitaka.
Irak, Baghdad - Aliyekuwa mmoja wa viongozi na msemaji mkuu wa kutete serikali ya hayati rais Saddam Hussein, bwana Tarik Aziz, amefikishwa mahakamni hivi karibuni kujibu mashitaka ya kuwa alihusika kwa njia moja katika mauaji ya wafanyabiashara wapatao 42, waliopanadisha bei vyakula, wakati Irak ilipo wekewa vikwazao vya kiuchumi na serikali za Magharibi miaka 15
iliyo pita.
Kesi hiyi imeanza 29/04 mjini Baghdad.
Dunia itamkumbuka bwana Tarik Aziz, kuwa mtu wakaribu saana wa aliyekuwa rais wa Irak, marehemu, Saddama Hussein wakati wa utawalawake, bwana Tarik Aziz kwa jina jingine alijulikana kama Alikuwa Mikhail Yuhanna, ni mmoja ya mawaziri ambao walikuwa waumini wa dini ya Kikristu.
Pichani anaonekana bwana Tarik Aziz, akiwa amevalia nguo za munga'nda, sare ya jela, tangu alipowekwa kizuizini na jeshi la Amerika mjini Baghdad.
Picha ya chini anaonekana bwana Mikhail Yuhanna au kwa jina Tarik aziz, enzi hizo alipo kuwa ofisini akisikiliza nini anaelezwa na mmoja wa washauri wake.
Irak bado kitendawili miaka ya zidi kujiongeza, lawama kila kukicha.
USA, Washingtone - Leo ni siku amabyo rais wa Amerika bwana George Bush , alipo tangaza ya kuwa shughuli zote za kivita nchini Irak zimekwisha.
Rais George Bush, aliyaongea haya, mbele ya meli ya kivita ijulikanayo kama Abraham Linchon, huku nyuma kukiwa na tangazo kubwa la kuonyasha ya kuwa kazi imetimizwa/timilika. au kwa kingereza Mission Accompilish.
Lakini hata hivi, tangazo hilo limekuwa kama kitendawili, kwenye vichwa vya wanasiasa na wataalamu wa mambo ya kijamii na maendeleo, hivyo kumkosoa kwa kila hali rais George Bush kila kukicha.
Nimiaka mitano sasa tangu vita dhidi ya Irak vianze na mpaka sasa hakuna jibu kamili lini vita hivi vita kwisha rasmi, alisema mmoja wa wanawakitaaluma kuhusu maendeleo ya kijamii.
Pichani nhapo juu wanaonekana baadhi ya wananchi amabo wanapinga kuendelea kwa vita nchini Irak wakiwa wameshilia kitambala kikubwa chenye maandishi yasemayo kazi imetimizwa/imetimilika, kwadhiaka wakati wa maandamano na mmoja ya wnaandamanaji hawa akiandika idadi ya wanajeshi ambao wamepoteza maisha yao kwenye vita hivi.
Chini anaonekana rais wa Amerika bwana George Bush, akiashiria kwa kidole gumba wakati alaipo tangaza rasmi yakuwa vita vya Iraki vimekwisha.
Mgogoro wa Mashariki ya kati, bado joto ya jiwe kwa kila mwana siasa.
Mashariki ya kati, Gaza - Mgogoro unao endelea kati ya, Wapalestina na Waisrael unazidi kuleta utata, hivi karibuni jeshi la Israel limeshambulia maeneo ya wakazi wa Palestina na kusababisha vifo ya watu wasiopungua watano ambao ni jamaa wa famila moja.
Lakini hata hivyo, msemaji wa jeshi la Israel, alisema walishambulia eno hilo baada ya wapiganaji wa jeshi la Hamas kuanza mashambuli dhidi ya jeshi la Israel.
Kutokana na mgogoro huo imekuwa nivigumu hata wakazi wanao ishi karibu na mpaka unao tenganisha Israel na Palestina kuwa na wakati mgumu , hasa kwa ndugu kutembeleana. Picha hapo juu ni picha ya mmoja ya wakazi wanao ishi karibu na mpaka wa Israel akionyesha ishara ya kuomba aruhusiwe aingie nchi Israel
Picha nyingine ya chini wanaonekana baadhi ya wakazi wa Kipalesstina wa kiombea dua miili ya watu walio fariki dunia baada ya Israel kushambuali kufanya shambilizi hivi karibini.
Mmoja wa viongozi wa jeshi linalo pigana na jeshi la serikali auwawa.
Somali, Mogadishu - Jeshi la Amerika , limesema yakuwa limemua, aliyekuwa kiongozi wa kundi la Al Shabaab ambalo limekuwa likipingana na serikali ya Somalia inayo saidiwa serikali ya Ethiopia.
Kiongozi huyo anayejulikana kama Aden Hashi Eyrow,alikuwa ndiyo nguzo moja ya kikundi hiki cha UIC (Union of Islamic Courts) na kundi la Al Shabaab.
Hata hivyo msemaji wa kundi hilo, amesema ya kuwa kuuwawa kwa bwana Eden Hashi Eyrow, siyo mwisho wa mapambano bado yataendelea na wale wote walio husika na mauaji ya kiongozi huyu wajihadhali.
Pichani anaonekana mmoja wa wapiganaji wa kundi la Al Shabaab , akiwa ameshikilia mtutu tayari kupigana na wanajeshi wa serikali.

Wednesday, April 16, 2008

Tuache kutumia pesa za Amerika, US $ dollar,tuanzishe benki zetu,rais wa Iran.

Nyota ya sinema ya big mama, atimiza miaka 43 ya kuzaliwa.

Holly Wood, Los Angels - Masani maarufu duniani Lawrance Martin, leo ametimiza miaka 43 tangu kulzaliwa.
Martin Lawrance, ambaye alizaliwa tarehe 16/4/1965, nchini Ujerumani Frankfrut,ametokea kuwa msanii maarufu ambaye amecheza sinema nyingi, na vilele amecheza sinema na wasanii kama,Willy Smith na wasinii wengi duniani anasifika kwa kuchekesha saana hasa hawapo jukwaani.
Pichani anaonekana akiwa anafanya vitu vyake kwenye sinema ya big momma.
Picha nyingine anaoneka,Martin Lawrence,akiwasalimia baadhi ya washabiki wake.
Hapo juu anaonekan Martin Lawrence, akiwa ametana shati.
Vatican haitaruhusu vitendo vingine vya aibu kutokea"Pope"
New York, Amerika - Pope Benedict, amewasili nchini Amerika kwa ziara rasmi,ili kuimarisha uhusiano kati ya serikali ya Amerika na Vatikani.
Kufanyika kwa ziara hii ya Pope Benedict kumetonesha donda kwa baadhi ya watu ambao, wanadai yakuwa,baadhi ya watumishi wa kanisa hili la Katoliki kutuhumiwa kuwalawiti baadhi ya waumini wao.
Pope Benedict , alihaidi atahakikisha ya kuwa Vaticani haita ruhusu tena hali hii kutokea.
Hata hivyo,Pope Benedict, atarajiwa kuzungumzia swala hili na swala la Iraki,pindipo watakapo kutana na rais wa Amerika bwana George Bush.
Na wakati huo huo, Pope Benedict, atasherekea siku yake ya kuzaliwa kwenywe Ikuru ya Amerika, sherehe hizi zimeandaliwa na George Bush,na inatarajiwa kuhudhuriwa na watu wasiopungua 9,000
Picha anaonekana,Pope Benedict, akisalimia baadhi ya waumini waliokuja kuudhulia misa hivi karibuni.
Chini ni picha za Pope Benedict tangu alipo kuwa kijana na mpaka anatimiza miaka mwaka 81 leo.
Urusi yataka zidi kutanua misuri yake, Georgia yawa na homa.
Moscow, Urusi - Serilakai ya Urusi imetangaza ya kuwa itaanzisha uhusiano na majimbo ya Kusini mwa Ossetai ,na Abkhazia, yaliyopo Georgia.
Uhusiano huu na majimbo haya utakuwa wa kiuchuni, kijamii na pamoja na kisayansi mbinu.
Hata hivyo serikali ya Georgia, imesikitishwa na kitendo hicho, kwani imedai inakwenda kinyume cha sheria za kimataifa alisema waziri wa mambo ya nje ya Georgia bwana David Bakradze.
Pichani zinaonekana baadhi ya nguvu za serikali ya Urusi, zikionekana amabzo zinaipa homa nchi ya Georgia.
Hapa anaonekana rais wa Georgia,ametangaza ya kuwa atahakikisha yakuwa hali hii aita endelea.
Tuache kutumia pesa za Amerika, US dollar, tuanzishe benki zetu,
Teheran,Irani - Rais wa Iran, bwana Mohmoud Ahamadinejad amewataka wanachama wa OPEC, waache kutumia ($dollar), pesa inayo tumika nchini Amerika katika kufanya biashara.
Akiongezea, ameagiza ya kuwa lazima waanzishe benki itakayo milikiwa na wanachama na pesa zao.
Mvutano kati ya serikali ya Iran na Amerika umekuwa wamuda mrefu, na Iran kuungana na baadhi ya nchi kama, Venezuela, na Syiria,zinazo pingana na sera za serikali ya Amerika.
Wakati huo huo, serikali ya China imaeanza mazungumzo na serikali ya Irani na kwa kuongoza mazungumzo kuhusu swala zima la kuwepo kwa nyuklia na mitambo yake nchini Irani.
Mazungumzo haya yamekuja , baada ya serikali ya Iran kutangaza ya kuwa imewekeza zaidi viini vya nyuklia vipatavyo 6,000.
China ni nchi ambayo inafanya biashara na Iran, japo baadhi ya nchi za magharibi zimeweka vikwazo kwa serikali ya Irani.
Baadhi ya wananchi wa Irani wakiwa wameshikilia bango lenye picha za maris ambao wanapinga sera za nje za serikali ya Amerika.
Pichani hapo juu, wanaonekana marais wa Venezuela bwana Hugo Chavez na Iran bwana Mahmoud Ahamadinejad wakionyesha ushirikiano wao ulivyo komaa.
Picha nyingine wanaonekana rais wa Syiria bwana, Bashar al Assad na rais wa Irani, Mohamoud Ahamadnejad walipokutana hivi karibuni.
Picha nyingine wanaokena baadhi ya wajumbe wa serikali ya China na Iran walipo tia saini baadhi ya mikataba ya kibiashara hivi karibuni.
Ajali ya ndege, nchini Jamuhuri ya Kongo, yaleta wasiwasi kuhusu ubora wa ndege .
Goma, Jamuhuri ya Kongo - Serikali ya Jamuhuri ya Kongo, imetangaza ya kuwa ajali ya ndege iliyo tokea mjini Goma,imesababisha zaidi vifo vya watu wasiopungua 40 kupoteza maisha yao.
Ndege hiyo ambayo inasemekana ya kuwa ilipata itilafu kwenya tairi lake moja, ambolo inaaminika ndiyo chamzo cha ajalihiyo.
Kutokana na ajari hii, kutokea hivi karibuni, kuna leta wasiwasi kuhusu hali nzima ya usalama wa ndege hizi, kwani kampuni inayo miliki ndege hizi ijulikanayo kama Hewa Bora, ni moja ya kampuni ambayo imefungiwa na mashirika ya kimataifa kwa ndege zake kutumika kwenye anga za kimataifa.
Pichani hapo juu wanaonekana baadhi wenye huruma wakiwa katika harakati za kuwaokoa watu ambao wamo ndani ya ndege hii iliyo pata ajali.
Picha nyingine, inaonekana sehemu ya ndege hii ambayo imepata ajali, na kuuwa zaidi ya watu wasiopungua 40.