Friday, July 18, 2008

Rolihlahla Nelson Mandela Madiba, atimiza miaka 90 tangu kuzaliwa"Leo pia watimiza miaka 10 ya ndoa"

Rolihlahla,Mandela Madiba atimiza miaka 90 tangu luzaliwa"Leo pia watimiza miaka 10 ya ndoa".

Eastern Cape - Afrika ya Kusini - Mtetezi wa haki za binadamu,kiongozi, mwanamapinduzi na aliyekuwa rais wa kwanza mzawa wa Kiafrika (Mweusi) Nelson Rolilhahla Mandela (Madiba) ametimiza miaka 90, leo 18/07/08.
Bwna, Nelson Mandela alichaguliwa kuwa rais wa Afrika ya Kusini mwaka 1994 baada ya kuchaguliwa katika uchaguzi uliyo usisha vyama vingi nchini humo.
Katika kuadhimisha sherehe ya kuzaliwa kwake miaka 90. ameagiza ya kuwa wale wote walio kuwa na mali na matajili waanze kuwasaidi wale watu masikini ambao hawana uwezo wa kimaisha.
Akiongezea agizo lake, Nelson Mandela , alisema mtu akiwa masikini nivigumu kuishi maiaka mingi.
Rais huyo wazamani wa Afrika ya Kusini, alishukuru kwa kusema nanafuraha ya kuwa bado yupo hai hadi sasa.
Nawakati huo huo, leo siku ya ijumaa 18/08, Nelson Mandela anasherehekea miaka kumi ya ndoa yake na bi Gracel Machel.
Mwana mapinduzi Nelson Mandela, alijiudhulu katika kazi za kisiasa ya jamii mwaka 2004.
Picha ya kwanza anaonekan Nelson Mandela wakati alipokuwa na miaka 42.
Picha ya pili anaonekan bwana Nelson Mandela kushoto akiwa na bi Winnie Mandela wakiwasalimi watu waliokuja kuwalaki wakati, wakuachiwa kwake kutoka gerezani mwaka 1990.
Picha ya tatu anaonekana rais, mstahafu, Nelson Mandela katikati na kushaoto kwake anaonekan waziri mkuu wa Uingereza bwana, Gordon Brown akipiga makofi wakati wwalipo kutana hivi karibuni mjini London, na kulia ni bi Gracel Macheli.
Picha ya tatu anaonekan,rais mstahafu Nelson Mandela, akipigwa kisi na mmoja wa wageni waliokwenda kumtembelea hivi karibuni.
Picha ya nne , anaonekan Nelson Mandela kabla ya kutimiza miaka 18.
Picha ya tano ,anaonekana rais mstahafu, Nelson Mamdela akifanya mazoezi ya ngumi,mchezo wa ngumi ulikuwa ndiyo mchezo aliokuwa akiupenda wakati wa ujamna wake.
Picha ya sita, anaonekana mwanamapinduzi, Nelson Mandela alipo kwenda kutembela gereza lililopo kwenye kisiwa cha Robin, ambapo alitumika kifungo cha wakati alipokuwa anatetea haki za wengi nchini Afrika ya Kusini.
Picha ya mwisho, anaonekana ,rais mastahafu ,mwanamapinduzi na mtetezi wa haki za binadamu Nelson Mandela akitabasamu kwa furaha baada ya kyadhimisha miaka 90 tangu kuzaliwa kwake. "Long live Nelson Rolihlahla Mandela'' Mungu akubariki na Mungu atubariki" Amin.
Mwanariadha akatishwa ndoto yake ya Olimpiki nchini China .
London,Uingereza - Mkimbiaji wa mbio fupi duniani, Dwain Chamber amekataliwa kushiriki katika mashindano ya Olimpiki 2008 nchini China.
Kwamujibu wa semaji wa wa mwanamichezo huyo, alisema mahakama imekataa kumrusu Dwain Chamber kushiriki mashindano hayo ya Olimpiki 2008 nchini China, kwa kutaaa kutengua kifungo ambacho, Dwain Chamber alipewa kushiriki katika mbio za kimataifa, baada ya kukutwa na kashfa ya kutumia madawa ya kuongeza nguvu mwilini. Picha hapo juu ni picha ya Dwain Chamber, akitoka ndani ya mahakama kusikiliza kesi yake iliaruhusiwe kushiriki mashindano ya Olimpiki nchini 2008 nchini China.
Picha ya pili anaonekana Dwain Chamber akimaliza mbio za majaribio aliyoshiriki hivi karibuni nchini Uingereza.
Kanisa la Anglikana lawa na mvutano mkubwa"Askofu azuiliwa kuhushulia mkutano".
London,Uingereza - Askofu Gene Robinson, ambaye alikubali ya kuwa yeye ni shoga,amezuiliwa kuhudhulia mkutano wa wakuu wa kanisa la kikristu la Anglikani unaoendela nchi Uingereza.
Mgogoro katika kanisa la Anglikani, ulianza wakati askofu Gene Robinson alipo tangaza ya kuwa yeye ni shoga.
Kuzuiliwa kwake, kulifahamika baada ya askofu mkuu wa kanisa la Anglikani Askofu, Rowan Williams kutomwalika katika mkutano huu ambao hufanyika kila baada ya miaka kumi. Mkutano huu ambo umeanza usiku wa kuamkia tarehe 15/07/08, utazungumzia mswala ya kiimani na kujadili ikiwa wanawake wataruhusiwa kuwa wachungaji na maaskofu.
Picha ya askofu mkuu wa Kanisa la Anglikani, Rowan Douglas Williams, ambaye kanisa la Anglikana lenye waumini million 77, kote duniani, lina mwangalia kwa macho yote kutatua mgogoro ulipo katika kanisa hilo.
Picha pili ni ya kanisa kuu la Anglikana lililopo nchi Uingereza, lijulikanalo kama" St Paul's Cathedral".
Picha ya tatu ni ya Askofu,,Gene Robinson, ambaye amekuwa gumzo na chanzo cha mvutano katika kanisa la Anglikana , baada ya kueleza adhalani ya kuwa yeye ni shoga.
Nchi za Ulaya kuzidi kukaza nati kwa serikali ya Zimbabwe"Vikwazo kuongezeka".
Brussels, Belgium - Muungano wa nchi za Ulaya umezidi kuiwekea vikwazo zaidi serikali ay Zimbabwe inayo ongozwa na rais Robert Mugabe na washirika wake.
Kimsingi vikwazo hivyo vimekwisha kubalika baada mabalozi wa wa nchi hizi za jumuia ya Ulaya kukubaliana siku ya jumanne15/07/08,"Alisema mmoja wa viongozi aliyeudhulia kikao hicho".
Hata hivyo msemaji huyu alisema yakuwa uamuzi huu, uatakubalika na kupitishwa wakati wa kikao cha mawaziri wa mambo ya nchi za nje wa jumuia hii ya Ulaya.
Picha ya hapo juu ni ya bendera ya Umoja wa nchi Ulaya, ambazo zimekubaliana kimsingi kuwekewa vikwazo serikali ya Zimbabwe.
Picha pili ni ya rais, Robert Mugabe ambaye serikali yake ipo katika hali ya kususasua kwenye jumuia ya kimataifa.
Picha ya tatu, wanaonekana kushoto, aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza bwana, Tony Brair wakati walipokutana miaka ya nyuma wakati nchi hizi mbili zilipo kuwa marafiki wa damu.
Picha ya mwisho ni ya bendera ya Zimbabwe, nchi ambayo serikali yake ina vutana na nchi nyingi za jumuia ya Ulaya.

Afrika ya Kati kuwa na amani tena,"Sudan na Chad kurudisha uhusiano".
Dakar,Senegal - Serikali ya Senegal chini ya uongozi wa rais Abdoulaye Wade, umeweza kuondoa mgogoro ambao ulikuwa unaleta matatizo kati ya Chad na Sudan.
Kufuatia mazungumzo yaliyo chukua siku kadhaa na kufila makubaliano siku ya alkhamisi 17/07/08, wiki hii.
Rais wa Sudana bwana, Omar Al Bashir alihaidi mgogoro huu umefika mwisho baada ya serikali za Sudani na Chad kufungua ofisi zao za kibalozi, ili kuendeleza mausiano yaliyo dholota, kutokana na kila upande kulaumu ya kuwa zinasaidiana na wapinzani wa serikali kuleta mchafuko katika nchi zao.
Picha ya hapo juu ni picha ya rais Omar Al Bashir, ambaye serikali yake ilikuwa na matatizo na seriikali ya Chad.
Picha ya pili na ya tatu, wanaonekan baadhi ya wapiganaji wa pande zote, ambao walikuwa wanashambuliana wakati wa mzozo ambao umekwisha.
Picha ya chini ni ya rais Idris Deby, ambaye alikuwa na hali ngumu kiusiano na rais wa Sudan bwana Omar Al Bashir.
Picha za kuchorwa hazita tiliwa maanani kwa watu wenye kuelewa"Mgombea urais wa Amerika - Baraka Obama"
New York, Amerika - Mgobani pekee wa urais, kupitia chama cha Demokrati cha Amerika, bwana, Baraka Obama amesema ya kuwa, kuchorwa kwake kwenye moja ya gazeti la mjini New York , niyakutotiliwa maaanani na watu wanao elewa hawatafuatilia na hakuna kigeni.
Katika michoro hiyo, wameonekana bwana, Baraka Obama naakiwa amevaa kama Osama Bin Laden na mkewe bi Michelle akiwa ameba bunduki na wote wana gongeana mikono.
Pichani hapo juu anonekana akihutubia katika moja ya mikutano yake hivi karibuni.
Picha ya pili anaonekana, bwana na bibi Obama wakiwa na watoto wa katika moja ya kampeni za awali ili kuweza kuwakilicha chama cha Demokrati katika kuwani kuwa mgombea pekee wa uraisi kupitia chama hicho.
Picha ya tatu ,anaonekana bi, Michelle Obama akisalimia, kabla ya kuanza kuhutubia moja ya mikutano hivi karibuni.
Picha ya chini ni picha ya kuchorwa ambayo imechorwa katika gazeti moja mjini New York.
Waasimu wawili kukutana anakwaana?"Inawezekana asema waziri wa mambo ya nje"
Ankara,Uturuki - Mazungumzo kati ya Iran na Amerika huenda yakawezekana kwa viongozi wa serikali hizi mbili kuzungumza anakwaana.
Akizungumza haya alipo kuwa ziarani Uturuki siku ya ijumaa, waziri wa mambo ya nje ya Iran, alisema yakuwa serikali ya Iran inaelewa haya kupitia vyombo vya habari, kama srikali ya Amerika itakuwa tayari basi tunaweza kukaa na kuongea.
Kufuati wasemaji wa serikali wa pande zote mbili, wanasema huenda kukawepo na mawasiliano hivi karibuni.
Kuzorota kwa Amerika na Iran , kulianza baada ya mapinduzi yaliyo ongozwa na viongozi wa dini mwaka 1979.
Picha hapo juu ni picha ya bendera ya Iran ambayo serikali ya nchi ya Iran haikubaliani na serikali ya Amerika, hasa katika swala la nyuklia.
Hapo katikati, anaonekana waziri wa mambo ya nje wa serikali ya Iran bwana Monauchehr Mottaki.
Picha ya tatu, nipicha ya bendera ya Amerika, nchi ambayo imekuwa ikivutana na na serikali ya Iran, tangu mapinduzi ya mwaka 1979.

Wednesday, July 16, 2008

Hezbollah na Israel zatimiziana ahadi" Wabadilishana wafungwa na miili ya wapiganaji wao".

Brad na Angelina wawa baba na mama mapacha au (mapasa) "Picha za watoto kughalimu mamillioni".

Nice, Ufaransa - Mcheza sinema , balozi wa umoja wa mataifa kwa upande wa UNICEF na nyota maarufu duniani bi Angelina Jolie amejifungua watoto mapasa(Mapacha) wakiki na wakiume katika Hospitali ya French Riviera.
Watoto hao mapacha ambao walipishana dakika moja walizaliwa siku ya jumamosi 12/07/2008, jioni walikuwa na paundi 5 kila mmoja.
Watoto hao walioitwa Knox Leon na Vivienne Maecheline
Inatarajiwa picha zao za kwanza huenda zikauzwa kwa bei ya juu zaidi kufika kiasi cha $ 20 million,alisema mmoja wa mpiga picha bwana, Darryn Lyons, anayemiliki gazeti la Big Pictures la London.
Akiongea hay mganga aliyesaidia kuzaliwa kwa watoto hawa mapacha,alisema Brad Pitt alikuwa pembeni wakati Angelina anajifungua.
Pichani wanaonekana Brad na Angelina wakati walipo kuwa katika moja ya sherehe, kwa sasa wanitwa baba na mama MAPASA.
Picha ya pili wanaonekana Brad na Angelina, walipo udhulia pamoja katika maonyesho ya manyota wa dunia kabla ya Angela kujifungua.
Picha ya tatu, anaonekana Angelina akiwa amesimama wakati alipo kuwa mja mzito wa watotomapasa.
Hezbollah na Israel zatimiziana ahadi"Wabadilishana wafungwa na miili ya wapiganaji wao".
Beiruti,Labanoni - Wafungwa watano ambao walikuwa wanashikiliwa na serikali ya Israel kama wauwaji na magaidi leo 16/07/2008, wameachiwa huru na kurudishwa nchini Lebanon na miili ya wanajeshi wa jeshi la Israel kurudishwa nchini Israel, ikiwa ni moja ya makubaliano kati ya serikali ya Israel na kundi la Hezbollah.
Kwa upande wa Labanon ilikuwa ni sherehe na nderemo kwa kuachiwa kwa wapiganaji wao na kwa upande wa Israel ilikuwa ni masikitiko makubwa alisikika msemaji mmoja wa serikali akisema haya.
Miili ya wanajeshi, Ehud Goldwasser na Eldad Regev ambao waliuwawa wakati wa mapambano na Hezbolah.
Hata hivyo kuachiwa kwa wafungwa hao watano,kuliambatana na kutolewa kwa miili ya wapiganaji wa Hezbollah na Palestina ambao waliuwawa wakati wamapigano kwa kipindi tofauti na jeshi la Israel.
Pichani hapo juu anaonekana viongozi wa Hezbollah wakiwa na wanachama wao wakishangilia kuachiwa kwa wapiganaji wao.
Picha ya pili ni moja ya jeneza lililo beba mwili wa mmoja wa wapiganaji wa Hezbollh akitolewa ili kukabidhiwa kwa uongozi wa Hezbollah.
Picha ya tatu, wanaonekana badhi ya ndugu wa wanajeshi wa Israel wakilia kwa uchungu, mara baada ya kukabidhiwa miili ya wapiganaji wao.
Wazambia na chama cha upinzani wataka kujua kiundani kuhusu afya ya rais"Wapinzani"
Lusaka, Zambia - Chama kikuu cha upinzani nchini Zambia Patriotic Front(PF) kimetaka uwepo uwazi wa maelezo ya afya ya rais Levy Mwanawaswa kama bado kama anauwezo wa kuongoza nchi.
Akiongea haya, kiongozi wa wa chama hicho bwana, Michel Sata,amesema hawaamini taarifa ya serikali inayo sema hali ya afya inaendelea vizuri.
Rais, Levy Mwanawaswa mwenye miaka 59,amelazwa katika hospitali mjini Paris baada ya kupata ugonjwa wa kiarusi wakati alipo udhulia mkutano wa umoja wa Afrika nchini Misri. Picha ya hapo juu ni anaonekana rais Levy Mwanawasa, alipokuwa akihutubia balaza kuu la umoja wa mataifa.
Picha ya chini anaonekana rais,Levy Mwanawaswa, akikagua mradi wa maji safi hivi karibuni kabla ya kwenda kwenye mkutano nchini Misri.
Kampuni na serikali bado kuvutana" Waadhulika walitakakupewa malipo madogo".
Kano,Nigeria - Kampuni ya madawa ijulikanayo kama Pfizer imetangaza yakuwa mazungumzo kati ya srikali ya Nigeria umevunjika hivi karibuni.
Akiongea haya, wakili wa kampuni hii ya madawa Pfizer, alisema mkutano huu ulioudhuliwa na waziri wa sheria wa Nigeria na wakili mkuu bwana, Michel Andoakaa ,na mwakilishi wa wadhulika bwana, Alhaji Maisikeli.
Mwakilishi wa wadhulika alisema, mkutano huu haukufikia makubaliano,kwani kampuni ya Pfizer likuwa imetoa malipo ya kiasi cha $21million kwa maswala ya sheria na waathirika 200 kupata jumla ya $10million, na ni jambo ambalo haliwezekani, kwani watu waliotumia dawa hii aina ya "Trovan" kama majaribio mwaka 1996,walidhulika na wengine kupoteza maisha.
Picha ya picha ya bendera ya Nigeria.
Picha ya pili ni picha ya baadhi ya na dawa amabyo hutumiwa na binadamu karibu kila siku.
Afrika yawa na njia mbili kuhusu kukamatwa kwa rais wa Sudani.
Addis Ababa - Ethiopia - Umoja wa Afrika umeonya vikali yakuwa kitendo cha kumshitaki rais wa Sudan bwana, Omar Al-Bashir, kunaweza kuatarisha hali halisi ya usalama nchini Sudan hasa kwenye eneo la Darfur.
Na Umoja huu wa Afrika, umesema pia kushitakiwa huku kwa rais, Omar Bashir kunaweza kuwa ni njia moja ya kuanza kuwatishia viongozi wa Afrika kwa kutimika nguvu za mahakama pasipo kihalali hasa panapo kuwepo na swala la kisiasa.
Kushitakiwa kwa rais Bashir,kulitamkwa rasmi na wakili wa mahakama ya Hague bwana, Luis Moremo Ocampo, (ICC) wakati alipo kuwa akieleza mashitaka yanayo mkabili rais, Omar Al Bashir.
Mashitaka hayo yanayo muhusu rais Omar Al Bashir, ni kukiuka kwa haki za kibinadamu kwa serikali yake na vita vilivyo leta mauaji mauaji katika eneo la Darfur.
Hata hivyo Umoja huu wa Afrika , unapinga kukika kwa haki za binadamu katika nchi wanachama wake.
Juu ni picha ya alama ya mahakama, ambayo hutumika kutafutia haki kwa wale wanao onewa.
Picha ya pili anaonekana rais, Omar Al-Bashir akiwapungia mikono baadhi ya watu waliokuja kumuunga mkono kwa kupinga kushitakiwa kwake na mahakama ya mjini Hague.
Picha ya tatu wanaonekana baadhi ya watu wapatao maelfu ambao wanaathirika na kupata taabu kutokana na mgogoro unao kabiri eneo la Darfur.

Uchunguzi wa kifo cha bi,Benazir Bhutto kuanza "Umoja wa matifa"

Wachezaji lazima watimize makubaliano na timu zao "Pele"

London,Uingereza - Mfalme wa soka duniani Pele,amesema hivi karibuni yakuwa ni lazima wachezaji watimize na kutekeleza mikataba ambayo wamekubaliana na timu zao.
Pele,aliongezea kwa kusema yakuwa kauli ya kiongozi wa shirikisho la soka bwana, Sepp Blatter ya kuwa wachezaji wanakuwa kama watumwa ni kauli isiyo kuwa ya makini.
Picha hapo juu anaonekana mfalme Pele, akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.
Chini anaonekana Pele, akiwa ameshikilia moja ya nishani ambazo amekuwa akitunikiwa kutokana na umaili wake kwenye soka miaka ya nyuma.
Picha ya pili anaonekana, mfalme wa soka duniani, Pele akishangilia baada ya kufunga moja ya magoli ambalo liliifanya Brazil kuwa bingwa wa soka duniani mara ya tatu wakati wa enzi zake.
Chavez na Uribe wakutana mjini Caracas"Uhusiano utaimarika tena wasema marais hawa".
Caracas, Venazuela - Rais wa Venezuela bwana Hugo Chavez amekutana na rais wa Kolombia bwana, Alvaro Uribe.
Katika mkutano huu viongozi hawa walizungumzia ni jinsi gani wataweza kujenga na kudumisha uhusiano wao upya ambao ulikuwa si mzuri kwa kipindi kilefu.
Kwa upande wake rais Uribe , alisema yakuwa mkutano huu na rais Chavez,umefungua upya uhusiano wa nchi hizi mbili.
Hapo juu wanaonekana rais wa Kolombia bwana,Uribe akipunga mkono na rais Charvez akiwa amesima karibu, wakati rais,Uribe alipo wasili nchini Venezuela.
Chini wanaonekana rais Chavez , akiongea kitu fulani kwa rais wa Kolombia Alvaro Uribe.
Uchunguzi wa kifo cha bi,Benazir Bhutto kuanza"Umoja wa mataifa".
Islamabad, Pakistan - Umaoja wa mataifa umesema ya kuwa uchunguzi wa mauaji ya waziri mkuu wa zamani wa Pakistani, bi Benazir Bhutto.
Kukubalika kwa uchunguzi huo, kumekuja baada ya katibu mkuu wa umoja wa Mataifa bwana Ban Ki - Moon kukutana na waziri wa mabao ya nchi za nje wa Pakistan bwana ,Shah Mahamood Qureshi.
Kwa kusisitiza swala hili , bwana Shah Qureshi , alisema ya kuwa serikali ya Pakistani itatoa kila msaada katika kukamilisha uchunguzi huu wa mauaji ya bi Benazir Bhutto.
Picha ya kwanza , anaonekana bi Benazir Bhutto akiwa kwenye gari wakati wa kampeni ya kuimarisha chama chake, siku chache kabla ya mauaji yake. Picha ya pili, anaonekana bi,Benazir Bhutto na mumewe,wakati walipo kutana na rais wa zamani wa Palestina,hayati Yasir Arafat.
Picha ya tatu anaonekana waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, akiandika rambi rambi za serikali ya Amerika baada ya kifo cha bi Benazir Bhutto.
Chini picha ya mwisho, wanaonekana baadhi ya wapenzi na ndugu wa hayati bi Benazir Bhutto, wakiomboleza baada ya kifo cha bi Benazir Bhutto.
Amani ya Mashariki ya Kati ipo karibu "Asema waziri mkuu"
Paris, Ufaransa - Rais wa Ufaransa bwana, Nicholas Sarkozy amezungumza na viongozi wa Izrael na Palestina wakati wa kufunguliwa kwa mikutano ushirikiano wa nchi za ukanda wa Mediteranian uliofanyika katika jiji la Parisi.
Katika mkutano huo, viongozi hawa aliongea kwa pamoja ni amani tu, itakayo leta uelewano na ujirani mwema kati ya Israel na Palestina.
Akisisitiza hayo waziri mkuu wa Izrael kwa kusema ya kuwa hii inaonyesha yakuwa amani ya mashariki ya kati ipo karibu, na hasa kati ya Waizrael na Wapalestina.
Pichani hapo juu ni wanaonekana viongozi wa Israel kulia bwana Ehud Olmert , kati ni rais wa Ufaransa Nicholas Sarkozy na rais wa Parestina bwana Mohmoud Abbas, wakati walipo kuwa wakiongea na waandishi wa habari.
Picha ya pili anaonekana rais Nicholas Sarkozy, akipita na gari wakati wa sherehe ya kitaifa iliyo hudhuliwa na viongozi wa jumuia ya mwakanda wa Mediteraniani.
Kanisa Katoliki kuomba radhi tena kwa matukio yaliyofanywa kutumia jina la kanisa.
Sydeney, Australia - Askofu mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Baba Mtakatifu Benedict, amewasili nchini Australia siku ya tarehe 13/07/2008 tayari kunza ziara yake ya kidini.
Katika ziara hiyo Baba Mtakatifu, amesema yakuwa atawaomba radhi wale wote waliotendewa vibaya na baadhi ya wafanyaka au naviongozi wa dini wa dhehebu la katoliki.
Akiongea hayo , Baba Mtakatifu, alisema ni muhimu kwa Kanisa kukubali na yakuwa kuna mambo mabaya yalitendeka kwa kutumia jina la Kanisa Katoliki na hivyo ni lazima kanisa lifanye kila njia kuweka sawa na kuendelea kutangaza na kufanya kazi yake kama kanisa na kutangaza neno la Mungu.
Pichani hapo juu anaonekana, Baba Mtakatifu,anaonekana akiwabariki waumini waliokuja kuhudhulia misa.
Picha ya pili anaonekana , Baba Mtakatifu akifunga mikono kukubali kukaribishwa kwake katika ziara yake nchi Australia.
China na Urusi zakataa na kuonyesha misuri yake ndani ya Umoja wa Mataifa.
New York, Amerika - China na Urusi zimepinga hatua yoyote ya kuiwekea vikwazo serikali ya Zimbabwe inayo ongozwa na rais Robert Mugabe.
Akiongea haya waziri wa mambo ya nchi za njee wa Urusi, alisema itakuwa ni wahatari na kitendo cha kamati ya ulinzi ya umoja wa mataifa kuingilia maswala ya nchi hasa hasa katika maswala ya kisiasa.
Hata hivyo,waziri wa mambo ya njee wa Urusi aliongezea kwa kusema ya kuwa serikali ya Urusi, inapinga kitendo chochote cha kukandamiza haki za binadamu popote duniani na kulaani matukio yote yaliyotokea nchini Zimbabwe.
Picha hapo juu ni picha ya bendera ya Urusi na bendera ya China, nchi ambazo zimepinga kuwekewa vikwazo kwa serikali ya Zimbabwe.