Monday, July 6, 2009

Urussi na Amerika zakubaliana kushirikiana katika swala la nyuklia. Moscow, Urussi - 06/07/09. Urussi na Amerika zimekubaliana kupunguza siraha za nyuklia, wakati marais wa nchi hizo walipo kutana leo siku ya jumatatu jijini Moscow. Makubaliano hayo,yamefanyika wakat Rais wa Amerika , baraka Obama, akiwa ziarani Urussi, kuongea na viongozi wa Urussi,ili kudumisha uhusiano, ambao ulikuwa umeingia utata, baada ya Amerika kutaka kuweka makombo yake katikati mwa Ulaya, kwa kudai ni kaajili ya kulinda mashambulizi ambayo yanaweza kutokea Iran au Korea ya Kaskazini, lakini Urussi ilililikataa jambo hilo na likazusha mgogoro. Picha hapo juu, wanaonekana rais wa Amerika, Baraka.H.OBama, akiongea na rais wa Urussi Dmitri . A. Medvedev wakati walipo kutana kwa mazunguzo ya kikazi jijini Moscow.

Sunday, July 5, 2009

Serena na Venus Williams Malkia wa tenis wa Wimbledon 2009.

Serena na Venus Williams, Malkia wa tenis wa Wimbledon 2009.

Wimbledon, Uingereza 05/07/09. Kwa mara nyingine tena, Serena na dada yake Venus, wameweza kushinda mchezo wa tenis kwa wanawake na kuchukua kikombe cha Wimbledon kwa ushindi wa seti 7-6, 6-4 zidi ya Samantha Stosur na Rennae Stubbs.
Huku wakiwa na furuha, Venus alisema ya kuwa ushindi huu umekuja kutokana na jitihada yao, na kwa kuzingatia tumecheza zaidi ya masaa matatu jana na leo,hivyo inabidi tuwe na furaha kwa kutokubali kuruhusi uchovyo ututalawale.
Senena, ambaye alishinda siku ya jumamosi kwa upande wa wanawake, alisema huwa anajisikia furaha saana anaposhinda huku akiwa na dada yake pamoja katika mchezo wa wawili wawili.
Picha hapo juu wanaonekana , Serena na Venus Williams, wakiwa wamechikia vikombe vya ushindi baada ya kushinda tenis fainali wanawake katika mchezo wa wawili wawili.
Picha ya pili, wanaoneka Venus kulia akienda kumkumbatia mdogo wake Serena, mara ya kushinda seti ya mwisho iliyo wapa ubingwa.
Picha ya tatu, anaonekana , Serena akiangalia kwa tabasamu sahani ya ubingwa wa tenis wa Wimbledon,mara baada ya kukabidhiwa.
Picha ya nne, anaonekanam Serena , akilionyesha sahani la ubingwa wa tenis, kwa upande wa wanawake, baada ya kushinda dada yake Venus.
Picha ya tano, anaonekana, Venus hali siyo nzuri, wakati alipo kuwa akishindana na mdogo wake kugombania ubingwa wa kombe la teni wanawake la Wimbledon.
Picha ya sita, wanaonekana, Serena akimkubatia dada yake, Venus , mara baada ya mpambano kati yao, ambao Serena aliweza kumshinda dada yake.
Picha ya saba, anaonekana, Serena , akiwa amepiga magoto kushangilia, ushindi zidi ya dada yake.
Roger Federer,aweka rekodi ya mchezo wa tenis duniani.
Wimbledon Uingereza - 05/06/07.Roger Federer, ameshinda kombe la Wimbledon katika mchezo wa tenis , na kuweka rekodi ya kuwa ushindi wa mashindano makubwa ya tenis kwa mara ya 15.
Katika pambano hili ambalo lilimpa Roger Ushindi zidi ya Andy Rodick, kwa kumshinda kwa seti 5-7 (6) ,7-6,(5), 3-6 na 16-14.
Roger Federer, ambaye ameshinda fainali za Wimbledon mara 6,katika mchezo uliowachukua muda wa masaa 4 : 18dk.
Picha hapo juu anaonekna Roger Federer, akiuchonga mpira ambao ulimshinda, Andy Rodick, na kumpa ushindi, Roger Federer kwa seti 16-14.
Picha ya pili, anaonekna Roger Fedrer, akiwasalimia kwa furuaha wapenzi wa mchezo wa tenis waliokuja kushuhudia pambano kali kati yake na Andy Rodick.
Picha ya tatu, anaonekana, Roger Fedrer, akibusu kikombe cha ubingwa cha mchezo wa tenis, mara baada ya kukabiziwa kikombe hicho.
Amerika na Urussi kuziba ufa uliopo?
Moscow Urussi -05/07/09. Rais wa Urussi, Dimirti Medvedev, atakuwa mwemyeji wa rais wa Amerika, Baraka Obama hivi karibuni, ili kuzidi kuimarisha uhusiano wa karibu.
Ziara ya rais Baraka Obama nchini Urussi, itakuwa ni pili katika bara la Ulaya, baada ya mkutano wa kiuchumi ulifanyika mjini London Uingereza.
Mambo mengine yatakyo zungumziwa ni maswala ya makombora ya kivita ambayo Amerika inampango wa kuyakeka katika moja ya nchi moja ya Ulaya, jambo ambalo Urussi inalipinga vikali.
Picha ya hapo juu wanaonekana, raia wa Urussi, Dimitri Medvedev, akiwa anamnongoneza waziri mkuu wa Urussi, Vladamir Putin.
AU haihukubaliana na mahakama ya kimataifa. rais, Al - Bashir yupo huru kusafiri.
Tripol Libya - 04/07/09. Kikao cha viongozi wa Afrika kimamua kwa pamoja ya kuwa nchi za Afrika hazita husika katika kumkamata au kumkamata rais wa Sudan, Omar Al - Bashir.
Uamuzi huo ulichukuliwa na wakati viongozi wa muungano wa nchi za Afrika walipo kutana chini ya uwenyekiti wa rais wa Libya Muhamar Ghadafffi.
Rasi wa Sudan, anakabiliwa na kesi ambayo imefunguliwa zidi yake na mahakama inayo shughulikia kesi za ukiukaji wa haki za binadamu iliyopo nchi Nederland (The Hague).
Kufuatia uamuzi huo, rais wa Sudan anaweza safiri katika nchi yoyote ya Afrika bila kuwa na wasiwasi, kwa kuzingatia nchi 33 za Afrika zilikubaliana na kutia sahii makubaliano ya mjini Rome Itali,ya kufungua mahakama itakayo shughulikia kesi za ukiukwaji wa haki za binadamu iliyopo nchi Nederland.
Picha hapo juu, anaonekna rais , wa Sudan, Omar Al bashir , akiwa katika kikao cha viongozi wa Afrika kilicho fanyika hivi karibuni.

Thursday, July 2, 2009

Binti aliyepona katika ajali ya ndege akutana na baba yake.

Historia na ndoto za Williams za jirudia nchini Uingereza. Wimbledon, Uingereza - 02/07/09. Historia ya mchezo wa tenisi, imejirudia tena, baada ya ndugu wawili mkubwa na mdogo,kukutana tena katika fainali ya kugombea kikombe cha Wimbledon. Ndugu hao , mabao pia ni Dada mdogo Serena Williams na dada mkubwa Venus Williams, watakutana mara ya kibarua kigumu cha kupambana na kushinda michezo yote ya tenisi kwa upande wa wanawake, kutoka hatua ya mwanzo hadi kufikia kukutana fainali. Katika, mchezo wa nusu fainali, Serena aliweza kumshinda, Elena Demetieva kwa seti 7-5,8-6, japo kayika seti ya kwanza Serena alishindwa kwa seti 6-7. Naye dada Venus, alishinda , bila huruma Dinara Safina kwa seti 6-1,6-0. Kufuatia ushindi wa madada hawa, Venus na Serena , ambao wanazaliwa na mama na baba mmoja, kumewafanya wakutane tena katika fainali ya Wimbledon kwa mara ya nne. Kukutana kwa madada hao,kunazidi dhihirisha ya kuwa ndoto zao walizo kuwa wakiziota miaka 20 iliyo pita kwenye mji walio kulia, Compton Califonia za kukutana kwenye fainali ya mashindano makubwa inakuja kila wanapo amua kufanya kazi ya ziada, alisema Venus. Picha hapo juu wanaonekana, madada mgogo Serena Williams kulia na mkubwa Venus Williams, wakiwa wameshikilia vikombe vya ubingwa wa tenisi kwa upande wa wanawake, baada ya kushinda (DOUBLES) wawili kwa wawili hapo miaka ya nyuma nchi Uingereza. Korea ya Kaskazini, yazidi kutunisha misuri kwa jumuia ya Kimataifa. Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 02/07/09.Kora ya Kusini, imerusha makomora ya masafa mafupi hivi karibuni. Kwa mijibu wa Yanhap, shirika la utangazaji, limesema, makombora hayo yalirushwa kuelekea upande wa mashariki ya pwani. Makombora ambayo yallirushwa nia nchi kavu , hewani kuelekea kwenye melikebu. Makombora hayo yanajulikana kama, Silkwom. Kurushwa kwa makombora hayo, kumeweka hali ya wasiwasi katika eneo zima, hasa kati ya Korea ya Kusini na Korea ya Kaskazini. Picha hapo juu, nia moja ya michongo ya makombora yakiwa yamewekwa kama minara kwenye sehemu moja ya mji, nchini Korea ya Kaskazini. Binti aliyepona katika ajali ya ndege, akutana na baba yake.

Paris, Ufaransa - 02/07/09. Baba ya msichana aliyepona katiaka ajaili ya ndege ya shirka la Yemen,amempokea binti yake, Bahia Bakari, wakati alipo wasili nchini Ufaransa baada ya kupata matibabu ya kwanza nchini Komoro.
Binti huyu, Bahia Bakari, ndiye abiria pekee, aliye jaliwa kuwa hai katika jali hiyo.
Ndege aina ya Airbus, ilianguka siku ya jumanne alfhajiri katika bahari ya Indi wakati ikitokea, Sanaa Yemen kuelekea visiwa vya Komoro.
Picha, hapo juu wanaoneka,Kassim Bakari, babaya Bahia Bakari, akiwa ameshikilia, binti yake, huku wakiwa njiani kuelekea hospital, mapema alipo wasili Paris.
Picha ya pili ni ya shrika la ndege la Yemen,ambapo moja ya ndege yake, ilianguka siku ya jumanne alfhajiri.
Umoja wa mataifa wapata mkurugenzi mkuu mpya wa kusimamia atomi na nyuklia.
Viena , Austria - 02/07/09. Shirika la Umoja wa Mataifa linalo shughulikia ukaguzi wa nguvu za atomi na nyuklia ( International Atomic Enegy Agency), limemchagua Yukiya Amano kuwa mkurugenzi wake mkuu, ili kushika nafasi itakayo achwa wazi na mkurugenzi wa sasa, Mohamed El Baradei kuanzia mwezi November 2009.
Katika uchaguzi, huo,Yukiya Amano, alimshinda mpinzani wake mkuu, Abdul Samad Minty, kutokea Afrika ya Kusini kwa kupata kura 35,kutoka kwa nchi wanchama.
Picha hapo juu, anaoneka Yukiya Amano,ambaye atashikia kiti cha ukurugenzi mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalo shughulikia ukaguzi wa nguvu za atomi na nyuklia,kuanzia mwezi wa November 2009.
Picha ya pili, wanaonekana, kushoto mkurugenzi mkuu wa sasa,Mohamed El baradei, akiwa na mkurugenzi mchaguliwa Yukiya Amano, wakati walipo pokea zawadi ya nishani ya Nobel nchini Norway mwaka 2005.

Monday, June 29, 2009

Kamati ya uchaguzi Iran, rais,Mahmoud Ahmadinejad,badao ni mshindi.

Chaji za simu kuwa za aina moja kiviwango. Brussels, Ubeligiji - 29/06/09. Kampuni zilazo shughulikia, utengenezaji wa simu, zimekubaliana kwa pamoja kuanza kutengeneza chaji za aina moja, kwa ajili ya matumizi ya simu zote. Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya ofisi inayaoshughulikia, maswala ya mawasialiano katika nchi za jumuia ya Ulaya, zimesema ya kuwa kampuni za Nokia ,Motorola, Sumsung, Sony Ericsson., Apple,na LG, ambazo zina tengeneza simu na kutukiwa na wakazi wa Ulaya, zimekubaliana na kamati ya mawasiliano kwa kukubaliana kutengeneza chaji zitakazo tumika kwa kiwango kimoja. Kwa mujibu, wa habari hizi , kuanza kutumika kwa chaji hizi mpya, kuaanza mapema mwakani. Picha hpo juu, zimnaonekana, aina tofauti za chaji , ambazo hutumika kwa simu tofauti,na huwa zinaleta matatizo kwa watumiaji wa simu katika nchi Ulaya. Millionea ahukumiwa kwenda jera miaka 13 nchini Urussi. Moscow, Urussi, -29/06/09. Mahakama mjini Moscow, imemuhukumu, milionea Boris Berezovsky kwenda jela miaka 13, baada ya kukutwa na hatia ya kulaghai kwa kujipatia kiasi cha $million kutoka kwa kampuni ya Avtovaz. Boris Berezovsky,alihukumiwa, wakati yeyemwenyewe hakuwepo mahakamani. Mtuhumiwa huyo, Boris Berezovsky, anaishi ukimbizini nchi Uingereza. Picha hapo juu, anaonekana, Boris Berezovsky,akiingia ndani ya gari, ambapo kuonekana kwake huwa nadra saana.

Kamati ya uchaguzi Iran,rais, Mahmoud Ahmadinejad bado ni mshindi.
Tehran, Iran - 29/06/09. Kamati inayosimamia uchaguzi nchini Iran, imetoa matokeo ya kura zilizo hesabiwa upya na kusema ya kuwa rais, Mahmoud Ahmadinejad, mchaguliwa, ameshinda kwa kura nyingi na kusisitiza ya kuwa hata kura ambazo zimehesabiwa hivi sasa bado zina mpa kura nyingi rais.
Kura hizo za asilimia kumi,ambazo ndizo zilizodaiwa kuwa hazikuhesibiwa na kuleta utata.
Hata hivyo, wapinza ambao walikuwa wanagombea kiti hicho cha urais, waligomea uchaguzi kwa kudai ya kuwa kulikuwa na matatizo ya kura katika mahesabu yake.
Picha hapo juu, anaonekna rais, wa Iran, Mohmoud Ahmadinejed, akiongea katika moja ya mikutana , mara baada ya kutangazwa matokeao ya uchaguzi na kumpa ushindi mkubwa.
Picha ya pili wanaonekana, baadhi ya watu wakiandamana kupinga matokeo ya uchaguzi, kwa madai ya kuwa kura zao hazikuhesibiwa.
Rais aomba ukimbizi,baada ya mapinduzi.
Honduras,Tegucigalpa - 29/06/09.Rais mpya aliyeapishwa nchini Honduras, Roberto Micheletti, kuchukua nafasi ya rais, Manuel Zelaya, ambaye yupo ukimbizini Kosta Rica.
Kufuatiwa kupinduliwa kwa rais, Emanuel Zelaya, baada ya rais huyo, kukataa kumrudisha kazini amir jeshi mkuu, ambaye alimfukuza kazi.
Kupinduliwa kwa, rais wa Honduras, Emanuel Zelaya, kumelaniwa na umoja wa mataifa.
Picha hapo juu, anaonekana, rais Emanuel Zeyala, ambaye yupo ukimbizini Kosta Rica.
Picha ya pili, anonekana, rais mpya wa Homduras, Micheletti, akiapishwa kuwa rais wa Honduras.
Picha ya tatu,kinaonekana , kifaru cha jeshi kikiwa mbele ya ikulu,kulinda serikali mpya ya rais, Robert Michelitti.
Aliyetikisa wawekezaji kutumikia kifungo miaka 150.
New York, Amerika - 29/06/09. Mahakama ya jijini, New York , imemuhukumu miaka 150 kwenda jela,Bernard Madoff,aliyekuwa mwenyekitia wa Nasdaq soko la wawekezaji na wabadishaji lililopo jijini New York.
Hukumu hiyo, ilitolewa na jaji Danny Chin, baada ya Bernadr Madoff, kukili kosa lake, la kuwatapeli mamia ya wawekezaji, wakiwepo watu mashuhuri kutoka ,Hollywood, wastaafu,na wafanya biashara wengine.
Kutolewa kwa hukumu hiyo, kunaaminika kutajaribu kupunguza jazba au machungu waliokuwa nayo wale wote waliotapeliwa na Bernard Madoff.
Pichani hapo juu, anaonekna Bernard Madoff, akielekea mahakamani ,huku paparazzi wakiwa kazini kupata picha za kumbukumbu.

Friday, June 26, 2009

Mfalme wa Muziki wa Pop atutoka,MUNGU BABA TUNAKUOMBA UILAZE ROHO YA MICHAEL JACKSON PEPON.AMINA.

Mfalme wa Muziki wa Pop atutoka,MUNGU BABA TUNAKUOMBA UILAZE ROHO YA MICHAEL JACKSON PEPON.AMINA.

Picha ya familia ya Mzee Joseph Jaskson, akiwa na watoto wake, Jackon Five, wa kwanza kushoto ni Michael Jackson, ambaye alikuwa ndiye nyota katika kundi zima la musiki wa Jackson 5.

Michael Jackson, alikuwa na umri wa miaka 50.

Los Angeles, Amerika - 26/06/09.Wapenzi wa Muziki Duniani twapigwa na wingu zito.
Picha zilizopo hapo juu, zineleza ni jinsi gani, marehemu Michael Jackson,alivyo pendwa kutokana ma kubarikiwa kipaji na Mungu.
Mzee Joseph Jackson, baba, ya Michael Jackson, alikuwa anampenda mwanae Michael ,kwa hali na mali, hapo anaonekana kwenye picha ya tano, akiwa ameshikilia moja ya CD(Album) ambayo ina picha ya Michael Jackson na ndani ya CD hiyo kuna nyimbo za Michael jackson.
Hamas yasema taifa la Israel hapana.
Damascus, Syria 26/06/09.Kiongozi wa Hamas,Khaled Mashaal, amesema Hamas, haitalitambua taifa la Israel.
Kiongozi huyo wa Hamas, Khaled Mashaal, aliyasema haya, siku ya Alkhamisi, mbele ya wanachama na wadau katika mkutano wa Hamas nchini Syria, ambapo kunawanachama na wadau wengi wa Hamas.
Hata hivyo, kiongozi huyo alikubaliana na mpango wa kuwa na mataifa mawili, ikiwa kutazingzatiwa makubaliano ya mwaka 1967 na Jerusalem mji mkuu.
Picha hpo juu, anaonekana, kiongozi wa Hamas, Khaled Mashaal, akihutubia mamia wanachama wa Hamas siku ya Alkhamis.
Serikali ya Somali kupata msaada kutoka Amerika.
Washington, Amerika - 26/06/09.Serikali ya Somalia ina karibia kupata msaada wa kijeshi kutoka serikali ya Amerika, ili kukabiliana na makundi yanayo pingana na serikali.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana,kutoka serikali ya Amerika,zina sema ya kuwa ipo haja ya kuisaidia serikali ya Somali, inyo ongozwa na Shariff Shabab.
Ili kukabiliana na hali ya hatari iliyopo nchi Somali, hasa Mogadishu, serikali ya Somalia, imetangaza hali ya hatari siku ya jumatatu katika jiji hilo.
Picha hpo juu, anaonekana, mmoja wa wapiganaji wa kundi la Al Shabab, akishambulia moja ya mitaa mjini Mogadishu.
Uturuki ipo karibu kuanza mazungumzo na muungano wa Ulaya.
Brussels, Ubeligiji - 26/06/09. Waziri mkuu wa Uturuki,Recep Tayyip Erdogan, amesema ya kuwa nchi yake, inampango wa kuanza upya mazungunzo ya kujiunga na muungano wa Ulaya.
Waziri, Recep Tayyip Erdogan, aliyasema haya, wakati alipo kuwa nchini Ubelingiji kwa mazungumzo na viongozi wa jumuia ya muungano wa nchi za Ulaya.
Hata hivyo, Uturuki imekuwa na wakati mgumu kujiunga na jumuia ya nchi za Ulaya kwa kuto kukubali kuitambua Syipras(Cyprus) na katiba yake, nakushinda kushirikiana kikamilifu na Ugiliki katika swala zima la Cyprus.
Picha hapo juu, wanaonekana, waziri mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, akisalimiana na Olli Rehn, mkuu anaye shughulika kujiunga na Muungano wa nchi za ulaya, walipo kutana Brussels siku ya Ijumaa.
Waandamanaji na viongozi wao wawekwa karibu na kiti moto nchini Iran.
Tehran, Iran - 26/06/09.Mmoja wa viongozi wa kidini nchini Iran,Ahmad Khatami, amesema ya kuwa wale watu wote ambao wanaandamana kupinga matokeo ya uchaguzi ya juni 22, ni lazima waadhibiwe vikali.
Ayatollah, Ahmad Khatami, ambaye ni mbuge katika kamati ya wabunge teule, ameagiza kwa kusema ya kuwa viongozi waliosababisha au kusimamia maandamano lazima waadhibiwe ili wawe mfano kwa wengine.
Ayatollah, Ahmad Khatami, aliyasema hayo wakti wa swala ya Ijumaa,na kutangazwa na radio moja kwa moja.
Picha hapo juu, anaonekana, Ayatollah, Ahmad Khatami, akiwahutubia maelfu waliokusanyika katika ukumbi wa chuo kikuu cha Tehren siku ya Ijumaa baada ya swalat Ijumaah.
Picha ya pili wanaonekana , watu walioudhulia swalat Ijuma, wakishangilia na kukubaliana na Ayatollah, Ahmad Khatami kwa yale anayo yaongea.

Tuesday, June 23, 2009

Urussi yatamka kushirikiana kuhusu swala la mashariki ya Katu

Wapigania uhuru kuishitaki Uingereza.

London,Uingereza - 23/06/09.Wapigania uhuru watano wa Kenya ambao walikuwa kundi la Maumau, wamefungua kesi ya mashitaka zidi ya serikali ya Uingereza kwa kuvunja haki za binadamu wakati wa utawala wa kikoloni wa Uingereza ulipo kuwa ukitawala miaka ya 60 kurudi nyuma.
Wapigania uhuru hao ambao wanamiaka kati ta 70 na 80. wanadai ya kuwa serikali ya Uingereza inatakiwa kulipa fidia na kuomba msamahaa kwa matendo yaliyo fanywa na Uingereza wakati Inaitawala Kenya.
Msemaji wa wapigania uhuru hao, Gitu wa Kahengeri, alisema wanafanya hivyo kwa ajili ya wapigania uhuru wenzao, wa kundi la Mau mau ambao walipoteza maisha kwa ajili mya kutetea uhuru.
Hata hivyo serikali ya Uingereza, imedai ya hali halisi ilipewa serikali ya Kenya baada ya kupata uhuru.
Picha hapo juu, ni ya bendera ya Kenya, nchi ambayo ilikuwa chini ya utawala wa Uingereza hadi ilipo pata uhuru 1963.
Picha pili, wanaonekana, baadhi ya wapigania uhuru wa mau mau wakiwa chini ya ulinzi, ambao wengi wao walipoteza maisha wakati wa kutetea uhuru wa nchi yao
Urussi yatamka kushirikiana na Misri kuhusu swala la Mashariki ya Kati.
Kairo, Misri-23/06/09.Rasi wa Urussi, Dmitri Medvedev, yupo nchini Misri kwa ziara ya kiserikali. Katika ziara hiyo, rais,Medvedev, amekutana na rais wa Misri, Hosni Mubaraka, kuzungumzia swala zima la mashariki ya kati. Picha hapo juu, wanaonekana marais wa Urussi na Misri wakiwa katika mazungumzo, wakati rais,Dmitri Medvedevwa Urussi alipo kutana na rais, Hosni Mubaraka wa Misri. Israel ya mwachia kiongozi wa Hamas.
Jerusalem,Israel- 23/06/09.Serikali ya Israel imemwachia huru spika bunge wa Hamas bwana, Abdul Aziz Dweik, baada ya kukaa miaka mitatu jela kwa kuso la kujihusisha na kundi hilo ambalo linamshikilia, Gilat Shalit.
Pichani hapo juu, anaoneka bwana, Abdul Aziz Dweik, akitolewa pingu na polisi kabla ya kuwa huru.
Picha pili anaonekana,Abdul Aziz Dweik, akitabasamu kabla ya kutoka kizimbani kuelekea nyumbani.

Tuesday, June 16, 2009

Rais wa zamani wa Amerika atembelea Gaza.

Wananchi wa Niger, kupiga kura ya maoni ya hatma ya urais. Niamey, Niger 16/06/09. Maelfu ya wanchi Niger, wameandamana kudai ya kuwa rais,Mamadou Tandja, aliyepo madarakani,asibadilishe katiba, ili aweze kugombea tena kiti cha uchaguzi kwa mara ya tatu. Maandamano hayo, nayamefanywa kufatia kupangwa tarehe ya kupiga kura ya maoni 4/Agusti,ikiwa kama rais Mamadou Tandaja ataweza endelea kugombea kiti cha uraisi. Rasi, Mamadou Tandja, anatarajiwa kumaliza muda wake wakuongoza nchi hivi karibuni. Picha hapo juu, anaonekana, rais Mamadou Tandja, akiwa katika moja ya mikutano ya kimataifa.

Makamu wa rais wa Kongo DRC, afunguliwa mashitaka.
Hague, Holland - 16/06/09. Mahakama inayo shughulikia kesi za kimataifa za jinai na maafa yanayo sabaishwa na vita, imemfungulia kesi makamu wa rais wa Kongo (DRC), Jean - Pierre Bemba, ya kuhusika na vita nchini Kongo na kusababisha kuvunjwa kwa haki za binadamu wakati wa vita vilivyo tokea kati ya mwishoni mwa mwaka 2002 hadai mwanzoni mwa mwaka 2003
Kwa mujibu wa mwanasheria wa mahakama alidai ya kuwa Jean Piere Bemba, alikuwa ana fahamu yote yaliyo tokea.
Hata hivyo mwanasheria anayemtete bwana, Bemba , amesema yakuwa, mteja wake hakuhusika na wala alikuwa hajui nini kilichokuwa kinaendelea, hii ni yote ninakuja kutokana na mrindimo wa siasa.
Rais wa zamani wa Amerika,atembelea Gaza.
Gaza,Ukingo wa mto Magharibi - 16/06/09.Rais wa zamani wa Amerika, Jimmy Carter,ametembela maeneo yaliyo shambuliwa na Israel mwishoni mwa 2008 na mapema mwaka huu 2009, na kusema yakuwa imestua saana.
Bwana, Carter, alisema ya kuwa mstuko huo, unaonyesha ni jinsi gani, Wapalestina wanavyo fanywa kama siwatu, na kuagiza ya kuwa kuna haja ya Wapalestina kupata haki kama watu wengine.
Picha hapo juu, wanaonekana, rais wa zamani wa Amerika, Jimmy Carter,na kiongozi wa Hamas,Ismail Haniyeh,kulia wakitembea kuelekea ofisini, kabla ya kuongea na waandishi wa habari.
Picha ya pili, wanaonekana, rais wazamani wa Amerika, Jimmy Carter kushoto na kulia kiongozi wa Hamas, Ismail Haniayeh, wakiongea na waandishi wa habari.
Kamati yaamua kura kuhesabiwa upya.
Tehran, Iran - 16/06/09.Kamati iliyo simamia uchaguzi wa urais wa Iran,imetangaza yakuwa watatizama kiundani na kuanza kuziehesabu kura upya.
Hata hivyo, Mir Hussein Mousavi, ambaye ameshindwa katika uchaguzi huu, ametaka kura zipigwe upya, swala ambalo kamati iliyo simamia uchaguzi imelikataa.
Mvutano huo wa matokeo ya kura,yameleta wasiwasi wa kisiasa nchini Iran, jambo ambalo linaufanya uongozi wa Iran, chini ya Ayatollah Ali Khamenei kuwa na wakati mgumu.
Picha hapo juu, ni picha ya rais,Mahamoud Ahamdinejad katikati, akiwasiri nyumbani,baada ya kukatiza ziara yake ya kikazi nchini Urussi.
Picha ya pili, anaonekana, Ayatollah Ali Khamenei, ambaye uongozi mkuu wa Iran,ambaye Iran inategemea uwezo wake.