Urussi na Amerika zakubaliana kushirikiana katika swala la nyuklia.
Moscow, Urussi - 06/07/09. Urussi na Amerika zimekubaliana kupunguza siraha za nyuklia, wakati marais wa nchi hizo walipo kutana leo siku ya jumatatu jijini Moscow.
Makubaliano hayo,yamefanyika wakat Rais wa Amerika , baraka Obama, akiwa ziarani Urussi, kuongea na viongozi wa Urussi,ili kudumisha uhusiano, ambao ulikuwa umeingia utata, baada ya Amerika kutaka kuweka makombo yake katikati mwa Ulaya, kwa kudai ni kaajili ya kulinda mashambulizi ambayo yanaweza kutokea Iran au Korea ya Kaskazini, lakini Urussi ilililikataa jambo hilo na likazusha mgogoro.
Picha hapo juu, wanaonekana rais wa Amerika, Baraka.H.OBama, akiongea na rais wa Urussi Dmitri . A. Medvedev wakati walipo kutana kwa mazunguzo ya kikazi jijini Moscow.
Monday, July 6, 2009
Posted by
Kibatala
at
Monday, July 06, 2009
0
comments
Sunday, July 5, 2009
Serena na Venus Williams Malkia wa tenis wa Wimbledon 2009.
Serena na Venus Williams, Malkia wa tenis wa Wimbledon 2009.
Wimbledon, Uingereza 05/07/09. Kwa mara nyingine tena, Serena na dada yake Venus, wameweza kushinda mchezo wa tenis kwa wanawake na kuchukua kikombe cha Wimbledon kwa ushindi wa seti 7-6, 6-4 zidi ya Samantha Stosur na Rennae Stubbs.
Wimbledon Uingereza - 05/06/07.Roger Federer, ameshinda kombe la Wimbledon katika mchezo wa tenis , na kuweka rekodi ya kuwa ushindi wa mashindano makubwa ya tenis kwa mara ya 15.
Moscow Urussi -05/07/09. Rais wa Urussi, Dimirti Medvedev, atakuwa mwemyeji wa rais wa Amerika, Baraka Obama hivi karibuni, ili kuzidi kuimarisha uhusiano wa karibu.
Tripol Libya - 04/07/09. Kikao cha viongozi wa Afrika kimamua kwa pamoja ya kuwa nchi za Afrika hazita husika katika kumkamata au kumkamata rais wa Sudan, Omar Al - Bashir.
Posted by
Kibatala
at
Sunday, July 05, 2009
1 comments
Thursday, July 2, 2009
Binti aliyepona katika ajali ya ndege akutana na baba yake.
Historia na ndoto za Williams za jirudia nchini Uingereza.
Wimbledon, Uingereza - 02/07/09. Historia ya mchezo wa tenisi, imejirudia tena, baada ya ndugu wawili mkubwa na mdogo,kukutana tena katika fainali ya kugombea kikombe cha Wimbledon.
Ndugu hao , mabao pia ni Dada mdogo Serena Williams na dada mkubwa Venus Williams, watakutana mara ya kibarua kigumu cha kupambana na kushinda michezo yote ya tenisi kwa upande wa wanawake, kutoka hatua ya mwanzo hadi kufikia kukutana fainali.
Katika, mchezo wa nusu fainali, Serena aliweza kumshinda, Elena Demetieva kwa seti 7-5,8-6, japo kayika seti ya kwanza Serena alishindwa kwa seti 6-7.
Naye dada Venus, alishinda , bila huruma Dinara Safina kwa seti 6-1,6-0.
Kufuatia ushindi wa madada hawa, Venus na Serena , ambao wanazaliwa na mama na baba mmoja, kumewafanya wakutane tena katika fainali ya Wimbledon kwa mara ya nne.
Kukutana kwa madada hao,kunazidi dhihirisha ya kuwa ndoto zao walizo kuwa wakiziota miaka 20 iliyo pita kwenye mji walio kulia, Compton Califonia za kukutana kwenye fainali ya mashindano makubwa inakuja kila wanapo amua kufanya kazi ya ziada, alisema Venus.
Picha hapo juu wanaonekana, madada mgogo Serena Williams kulia na mkubwa Venus Williams, wakiwa wameshikilia vikombe vya ubingwa wa tenisi kwa upande wa wanawake, baada ya kushinda (DOUBLES) wawili kwa wawili hapo miaka ya nyuma nchi Uingereza.
Korea ya Kaskazini, yazidi kutunisha misuri kwa jumuia ya Kimataifa.
Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 02/07/09.Kora ya Kusini, imerusha makomora ya masafa mafupi hivi karibuni.
Kwa mijibu wa Yanhap, shirika la utangazaji, limesema, makombora hayo yalirushwa kuelekea upande wa mashariki ya pwani.
Makombora ambayo yallirushwa nia nchi kavu , hewani kuelekea kwenye melikebu.
Makombora hayo yanajulikana kama, Silkwom.
Kurushwa kwa makombora hayo, kumeweka hali ya wasiwasi katika eneo zima, hasa kati ya Korea ya Kusini na Korea ya Kaskazini.
Picha hapo juu, nia moja ya michongo ya makombora yakiwa yamewekwa kama minara kwenye sehemu moja ya mji, nchini Korea ya Kaskazini.
Binti aliyepona katika ajali ya ndege, akutana na baba yake.
Viena , Austria - 02/07/09. Shirika la Umoja wa Mataifa linalo shughulikia ukaguzi wa nguvu za atomi na nyuklia ( International Atomic Enegy Agency), limemchagua Yukiya Amano kuwa mkurugenzi wake mkuu, ili kushika nafasi itakayo achwa wazi na mkurugenzi wa sasa, Mohamed El Baradei kuanzia mwezi November 2009.
Posted by
Kibatala
at
Thursday, July 02, 2009
0
comments
Monday, June 29, 2009
Kamati ya uchaguzi Iran, rais,Mahmoud Ahmadinejad,badao ni mshindi.
Chaji za simu kuwa za aina moja kiviwango.
Brussels, Ubeligiji - 29/06/09. Kampuni zilazo shughulikia, utengenezaji wa simu, zimekubaliana kwa pamoja kuanza kutengeneza chaji za aina moja, kwa ajili ya matumizi ya simu zote.
Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya ofisi inayaoshughulikia, maswala ya mawasialiano katika nchi za jumuia ya Ulaya, zimesema ya kuwa kampuni za Nokia ,Motorola, Sumsung, Sony Ericsson., Apple,na LG, ambazo zina tengeneza simu na kutukiwa na wakazi wa Ulaya, zimekubaliana na kamati ya mawasiliano kwa kukubaliana kutengeneza chaji zitakazo tumika kwa kiwango kimoja.
Kwa mujibu, wa habari hizi , kuanza kutumika kwa chaji hizi mpya, kuaanza mapema mwakani.
Picha hpo juu, zimnaonekana, aina tofauti za chaji , ambazo hutumika kwa simu tofauti,na huwa zinaleta matatizo kwa watumiaji wa simu katika nchi Ulaya.
Millionea ahukumiwa kwenda jera miaka 13 nchini Urussi.
Moscow, Urussi, -29/06/09. Mahakama mjini Moscow, imemuhukumu, milionea Boris Berezovsky kwenda jela miaka 13, baada ya kukutwa na hatia ya kulaghai kwa kujipatia kiasi cha $million kutoka kwa kampuni ya Avtovaz.
Boris Berezovsky,alihukumiwa, wakati yeyemwenyewe hakuwepo mahakamani.
Mtuhumiwa huyo, Boris Berezovsky, anaishi ukimbizini nchi Uingereza.
Picha hapo juu, anaonekana, Boris Berezovsky,akiingia ndani ya gari, ambapo kuonekana kwake huwa nadra saana.
Tehran, Iran - 29/06/09. Kamati inayosimamia uchaguzi nchini Iran, imetoa matokeo ya kura zilizo hesabiwa upya na kusema ya kuwa rais, Mahmoud Ahmadinejad, mchaguliwa, ameshinda kwa kura nyingi na kusisitiza ya kuwa hata kura ambazo zimehesabiwa hivi sasa bado zina mpa kura nyingi rais.
Honduras,Tegucigalpa - 29/06/09.Rais mpya aliyeapishwa nchini Honduras, Roberto Micheletti, kuchukua nafasi ya rais, Manuel Zelaya, ambaye yupo ukimbizini Kosta Rica.
New York, Amerika - 29/06/09. Mahakama ya jijini, New York , imemuhukumu miaka 150 kwenda jela,Bernard Madoff,aliyekuwa mwenyekitia wa Nasdaq soko la wawekezaji na wabadishaji lililopo jijini New York.
Posted by
Kibatala
at
Monday, June 29, 2009
0
comments
Friday, June 26, 2009
Mfalme wa Muziki wa Pop atutoka,MUNGU BABA TUNAKUOMBA UILAZE ROHO YA MICHAEL JACKSON PEPON.AMINA.
Mfalme wa Muziki wa Pop atutoka,MUNGU BABA TUNAKUOMBA UILAZE ROHO YA MICHAEL JACKSON PEPON.AMINA.
Picha ya familia ya Mzee Joseph Jaskson, akiwa na watoto wake, Jackon Five, wa kwanza kushoto ni Michael Jackson, ambaye alikuwa ndiye nyota katika kundi zima la musiki wa Jackson 5.
Michael Jackson, alikuwa na umri wa miaka 50.
Damascus, Syria 26/06/09.Kiongozi wa Hamas,Khaled Mashaal, amesema Hamas, haitalitambua taifa la Israel.
Washington, Amerika - 26/06/09.Serikali ya Somalia ina karibia kupata msaada wa kijeshi kutoka serikali ya Amerika, ili kukabiliana na makundi yanayo pingana na serikali.
Brussels, Ubeligiji - 26/06/09. Waziri mkuu wa Uturuki,Recep Tayyip Erdogan, amesema ya kuwa nchi yake, inampango wa kuanza upya mazungunzo ya kujiunga na muungano wa Ulaya.
Tehran, Iran - 26/06/09.Mmoja wa viongozi wa kidini nchini Iran,Ahmad Khatami, amesema ya kuwa wale watu wote ambao wanaandamana kupinga matokeo ya uchaguzi ya juni 22, ni lazima waadhibiwe vikali.
Posted by
Kibatala
at
Friday, June 26, 2009
0
comments
Tuesday, June 23, 2009
Urussi yatamka kushirikiana kuhusu swala la mashariki ya Katu
Wapigania uhuru kuishitaki Uingereza.
Kairo, Misri-23/06/09.Rasi wa Urussi, Dmitri Medvedev, yupo nchini Misri kwa ziara ya kiserikali.
Katika ziara hiyo, rais,Medvedev, amekutana na rais wa Misri, Hosni Mubaraka, kuzungumzia swala zima la mashariki ya kati.
Picha hapo juu, wanaonekana marais wa Urussi na Misri wakiwa katika mazungumzo, wakati rais,Dmitri Medvedevwa Urussi alipo kutana na rais, Hosni Mubaraka wa Misri.
Israel ya mwachia kiongozi wa Hamas.
Jerusalem,Israel- 23/06/09.Serikali ya Israel imemwachia huru spika bunge wa Hamas bwana, Abdul Aziz Dweik, baada ya kukaa miaka mitatu jela kwa kuso la kujihusisha na kundi hilo ambalo linamshikilia, Gilat Shalit.
Posted by
Kibatala
at
Tuesday, June 23, 2009
2
comments
Tuesday, June 16, 2009
Rais wa zamani wa Amerika atembelea Gaza.
Wananchi wa Niger, kupiga kura ya maoni ya hatma ya urais.
Niamey, Niger 16/06/09. Maelfu ya wanchi Niger, wameandamana kudai ya kuwa rais,Mamadou Tandja, aliyepo madarakani,asibadilishe katiba, ili aweze kugombea tena kiti cha uchaguzi kwa mara ya tatu.
Maandamano hayo, nayamefanywa kufatia kupangwa tarehe ya kupiga kura ya maoni 4/Agusti,ikiwa kama rais Mamadou Tandaja ataweza endelea kugombea kiti cha uraisi.
Rasi, Mamadou Tandja, anatarajiwa kumaliza muda wake wakuongoza nchi hivi karibuni.
Picha hapo juu, anaonekana, rais Mamadou Tandja, akiwa katika moja ya mikutano ya kimataifa.
Hague, Holland - 16/06/09. Mahakama inayo shughulikia kesi za kimataifa za jinai na maafa yanayo sabaishwa na vita, imemfungulia kesi makamu wa rais wa Kongo (DRC), Jean - Pierre Bemba, ya kuhusika na vita nchini Kongo na kusababisha kuvunjwa kwa haki za binadamu wakati wa vita vilivyo tokea kati ya mwishoni mwa mwaka 2002 hadai mwanzoni mwa mwaka 2003
Gaza,Ukingo wa mto Magharibi - 16/06/09.Rais wa zamani wa Amerika, Jimmy Carter,ametembela maeneo yaliyo shambuliwa na Israel mwishoni mwa 2008 na mapema mwaka huu 2009, na kusema yakuwa imestua saana.
Tehran, Iran - 16/06/09.Kamati iliyo simamia uchaguzi wa urais wa Iran,imetangaza yakuwa watatizama kiundani na kuanza kuziehesabu kura upya.
Posted by
Kibatala
at
Tuesday, June 16, 2009
0
comments

