Wednesday, June 23, 2010

Rasi Obama amteua mkuu wa majeshi mpya kuongoza NATO

Rais Obama amteua mkuu wa majeshi mpya kuongoza NATO.

Washington,USA - 23/06/2010. Rais wa Amerika Baraka Obama, ametangaza kujiudhulu kwa General Stanley McChrystal kuwa kiongozi mkuu wa majeshi ya NATO na kumteua General David Petraeus kuchukua nafasi yake.
Kutangazwa huko kunakuja baada ya General McChrystal kushutumu uongozi wa serikali ya USA kwa kuwa na myumbo katika kuendeleza vita nchini Afghanistan.
General Mc Chrystal aliyasema hayo wakati alipofanya mazungumzo na mahojiano na gazeti la Rolling Stone.
Rais Baraka Obama, alisema kujiudhuru huko kwa General McChrystal, hakuta badilisha msimamo wa USA nchini Afghanistan kupambana na kundi la Taliban. Picha hapo juu anaonekana General Stanley McChrystal akielekea ofisi za Ikulu ya Amerika kunana na rais Baraka Obama.
Picha ya pili anaonekana rais wa Amerika Baraka Obama akielekea kutangaza kujiudhulu kwa General Stanley McChrystal, na nyuma anaonekana General David Petraeus akimfata rais kumtangaza rasmi kuwa kiongozi wa majeshi ya NATO.

Meli ya siraha yazuiliwa nchini Sypras.

Meli ya siraha yazuiliwa nchini Sypras. Nikosia,Syipras - 23/06/2010. Serikali ya Syipras imeizuia meli ijulikanayo kama Santiago ambayo inasadikiwa kubeba siraha kuelekea nchini Sudani. Waziri wa biashara Antonis Passchalides alisema, vifaa vilivyopo kwenye meli hii lazima vifanyiwe uhakiki. Uamuzi wa serikali ya Sypras kuzuia meli kufuatia vikwazo vilivyo wekwa zidi ya Sudan. Picha hapo juu inaonekana meli ambayo imezuiliwa nchini Sypras.

Saturday, June 12, 2010

Afrika ya ikaribisha dunia"Soka, Kombe la dunia

Afrika ya ikaribisha dunia "Soka, Kombe la duni."

Johannesburg, Afrika ya Kusini-12/06/2010. Mashindano ya kugombea kombe la dunia la mpira wa miguu yameanza rasmi nchini Afrika ya Kusini.
Mashindano hayo mbayo kwa mara ya kwanza yana fanykia barani Afrika tangi kuanzishwa yarifunguliwa rasmi na raia wa Afrika ya Kusini Jakob Zuma na kuhudhuliwa na wageni waalikwa wakunchi,viongozi wa bara la Afrika na dunia nzima.
Picha hapo juu wanaonekana wachezaji wa timu ya taifa ya Afrika ya Kusini wakimenyana vikali na timu ya taifa ya Mexico katika mechi ya kwanza ufunguzi wa mashindano la kombe la dunia.
Picha ya pili wanaonekana rais wa FIFA Sept Platt na raia wa Afrika ya Kusini Jakob Zuma wakiwasalimia wananchi mara baada ya ufunguzi wa mashindano ya kombe la dunia.
Picha ya tatu wanaonekana maelfu ya watu walioudhulia kwenye sherehe za ufunguzi wa kombe la dunia jiji Johannesburg Afrika ya Kusini.
Picha ya nne anaonekana mmoja ya wanachi wa Afrika ya Kusini akiwa ameinyanyua juu bendera ya Afrika ya Kusini nchi ambayo kwa mara ya kwanza imekuwa mwenyeji wa mashindano ya kombe la dunia katika bara la Afrika.
Mchungaji haukumiwa kifungo cha maisha.
Helsink, Finland-13/06/2010. Mahakama nchini Finland imemkuta na hatia Francois Bazaramba kwa kuhusika na mauaji ya kimbari yaliyo tokea nchini Rwanda 1994 na kumuhukumu kifungo cha maisha.
Francoi Bazaramba 59, ambaye alikuwa mchungaji amekutwa na kosa la kushirikiana watu wa jamii ya Kihutu katika mauaji wakati akiwa kiongozi wa dini.
Hata hivyo Francoi alikanana mashitaka hao, na wakili wake amesema watakata rufaa.
Pichani hapo juu anaonekana Francois Bazaramba akiwa mahakamani akisikiliza hukumu ya kesi yake.

Wednesday, June 9, 2010

Iran yaongezewa vikwazo.

Iran yaongezewa vikwazo.

New-York, Amerika- 09/06/2010. Kamati ya usalama ya umoja wa mataifa imepitisha makubaliano ya kuwekewa vikwazo kwa serikali ya Iran.
Mswaada huo ambao ulipitishwa kwa kura 12 na mbili kupinga mswaada huo na moja kutopiga kura. Nchi ambazo zilipinga mswaada huo ni Brazil na Uturuki nchi ambazo ziliongoza mazungumzo na kuifanya Iran kukubali kuruhusu baadhi ya madini yanayo timika kutumika kuzalisha nguvu za nyuklia.
Hata hivyo serikali ya Iran imekilaani kitendo hicho na kusema, "Hatuta hathirika na vikwazo hivyo kwa kuto kuendelea na mpango wetu wa kuendeleza nyuklia ya kisayansi."
Picha hapo juu wanaonekana wanasayansi wa Iran wakiwa wanajadili maendeleo ya mitambo ya kuzalisha nguvu za nyuklia.
Picha ya pili wanaonekana wajumbe wa kamati ya usalama ya umoja wa mataifa wakiwa katika mkutano kujadili mswaada wa Iran.

Friday, June 4, 2010

Mafua ya nguruwe yaleta saga WHO

Mafua ya nguruwe yaleta saga WHO. London,Uingereza - 04/06/2010. Gazeti linalo toa ripoti za kiafya za binadamu nchini Uingereza limesama '' kunaukweli ya kuwa wataalamu wa liotoa habari za kuoenea kwa ugonjwa wa mafua ya nguruwe walizidisha vitisho katika kuelezea hatari ya ugonjwa huo.'' Kwa mijibu wa gazeti hilo lilisema ''yakuwa wataalamu hao walikuwa wanahisa katika uuzaji wa madaya ya kutibu na kukinga ugonjwa huo'' Ugonjwa huo unaojulikana kama H1N1 virus ulitishia dunia nzima hata kusababisha baadhi ya nchi kuingiwa na wasiwasi kwatumia pesa zaidi kununu madawa ya kutibu ugonjwa kwa wingi. Kuthibitisha hali hiyo kamati ya kiafya ya Ulaya melilaumu shirika la afya dunia WHO kwa kutofanya uhakiki wa habari wakati zilipo tolewa na wataalamu hao. Picha hapo juu wanaonekana badhi ya watu wakipata chanjo wakati wa kuvuma ugonjwa wa mafua ya nguruwe.

Tuesday, June 1, 2010

Uturuki ya laani vikali kitendo cha Izrael.

Umefikia afrika kuwa na kiti ndani ya UN. Nice,Ufaransa- 01/06/2010. Rais wa Ufaransa Nicalas Sarkozy amesema "umefika wakati wa bara la Afrika kuwa na kiti maalumu katika baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa." Rais, Sarkozy aliyasema hayo wakati alipo kutana na viongozi wa bara la Afrika kwa kusisitiza ya kuwa "hatuwezi kuongea habari za ulimwengu na dunia bila kuhusisha bara la Afriaka"

Mkutano huo ambao uliitishwa na Ufaransa, na kwa mara ya kwanza ulizishirikisha nchi zilizo kuwa makoloni ya Mwingereza ili kuzidisha uhusiano wa karibu na nchi za bara la Afrika.
Picha hapo juu wanaonekana viongozi kutoka bara la Afrika pamoja na rais wa Ufaransa, wakati walipomaliza mkutano na serikali ya Ufaransa ili kudumisha uhusiano.
Uturuki ya laani vikali kitendo cha Izrael.
Ankara, Uturuki-01.06/2010. Waziri mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, amelaani kitendo cha jeshi la Izrael ni la kinyama na yamefanywa kinyume cha sheria za kimataifa.
Akiongea na viongozi wa serikali na kutangazwa karibu dunia nzima na mashirika tofauti ya habari waziri mkuu huyo alisema, "Asitokee mtu kuijaribu uvumilivu wa Waturuki, kwani tuna heshimu marafiki, na kukosanana na Waturuki ni gharama kwa mtu huyo na hatuacha kuisaidia watu wa Gaza na tutazidi kukemea vitendo vya Izreal."
Waziri mkuu Recep Tayyip Erdogan, alikatisha ziara yake nchini Chile, mara baada ya tukio hilo kutokea.
Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, akihutubia kuhusu kitendo cha Waizrael kuvamia msafara wa misaada ya kibinadamu iliyo kuwa ikielekea Ukanda wa Gaza na kusababisha vifo na majeruhi katika msafara huo.
Picha ya pili anaonekana kijana mdogo akiwa amebebwa kwenye mabega wakati wa harakati ya kupinga kitendo cha Izrael kuvamia meli iliyo kuwa ilielekea Ukanda wa Gaza.
Al-Qaeda namba tatu asadikiwa kuuwawa.
Pakistan, Lahore - 01/06/2010. Jeshi la Amerika na washiriki wake wamesema, "wamefanikiwa kumua anayesadikiwa kuwa namba tatu wa kundi la Al-Qaeda Mustafa Abu al-Yazid au kwa majina mengine Sheikh Sa'íd al Masri."
Kuuwawa huku kwa Mustafa Abu al-Yazid kulitokea kaskazini mashariki mwa Pakistan, kwa shirikiana na majeshi shiriki.
Picha hapo juu anaonekana Mustafa Abu al Yazid, ambaye inasadikiwa aliuwawa wakati wamashambulizi yaliyo fanywa na jeshi la Amerika na washiriki wake hivi karibuni.

Monday, May 31, 2010

Izrael yasimamisha meli za misaada.

Izrael yasimamisha meli za misaada.

Tel-Aviv, Izrael- 31/05/2010. Makomando wa Kiizrael wamesimamisha meli iliyo beba misaada ambayo ilikuwa ikielekea kwenye Ukanda wa Gaza.
Katika harakati za kuizuia masafara wa meli Freedom Flotilla, watu wapatao kumi na tisa wamefariki dunia.
Kufuatia tukio hilo nchi nyingi zike kiaani kitendo hicho kwa kuitaka serikali ya Izrael itoe maelezo kwa undani kisa cha tukio hilo.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wauguzi wa jeshi la Izrael wakiwa wanamshusha mmoja wa majeruhi wakati wa kuzizuia meli ambazo zilikuwa zikielekea Ukanda wa Gaza.
Picha ya pili hapo juu wanaonekena baadhi ya wapiganaji wa Izrael wakiwa wanakagua meli ambayo waliisimamisha ililp kuwa ikielekea Ukanada wa gaza.
China yaingilia kati kuleta amani kwa Wakorea
Beijing, China- 31/05/2010. Serikali za China, Japan na Korea ya Kusini zimekutana ili kujadili njia mbadala ya kutuliza hali ya mchafuko ambayo ulizuka baada ya meli ya serikali ya Korea ya Kusini kuzama kwa madai ya kuwa serikali Korea ya Kaskazini ndiyo iliyo izamisha.
Hata hivyo serikali ya Korea ya Kaskazini ilikana kufanya kitendo hicho.
Picha hapo juu wanaonekana wanajeshi wa waliopo katika mpaka unao tenganisha Korea ya Kaskazini na Korea ya Kusini wakiwa kazini kulinda mipaka yao.

Monday, May 17, 2010

Iran yasahini mkataba na kuruhusu madini kinyuklia kurutubishwa Uturuki.

Iran yasahini mkataba na kuruhusu madini kinyuklia kurutubishwa Uturuki.

Tehran, Iran 17/05/2010. Ssrikali ya Iran imekubali na kutia sahii mkataba wa kusafirisha madini ya ambayo yanatumika kuzalisha na kurutubisha madini ya nyuklia kupelekwa nchini Uturuki kwa uzalishaji wa madini ya nyuklia.
Mkataba huo ambao ulishuhudiwa na viongozi wa Brazil na Uturuki.
Hata hivyo Amerika na nchini za Ulaya Magharibi zikiongozwa na Uingereza na Ufaransa zinasema yakuwa mkataba huo lazima usimamiwe na shirika la IAEA - International Atomic Energy Agency.
Picha hapo juu wanaonekana viongozi wa Uturuki kulia Recep Tayyip Erdogan,katikati ni rais wa Iran Mahmoud Ahmadinejad na rais wa Brazil kulia Lula Inacio da Silva wakati walipo kutana nchini Iran.

Friday, May 14, 2010

Swala la mto Nile lafikiwa muafaka na nchi nne.

Swala la mto Nile lafikiwa muafaka na nchi nne.

Kampala, Uganda - 14/05/2010. Serikali za nchi za Rwanda, Uganda, Ethiopia naTanzania zimetialiana sahii mkataba ili kuanza kuangalia ni kwa jinsi gani nchini hizi zitaanza kufaidika na malia asili ya mto Nile kwa manufaa ya nchi hizo na kutengua mkataba uliwekwa na ukoloni wa Uingereza mwaka 1929 ambapo Misri ilipewa haki ya kutumia maji ya mto huo kwa wingi kuliko nchi zote ambazo mto huo unatoka au kupita.
Wakiongea kwa nyakati tofauti mawaziri wa maliasili wa Ethiopia Asfaw Dingamo alisema " naamini hatimayake nchi zpte zitakubaliana kimsingi kuhusu swala zima la matumizi maji ya mto Nile."
Naye waziri wa maliasi wa Rwanda, Stansilas Kamanzi alisema " inasikitisha baadhi ya nchi ambazo mto una pita hazikuwepo kutokana na hali halisi ya swala lenyewe."
Kufuatia kitendo hicho, serikali ya Misriimepinga na kudai haikuwa haki na huenda ikachukua hatua za kisheria.
Picha hapo juu inaonyesha vyanzo vya mto Nile kutoka Afrika ya mashariki na kuishia nchini Misri.
Picha ya pili inaonyesha picha ya maji ya mto Nile ambayo yamekuwa yakitumiwa kwa njia mbalimbali na wanchi wa Misri kwa asilimia kubwa.
Rais wa Urussi akutana na kiongozi wa Hamas.
Dumuscas,Syria - 14/05/2010. Rais wa Urussi, Dmitry Medvedev amekutana na kiongozi wa kundi la Hamas aliyepo ukimbizini nchini Syria Khaled Meshaal wakati wa ziara yake aliyo ifanyanchini humo.
Kufuatia mkutano huo, ofisi za mambo ya nje ya Izrael zimesema"hazikufurahishwa na kitendo hicho."
Hata hivyo habari kutoka ofosi za serikali ya Urussi zinasema" kiongozi huyo huwa nakutana au kuwasialiana viongozi wengi wakiwemo wa serikali ya Amerika ila kutokana na sababu fulani huwa hawatangazwi kama walikutana au kuwasiliana na kiongozi huyo."
Picha hpo juu ni ya rais wa Urussi, Dmitry Medvedev, ambaye alikutana na kiongozi wa kundi la Hamas aliyepo ukimbizini nchini Syria.
Rais Obama, ataka muswada wa kutengenezwa mitambo ya ulinzi upitishwe.
Washington, Amerika - 14/05/2010. Rais wa Amerika Baraka Obama, amelitaka bunge la Congress kupitisha muswada wa pesa $205million kwa ajili ya kuisaidia Izrael kutengeneza mitambo ya kuzuia mashabulizi ya mabomu.
Mpango huo unao julikana kama "Iron Dome" utakuwa na mazumuni ya kuzuia mashambulizi kutokea nchini za jirani hasa Lebanon na Ukanda wa Gaza ambapo huwa mabomu mengi huwa yanarushwa upande wa Izrael kutokea sehemu hizo.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Amerika, Baraka Obama akiongea hivi karibuni kuhusu hali halisi ya Mashariki ya Kati.
Taliban wataka utawala wa Pakistan ung'olewe.
Karachi, Pakistan - 14/05/2010.Kiongozi mmoja wa kundi la Taliban liloponchini Pakistan Azam Tarik amelitaka kundi lake kuingusha serikali ya Pakistan na kusema ya kuwa nia na mipango ya Amerika haitafanikiwa.
Kiongozi huyo ambaye pia ni msemaji wa kundi hilo alisema "kundi lake halijahusika na milipuko ya mabomu iliyo tokea hivi karibuni katika maeneo yanayo kaliwa na raia, na ni mbinu za kutaka kulichafua kundi hilo."
Akisisitiza Azam Tarik, "hivi sasa umefika wakati wa kuwaondowa kwenye madaraka wale wote wanao shirikiana katika kupinga Uislaam na wananchi wa Pakistan."alimalizia kwa kusema.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Pakistan, Asif A Zardari, ambaye yupo madaraka na hali ya usalama wa Pakistani imekuwa nawakati mgumu kutona na tishio la kundi la Taliban.

Wednesday, May 12, 2010

Uingereza yapata serikali mpya ya shirikisho.

Uingereza yapata serikali mpya ya shirikisho.

London, Uingereza - 12/05/2010. Wananchi wa Uingereza wamepata viongozi wapya watakao iongoza serikali ya nchi hiyo baada ya makubaliano ya kimsingi kufikiwa kati ya chama cha Liberal Demokratik na Conservative.
Serikali hiyo mpya shirikisho itaongozwa na waziri mkuu mpya wa Uingereza David Cameron wa chama cha Conservative na makamu wa waziri mkuu atakuwa Nick Gregg wa chama cha Liberal Demokratik.
Picha hapo juu wanaonekana viongozi wapya wa serikali ya Uingereza, David Cameron kushoto akiwa na Nick Gregg kulia wakielekea kuingia ofisini kuanza kazi ya uongozi rasmi.
Picha ya pili, wanaonekana Nick Cregg kulia na David Cameron kushoto wakiwasalimia wananchi na waandishi wa habara mara baada ya kukubaliana kimsingi kuunda serikali ya shirikisho ya Uingereza.
David Miliband atangaza kugombea uongozi wa chama cha Labour.
London, Uingereza - 12/05/2010. Aliyekuwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza David Miliband ametangaza kugombe kiti cha uenyekiti cha cham cha Labour.
David Miliband ambaye ameshawahi kushika madaraka tofauti katika serikali iliyokuwa ikiongozwa na chama cha Labour kabla ya kuteuliwa kuwa waziri wa mabo ya nje wa Uingereza.
Picha hapo juu anaonekana David Miliband ambaye ametangaza kugombea uongozi wa chama cha Labour.
Picha ya pili anaonekana aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown akishuka kutoka kwenye gari baada ya kutoka kumwona Malkia wa Uingereza ya kuwa anaikabidhi serikali kwa chama cha Conservative na Libaral Demokratik.
Urusi na Uturuki kushirikiana kwa ukaribu.
Ankara, Uturuki - 12/05/2010. Serikali ya Urussi imetiliana sahii mkataba na serikali ya Uturuki wenye thamani ya $20 billion kwa ajili ya kujenga mitambo ya kinyuklia na miradi mingine.
Kwa mujibu wa wasemaji wa serikali zote mbili walisema "nchini hizo pia zimeondo visa kwa raia wa nchi hizo na kurahisisha shughuli nyingine za kujenga mahusiano kati ya nchi hizo mbili."
Picha hapo wanaonekana rais wa Urussi kulia Dmitry Medvedev na waziri mkuu wa Uturuki Tayyip Erdogon wakitia sahii mikataba kwaniaba ya nchi hizo mbili.
Ndege yaanguka na kuuwa abiria 103 nchini Libya.
Tripoli, Libya - 12/05/2010. Ngede iliyo kuwa ikitokea nchi Afria ya Kusini kuelekea nchini Libya imeanguka na kupoteza maisha ya watu 103 na kijana mmoja wa Kihollanzi ndiye aliye nusirika katika ajali hiyo.
Kwa mujibu wa habari zina sema "ndege hiyo ilianguka karibu na kiwanja cha ndege wakati inataka kutua."
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Afriqiya ilikuwa katika safari zake za kawaida kutoka jijini Johannesburg kuelekea jijini Tripoli.
Picha hapo juu yanaonekana mabaki ya ndege la Afriqiya ambayo ilianguka mapema alfajiri siku ya Jumatano ikitokea nchini Afrika ya Kusini.

Monday, May 10, 2010

Gordon Brown asema "Nangátuka madarakan."

Gordon Brown asema "Nangátuka madarakani."

London,Uingereza - 10/05/2010. Waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown amesema atajiudhuru uongozi katika chama chake cha Labour, na kuwaomba wanachama wenzake kujiandaa kumchagua kiongozi mwingine atakaye kiongoza chama cha Labour.
Akiongea mbele ya wandishi wa habari Gordon Brown alisema "nita jiudhuru uongozi wa chama ifikapo wa mwezi Septemba" Na kwa sasa kiongozi wa Liberal Demokratic, Nick Clegg,ameniambia ya kuwa angetaka kuongea na chama cha Labour wakati anaendelea kujadiliana na chama cham Consevative."
Akimalizi katika hotuba yake Brown alisema "Katika kipindi chote nitakacho kuwa kiongozi kabla ya kujiudhulu nitahakikisha mabadiliko ya kiuchumi yanakwenda haraka na kukamilisha yale yote yanayotakiwa kufanywa kwa maendeleo ya Waingereza wote."
Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown akiongea mbele ya waandishi wa habari mikakati na muda gani atajiudhulu uongozi.

Friday, May 7, 2010

Uchaguzi wa Uingereza wawa patupu.

Uchaguzi wa Uingereza wawa patupu. London Uingereza - 07/05/2010. Matokeo ya uchaguzi yaliyotolewa nchini Uingereza yameiacha nchii hiyo na wakati mgumu wa kisiasa baada ya matokeo hayo kutompa mgombea yoyote wa vyama vya, Conservatives, Labour na Liberal Demokrati ushindi kamili wa kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo. Matokeo hayo ambayo Conservatives ilipata viti 306 au asilimia 36%, Labour viti 258 asilimia 29% na Liberal demokrati 23%. Kufuatia matokeo hayo ya uchaguzi, serikali ya Uingereza itabidi iundwe na chama zaidi ya kimoja tangu hali hii ilipo tokea mwaka 1974. Picha hapo juu wanaonekana wagombea wa uongozi wa Uingereza wakati wa kampeni ya uchaguzi hivi karibuni, kutoka kushoto, David Cameroon, Nick Clegg na Gordon Brown. Taliban na Al Qaeda washirikiana zaidi.

Islamabad, Pakistan - 07/05/2010. Habari kutoka katika ofisi kuu za kijasusi za kimataifa zinasema yakuwa "kundi la Taliban na Al Qaeda zimekuwa na huusiano wa karibu zaidi kuliko hapo mwanzo na kuongea hali ya usamala kuwa wa mashaka kwa wanchi wa Afghanistan na nchi zinazo pakana na nchi hiyo."
Wachunguzi wa mambo ya kijasusi walizidi kusisitiza habari hizi hasa kwa kuzingatia uwezo wa mwanzo wa kundi la Taliban.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wapiganajiwa kundi la Taliban ambao wamekuwa wanapigana na majeshi ya kimataifa nchini Afghanistan.

Thursday, May 6, 2010

Nigeria yapata msiba mkubwa.

Nigeria yapata msiba mkubwa.

Lagos, Nigeria 06/05/2010. Aliyekuwa rais wa Nigeria,Umuru Yar'Adua amefariki dunia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Marehemu, Umuru Yar'Dua alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa na hata aliweza kwenda nchi za Kiaarabu kwaajili ya matibabu zaidi na baadaye aliweza kurudi nchi Nigeria mapema mwezi wa Februari.
Kufuatia kifo hicho, aliyekuwa makamu wa rais Jonathan Goodluck ameapishwa kuwa rais wa Nigeria baada ya kifo cha aliyekuwa rais umuru Yar'Dua. Picha hapo juu anaonekana hayati raia wa Nigeria, Umuru Yar'Dua enzi za uahai wake akiongea katika mkutano mmoja wapo.
Picha ya pili wanaonekana wanajeshi wa Nigeria, wakiwa wamebeba mwili wa marehemu rais wa Nigeria Umuru Yar'Dua kuelekea kijijini kwa ambapo alipewa pumuziko la milele mbele ya familia, ndugu,wananchi na raia wa sasa Goodluck Jonathan.
Picha ya tatu anaonekana akiapa kuwa rais wa Nigeria baada ya kutangazwa ya kuwa rais Umuru Yar'Dua amefariki dunia.
Jeshi la Urussi laokoa meli ya iliyotekwa nyara.
Moscow, Urussi - 06/05/2010. Jeshi la wanamaji la Urussi limeikomboa meli iliyo kuwa imetekwa na maharamia wa Kisomalia siku chache zilizo pita katika maeneo ya bahari ya Ghuba ya Uajemi.
Kwa mujibu wa msemaji wa jeshi alisema "Katika harakati za kutaka kuikomboa meli hiyo maharamia 10 walifariki dunia na wengine walikamatwa."
Meli hiyo ambayo ilikuwa inawafanyakazi wapatao 23 ambapo meli hiyo ilikuwa imebeba mafuta yenye thamani ya $52 million kuelekea nchini China.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya maharamia wa Kisomalia wakiwa katika ufukwe wa wa pwani ya Somali.

Saturday, May 1, 2010

Nchi ya Chad kukumbwa na janga la ukame na njaa.

Omar al Bashir ahaidi kutumikia Wasudani wote. Khatoum, Sudan - 01/05/2010. Rais mchaguliwa wa Sudan, Omar al Bashir, amwataka wananchi wa Sudan kushirikiana katika kukabiliana matatizo ambayo yanaikabili nchi hiyo.Omar al Bashir aliyasema hayo baada ya kushinda uchaguzi mkuu wa kugombea kiti cha urais uliofanyika mapema mwezi uliopita nchini Sudan. Uchaguzi huo wa kushirikisha vyama vingi ulifanyika huku baadhi ya vya kususia uchaguzi huo Kwa upande wake Omar al Bashir, alisema " mmenichagua kuwa kiongozi wenu na hivyo nitaingoza nchi yangu kwa manufaa ya wananchi wote wa Sudan." Picha hapo juu ni picha kubwa ya rais Omar al Bashir, aliyechaguliwa kuiongoza tena Sudan huku chini ya picha wanaonekana wanchi ambao wanamuunga mkono rais Omar al Bashir wakishangilia baada ya ushindi kura kutangazwa. Nchi ya Chad kukumbwa na janga la ukame na njaa. N'djamena,Chad-01/05/2010. Shirika moja la kimataifa linalo shughulika na kutoa misaada limedai nchi ya Chad inahali mbaya kutokana na ukame ambao unendelea kuikumba nchi hiyo. Hata hivyo shirika hilo limesema " Wanachi wa Chad, wanakabiliwa na hali hiyo ikichangiwa na vita ambavyo vimechangia kuwepo na wakimbizi wengi wa ndani ya nchi na kusababisha hali ya uzalishaji kuwa mgumu hasa kwenye sehemu zile ambazo kuna unafuu wa hali ya ukame." Picha hapo juu anaonekana mama akiwa na mtoto wake ambaye anaonekana kutokuwa na afya nzuri kutokana na utapia mlo. Madawa yatakiwa kurudishwa" Hayakufikia kiwango"

New York. Amerika - 01/05/2-10. Kampuni ya kutengeneza madawa imeitisha madawa ambayo yalikuwa tayari kutumika kutibu, baada ya kufahamika yahakuwa yamefikia kiwango cha bora.
Kwa mujibu wa msemaji wa McNEil, " imebidi dawa zote za aina ya,Tylenol,Zyrtec, Motrian na Benadryl zirudishwe ili kutathmini na kuzihakiki."
Nchi zitakazo athirika ni Amerika-US,Canada,Jamuhuri ya Dominika, Guan, Guatemala,Jamaika, Puerto Rico, Panama, Trinida & Tobago,Kuwait na Fiji.
Picha hapo juu zinaonekana baadhi ya madawa ambayo yanatakiwa yarudishwe kwaajili ya kutathminiwa upya na wataalamu wa madawa.

Saturday, April 24, 2010

G-20 bado ya simama njia panda.

Iran na Zimbabwe zakubaliana kushirikiana.

Harare,Zimbabwe - 24/04/2010. Rais wa Iran Mahmoud Ahmadinejad amemaliza ziara yake nchi Zimbabwe.
Katika ziara hiyo rais wa Iran, alifungua maonyesho ya biashara katika mji wa Bulawayo baada ya kumaliza kusaini mkataba wa kiuchumi kati ya Zimbabwe na Iran.
Picha hapo juu wanaonekana rais wa Iran kushoto akiwa na mwenyeji wake rais wa Zimbabwe mara baada ya rais wa Iran kuwasili nchini Zimbabwe.
G-20 bado ya simama njia panda.
Washington, Amerika - 24/04/2010. Serikali za nchi wanachama wa kundi la G-20 wameshindwa kuafikiana kuhusu kodi za mapato katika mabenki yote duniani.
Akiongea hayo waziri wa fedha wa Kanada alisema "katika kikao walikuwepo wajumbe walio kubali na wajumbe wengine walipinga kabisa." Kikao hicho kiliitishwa ili kujaribu kutafuta njia ya kukabiliana na hali ya mzunguko wa pesa za mabenki. Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya mawaziri wa fedha wakijadiliana mara baada ya kikao kilichofanyika kutathmini hali halisi ya mzunguko wa fedha. NATO yajadili mbinu za kukabidhi madaraka kwa Waafghanistan.
Talinn, Estonia 24/04/2010. Viongozi wa NATO wamekutana nchini Estonia kujadili kwa undani jinjia gani watafanya kujiandaa kuondoa majeshi nchini Afghanistan.
Mkutano huo ulioudhuliwa na viongozi wa nchi 28, walikubaliana kwa misingi ya kuimarisha jeshi na polisi la nchi ya Afghanistan ili washike madaraka na kusimamia ulinzi wa nchi.
Akiongea mbele ya wajumbe, katibu mkuu wa NATO, Anders Fogh Rasmussen, alisema"Serikali ya Afghanistani ina endelea vizuri katika ulinzi wa nchi na hivyo kuna haja madaraka yote yawe chini ya uongozi wa serikali ya Afghanistan."
NATO inatarajia kuanza kupunguza majeshi yake nchini Afghanistan kuanzia mwaka 2011.
Vita vya Afghanistan vilinza kwa ajili ya kupambana na makundi ya ugaidi ya Taliban na Al-qaeda.
Picha hapo juu wanaonekana viongozi wa nchi za NATO wakiwa katika mkutano kujadili mbinu mbada kuhusu Afghanistan.

Wednesday, April 21, 2010

Hatimaye mama asilia atoa ruhusa kwa ndege kuruka.

Hatimaye mama asilia atoa ruhusa kwa ndege kuruka.

Brussel,Ubeligiji - 21/04/2010. Ndege zimeanza kuruka tena angani baada ya kushindwa kuruka kutokana na mavumbi ya mlipuko wa volkano yaliyo tokea katika kisiwa cha Iceland kwenywe milima ya Eyjafllajoekull siku sita zilizo pita.
Kwamujibu wa habari kutoka kwa shirika la anga la Ulaya zinasema "bado kuna baadhi ya maeneo hali ya hewa hijawa safi kwa usafiri wa anga."
"Hata hivyo huenda safari za ndege zikaanza mapema mwisho wa wiki hii zilimalizia habari kutoka kwenye shirika hilo la anga la Ulaya".
Picha hapo juu inaonekana ndege ikielekea kutua kwenye kiwanja cha ndege cha Heathrow lilichopo Uingereza mapama hivi leo,baada ya siku sita za kushindwa kuruka angani kutokana na madhara yaliyo sababishwa na mama asilia.

Monday, April 12, 2010

Wapoland wakumbwa na msiba mkubwa

Warsaw, Poland 12/04/2010. Wananchi wa Polanda wamekumbwa na msiba mkubwa baada ya rais wa nchi hiyo na viongozi wengine wakuu wa idara mbalimbali walipo fariki kutokana na ajali ya ndege.
Rais Lech Kaczynski's na wajumbe wake walikuwa wakielekea Urusi, ambapo ndege iliyokuwa imewabeba kuanguka karibu na kiwanja cha ndege na kupoteza maisha ya watu wote waliokuwemo ndani ya ndege hiyo.
Picha hapo juu ni ya hayati raia Lech Kacznski's, enzi za huai wak, mara baada ya kumaliza kuakagua gwaride rasmi.
Picha ya pili mi msururuwa magari ambamo moja ya gari hizo imebeba mwili wa marahemu rais wa Poland kuelekea Ikulu ya Poland.
Picha ya tatu wanaonekana awanajeshi wa Poland, wakiwa wamebeba mwili wa marehemu rais wa Poland, Lch Kaczynski' mara baada ya kuwasili nchini Poland.
Rais wa Amerika akutana na viongozi wa dunia.
Washington, Amerika 12/04/2010. Rais wa Amerika anakutana na viongozi tofauti kutoka mabara yote ya dunia katika mkutano utakao zungumzia ni njia gani zinatakiwa kuhakikisha ya kuwa siraha za nguvu za kinyuklia hazita angukia katika mikono ya Al-qaeda na wafuasi wake, kwani huenda wakazitumia katika mashambulizi.
Rais, Baraka Obama, amemefanya uamuzi huo kama ule uliofanywa na rais Franklin D Roosevelt ambaye aliwaita viongozi wa wa dunia wakati wamkutano wakutaka kuanzisha umoja wa Matifa mnamo mwaka 1945.
Akiongea rais wa Obama alisema "lazima jumuia ya kimataifa iakikishe kuwepo na usalama na ilinzi kuhakikisha siraha za nyuklia aziangukii katika mikono potofu"
Picha hpo juu wanaonekana rais Baraka Obama na waziri wa mambo ya nje wa Amerika, Hirally Clinton wakielekea kujiandaa kuwapokea viongozi wa dunia.

Thursday, April 8, 2010

Waingereza wajiaanda kuchagua waziri mkuu mpya.

Waingereza wajiandaa kuchagua waziri mkuu mpya . London, Uingereze 08/04/2010. Kampeni za uchaguzi nchini Uingereza zimeaanza rasmi, mara baada ya waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown,kutangaza rasmi ya kuwa siku ya uchaguzi mkuu utakuwa April 6 /2010. Kwa mujibu wa wachunguzi wa maswala ya kisiasa. wanasema uchaguzi wa mwaka huu utakuwa wa ni wa kihistoria, kwa kuzingatia ya kuwa serikali iliyopo madaraka ni ya Gordon Brown, ina upinzani mkubwa sana kutoka kwa David Cameron ambaye anagombe kiti cha uwaziri mkuu kupitia chama cha Conservative. Picha hapo juu wanaonekana David Cameron kushoto na Gordon Brown kulia ambao wanagombe kiti cha uwaziri mkuu wa Uingereza katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu April 6/ 2010. Amerika na Urussi za tiliana sahihi mkataba wa kupunguza zana za kivita za kinyuklia. Prague,Cheksi - 08/04/1020. Marais wa Amerika na Urussi wametia sahii mkataba wa kupunguza uzalishaji wa nguvu za zana za kijeshi za kinyuklia. Maraias hao Baraka Obama na Dmitri Medvedev walisaini mkataba huo katika mji wa Prague uliopo Jamuhuri ya Cheksi. Akiongea mara baada ya kutia sahii, rais wa Amerika, Baraka Obama alisema " Amerika na Urussi haziwezi kufanyakazi ikiwa hazita shirikiana hasa katika maswala makubwa ambayo yana husu hali halisi ya dunia." Naye rais wa Urussi Dmitri Medvedev alisema , hii ni siku ya kukumbukwa kihistoria na itafungua ukurasa mpya na pande zote zitafaidika na mkataba huu." Picha hapo juu wanaonekana, ais wa Amerika Baraka Obama kushoto na rais wa Urussi, Dmitri Medvedev, wakisaini mkataba wa kupunguza nguvu za zana za kijeshi za nyuklia walipo kutana Prague.