Monday, February 28, 2011

Brussels, Ubeligiji - Jumuia ya Ulaya imekubaliana kwa pamoja kumwekea vikwazo kiongozi wa Libya kufuatia matukio ya nayo endelea kutokana na maandamano ya kupinga uongozi wa serikali.
Vikwazo hivyo vilivyo pitishwa ni pamoja na ununuzi wa siraha, kuzuiliwa kusafiri, na pesa zote ambazo zilikuwa zimewekwezwa na familia yake.
Serikali ya Misri ya mzuai Hosni Mubaraka na familia yake kusafiri.
Kairo, Misri - 28/02/2011. Serikali ya Misri imezua familia ya rais wa zamani wa Misri kusafiri nje ya nchi kufuatia uchunguzi unaoendelea.
Akiongea mbele ya waandishi wa habari msemaji wa mwanasheria mkuu wa serikali Abel el Saeed alisema " serikali imeamua kumzuia Hosni Mubaraka kutoka nje ya nchi yeye na familia yake kufuatia uchunguzi dhidi ya yake.
Rais Hosni Mubaraka, alitolewa madarakani baada ya wanachi wa Misri kuandamana kumtaka atoke madarakani kutokana na kutoridhishwa na uongozi wake wa miaka 32.
BMW na Citreon kuunangana kibiashara.
Geneva, Uswiss - 28/02/2011. Makampuni ya magari ya BMW na Peugeot Cirtoen yamekubaliana kuungana kibiashara ili kutengeneza aina mpya ya gari itakayo endana na teknolojia mpya.
Akongea na waandishi wa habari mwenyekiti wa PSA Peugeot Citreon Phillipe Varin alisema " huu ni mwanzo na muungano huu utaiwezesha jumuia ya Ulaya kutengeneza magari ya kisasa ambayo yataendana na teknologiajia mpya."
Utengenezaji wa magari hayo ambayo yatajulikana kama magari ya Hybrid yata leta ajira kwa watu wapatao 400.

Saturday, February 26, 2011

Umoja wa mataifa kuwekea vikwazo serikali ya Libya.

Umoja wa mataifa kuwekea vikwazo serikali ya Libya. New York, Marekani - Kamati ya usalama ya umoja wa Mataifa imekutana ili kujadili muswada wa kuiwekea vikwazo serikali ya Libya.

Uamuzi huo wa umoja wa mataifa umekuja baada ya serikali ya Libya chini ya kiongozi wa nchi hiyo Muammar Gaddafi kutumia nguvu kuvunja maandamano ambayo yanapinga serikali yake.
Kwa mujibu wa habari kutoka katika kamati hiyo ya umoja wa mataifa zinasema " serikali ya Libya inatumia nguvu zake za dola kimyume na kusababisha vifo na maafa katika jamii nzima ya Walibya."
Hali ya kiusalama nchini Libya imebadilika na kuwa uwanja wa vita mara baada ya maandamano ya kumtaka kiongozi wa nchi hiyo Muammar Gaddafi kutika madarakani jambo ambalo kiongozi huyo amekataa.
Picha hapo juu anaonekana kiongoziwa Libya Muammar Gaddafi akiwahutubiwa wananchi kwa mara ya tatu tangu kuanza maandamano ya kumtaka aachie madaraka.
Hali ya kuzuka vita vya wenyewe kwa wenyewe huenda ikatokea.
Abidjani, Ivory Coast-26/02/2011. Milio ya risasi imesikika katikati ya jijila Abidjani na kuwafanya wakazi wake kukimbia kwenye maficho huku katibu mkuu wa umoja wa mataifa akionya kuibuka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Mapigano hayo ambayo yalikuwa kati ya kundi la rais wa sasa wa nchi hiyo Laurence Gbagbo na Alassane Ouattara.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zimasema " halisiyo shwali katika jiji hilo."
Hali ya machafuko ilianza mara baada ya uchaguzi mkuu kufanyika na Gbagbo kudai yeye ndiye aliye shinda uchaguzi na huku mpinzani wake Ouattara kudai yeye ndiye mshindi wa uchaguzi huo.
Picha hapo juu ni viongozi wa makundi yanayo pigana nchini Ivory Coast, Watara kushoto na Gbagbo kulia

Thursday, February 24, 2011

Rufaa ya mwanzilishi wa WikiLeaks yakataliwa.

Rufaa ya mwanzilishi wa WikiLeaks yakataliwa.

London, Uingereza - 24/02/2011. Mahakama jijini London imetupilia mbali rufaa ya mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks ambayo inapinga kupelekwa kwake nchini Sweden ili kujibu mashitaka.
Jaji Howard Riddle alisema " tumuma zidi ya mshitakiwa ni za kisheria na zinatakiwa zijibiwe kisheria hivyo inatakiwa mshitakiwa akajibu mashitaka."
Akiongea baada ya hukumu mwanasheria wa mshitakiwa Julian Assange alisema " tutakata rufaa dhizi ya uamuzi huu."
Juliana Assange ambaye amekuwa shubiri katika jamii ya kidipromasia baada ya mtandao wake WikiLeaks kutoa siri za viongozi na mabalozi wanapo kutana kila mara.
Mahakama ya kimataifa ya muhukumu miaka 27 jela mkuu wa zamani wa Polisi wa Serbi.
Hague, Holland 24/02/2011. Mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi za Yugoslavia imemuhukumu aliyekuwa mkuu wa polisi Serb kwa miaka zaidi ya miongo miwili.
Vlastimir Djordjevic alihukumiwa na baada ya mahakama kumkuta na hatia ya kushiriki machafuko na mauaji ya Kosovo Albania.
Akitoa hukumu jaji Kevin Parker alisema " unahukumiwa kifungo cha miaka 27 jela kwa kukutwa na makosa ya kuhusika na mauaji ya watu 724 wa Kosovo Albania na kuleta mgawanyiko wa jamii katika eneo hilo."
Vlastimir Djordjevic alikamatwa mwaka 2007 huko Montenegro maada ya kukimbia na mafichoni kwa muda wa miaka minne.

Tuesday, February 22, 2011

Muhammar Gaddafi asema hatoki madarakani

Muhammar Gaddafi asema hatoki madarakani. Tripol, Libya - 22/02/2011. Rais wa Libya melihutubia taifa la Libya na kusema hataondoka nchi na yupo tayari kufa kwa ajili ya nchi yake.

Kanal Muhammaar Gaddafi alisema, " mimi ni shujaa na mpiganaji kutoka kwenya turubai, nipo tayari kufa na nitapigana hadi mwisho, mimi siyo rais uacha madaraka, mimi ni mpiganaji."
Akiongea kwa hasira aliongezea " wale wote wananifata naawagiza wawakamate watu wote wanlioleta machafuko na wafikishwe kwenyw sheria."
"Nitahakikisha tunasafisha kila nyumba kama wasipo jisalimisha."
"Kama Libya ita yumba itakuwa makao ya Al-Qaeda."
Maandamano siyo kuaribu na siyo waasi wa nchi.
Rais wa Libya aliyasema hayo baada ya Walibya kuandamana kumtaka aachie madaraka na kuruhusu mabadiliko ya kisiasa.
Manoari za Kiiran zapita Suez Kanal kwa mara ya kwanza.
Suez Kanal, Misri - 22/02/2011. Manoari mbili za kijeshi za Iran zimepita kwa mara ya kwanza kwenye mfereji wa Suezi Kanal. Meli hizo zimepita muda wa saa tisa na dakika arobaini na tano kwenye mfereji huo na zinategemewa kurudi mwezi Tatu mwaka 2011.
Meli za Iran zimepita kwenye mfereji huo kwa mara ya kwanza tangu kuanguka kwa serikali ya Hosni Mubaraka.
Kufuatia kupita kwa meli hizo serikali ya serikali ya Izrael imesema " tunatizama kwa uangalifu mwenendo huo wa Iran."
Uongozi wa Suez Kanal uliripoti ya kuwa Meli za Iran zimepita kwenye eneo hilo kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1974.
Rais wa Urussi aonya kuhusu mapinduzi katika nchi za Kiarabu.
Moscow, Urussi - 22/02/2011.Rais wa Urusi ameonya ya kuwa mabadiliko ya kisiasa yanatotokea katika nchi za kiarabu yanaweza kuleta athali kubwa.
Rais Dmitry Medveded alisema " siafiki na jinsi viongozi wa nchi za magharibi ambao wamekuwa wana unga mkono mapinduzi ya kisiasa yanayo tokea katika nchi za Kiarabu, kwani yanaweza kuleta machafuko na kugawa nchi hizo ambapo matokeo yake yatakuwa mabaya kwa muda mrefu."
Akiongezaa " Inawezekana nchi hizi zikaja kutawaliwa na viongozi ambao wataleta maafa katika jamii. alisema rais Medved.
Maoni ya rais wa Urussi yamekuja kufuatia machafuko na mabadiliko ya yanayoendelea katika nchi za Kiarabu ambayo yameishitua dunia.

Friday, February 18, 2011

Milipuko yatokea nchini Tanzania

Milipuko yatokea nchini Tanzania

Dar es Salaam, Tanzania - 18/02/2011. Milipuko ya mabomu imeua zaidi ya watu ishirini na kuleta maafa makubwa kwenye kambi moja ya jeshi iliyopo nje kidogo ya jiji la Dar es Saalam.
Mlipuko huo ambao ulitokea usiku wa kuamkia Jumatano na kusababisha wenyeji wa maeneo hayo kukimbia mji wao kwa uwoga.
Milipuko hiyo iliyo tokea katika kambi ya jeshi iliyolo Gongo la Mboto wilaya ya Ilala imesababisha maafa makubwa kwa jamii.
Mizengo Pinda alisema " milipuko hiyo imeleta maafa makubwa na huenda baadaye maafa yakaongezeka kutokana na hali halisi iliyo sababishwa na milipuko hiyo."
Milipuko ya mabomu katika kambi ya jeshi la Gongo la Mboto imetokea kwa mara ya pili baada ya milipuko uliyo tokea mwaka 2009 ambapo watu wapatao 27 walipoteza maisha yao.
Wamisri washangilia wiki moja tangu kuondoka Hosni Mubaraka.
Kairo, Misri - 18/02/2011. Maelfu ya wananchi nchini Misri wameandamana ili kushangilia kuanguka kwa utawala wa Hosni Mubaraka.
Rais Hosni Mubaraka ambaye alikuwa rais wa Misri kabla ya kuamua kuachia madaraka baada ya wanachi kuandamana kutaka serilikali ya Mubaraka iachie utawala.
Hata hivyo kulikuwa na maandamano mengine yalifanyika katika jiji la Kairo kuunga mkono Hosni Mubaraka kwa madai ameiniua nchi na kuleta amani.
Rais Hosni Mubaraka, alitoka madarakani baada ya maandamano ya siku kumi na nane ambayo yalimlazimisha kuachia madaraka ya urais.

Wednesday, February 16, 2011

Kachero alidanganya kuhusu uwezo wa Saddam Hussein.

Kachero alidanganya kuhusu uwezo wa Saddam Hussein. Berlin, Ujeruman - 16/02/2011. Wabunge nchini Ujerumani wameonya ya kuwa hunda kachero aliyejulikana kwa jina la Curveball akawekwa kizuizini mara baada ya kusema ya kuwa alidanganya.

Curveball jina la kazi, ambaye ni raia wa Irak amesema ya kuwa alitoa habari za uongo kwa makachero wa Amerika na washiriki wake ya kuwa rais wa Irak Saddam Hussein alikuwa na siraha za sumu ambazo ni zakuangamiza.
Raia huyo wa Irak, Rafid Ahmed Alwan, ambaye aliongea na gazeti la Guardian na kudai ya kuwa alidanganya ili rais Saddam Hussein atolewe madarakani.
Rafid Ahmed Alwan alisema " labda nilikuwa sawa au sikuwa sawa lakini nilipewa nafasi ya na hivyo nikaitumia ili Saddam Hussein atolewe madarakani na mimi na familia yangu tunajidai kwa kuchangia mageuzi ya kisiasa na kuleta demokrasi nchini Irak."
Curveball alikimbia kutoka Irak mwaka 1995 wakati wa utawala wa marehemu rais Saddam Hussein.
Serikali ya Libya ya macho yake kwa waandamanaji.
Benghazi, Libya - 16/02/2011. Polisi nchini Libya wamepambana na waandamanji ambao walikuwa wamendamano na kuelekea kituo kikuu cha polisi.
Katika maandamano hayo, polisi waliumia gasi na zana nyingine ili kuwatawanya waandamanaji ambo watu wapatao kumi na nne kuumia wakiwmo polisi.
Maandamano yaliyo fanyika nchini Libya yamefuatia maandamano yaliyo fanyika nchini Tunisia na Misri na kufanya serikali za chini hiyo kuondoka madarakani.
Waganda waajianda na uchaguzi wa rais.
Kampala, Uganda - 16/02/2011. Viongozi wa vyama tofauti vya siasa nchi Uganda wanamalizia kampeni zao za mwisho kabla ya uchaguzi siku ya Ijumaa.
Uchaguzi huo ambao matokeo yake yata wezesha wanchi wa Uganda kupata rais ambaye watamchagua baada ya muda wa rais wa sasa wa Yoweri Museni kumalizika.
Mpinzani wake wakuu wa rais wa sasa Yoweri Museni ni Kiiza Basigye ambaye amekuwa akimlaumu Musseven kwa kutoleta mabadiliko kwa wanchi wa Uganda.
Kufuatia uchaguzi huo serikali ya Uganda imetangaza kuwa siku ya Ijumaa itakuwa sikuku ya kitaifa.

Monday, February 14, 2011

Wasafiri wa anga wapata chombo kipya.

Wasafiri wa anga wapata chombo kipya.

New York, Amerika 14/02/2011. Kampuni ya ndege ya Boeing imezindua ndege mpya ambayo itakuwa hewani hivi karibuni.
Boeing imesema ndege "hiyo 747-8 Intercontinental itakuwa ikisafiri mwendo mrefu na waki huo ikitumia mafuta kiasi".
Ndege hiyo ambayo itakuwa na uwezo wa kuchukua abiria 467 ambao watakuwa wameongezeka kwa abiria 51 tofauti na ndege ya sasa 747.
Serikali ya Algeria yafuta amri ya dharula.
Algiers, Algeria 14/02/2011. Serikali ya Algeria imetangaza kusimamisha amri ya dharula ambayo ilikuwa imewekwa kwa kipindi cha miaka kumi na tisa.
Waziri wa mambo ya nchi za nje Mourad Medelci amesema " serikali imeamua kutoa amri ya dharula kama ilivyo haidiwa na rais Abdelaziz Bouteflika hiv karibuni."
Amri ya dharula iliwekwa mwaka 1992.
Kuondolewa kwa sheria hii imekuja baada ya serikali kuwa na wakati mgumu hasa kutoka kambi za nyama pinzani.

Sunday, February 13, 2011

Rais wa zamani wa Pakistani ashitakiwa.

Kiongozi wa Palestina ajiudhulu kazi yake. Ramallah, Palestine - 13/02/2011. Msemaji mkuu wa serikali ya Wapalestine amejiudhulu katika kazi yake baada ya habari zilizo patikana kwenye vyombo vya habari zimetokea kwenye ofisi yake. Saeb Erakat, ambaye amekuwa msemaji mkuu wa serikali ya Wapalestina kwa muda mrefu, amekuwa akiandamwa na mlolongo wa lawama ya kuwa amekuwa hafanya kama anavyotakiwa hasa katika majadiliano ya kuleta amani na Waizrael. Habari ambazo zilipatikana kwenye vyombo vya habari hivi karibuni zimeonyesha jinsi gani viongozi wa Palestina wanavyo jadiliana katika majadiliano ya amani na Waizrael ambayo yamesimama kutokana na tofauti za misimamo. Rais wa zamani wa Pakistani ashitakiwa.

Islamabad, Pakistan - 13/02/2011. Mahakama nchini Pakistan imetoa kubali cha kumtaka aliyekuwa rais wa zamani wa nchi hiyo kukamatwa ili ajibu mashitaka ya kuwa alihusika na mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo.
Musharaff, ambaye alikuwa rais wa Pakistan na amiri jeshi mkuu wa nchi hiyo, anatuhumiwa kwa kuhusika na mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu Benazir Bhutto.
Habaria kutoka kwa viongozi wa serikali zinasema " uchunguzi ulio fanywa unaonyesha kwa njia mojo au nyingine uongozi wa serikali ya Musharaff uliyo kuwepoe wakati wa mauji ya Benazir Bhutto unahusika."
Hata hivyo, upande wa Musharaff unakanusha madai hayo na kusema ni habari za uvumishi ndizo ambazo zimetumika na Musharaff hausiki na mauaji hayo.
Pervez Musharaff anatarajiwa kuwasili mahakamani tarehe 19 Februari 2011 ilikusikiliza kesi dhidi yake.

Saturday, February 12, 2011

Rais wa Misri Hosni Mubaraka ajiudhuru urais.

Rais wa Misri Hosni Mubaraka ajiudhuru urais. Kairo, Misri - 12/02/2011. Sherehe, shangwe vigeregere vilivyo andamana na vilio vilisikika nchi zima mara baada ya makamu wa rais wa Misri Omar Suleiman kutangaza ya kuwa rais Hosni Mubaraka amejiudhuru na kukabidhi madaraka mikononi mwa jeshi.

Akiongea kwa muda wa sekunde thelathini, makamu wa rais alisema " rais Hosni Mubaraka ameamua kujiudhuru na kuanzia sasa na amekabidhi madaraka yote kwa kamati itakayo ongozwa na jeshi."
Rais Hosni Mubaraka, ambaye ametawala Misri kwa miaka 30, amejiudhuru baada ya msukumo mkubwa kutoka kwa waandamanaji ambao walikuwa wanadai atoke madarakani.
Maandamano yaliyo mfanya rais wa Misri kuachia madaraka yamechukua siku kumi nane, na kusababisha maafa makubwa ja kijamii na kiuchumi.

Wednesday, February 9, 2011

Wakili wa Charles Taylor aondoka mahakamani.

Wakili wa Charles Taylor aondoka mahamani.

Hague, Uhollanzi - 09/02/2011. Mwanasheria anaye mtetea aliyekuwa rais wa Liberia Charles Taylor ametoka mahakamani baada ya ya majiji wanaosikiliza kesi hiyo kukataa ripoti iliyo wakilishwa wakati wa mwisho.
Mwanasheria huyo kutoka Uingereza alisema " Ikiwa mahakama na sisi hatuelewani, inakuwa vigumu kuamini na wamezuia kwa asilimia 90 utetezi wa mteja wangu?"
Charles Taylor anatuhumiwa kwa makosa ya kukiuka haki zabinadamu kwa wanachi wa Sierra Leone.
Waziri mkuu wa Itali kuenda akasimama kizimbani.
Milan, Itali- 09/02/2011. Waziri mkuu wa Itali huenda akajikuta amesimama kizimbani baada ya wanasheria kufungua kesi dhidi yake kwa madai ya kutumia cheo chake vibaya.
Silvio Berlusconi, ambaye ni waziri mkuu anatuhumiwa kwa kwa kufanya mapenzi na msichana ambaye hajafika miaka kumi nane.
Mahakama jijini Milan, imeombwa ifungungue kesi baada ya kukamilika kwa uchunguzi wa kashfa hio.
Hata hivyo waziri mkuu Silvio Berlusconi amekuwa akikanisha kashfa hizo zidi yake na kusema " ni za kisiasa, wapinzani wake ndiyo wanao shikilia madai hayo ili kumchafulia jina lake."
Kampuni ya magari ya Toyota yapata hafueni.
Washington, Marekani -09/02/2011. Kampuni ya magari ya Toyota imepata hafueani baada ya ripopti ya uchunguzi kuonyesha yakuwa matizo yaliyokuwemo kwenya magari yake hayakusababishwa na mtiririko wa umeme kwenye gari.
Akiwakilisha ripoti ya uchunguzi iliyo fanywa na wanasayansi wa NASA, waziri wa mawasiliano Ray LaHood alisema "matatizo ya kuongezeka kasi ya gari wakati waundeshaji hayakusabaishwa na mtiririko wa umeme bali matatizo ya kiufundi - makeni."Baada ya ripo ti hiyo kutolewa uongozi wa kampuni ya magari ya Toyota, ulisema tutajitahidi kuimarisha magari yetu na tupo tayari kusilikiza mawazo ya wateja wetu ili kuhakikisha usalama wa kila mteja wetu.''
Kampuni ya magari ya Toyota ilipata msukosuko hivi karibuni baada ya baadhi ya wateja wake kudai yakuwa magari take yana matatizo.

Saturday, February 5, 2011

Thamani ya Euro kuimarishwa kwa kila hali.

Thamani ya Euro kuimarishwa kwa kila hali. Brussels, Ubelgiji 05/02/2011. Mkutano wa viongozi wa jumiya ya Ulaya umeamua kuahakikisha thamani ya pesa ya Uero in tengemaa.

Kanselah wa Ujerumani Angela Markel alisema " kwa kushirikiana na nchi wanachama wa jumuia ya Ulaya Ujerumani na Ufaransa tutailinda Uero siyo kipesa tubali pia kiuchumi na kisiasa na kuifanya iwe madhubuti katika mashindano na kuinua uchumi kwa pamoja."
Uamuzi wa viongozi wa jumuia ya Ulaya kuilinda sarafu ya Euro, kumekuja baada ya myumbo wa kiuchumi wa nchi wanachama.
Waandamanaji nchini Misri bado kushikiria msimamo wao.
Kairo, Misri -05/02/2011. Waandamanaji nchini Misri bado wanashikiria haja yao kutaka rais sasa kutoka madarakani.
Wakiongoea kupinga ombi la mkuu wa jeshi la kuwataka warudi majumbani, waandamanaji walisema "hatuwezi kuondoka hapa tulipo mpaka rais Hosni Mubaraka ametoka madarakani."
Hata hivyo jumuia ya kimataifa bado inasugua vichwa ni kwa jinsi gani wataweza kusaidia kutatua mgogoro wa kisiasa uliopo nchini Misri kwa kuzingztia nchi yenyewe ni kiungo muhimu katika eneo zima la mashariki ya kati.
Wakati maandamano ya kumpinga rais Mubara yanaendelea, bombo la kupisha gasi kuelekea nchi Jordani lilipasuka na kunamadai ya kuwa bomba hilo limelipuliwa na watu wasio julikana.
Bomba hilo lililopo Ghuba ya Sinai liliupasuka na kusababisha wimbi kubwa la moto kuelekea hewani na kuathiri usambazaji wa gasi kuelekea nchini Jordani,
Picha hapo juu ni picha ya poto ulio lipuka mara baada ya bomba la gasi kuasuka na kuathiri usambazaji wa zao la gasi kuelekea nchini Jornan.
Pichaya pili hapo juu inaonyesha waandamanaji waliopo katikati ya jiji la Kairo kwenye viwanja vya Tahrir kwa siku ya kumi na mbili tangu kuanza maadamano ya kutaka rais Mubaraka aachie madaraka.

Wednesday, February 2, 2011

Rais Mubaraka kutogombania urais tena.

Rais Mubaraka kutogambinia urais tena.

Kairo, Misri- 02/02/2011. Rais wa Misri ametangaza yakuwa hatagombea tena kiti cha urais tena na kusema atatoka madarakani baada ya kuhakikisha mabadiliko yana fanyika bila matatizo.
Rais Hosni Mubara alisema " sitagombea tena urais na sikutarajia kugombea tean kiti cha urais. Serikali itahakikisha kuwa hali ya sasa itakuwa shwari na nahaaidi ya kuwa sitakakimbia nchi na nita kufa hapa nyumbani na kuzikwa hapa, Mirsi ni nchi yangu nimeipigania na hivyo sitaondoka."
Mubaraka amehutubia kwa mara ya pili tangu kuanza maandamano ya kupinga serikali yake.

Tuesday, February 1, 2011

John Kerry ataka rais wa Misri kuachia madaraka. New York, Marekani - 01/02/2011. Mbuge na kiongozi muhimi katika chama cha Demokratik cha Marekani amemtaka rais wa Misri kujiudhuru.

John Kerry alisema " Mubaraka lazima akubaliane na matakwa ya wananchi na raia wa Misri kwa ajili ya usalama na kulinda hadhi ya Wamisri na mtoto wake asigombanie kiti cha urais wakati wa uchaguzi, pia Marekani inatakiwa kuangalia mbele na kujua ya kuwa kipindi cha Mubaraka kimekwisha."
John Kerry amekuwa kiongozi wa kwanza wa ngazi ya juu kutoka Marekani kutamka wazi ya kuwa rais Mubaraka aachie madaraka.
Picha hapo juu ni ya mbuge John Kerry, ambaye amekuwa wa kwa kutamka wazi kuwa rais wa Misri Hosni Mubaraka atoke madarakani.
Rais wa zamani wa Haiti kurudi nyumbani.
Port au Price, Haiti - 01/02/2011.Serikali ya Haiti imekubali kumpa kibali cha kurudi nyumbani aliye kuwa rais wa nchi hiyo ambaye alikimbilia Afrika ya Kusini.
Jeans Bertrand Aristide aneyeishi ukimbizini nchi Afrika ya Kusini amekuwa akisema kila mara yupo tayari kurudi nyumbani ikibidi kufanya hivyo.
Ira Kurzban, mwanasheria wa wa Aristide amesema " ninacho fahamu ni kwamba rais Jeans Bertrand Aristide amepewa pasipoti tayari kurudi nyumbani na kamati ya serikali ya Haiti."
Kurudi kwa Aristide kutakaribiana na uchaguzi wa mara ya pili wa kumchagua rais wa Haiti ambao utafanyikahivi karibuni.
Picha hapo juu ni ya rais wa zamani Jean Bertrand Aristide ambaye anatarajiwa kurudi nyumbani kutoka ukimbizini.
Mfalme wa Jordani avunja serikali.
Aman Jordan - 01/02/2011. Mfalme wa Jordani amevunja serikali baada ya kushindwa kuimarisha uchumi wa nchi na kusababisha wananchi kuandama.
Maandamano hayo ambayo yamefanyika zaidi ya wiki, yalianza baada ya kupanda kwa mafuta na bei ya vyakula.
Habari kutoka ofisi ya mfalme zinasema " mkuu wa jeshi wa zamani Marouf Bakhit ambaye aliyewahi kuwa waziri mkuu hapo awali amechaguliwa kuwa kuunda serikali mpya baada ya serikali ya Samir Rifai kushindwa kuimarisha uchumi."
Wananchi wa Jordan wamekuwa wakilalamikia serikali kwa kushindwa kuimarisha uchumi na kusababisha maisha ya raia kuwa magumu.
Picha hapo juu ni ya Mfalme wa Jordan ambaye amevunja serikali baada ya kushindwa kuongoza wananchi na kuinua uchumi Jordan.

Saturday, January 29, 2011

Maandamano yafanya rais wa Misri kuvunja serikali.

Maandamano yafanya rais wa Misri kuvunja serikali.

Kairo Misri - 29/01/2011. Rais wa Misri amevunja serikali baada ya mandamano makubwa kufanyika kwa nchi nzima.
Rais Hosni Mubaraka, alisema " naelewa kwa jinsi gani wanchi wenzangu wanavyo sumbuka kutokana na hali zao za kiuchumi, mahitaji ya mabadiliko ya kisiasa na demokrasi, hivyo nitaunda serikali mpya ambayo itahakikisha yakuwa inatekeleza kwa vitendo hayo yote ili kuleta mabadiliko.
Wakati huo huo, rais wa Amerika Baraka Obama, amemtaka rais Hosni Mubara kufungua njia ya mabadiliko na kuacha demokrasi ichukue mkondo wake.
Rais Mubara, alihutubia taifa mara baada ya maandamano ya kupinga serikali yake kuwa makubwa na kuleta maafa karibu nchi nzima.
Picha hapo juu anaoekana rais Hosni Mubaraka akihutubia taifa na kuhaidi kuleta mabadiliko.

Friday, January 28, 2011

Serikali ya Misri ipo njia panda.

Nelson Mandela aruhusiwa kutoka hospital. Main Image Johannesburg, Afrika ya Kusin - 28/01/2011. Aliyekuwa rais wa kwanza baada ya kuanguka kwa utawala wa kibaguzi wa makaburu ameruhusi kutoka hospital Mill Park ambako alikuwa amekwenda kwa matibabu. Nelson Mandela mwenye umri wa miaka 92 alikuwa hospitalini kwa matibabu baada ya kutojisikia vizuri kiafya. Makamu wa rais Kgalema Motlanthe aisema " Mandela ana nafuu na alikuwa anataniana nasi na tuzidi kumwombea afya yake iwe nzuri." Picha hapo juu anaonekana Winnie Mandela akitokea hospital kumwangalia mumewe Nelson Mandela ambaye alikuwa amelazwa hospital. Serikali ya Misri ipo njia panda. Kairo, Misri 28/01/2011.Maelfu ya wananchi nchini Misri wameandamana kupinga serikali iliyopo madarakani na huku polisi wakipambana na waandamaji kwa kutumia gasi na maji.

Kwa mujibu wa mashaihidi waliokuwemo kwenye maandamano walisema watu wengi wamejeruhiwa wakiwemo wakinamama.
Katika maandamano hayo alikuwemo aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la kukagua na kumiliki mmatumizi ya nyuklia Mohamed ElBaradei.
Kufuatia maandamano hayo serikali imefunga matumizi yote ya mtandao, jambo ambalo jumuia ya kimataifa imelitilia mashaka kitendo hicho.
Picha hpo juu wanaonekana polisi wa kuzuia ghasia wakiwa wamesimama kuwazuia waandamanaji.

Wednesday, January 26, 2011

Uchumi wa dunia kujadiliwa tena Davos.

Uchumi wa dunia kujadiliwa tena Davos. Davos,Swiss - 26/01/2011. Viongozi wa serikali, wafanya biashara,,wanasiasa na wanauchumi, wanakutana nchi Uswisi ili kujadili mpangilio mzima wa uchumi dunia. Mkutano huo ambao utachukua siku tano, unatarajiwa kujadili mbinu za kuinua uchumi baada ya mtikiso mkubwa wa uchumi ulio ikumba dunia miaka miwili iliyo pita. Kwa mujibu wa wachunguzi wa maswala ya kiuchumi wanasema " inabidi katika mkutano huu viongozi, wanasiasa,wafanya biashara na wanauchumi watafute ufumbuzi wa kuinua uchumi na siyo kuweka ahadi ambazo zimekuwa ziki tawaliwa na mzunguko wa siasa na hai halisi ya kiuchumi. Picha hapo juu ni mji wa Davos, ambao viongozi wa nchi tofauti, wafanya biashara, wanasiasa na wanauchumi wanakutana kujadili hai halisi ya uchumi duniani.

Interpol yaombwa kumkamata rais wa Tunisia.
Tunis,Tunisia - 26/01/2011. Polisi wa kimataifa wameombwa kukamata aliye kuwa rais wa Tunisia, mkewe na washiriki wa karibu wa familia yake ili wajibu mashitaka mbele ya mahaakama.
Zine Kwa mujibu wa habari kutoka wizara ya sheria ya Tunisia zinasema "El Abidine Ben Ali, ambaye alikuwa rais wa Tunisi anakabiliwa na kesi za kuiba mali ya uma,kuiba pesa za nchi na kuziwekeza nje ya nchi kwa matumizi yake na familia yake."
Akisisitiza kuhusu habari hizo, Lazhar Karoui Chebbi, alisema tumeiomba Interpol kumkamata iliaje kujibu mashitaka ya kuhujumu mali umma.
Rais wa Tunisia alikimbia nchi baada ya wanchi wa Tunisia kuanamana kwa kutaka ajitoe madarakani kutona na serikali yake kushindwa kuwainua wanachi kiuchumi.
Umoja wa mataifa watakiwa kufungua mahakama za kiharamia.
New York, Amerika - 26/01/2011. Umoja a Mataaifa umeombwa kuchangia mbinu mbadala za kupambana na maharamia waliopo katika pwani ya Somalia hadi kufikia pwani za Afrika ya Mashariki na kuanzisha koti maarumu itakayo husika na kesi za kiaaramia.
Jack Lang, ambaye alikuwa waziri wa utamaduni wa Ufaransa, alisema " inabidi kuanzishwa koti ya kushughulkia kesi za kiaramia ili kukabili mlolongo wa watuhumiwa ambao huwa wanaachiwa huru.
Hadi kufikia sasa serikali ya Kenya na Ushelisheli ndizo zilizo weza kuwahukumu maharamia kwa kutumia sheria zilizpo nchini mwao.
Picha hapo juu wanaonekanaa baadhi ya maharamia wakinyoosha mikono mara baada ya kuwekwa chini ya ulinzi.

Tuesday, January 25, 2011

Serikali ya Palestina yakanusha kuridhia Waizrael.

Serikali ya Palestina yakanusha kuridhia Waizrael.
Ukanda wa Magharibi, Palestina - 25/01/2011. Serikali ya Wapalestina imekanusha vikali habari zilizo patikana ya kuwa uongozi huo umeridhia swala Wakimbizi wa Kipalestina.
Kwa mujibu wa habari zinasema "uongozi wa Wapalestina umekuwa na ukifikilia kukubaliana na serikali ya Izrael kuhusu swala la kurudi kwa wakimbizi wa Kipalestina waopo nje ya Palestina, ambapo zinasema itakuwa vigumu kwa wakimbizi wote kurudi Palestina."
Swala la kurudi kwa wakimbizi wa Kipalestina imekuwa moja mjadara unao letamvutano kati ya Waizrael na uongozi wa Wapalestina.
Picha hapo juu wanaonekana rais wa Amerika Baraka Obama katikati na kushoto ni Benyamin Netanyahu akitaka kupeana mkono na rais wa Wapalsetina Mahamoud Abbas mwaka jana wakati walipo kutana kujadii njia mbadala za kumaliza mgogoro kati yao.

Saturday, January 22, 2011

Tony Blair awelwa kiti moto tena.

Tony Blair awekwa kiti moto tena London, Uingereza - 22/01/2011. Aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza wakati wa vita vya Irak na kumtoa madarakani hayati Saadam Hussein ameojiwa kwa mara nyingine tena na tume ya uchunguzi wa mwenendo mzima wa vita vya Irak. Tony Blair ambaye alikuwa waziri mkuu wa Uingereza, chini ya serikali yake alishirikiana na serikali ya Amerika iliyo kuwa ikiongozwa na rais George Bush na kumn'goa madarakani rais Saadam Hussein wa Irak. Akiongea mbele ya tume hiyo Tony Blair alisema " nasikitika kwa kwa wale wote waliopoteza maisha au kuathirika kutokana na vita hivi." Na nilimwahidi rais wa Amerika ya kuwa kutakuwa bega kwa bega katika vita hivi kwani niliamini Saadam Hussein alikuwa kiongozi hatri kwa jumuia ya kimataifa." Uingereza na Amerika kwa kushirikiana na washiriki wengine ziliongoza vita vilivyo vikia kungólewa madarakani kwa rais wa Irak, Saadam Hussein. Picha hpo juu ni ya aliye kuwa waziri mkuu wa Uingereza Tony Blair ambaye aalikuwa akijibu maswali kutoka katika tume ya kuchunguza mwenendo mzima wa vita vya Irak.

Kiongozi wa Al Qaeda atishia Wafaransa.
Paris,Ufaransa - 22/01/2011. Kiongozi wa kundi la Al Qaeda ametishia na kuitaka serikali ya Ufaransa kutoa wanajeshi wake aliopo katika nchi za Kiislaam.
Osama Bin Laden alisema kwa kupitia habari zilizo patikana katika vyombo vya habarai kwa kudai " ili raia wa Ufaransa waachiwe inategemea uamuzi wa serikali yao kutimiza moja ya masharti ambapo ni kwa serikali ya Ufaransa kutoa majeshi yake katika nchi za Kiislaam."
Kuongea huko kwa kiongozi wa Kundi la Al Qaeda kunaendana na kuungwa mkono m\na na kundi la AQIM ambalo ndilo kundi kubwa lililopo Kaskazini Magharibi mwa Afrika linalo shirikiana na Al Qaeda, na hivi karibuni limehusika katika mauaji na utekaji nyara wa wengi raia wa Ufaransa.
Picha hpo juu ni ya Osama Bin Laden, ambaye ni kiongozi wa kundi la Al Qaeda, na hajulikani mahali alipo au anapo ishi.

Wednesday, January 19, 2011

Ombi la kukamatwa kwa Tzipi Livni lakataliwa.

Odinga, Ouwattara na Gbagbo hakuna maelewano.

Abidjan, Ivory Coast-19/01/2011. Msuruhishi wa mgogoro wa kisiasa nchini Ivory Coast ambaye pia ni waziri mkuu wa Kenya ameondoka nchi humo bila kupata suruhisho la mgogoro huo.
Raila Odinga ambaye alipewa jukumu la kusuruhishwa mgogoro huo wa kisiasa aliwaambia waandishi wa habari ya kuwa imekuwa vigumu kufikia muaafaka kati ya pande zote mbili za kisiasa.
Akisisitiza Odinga alisema "muda wa mazungumzo ya hiyari unazidi kuwa finyu."
Hata hivyo msemaji wa serikali ya rais Laurent Gbagbo alisema "hatutakubali tena kuongea na Raila Odinga kwani anapendelea upande mmoja wa bwana Ouawattara na hatuko tayari kumpokea."
Picha hapo juu anaonekana Raila Odinga akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mazungumzo na Laurent Gbagbo pichani kulia na Alassana Ouwattara pichani kushoto.
Amerika na China kushirikiana kwa karibu zaidi.
Washington, Amerika- 19.01/2011. Serikali ya Amerika na Uchina zimekubaliana kushirikiana katika usalama wa maswala ya kinyuklia na sekta za kibiashara. Kufuatia mikataba hiyo China itanunua ndege za aina ya boingi 200 na kuwekeza nchini Amerika vitega uchumi katika kilimo,mawasiliano. Wakiongea mbele ya waandishi wa habari marais hao walisema kukutana kwao kumeweka msingi mzuri ambao nchi zote mbili zitanufaika." Picha hapo juu wanaonekana rais wa Amerika Baraka Obama kushoto na rais wa China Hu Jintao wakiwasalimia wanchi waliokuja kuwalaki kabla ya kuanza mazungumzo rasmi kati yao jinsi ya kushirikiana kwa ukaribu zaidi. Watunisia watakiwa kuungana. Tunis, Tunisa- 19/01/2011. Rais wa kipindi cha mpito nchini Tunisia ametangaza yakuwa atahakikisha maswala yaliyo leta kutokuelewana na kunyanyasa wanachi hayatarudiwa tena na kutaka wanchi wa Tunisia kufungua ukurasa mpya. Fouad Mebazaa, akitangaza kupitia TV na vyombo vingine vya taifa na kimataifa alisema, sisi sote kwa pamoja tunaweza kuiongoza na kuijenga nchi yetu na hivyo tufungue ukurasa mpya ili kuijenga nchi yetu ambayo imeyumba kisiasa na kiuchumi." Hata hivyo bado kunahali ya mvutano wa kisiasa nchini Tunisia huku wanchi wakudai ya kuwa bado serikali hiyo inaviongozi waliokuwa wakati wa utawala wa rais Zine Ben Ali ambaye ameikimbia nchi baada ya wanachi kutaka atoke madarakani. Nayo serikali ya Swissi imezizuia mali zote za aliyekuwa rais wa Tunisia Zine Ben Ali. Picha hapo juu anaonekana rais wa mpito wa Tunisia Fouad Mebazaa akishuka kutoka kwenye gari, huku akiwa analindwa vikali na walinzi wake tayari kuelekea ofisini kuanza kazi rasmi ya kuongoza nchi. Ombi la kukamatwa kwa Tzipi Livni lakataliwa. Pretoria, Afrika ya Kusini- 19/01/2011. Serikali ya Afrika ya Kusini imekataa ombi la kutaka akamatwe aliyekuwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Izrael ambaye anatarajiwa kufanya ziara nchini humo. Ombi hilo lilitolewa na Shirika la Uhusiano la Wapalestina, kwa adai ya kuwa aliyekuwa waziri wa mamboya nje wa Izrael Tzipi Livni alihusika katika wakati jeshi la Izrael lilipo shambulia eneo la Gaza mwidho wa mwaka 2008 hadi mwanzoni mwa mwaka 2009. Mclntosh Polela ambaye ni msemaji wa ofisi ya usalama na makosa ya jinai alisema "tumepata ombi la kutaka kukamatwa kwa aliyekuwa waziri wa mambo ya njee wa Izrael na hatutachukua hatua hiyo na Tzipi Livni hatakamatwa kwani hakuna ushahidi wa kutosha zidi yake." Picha hapo juu ni ya Bi Tzipi Livni, ambaye alikuwa waziri wa mambo ya njee kati ya miaka ya 2009-9.
Mtoa siri za benki za Swisi ahukumiwa.
Zuriki, Uswisi - 19/01/2011. Mahakama jijini Zuriki imemkuta na makosa aliyekuwa mfanyakazi wa benki aliyehusika kutoa nyaraka za siri kwa Wikileaks ambazo zinaonyesha majina ya watu ambao wameweka pesa katika benki nchini humo.
Mshitakiwa huyo Rudolf Elmer alihukumiwa kwa kutozwa faini ya kiasi cha Swiss 7,200 ($7,505) na kuwa chini ya uangalizi kwa muda wa miaka miwili.
Akitoa hukumu hiyo hakimu alikataa ombi la mwasheria kwa upande wa mashitaka kwa kutaka adhabu ya kifungo itolewe kwa bwana Ridolf Elmer.
Rudolf Elmer alikubali makosa yake kabla ya hukumo hiyo kutolewa.
Picha hapo juu anaonekana Ridolf Elmer ambaye alikutwa na hatia ya kutoa nyaraka za siri za benki kwa mtandao wa habari wa Wikileaks. Jumuiya za nchi za kiarabu za tahadhalishwa.
Sharm el Sheikh, Misri-19/01/2011. Viongozi wa nchi za Kiarabu wamekutana nchini Misri ili kutasmini hali halisi ya jumuiya hiyo na kujadili wimbi la magauzi ambalo linaelekea kuzikumba nchi za Kiarabu.
Amir Mussa ambaye ni katibu mkuu wa jumuia ya nchi za Kiaarabu waliwaambia viongozi wa nchi wanachama ya kuwa hali ya kiuchumi katika nchi hizo inabidi ziangaliwe kwa undani sana, na "inatakiwa kuwepo na mabadiliko ya kiuchumi kwa serikali hizo kuwekeza rasilimali vitega uchumi ilikuinua maisha ya wanchi wa nchi hizo."
Akiongezea Amr Mussa alisema "mapinduzi yaliyo tokea nchini Tunisia lazima ma yaangaliwe kama mfano kwa serikali za nchi hizo."Na aliwataka wanchi wa nchi za Kiarabu kuwa pamoja ili kujenga nchi zao na eneo zima kwa ujumla.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Misri Hosni Mubaraka akipokea ujumbe toka kwa moja ya washuri na huku katibu Amr Muoussa, akiangalia kwa makini.

Saturday, January 15, 2011

Rais wa Tunisia akimbia nchi.

Rais wa Tunisia akimbia nchi.

Tuinis, Tunisia 14/01/2011. Rais wa Tunisia amekimbilia nchini za Uarabuni baada ya hali ya kisiasa kuwa katika hali mbaya kwa upande wa uongozi wake.
Zine El Abidine Ben Ali ambaye ametawala nchini Tunisia kwa zaidi ya miongo miwili na nusu alikimbia nchi huku hali ikiendelea kuwa mbaya kufuatia maandamano yalifanywa na wanchi wa Tunisia kupinga hali ya kiuchumi kuwa ngumu.
Kufuatia kuondoka nchi kwa rais huyo, spika wa bunge Fouad Mebezaa ameapishwa kuwa rais wa muda ili kuiongoza Tunisia mpaka hapo uchaguzi mpya utakapo fanyika.
Picha hapo juu anaonekana rais wa zamani wa Tunisia enzi zake wakati alipo kuwa akiwasalimia wananchi mara katika moja ya sheehe za kitaifa.

Thursday, January 13, 2011

Wahaiti wakumbuka siku ya tetemeko la ardhi.

Wahaiti wakumbuka siku ya tetemeko la ardhi. Port au Prince, Haiti - 13/01/2011. Maelfu ya wananchi wa Haiti wamekutana katika jiji la Port au Price kukumbuka siku ambayo tetemeko la ardhi lilitkea na kupoteza maisha ya watu na kuleta maafa makumbwa kwa kila jamii kiuchumi na kiafya. Tetemeko hilo ambalo lilipoteza maisha ya watu wapatao 316,000 kupoteza maisha yao na wengine kujeruhiwa vibaya. Kwa mujibu wa mashirika tofauti yanayotoa misaada nchini Haiti yamesema " hadi kufikia sasa hali nchini humo bado siyo ya kulizisha na juhudu zinatakiwa kuongezeka ili kuijenga nchi hiyo na kuinua hali ya misha ya watu wake." Picha hapo juu ni misaraba ikiwa inawakilisha watu waliopoteza maisha wakati wa tetemeko la ardhi lililo tokea mapema mwaka 2010. Waamerika waombwa kuungana na kushirikiana. Tucson, Amerika - 13/01/2011. Rais wa Amerika amewataka Waamerika wote kuungana na kuishi kwa ushirikiano ijapokuwa kunatofauti za kisiasa. Rais, Baraka Obama aliyasemahayo wakati alipo udhulia siku maalumu ya kuwakumbuka watu walioshambuliwa kwa risasi na kupoteza maisha ya kwenye jimbo la Arizona. Baraka Obama alisema " mambo mabaya hutokea na nilazima tujitahidi kuwa wavumilivi hasa tukizingatia tumepoteza watu sita kutokana na ukatili uliofanyaka." Mtu anayehusika na mauaji hayo Jared Lougher 22 anashikiliwa kutokana na kufanya kitendo hicho cha kikatili. Picha hapo juu wanaonekana rais Baraka Obama akiwa na mke wake Micheel wakishika kwenye ndege kuelekea kuhudhulia siku maalumu ya kuwakumbuka watu waliopoteza maisha wakati wa mashambulizi ya kikatili.

Wednesday, January 12, 2011

Kesi ya Julian Assange yaanza kusikilizwa.

Kesi ya Julian Assange yaanza kusikilizwa.

London, Uingereza - 12/01/2011. Mwanasheria wa mwanzilishi wa WikiLeaks ameiambia mahakama ya kuwa mteja wake atahukumiwa kifo ikiwa atapelekwa nchini Amerika. Mwanasheria huyo, alisema " ikiwa Julian Assange atapelekwa nchini Sweden, basi kunauwezekano mkubwa wa mteja wake kupelekwa nchini Amerika na kuhukumiwa adhabu ya kifo." Julian Assange, ambaye anatakiwa nchini Sweden kwa kosa la kufanya mapenzi rubuni amekuwa anapinga na kuwa alifanya kitendo hicho kama kinavyo elezwa.
Picha hapo juu anaonekana Julian Assange,akielekea mahakamani kusikiliza kesi yake.
Mafuriko yazidi kuleta athari kubwa nchini Australia.
Brisbane, Australian - 12/01/2011. Maelfu ya wakazi wa mji wa Brisbane wamehama mji mara baada ya mji mzima kukumbwa na mafuriko ya kihistoria.
Anna Bligh, alisema "zaidi ya makazi 20,000 huenda yakakumbwa na mafuriko na kuwaacha wakazi wake bila kitu."
Hali ya mafuriko nchini Australia imekuwa ikeendelea kwa kasi na kusabababisha hasara kubwa sana kwenye maeneo ambayo yamekumbwa na mafuriko.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya waokoaji wa huduma ya kwanza wakiwa ndiani ya boti tayari kutoa msaada.
Serikali ya Rebanon yavunjika.
Beiruti, Lebannon - 12/01/2011. Serikali ya Lebanon imevunjika baada ya washiriki katika serikali ya muungano Hezbollah kujitoa.
Kuvunjika huko kwa serikali kumekuja baada ya kuzuka mabishano makubwa jinsi ya kupiga kura ili kuunga mkono matokeo ya uchunguzi wa mauaji aliyekuwa waziri mkuu Rafik al Hariri
mwaka 2005.
Serikali ya Lebanon imevunjika wakati waziri mkuu wa Saad Hariri akiwa ziarani Amerika kukutana na rais Baraka Obama.
Katibu mkuu wa umoja wa Matifa Ban Ki-moon alisema " ningependa kuwataka Walebanon kutatua maswala yao kwa amani na huru na umoja wa mataifa upo pamoja nao."
Hadi kufikia sasa uchunguzi wa kessi hiyo na matokeo yake yamekuwa yakipingwa na kundi la Hezbollah kwa madai ya kuwa matokeo yaina yoyote yatakuwa ya kisiasa hivyo haita yatambua.
Picha hapo juu ni ya aliyekuwa waziri mkuu wa Rafik al Hariri ambaye aliuwawa na bomu lililolipuliwa na watuwasiojulikana.

Sunday, January 9, 2011

Wasudan wapiga kura kuamua muungano wa nchi yao

Wasudan wapiga kura kuamua muungano wa nchi yao.

Juba, Sudan - 09/01/2011. Wananchi wa Sudan wamepiga kura ili kuamua kama nchi yao itabaki moja au kugawanyika kuwa Sudan ya Kusini na Sudan ya Kaskazini.
Kwa mujibu wa wasimamizi wa uchaguzi huo wamesema wanchi wa Sudan wameudhulia katika vituo vya kula kwa wingi.
Salva Kiir ambaye ni kiongozi wa Sudan ya Kusini alisema " upigaji wa kura waleo ni kumaizia kazi iliyo anzwa na kiongozi wetu John Garang na inathibitisha kazi yake haikupotea bure.
Picha hapo juu anaonekana kiongozi wa Sudan Kusini Salva Kiir akipiga kura katika moja ya vituo vya kupigia kura.