Wednesday, July 25, 2012

Wananchi Ghana waanza maombelezi baada ya kifo cha rais.

Wananchi  Ghana waanza maombelezi baada ya kifo cha rais.


Akkra, Ghana - 25/07/2012. Wananchi na wakazi waishio nchi Ghana, wameanza maombelezi bada ya rais wa nchi hiyo kufariki baada ya kuugua kwa  muda fupi.
Hayati rais John Atta Mills 68 ambaye alichaguliwa kuwa rais wa Ghana kwa kumshinda mpinzani wake Nana Akufo-Addo kwa kiasi kidogo cha kura mwaka 2008.
Kufuatia kifo cha rais Attap-Mill, makamu wake wa urais John Dramani Mahama ameapishwa kuwa rais wa Ghana kuanzia sasa mpaka hapo uchaguzi wa rais mpya utakapo anza mwisho wa mwaka huu.

Kesi zidi ya makamu wa rais wa Irak yaharishwa.

Baghdad, Irak 25/07/2012. Kesi inayo mkabili makamu wa rais wa Irak na ambaye yupo ukimbizi nchi Uturuki imeharishwa.
Kesi hiyo ambayo inamkabili aliyekuwa makamu wa rais  Tariq al-Hashimi ilihairishwa baaada ya rais wa Irak Jalala Talabani kukataliwa kutoa ushahidi mbele ya mahakama.
Makamu wa rais Hashimi anakabiliwa na kesi ya kuhusika katika mauaji na mateso ambayo amekanusha.

Nchi zajumuiya ya  Ulaya hakuna mafikiano juu ya Hezbollah

Brussels, Ubeligiji - 25/07/2012. Jumuiya ya nchi za Ulaya imelikataa ombi la Izrael la kutak kundi la Hezbollah llilipo Lebanoni kuingizwa katika makundi yanayo husika na ugaidi.
Waziri wa mambo ya nje ya nchi wa Cyprus Erato Kozakou-Marcoullis ambaye nchi yake ndiyo inayoshikilia urais wa nchi za jumiya ya ulaya alisema "kwa sasa hakuna makubaliano ya kuliunganisha kundi la Hezbollah kama kundi la kigaidi."
Waziri Kozakou-Marcoullis aliyasema hayo baada ya Izrael kuzitaka nchi za jumuiya ya Ulaya kuliunganisha kundi la Hezbollah kuwa moja ya makundi ya kigaidi.
Izrael imeilaumu kundi la Hezbollah kwa kuhusika na bomu lililo lipuliwa nchini Bulgaria na kusabababisha vifo vya raia wa Izrael na wengine kujeruhiwa wakati wakiwa matembezini nchi humo.

Saturday, July 21, 2012

Mkuu wa polisi wa Afrika ya Kusini kutolewa jela.

Mkuu wa polisi wa Afrika ya Kusini kutolewa jela.


Johannesburg, Africa ya Kusini - 21/07/2012. Aliyeuwa mkuu wa polisi nchini Afrika ya Kusini na ambaye anatumikia kifungo, anatarajiwa kutolewa hivi karibuni kutoka jela.

Waziri wa magereza wa Afrika ya Kusini Sibusiso Ndebele alisema "Jack Selebi ataachiwa kutaokana na kuwa na matatizo ya figo na mtatizo mengine ya kiafya.
Jackie Selebi 62 alihukumiwa kwenda jela baada ya kukutwa na hatia ya kuopea rushwa mwaka 2010 nakuhumiwa kifungo cha jela miaka 15.
Mahakama ya kimataifa yataka rais wa zamani wa Chad akamatwe.

Brussells, Ubeligiji -21/07/2012. Mahakama ya kimataifa inayoshughulikia makosa ya ukiukwaji wahaki za binadamu ya Ubeligiji, imetaka aliyekuwa rais wa Chad akamatwe ili ajibu mashitaka ya kukiuka haki za binadamu.
Hissene Habre ambaye alikuwa rais waChad, anashitakiwa kwa makosa ya kukiuka haki za binadamu wakati wa utawala wake katika ya miaka ya 1982 - 1990.
Kesi zidi ya Hissene Hebre ilifunguliwa na raia wa Ubeligiji mwenye asili ya Chad kwa madai ya kuwa wakati wa utawala wa  Hissene Hebre watu wapatao 40,000 waliteswa na hata wengine kupoteza maisha.
Hissene Hebre yupo ukimbizini nchi Senegal ambako alikimbilia baada ya utawala wake kuondolewa.
Izrael ya ombeleza vifo vya watu walo fariki na mlipuko wa basi

Burgas, Bulgaria - 21/07/2012. Polisi nchini Bulgaria bado wanatafuta muhusika katika tukio la kulipua basi lililo kuwa limewabeba abiria wa Kiizrael.
Akiongea na waandishi wa habari, waziri wa mambo ya ndani wa  Bulgaria Tsvetan Tsvetanov alisema "hadi sasa tumetambua ya kuwa aliyelipua basi hakuwa raia wa Kibulgaria na uchunguzi bado unaendelea."
Jiji la Burgas lilikumbwa na mshituko mkubwa baada ya basi lililo beba abiria wa Kiizrael kulipuka na kusababisha vifo na majeruhi walokuwa katika matembezi jiji humo.
Kufuatia mlipuko huo serikali ya Izrael imezilaumu Iran na washiki wake kwa kuhusika na mlipuko huo, jambo ambalo Iran imekanusha.

Friday, July 13, 2012

Venezuela yapelek mafuta nchi Syria.

Venezuela yapelek mafuta nchi Syria.


Karakas, Venezuela - 13/07/2012.  Serikali ya Venezeula imepeleka mafuta nchini Syria kufuatia viwazo vilivyo wekewa nchi hiyo.
Uamuzi wa serikali ya Venezuela kupeleka mafuta nchini humo umekuja kutokana na uhusiano uliyopo kati ya nchi hizo mbili.
Habari kutoka serikali ya  Venezuela zinasema  "mafuta yatazidi kupelekwa nchini Syri kma kawaida."
Serikali Venezuela imetumia meli zake za kusafirisha mafuta kufuatia mashirika ya meli na bima za nchi za Ulaya na Marekani kukataa kuzidhamini meli za mafuta zinazo peleka mafuta nchi Syria baada ya vikwazo kuwekwa kwa serikali ya rais Bashar al Assad.

Ruksa kutailiwa kufuatia imani za dini nchini Ujerumani.

Berlin, Ujerumani - 13/07/2012.  Kansela wa Ujerumani ameunga mkono jamii za Kiyaudi na za Kiislaamu zinazo taka kitendo cha kutahiriwa kiendelee katika jamii zao.
Mseamji wa Kansela Angela Merkel, Steffen Seibert alisema " kutailiwa kwa watoto wa kiume ni kitendo ambacho kinakwenda sambamba na imani ya dini hizo na hakuna adhabu itakayo tolewa.
"Na ieleweke serikali inaruhusu haki ya kiimani na Wayahudi na Waislaam ni Wajeruamani hivyo wanahaki sawa na Wajerumani wangine."
Kuungwa mkuno huko kwa kitendo cha kutailiwa kumekuja baaada ya dakitari mmoja kutokutwa na hatia ya kusababisha maumvu kwa mtoto aliye mtairi, ambapo idaiwa mtoto huyo alikutwa na matatizo ya kiafya kutokana kutailiwa huko.
Hata hivyo kitendo cha kutailiwa kimekuwa kinaleta mvutano katika jamii nchi Ujerumani huku wengine wakipinga na wengine wakiunga mkono.

Marekani yaongeza nguvu za kijeshi kanda za Ghuba

Washington, Marekani - 13/07/2012.  Serikali ya Marekani kimeongezea siraha na nguvu za kijeshi katika nchi zenye makao yake ya kijeshi zilizopo katika nchi za Ghuba.
Kwa mujibu wa habari zilizo tolewa zinasema " uamuzi wa serikali ya Marekani kuogeza nguvu zake za kijeshi katika eneo hilo jimekuja katika harakati za kutaka kuizuia Iran isiweze kuzuia ghuba ya Hormuz kama ilivyo tangaza hapo awali."
Iran ambayo imewekewa vikwazo na Marekani na nchi washiriki wake ilitangaza hapo awali yakuwa itafunga njia ya Hormuz ambayo inatumika kusafirisha mafuta kutoka katika nchi zilizopo maeneo hayo.

Sunday, July 8, 2012

George Bush ashiriki ujenzi wa Zahanati nchi Zambia

Roger Federer akata ndoto ya Waingereza.

London, Uingereza - 08/07/2012. Roger Federer amekata ndoto ya Waingereza baada ya kushinda kwa mara ya saba kombe la tenisi la Wimbledon kwa upande wa wanaume.
Roger Feder ameweka kibindoni makombe makubwa 17 (Grand Slam) na kuwa sawa na mchezaji maarufu wa mchezo huo Peter Sampras katika ushindi wa kombe la Wimbledon.
Ushindi huo wa Roger Federer alipata baada ya kumshinda Andy Murry kwa seti 4-6, 7-5, 6-4 jambo ambalo limezima ndoto ya wapenzi wa mchezo wa tenis nchi Uingereza ya kuwa huenda mwaka 2012 ungekuwa wao kwa mchezji  Mwingereza kushinda kombeli hili ambalo kwa mara ya mwisho mchezaji wa Uingereza alishinda mwaka 1936.

George Bush ashiriki ujenzi wa Zahanati nchi Zambia
Lusaka, Zambia- 08/07/2012. Aliyekuwa rais wa Marekani alifanya ziara nchi Zambia na  Botswana ili kuimarisha ufahamu wa ugonjwa wa saratani ( Kansa).
Akiwa nchi Zambia, George Bush, alishiriki katika ujenzi wa  zahanati itakayo toa matibabu ya ugonjwa wa kansa ( saratani) katika mji wa Kabwe na baadaye alizungumza na viongozi wa serikali na viongozi wa maswala ya afya ya Zambia.
George Bush ambaye alisha wahi kufanya ziara barani Afrika, amekuwa akitoa kipao mbele katka harakati za kupambana na magonjwa yanayo tisha ikiwemo ukimwi na malaria katika bara la Afrika tangu alipo kuwa rais wa Marekani na hadi sasa.

Jeshila Bosco Ntaganda lazidi kuteka miji nchi JM-Kongo.


Rutshuru, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo - 08/07/2012. Jeshi la upinzani wa serikali ya JD-Kongo limeteka nyara mjiwa Rutshuru uliyopo km 70 Kusini mwa mji wa Goma baada ya jeshi la serikali kuzidiwa nguvu.
Jeshi hilo la upinzani wa serikali ya Komgo linalo ongozwa na  Generali Bosco Ntaganda,lili chukuwa mji huo muhimu baada ya mapigano makali na jeshi la serikali na baadhi ya wanajeshi wake kukimbilia nchi Uganda.
Wakati huo huo mwanajeshi wa kulinda amani wa umoja wa mataifa kutoka India aliuwawa katika harakati za jeshi laupinzani wa serikali lilipo fanya mashambuli katika mji wa Bunagana.

Rais wa Misri atengua uamuzi wa jeshi la Misri.

Kairo, Misri - 08/07/2012. Rais wa Misri ametengua uamuzi wa jeshi la nchi hiyo kwa kuamuru baraza la bunge la nchi hiyo kurudi bungeni mara moja na kuanza kazi yake ya bunge.
Rais Mohamed Musri alitoa mri hiyo kwa kuvunja amri ya koti kuu ya nchi yakuwa bunge  lazima lirudi kazini mpaka hapo uchguzi mpya utakapo fanyika.
Amri hiyo ya kuvunjwa kwa bunge nchi Mirsi ilitolewa na jeshi wakati lilipo kuwa limeshikilia madaraka baada ya kuangushwa kwa utawala wa rais Hosni Mubarak.
Kufuatia kuvunjwa kwa amri hiyo na rais Mohamed Musri, wakuu wa jeshi nchi Mosri wameitisha kikao cha dharula ili kujadili uamuzi huo wa rais. 

Rais wa Syria aishutumu Marekani.

Damascus, Syria - 08/07/2012. Rais wa Syria ameishutumu Marakani kwa kusababisha vurugu nchi Syria ambazo zinaleta myumbo wa kisiasa, kijamii na kiuchumi.
Rais Bashar al Assad akiongea  alisema " Marekani kwa kusaidiana na Katar na Saudi Arabia wana saidia magaidi  ambao ndiyo chanzo cha vurugu nchini Syria.
" Pia majirani zetu Uturuki wanawapa magaidi hawa waliopo Syria kila msaada wanao uhitaji, na kama hali hii ikiendelea basi magaidi watakuwepo na wapo tayari kushirikiana na Marekani.
"Tumekamata wapiganaji wengiwa kundi la Al Qaeda waliotokea nchini Tunisia na Libya na Marakani inahusika pia katika mauaji ya raia wa Syria."
Wakati huohuo jeshi la Syria limeaanza mazoezi ya kijeshi ili kujua kwa kiasi gani jeshi la nchi hiyo lipo tayari  ikiwa vita vikubwa  vitaanza katika nchi hiyo.

Saturday, July 7, 2012

Afghanistan kuwa mwanachama huria wa NATO.

Serena Williams ashinda Wimbledon kwa mara ya Tano.

London, Uingereza - 07/07/2012. Serena Willliams ameshinda tena kwa mara ya tano kombe la mashindano ya tennis ya Wimbledon.
Serena alimshinda Agnieszka  Rwadwanska kwa 6-1, 5-7, 6-2 na katika mchezo ambao ulikuwa wa vuta ni kuvute.
Ushindi huu Serena Williams wa mara ya tano katika kombe la tennis la Wimbledon  umekamilisha hatua ambayo dada yake Venus alisha wahi kushinda kombe hilo.
Serena Williams ameshinda kombe hilo mwaka 2002,2003,2009, 2010, 2012  na kuwa mmoja ya wacheza tennis kwa upande wa wanawake kushinda kombe tennis la Wimbledon  hilo mara nyingi

Rais wa Afrika ya Kusini achorwa magazetini na sehemu za siri.

Johannesburg, Afrika ya Kusini - 07/07/2012.  Chama tawala nchi Afrika ya Kusini kimelaani kitendo cha mchoraji wa vikatuni wa gazeti la Gurdian na Mail wa Afrika ya Kusini kumchora rais wa nchi hiyo na kuonyesha sehemu zake za siri.
Jonathan Shapiro alichora kikatuni ambacho kinamwonesha rais Jacob Zuma sehemu zake za siri, jambo ambalo limepingwa vikali na serikali ya Afrika ya Kusini.
Kuchorwa huku kwa rais Jacob Zuma kumekuja baada ya siku za nyuma baada ya msaani mmoja kuandaa maonyesho ya sanaa za uchoraji ambapo zilikuwepo picha za zinazo onyesha sehemu za siri  za rais Jacob Zuma.

Jeshi la Iran la tangaza kugundua miali siraha.

Tehran, Iran - 07/07/2012. Jeshi la Iran limetangaza ya kuwa limetengeneza miali siraha ambayo inaweza kuongoza mitambo yake ya kivita.
Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia General Ahmad Vahidi akiongea na waandishi wa habari alsema " miaali siraha ambayo tumeitengeneza itatusaidia katika kutuongoza kujua adui yupo wapi,kuongoza katika kushambulia siraha ya angani na siraha za aina nyingine.
"Miali siraha hii ni ya kisasa na inauwezo mkubwa na kwa jina ni Dehlavieh na itasaidia katika kuimarisha ulinzi wetu.
Kitendo cha Iran kutangaza kugundua miali siraha hii kumekuja siku chache baada ya jeshi la nchi hii kufanya mazoezi ya kijeshi na kurusha makombora katika harakati za kujua uwezo wa jeshi na nguvu za jeshi hilo.  

Tumbaku bado haijafa thamani yake nchi Marekani.

Kentuck, Marekani - 07/07/2012. Ukulima wa zao la tumbaku umeongezeka nchi Marekani kufuatia mahitaji makubwa ya uvutaji wa sigara.
Katika mji wa Kentuck, wakulima wa mashamba hayo wamekuwa wakiongeza ukulima huo, baada ya faida kuonekana kutokana na mahitaji ya sigara kuongezeka katika bara la Afrika na  Asia.
Hata hivyo wakati mahitaji ya uvutaji wa sigara yakiongezeka katika nchi za Afrika na Asia, barani Ulaya na Marekani uvutajiwa wa sigara umekuwa ukipigwa vita na vyama, mashirika yasiyo ya kiserikali na serikali zenyewe ili kuweza kupunguza vifo vinavyo sababishwa na uvutajiwa wa sigara.

Walibya wapiga kura ya vyama vingi kwa mara ya kwanza.

Tripol, Libya - 07/07/2012. Wanachi wa Libya wamepiga kura kwa mara ya kwanza katika uchaguzi uliyo husisha vyama vingi tangu kuangushwa kwa utawala wa Muammar Gaddafi.
Zaidi ya watu million 2 walijiandikisha kupiga kura ili kuwachagua wabunge 200 ambao wata unda bunge ambalo litakuwa naserikali ambayo itachukua madaraka kutoka katika serikali ya mpito.
Walibya ambao wamepiga kura kuwachagua wabunge wao nakimekuwa ni kitendo ambacho hakijawahi kufanyika zaidi ya miaka 40 iliyo pita tangu Muaamar Gaddafi achukue madaraka.

Afghanistan kuwa mwanachama huria wa NATO.

Kabul, Afghanistan - 07/07/2012. Afghanistan inatarajiwa kuwa mwanachama huria wa nchi za NATO.
Maelezo hayo yalitokewa na waziri wa mambo ya nje ya nchi wa Marekani baada ya kukutana na rais wa Afghanistan.
Hillary Clinton akiongea na waandishi wa habari alisema " uamuzi wa kuikaribisha Afghanistani katika NATO ni moja ya majukumu ya kudumisha uhusiano wa muda mrefu ambao utasaidia katika kujenga serikali ya mpito kuelekea kujenga demokrasi ya kweli na serikali imara ya  Waafghanistan."
Maelezo hayo ya waziri wa mabo ya nje wa Marekani Bi Hillary Clinton yamekuja wakati Marekani na washiriki wake katika NATO wakiwa katika harakati za kuondoz majeshi yao nchi Afghaniztani ifikapo mwaka 2014.
Nchi nyingine ambazo ni wanachama huria wa  NATO ni Pakistan, Izrael, Misri, Japan, Jodan, Korea ya Kusini, Australia na New Zealand

Thursday, July 5, 2012

Urusi yakanusha kuwa rais wa Syria kuchukua ukibizi.

Ligi kuu ya Uingereza kuanza kutumia teknolojia ya goli line.

London, Uingereza - 05/07/2012. Shirikisho la Soka Duaniani FFA limekubaliana kwa pamoja yakuwa teknolojia inayo julikana kama Hawk eye ya kutumia mtandao katika kuhakikisha mpira umevuka mstari wa goli inatumika.
 Kufuatia uamuzi huo wa FIFA, chama cha mpira nchi Uingereza kimeamua kuanzia msimu wa ligi wa mwaka 2012/13 teknologia hiyo itaanza kutumika.
Uamuzi wa kutumia teknolojia hiyo umekuja baada yamechi kati ya Uingereza na Ukraine kuleta matata ya umuzi wakati Ukraine ilipo pata goli lakini waamuzi wa mechi hiyo hawakona kama goli lilikuwa limeingia.

Urusi yakanusha kuwa rais wa Syria kuchukua ukibizi.

Moscow, Urusi - 05/07/2012. Serikali ya Urusi imekanusha uvumi iliyokuwa umevuma ya kuwa rais wa Syria  Bashar al Assad anampango wa kuchukua ukimbizi nchini humo.
Waziri wa mambo y kigeni wa Urusi Sergei Lavrov alisema " hakuna kitu kama hicho na wanaovumisha habari hizo wana njama zao binafsi na inaelekea wanaupungufu wa uelewa wa hali halisi."
Uvumi huo ya kuwa Urusi inampango wa kumpa rais wa Syria ukimbizi umekuja baada ya China na Urusi kuwa kinara katika kutetea serikali ya rais Bashar al - Assad ambayo inapingwa na nchi za Ulaya Magharibi na Marekani.

Wikileaks yachapisha habari za siri za Syria na washiriki wake.

London, Uingereza - 05/07/2012. Wikileaks imetoa mafaili yenye habari za nchi ya Syria na jinsi ilivyo jihusisha na nchi nyingine kisiasa, kiuchumi na kibiashara tangu mwaka 2006 hadi 2012.
Msemaji wa Wikileaks Sarah Harrison akiwakilisha maelezo ya Julian Assange aliseme " maelezo yaliyopo kwenye mafaili hayo yataleta aibu kwa serikali ya Syria na wale wanaojiita wapinzani wa Syria.
"Na itasaidia kuelewe ni kwa kiasi gani ukweli uliyopo na  ni kwanini vita vimetokea nchi Syria.
Wikileaks imelipa jina tukio hil kama " The Syria Files" na kudai ya kuwa kuna mafaili  zaidi ambayo yatafuta ikiwa ni mpango wake wakuchapisha habari hizo ambao ulianza 2010.

Tuesday, July 3, 2012

Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat watoa majibu nusu.

Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat watoa majibu nusu.

Paris, Ufaransa - 03/07/2012. Uchunguzi wa kisayansi uliyofanywa kuhusu kifo cha aliyekuwa kiongozi na rais wa Wapalestina umetoa majibu nusu tangu kuanza kwa uchunguzi huo.
Rais Yasir Arafat ambaye alifariki dunia nchini Ufaransa ambapo alipelekwa kwa ajili yamatibabu baada ya kuugua wakati akiwa amefungiwa  kutoka katika mji wa Ramallah na serikali Izrael.
Dr Francois Bochud ambaye ni mtaalamu wa Radiophysique iliyopo nchini Switzerland alisema " naweza kusema tumekuta aina ya gesi inayo julikana kama polonium-210 ambayo inaweza kuwa chanzo ca kifo chake na tunaweza kupata jibu sahihi ikiwa baadhi ya viungo vya marehemu Yasir Arafat vitapatikana kwa  uchunguzi zaidi."
Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat ulikuja baada ya mkewe Suha Arafat  kuruhusu uchunguzi kuendelea na kutoa ruhusa ya kuwa mwili wa Yasir Araf ufukuliwe kwa uchunguzi zaidi  na kuiomba serikali ya Wapalestina kushirikiana naye.

Iran yadia kupata ufahamu wa ndege ya Marekani waliyo iteka.

Tehran, Iran - 07/03/2012.  Jeshi la Iran limedai ya kuwa limepata uwezo wa kuisoma ndege inayo endeshwa kwa kutumia mtandao (Drone) ambao utasaidi jeshi hilo kiutaalamu.
Brigadia Generali Amir -Ali Hajizadeh aliema " ndege ya Marekani RQ - 170 ambayo tumeikamata itasaidia saana kwani tulicopata ni kitu ambacho maadui zatu hawakuta tukijue."
Maelezo hayo ya mkuu huyo wa jeshi la Iran yamekuja wakati jeshi la nchi hiyo likuwa katika mazoezi ya kijeshi ambayo yameanza hivi karibuni.

Ofisi na nyumba za Nikolas Sarkozy za vamiwa na polisi.

Paris, Ufaransa - 03/07/2012. Ofisi na nyumba anayoishi aliyekuwa rais wa Ufaransa Nikolas Sarkozy zimevamiwa na polisi katika haraki za kufanya uchunguzi zidi ya rais huyo wakati wa kampeni za uchaguzi.
Polisi hao ambao waliaandamana na wapelelezi waiiingia katika ofisi hizo na nyumbani kwa rais huyo na kuchukua baadhi ya mafaili na vitu vingine ambavyo vinashukiwa kuhusika katika uchunguzi huo.
Hata hivyo Nikolas Sarkozy amekanusha kuhusuka na tuhuma hizo na wala hakuhusika.
Uchnguzi huo umekuja ikiwa ni katika harakati za kutafuta ukweli kama kuna kitendo cha rushwa kilitendeka wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2007.


Rais wa Syria hatuta jenga huhasama na Uturuki kamwe.

Iran yazidi kujimarisha kijeshi.

Tehran, Iran - 03/07/2012. Jeshi la mapinduzi la Iran lmeanza mazoezi yake ya kijeshi siku chache kabla ya kuanza rasmi ka vikwazo kwa mafuta ya Iran katika nchi za jumuiya ya nchi za Ulaya.
Katika mzoezzi hayo jeshi la Iran limejaribu siraha zinazo julikana kam ShababMeteor) 1,2,3, Khalij Fars (Persian Gulf), Tondar(Lightning), Fateh (Victor),  Zelzal (Quake) na Qiam(Uprising).
Mazoezi hayo yaklijeshi ya Iran, yanafuati yale yaliyofanywa  mwezi wa Februari ambayo yalijlikana kama Val Farj.
Iran imekuwa ikivutana na nchi za Ulaya gharibi na Marekani kuhusu mradi wake wa kuendeleza nguvu za kinyuklia jambo ambalo hadi sasa halijapagtiwa ufumbuzi.

Kashfa zasabisha mkuu wa beni ya Barclays kujiudhulu uongozi wake.

London, Uingereza - 03/07/2012. Mkuu wa benki kubwa ya tatu nchi Uingereza Barclays, amejiudhulu uongozi wake kufuatia kashfa za benki hiyo kukiuka maadili ya kibenki.
Mkuu huyo Bob Diiamond imembidi ajiuzuru uongozi wake baada ya banki ya Barclays kukutwa na hatia ya kuwalipisha riba wateja wake kinyume na maadili ya kibenki jambo ambalo limeleta msituko mkubwa katika jamiii nzima ya mfumo wa benki unavyo endeshwa nchini Uingeereza.
Kujiudhulu huko kwa mkuu huyo waa benki kumekuja bada ya waziri mkuu wa Uingereza David Cameron kusema" nitaunda tume kupitia bunge ili kuchunguza uarifi huu uliyo tokea katika benki, kwa watu wanataka kujua ukweli na lazima tujifunze hali hi isije klutokea tena."

Rais wa Syria hatuta jenga huhasama na Uturuki kamwe.

Damascus, Syria - 03/07/2012. Rais wa Syria amesikitishwa na kitendo cha kuangushwa ndege ya jeshi la Uturuki wakati ilipo ingia anga za Syria.
Rais Bashar Al Assad alisema " tulijua ni ndege ya Uturuki baada ya kuiangusha, na naomba nieleweke kama tungejua ni ndege ya kijeshi ya Uturuki tusinge iangusha kamwe.
"Na hatutaruhusu uhasama kujengeka kati yetu na Uturuki kwani watu wapande zote mbili wataathirika kijamii na kiuchumi, na sisi hatutaweka jeshi letu karibu na mpaka na Uturuki japo serikali ya waziri mkuu Tayyip Erdogan imeweka jeshi lake mpakani na Syria."
Kuongea kwa rais Bashar al Asssad, kuhusu kuangushwa kwa ndege ya kijeshi ya Uturuki, huku hali kati ya nchi hizo mbili zikiwa katika utata.


Kampuni ya madawa ya Uingereza yapigwa faini.

Massachusetts, Marekani - 03/07/2012. Kampuni ya madawa ya Uingereza imepigwa faini baada ya kujulikana  kuepuka kwa makusudi kutoa maelezo ya dawa zake kwa watumiaji nchini Mareakani.
GlaxoSmithKline, imekubali kulipa kiasa cha dola za Kimarekani $3billion, baada ya kukutwa  na hatia na mahakama iliyopo Massachusetts.
Mwanasheria mwandamizi  wa serikali James M Cole alisema " hatutakubali wala kuachia afya za watu kuchezewa au kufanyiwa mchezo wa kirushwa,na kuanzia sasa hii ni onyo kwa makampuni mengine ya madawa."
Faini hiyo imekuja baada ya dawa zilizo tolewa na GlaxoSmithKline kwa ajili ya watu waliochini ya miaka 18 na kutumiwa kwa wagonjwa waliozidi umri wa miaka 18.


Sunday, July 1, 2012

Watu wauwawa kanisani nchini Kenya.

Uispania yaweka rekodi kwenye mchezo wa soka barani Ulaya.

Kiev, Ukraine - 01/07/2012. Uispania imeshinda  kwa mara ya tatu mfululizo ubingwa wa kombe la nchi za Ulaya baada ya kuifunga Itali magoli 4 bila.
Ushindi huo ulikuja baada ya wachezaji wa timu ya Uispania David Silva, Jordi Alba Fernando Torres na Juan Mata kufunga magoli ambayo yalizamisha matumaini ya Itali kuwa mabigwa.
Kocha mkuu wa Itali Cesare Pandelli akiongea baada ya mechi kuisha alisema "tumekunaa na timu yenye kustaili kushinda mechi hii."
Uispaania imekuwa nchi ya kwanza kihistoria kufunga magoli manne katika fainali ya kombe la Ulaya.

Watu wauwawa kanisani nchini Kenya

Geissa, Kenya 01/07/2012. Watu 17 wamepoteza maisha yao baada ya kushabuliwa wakati wakiwa kanisani.
Mashahidi walitoa habari kwa kusema " miili ya watu walio poteza maisha kutokana na mshambuliz hayo ilikutwa ndani ya kanisa na ndani ya kanisa kulikuwa kumetapakaa damu."
Mashambulizi hayo yalitokea katika kanisa wakati watu hao walikuwa wakisali baada ya  watu wenye siraha kuingia kanisani humo huku wakiwa wamejifunika nyuso zao na kufanya mashambulizi ambayo yaameleta mshutuko mkuu katika eneo hilo la Gerissa lililopo mpakani na Somalia.
Mashambulizi ya kigaidi nchi Kenya yamekuwa yakitokea  tangu serikali ya Kenya ilipoanzisha kampeni ya kupambana na wapiganji wa kundi la Al - Shabab la Somali na kundi hilo kushukiwa kuhusika na mashambulizi yanayo tokea nchini Kenya.

Mpango wa Kofi Annan juu ya Syria wakubalika.

Geneva, Uswisi 01/07/2012. Viongozi wa nchi zenye nguvu duniani wamekubaliana kwa pamoja  na mpago wa Kofi Annan ya kuwa Syria inahitaji serikaali ya mpito.
Kofi Annan, ambaye anasimamia upatikanaji wa amani nchi Syria alisema " wakati umefika sasa wa kushirikiana na serikali ya Syria inatakiwa iwajumuishe wapinzani wake katika kuongoza serikali."
Mkutano huo ambao uliudhurriwa na viongozi wa Urusi, Marekani, Uingereza China na wajumbe wa jumuiya ya Ulaya walikubaliana kwa pamoja ya kuwa  ufumbuzi wa tatizo la kisiasa nchini Syria  ni kuhakikisha ya kuwa serikali ya mpito inaundwa ili kusimamisha   vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vinaendelea kwa sasa.

Friday, June 29, 2012

Marais wa Somalia wakutana UAE - Dubai.

Mohamed Morsi aapishwa rasmi kuwa rais wa Misri.

Kairo, Misri - 29/06/2012. Aliyekuwa mshindi wa uchaguzi wa Urais nchini Misri atapishwa rasmi kuwa rais wa nchi hiyo kesho Jumamosi.
Rais Mohamed Morsi  akiongea mbele ya watu walio kuja kumsikiliza siku moja kabla ya kuapishwa na kuhaidi ya kuwa ataijenga nchi kwa kufuata misingi ya katiba na kisisitiza ya kuwa "hakuna mwananchi ambaye atakuwa juu ya sheria na sitaogopa mtu isipokuwa Mungu.
"Nitalinda nchi yangu na mkipaka yake na kuhakikisha safari  ya kuwa serikali ya kiraia inafikiwa."
Hotuba ya rais Mohamed Morsi imeonyesha kuwa hali ya jeshi kuchukua madaraka kama ilivyo fikiriwa itakuwa ngumu kwa kiasi kikubwa.

Nchi za jumuiya ya Ulaya zachukua hatua ya mbadala ilikuinua uchumi

Brussels, Ubeligiji - 29/06/2012. Viongozi wa jumuiya ya nchi za Ulaya wamekubaliana kwa pamoja kuinua benki zao kwa kuzipatia fedha ili kusaidi kuinua biashara  na uchumi.
Viongozi hao ambao walichukua karibu usiku mzima nakukubaliana kimsingi ya kuwa ipo haja ya kuinua hali ya mtiririko wa fedha ili kusaidi mwamko wa kiuchumi na kibiashara.
kansela Angela Merkel ambaye nchi yake ilikuwa inaaonekana kama ni kikwazo hapo awali alisema  " Nimeridhika na matokeo ya mkuno huu japo ulichukua muda mferu, lakini matokeo ya mkutano huu ni mazuri kwa nchi zote wanchama wa nchi za jumuiya ya Ulaya."
Makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano huo yameleta matumani makubwa kwa nchi za ispania na Itali nchi ambazo hali zake za kichumi fedha zilikuwa katika hali ya kuyumba.


Kampuni ya Nestle yalaumiwa.

London, Uingereza - 2012. Kampuni inayo shughulikia vyakula ya Nestle imelaumiwa kwa kutofanya uchunguzi mazingira ya kazi ambayo yanahusisha watoto wadogo.
Habari zilizo tolewa hivi karibuni na shirika linalo shughulikia na kusimamia ufanyaji wa kazi na usawa ( Fair  Labor Association - FLA) zimesema, " Nestle hakutilia maanani ni kwa jinsi gani  mazao yanayo uzwa na kuzalishwa na wakulima yana patikana kwa namna gani, kwani kuna ushaidi ya kuwa kuna watoto 1.8 million ambao wanafanyishwa kazi katika uzalishwaji wa mazo ya kampuni ya Nestle,  hasa  mashamba ya kakao yaliyopo Afrika ya Magharibi."
Nestle nikampuni kubwa duniani ambayo inajihusisha  na uzalishaji wa chokoleti duniani
hata hivyo makamu wa rais wa kampuni hiyo Jose Lopez alikanusha kwa kusema " Hatutumi watoto katika uzalishaji na tunapinga kitendo hicho katika nyanja  zetu zote za uzalishaji wa mazao ya Nestle. na huwa tunahakikisha ya kuwa hakuna watoto wanao tumiwa katika uazlishaji hasa katika zao la kakao kama ilivyo ripotiwa. na huu ndiyo msimamo wetu" 

Wafanyazi wa kutoa misaada watekwa nyara nchini Kenya.

Nairobi, Kenya - 29/07/2012. Wafanyakazi wa shrika linalo toa msaada wa kibinadamu wametekwa nyara nchini Kenya katika kambi ya wakimbizi iliyopo Dadaab.
Masemaji wa Polisi nchini Kenya  Philp Ndolo alisema " raia wanne wa kutoka Kanada, Pakistan, Norway na Phillippin walitekwa nyarawakati wakiwa maeneo ya kambi ya wakimbizi ya Dadaab baada ya gari walilikuwa wakisafiria kushambuliwa."
Utekwaji nyara wa wafanyakazi wa mashirika ya kigeni wamekuwa wakifanya kazi za kuhudumia wakimbizi katika eneo hilo kwa mashaka na kusababisha baadhi ya mashika kusimamisha utoaji misaada katika eneo hilo.

Marais wa Somalia wakutana UAE - Dubai.

Dubai, United Arab Emirates - 29/06/2012. Marais wa Somaliland na Somalia wamekutana Dubai kwa mara ya kwanza tangu kuvunjika kwa muungano wa nchi hizo miaka karibuni 20 iliyopita.
Rais Sheikh Sharif Ahmed na Ahmed Silanyo walikutana  kufuatia mkutano wa kwanza  wa wawakilishi wa nchi hizo  uliyofanyika  nchini Uingereza hivi karibuni.
Lengo la kuaza kwa mazungumzo hayo ni kukubaliani nchi hiyo kuwa moja kama Somalia, tangu kujitenga kwa Somaliland 1991, kufuatiqa kuangushwa kwa serikaliaki ya rais Mohmed  Seyyid Bare.
Rais wa Syria ahaidi kutoruhusu nchi nyingine kumwekea msharti.

Damascus, Syria - 29/06/2012. Rais wa Syria amehaidi ya kuwa hataruhusu na kukubali nchi yoyote kuiwekea masharti serikali yake katika harakati za kutaka kuleta amani nchi humo.
rais Bashar al Assad alisema " matatizo yaliopo nchini Syria ni ya wanachiwa Syria na ni ya ndani ya Syria, na  hayahusiani na nchi za kigeni kama nchi hizo zinavyo dai na Wasyria ndiyo watakao maliza  hili suala bila  msukumo au masharti kutoka nchi nyingine."
Bashar al Asssad amefanya mazungumzo hayo kwa mara ya kwanza tangu vurugu na kutokuwepo na amani  nchi Syria kuanza jambo ambalo linaaminika kuipilekea nchi hiyo kuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Thursday, June 28, 2012

Watu 40 wapoteza maisha katika lori baada ya kukusa hewa.

Ururiki yapeleka majeshi yake kwenye mpaka na Syria.


Ankara, Uturuki - 28/06/2012. Serikali ya Uturuki imeamua kuimarisha ulinzi katika mipaka yake na Syria kwa kuamua  kupeleka siraha  na wanajeshi mpakani na nchi hiyo kufuatia kuangushwa kwa ndege yake ya kivita  hivi karibuni na Syria.
Siraha hizo ambazo ni  za kutungulia ndege na za kuzuia mabomu zimlipelekwa kwenye mpaka na Syria baada la  tamko la serikali ya kuwa hawataruhusu tena kitendo hicho kutokea.
Kutokuelewana kati ya Syria na Uturuki kumekuja baada ya serikali ya Uturuki kuwaunga mkono na kuwahifadhi wapinzani waserikali ya Syria ambao kwa sasa wanapambana kivita na serikali ya Syria.

Benki maharufu duniani yapigwa faini.

London, Uingereza - 28/06/2012. Benki ya Barclays nchini Uingereza imepigwa faini kwa makosa ya kukiuka misingi ya mikopo na kupandisha riba.
Benki ya Barclays ilipigwa faini kiasi cha $453millioni dola za Kimarekani  baada ya wachunguzi wa maswala ya masoko fedha na mikopo kugundua ya kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa masharti na maadili ya kibenki.
Hali hii ya  benki ya Barclays kupigwa faini imezidi kuleta msuguano mkubwa nchini Uingereza, kufuatia uamuzi wa serikali uliyo ufanya hapo wali kwa kuzisaidia benki kifedha baada ya benki hizo kuyumba kibiashara. 

China yakamulisha harakati za kianga kwa njia ya kawaida.

Beijing, China - 29/07/2012. Wanaanga watatu wa wa Kichina wamerudi duniani baada ya kumaliza  harakati zao za kisayansi katika anga (orbit)
Wanasayansi hao watatu ambao kati yao alikuwa mwanamke na  walitumia vyombo ambavyo vilikuwa vinaongozwa kwa njia ya kawaida (manual),  walitua duniani bila matatatizo yoyote kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya Uchina.
China imewarusha wanaanga hao kufuatia kitendo kama hicho kilicho fanywa na Marekani na Urusi miaka ya sitini.

Watu 40 wapoteza maisha katika lori baada ya kukusa hewa.

Dodoma, Tanzania - 28/06/2012. Polisi nchini Tanzania wamewakuta watu wapatao 40 wamekufaa ndani ya lori lililo kuwa limewabeba.
Watu hao 40 ambao walikuwa raia wa Somalia na Ethiopia walikufa kutokanaa na kukosa hewa ndani ya lori hilo ambalo walikuwa wanasafiria na  halikujulikana lilikuwaa limetokea sehemu gani na watu hawa.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa  Tanzania Isaac Nantanga alisema " kumekuwa na ongezeko la watu kutoka Somalia na Ethiopia ambao wamekuwa wakielekea nchini Afrika ya Kusini kutokana hali zilizopo katika nchi hizo."
Usafirishwaji wa watu katika  malori umekuwa ukitumika sana katika baadhi yaa nchi za Afrika jambo ambalo limekuwa likihatarisha maisha ya watu wanao tumia maroli hayo.

Sunday, June 24, 2012

Misri yapata rais wa kwaza wa kirahiya baada ya miaka zaidi ya 30 kupita.

Mji wa Mombasa washambuliwa kwa mabomu.

Mombasa, Kenya - 24/06/2012. Mmtu mmoja ameuwaa na wengine kujeruhiwa na mabomu mjini Mombasa siku moja baada ya onyo kutolewa na  ofisi za ubalozi wa Marekani. 
Polisi mjini Mombasa imesema " mashambulizi hayo yalitokea saa nne usiku kwa muda wa masaa ya Kenya wakati wakazi wa mji huo wanaangalia mshindano ya kombe la Ulaya kwenye bar moja iliyopo Mombasa mjini."
Onyo la mashambulizi katika mji wa Mombasa, lilitiliwa maanani na kuzifanya serikali za nchi za Magharibi kuwaonya wananchi wao kuwa waangalifu watakapo kuwa katika matembezi ya kitalii katika mji wa Mombasa.

Marekani ya rudisha msaada wa pesa kwa Malawi.

Lilongwe, Malawi - 24/06/2012. Serikali ya Marekani imerudisha msaada waki fedhe ambao ulikuwa imeizuia kwa serikali ya Malawi, baada ya serikali  iliyopo madaraka ya rais  Joyce Banda kurudisha misingi ya kidemokrasi inayo takiwa.
Dola za  Kimarekani million $350 ambazo zilisimamishwa kutolewa na serikali ya Marekani,  baada ya serikali ya marehemu  Bingu wa Mutharika kukataa makubaliano na nchi za Magharibi na hata kufikia kuvunja uhusiano wa kiplomasia na Uingereza nchi ambayo inatoa misaada mkubwa kwa Malawi.
Malawi nchi ambayo ni moja ya nchi zenye uchumi duni duniani, imekuwa na myumbo wa kisiasa kwa muda tangu mabadiriko ya kisiasa ya vyama vingi kuingia nchini humo.


Misri yapata rais wa kwaza wa kirahiya baada ya miaka zaidi ya 30 kupita.

Kairo, Misri - 24/062012. Matokeo ya uchaguzi nchini Misri yametangazwa na mgombea urais kwa kupitia chama cha Kiislaam cha Muslim Brotherhood nchini huo  amatangazwa kuwa mshinda kwa 51% zidi ya mpinzani wake.
Mohamed Mosri  alitangazwa kuwa mshindi na kamati  ya uchaguzi ya  Misri na huku waananchama wa chama cha Muslimu Brotherhood wakishangilia kwenye makutano maaruufu ya Tahrir yaliyopo katikati ya jiji la Kairo.
Akiongea baada ya kutangazwa kuwa mshindi Mohamed Mosri alisema " sina haki bali ninamajukumu makubwa na kama sitawajibika basi haina haja ya kukubali uongozi wangu na nitawatukumia wa Misri wote  kufanya kazi kwa ajili ya nchi ya yangu."
Matokeo ya uchaguzi nchi Misri yametolewa sikuchache mbele baada ya ya siku iliyo tarajiwa matokeo kutolewa Alhkamisi kuarishwa ili hadi leo siku ya Jumapli ilikuweza kupata matokeo sahihi yasiyo na shaka, baada ya pande zote mbili kulalamika juu ya uchuguzi ulivyo endeshwa.

Saturday, June 23, 2012

Marekani yatoa onyo la mashambulizi katika mji wa Mombasa.

Serikali ya Uganda kupiga marufuku wapenzi wa jinsia moja.

Kampala, Uganda - 23/06/2012. Serikali ya Uganda imezifuta ofisi na mashirika yasiyo yanayo husika katika kuunga mkono ushoga na watu wanao pendana kwa jinsia moja.
Waziri Simon Lokodo ambaye ni waziri wa maadili ya jamii alisema "  pendekezo la kuzisimamisha na kuzifuta ofisi hizo  zimekuja baada ya mimi  kuangalia kiundani na bila kuwa na shaka ya kiubinadamu yakuwa  mashirika  haya 38 yanahusika katika kampeni ya kukuza ushoga, jambo ambalo ni kinyume na maadili yetu na kiimani.
Kampeni hya kuponga ushoga nchini Uganda, imekuwa ikikua siku hadi siku, na kuungwa mkono na wakuu wa dini nchini humo.


Marekani yatoa onyo la mashambulizi katika mji wa Mombasa.


Mombasa, Kenya - 23/06/2012. Mji wa Mombasa umeongezewa ulinzi baada ya ofisi za ubalozi wa Marekani kuaagiza  raia wake waliopo katika mji huo kuondoka.
Uamuzi wa Marekani kuaagiza raia wake kuondoka katika mji wa Mombasa, umekuja baada ya kupata habari ya kuwa "bandari iliyopo katika mji huo, inaweza shambuliwa muda wowote."
Nayo serikali ya Ufaransa imewataka wananchi wake kuwa waangalifu kwa kipindi chote watakapo kuwa katika mji huo wa Mombasa.
Hata hivyo maafisa usalama wa Kenya kwa kushirikiana na polisi, wameeomba "kuwepo na utulivu kwani wanafuatilia habari hizo."
Kenya imekuwa ikikimbwa na mashambulizi ya mabomu kwa muda zaidi ya mwaka mmoja, tangu serikali hiyo ilipo amua kupambana na kundi la Al Shabab nchini Somalia, na kundi la Al Shabab kuhaidi kufanya mashambulizi nchi Kenya ikiwa ni njia ya kulipiza kisasi.


Syria yaangusha ndege ya kijeshi ya Uturuki.


Ankara, Uturuki - 23/06/2012. Serikali ya Uturuki imedandege  iliyoangushwa  na jeshi la Syria ni ndege yake ya  kivita.
Kwa mujibu wa habari kutoka jeshi la Syria, zinasema " ndege hiyo ilivuka mpaka na kuingia ndani ya  anga za Syria na jambo ambalo ililazimisha jeshi hilo kuiangusha ndege hiyo."
Nayo serikali ya Uturuki imedai ya kuwa kitendo cha kuingusha ndege yake, sikitendo cha kuchukuliwa juju juju, na bado inafanya uchunguzi ili kujua ukweli kamili, na itafanya uamuzi baada ya uchunguzi kuisha.