Tuesday, December 10, 2013

Maelfu wasema Amba Kalhe Utata Nelson Rolihlahla Mandela.

Nelson Rolihlahla Mandela aombewa  na maelfu.



Johannesburg, Afrika ya Kusini - 10/12/2013. Viongozi kutoka nchi 91, marais, wakuu wa nchi,  na maelfu ya watu, wameudhuria ibada ya maombolezi ya kumwaaga aliyekuwa rais wa kwanza wa Afrika ya Kusini Nelson Mandela ambaye alifariki  ya tarehe 05/12/2013 huku akiwa na umri wa miaka 95.


Viongozi mbali mbali walitoa hotuba zao za mwisho kwa  Nelson  Mandela ikiwa ni ishara ya kukubali kwao kuwa yote aliyo simamia Nelson Mandela yalikuwa ni ya haki na kukubalika katika harakati zake za kupigania kuung'oa utawala wa kibaguzi wa Makaburu.

Akiongea  rais wa Afrika ya Kusini, Jacob Zuma alisema "Nelson  Mandela - Madiba alikuwa mtu wa aina yake na hakuna mwingine atakaye kuwa kama Madiba."



Naye rais wa Marekani Baraka Obama akihutubia katika siku ya kumuuga Nelson Mandela alisema" Hatuta mwona tena Nelson Mandela.
Mandela ulikuwa mtu wa watu na tunakushukuru kwa kila jambo ulilofanya, ulikuwa unampenda kila mtu, na wala ukujali rangi yake au wapi alitokea na umetuachia kumbukumbu kubwa na tumejifunza mengi toka kwako."

Ili kuthibitisha aliyo simamia Nelson Mandela ya kumpendana na maadui zetu na ndiyo njia pekee ya kufikia kuwepo na amani  kwa maasimu wa kubwa wa kisiasa wa kihistoria ni pale rais wa Baraka Obama alipo peana mkono na rais wa Kuba Raul Castro wakati alipo wasili kwenye jukwaa la tayari kwa kuanza misa rasmi ya maombelezi ya rais wa kwanza Mwafrika mweusi Nelson Mandela.

Wajane, Winnie Mandela na Graca Machel wakiwa wamekaa kwa huzuni katika misa ya maombelezi ya mume wao Nelson Mandela na picha ya chini wakipusiana kabla ya kukaa tayari kwa misa.

Nelson Mandela hata wakati wa hatupo naye kimwili, lakini  anauwezo wa kuwakutanisha viongozi wenye mitazam tofauti katika jamii.

Mwili wa Neslon Mandela utawekwa katika jengo kuu la serikali - Union Bulding kwa siku tatu, kwa ajili ya watu kumwaga kwa mara  mwisho kabla ya kuhifadhiwa katika kijiji alichokulia Qunu siku ya tarehe 15/12/2013.

Saturday, December 7, 2013

Nelson Rolihlahla Mandela atutoka na hatupo naye kimwili.

Afrika yampoteza shujaa mwingine.


Pretoria, Afrika ya Kusini - 07/12/2013. Ulimwengu mzima upo katika  maombelezi ya kifo cha  Nelson Mandela 95, kiongozi mashuhuri aliyeingia katika madaftari ya historia ya karne ya 20.



Enzi za ujana wa Nelson Rolihlahla Mandela.

 Serikali duniani kote  zimeshushwa bendere za nchi zao nusu milingoti ikiwa ni ishara ya  maombolezi  baada ya rais  wa kwanza Mwanaafrika Nelson Rolihlahla  Mandela - Madiba kutangazwa kuwa ameaaga dunia.  

Kufuatia kifo chake, viongozi wa kimataifa wameelezea masikitiko yao na kusifu mchango wake wakati wa uhai wake na jinsi alivyo weza kupambana na ubaguzi wa rangi na mtu aliyekuwa akipigania haki, uhuru na usawa.
Nelson Mandela baada ya kuachiwa huru akiwa na mkewe Winnie Madikizela Mandela.


Ahaahaaa "Rolihlahla, usiwaambie kitu, tuonyeshe vitendo"Hapa anaoekana hayati Nelson Mandela akiwa na mkewe Winnie Mandela  siku kadhaa baada ya Nelson Mandela kutoka gelezani ambapo alikaa jela miaka 27 na Winnie Mandela alikuwa imara katika hali na mali kuendeleza harakati za kumuunga mumewe huku akitunza watoto wao.

Wakiongea kwa nyakati tofati.

Rais Barack Obama wa Marekani amesema kwa kufariki dunia Nelson Mandela " ulimwengu umempoteza mmojawapo wa binaadam mwenye ushawishi mkubwa kabisa, mwenye moyo wa kijasiri kupita kiasi na mwenye imani kupita kiasi. 

Akinukuu  aliyosema wakati  Mandela anahukumiwa  kwende jela maisha, rais Obama 
"Madiba alipofikishwa mahakamani mwaka 1964  alisema nimepigana dhidi ya utawala wa kimabavu wa waupe na nimepigana dhidi ya utawala wa kimabavu wa watu weusi. napiganiamaadili ya kuwepo jamii huru na ya kidemokrasia ambapo watu wote wataishi pamoja kwa furaha na kuwa na fursa sawa  na pia ni  maadili ninayotaraji kuyaendeleza maishani mwangu na ikihitajika, basi pi niko tayari kufa kwa ajili ya maadili hayo."

Naye rais wa Brazil Dilma Roussel amemtaja Nelson Mandela kuwa  "mtu mashuhuri mwenye ushawishi mkubwa kabisa wa karne ya 20 na  ameongoza utaratibu wa maendeleo katika historia ya binaadam kwa busara na mapenzi ,  utaratibu uliopelekea kumalizika kwa ubaguzi wa rangi na mtengano nchini Afrika ya Kusini"
Nelson Mandela akiwa jela katika kisiwa cha Roben kilichopo katika bahari ya Atlantiki karibu na jiji la Cape Town - Afrika ya Kusini.


Malkia Eliabeth wa pili wa Uingereza pia ameelezea masikito yake kutokana na kifo cha Nelson Mandela akisifu juhudi za Nelson Mandela nakusema  "Juhudi zake ndizo zilizopelekea kuwepo Afrika kusini yenye amani hii leo."
Baadi ya viongozi ambao walikuwa na urafiki wa karibu na Nelson Mandela.


Enzi za uhai wao, Nelson Mandela akiwa na rais wa kwanza wa Tanzania Julius Nyerere ambaye serikali yake ilichangia kwa kiasi kikubwa  katika  vita ya kuuong'oa utawala wa  serikali ya Kikaburu ya  Afrika ya Kusini.


"Comredi karibu" haya ndo maeneo aliyosema Hayati Nelson Mandela wakati akimkaribisha rais wa Kuba Fidel Castro.

Nelson Mandela alikuwa mtu wa shukurani, hapa anaonekana akiwa na kiongozi wa Libya hayati Muammar Gaddafi wakati alipo kwenda kumwona japo dunia ilimtenga Gaddafi.


Hadi kukutwa na umauti, Nelson Mandela na Robert Mugabe urafiki wao ulikuwa waukaribu, hapa wanaonekana wakibadirishana mawazo wakati viongozi hawa walipo kutana, enzi za uhai wa Nelson Mandela.
Kila mpigania  haki za binadamu mabdela alikuwa rafiki ya Mandela. Hapa Hayati Yasir Arafat na Hayati Nelson Mandela enzi za uhahi wao walipokutana.

Hayati Nelson Mandela  alizaliwa July 18/ 1918 na kufariki Desemba 05/ 2013 anatarajiwa kupunzishwa 15/12/2013, hii ni kwamujibu wa serikali ya Afrika ya Kusini.


Sunday, November 24, 2013

Mabaki ya mwanzilishi wa Kanisa Katoliki dunia yaonyeshwa.


Mabaki ya mwanzilishi wa Kanisa Katoliki dunia yaonyeshwa.


Vatican City, Vatican - 24/11/2013. Waumini wa Kanisa Katoliki duniani wameonyeshwa kwa mara ya kwanza mabaki  ya aliyekuwa mwanzilishi wa kanisa Katoliki Mtakatifu  Peter.

Mabaki hayo ya Mtakatifu Peter, yalionyeshwa kwa waumini hao huku yakiwa yamewekwa katika kisanduku katika misa  iliyo ongozwa na Papa Fransisco.

Kuonyeshwa kwa mabaki hayo kwa waumini wa Kikristu na hasa kwa waumini wa kanisa Katoliki inaaminika kutaongeza kukuza imani ya waumini wa kanisa la Katoliki, hasa baada ya kukubwa na  mikasa na utovu wa nidhamu ya kimaadili kwa wafanyakazi na wahudumu wa kanisa hilo katika sehemu tofauti duniani

Iran yafikia makubaliano na 5+1 juu ya Nyuklia.

Geneva, Uswis - 24/11/2013. Nchi 5+1 ambazo ni Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa,  China na Urusi, zimefikia makubaliano na Iran  kwa mara ya kwanza tangu kuanza mazungumzo kwa miaka kumi iliyo pita.

Katika makubaliano hayo Iran imekubali kusimamisha baadhi ya mikakati yake ya kuendelea kuzalisha madini ya kinyuklia na badala yake itapewa  kiasi cha $ dola za Kimarekani 7 billion ikiwa ni moja ya afuheni katika vikwazo ambavyo Iran ilikuwa imewekewa na jumuiya ya kimataifa kutokana na mpango wake wa kuzalisha madini ya kinyuklia ambao unashukiwa huenda yakatuka  katika kuunda siraha za sumu.


Akongea baada ya makubaliano hayo, rais wa Iran Hassan Rouhani amesema " hii ni historia na kwa wale ambao walikuwa wana nia tofauti na Iran, sasa watafahamu ya kuwa Iran inahaki ya kuuendelea na mpango wake wa amani wa kuzalisha nyuklia kwa matumizi ya  kisayansi na kijamii."


Kwenye makubaliano hayo ni kwamba Iran imekubali "kutokuzalisha madini ya Uraniam kupita kiasi cha asilimia 5% na kutoa ruhusa ya wakaguzi kutembelea na kukagua katika viwanda vya kufulia madini ya kinyuklia katika miji ya Natanz, Fordo na hakutakuwa na uendelevu wa uzalishaji wa na ufuaji wa madini ya kinyuklia katika kiwanda cha Arak."

Hata hivyo serikali ya Izrael haikupendezwa na makubaliano hayo na  waziri mkuu wa Benyamin Netanyahu amesema ya kuwa " kitendo cha kufikia makubaliano na Iran ni makosa ya kihistoria na Izrael haina imani na Iran, kwani tangu mwanzo Iran Ilisha sema yakuwa inataka kuifuta Izrael katika ramani ya dunia."

Makubaliano hayo hayataifanya Iran kusimamisha mpango wake wa kuzalisha nyuklia ambao imekuwa ikipigania toka kuanza kwa mazungumzo miaka kumi iliyo pita na vile vile makubaliano hayo yatakuwa katika mtazamo katika kipindi cha miezi sita kuanzia sasa.

Saturday, November 23, 2013

Mwili wa mwanzilishi wa Kanisa la Kikrisu Duniani kuonyeshwa hadharani.

Siri za Majasusi  wa kimataifa wa  za zidi fichuliwa.

Moscow, Urusi - 23/11/2013. Mashirika ya kijasusi ya Kimarekani na washiriki wake wamewekwa wazi tena na habari ambazo zimetolewa wiki hii katika mlolongo wa kufichuliwa  habari za siri na aliye kuwa mfanyakazi wa shirika la kijasusi la Marekani CIA na NSA.


Katika habari hizo ambazo zina kurasa tano, zimeonyesha nia ya mashika ya kijasusi ya Marekani na washiriki wake ya kuwa  yalikuwa na mpango endelevu wa kuendelea kuchunguza na kurekodi habari na nyendo za watu kwa muda mrefu zaidi.


Kurasa tano ambazo zipo mikononi mwa  gazeti la New York Times na kuthibitishwa na gazeti hilo zimesema " Makampuni hayo ya kijasusi yalikuwa na mpango wa kumrekodi, kumchunguza na kumfuatilia kila mtu mahali alipo na kwa muda wowote na hii ni kwa mujibu wa nyaraka za mwaka 2012."


"Habari hizi ambazo ni moja ya mikakati ya  mashika ya kijasusi kwa kuitwa PRISM na kueleza mpango wa miaka minne  2012 - 2016 wa NSA na kuita SIGNINT kwa jina na kiupelelezi."


Edward Snowden ambaye ndiye mwanzilishi wa mlolongo mzima wa kufichuliwa kwa siri za mashirika ya kijasusi ya Marekani na washiriki wake, umekuwa ikileta mtafaruku katika jamii ya kimataifa  na kukuza kutokuamniana katika jamii ya kijasusi ya kimataifa na kusababisha wakuu wa mashirika ya kijasusi kutoa maelezo ya kujitete kwa jamii za kimataifa ili kuweza kuimarisha na kurudisha imani kwa jamii nzima ya kimataifa.


Mwili wa mwanzilishi wa Kanisa la Kikrisu kuonyeshwa hadharani.

Rome, Itali -23/11/2013. Kanisa Katoliki duniani limepanga kuionyesha kwa waumini wa dhehebu la Katoliki dunia mabaki ya mifupa ya Mtakatifu Peter, ambaye inaaminika ndiye mwanzilishi wa Kanisa la Kikristu.

Aliongea kabla ya kuonyeshwa kwa mabaki hayo ya Mtakatifu Peter, Askofu Rino Fisichelle amesema " kitendo hiki kitakuwa ni kitendo cha kitamaduni na cha asili ya Kikanisa  katika kuonyesha uhalisia wa wale wote walio toa misha yao kwa ajili ya kumumika Mungu."


Inaaminika ya kuwa Mtakatifu Peter aliuwawa baada ya kutundikwa kichwa chini miguu juu jijini Roma mwaka wa 64 baada ya  Kristu na kuzikwa katika  mjini Rome na baadaye  Mfalme  Constantine kujengea hekalu mahali alipo zikwa katika karne ya (4) nne.

Kanisa Katoliki chini ya uongozi wa Papa Fransisco limekuwa likijitahidi kufanya mabadiriko ili kuweza kurudisha imani  kwa waumini wa Kikristu na hasa kwa Wakatoliki duniani , na hii inatokana na kupungua kwa waumini waendao makanisani  baada ya imani  kupungua kwa baadhi ya waumini wa Kikristu.


Mabaki hayo ya mifupa ya Mtakatifu Peter, yamekuwa ni kitendawili kwa muda mrefu na hivyo kitendo cha Kanisa kuamua  kuonyesha mabaki hayo ikiwa ni ishara na nia ya kukuza imani ya waimini ya wa Kikristu ambayo kwa sasa imekuwa inakubwa misuko suko kutokana na baadhi ya watumishi wa Kanisa hilo  kukumbwa na kashfa ya kuvunja maadili ya Kikristu katika jamii.

Hali ya Nelson Mandela kiafya njia panda.

Johannesburg, Afrika ya Kusini - 23/11/2013. Rais wa kwanza wa Afrika ya Kusini na mpigania uhuru wa Afrika ya kusini, bado yupo katika hali tete kiafya.
Nelson Mandela ambaye  yupo katika matbabu na hadi sasa hawezi kuongea na anawasiliana kwa kutumia ishara.

Akiongea na waandishi wa habari, Winnie Madigizela Mandela alisema " Hali ya Nelson Mandela ni tete, na  pale alipo nyumbani kwenye kitanda ni sehemu ambayo tunaweza kuita kama ICU ( Chumba cha wagonjwa wadharula na uangalizi wa hali ya juu) na mipira ambayo amewekewa kusaidia kusafisha mapafu inasaidi kutopa magojwa mengine kirahisi na anaendelea kupata hauheni kila kukicha."

Nelson Mandela 95, alilazwa  June 8  kwa ugonjwa wa mapafu na amekuwa anaumwa kwa muda mrefu na kwa sasa yupo nyumbani kwake Houghton moja ya kitongoji kilichopo katika jiji la Johannesburg.

Mandela ambaye alikuwa amefungwa jela miaka 27 na serikali ya kikaburu na kuachiwa mwaka 1990 na 1994 kuchaguliwa kuwa rais wa kwanza mzawa wa Afrika ya Kusini  chini ya chama cha ANC (African Nation Congres) had alipomaliza kipindi chake mwaka 1999.

Ujerumani yadai bado kazi ngumu kuhusu Iran na  nyuklia.



Berlin, Ujerumani - 23/11/2013.Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani amesema kuwa  mazungumzo ya kidiplomasia kati ya Iran na jumuiya ya Ulaya na washiriki wake kuhusu mpango wa kuendelea na uzalishaji wa kinyuklia ambayo jumuiya ya kimataifa inautilia wasiwasi.

Waziri Guido Westerwelle alisema " Kunauwezekano makubaliano yakafikiwa, lakini kazi ya ziada inatakiwa kufanyika".

Mazungumzo kati ya Irani na mpango wake wa  kuendeleza uzalishaji wa kinyuklia na jumuiya ya kimataifa umekuwa ukileta vichwa kuuma  kwa jumuiya ya kimataifa, kwani tangu mazungumzo hayo kuanza hayajawahi kuleta jibu kamili au kufikia muafaka.

Rais wa Nigeria apata nafuu.



London. Uingereza- 23/11/2013 Rais wa Nigeria anaendelea kupata nafuu baaada ya kulazwa hospital jijini  London.
Rais Goodluck Jonathan 56, alilazwa baada ya kuzidiwa wakati alipokuwa akijiindaa kuudhuria mkutano wa  kamati ya wakuu wa kiuchumi ambao alitakiwa kuwepo kwenye mkutano huo tangu siku ya Jumatano.

Akiongea katika mkutano wa kuvutia  wawekeshaji, rais Jonathan  alisema " kwanza napenda kuomba kuwaomba radhi kwa kushindwa kuudhuria mkutano huu tangu kwanza, na ningependa kuwahakikishia yakuwa Nigeria chini ya uongozi wangu tumeweka mikakati na mipango madhubuti ambayo itarahisisha wawekezaji kuweza kuwekeza kwa unafuu."

Hii ni mara ya kwanza kwa rais Jonathan kuuugua na kushindwa kuudhuria mkutano wa kimataifa, na itakumbukwa kuwa Goodluck Jonathan alishinda uchaguzi wa urais mwaka 2011 na kuapa kuiongoza Nigeria nchi ambayo ina utajiri mwingi wa malighafi mafuta ambayo ni moja ya kitega uchumi cha nchi ya Nigeria.

Sunday, September 29, 2013

Marekani na Urusi zavutana kuhusu muuza siraha raia wa Urusi.

 Rais wa Iran akumbwa na maandamano tofauti.

Iran, Tehran - 29/09/2013. Rais wa Iran amerudi nyumbani na kukaribishwa na mapokezi tofauti, baada ya kumaliza ziara ya kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi wa kila mwaka wa umoja wa mataifa.

Akiwa amewasili kwenye uwanja wa ndege wa  Mehrabad, rais Hassan Rouhani, alipokelewa na ba baadhi ya makundi yaliyo kuwa ya kipiga ukelele kupinga Marekani na Izrael na wengine wakimuunga mkono kwa kusema "aksante rais Hassan Rouhani"
Katika msafara wake kutoka uwanja wa ndege, gari la rais Rouhani lilipigwa na viatu  na kurushiwa mayai.

Rais Rouhani amekutwa na mapokezi hayo tofauti baada ya kufanya mazungumzo ya kihistoria na rais wa Marekani Baraka Obama kwenye simu kwa muda wa dakika 15, na kuwa nikitendo cha kihistoria tangu serikali ya mapinduzi ya Irani ilipochukua madaraka baada ya kuupindua uongozi wa kifalme Shah ambao ulikuwa unaurafiki na serikali ya Marekani na marafiki zake.

Marekani na Urusi zavutana kuhusu muuza siraha raia wa Urusi.



 Moscow, Urusi - 29/09/2013. Serikali ya Urusi imelaani kitendo cha serikali ya Marekani na mahakama ya nchi hiyo kukataa rufaa iliyo ombwa na raia wa Urusi Victor Bout ambaye anahusishwa na kosa la kuuza siraha kinyume cha sheria.

Victor Bout anashutumiwa kwa kuuza siraha na kuhatarisha vitega uchumi na masrahi ya Marekani, alikamatwa nchi Thailand na kuamishiwa nchi Marekani ili kujibu mashitaka ya kufanya biashara ya kuuza sirha kinyume na sheria  na kuhukumiwa kifungo cha miaka 25 jela mwaka 2012 April, jambo ambalo serikali ya Urusi inalipinga kwa madai ni uamuzi wa kisiasa umeshinikiza maaamuzi hayo ya mahakama.

Kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya Marekani Victor Bout, alihusika katika kuuza siraha kwa kundi la Revolutionary Army Force of Colombia ambalo limetangaza kuwa kundi la kigaidi na serikali ya Marekani.

 Boko Haram wafanya mashambulizi tena kwa wanafunzi.


Jimbo la Yobe, Nigeria - 29/09/2013. Kundi linalo pingana na serikali ya Nigeria la Boko Haram limefanya  mauaji katika chuo kilichopo katika mji wa Damaturu kwenya jimbo la Yobe wilaya ya Gujba.
Akiongea kuhusu mauaji hayo msimamizi wa Molima Idi Mato alisema " watu zaidi ya 50 wameuwawa baada ya wapiganaji wa kundi la Boko Haram kushambulia kwa bunduki na kuchoma moto mabweni ambayo wanafuni walikuwa wamelala wakati wa usiku."

Naye msemaji wa serikali katika jimbo la Yobe, Laarus Eli amesema " hadi kufikia hivi sasa tumesha kusanya adi ya miili ya watu 50 na polisi bado wanaendelea na kutafuta miili ya watu wengiene."
Akiongezea Lazarus Eli alisema " zaidi ya wanafunzi 1,000 walikimbialia mafichoni, mara baada ya kuanza mashambulizi hayo"

Shambulio hilo la Boko Haram limefuatia mashambulizi yaliyofanywa na kundi hilo mwezi wa Kuni ambapo walishambulia shule mbili katika eneo hilo.



Sunday, June 16, 2013

Wairan wapata rais mpya.

Rais wa Urusi aweka wazi nani mwenye damu ya za Wasyria.



London, Uingereza -  16/06/2013. Rais wa Urusi Vladmir Putin  amefanya mazungumzo na waziri mkuu wa Uingereza David Cameron siku moja kabla ya kuanza kwa mkutano wa wakuu wa G8 ambao utafanyika katika mji wa Enniskillen uliyopo Ireland ya Kaskazini.

Wakiongea na waandishi wa habari mara baada ya mazungumzo ya faragha, viongozi hao wa Uingerza na Urusi, wamepishana kuhusu hali halisi ya matukio yanayo tokea nchini Syria.

Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron alisema "rais wa Syria Bashar al Assad mikono yake imejaa damu inayo mwagika nchini Syria na lazima awajibike na ataoke maarakani."

"Na wale wanaopigana na serikali ya Assad tunawasaidia ili kuweza kuikomboa nchi yao na baadaye waweze kujenga nchi yenye misingi ya kidemokrasi."Alimalizia Waziri mkuu Cameron

Naye rais wa Urusi Vladmir Putin alisema " Damu inayo mwagika nchi Syria ni damu ambayo impo mikononi mwa wale wote wanao pigana vita nchini humo. Na hao wanaopigana na serikali ya Assad ni watu ambao wanakula viungo vya watu, je hawa ndiyo watu wanaotakiwa kuisaidiwa?" Alihoji rais Putin.

"Serikali ya Urusi imekuwa ikitoa siraha kwa serikali halali ya Syria  na hakuna sheria ambayo imemevunjwa kimataifa na hilo linajulikana katika sheria za kimataifa." Alimalizia rais Putin.

Mkutano kati ya rais Putin na waziri mkuu David Cameron  umeonyesha kuwa kwenye mkuutano wakuu wa G8 wa mwaka huu, ambao utawakutanisha wakuu wa  nchi za Kanada, Japan,  Ujerumani, Itali Urusi, Marekani Ufaransa na Uingereza huenda ukawa na changamoto kubwa katika maamuzi yao kwa kuzigatia kuwepo na  misimamo tofauti ya nchi hizo kuhusu hali ilivyo nchini Syria.

Wairan wapata rais mpya.


Tehran, Iran - 1/06/2013. Wananchi wa Iran wamemchagua Hassan Rouhani kuwa rais mpya wa Iran, baada ya kupata  kura nyingi kuliko wapinzani wake katika uchaguzi mkuu wa kumchagua rais uliyofanyika nchini humo tarehe 14/06/2013.

Hassani Rouhani alishinda kwa kupata kura  millioni 18.6 zidi ya wapinzani wake Mohammad Baqer Qalibar aliyepata kura millioni 6.07  na Saeed Jalili aliyapata kura million 4, na hivyo kutangazwa rasmi ya kuwa atashika kiti cha urais kilicho achwa wazi na rais Mohmoud Ahmedinejad baada ya kumaliza muda wake wa urais.

Akiongea mara baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa kiti cha urais, Rouhani alisema "nawashukuru ndugu zangu wa Iran kwa kunipa fursa ya kuwa kiongozi, na nitamtumikiwa kila Muiran kwa moyo wangu wote ili kuleta maendeleo kwa nchi yetu Iran."

Hassani Rouhani anajulikana kuwa mmoja ya watu wanaosimamia mageuzi ya kimaendeleo na alisha wakuwa kiongozi katika majadiliano ya kinyuklia kati ya Iran na shirika linalo shughulikia maswala ya kinyukilia hapo mwanzo kabla ya kuchaguliwa kwake kuwa rais wa Iran.

Moto wa Snowden bado wawaka ndani ya Kongesi ya Marekani.


Washington, Marekani - 16/06/2013.  Gazeti la serikali nchini Marekani  limetoa ripoti kamili ya idadi ya simu ambazo zilisikilizwa,  kuufuatia  kutolewa siri  yakuwa serikali ya Marekani ilikuwa ikizichunguza na kusikiliza kwa siri simu zote zilizo kuwa zikiingia na kutoka nchini Marekani.

Gazet hilo la serikali lilisema yakuwa  ni simu 300 tu ndizo zilizo sikilizwa kwa msimu wa mwaka jana kati ya mamilioni ya simu na email ambazo zilikuwa zikifuatiliwa na (NSA) shirika la usalama la Marekani.

Kutangazwa kwa idadi ya simu zilizosikilizwa kumekuja baada ya aliyekuwa mmoja wa mfanyakazi
 wa shirika la usalama Edward Snowden kutoa siri ya kuwa Marekani ilikuwa inazisikiliza simu na kusoma email zote zilizo kuwa zikingia na kutoka nchini humo.

Hata hivyo viongozi wahusika katika maswala ya usalama wa Marekani, wamelaani kitendo cha Snowden na kusema kuwa kimehatarisha usalama wa Marekani na washiriki wake katika harakati za kupambana na ugaidi  duniani.

Korea ya Kaskazini yatoa mthiani kwa Marekani.



Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 16/06/2013. Serikali ya Korea ya Kaskazini ipendekeza kwa serikali ya Marekani kuandaa mazungumzo mapya ambayo yatafaidisha pande zote mbili.

Kwa mijibu wa habari kutoka Korea ya Kaskazini zinasema "tunapendekeza mazunguzo na serikali ya Marekani ili kuweza kuzungumzia hali ya usakama katika eneo la Korea ya Peninsula na kuweza kupata suruhisho litakalo leta amani ya kudumu."

Hata hivyo baada ya pendekezo hilo kutoka kwa Korea ya Kaskazini, serikali ya Marekani haijatoa jibu lolote.

Korea ya Kaskazini imesisitiza ya kuwa pendekezo hilo ni muhimu kwa Marekani kulifikiria kwani ni nafasi muhafaka ili kufikia makubaliano kati ya nchi hizo mbili kuhusu hali ya usalama katika eneo la Korea Peninsula.

Uhusiano wa Misri na Syria wazidi kuwa  mchungu.


Cairo, Misri - 16/06/2013.  Rais wa Misri ametangaza kufunga mahusiano ya kidiplomasia na Syria na kuangiza ofisi za kibalozi zilizopo nchini Misri na Syria kufungwa.

Rais Mohamed Mosri, aliyasema hayo mbele ya maelfu ya watu waliokusanyika ili kumuunga mkono na serikali yake ambayo imetimiza mwka tangu kuchukua madaraka Juini 30/2012.

Akizungumza katika hotuba hiyo Mosri alisema " lazima jumuiya ya kimataifa kukemea kitendo cha  jeshi  la Hezbollah katika harakati zake za kumsaidia   Bashar al Assad na kundi la Hezbollah lazima lifahmu yakuwa halina nafasi nchi Syria."

Akiongezea Mosri alimtaka rais wa Syria Bashaar al Assad kuondoka madarakani,  na vile vile aliukuunga mkono nia ya Marekani yakutaka kuwekewa vikwazo kwa serikali ya Syria kutokutumia anga lake katika vita zidi ya makundi ya kivita yanayo pingana na rais  Assad.



Tuesday, April 9, 2013

Uhuru Kenyatta aapishwa kuwa rais Kenya


Uhuru Kenyatta aapishwa kuwa rais Kenya

Nairobi Kenya -  09/04/2013. Uhuru Kenyatta ameapishwa kuwa rais wa nne wa Kenya. Viongozi kutoka mataifa kadhaa ya Afrika wameudhuria kuungana na Wakenya kwenye sherehe za kuapishwa kwa rais  huyo mpya wa Kenya kwenye uwanja wa mpira wa Kasarani.
Kenyatta mwenye umri wa miaka 51 ni mtoto wa rais wa kwanza wa Kenya, Jomo Kenyatta. Ushindi wake wa asilimia 50.07 katika uchaguzi wa tarehe 4 Machi ulihalalishwa na Mahakama ya Juu baada ya pingamizi lililowekwa na Waziri Mkuu anayemaliza muda wake, Raila Odinga, kutupiliwa mbali na mahakama hiyo.

Kenyatta anayekuwa rais wa nne wa taifa hilo la Afrika ya Mashariki tangu lilipopata uhuru wake kutoka Uingereza mwaka 1963, anakuwa rais wa pili barani Afrika kuwa madarakani hali anakabiliwa na mashitaka kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kwa tuhuma za kusaidia kuchochea ghasia za kikabila zilizoukumba uchaguzi wa urais wa Kenya wa mwaka 2007. Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa mwezi Julai, ambapo Kenyatta na naibu wake, William Ruto, wanakabiliwa na mashitaka ya aina moja.

Mtaalamu wa masuala ya Kenya katika Chuo Kikuu cha Warwick, Daniel Branch, amesema "mataifa ya Magharibi yamejikuta kwenye hali ngumu sana, lakini huenda kila nchi ikatafuta njia yake yenyewe na mahusiano na Kenya.
Hata hivyo rais Uhuru Kenyatta amehaidi kushirikiana na yote yanayo husu maswala ya kimataifa atayafuatilia na kuyatekeleza.








Monday, April 8, 2013

Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza aaga dunia.

Margaret Thatcher  aaga dunia

London Uingereza - 08/ 04/ 2013Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Margaret Thatcher ambaye alikuwa akijulikana kama "Iron Lady" kwa ukakamavu wake ambaye amezifanyia marekebisho siasa za kizazi cha Uingereza amefariki dunia baada ya kupigwa na kiharusi leo akiwa na umri wa miaka 87. Mengi zaidi na Mohammed Dahman.
Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza na Waziri Mkuu David Cameron wameongoza katika salamu za rambi rambi kwa waziri mkuu huyo wa kwanza mwanamke nchini Uingereza, muumini mashuhuri kabisa wa sera za mrengo wa kulia na mtu muhimu wakati wa Vita Baridi.
Msemaji wa familia ya Thatcher amekaririwa akisema "kwa masikitiko makubwa Mark na Carol Thatcher (watoto wa marehemu) wanatangaza kwamba mama yao Bi. Thatcher amefariki kwa utulivu baada ya kupigwa na kiharusi leo asubuhi."

Waziri Mkuu huyo wa zamani ambaye aliiongoza Uingereza kuanzia mwaka 1979 hadi mwaka 1990 alikuwa akikabiliwa na maradhi ya kupoteza kumbukumbu na mara chache amekuwa akionekana hadharani katika miaka ya hivi karibuni.

Mara ya mwisho alilazwa hospitalini hapo mwezi wa Disemba mwaka jana kwa ajili ya operesheni ndogo ya kuondowa uvimbe kwenye nyonga yake.
Kiongozi huyo wa zamani wa chama cha Conservative amebakia kuwa waziri mkuu pekee mwanamke katika historia ya Uingereza na kiongozi aliekaa mfululizo kwa muda mrefu kabisa katika makao makuu ya serikali ya Downing Street katika karne ya 20.
Binti yake wakati fulani aliwahi kusema kwamba waziri mkuu huyo wa zamani inabidi akumbushwe mara kwa mara kwamba mume wake Denis amefariki mwaka 2003.
Thatcher alitakiwa na madaktari kuacha kuhutubia hadharani muongo mmoja uliopita baada ya kukumbwa mara kadhaa na kiharusi kidogo.

Kasri la Kifalme la Uingereza Buckingham Palace limetowa taarifa ikisema kwamba Malkia amesikitishwa kusikia habari za kifo cha Thatcher na kwamba atatuma ujumbe binafsi wa masikitiko kwa familia.

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron amekatisha ziara yake katika nchi kadhaa za Ulaya na amesema kwamba kwa huzuni kubwa amepokea habari za kifo cha Bibie huyo na kwamba wamempoteza kiongozi adhimu,waziri mkuu adhimu na Muingereza adhimu.Ameongeza kusema kwamba Thatcher " ameitumikia nchi yake vizuri sana,ameiokoa nchi yake na ameonyesha ushujaa mkubwa sana katika kufanya hivyo.Watu watakuwa wanajifunza juu ya kile alichokifanya na mafanikio yake kwa miongo kadhaa inayokuja na yumkini hata kwa karne kadhaa.Hiyo dio haiba yake.”

Michael Howard kiongozi wa chama cha Conservative kuanzia mwaka 2003 hadi mwaka 2005 amekiambia kituo cha televisheni cha Sky kwamba ni habari za kuhuzunisha sana kwani alikuwa ni mashuhuri sana katika siasa za Uingereza.

Howard anaamini kwamba Thatcher ameiokoa nchi yao, ameubadili uchumi wa nchi hiyo na anaamini kwamba ataingia katika historia akiwa kama mmojwapo wa mawaziri wao wakuu walio adhimu kabisa.

Wafuasi wa sera za mrengo wa kulia wanampongeza mama huyo kwa kuitowa Uingereza kwenye msononeko wa kiuchumi lakini wafuasi wa mrengo wa shoto wanamshutumu kwa kuving'owa viwanda vilivyokuwepo tokea enzi za jadi na kuvunja kiini cha mshikamano wa jamii.

Katika jukwaa la kimataifa alijenga uhusiano maalum na Rais Ronald Reagan wa Marekani jambo ambalo limesaidia kuuangusha ukomunisti katika Muungano wa Kisovieti.Pia alikuwa akipinga vikali uhusiano wa karibu wa Ulaya.

Thatcher alizaliwa akiwa anajulikana kwa jina la Margaret Hilda Roberts hapo tarehe 13 Oktoba mwaka 1925 katika mji wa sokoni wa Grantham mashariki ya Uingereza akiwa ni binti wa muuza duka la vyakula na bidhaa ndogo ndogo.

Baada ya kumaliza shule na kujipatia shahada yake ya Kemia katika Chuo Kikuu cha Oxford alifunga ndoa na mfanyabiashara Denis hapo mwaka 1951 na miaka miwili baade walibarikiwa watoto mapacha Carol na Mark. Mara ya kwanza alichaguliwa katika bunge hapo mwaka 1959 na alichukuwa nafasi ya waziri mkuu wa zamani Edward Heath kama kiongozi wa chama cha upinzani cha Conservative hapo mwaka 1975 kabla ya kuwa waziri mkuu miaka minne baadae.

Haiba yake ya kudumu inaweza kuelezwa kwa muhtasari kuwa ya "Thatcherism " yaani mkusanyiko wa sera ambapo wafuasi wake wanasema zimeendeleza uhuru wa mtu binafsi na kusambaratisha mgawanyiko wa kitabaka ambao ulikuwa umeipasuwa Uingereza kwa karne kadhaa.

Hata hivyo kushinikiza sera zake kuliiweka serikali yake katika mapambano kadhaa magumu.Itakumbukwa wakati Argentina ilipovivamia visiwa vya Falklands vilivyoko chini ya himaya ya Uingereza hapo mwaka 1982, Thatcher alituma vikosi na meli za kivita na kuvikombowa katika kipindi cha miezi miwili.
Na hadi sasa visiwa kisiwa cha Falklands kimekuwa na mzozo kati ya Argentina na Uingereza nani ni mmiliki halali wa ene hilo.



Tuesday, April 2, 2013

Wavenezuela kuchagua upya baada ya Chavez.

Karaca , Venezula - 02/04/2013. Viongozi wa wanao gombania kuwania kiti cha urai wa Venezuela kilicho achwa wazi na hayati Hugo Chavez wameanza kampeni za uchaguzi ili kuongoza nchi yao.
Nikolas Maduro ambaye nimgombea wa chama tawala na aliye pewa baraka na Hugo Chavez kugombe kiti cha urais kabla ya kifo chake, anatarajiwa kuwa na wakati mgumu kumpiku kiongozi wa chama cha upinzani Henrique Kapriles ambaye alishindwa Hugo Chavez  wakati wa uchaguzi wa kwanza wa urais. Tangu kifo cha Hugo Chavez kumekuwa na maoni tofuti juu ya nani atashinda kiti hicho cha urais nchini Venezuela.

Korea ya Kaskazini ya zidi kuwa kichwa ngumu.

 Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 02-03-2013. Serikali ya Korea ya Kaskazini imetangaza kufungua kinu chake cha kinyuklia ambacho ilikuwa imekifunga hapo awali.
Kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya Korea ya Kaskazini zinasema " tunaamua kufungua kinu hicho  kwani kitawasaidia katika miradi ya umeme."
Uamuzi wa huo wa Korea ya kaskazini kufungua kinu hicho walichokifunga mwaka 2007, umekuja huku kuna hali kutishiana kivita kati yake na Korea ya Kusini.
Hata hivyo Korea ya Kusini imesema ikiwa itashambuliwa na Korea ya Kaskazini itajibu mashambulizi hayo.

Wednesday, March 27, 2013

Makubaliono ya kuundwa benki ya nchi za BRICS bado kufikiwa.

Makubaliono ya kuundwa benki ya nchi za BRICS bado kufikiwa.

Durban, Afrika ya Kusini - 27/03/2013.Viongozi wa nchi zinazo kua kiuchumi duniani wamekutana nchini Afrika ya Kusini ili kuangalia ni kwa kiasi gani nchi hizo zitashirikiana katika kukuza uchumi.
Viongozi wa nchi hizo zinazo julikana kama BRICS ambazo zinajumuisha nchi za Brazil, Urusi, India, China na Afrika ya Kusini wamekutana na kujadili  muundo wa benki ya nchi hizo na itakavyo weza  kushindana na mabenki ya nchi za Ulaya Magharibi ambazo zimekuwa zikitawala mfumo wa fedha wa dunia.
Katika kikao hicho, viongozi hao hawakufikia muafaka kamili juu  kuundwa kwa benki yao na kukubaliana kutoa muda wa kuliangalia swala hilo kiundani.
Mwenyekiti wa kikao hicho, rais wa Afrika ya Kusini Jakob Zuma alisema " tunayo matumaini ya kuunda benki hiyo na kwa sasa ni wajibu wa viongozi kwenda kukaa, kupanga na kuliangalia jambo hili kiundani ili kulifanikisha."
Benki hiyo ambayo inatarajiwa kuhitaji pesa za euro billioni 50, ambazo zitachangwa na nchi hizo za BRICS ili benki hiyo iweze kufanya kazi kikamilifu.
Viongozi hao walikutana ili kutimiza mazungumzo yaliyo fanyika nchini India New Dheli, mwaka mmoja uliyo pita ambapo  azimio la kuundwa kwa benki hiyo  lilijadiliwa.

Korea ya Kaskazini yazidisha uhasama na Korea ya Kusini.

Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 27/03/2013. Serikali ya Korea ya Kaskazini imesimamisha mawasiliano ya aina zote  kati yake na serikali ya Korea ya Kusini.
Uhasama huo kati ya nchi hizi mbili umekuja baada ya Korea ya Kusini kuendelea kufanya mazoezi ya kijeshi na Marekani, jambo ambalo Korea ya Kaskazini imelitaja ya kuwa ni la kutishia usalama wake.
Habari kutoka Korea ya Kaskazini zilisema "kutokana na hali iliyopo tunaona  vita vinaweza kutokea muda wowote na hivyo kuanzia sasa mawasilino ya aina yoyote na Korea ya Kusini hayatakuwepo."
Msemaji wa serikali ya Marekani amesema "hiki ni kitendo ambacho hakitaijenga serikali ya Korea ya Kaskazini, na inabidi serikali ya nchi hiyo iangalie kama vitendo inavyo fanya ni sawa na havitasaidia katika kuleta uimara wa usalama katika eneo zima la Peninsula."
Korea ya Kaskazini imekuwa ikitishia kuishambulia Marekani na kusema ya kuwa kitendo cha kufanya mazoezi ya kijeshi kwenye Korea Peninsula kumevunja mkataba  uliyo wekwa wa vita wa mwaka 1950-53.

Sheria ya mlinda Abuu Qatada nchini Uingereza.

London, Uingereza - 27/03/2013.  Mahakama ya rufaa ya Uingereza imelitupilia mbali ombii la serikali  ya Uingereza la kutaka muhubiri maarufu wa dini ya Kiislaam arudishwe nchini kwao.
Abuu Qatada ambaye ni raia wa Jordan ameruhusiwa na mahakama ya Uingereza kuendelea kuishi nchini humo, japo serikali ya Uingereza kupitia ombi la waziri wa mambo ya ndani ya nchi hiyo Thereza May kutaka Abuu Qatada kuondolewa nchi Uingereza kwa madai anahatarisha usalama wa nchi.
Jopo la majaji wa mahakama ya rufaa lilitoa hukumu kwa kusema "hakuna ushahidi wa kutosha ya kuwa kesi inayo mkabili  Abuu Qatada nchini Jordani itaendeshwa kwa kufuata sheria na haki za binadamu."
Kufuatia uamuzi huo wa mahakama, waziri kimvuli wa mambo ya ndani, Yvette Cooper alisema " hii inasikitisha saana, na waziri Thereza anatakiwa kutumia kila sheria ili kufanikisha kuondelewa nchi kwa Abuu Qatada."
Abuu Qatada ambaye ni raia wa Jordan aliomba hifadhi nchi Uingereza mwaka 1993, baada ya jaribio la kutaka kuiangusha serikali ya Jordan kushindwa, na mwaka 1999 alikutwa na hatia  kwa kosa la uhaini nchini Jordan, baada ya kesi kuendelea japo hakuwepo nchini humo.

Sunday, March 24, 2013

Pervez Musharaf arudi nchini Pakistan.

Rais wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati aikimbia nchi.

Bangui, Afrika ya Kati - 24/03/2013. Kundi la waasi  linalo julikana kwa jina la Seleka, limevamia makazi ya rais wa  Jamuhuri ya Afrika ya Kati, na kumfanya akimbiliea nchini Kameron.
Rais Francois Bozize ambaye inasemekana amekimbia kwa kuvuka mto Oubangi baada ya waasi wa kundi la seleka kuchukua mji wa Bangui na baadaye kufanikiwa kuvamia ikulu ambapo alikuwa akiishi rais huyo.
Kufuatia mashambulizi hayo ya ikulu ya rais, Ufaransa imeomba kamati ya usalama ya umoja wa taifa kukutana ili kujadilli tukio hilo.
Hapo awali kundi la Seleka lilidai ya kuwa litamwondoa madarakani rais Bozize, kwani lilidai kwa kusema " haturiziki na jinsi serikali inavyo ongozwa na  hakutimiza makubaliano tuliyo saini pamoja."
Jamuhuri ya Afrika ya Kati imekuwa ikikumbwa na matatizo ya kisiasa na kusababisha zaidi ya wati 200,000 kukimbia nchi na wengine wengi kupoteza maisha yao.

Pervez Musharaf arudi nchini Pakistan.

Karachi,Pakistan- 24/03.2013.   Rais wa zamani wa Pakistan  amerudi nyumbani baada ya kuwa nje ya nchi kwa kipindi miaka minne na miezi kadhaa.
Pevez Musharraf  69, ambaye alishawahi kuwa rais wa Pakistan alikuwa akiishi nchini Dubai tangu alipo achia madaraka ya urais na kuondoka nchini humo.
Pervez Mushar ambaye amerudi nchini  Pakistan ili kujiandaa kugombea kiti cha urais,  amehaidi ya kuwa akichaguliwa kuwa rais atapambana na wale wote ambao wanavuruga amani nchini Pakistan.
Hata hivyo makundi ya Taliban na  na Alqaeda yametishia kuwa watatuma watu wakujitolea muhanga ili kupoteza maisha yake Pervez Musharraf.
Pervez Musharraf anakabiliwa na kesi ya kutotoa ulinzi wa kumlinda aliye kuwa kiongozi wa chama cha upinza marehemu bibi Benazir Bhutto, ambaye aliuwawa na mlipuko wa wa mabomu wakati alipo kuwa katika kampeni ya uchaguzi katika mji wa Rawalpindi.

Thursday, March 21, 2013

Baraka Obama Wapalestina na Waizrael lazima wafikilie upya ili amani iwepo.

Baraka Obama  Wapalestina na Waizrael lazima wafikilie upya ili amani iwepo.

Ramallah, Palestina - 21/03/2013. Rais wa Marekani amewataka viongozi wa Palestina na Izrael kukutana tena ili kuongelea swala la kuwepo na kuundwa taifa la Wapalestina litakalo pakana na Izrael.
Rais Baraka Obama akiongea kwenye mkutano  wa pamoja na waandishi wa habari, alisema "Inabidi viongizi wote lazima wafikilie upya ili kuweza kufanikisha kupatikana kwa amani kati ya Waizreal na Palestina na ni haki kwa Wapalestina kuwa na Taifa lao ili waweze kujenga maisha yao ya baadaye kwa kizazi kijacho."
Naye rais wa Wapalestina Mahamoud Abbas akichangia katika mkutano huo alisema " kikwazo kikubwa ni kuendelea kujengwa kwa makazi ya Kiyaudi katika eneo letu sisi Wapalestina na inabidi ujenzi huu usimamishwe na hali hii imekuwa ikipingwa na kulaaniwa na jumuiya ya kimataifa na hata umoja wa mataifa umesha piga kura zaidi ya mara 13 kupinga ujenzi huo."
"Hivyo ujenzi wa makazi lazima usimame ili kufanikisha mazungumzo na Waizrael."Alisema rais Abbas.
Ziara ya rais Obama katika eneo la Westbank ni ya kwanza tangu kuwa rais wa Marakani na kbla ya kuonana na viongozi wa Wapalestina aliongea kwanza na viongozi wa Izrael ambao walisisitiza nia yao ya kutaka mazungumzo ya amani kati yao na Wapalestina yaendelee.

Tuesday, March 19, 2013

Kadinali Jorge Mario Bergoglio asimikwa rasmi na kuitwa Papa Fransisko.

Kadinali Jorge Mario Bergoglio asimikwa rasmi na kuitwa Papa Fransisko.

Vatican, Vatican City - 19/03/2013. Maelfu ya waumini wa Kanisa Katoliki, viongozi wa serikali na marais wameudhuria kusimikwa kwa Kadinali Jorge Mario Bergoglio kuwa mkuu wa Kanisa Katoliki duniani.
Kabla ya kuongoza misa Kadinali Jorge Mario Bergoglio 76, alisimikwa uongozi huo na kupewa cheo cha Upapa kwa jina alilo chagua la Fransisko na kuwa ni Papa wa kwanza kutoka katika bara la Amerika.
Papa Fransisko akiongea baada ya kusimikwa na kuongoza misa alisema " nawaomba  wale wote wenye madaraka   wawajibike vyema katika nyazifa zao za kiuchumi, siasa na kijamii ili tuweze kulinda na kujenga jamii bora na mazingira yake."
Papa Fransisko, amechuku jina la Fransisko wa Assis ambaye alikuwa mtoto wa tajiri, lakini aliamua kwenda kuishi  na watu masikini wakati wa karne ya 13, na hivyo Papa Fransisko kusisitiza ya kuwa kanisa ni kanisa la watu masikini.
Papa Fransisko ni mzaliwa wa Argentina.

Wazimbabwe wakubaliana katika kura ya muda wa urais.

Harare, Zimababwe - 19/03/2013. Wananchi wa Zimbabwe wamepitisha kwa wingi wa kura kuunga mkono sheria itakayo tumikika kumruhusu rais kuongoza nchi kwa mihula miwili ikiwa atachaguliwa baada ya kumaliza awamu ya kwanza.
95% ya watu walio piga kura walikubaliaana na sheria hiyo ambayo itaanza kutumika baada ya uchaguzi mkuu wa urais utakao tarajiwa kufanyika  mwaka huu mwezi wa Julai.

 Siraha za sumu zatumika katika vita nchini Syria. 

Damascus, Syria - 19/03/2012. Serikali ya Syria  imelaumu vikundi vinavyo pigana na serikali kwa kutumia siraha zenye sumu.
Msemaji wa serikali ya rais Bashar al Assad  alisema' wapiganaji wanaopigana naserikali wametumia siriha zenye sumu katika mji wa Aleppo."
Hata hivyo msemaji wa kundi linalo pigana na serikali alikanusha madai hayo kwa kusema " huu ni uzishi mtupu, na tunaamini jeshi la serikali limetumia mabomu aina ya scud ambayo huenda ya na sumu."
Kufuatia habari hizi serikali ya Urusi imeonya na kulaani na kusema  linabidi lichunguzwe ukweli wake kwani " ikiwa  siraha za sumu zimeanguka mikononi mwa wapiganaji basi hali inaweza kuwa mbaya zaidi."
Habari hizi za matumizi ya siraha za sumu zimekuja baada ya wapinzani wa serikali ya Syria kufanya uchaguzi na kumchagua Ghasssa Hitto, kuwa waziri mkuu wa serikali inayo pingana na rais Bashar al Assad katika uchaguzi uliyofanyika nchini Uturuki jijini Instambul.
Ghasssan Hitto ambaye alikuwa akiishi nchi Marekani amesema  " hakuna  majadiriano na serikali ya Bashar al Assad."
Syria ina limbikizo la siraha za sumu na za kinyuklia ambazo kama zikitumika katika vita hivi vya wenye kwa wenye huenda eneo zima la bara Arabu likawa katika hali mabaya. 

 Irak bado mabomu yalipuka na ni miaka 10 tangu kuangushwa kwa Saddam Hussein

Baghdad, Iraq - 19/03/2013. Watu zaidi ya 48 wamepoteza maisha yao na zaidi ya watu 120 kujeruhiwa vibaya, baada ya mfululizo wa mabomu kulipuka wakati Wairak wanatimiza miaka 10 tangu kuangushwa kwa Saddam Hussein.
Mashambulizi hayo ya mabomu ambayo yalitokea katika masoko, holetini nakwenye kituo cha basi katikati ya jiji la Badhdad kwenye eneo linalo kaliwa na  watu jamii ya Kishia.
Uvamizi nchini Irak uliongozwa na Marekani mwaka 2003/19, kwa madai ya kuwa Saddam Hussein alikuwa amelimbikiza siraha hatari za sumu ya kinyuklia.
Tony Blair ambaye alikuwa waziri mkuu wa Uingereza na aliye unga mkono na kushirikiana na serikali ya Marekani katika uvamizi nchini Irak amesema " hajutii uamuzi wake wa kushiriki katika kung'oa  Saddam Hussein madarakani kwani hata kama vuguvugu hili la mapinduzi inalo endelea katika bara la Waaraabu lingefenikiwa kumuondoa madarakani Saddam Hussein, basi ingekuwa ni tukio ambao linge jawa na majuto makubwa kwa jumuiya ya kimataifa kwa kuzingatia ni nini kinacho endelea nchini Syria,  ambapo rais Bashar al Assad anavyo wafanyia wananchi wake."
Vita vya kuivamika Irak vilipoteze maisha ya Wairak zaidi ya 100,000 na wengi kujeruhiwa na mali nyingi za Wairak kuharibika.