Saturday, January 18, 2014

Rais Yoweri Kaguta Museven awapa hafueni mashoga.

Rais Yoweri Kaguta Museven awapa hafueni mashoga.

Kampla, Uganda - 18/01/2014. Rais wa Uganda, Yoweri |Mseven, amkataa kusaini muswada wa kupinga ushoga nchini Uganda.

Akiandika kupinga kwa sasa kutia sahii rais  Museven amesema " kweli ushoga si kitu cha kawaida na wanatakiwa kuokolewa na siyo kuhukumiwa."

Kitendo cha rais Museven kupinga kutia sahii muswada huo, kimetafsiliwa kuwa, ni kugopa msukomo wa kimataifa, ambapo ingepelekea kuleta mvutano kati ya serikali yake na mashirika ya kimataifa yanayo unga mkono ushoga ambapo mashirika hayo yanaushawishi mkubwa kimataia na kuweza kusababisha myumbo wa serikali ya Uganga kimataifa.

Thursday, January 16, 2014

Kesi ya Rafiki Hariri yaanza na kuhamishia masikio ya Walebanoni jijini Hague.

Kesi ya Rafiki Hariri  yaanza na  kuhamishia  masikio ya Walebanoni jijini Hague.

Hague, Uhollazi - 16/01/2014. Mahakama maalumu inayoshughulikia kesi ya mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu wa Lebanoni Rafiki Hariri imeaanza rasmi jijini Hague Uhollanzi ambapo watu wanne wanatuhumiwa kuhusika katika mauaji hao.

Kesi hiyo imefunguliwa dhidi ya watu nne  Mustafa Badreddine, Salim Ayyash, Hussin Oneissi na Assad Sabra  ambao pia inasadikiwa kuwa ni wanacham wa kundi la Hezbollah kundi ambalo linashutumiwa kuhusika katika mauji ya Rafiki Hariri.

Hata hivyo kesi hiyo imeanza huku watuhumiwa kutokuwepo mahakamani na jaji David Re kuamua kuwa kesi itaendelea kwa "watuhumiwa kukana kosa hilo."

Rafiki Hariri, na watu wengine 22 waliuwawa mwaka 2005, baada  milipuko ya abomu kutoe katika eneo ambalo walikuwepo na kundi la Hezbollah kushutumiwa kuhusika na mauaji hayo, japo kundi hilo limekana  kuhusika na  mauaji hayo na pia kuipinga mahakama hiyo.

Hata hivyo baada ya kuuwawa kwa Hariri, jeshi la Syria lililazimika kuondoka nchini Lebanoni ambapo jeshi hilo lilikuwa likilinda amani nchi  Lebanoni.

Monday, January 13, 2014

FIFA ya Sepp Blatter yafanya alicho takiwa kupewa Pele.

FIFA ya Sepp Blatter yafanya alicho takiwa kupewa Pele.

Zurich, Uswizi - 13/01/2014. Edson Arantes Nascimento alimaarufu kama Pele, ametunukiwa zawadi maarumu ya mpira wa dhahabu  na kutambulika kuwa yeye  ndiye alikuwa mchezaji bora wa dunia katika karne 20 na mpa sasa hakuna ambaye amamesha wahi kuvunja rekodi yake ya usakataji wa soka na ufungaji wa magoli duniani kote hadi sasa.

Akiongea baada ya kupokea zawadi hiyo ya mpira wa dhahabu, ambao umeanzishwa kwa mara ya kwanza, Pele alisema "sasa naona ndoto yangu imekamilika, kwani nimekuwa na wivu kuona wengine wakitunukiwa na hivyo kwa sasa nina kombe vyote nilivyo kuwa navihitaji"

Sepp Blatter ambaye ni rais wa shirikisho la mpira wa miguu FIFA akimsifu Pele alisema" Hakuna mchezaji ambaye amemfikia Pele katika historia ya mpira wa miguu duniani.
"Amefunga magoli zaidi ya alfu moja na kuwafanya watu wapende mchezo wa mpira wa miguu pote duniani na kwa uwezo wake wakusakata soka, na ni mchezaji wa karne ya 20"

Pele hakuweza kupata zawadi hii ya mpira wa dhahabu kwa kuwa mchezaji bora wa dunia enzi za uchezaji wake,  kwa sababu alikuwa hajawahi kucheza ligi za Ulaya japo alikuwa akitikisa dunia kwa umairi wake wa kusakata soka na kuwanyanyasa mabeki na makipa kugalagala na kurudi nyavuni kuotoa mpira ulio tikisa nyavu.


Cristiano Ronaldo atunzwa mpira wa dhahabu kwa mara ya pili.

Cristiano Ronaldo atunzwa mpira wa dhahabu kwa mara ya pili.

Zurich, Uswizi - 13/01/2014. Mchezaji wa Real Madrid  Cristiano  Ronaldo amechaguliwa kuwa mcheaji bora wa dunia wa mwaka 2013

Cristiano Ronaldo 28, amechaguliwa  kwa kura 1,365  na kuwashinda wachezaji wenzake wawili Lionel Messi  1,205 wa timu ya Barcelona.



 Na Frank Ribery 1,127 wa Buyen Munich ambao walifikia fainali katika uchaguzi huo.

Akiongea baada ya kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa dunia wa mwaka 2013, Cristiano Ronaldo alisema, " sina cha kusema, na nawashukuru wachezaji wenzangu, uongozi kwa jumla, kwani kupata tunzo hili siyo rahisi."

Tuzo hili la kuwa mchezaji bora wa dunia litakuwa ni la mara ya pili katika maisha yake Cristiano Ronaldo ya kimpira kufuatia la kwanza alilopata mwaka 2008.



Areal Sharon alazwa nyumba yake ya milele.

Areal Sharon alazwa nyumba yake ya milele.

Tel Aviv, Izrael - 13/01/2014. Mamia ya Waizrael wameudhuria mazishi ya aliyekuwa waziri mkuu na amiri jeshi wa nchi hiyo Areal Sharon.

Mazishi ya waziri Areal Sharon yalifanyika katika shamba leke  kwenye eneo la jangwa la Negev.

Waziri mkuu wa sasa wa Izrael Benyamin Netanyahu ambaye aliongoza mazishi kwa niaba ya serikali, alisema " Sharon ni moja ya komanda wa Kiizrael ambao watakumbukwa kwa kuitete Izrael na Wajuishi "












Mazishi ya Areal Sharon yameudhuliwa na makamu wa rais wa Mareakani Joe Biden, waziri wa mambo ya nje wa Urusi, Sergi Levrov, aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Tony Brair na viongozi wengi kutoka sehemu tofauti duniani kasoro viongozi kutoka Afrika na Amerika ya Kusini.

Areal Sharon 85, alifariki kutokana na kuugua kwa  baadhi ya viongo vyake vya ndani ya mwili, na hii ilitokana hapo mwanzo wa mwaka 2006 kupata ugonjwa wa kiaharusi ambao ulimsababishia kulazwa kwa muda wa miaka saba.

Saturday, January 11, 2014

Waziri wa ulinzi wa Uingereza hausishwa na mateso wafungwa Irak.

Waziri wa ulinzi wa Uingereza hausishwa na mateso ya wafungwa Irak.

London, Uingereza - 11/01/2014. Shirika la kutete haki za binadamu na katiba ya Ulaya lenye makao yake nchini Ujerumani limeiomba mahakama inayoshughulikia makaosa ya jinai ICC, kuchunguza matendo ya uvunjwaji wa haki za binadamu uliofanywa na viongozi wa serikali wa Uingereza.

Likiataja shirika hilo limesema "Geoff Hoon ambaye alikuwa waziri wa ulinzi na katibu mkuu  Adam Ingram kuwa walihusika kwanjia moja au nyingine katika mateso na mantendo yaliyo kuwa yanakuiuka haki za binadamu kati ya mwaka 2003 na 2008 na kuvunja sheria ya Geneva ya kulinda wafungwa wa kivita."

Hata hivyo watu hao ambao wanashukiwa kufanya makosa hayo wamekana kuhusika na makosa hayo.

Kesi hiyo ambayo ina kurasa 250,  ilikabidhiwa kwa ICC, huku ikiwa na makosa 85 ambayo inasemekana yamevunjwa  na viongozi hao, na hivyo kuomba wachunguzwe.

Wakati wa vita vya Irak, wanajeshi wa Uingereza walishutumiwa kwa kuhusika katika kutesa wafungwa wa kivita, ambapo Geof Hoon alikuwa ndiye mkuu wa wizara ya ulinzi ya nchi ya Uingereza.





Aliyekuwa waziri mkuu wa Izrael hatupo naye tena kimwili.

Aliyekuwa waziri mkuu wa Izrael hatupo naye tena kimwili.

Tel Aviv, Izrael - 11/01/2014. Wanachi wa Izrael wamekubwa na msiba mkubwa kufutia kifo cha aliyekuwa waziri mkuu na amiri jeshi wa nchi hiyo kutokea leo hii.

Ariel Sharon 85, ambaye alikuwa amelazwa hospital kwa muda mrefu, baada ya kukumbwa na ugonjwa wa kiharusi mwaka 2006  na ambapo  ulisababisha akupata madhara ndani ya viongo vya mwili wake na kupelekea kifo.

Shlomo Noy, ambaye ni msemaji wa hospital ambayo alikuwa amalazwa Sharon alisema " matibabu ya kila aina yalifanyika ili kummponya Sharon, lakini haikuwezekana na hivyo hatupo naye tena."

Msemaji wa familia ya Areal Sharon, Yoram Ravid amesema " kwa kuwa Sharon alikuwa ni mwanajeshi na hivyo naimani mazishi yake yafafanywa kwa taratibu za kijeshi."

Areal Sharon, atakumbukwa kwa hisia tofauti, kwa wengine kumwita shujaaa na wengine muuaji.

Kufuatia kifo cha Areal Sharon, Viongozi mbali mbali duniani wametuma salamu zao za rambi rambi kwa watu na serikali ya Izrael.

Friday, January 10, 2014

Risasi zalipuka baada rais Michel Djotodia kutagaza kuachia urais.

Risasi zalipuka baada ya rais Michel Djotodia kutagaza kuachia urais.


Bangui, Afrika ya Kati - 10/01/2014.  Rais wa mpito wa Afrika ya Kati ameachia madaraka baada ya serikali yake kushindwa kuhimili vishindo vya mvurugano wa kisiasa nchi humo.

Tangazo hilo la rais Michel Djotodia kuachia madaraka limetolewa, huku mkutano wa kuleta amani ukifanyika nchini Chad.

Baada ya kutangazwa kujiudhuru kwa Djotodia, milio ya risasi ilisikika katika sehemu tofauti jiji Bangui, na kambi ya wakimbizi  Kikiristu 100,000 iliiingiwa na nderemo, na huku hakukuwa na hata mmoja wa wapiganaji wanaomuunga mkono Djotodia mitaani.

Kufuatia habari za kujiudhuru Michel Djotodia, waziri Ufaransa Ulinzi wa Jean-Yves le Drian amesema " tunatarajia kuwepo na uongozi mpya ambao utaiongoza Afrika ya Kati hadi kipindi cha uchaguzi na kuunda serikali itakato ongoza nchi kwa  kufuata sheria."

Afrika ya Kati nchi ambayo ilikuwa koloni la Ufaransa, imekumbwa na mvurugo wa kisiasa ambao umepelekea kuleta matabaka ya kidini kati ya Waislaam na Wakristu ambayo  kwa sasa makundi hayo yanapigana.
Na tangu kuanza kwa vurugu za kisiasa nchini Afrika ya Kati,  maelfu ya watu wamesha poteza maisha, mali zao na hata kukimbia na kuchukua ukimbizi nje ya nchi ya Afrika ya Kati.

Thursday, January 2, 2014

Mwaka 2014 waanza kwa Wakenya kujeruhiwa na bomu.

Mwaka 2014 waanza kwa Wakenya  kujeruhiwa na bomu. 



Mombasa, Kenya - 02/01/2014. Mlipuko wa  bomu umetokea  baada ya watu walio kuwa kwenye pikipiki kurusha bomu katika hotel moja mjini Mombasa.

Akiongea kuhusu shambulizi hilo, Evans Achoki ambaye ni mkuu wa tarafa ya Kwale alisema " nilisikia mlipuko uliotokea katika hotel kwa jina Tandoori na baadaye nilipofika pale nilikuta watu wamejeruhiwa"

Kuthibitisha mlipuko huo, msemaji wa polisi Jack Ekakuro amesema " watu 10 wamejeruhiwa kutokana na mlipuko wa bomu na kwa sasa majeruhi wapo hospital kwa matibabu."

Kenya imekuwa ikikumbwa na mashambulizi ya mara kwa mara ya mabomu, tangu nchi hiyo ilipoamua kulisaidia jeshi la serikali ya Somalia katika harakati zake za kupambana na kund la Al Qaeda. Na kundi hilo la al Qaeda kuhaidi kufanya mashambulizi nchini Kenya.

Mwaka 2013 haukuwa mwaka wa heri kwa Wairak.


New York, Marekani 02/01/2014. Umoja wa mataifa umetoa taarifa kuwa mwaka 2013 umekuwa mwaka ambao mauji kwa Wairak yalizidi kulinganishwa na miaka ya nyuma nchi humo.

Ripoti hiyo ya Umoja wa mataifa inasema kuwa "watu wapatao 8,868  wamepoteza maisha yao, na mauaji ya kutisha yametokea mwezi wa Desemba 2013 ambapo watu 759 ambapo 69 kati yao walikuwa ni walinzi na  maafisa usalama wa taifa."

Mauaji mengi yanayo tokea nchini Irak yamekuwa ni ya kisiasa au ya kimakundi  ambayo yanahusisha Washia na Wasuni, ambapo wamekuwa wakivutana katika  kuongoza nchi,  tangu kuangushwa kwa utawala wa Saadam Hussein na jeshi la Marekani na washiriki wake miaka 10 iliyopita.

Wednesday, January 1, 2014

Hali ya afya ya waziri mkuu wa zamani wa Izreal ipo tete.

Hali ya afya ya waziri mkuu wa zamani wa Izreal ipo tete.

Jerusalemu, Izrael 01/01/2014. Afya ya aliyekuwa waziri mkuu wa Izrael, Ariel Sharon inazidi kudorola siku hadi siku toka alipofanyiwa upasuaji wa na kuwekewa mirija ya kupitishia chakula mwezi Septemba mwaka jana.

 Amir Marom, ambaye ni msemaji wa hospital ya Hashomer alipo lazwa Sharon alisema kuwa " nikweli hali ya Sharon siyo nzuri kiafya na madakitari bado wapo wanafuatilia afya yake kwa ukaribu."

Kwa mijibu wa habari zinasema kuwa hali ya afya ya Ariel Sharoni ilianzakudhoofika  mara baada ya viungo vyake vya ndani ya mwili  kushindwa kufanya kazi vizuri. Lakini hazikueleza lini matatizo hayo yaliianza.

Waziri mkuu Arel Sharon 85 ambaye ni mwanzilishi wa chama cha Kadima, alilazwa hospital tangu mwaka January 4, 2006, baada ya kupata ugonjwa wa kiharusi, ambao ulimsababishia kutoka katika ulingo wa siasa nchi Izrael. 

Balozi wa Palestina auwawa kwa bomu.
Prague, Czecheslovakia - 01/01/2014. Balozi wa Palestina nchini  Czecheslovakia, ameuwawa kwa  bomu kwenye jengo analo ishi katika jiji la Prague.

Akithibitisha kuwepo na mlipuko wa bomu, msemaji wa polisi Andrea Zoulova amasema "balozi Jamal al Jamal   alifariki mara baada ya kufikishwa hospitali"

Na habari kutoka kwa ofisi ya mambo ya nje ya nchi  ya Wapalestina imesema " mlipuko wa bomu ulitokea wakati balozi, Jamal al Jamal alipo kuwa akijaribu kufungua kabati iliyokuwa imeletwa kutoka ofisi za zamani za ubalozi huo"

Hata hivyo serikali ya nchi Czechslovakia haija thibitisha kuwa mlipuko huo unahusika na ugaidi.



Tuesday, December 31, 2013

Jeshi la serikali la rais Salva Kiir lazidiwa nguvu.

Jeshi la serikali la rais Salva Kiir lazidiwa nguvu.


Bor, Sudani ya Kusini - 31/12/2013. Wapiganaji wanao pingana na  serikali ya Sudan Kusini, wa mekamata  mji wa Bor, baada ya kupambana vikali na  wajeshi wa serikali na kulizidi nguvu.

Akiongea baada ya kuukamata mji huo,  Moses Ruai ambaye ni msemaji wa jeshi la upinzani amesema " Mji wa Bor upo mikononi mwetu, na hivyo makao makuu wa jimbo la Jonglei ni yetu pia."

Wakati mapambano yanaendelea, kiongozi wa upinzani  na ambaye jeshi lake limetwaa mji wa Bor Riek Machar amekataaa kukutana na rais Salva Kiir ili kufanya mazungumzo ya kuleta amani ambayo yalitarajiwa kufanyika jijini Addis Ababa Ethiopia hii karibuni.

Hata hivyo kwa upande wa serikali, waziri wa mambo ya nchi za nje wa Sudan ya Kusini, Barnaba Marial Benjamin, amesema " mpango wa Riek Machar kushirikiana na kugawana madaraka na rais Salva Kiir haupo tena, na hii ni kutokana na kuwa Machar ni kiongozi wa jeshi linalotaka kupindua serikali halali ya wanchi wa Sudan ya Kusini."

Tangu kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe,  kwenye nchi changa ya Sudan ya Kusini na ambayo ilipata uhuru wake 2011, watu wapatao 1000 wamesha poteza maisha yao, wengi kujeruhiwa na mali nyingi kuharibiwa kutokana na vita hivyo.

Urusi ya shutuliwa na milipuko ya mabomu mfululizo.


Urusi ya shutuliwa na milipuko ya mabomu  mfululizo.

Moscow. Urussi - 31/12/2013. Muuaji ya kigaidi yametolea tena kwa mara ya pili katika mji wa Volgograd na kuuwa watu wapatao 14 na wengi 41 kujeruhiwa vibaya ja.

Mauji hayo yalitokea baada ya  bomu kulipuka katika basi la abiria linalo fanya mizinguko ya kuchukua abiria katika mji huo na kuwashitua wananchi wengi wa Urussi ambapo nchi yao ipo mbioni kuandaa mashindano ya michezo ya Olympic Baridi siku chache zijazo.

Mlipuko wa bomu  ndani ya basi umefuatia mlipuko mwingine ambao umetokea siku moja katika kituo cha treni cha mji huo na kusababisha vifo vya watu 18 na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa vibaya baada ya muuaji wa kujitolea muhanga kusimamishwa katika kizuizi cha kuingilia katika kituo hicho.

Kufuatia milipuko hiyo katika mji wa Volgograd, rais wa Urusi Vladimir Putin ameagiza ulinzi uongezwe na kuhaidi kuwa wale wote ambao wanahusika na milipuko hiyo ambayo ina nia ya kutishia wananchi wa Urusi watatiwa nguvuni na sheria itapitisha panga lake kwao.

Friday, December 27, 2013

Rais wa Sudan ya Kusini akubali suruhu.

Rais wa Sudan ya  Kusini akubali suruhu.

Juba, Sudan ya Kusini - 27/12/2013. Rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir  amekubali kusimamishwa mapambano ya kivita kati yake na kundi ambalo linaunga mkono mpinzani wake Riek Machar ambaye alikuwa makamu wake wa urais.

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya  na waziri mkuu wa Ethiopia  Hailemariam Desalegn waliweza  kumshawishi rais Kiir kukubali kusimamishwa kwa vita baada ya kukutana na kujadiliana katika mji mku  wa Juba.

Akiongea  baada ya rais Kiir  kukubali kusimamishwa kwa vita , rais Uhuru Kenyatta amaesema " nimefurahishwa na kitendo cha rais Kiir kukubali kusimamisha vita, kwani nafasi iliyopo ni finyu, na naomba ijulikane kuwa  IGAD haitaruhusu kuona rais aliyechaguliwa kihalali anatolewa madarakani kwa nguvu"

" Na nawaomba Riek Machar na rais Salva Kiir  kuhakikisha amani inarudi nchini Sudani ya Kusini kwani vita siyo suruhu ya kuleta maendeleo ya nchi." Aliongeza  rais Uhuru Kenyatta.

Jitihada za kusimamisha vita nchini Sudan ya Kusini  zinasimamiwa na  (Inter-Government Authority on Develoment -IGAD) ikiwa  na nia ya kusimamia uongozi bora na kuhakikisha kuondoa migogoro ya kisiasa katika nchi zilizopo  Afrika ya Mashariki na Kati.

Mvutano kati ya Udugu wa Kiislam na serikali waiweka amani ya Misri njia panda.


Kairo, Misri -27/12/2013. Waandamaji wanaounga mkono kundi la Undugu wa Kiislaam ( Muslim Brotherhood) wamepambana polisi katika matukio tofauti yaliyo tokea nchi Misri tangu kutangazwa kuwa kudi hilo ni kundi la kigaidi nchi Misri.

Katika maandamano hayo watu watatu wamepoteza maisha jiji Kairo, na wengine kujeruhiwa vibaya wakati polisi wa kuzuia ghasia  walipo pambana na waandamanaji,  na zaidi ya watu 265 wamekamatwa kutokana na vurugu hizo,  

Tangu kutolewa madarakani kwa nguvu kwa rais Mohammed Morsi, hali ya amani na utulivu imechafuka nchini Misri, na hii inatokana na wanachama  wanaounga mkono kundi la Undugu wa Kiislaam kutaka rais Mohammed Morsi arudishwe madarakani na pia wanapinga kitendo cha serikali kukitangaza cha chama cha Udugu wa Kislaamu kuwa cha kigaidi.

Saada al Hariri alia na Hezbollah.

Beiruti, Lebanon - 27/12/2013.  Saad al Hariri ambaye alisha wahi kuwa waziri mkuu wa Lebanoni, amelilaumu kundi la Hezbollah kwa kuhusikia na shambulizi la bomu ambalo limemuua mmoja ya mshauri wake mkuu.

Mohamad Bahaa Chatah 62, aliuwawa baada bomu kulipuka  katikati ya msafara wake wakati  alipo karibia ofisi za majengo ya serikali ambapo alikuwa njiani keelelea kwenye mkutano wa kuipinga Syria uliyokuwa ukiongozwa na Saad al Hariri

Mlipuko huo pia uliharibu majengo na kusababisha baadhi kushika moto na kuungua vibaya.

Akiongea kuhusu mauaji ya Chatah, Saada al Hariri alisema " watu walio muua Chatah ni wale ambao wanataka haki isitendeke kufuatia kuwepo na kesi inayotarajiwa kuanza kwenye koti ya kimataifa mjini  Hague Uholanzi mapema mwezi January 2014."

Mohamad Chatah, alikuwa mkosoaji mkuu wa serikali ya Syria,  amekuwa akipinga na kulaumu kundi la Hezbollah kwa kushirikiana na rais Bashar al Assad katika vita vinavyo endelea nchi Syria.

Kifo cha Chatah kimekuja wiki tatu kabla ya kuanza kesi zidi ya baadhi ya wanachama wa Hezbullah ambao wanasadikiwa kuhusika katika mauaji ya  mwaka 2005 ya waziri mkuu wa Lebanoni  Rafik al Hariri ambaye ni baba wa Saad al Hariri,



Wednesday, December 25, 2013

Rais wa Uruguay awapa zawadi ya kufunga mwaka 2013 wanachi wake.

Rais wa Uruguay awapa zawadi  ya kufunga mwaka 2013 wanachi wake.


Montevideo, Uruguay - 25/12/2013. Rais wa Uruguay amewapa salamu za Kristmas na mwaka mpya wanchi wake wa Uruguay kwa kusaini mkataba wa kuruhusu kilimo cha bangi na matumizi yake  nchini humo.

Akithibitisha kusainiwa kwa muswada huo, Diego Canepa ambaye ni msemaji kutoka ofisi ya rais amesema " rais Jose Mujica ametia sahii kuwa sheria kuruhusiwa kulima na kuuzwa bangi nchini humo siku ya Jumatu, na hii inatokana na wabunge kupiga kura kuunga mkono muswada huo,  na sheria hii itaaanza rasmi kutumika kuanzia April 9 2014."

Rais  Jose Mujica ambaye ndiye mwanzishi wa kampeni ya kuruhusiwa matumizi ya bangi nchini humo kwa kuamini kuwa kuruhusu  kilimo cha zao hilo nchini mwake kutapunguza uharamia na biashara haramu ambayo mara kwa mara umesababisha mauaji na kupunguza amani katika jamii ya Wauruguay.

Hata hivyo shirika la ukimataifa la kupambana na madawa ya kulevya limelaani kupitishwa kwa sheria hiyo na kudai ya kuwa Uruguay imevunja sheria za kimataifa ambapo ni nchi wanachama.

Papa Fransis aomba kuwepo na amani duniani.

Vatican City, Vatican - 25/12/2013.Mkuu wa kanisa Katoliki dunia Papa Faransis ameto wito kwa kila mtu kushiriki katika kulinda na kuleta amani duniani.

Akizungumza katika misa ya kusherekea siku ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu, Papa Fransis amesema " amani ni imekuwa ikivurugwa na watu wenye nia mbaya na pia  dunia na mazingira yake yamekuwa yakiharibiwa na watu wenye tamaa na ambao wanaleta maafa kwa jamii nzima."

Katika salamu za Kristmas, Papa Fransis pia aliongezea kwa kueleza ya kuwa nchi kama DRC Kongo, Nigeria, Sudani ya Kusini na Syria zimekuwa na migogoro ambayo imekuwa  inatakiwa iishe haraka " lakini kutokana na kukosa imani kwa wahusika  watu wamekuwa wakipoteza maisha  kila siku kitu ambacho ni kinyume na maadili a kiutu."

Papa Fransis ametimiza miezi tisa sasa tangu kutawazwa rasmi kuwa mkuu wa kanisa katoliki lenye waumini zaidi ya 1.2 billion na amekuwa akipinga vitendo vya kuvuruga amani vinavyo tokea duniani na  amekuwa akiwaagiza viongozi kwa kushirikiana na wananchi  kuhakikisha amani inakuwepo kwa kila mtu na kila jitihada zifanyike ili watu masikini wasaidiwe kuinua maisha yao.

Umoja wa Mataifa kichwa kuuma kwa Sudani ya Kusini.

New York, Marekani - 25/12.2013. Kamati ya usalama ya umoja wa mataifa imekubali kuongeza zaidi ya wanajeshi wake nchi Sudani ya Kusini kufuatia vita vinavyoenedelea katika ya wanajeshi wanao muunga mkono rais  wa sasa wa nchi hiyo Salva Kiir na mpizani wake na ambaye alikuwa makamu wa Riek Machar.

Toby Lanzer akithibitisha uamuzi huo wa UN alisema "Wanajeshi, 12.000 watakuwepo nchi Sudani ya Kusini  na  polisi 1,323 ili kuweza kulinda na kurudisha amani nchini Sudan, kwani wanajeshi na askari UN waliokuwepo hapo mwanzo walionekana kuzidiwa nguvu kutokana na vita vinavyo endelea hadi sasa nchini humo."

Kwa mujibu wa shirika la kimataifa la  kutete haki za binadamu limesema kuwa zaidi ya watu 1000 wamesha poteza maisha yao kutokana na vita hivyo na hadi sasa kuna makaburi yamegunduliwa yamezikwa watu wengi  jambo ambalo huenda likaleta mstuko mkubwa kwa jamii ya kimataifa.

Tangu kuanza vita kati ya wanajeshi wanao muunga mkono makamu wa rais wa Riek Machar na wanajeshi wa serikali ya rais Salva Kiir, maelfu ya Wasudani ya Kusini wamekimbilia katika makazi ya ofisi na maeneo yanayo tumika na umoja wa mataifa nchi humo ili kupata usalama wa masha yao.

Chama cha rais Mohammed Morsi matatani nchini Misri.

Kairo, Misri -25/12/2013. Serikali inayo ungwa mkono  na jeshi nchini Misri imetangaza imetangaza kuwa chama cha washirki na undugu wa Kiislaam ( Muslim Brotherhood)  ni chama cha kigaidi.

Akitangaza uamuzi huo, makamu wa waziri mkuu Hossam Eissa amesema ". chama cha Muslim Brotherhood ni chama cha kigaidi na kuanzia sasa tunakipiga marufuku na mtu yoyote atakaye husika na chama hicho atachukuliwa hatua  na hii  ikiwemo kushiriki katika kukichangia kipesa na kujumika katika maanadamano yatakayo pangwa na chama  hicho"

Chama hicho ambacho ndicho alichokuwa akiongoza rais Mohammed  Morsi aliyetolewa madarakani na jeshi na kushitakiwa kwa makosa  tofauti kinashutumiwa kwa kushiriki katika mashambulizi na kuvuruga amani nchini Misri, jambo ambalo chama hicho kimekanusha kushiriki katika kuchafua amani nchini humo.

Kufuatia kutangazwa kwa Muslim Brotherhood kuwa chama cha kigaidi, jeshi la Misri limepewa nguvu zaidi kutumi ikiwa wanachama cha chama hicho cha Kislaam watavunja sheria hiyo.

Edward Snowdon bado mwiba kwa shirika la ujasusi la Marekani.

Moscow, Urusi - 25/12/2013.Aliyekuwa mfanyakazi wa maswala ya kimtandao katika ofisi za kijasusi za NSA na ambaye alitoa siri za kijasusi za serikali ya Marekani na mshiriki wake  Uingereza hivi karibuni amezidi kupigilia msumari wa moto katika sekta ya ujasusi za washiriki hao.

Edward Snowden raia wa Marekani,  ambaye alikuwa mfanyakazi wa kijasusi katika maswala ya kimtandao na kwa sasa anaishi ukimbizini nchi Urusi amepigilia msumari huo wa moto kwa kusema  vitendo vya serikali kuchunguza watu wake umefikia hali ya kutisha.

"Na hata mtoto ambaye atazaliwa leo atakuwa hakuna kitu chake ambacho akijulikani, kwani serikali kwa kutumi vitu kama runinga, simu na vifaa vingine vya kisayansi ambavyo tunavitumia kila siku katika maisha yetu ndivyo vinatumika katika kuchunguza nyendo zetu za kila siku."

"Napenda kuwakumbusha kuwa kuishi kwa kuchunguzwa na serikali ni kinyume cha sheria, na nijambo ambalo serikali za Marekani na mshiriki wake wamevunja haki zetu za kibinadamu"

Edward Snowden ambaye kwa sasa amefunguliwa kesi nchi Marekani kwa kuiba nyaraka za siri za serikali akiwa kama mfanyakazi wa shirika la kijasusi la NSA nchini Marekani na kuifanya nchi hiyo kuwa na mvutano wa kidiplomasia na washiri wake wakaribu, baada ya  kutoa siri  kuwa Marekani inawachunguza raia na viongozi wa nchi tofauti duniani kinyume cha sheria.

Monday, December 23, 2013

Viongozi wa siasa nchi Nigeria wavutana.

Viongozi wa siasa nchi Nigeria wavutana.

Lagos, Nigeria - 23/12/2013.Mvutano kati ya rais wa sasa wa Nigeria Goodluck Jonathan  na rais mstaafu wa nchi hiyo Olusegun Obasanjo umefikia hatua nyingine baada ya malumbano ya chini kwa chini ambayo yamekuwa yakiendelea kwa muda sasa kati ya viongozi hao.

Mvutano huo umewekwa wazi na  rais Goodluck Jonathan baada ya kuamua kujibu barua iliyotumwa na aliyekuwa rais wa nchi hiyo Olugun Obasanjo kwa kuandika "baba Obasanjo, nasikitika saana kwa kunishutumu mimi na serikali yangu kuwa inafanya kila njia kuwauwa baadhi ya wanasiasa na kuna watu 1000  ambao wanafuatiliwa na wafanyakazi wa usalama ambao wamefundishwa kuuwa wale wote wanao onekana kuenda kinyume na serikali."

"Napenda kuualifu kuwa hayo unayo sema na kuandika siyo kweli, na nimeagiza uchunguzi ufanywe ndani ya serikali na pia mashirika ya kutetea haki za binanadamu niemaagiza yahusishwe katika uchunguzi huu ambao unania ya kuweka ukweli bayana.

Hali ya kutoelewana kwa viongozi hao kulianza baada ya rais mstaafu Obasanjo kumtaka rais Goodluk Jonathan kutogombe tena kiti cha urais, baada ya kupoteza viti 37 katika bunge la wawakilishi  kutoka na  wabunge 37 wa chama cha PDP kukuacha chama hicho na kujiunga na chama cham APC.

Rais Goodluck Jonathan na rais mstaafu Olugun Obasanjo wote ni wanachama wa PDP na wameweza kupata viti vya urais kupita chama cha PDP. 

Kwa mara ya kwanza Walibya wakubwa na mauaji ya kujitolea muhanga.

Tripol, Libya - 23/12/2013. Watu saba wamefariki baada ya muuaji wakujitolea muhanga kujilipua karibu na kizuizi kilichopo km 30 kutoka  jiji la Tripol.

Hii ni mara ya kwanza kwa  mauaji ya kujitolea muahanga  kutokea nchini Libya tangu kuangushwa kwa  utawalawa Muammar Gaddafi 2011.

Habari kutoka idara ya usalama ya nchi zinasema " hali imezidi kuwa siyo nzuri hasa katika swala la kiusalama, na hali ya kiusalama ya miji wa Benghazi na Tripol imekuwa katika hali tete kila kukicha "

Tangu kuangushwa kwa utawala wa Muammar Gaddafi, Libya imekuwa na vikundi tofauti vya kijeshi ambavyo vimegawanyika kutokana na kutoa afikiana baada ya vita vya kuipindua serikali kwa msaada wa Uingereza, Ufaransa na chini ya NATO jambo ambalo limekuwa likiangaliwa kuwa huenda likaleta mzuko wa kuanza vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Libya.

Mgunduzi wa AK-47 afariki dunia.



Moscow, Urusi - 23/12/2013. Mgunduzi wa siraha ya aina ya AK-47 ambayo imekuwa maarufu na kuwa moja ya siraha kipenzi  kimapambano amefariki dunia.

Mikhail Kalashnikov 94, amefariki dunia na kuacha historia ambayo itakuwa akikumbukwa  kwa muda mrefu kwa umairi wake wa kugundua siraha ambayo hadi leo inaleta  changa moto katika matumizi yake sehemu mbali mbali duniani.

Akiongea baada ya kupata habari ya kifo Mikhail Kalashnikov, rais wa Urusi Vladmir Putin alisema " nivigumu kukubali ya kuwa  hatupo naye tena Mikhail Kalashnikov, na tumepoteza mtu muhimu katika jamii nzima ya Kirusi kwani Kalashnikov alikuwa  mzalendo aliye tetea kwa  kupigania nchi yake wakati wa maisha yake yote."Alimalizia rais Putin.

Mikhail Kalashnikov, aligundua siraha ya AK-47  mwaka 1947 baada ya kupona majeraha ya bega ambayo aliyapata wakati akiwa vitani alisema " nilipata hili wazo baada ya kuzinduka kitandani wakati nilipo kuwa nimelazwa hospital kwa matibabu."

Wakati wa uhai wake mara kwa mara Mikhail Kalashnikov, amekuwa akisema yakuwa hajutii ugunduzi wake, kwani ulisaidia kulinda  heshima ya Urusi."

Siraha ya AK-47 imekuwa ikitumika katika kila aina ya mazingira ya kivita na inasifika kwa kutokuwa na matatizo ya aina yoyote katika matumizi kama siraha nyingine,  na kwa miaka 60 sasa imekuwa ni siraha hatari duniani kutokana na umairi wake.

Sunday, December 22, 2013

Mahakama ya Uingereza yatupilia mbali kesi ya mwanasiasa wa Libya.

Mahakama ya Uingereza yatupilia mbali kesi ya mwanasiasa wa Libya.


Tripol, Libya -22/12/2013.  Mahakama  jijini London imetupilia mbali kesi ya mmoja wa kiongozi waliosaidia kuung'oa utawala wa Muammar Gaddafi 2011.

Akitoa hukumu kabla ya kutupilia mbali kesi ya Belhaj imedai Jaji  Simon alisema, " kwa kuangalia mwenendo mzima wa kesi hii, matendo mengi yalitendeka Malasyia, Thailand and  Libya na ambapo ni  nje ya nchi na hivyo hayahusiki na Uingereza."

Akiongeaa baada ya  hukumu kutolewa Belhaj  alisema " Maelezo ninavyo fahamu ni kuwa ikiwa kesi hii itaendelea, wanadai kuwa itawaaibisha Marekani, navilevile itahatarisha usalama wa taifa la Uingereza."

" Lakini hata hivyo kwa kupitia mwanasheria wangu tutapambana hadi tupate ushindi na kwani haki itatendeka mwisho wa siku."

Abdul - Hakim Belhaj,ambaye kwa sasa amekuwa mmoja wa viongozi wa siasa nchi Libya, ambaye amemeushitaki uongozi wa juu wa ofisi ya mambo ya nje wa Uingereza na mkuu wa MI6, Sir Mark Allen  kwa kosa la kumkamata kwa nguvu na kumpeleka  Libya wakati wa utawala wa Gaddafi na kuteswa.

Kesi ya kuwakamata watu kwa nguvu na kuwapekeka katika maeneo ya mateso, zimekuwa zikiiandama serikali ya Uingereza, na hata baadhi ya majaji kudai kuwa sheria ilivujwa na wakuu wa usalama wa Uingereza katika kufanya vitendo hivyo.

Mkwe wa Bin Osama Bin Laden aongezewa mashitaka.

New York,Marekani - 22/12/2013. Mahakama jijini New  York katika kitongoji cha Manhattan, imemuongezea mashitaka mawili zaidi aliyekuwa mkwe wa mkuu wa kundi la Al Qaeda Osama Bin Laden.

Suleiman Abu Ghaith, ameongezewa mashitaka ya  kusaidia kimali na kutoa habari katika kundi la Al Qaeda kuweza kufanya mashambulizi yake nchini  Marekani ya Sept 11 2001.

Suleiman Abu Gaith ambaye ni mzaliwa wa Kuwait alikutwa hapo awali na kosa baada ya kuongea maneno yakuunga mkono mashambulizi ya Sept 11. kwa kusema " tunafuraha kuona wapiganaji wa Mijaidini wameweza kushambulia nchi Marekani kwa uwezo wa Mungu na mapema dunia itashuhudia kushambuliwa kwa miradi ya Marekani na Waizrael."

Mashambuzi ya Sept, 11-2001 nchini Marekani yalisababisha vifo vya watu 3000, na watu kadhaa kuumia na mali nyingi kuharibiwa baada ndege zilizo kuwa zimetekwa na magaidi wa kundi la Al Qaeda kufanya mashambulizi Trade Centre New York, Pentagon na Pennsylvania.

Suleiman Abu Gaith anatarajiwa kufikishwa mahakamani kusikiza kesi zake Februri 3, 2014.

Friday, December 20, 2013

Rais Vladmir Putin aonyesha huruma yake. 
 

Moscow, Urusi -20/12/2013. Rais wa Urusi Vladimir Putin ametoa msamaha kwa aliyekuwa bilionea ambaye alikuwa amefungwa kwa makosa ya rushwa na kukiuka matumizi ya usambazaji wa pesa wa nchi ya Urusi.
 
Mikhail Khodorkovsky, ambaye amekaa jela miaka 10, baada ya kuhukumiwa kwenda jela mwaka 2003 aliachiwa huru leo kutoka katika gereza lililopo katika mji wa Karelia km 1,000 toka jiji la Moscow, baada ya rais Putin kutoa msamaha kutokana na sababu za kibinadamu na kiutu.
 
Akithibitisha kuachiwa na kuwasili Ujerumani, aliyekuwa waziri wa mambo ya nje Hans-Dietrich Genscher amesema " Mikhail Khodorkovsky amewasili katika jiji la Berlin kwakutumia ndege binafsi na mimi ndo nimemchukua toka kiwanja cha ndege."
 
Kuachiwa kwa Khodorkovsky kumekuja baada ya jitihada za Kansela  Waujerumani Angela Markel kukubalika na rais Putini ambapo kila walipo kutana aliomba serikali ya Urusi kumwachia Mikhail Khodorkosky.
 
 
Edward Snowden azidi kuziumbua Marekani na Uingereza.
 
 
London Uingereza - 20/12/2013. Sakata la shirila la kijasusi la Uingereza  na mshirikiwa wake Marekani kugundulika kuwa walikuwa wanachunguza na kusikiliza mazungumzo na mawasiliano ya simu na mtandao yamefichuliwa kwa mara nyingine tena.
 
Magazeti ya The Guardian Uingereza, The New York Time Marekani  na Der Spiegal la Ujerumani yameandika zaidi ya  majina 1000 ya watu wambao walikuwa wakuchunguzwa, kufuatiliwa nyendo zao kimtandao na kusikilizwa simu zao na  mashirika ya kijasusi ya NSA ya Marekani na GCHQ ya Uingereza  kinyume cha sharia za kimataifa.
 
Magazeti hayo yameandika kuwa "NSA na GCHQ wamechunguza nyendo za viongozi umoja wa Ulaya, mashirika ya haki za binadamu, waziri mkuu wa Izrael na pia zaidi ya nchi 60  hasa viongozi wa Afrika na familia zao, na pia  shughuli zinazo endeshwa na Umoja wa Mataifa na viongozi wake."
 
Kutolewa kwa ripoti hizi mpya ambazo chanzo chake ni raia wa Marekani Edward Snowden ambaye alikuwa mfanyakazi wa NSA na  kwa sasa yupo ukimbizini nchini Urusi, kumekuja baada ya ile kashfa ya kuwa mashirika hayo kwa pamoja yalikuwa yanashirikiana kusiliza mazungumzo ya  Kansela wa Ujerumani Angela Markel na kuleta mtafaruku wa kidiplomasia kati ya nchi hizo.
 
 
 Chama tawala Afrika ya Kusini njia panda na washirika wake.
 
Pretoria, Afrika ya Kusini - 20/12/2013. Moja ya chama kikuu  cha wafanyakazi nchini Afrika ya Kusni kimetangaza kutounga mkono chama tawaza cha ANC - (African National Congress) wakati wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika 2014. 
 
NUMSA ambacho ni chama cha wafanyakazi wa viwanda vya vyuma,  ambacho kinawanachama zaidi ya 3,00,000, kimetoa azimio hilo wakati wa mkutano wa wanchama hao uliyofanyika hvi karibuni jijini Johannesburg.
 
Kiongozi wa chama hicho Irvin Jim  alisema  "NUMSA inajitoa katika kuunga mkono ANC, kwani chama cha ANC kimekuwa hakifanyi jitihada ya kupambana na rushwa na kupunguza umasikini na ufukara kwa wanachi wake na pia kukiuka ilani ya chama."
 
NUMSA imekuwa bega kwa bega na ANC tangu mwaka 1994, na hivi miaka ya karibuni imekuwa ikivutana na ANC kwa kudai ya kuwa chama cha ANC hakitekelezi kazi zake vizuri na kuwa kinatizama sana upande wa uchumi huria ambao haunufaishi watu walio wengi nchi Afrika ya Kusni.
 
ANC imekuwa na wakati mgumu katika sera zake kukuza uchumi chini Afrika ya Kusini, kutoka na na msukumo nguvu uchumi wa kuleta mabadiliko kuruhusu kuwepo na uchumi huria, jambo ambalo vyama vingi vya wafanyakazi vimekuwa vikiupinga mfumo huo.
 
 
Jela maisha ukiwa shoga nchini Uganda.
 
 
Kampala, Uganda - 20/12/2013. Bunge la Uganda limepitisha musuada ambao utakuwa wa kifungo cha maisha kwa mashoga wa kiume na wakike katika kura zilizo pigwa bungeni humo leo.
 
Uamuzi wa bunge la Uganda kupigia kura ya ndiyo ya kupitisha adhabu ya kukaa jela maisha, imekuja maada ya adhabu ya awali ya kunyongwa ambayo ilipingwa vikali na wana harakati wa kimataifa wa kutete haki za mashoga.
 
Msemaji wa bunge la Uganda amesema "Ushoga  ulikuwa ni haramu tangu enzi za serikali ya kikoloni nchini Uganda na kama tukiachia tabia hii itatualibia jamii nzima ya Waganda."
 
Sheria ya kuukataza  ushoga nchini Uganda  ilipitishwa kwa mara ya kwanza nchini humo mwaka 2009 ambapo spika wa bunge Rebeka Kadaga alisema "kupitishwa kwa sheria ya kupinga ushoga ni zawadi nzuri ya Krismasi kwa Waganda."
 
Wabunge wa Uganda wamekuwa wakidai yakuwa kanisa la Kievanjilisti la asili ya kuutoka Marekani limekuwa likiunga mkono ushoga na linakampeni ya kuusambaza ushaoga barani Afrika, madai ambayo wakuu wa kanisa hilo kutoka Marekani walikanusha.
 
Hata hivyo musuada huo utakuwa sheria baada ya rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museni kusaini kuwa sheria.
 
 
Baraka Obama aonya kuhusu mapigano nchini Sudani Kusini.
 
Juba, Sudani ya Kusini - 20/12/1213. Rais wa Marekani amezitaka pande zote zinazo pigana nchini Sudani Kusini kusimamisha mapigano haraka iwezekenavyo.
 
Baraka Obama alionya kwa kusema kuwa " Inabidi pande zote zinazo pigana nchi Sudani ya Kusini kucha mara moja vita, kwani vinaweza kuleta maafa makubwa kwa jamii na hatimayake kuwa vita vya wenyewe kwa wenyewe."
 
" Kitendo cha kutumia siraha ili kuweza kupata nguvu za kisiasa ndani ya nchi ni kitendo kibaya, na kila upande lazima wasikilize busara za kimataifa." Alimalizia rais Obama.
 
Wakati amani nchini Sudani ya Kusini imevurugika, mwanajehi wa umoja wa Mataifa kutoka nchi Indi amefariki dunia na mmoja kujeruhiwa, baada ya kushambuliwa ya wapiganaji wanao muunga mkono mpinzani wa serikali ya  ambaye alikuwa makamu wa rais Riek Machar kwa  kushambulia ngome ya makazi ya wafanyakazi wa umoja wa mataifa katika mji wa Bor.
 
Hadi kufikia sasa, zaidi ya watu 500 wamesha potea maisha yao wakiwemo wanajeshi 100, tangu mapambano yalipo anza, baada ya serikali ya rais Salva Kiir kudai ya kuwa imegundua mbinu za kutaka kuipindua serikali, zilizo kuwa zimepangwa na makamu wa rais Riek Machar, ambaye mmpaka sasa ajulikaani mahaali alipo.
 
 
Rwanda kupeleka majeshi yake Afrika ya Kati.
 

Kigali, Rwanda - 20/12/2013.Serikali ya Rwanda imekubali ombi la umoja wa Afrika kupeleka wanajeshi wake katika nchi ya Afrika ya Kati ili kusaidia kurudisha amani.

Akithibitisha hayo, kwa kutukia mtandao wa twiter, waziri wa mambo ya nje wa Rwanda, Louise Mushikiwabo aliandika " Rwanda iliombwa kuchangia wanajeshi nchini Afrika ya Kati, na wanajeshi wa Rwanda wapo katika matayarisho kuwasili jiji Bangui mapema iwezekanavyo"

Uamuzi wa Umoja wa Afrika kuomba msaada kwa jeshi la Rwanda umekuja baada ya ya hali ya amani katika nchi ya Afrika ya Kati kuwa mbaya zaidi, ambapo imefikia kuwa ugomvi wa kidini, kati ya  kundi linalo julikana kama Anti-Balaka la Wakristu kuanza kushabuliana na kundi la  Kiislaam la Seleka.

Kuchafuka kwa amani katika nchi ya Afrika ya Kati, kumesababisha zaidi ya watu 6,00,000 kukimbia makazi yao na huku kati yao 2,00,000 wakiokea jiji Bangui.