Sunday, September 9, 2012

Mtoto wa Muammar Gaddafi kuondoka nchini Niger.

Mtoto wa Muammar Gaddafi kuondoka nchini Niger.


Niamey, Niger - 09/09/2012. Mtoto wa aliyekuwa rais wa Libya Muammar Gaddafi anatarajiwa ,kuondoka nchini Niger.
Saadi Gaddafi mtoto ambaye alikimbilia nchini Niger baada ya serikali ya baba yake Muammar Gaddafi kuangushwa na baadaye kuuwawa.
Kwa mujibu wa habari zinasema " Waziri wa mambo ya nje wa Bazoum Mohamed ameshatoa rukhusa kwa Saadi Gaddafi kuondoka nchini Niger."
Habari zilizo patikana zimedai ya kuwa huenda Saadi akaamia nchini Afrika ya Kusini, japo hadi sasa hakuna  habari za huakika kutoka katika serikali ya Afrika ya Kusini.


Moscow yaonya mashabulizi zidi ya Iran.
Moscow, Urusi - 09/09/2012. Waziri wa mambo ya nje wa Urusi ametoa onyo ya kuwa kitendo chochote cha kuishambulia Iran kijeshi kitaleta madhara makubwa.
Akiongela swala hilo makamu wa waziri wa mambo ya ndani y Urusi  Sergey Ryabkov alisema "tunapenda kuonya ya kuwa mashambulizi ya kijeshi zidi ya Iran yataleta maafa makubwa ambayo yatavuka mipaka ya nchi za Mashariki ya Kati,  na napenda kusisitiza suala la Iran na nguvu zakinyuklia nivizuri kujadiliwa katika meza kuliko kutumia nguvu za kijeshi."
Mazungumzo hayo yamekuja huku nchi za Ulaya na Marekani zikiwa zimezidisha jitihada za kutaka Iran iwekewe vikwazo vya kiuchumi ambavyo vitaifanya nchi hiyo kuachana na mradi wake wa kinyuklia.