Wednesday, September 24, 2008

Israel yapata waziri mkuu mpya"Ni mwanamke wa kwanza kuwa waziri mkuu".

Nitarudi kuonyesha uwezo wangu muda si mrefu"Asema aliye kuwa nyota wa soka wa dunia mara tatu".

Rio De Janeiro, Brazil-22/09/08.Nyota wa soka wa dunia wa miaka ya ipatayo kama sita iliyo pita Ronaldo, amesema hivi karibuni ya kuwa hatakubali kukaa chini na kuacha kipaji chake cha kutikisa nyavu kina pote hivi hivi.
Aliyasema haya mara baada ya kuanza mazoezi tayari kurudi uwanjani, mara baada ya kufanyiwa upasuaji wa goti,ambalo lilikuwa linamsumbua saana , na kushindwa kufanya vitu vyake awapo uwanjani.
Alisistiza yakuwa, hatasimamishwa na kitu chochote, kwani mpria ndiyo starehe yake,na wapenzi wa soka wasubiri pindipo atakapo rudi uwanjani, ndipo wata jaji wenyewe.
Picha hapo juu, anaonekana Ronaldo, akianza kufanya mazoezi ya kuchedzea mpira , mara baada ya kupata kupona upasuaji wa giti.
Picha ya pili anaonekan Ronaldo , enzi zake kabla ya kuwa mgonjwa wa giti, akishangilia goli huku akiwa amavalia jezi ya timu yake ya taifa ya Brazil.
Picha ya chini, wanaonekana wafalme walio weka historia ya kusakata soka wa karne ya sasaa 21, Ronaldo na Zidane, wakipeana mikono kabla ya mechi ya kuchangisha pesa kwa ajili ya kupiga vita umasikini duniani.
Israel yapata waziri mkuu mpya" Ni mwanamke wa kwanza kuwa waziri mkuu".
Jerusalem,Israel-22/09/08-Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Israel bi Tzipi Livni , amechaguliwa kuwa waziri mkuu, kuchukua nafasi ya aliyekuwa waziri mkuu Ehud Olmert.
Bi, Livni mwenye miaka 50, amekuwa mwanamke wa kwanza kuwa waziri mkuu wa Israel tangu mwaka 1974 na alishawai kuwa mfanyakazi katika ofisi za maswala ya usalama wa Israel (Mossad).
Kwa kufuatia kuchaguliwa kwakwe kuwa waziri mkuu, bi Livni, amepewa ruhusa na rais wa Israel, Shimon Peres, kuunda serikali kwa muda usiopungua siku 42.
Picha hapo juu ni ya bi Tzipi Livni,akiongea mara baada ya kuchaguliwa kuwa waziri mkuu wa Israel.
Chini, wanaonekana waziri mkuu mpya wa Israel bi, Tzipi Livni na rais Shimon Peres, wakiwa pamoja, wakati bi Livni ,alipo kwenda kumwona na kupewa ruhusa kuunda serikali mpya.
Uchungu kuondoka kwa rais,asema Zuma,"na rais mpya wa muda ateuliwa".
Pretoria,Afrika ya Kusini-23/09/08.Rais wa ANC,(African National Congress), Jacob Zuma, amesema ya kuwa kujiuzuru kwa rais, Thabo Mbeki ni kitendo ambacho kinacho tia uchungu, kwa chama na kwa wananchi wote na wanachama wa ANC.
Hata hivyo, alisema ya kuwa rais, Mbeki, ameshajiuzuru,basi inabidi tuendele mbele kuendeleza nchi.
Na wakati huo huo, bunge la Afrika ya Kusini, limemteua Kgalema Motlanthe, kuwa rais wa wa muda , mpaka hapo uchaguzi mpya wa nchi utakapo fanyika mwezi wa nne - 2009.
Motlanthe, ambaye amekuwa yupo kati ya bwana Zuma na rais Mbeki, kwa kuzingatia ni mmoja wa viongozi ambao walio tetea nchi wakati wa ubaguzi wa rangi nchi humo na kufungwa pamoja na rais wa kwanza wa Afrika ya Kusini , Nelson Mandela.
Picha hapo juu ni ya rais mpya wa Afrika ya Kusini,Kgalema Motlanthe, akoingea mara baada ya kuteuliwa kuwa rais wa mpito hadi hapo uchaguzi wa mapema 2009.
Picha ya pili wanaonekana rais,mstaafu wa Afrika ya Kusini, Thabo Mbeki, akiongea na Kgalema Motlanthe, wakati wa mkutano mkuu wa chama cha ANC.
Picha ya nchini ni ya rais wa chama cha ANC, Jacob Zuma, ambaye kesi zidi yake imepelekea kujiuzuru kwa rais Mbeki.
Iran, haina mpango wa kutengeneza bomu la nyuklia "Asema rais wa Iran".
New York Amerika-24/09/08.Rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad ameutubia tena umoja wa Mataifa, kwa kulaumu nchi zenye nguvu duniani kwa kutumia uwezo wake visivyo.
Aliongeza kwa kusema yakuwa nchi hizo zikiongozwa na Amerika, zimekuwa zinatumia nguvu zao kuonea nchi zisizo na nguvu.
Rais Ahmadinejad, alisema yakuwa sasa Amerika imekuwa ikijihusisha na mambo mengi ya dunia na ndiyo maana uwezo wake kiuchnumi unaporomoka na Amerika inaelekea mwisho wa njia yake.
Na kuhusu mpango wa Iran , kuendelea na kujenga mitambo ya kinyuklia, rais Ahmadinejad, alisema yakuwa nchi yake, ina jenga mitambo kwa matumizi ya kawaida na siyo mitambo ya kutengeneza mabomu,na huo ndio msimamo wa Iran na wananchi wa Iran.
Picha hapo juu, anaonekana rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad, akihutuubia mkutano mkuu wa umoja wa matifa katika kikao cha mwaka 2008, ndani ya jiji la New York.

Saturday, September 20, 2008

Rais, Thabo Mbeki, akubali kung'atuka madarakani"ANC yashinikiza"

Bi,Oprah Winfrey, akonga nyoyo za wanamama na wasichana nchini Saudi Arabia.

Dammam, Saudi Arabia-20/09/08. Maonyesho vipindi vinavyo tangazwa na bi Oprah Winfrey kwenye runinga za nchi Saudi Arabia yamezidi kupendwa na kusaidia upeo wa wanawake nchini humo.
Akiongea haya, mmoja ya wapenzi wa maonyesho ya vipindi ya Opra Winfrey, bi Nayla, alisema vipindi vya Oprah , huwa vinamfanya ajisikie kama anamwongelea yeye(Bi Nayla), na kusema, huwa vinamsaidia kuelewa baadhi ya mambo ambayo alikuwa haya elewi vizuri.
Maonyesho ya Oprah Winfrey,nchini Saudu Arabia, yalianza kuonyeshwa rasmi kwenye runinga nchini humo mwisho wa mwaka 2004 na yamekuwa yaklizidi kupendwa wasichana na wanawake , hasa wenye umri kati ya miaka 25 na kuemdela, kwa mijibi wa ripoti ya wachunguzi wa mambo ya utazamaji wa runinga nchini Saudi Arabia.
Picha hapo juu anaonekana bi Oprah Winfrey akiwa amekaa kwenya kochi, katika moja ya maonyesho yake, huku ameshikilia viatu.
Picha ya pili anaonekana, bi Oprah Winfrey kwenye mtandao, ambao umeandikwa maandishi ya kiarabu.
Chini ni picha ya bi Oprah Winfrey, akiwa amependeza kwa vazi lake la heshima, moja ya mavazi yanayo wavutia wanawake wengi nchini Saudi Arabia.
Rais wa Pakistan atoa onyo"Pakistan haitaruhusu uvamizi wa aina yoyote ndani ya nchi yake" Wakati huo hotel kulipuliwa na bomu.
Islamabad, Pakistan-20/09/08.Watu wapatao 60 wamepoteza maisha yao na wengine 200 kujeruhiwa baada ya bomu kulipuka kwenye maeneo ya hotel Marriot.
Mlipuko huo ulitokea wakati, roli moja lilipo ingia kwenya maeneo haya hotel,na kulipuka.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya Pakistan, huu mlipuko ni ule wa kujitolea muhanga.
Hotel Marriot, huwa inapokea wageni wengi kutoka nje ya nchi ya Pakistan, na muda wote huwa na ulinzi mkali, alimalizia kwa kusema.
Mlipupo huu ni wapili , baada ya ule ulio tokea siku ya jumatano katika majengo ya shule za kidini.
Mlipuko huu , umekuja wakati rais,mpya wa Pakistan, Asif Ali Zardari, alipo maliza kuongea mbele ya bunge la Pakistan mapema mchana, na kuhaidi yakuwa nchi yake aitakubali kushambuliwa au kutumika na ugaidi wa aina yoyote, au kushambulia nchi yaye katika jina la gaidi.
Picha hapo juu ni moto mkubwa unaunguza majengo ya hotel Marriot, baada ya kulipuliwa kwa bomu.
Picha ya pili anaonekana rais wa Pakistan , Asif Ali Zardari, akiongea mbele ya bunge, kabla ya mlipuko mkubwa kwenye hotel ya Narriot.
Picha ya tatu wanaonekana baadhi ya watu wakisaidina kuondoa mmoja ya majeruhi wa mlipuko wa bomu lililo tokea kwenye maeneo ya hotel Marriot.
Picha ya chini, wanaonekana, wananchi wakijaribu kuangalia bila mafanikio nini la kufanya kuokoa baadhi ya vitu vyao ambayo vimearibika kutokana na mlipuko wa bomu.
Rais, Thabo Mbeki, akubali kung'atuka madarakani"ANC yashinikiza".
Pretoria, Afrika ya Kusini-20/09/08. Chama tawala nchini Afrika ya Kusini ANC,-African National Congress, kimetangaza rasmi yakuwa rais wa wa nchi hiyo, Thabo Mbeki, ang'atuke madarakani.
Akiongea haya katibu mkuu wa ANC, bwana Gwede Mantashe, alisema yakuwa ANC, imeamua ya kuwa rais Thabo Mbeki, inabidi ang'atuke madaraka.
Kwamujibu wa msemaji wa rais, Mbeki,aliseama yakuwa rais, Thabo Mbeki, amekubali kujing'atua madarakani.
Picha hapo juu anaonekana rais, Thabo Mbeki, akiwa anaongea katika moja ya mikutano na wawekeza vitega uchumi wakati alipo tembelea nchini Nigeria.
Picha ya pili, anaonekana rais Mbeki,alipo kuwa anasalimiana na wananchi wakati wa moja ya kampeni za uchaguzi nchini Afrika ya Kusini.
Picha ya mwisho, inaonesha rais, Thabo Mbeki akiwa maeshikilia kichwa na kuonyesha ya kuwa huwa anakuwa na wakati mgumu kutatua mambo ya kisiasa na kiuchumi, hasa yanapo kuwa yanaleta mvutano.
Mtandao wa kundi la Shia nchini Iraki wakumbwa na virusi.
Baghdad,Iraki-20/09/08. Mtandao unao milikiwa na mkuu wa ya waumini wa jumuia ya Shia, ume kumbwa na matatizo ya mawasiliano,baada yakuingiliwana virusi ambavyo vinazuia kuonekana kwa habari na maelezo ya kidini kwa wafuasi wa jumuia ya Shia.
Kwa mujibu wa kumdi la XP, limesema ya kuwa hayo yamekuwa ni ajili ya kulipiza, kwa yale waliotendewa waumini wa jumuia ya Suni.
Waasimu wakubwa wasiasa wakubalina kuiongoza nchi"Rais ni Mugabe na Tsvangirai ni waziri mkuu".
Harare,Zimbabwe-15/09/08. Rais Robert Mugabe na mpinzani wake bwna Morgan Tsavangirai, wametiliana sahii makubaliano ya kugawana madaraka ya kuongoza wananchi Wazimbabwe.
Makubaliano haya yamefikiwa baada ya muda mrefu wa mvutano wa kisiasa tangu kufanyika uchaguzi wa urais kati ya wafuasi chama cha ZANU-PF na MDC.
Mgogoro huo ulianza tatuliwa kwa majadiliano ya usuruhisi na rais wa Afrika ya Kusini, Thabo Mbeki, na hatimaye walifikia makubaliano, ambapo Rais Mugabe atabaki kuwa rais, Tsvangirai atakuwa ni waziri mkuu wa nchi.
Hapo juu ni picha ya bendera ya bendera ya Zimbabwe, nchi ambayo imekuwa ina mgogoro wa kisiasa tangu kufanyika uchaguzi, na kutatuliwa chini ya uongozi wa rais wa Afrika ya Kusini, bwana Thabo Mbeki.
Picha ya pili wanaonekana rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe,waziri mkuu mpya wa Morgani Tsvangirai na msuruhishi wa mgogora wanasiasi wa Zimbabwe, rais Thabo Mbeki.
Picha ya mwisho, wanaonekana viongozi wapya wa Zimbabwe rais Mogabe na Tsvangirai wakipeana mikono baada ya kukubali kuongoza nchi kwa pamoja.

Wednesday, September 17, 2008

Biashara za hisa zapigwa na tetemeko la ukwasi.

Baba wa Kiafrika, aonyesha uwezo wake, "sitoi taraka kwa wake zangu"Hii ni baraka.

Jimbo la Niger , Nigeria- 2/09/09. Bwana mmoja kwa jina, Mohammed Bello, ametakiwa na mahakama ya kislaamu, awape taraka baadhi ya wake zake, ama atachukuliwa atua za kisheria.
Lakini kwa mujibu wa msemaji wa bwana Mohammed Bello,alisema yakuwa hawezi kuwapa taraka wake zake na anampango wakuoa wake wengine, kuoa kwake wanawake hawa ni mipango ya Mungu na anabarikiwa na Mungu kuweza kuwahudumia na kukidhi mahitaji ya famila yake yote, ni kifo ndicho kitakacho tutenganisha.
Picha hapo juu ni ya bwana Mohammed Bello, ambaye ana ameoa wanawake 86, na anadaiwa na mahakama awape taraka wanawake wengine.
Picha ya katikati ni ya nyumba ya bwana Mohammed Bello , ambapo wanaonekana baadhi ya wake na watoto wa bwana Mohammed Bello wakiwa wana endelea na shughuli zao.
Picha ya chini ni ya famili ya bwana, Mohammed Bello,wake zake pamoja na watoto.
Bwana Mohammeda mwenye umri wa miaka 84, ameoa wanawake 86 na watoto 170.
Ofisi za kibalozi za Amerika zashambuliwa na magaidi.
Sanaa, Yamen-17/09/08. Watu wapatao 16 wamepoteza maisha yao, baada ya ubalozi Amerika kushambuliwa kundi moja la kigaidi lijulikanalo Islamiki Jihad lililopo nchini Yamen. Mauaji hayo yalifanya kwa mtu mmoja aliyekuwa akiendesha gari kuelekea ofisi za ubalozi wa Amerika na kulipua gari ambapo ofisi zilishika moto.
Matukio hayo yamelaniwa vikali na serikali ya Amerika, na rais Bush amesema ya kuwa hii inaonyesha ya kuwa vita dhidi ya ugaidi bado kubwa na Amerika itashida vita hivi.
Juu ni picha ya moja ya majengo yakiwa yameshika moto na moshi ukiwa unaonekana mara baada ya kutokea mlipuko wa bomu.
Chini ni jengo la ofisi za ubalozi wa Amerika , ambazo zimeshambuliwa na magaidi.
Biashara za hisa zapigwa na tetemeko la ukwasi.
New York, Amerika- 16/09/08. Masoka ya hisa nchini Amerika yameikumbwa na wakati mgumu, mara baada ya kushindwa kuhimiri mzunguko wa hisa , kutokana kupata hasara ya kifedha na kushuka kwa kiasi cha alama 150.
Hii imekuja mara baaada ya kampuni mama, benki ya kuwekaza, Lehmana Brothers kushindwa kuendelea na shughulizake za kimasoko.
Hata hivyo msemaji mmoja wa serikali alisema yakuwa hali hii ni ya muda tu, na kuwa hali ya masoko na hisa yatarudi katika hali yake ya kawaida hapo baadaye.
Picha hapo juu ni ya jengo ambalo, shughuli za kibiashara za hisa huwa zinaendelea.
Chini ni picha ya mmoja ya wana hisa akiwa ameshikiria masikio, huku akiwaaamini macho yake nini kinaendelea, kwani mtandao wa biashara yake unaelekea kwenye mshare wa hasi, na ajui afanya nini.
Iraq kupata Amiri jeshi mpya" Amiri jeshi wa zamani amaliza muda wake".
Baghdad, Iraq-16/09/08- Aliyekuwa Amir jeshi mkuu wa jeshi la Amerika linalo simamia ulinzi na kupamabana na makundi yanayo pinga demokrasi nchini Iraq Generali, David Petraeus amemaliza muda wake hivi karibuni na kumkabidhi madaraka Generali Ray Odirno ambaye alikuwa makamu wake.
Katika kukabidhiana madaraka haya, kulishuhudiwa na waziri wa ulinzi wa Amerika bwana Robert Gates.
Gen, Petreaus, ndiye aliye fainikwa kuweza kupunguza mashambulizi nchini Iraq kwa mpango na mikakati yake ambayo iliwezesha wanajeshi kuwa karibu na wananchi na kusaidia kushinda na kugundua njama, dhidi ya makundi yanayo pinga serikali na kuwepo kwa majeshi ya Amerika na washiriki wake.
Picha hapo juu wanaonekana , Gen Ray Odierno kushoto akipokea bendera ikiwa ni ishara ya kukubali madaraka ya kuwa mkuu wa majeshi yaliyopo nchini Iraq, huku aaliyekuwa amiri jeshi mkuu wa zamani Gen, David Petreaus na kulia ni waziri wa ulinzi wa Amerika bwana Robert Gates.
Picha ya kati anaonekana, Gen, Ray Odierno akiwa na rais, Geogre Bush, wakati walipo onana hivi karibuni kwenye ikulu ya Amerika.
Chini wanaonekana maamiri jeshi, David Petreaus na Ray Odierno wakipeana mkono mara, baada ya kumaliza kukabidhiana madaraka.
Vita dhidi ugaidi bado, maelfu wakumbuka siku ya Sept 9/11.
New York,Amerika-11/09/08.Siku ya tarehe 11/09/, ya kila mwaka, wananchi wa Amerika huwa wanakumbuka watu waliopoteza maisha yao kutokana mashambulizi yanayo sadikiwa yalifanywa na kundi la Alqaeda.
Katika tukio hilo zaidi ya watu wapatao 2,900 walipoteza maisha yao na wengi kujeruhiwa vibaya.
Mashambulizi hayo yaliustua ulimwengu mzima, na katika hotuba yake rais wa Amerika, alisema ya kuwa vita dhidi ya magaidi bado, na inabidi wananchi kwa kushirikiana na serikali ili kushinda vita hivi.
Picha hapo juu ina onyesha majengo yakiwa yameshika moto mara baada ya kushambuliwa na magaidi.
Picha ya pili ni sehemu ya mabaki ya eneo ambapo majengo hayo yalikuwa yamejengwa yakiwa yametundikwa bendera ya taifa la Amerika wakati wamaombelezo hivi karibuni.
Picha ya tatu ni maua yakiwa yanaelea, baada ya waombelezaji kutoa heshima zao kwa watu waliopoteza maisha yao katika mashambulizi ya kigaidi.

Friday, September 12, 2008

Putin aonya nchi za Ulaya Magharibi, kukubali Amerika kuweka mitambo yake ya kivita.

Moto wasababisha usafiri kuwa mgumu kwa wakazi wa Ulaya watumiao daraja.

Paris,Ufaransa-11/09/08.Daraja linalo unganisha Ufaransa na Uingereza ambalo linapita chini ya maji lime ungua na moto kutokana na moja ya magari yanayopita kwenye daraja hilo kulipuka na kusababisha moto.
Kampuni inayo shughulikia daraja hilo, (Eurotunnel's) lilisema yakuwa daraja hilo limeungua kiasi cha maili 7 za urefu na bado wanaendelea na uchunguzi.
Kufuatia moto huo,daraja limefungwa mpaka hapo litakapo fanyiwamatengenezo upya, alisema mmoja ya viongozi wanao simamia daraja hili.
Picha hapo juu wanaonekana wafanyakazi wanaoshughulikia kuzima moto wakiwa wanajadiliana jinsi gani ya kukabiliana na moto huo.
Chini ni msururu wa magari ambayo yamekwam, baada ya daraja kuungua na kuzuia usafiri katika eno hili.
Putin, aonya nchi za Ulaya Magharibi, kukubali Amerika kuweka mitambo yake ya kivita.
Moscow,Russia-11/09/08-Aliyekuwa rais wa Urusi na sasa ni waziri mkuu wa nchi, Vladimir Putin ,ameonya yakuwa nchi za jumuia ya Ulaya zishiruhusu mitambo ya kijeshi kutoka Amerika kuwekwa katika nchi zake.
Bwana, Putin aliyaongea haya, wakati alipo kutana na waandishi wahabari katika maeneo ya Bahari Nyeusi.
Alisistiza kwa kusema ya kuwa nchi za Ulaya magharibi na Amerika zimekuwa zikilaumu na kuchafua Urusi, kwa kudai ya kuwa Urusi ina fanya mambo yake kwa kufuata njia za zamani za enzi za vita baridi kati ya NATO na Rusia(USSR).
Nchi ambazo, alizizungumzia, ni Poland na Czech, nchi ambazo zimekuwa zinampango wa kuruhusu mitambo ya kijeshi kuwekwa katika nchi zake na Amerika.
Picha hapo juu ni bendera ya Jumuia ya Ulaya, ambapo nchi za jumuia wanachama zinadaiwa yakuwa zisiruhusu Amerika kuweka mitambo yake ya kijeshi.
Picha ya pili ni ya waziri mkuu wa Urusi, Vladimir Putin akionga mapema na wandishi wahabari, alipo kutana noa kuzungumzia hali halisi ya Urusi kuhusu siasa na uchumi kwenye jumuia ya kimataifa.

Wednesday, September 10, 2008

Urusi ya aidi kutoa majeshi yake nchini Georgia" Yataka vikwazo zidi ya Georgia"

Waziri mkuu apoteza kibarua cha uongozi wa nchi "Chaota majani" , kazi ya zamani yawa chanzo".

Bengkok, Thailand-10/09/08.Aliyekuwa waziri mkuu wa Thailand, Samak Sundaravej, amefukuzwa kazi na hakama ya katiba.
Uamuzi huu umekuja baada ya kuonekana ya kuwa bwana, Samak Sundaravej, amekiuka miko ya kuwa kiongozi wa serikali na wakati huo huo ana fanya kazi na kampuni binafsi.
Kufukuzwa huko kwa bwana Sundaravej, kuendela kufanya maonyasho ya mapishi katika runinga.
Kabla ya kuwa waziri mkuu , bwana Sundaravej, alikuwa anajulikana saana hasa ka kipindi chake cha mapishi katika runinga za nchini Thailand.
Picha hapo juu anaonekana bwana, Samak Sundaravej, akisalimiana na wapenzi na wanachama wake mara baada ya kuchaguliwa kuwa zaziri mkuu wa Thailand.
Picha ya pili, anonekana bwana Samak Sundaravej, akinunu anyama tayari kwa maandalizi ya mapishi ambayo huonyeshwa kwenya runinga nchini Thailand.
Urusi ya aidi kutoa majeshi yake nchini Georgia," Yataka vikwazo zidi ya Georgia".
Moscow ,Urusi-09/09/08. Serikali ya Urusi imesema itataoa majeshi yake nchini Georgia, baada ya kukutana na viongozi wa jumuia ya Ulaya.
Ujumbe huu wa Jumuia ya Ulaya, uliongozwa na rais wa Ufaransa , Nicolas Sarkozy pamoja na Jose Manuel Baros, ulikutana na uongozi wa Urusi, ukiongozwa na rais wa Urusi, Dmitry Medvedev mjini Moscow.
Wakati huo huo Urusi imepeleka mswada kwenye kamati ya usalama ya umoja wa mataifa ya kuwa serikali ya Georgia iwekewe vikwazo vya kuuziwa siraha, lakini hata hivyo, serikali ya Amerika imepinga mswada huo na kudai ya kuwa ni mbinu za Urusi za kutaka kuamisha hoja ya kutaka kutoa majeshi nchini Georgia.
Picha hapo juu wanaonekan rais wa Urusi Dmitry Medvedev akisalimiana na rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy, wakati walipo kutana mjini Moscow kujadili hali ya Georgia.
Chini ni vinaonekan vifaru vya Urusi, vikiwa ninapiga doria kwa ajili ya usalama wa raia wake.
Kundi la Alqaeda la zishambuaria kwa maneno baadhi ya nchi"Ikiwemo Iran".
Tehran, Iran-08/09/08. Kiongozi msaidizi wa kundi la Alqaeda bwana Ayaman al Zawahiri, ameonekana kupitia mikanda ya video iliyopatikana kupitia vyombo habari na kuonya na kulaumu dhidi ya baadhi ya serikali ambazo zinashirikiana na Amerika kupambana na kundi lake.
Nchi ambazo zilitajwa ni pamoja na Iran na Lebanese Afganistani na Pakistani.
Katika video hii , Al Zawahiri, aliilaumu Iran kwa kushiriki katika kuhiruhusu Amerika kuishambulia Afganistan na Irak.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Iran, nchi ambayo inadaiwa na kushirikiana na Amerika kwa njia moja au nyingine.
Picha ya pili ni ya Ayan al Zawahiri, akiongea kwenya video hivi karibuni.
Korea ya Kaskazini yadai ya kuwa kiongozi wao yupo mzima.
Pyongyang,Korea ya Kaskazini-10/09/08. Serikali ya Korae ya Kaskazini imetangaza yakuwa Kiongozi wa nchi yao bwana, Kim Jong II ya kuwa anaumwa ugonjwa wa kupooza, siyo ya kweli.
Kiongozi msaidizi wa nchi hiyo bwana, Yong Nam, alisema ya kuwa habari ya kuugua kwa kiongozi wao ni wa uzushi mtupu japokuwa hakueleza ni kwanini kiongozi huyo hakuudhulia sherehe hiyo..
Habari hizi zili kuja baada ya Kim Jong II, kushindwa kuudhulia maazimisho ya miaaka 60 ya kutengana kwa Korea moja, na kuwa Korea ya kusini na Korea ya Kaskazini.
Picha hapo juu ni ya kiongozi wa Korea ya Kaskazini bwana, Kim Jong II,ambaye inasadikiwa anamatatizo ya kiafya.
Chini ni picha ya baadhi ya viongozi wa Korea ya Kaskazini, wakiwa wanashangilia wakati gwaride la askari walinzi wa nchi walipo pita mbele yao siku ya 09/09/08 mjini Pyongyang.

Saturday, September 6, 2008

Rais wa Bolivia atembelea Iran.

Afrika ya Kusini na Venezuela za endeleza huusiano"Watiliana mkataba wa kimaendeleo" Pretoria,Afrika ya Kusini-2/09/08.Serikali ya Afrika ya Kusini na serikali ya Venezuela, zimetiliana sahii mkataba wa kiushirikiano katika nyanja za kiuchumi na viwanda na hasa mafuta na gesi. Mkataba huu ulisainiwa wakati rais, Hugo Charvez, alipo tembelea nchini Afrika ya Kusini, Rais, Charvez, alitoa mwanya kwa wananchi wa Afrika ya Kusini kuweka vitega uchumi nchini Venezuela. Picha hapo juu, wanaonekana rais, Thabo Mbeki na Hugo Charvez ,wakielekea kwenye ofisi za Ikulu ya serikali ya Afrika ya Kusini mjini Pretoria, mara baada ya rais Charvez alipo wasili nchini Afrika ya Kusini.

Angola yaingia katika sura mpya ya kidemokrasi, waaanza uchaguzi leo.
Luanda, Angola,6/09/08-Wananchi wa Angola wanaanza kupiga kura leo.
Uchaguzi huu utakuwa ni wa kihistoria kwa kipindi kisicho pungua miaka 16 iliyo pita.
Kwa mujibu wa wasemaji wa na wasimamizi wa uchaguzi, wamesema ya kuwa kumekuwa na utata katika siku za mwanzo za uchaguzi.
Hata hivyo inasadikiwa chama tawala cha MPLA huenda kikashinda dhidi ya vyama vaya upinzani vikiongozwa na chama cha UNITA.
Picha ya kwanza kina mama wakishangilia katika kampeni za uchaguzi hivi karibuni.
Juu ni picha ya bendera ya Angola nchi ambayo wanachi wake wanapiga kura kumchagua rais wa nchi yao.
Rais wa Bolivia atambelea Iran.
Tehran,Iran- 2/09/08. Rais wa Bolivia Evo Morales, alifanya ziara ya kiserikali nchini Iran siku ya jumatatu.
Katika ziara hiyo rais Evo Morales,alikutana na rais wa wa Iran Mahamoud Ahamadinejadna kujadili mbinu za kudumisha uhusiano wao. Rais, Evo Morales, aliwasili nchini Iran akitokea nchini Libya.
Picha hapo juu ni ya marais wawilli walipo kutana hivi karibuni nchini Iran, kulia ni rais wa Iran Mahmoud Ahamadinejad na kushoto ni rais wa Bolivia Evo Morales.
China na Iraki zaingia mkataba wa karne tangu kuangushwa kwa serikali ya Saddam Hussein.
Baghdad, Iraki-30/08/08.Serikali ya Iraki imetiliana mkataba na serikali ya China tangu kuangushwa kwa serikali ya Saddam Hussein.
Mkataba huo wenye thamani ya $ 3 billion utawezesha makampuni kutoka China kuanza kuchimba mafuta na kutoa misaada ya kiufundi kwa ushirikiano na serikali ya Iraki.
Kwa mujibu wa wataalamu wa mafuta wanasema yakuwa Iraki, inauwezo wa kutoa mapipa ya mafuta 2.5 million.
Picha hapo juu ni ya sehemu moja ambapo mafuta yatachimbwa kwa ushirikiano wa serikali ya China na serikali ya Iraki
Kutokukubaliaana kimsingi''serikali ya ya Korea ya Kaskazini ya anza upya ujenzi wa mitambo ya Nuklia".
Yongbyon,Korea Kaskazini- 3/09/08. Serikali ya Korea ya Kaskazini, imeanza upya kujenga mitambo yake ya nuklia, baada ya kusimamisha kwa muda mpango wake.
Kuanza kwa ujenzi huu kumekuja baada ya serikali ya Kora ya Kaskazini kudai ya kuwa serikali ya Amerika imeshindwa kuifuta Korea ya Kaskazini ya kuwa ni moja ya nchi zinazo shirikiana na makundi ya kigaidi yanayo daiwa kutishia amani duniani.
Picha hapo juu ni ya moja ya majengo ambayo mitambo ya nuklia ilikuwamo, ilipo bomolewa kipindi cha siku za nyuma.