Wednesday, July 30, 2008

Idadi ya vifo vinavyosababishwa na ugonjwa wa ukimwi duniani wapungua"Umoja wa mataifa"

Mkutano wa Kiuchumi wavunjika Geneva"Pigo kwa uchumi wa dunia OXFAM " Doa yawa ndoto"

Geneva , Uswis - 30/07/08. Mazungumzo ya kuletaunafuu katika biashara na kilimo yaliyo kuwa yakifanyika Geneva yamevunjika baada ya nchi za, Amerika, China na India kutofikia maafikiano na kuzika mandhumuni ya mkutano wa Doa,Katar,liofanyika miaka saba iliyo pita.
Kwa mujibu wa mkurugenzi mkuu wa WTO - World Trade Organisation, bwana Pascal Lamy, alisema nchi hizi zimeshindwa kufikia maafikano na hivyo kusababisha mkutano kuvunjika bila kuwa na mafanikio.
Hata hivyo, bwana Pascal Lemy, alisema kuvunjika kwa mkutano huo, siyo kusikatishe tamaa, kwani bado kuna matumaini ya hapo baadaye nchi hizi zikifafika makubaliano.
Kufuatia kuvunjika kwa mkutano huo, kamishna wa biashara wa jumuia ya Ulaya, bwana Peter Mendelson, amesema kuvunjika kwa mkutano huu kumeleta uchungu,na hasa katika kuinua uchumi wa dunia.
Naye mkurugenzi wa OXFAM International, bwana Jeremy Hobbs, alisema hii ni pigo kwa dunia na inasikitisha kwani, kuvunjika kwa mkutano huu , kumekuja wakati chakula na mafuta vinazidi kupanda bei na italeta hali mbaya ya kiuchumi duniani.
Kuvunjika kwa mkutano huu, kumeonyesha ni jinsi gani nchi tajiri na masikini duniani, zinavyo vutana katika maswala ya kimaslahi, alisema mmoja wa wajumbe walioudhulia mkutano huu.
Picha hapo juu anaonekana mkurugenzi mkuu wa WTO,bwana,Pascal Lamy akiwa ahamini yakuwa mkutano umevunjika bila kuleta mafanikio ya kiuchimi kwa dunia.
Chini ni picha ya anaonekan mmoja ya wakulima wa nchi za dunia ya tatu, akilima kishamba chake, tayari kuuza mazo ili apate pesa, lakini kudumu kwa kilimo chake kunategemea saana mikutano kama huu ulio vunjika,ambapo angepata nafuu ya pembejeo na soko la kuuza bidhaa zake.
Picha ya mwisho mwanaonekan majumbe, walioudhulia mkutano mjini Geneva, wengine wamesimama na wengine wamekaa , na kuashiria ya kuwa hali katika mkutano huu , mambo yalikuwa ya vuta ni kuvute.
Idadi ya vifo vinavyo sababishwa na ugonjwa wa ukimwi duniani wapungua"Umoja wamataifa ".
Umoja wa mataifa, New York - 30/07/08. Umoja wa mataifa umesema vifo vinavyo sababishwa na ugonjwa wa ukimwi vimekuwa vichache kulinganisha miaka ishirini iliyo pita.
Ripoti hii ilitolewa katika mkutano wake wa mwaka, ambao ulikuwa ukitathmini hali halisi ya ugonjwa huu wa ukimwi, na jinsi ya kuukabilina nao tangu ulipo anzaa kuongezeka mapema miaaka ya 1990.
Hata hivyo, Umoja wamatifa , umeziagiza serikali kuzidi kupupambana na ugojwa huu kwa kuwekwa fungu la fedha za kutosha ili kuokoa maisha ya watu wengi.
Ofisi zinazo shughulika kupambana na ugonjwa wa ukimwi, zilizopo nchini Uswis -Geneva, zimesema yakuwa idadi ya vifo vya wagonjwa wa ukimwi vimepungua hadi kupunga kwa kiasi cha 200,000, kulnganisha miaka mitatu iliyo pita.
Kwa mujibu wa mkurugenzi mkuu wa (NAids), Peter Piot,alisema yakuwa hadi hivi sasa kuna watu wapatao million 33 duniani ambao wanaishi na virusi ya ukimwi.
Akiongezea kusema , mkurugenzi huyu Piet Pot, alisema yakuwa tangu 2007 , watu wapatao million 3 wanatumia vidonge , kulinganisha na mwaka 2003, na hii inatokana na madawa kwa rais kupatikana na kuuzwa kwa bei nafuu.
Picha hapo juu ni picha ya virus vya ukimwi ambavyo uhathili aafya ya mtu,pindipo vinapo ingia ndani ya mwili na hasa ukiwa huja pata matibabu au kuanza kutumia madawa na kula lishe bora.
Picha ya pili ni picha alama ya Ukimwi (AIDS) ikiwa imechorwa katika moja ya ofisi zinazo shughulika Ugonjwa huu.
Hali ya usalama nchini Irak bado ya kusuasua" Wengi wajeruhiwa ".
Bagdad, Irak -28/07/08. Watu wapao 28 wamepoteza maisha yao na wengine 92 kijeruhiwa vibaya, wakati wanawake watatu walipo jilipua katika kadamnasi ya watu waliokuja kuhiji kushereheka siku ya kidini ya watu wenye madhehebu ya Kishia.
Kwa mujibu wa masemaji wa serikali alisema yakuwa wanawake hawa walikuwa katika kundi la mahujaji na walipo jililipua walisabisha maafa makubwa ya watu kupoteza maisha na kujeruhi watu wengi.
Picha hapo juu, anaonekan mmoj wa wanajeshi wa Amerika akiwa kazini kulinda usalama wa raia wa Irak.
Picha yapili anaonekana mzee wa Kiirak, akiangalia kwa uchungu miili ya watoto wadogo, waliopoteza maisha yao, baada ya mabomu kulipuka na kisababisha maafa makubwa katika jamii ya Wairak.
Picha ya tatu anaonekana raia mmoja wa Irak , akiwa anaondoka kwenye eneo ambalo limetoke mlipuko huku akiwa anamajeruha kwenye uso wake na damu zikimtoka wakati akitembea.
Polisi wa Irak, wanaonekana wakijaribu kuashiria kuomba msaada kuzimisha moto ambao umesababishwa na mlipuko wa wabomu.
Uchimbaji wa mafuta Niger Delta hali ni ngumu"MEND wadai watendelea na uharibifu".
Niger Delta , Nigeria - 28/07/08. Kukundi kinajulikana kam( MEND au Movement for Emancipation of the Niger Delta), kimedai yakuwa kimeharibu mitambo na mabomba ya kupitishia mafuta ya nayo milikiwa na kampuni ya Shell.
Kikundi hicho kilitoa maelezo hayo kwa kupitia barua pepe na kudai kitaendelea na mashambulizi yake ikiwa akitapatiwa mahitaji yake kutoke serikalini.
Kampuni ya shell, ilianza kuchimba na kusafirisha mafuta katika kitongoji cha Bonga mwaka 2205, hadi kufikia 2007 zaidim ya mapipa million 100 yalikuwa yamesha safilishwa kutoka eneo hili, ambali lipo km 120 kwenye maeneo ya ufukwe wa bahari.
Pia eneo hili lina gasi lenye ulefu wa kubic 150 millioni.
Pichani hapo juu ni wapiganaji wa kikundi cha MEND wakiwa ndani ya boti huku wakizunguka maeneo ambayo yana mafuta.
Picha pili ni ya boti inayo tumiwa na MEND.
Hatimaye bwana Radovan Karadzic awasili mjini Hague tayari kukabiliana na mashitaka yanayo amkabili" Hataki kuwakilishwa na mwana sheria".
Hague, Uhollanzi - 30/07/08. Aliyekuwa kiongozi wa Bosnia - Serbia, bwana Radovan Karadzic, amewasilishwa leo nchini Uhollanzi tayari kwa kukabiliana na mashitaka yanayo mkabili dhidi yake.
Mashitaka hayo ambayo yanamkabili bwana,Radovan Karadzic, ni ya yale yanayoambatanishwa na vita vilivyotokea Bosnia mwaka 1992 - 1995, na ni kwanza tangu kumalizika vita vya pili ya dunia katika bara la Ulaya.
Kwa mujibu wa mwanasheria wa mahakama ya kimataifa ya mjini Hague,alisema yakuwa bwana, Radovana Karadizdic atafikishwa mahakamani hivi karibuni,ili kujibu mashitaka yanayo mkabili.
Mashitaka yanayo mkabili bwana Radovan Karadzic, ni ya mauaji ya ya zaidi ya watu 8,000 waumini wa dini ya Kiislaam katika kitongoji cha Srebrenika.
Hata hivyo, kwamujibu wamsemaji wa bwana, Radovan Karadzic,alisema yakuwa bwana Karadizic atajitetea peke yake na hataki kuwawakilishwa na mwana sheria yoyote katika kujibu mashitaka yake.
Pichani hapo juu anaonekana bwana Radovan Karadzic, enzi hizo alipo kuwa kiongozi wa Serbia , akiongea na baadhi ya viongozi wenzake.
Picha ya pili ni chumba ambacho, inasadikiwa bwana,Radovana Karadzic atakuwa anaishi wakati kesi yake ikiwa inaendelea.
Picha ya tatu wanaonekana polisi wakipambana na baadhi ya wananchi wa wapenzi mjini Bergedi, Yugoslavia wakiandamana kupinga kukamatwa na kupelekwa kwa bwana, Radovan Karadzic mjini Hague, tayari kusikiliza kesi zinazo mkabili dhidi yake.
Picha ya tatu, inaonekana helkopta iliyombebe bwana Radovan Karadzic ikitua ndani ya gereza mjini Hague,kwenye gereza hili ndimo bwana, Radovan Karadzic, atakaa kwa kipindi chote atakapo kuwa akisikiliza kesi yake.
Pichani anaonekana kaka ya bwana, Radovan Karadzic, akijitahidi bila mafanikio kuwasialiana na wanasheria na wana ndugu, iliwajaribu kuzuia kupelekwa kwa kaka yake nchini Uhollanzi kujibu mashitaka.

Monday, July 28, 2008

Uispania na Venezuela wasuruhisha mgogoro wao, na sasa kuganga ya jayoo.

Baraka Obama, hawa kuvutio cha wengi nchi za Ulaya "Matumaini yao atachaguliwa kuwa rais".

London , Uingereza - Mgombea kiti cha urais nchini Amerika kwa kupitia cham cha Demokratiki, bwana Baraka Obama, amemaliza ziara yake ya kutembelea nchi za Ulaya na nchi za Mashariki ya Kati.
Ziara hiyo aliyoifanya alitembela nchi za, Jordani, Israel, Ujerumani, Ufaransa na Uingereza.
Katika ziara zake hizo bwana Obama , alisisitiza uhusiano uliopo kati ya nchi za Ulaya na Amerika ni muhimu kudumishwa, na haukuna nchi inata kayoweza kutatua matatizo ya dunia peke yake.
Kufanyika kwa ziara hii ya bwana Baraka Obama, kuliwezesha wanchi na hasa wanachama wa chama cha demokratiki waishio nchi za Ulaya, kuweza kuhudhulia kwa wingi kwenye mikutano aliyo hutubia, huku wakiwa wameshikiria mabango yaliyo andikwa Baraka Obama awe rais.
Picha ya kwanza hapo juu anaonekana bwana Baraka Obama , akiwa anajiandaa kuwapungia mkono watu walio kuja kumsalimia kabla ya kuingia kwenye ofisi kuu ya serikali ya Uingereza iliyopo kwenye mtaa wa Dawning 10.
Picha ya pili, wanaonekana wananchi waliokuja kumlaki na kumsalimia, bwana Baraka Obama wakati wa ziara yake nchini Uingereza.
Picha ya tatu, anaonekana bwana Obama alipokuwa akiongea na waandishi wa habari, mara baada ya kumaliza kuongea na waziri mkuu wa Uingereza bwana, Gordon Brown.
Picha ya nne wanaonekana Baraka Obama wakiwa pamoja na waziri mku wa zamani wa Uingereza bwana Tony Brair, wakati walipo kutana wakati wa ziara hiyo ya Obama nchini Uingereza.
Picha ya tano , anaonekana,waziri mkuu wa Uingereza bwana ,Gordon Brown akimwonyesha Baraka Obama, mazingira ya yaliyo izungu ofisi yake.
Picha ya sita anaonekana, Baraka Obama akiongea na waandishi wa habari wakati alipo kuwa nchini Ufaransa, kulia ni rais wa Ufaransa, Nicolaus Sarkozi.
Picha ya sita unaonekana umati wa watu wapato 2,00,000 waliokuja kusikiliza hotuba ya Baraka Obama, wakati alipokuwa ziarani nchini Ujerumani.
Chini mwisho wanaonekana, Kansera Angela Merkel akiwa na Baraka Obama, wakati wa ziara ya Obama nchini Ujerumani.
Idadi ya watu yazidi pungua nchini Swaziland" Wakina mama ndiyo hatarini"Umoja wa mataifa .
Mbabane,Swaziland -Ofisi za Umoja wa mataifa nchini Swaziland, imesema ya kuwa ya idadi ya watu inazidi pungua nchini Swaziland kutokana ma vifo vinavyo ambatana na ugonjwa wa ukimwi.
Ripoti hii ilitolewa hivi karibuni ilisisitiziwa na bi Aisha Kamara, ambaye ni mwakikilishi wa Umoja wa mataifa,alisema ya kuwa vifo vingi vinatokea hasa kwa kina mama na watoto, kwani ofisi inayo shughulikia idadi ya watu,iliseama wanawake 500,wanafariki dunia kati ya 1000 kwa mwaka kutokana na magojwa yanayo husiana ukimwi.
Kufuatia hali hiyo serikali ya Swaziland imetenga mfuko maalumu kwa ajili ya kupambana ha hali hii, haya yaliongelewa na waziri wa uchumi ,mipango na maendeleo Absolom Dlamini
Pichani ya kwanza hapo juu, anaonekana Mfalme Mswati kushoto,akiwa anasherekea siku muhimu y kihistoria ya nchi yake.
Picha ya pili, wanaonekana , wasichana wakiungana kwa pamoja kushereheka siku ya kihistoria ya nchi yao.
Picha ya tatu, wanaonekana wazee wa Kiswazilnd wamevalia mavazi ya kiasili, wakiwa wamekaa chini, baada ya kumalizika sherehe ya kihistoria ya nchi yao .
Picha ya nne, inaonesha mandhali nzuri ya asili nchini Swaziland, ambayo inasadikiwa wakazi wake wengi wanawakati mgumu wa kupambana na gojwa hatari la Ukimwi.
Picha ya mwisho ni bendera ya ya Swaziland, nchi ambayo mfalme ni kiongozi muhimu katika jamii nzima.
Uispania na Venezuela, wasuruhisha mgogoro wao, na sasa kuganga ya jayoo.
Madrid, Uispania - Rais wa Venezuela, Hugo Charvez, amekutana na wakuu wa serikali ya Uispania na kumtembelea mfame wa Uispania, mafalme Juan Carlos.
Ziara hii ya rais Charvez, ilikuwa ya kiserikali na kuimarisha uhusiano uliotetereka miezi ya nyuma, baada ya mfalme wa Uispania kufokeana na rais Charvez wakati walipo udhulia mkutano pamoja mapema mwaka jana.
Katika ziara yake hiyo ,rais Charvez aliweza kutaniana na mfalme Juan Carlos,kwa kumkaribisha waende ufukweni mwa pwani wakatembee kwani kulikuwa na hali ya joto saana.
Picha ya juu ni ben dera ya Venezuela nchi ambayo hapo zamani ilikuwa kolono la Uispania.
Picha ya kati wanaonekana rais Hugo Charvez kushoto, na mfalme Juan Carlos kulia wakikumbatiana na kuongea kuyamaliza yaliyo pita na kuganga ya jayo.
Picha ya chini ni bendera ya Uispania, nchi ambayo ilitawala Venezuela kwa muda mrefu.
Jiji la Istanbul, lipo katika mshituko mkubwa"Magaidi watega mabumu na kuuwa na kujeruhi wengi"
Istanbul,Uturuki - Watu wapatao 27 wamefariki dunia na kujeruhi wengini 150 ,baada ya mabomu kulipuka katika nyakati tofauti kwenye kitongiji kimoj mmoja jiji Istanbul .
Kwa mujibu wa mshihidi waliona tukio hilo,alisema ya kuwa mlipuko wa kwanza ulitokea na na baadaye ulifuatia mlipuko wa pili mkubwa na kusababisha vifo hivyo na majeruhi wengi.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, alisema yakuwa milipuko hiyo ilipishana kiasi cha madakika kwani inasadikiwa mabomu hayo yalikuwa yamewekwa kwenye mifuko ya taka-yakuwekea uchafu na alongeaza huenda maafa ya kaongezeka kwani kuna watu wengine bado hali zao siyo nzuri.
Kufuatia mlipuko huo, waziri mkuu wa Uturuki, bwana Tayyip Erdogan, alisema yakuwa milipuko ya mabomu ni ugaidi wa hali ya juu , nakuhaidi ya kuwa ,Waturuki, aita tetereka kwani wamekuwa wakipigana na ugaidi zaidi ya miaka 30, watapigana hadi kushinda.
Waziri huyo, pia aliongeza kwa kusema ugaidi hauna dini, hakuna dini inayo ruhusu ukaidi, na dini ya Kislaam hataruhusu Magaidi kutumia Uislamu kama njia ya kutekeleza ugaidi wao.
Picha hapo juu anaonekana, waziri mkuu wa Uturuki, bwana Tayyip Erdogan,wakati alipo tembelea maeneo ambayo mabumu yalilipuka na kusababisha maafa makubwa kwa kupoteza maisha ya watu.
Picha ya pili, wanaonekan wahudumu wa huduma ya kwanza, wakimpakiza mmoja ya watu walioumia kutokana na milipuko ya mabomu.
Picha ya tatu, wanaonekana raia wakimsaidia mmoja ya jamaa ya ambaye amelala chini huku damu zikimtoka, baada ya kujeruhiwa na mmoja ya milipuko ya mabomu yaliyo tokea katika kitongiji cha jiji la Istanbul.
Abiria wa tua salama"Tanki la gesi la Oksigeni ndiyo chanzo?"Uchunguzi bado unaendelea.
Manila, Phillipienzi - Ndege ya shilika la ndege Qantas, boeing 747, imeponea chupu chupu na kutua salama baada sehemu moja ya ndege hiyo kubomoka na kudondoka wakati ndege hiyo ilipo kuwa hewani kuelekea Australia.
Kufuatia tukio hilo, ndege hiyo ilibidi itue kwa dharula mjini Manila.
Hata hivyo wachunguzi wa maswala ya ndege wamesema, bado wanachunguza ni kwanini tukio hili lilitokea kwa kusababishwa na tanki dogo lenye hewa ya Oksigeni ambalo linasadikiwa lilidondoka wakati ndege hiyo ikiwa hewani.
Picha hapo juu ni picha ya ndege,ambayo inaonekana ikiwa na tundu kubwa ambalo lina onekana kwa chini ya ndege.
Picha ya chini wanaoneka wapendanao amabo walikuwa moja wa abiria waliokuwemo kwenye ndege boeing 747, ambayo ilitua kwa dharula mjini Manila, baada ya kumegeka katika moja ya sehemu ya ndege hiyo.
Chama cha Labour chapoteza kiti kingine"Waziri mkuu Gordon Brown anawakati mgumu".
London,Uingereza - Waziri mkuu wa Uingereza bwana, Gordon Brown amekuwa katika hali ngumu kisiasa nchini Uingereza baada ya chama chake cha Labour kushindwa vibaya katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni katika mji wa Glasgow Mashariki.
Kufuatia kushindwa kwa chama cha Labour ,mjini Glasgow kunaongezea idadi ya kuzidi kushindwa kwa chama hiki Labour kumekuwa ni mara ya tatu katika kwenye jimbo ka Scotland.
Hata hivyo chama cha Labour, kimekanusha yakuwa hakitaitisha uchaguzi wala kubadili uongozi wa juu wa kiserikali ambao unaongozwa na bwana Gordon Brown, na kufutilia mbali maoni na madai ya chama cha upinzani kinachoongozwa na bwana , David Camerron .
Kushindwa kwa chama cha Labour, kuna mweka waziri mkuu bwana, Gordon Brown kuwa na wakati mgumu kisiasa.
Picha hapo juu anaonekana akihutubia hivi karibuni katika moja ya mikutano nchini Uingereza.
Picha ya chini anaonekana, waziri mkuu wa Uingereza bwana, Gordon Brown akiwa anasikiliza moja ya maswali kutoka kwa waandishi wa habari.

Tuesday, July 22, 2008

Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini atolewa katika majina ya magaidi" Yupo huru kuingia Amerika"

Makelele asema sasa Uingereza basi"Arudi nyumbani".

Paris, Ufaransa - Mchezaji mairi na nyota wa timu ya taifa ya Ufaransa Claude Makelele, ametia saini mkataba wa kuchezea timu ya Paris ST Germain siku ya jumatatu 21/07/2008.
Hata hivyo makubaliano ya mkataba huo hayakuelezwa na vingozi wa timu PSG.
Hata hivyo kwa muujibu wa meneja wa Makelele, alisema nia ya Claude ni kucheza maika mingine miwili zaidi kabla ya kutundika madaruga juu.
Akiongea, Makelele alisema ya kuwa atajitahidi kadri ya uwezo wake kuweza kufanya kazi yake kama alivyo siku zote awapo kazini - Uwanjani.
Makelele mwenye miak 35, ambaye amechezea timu kubwa na maarufu duniani kama, Rael Madrid na Chelsea , alisema ni furaha kubwa kuja kuchezea timu ya Pars St Germain.
Picha ya hapo juu anaonekana Claude Makelele awapo kazini hana masihara, hata mkija wangapi ata shinda tu.
Picha ya pili anaonekana Makelele, akikokota kandanda huku mmoja ya wa chezaji wa timu ya Arsenal akijaribu bila mafaniko kumnyanganya kandanda hio .
Chini anaonekan Claude Makelele akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni wakati timu ya taifa ya Ufaransa ilipo kuwa ikijianda na kombe la mabingwa wa Ulaya.
Mmoja wa mtuhumiwa wa kesi ya mauaji ya alaiki akamatwa.
Serbia, Bosnia - Mmoja wa viongozi walioshukiwa kuhusika na mauaji ya watu wa Sarajevo na Serbia, ambaye alikuwa ni rais, wa Bosnia Radovan Karadzic amekamatwa siku ya 18/07/2008 ijumaa wiki ikiyo pita, kwa mujibu wa msemaji wa serikali.
Karadzic mwenye miaka 63, ashutumiwa kwa kutoa amri ya mauaji ya watu wasiopungua 8000, waumini wa dini ya kislaam katika kitongoji cha Srebrenica.
Kukamatwa kwa bwana Radovan Karadzic, kulitokea mnamo majira ya tatu na nusu usiku 21:30.
Hata hivyo bwana Radovan Karadzic, anatarajiwa kufikishwa mahakamani na baadaye huenda akapelekwa mjini Hague Uholanzi kujibu mashitaka ya nayao mkabili ya kivita na kuhusika na mauaji.
Pichani hapo juu anaonekana bwana, Radovan Karadzic wakati alipo kuwa raisi wa Bosnia, akionyesha maeneo fulani kwenywe ramani.
Picha ya pili wanaonekana baadhi ya wakaazi wa Sarajevo wakishangilia kukamatwa kwa bwana Radovan Karadzic.
Picha ya mwisho anaonekana, Radovan Karadzic kulia akiwa amefuga ndevu ambazo zilimsaidia kutojulikana kwa muda mrefu hadi alipo kamtwa hivi karibuni na picha ya kushoto anaonekana Radovan Karadzic kabla ya kufuga ndevu wakati huo alipo kuwa kiongozi wanchi..
Biashara ya umalaya yaleta kitendawili ''Viongozi wavutana"Afrika ya Kusini
Durban, Afrika ya Kusini -Serikali ya Afrika ya Kusini huenda ikaidhinisha biaashara ya umalaya wakati wa mashindano ya kugombania kutafuta bingwa wa soka wa kombe la dunia litakalo fanyka 2010 chini Afrika ya Kusini.
Kwa mujibu wa msemaji wa hamashauri ya jiji la Durban, alisema yakuwa wanajdili na serikali ni jinsi gani watashrikiana, hasa katika majumba ya starehe na maeneo mengine ya jiji la Durban.
Hata hivyo viongozi wa kidini jijini humo, wanapinga mpango huu kwani unakwenda kinyume na maadili ya dini na huenda ukawa wakudumu.
Picha hapo juu ni za baadhi ya watu ambao huwa wanafanya bishara ya umalaya nchini Afrika ya Kusini.
Raia wa Kipalestina aendesha gari aina ya katapilla na kujeruhi wengi.
Jerusalemu, Izrael - Dereva mmoja wa katapilla ambaye ana asili ya kiarabu ameuawawa na polisi nchini Izrael kwa kuliendesha gari aina ya katapilla kwa kwa fujo na kuanza kugonga magari na basi siku ya jumanne 22/07/208.
Dereva huyo amesababisha ajali kwa watu wasiopungua 20.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, tukio kama hili ni la pili kutokea katika mazingira tofauti.
Polisi wamesema ya kuwa dereva huyo, ambaye alijulikana kama Ghassan Abu Teir, ambaye ni raia wa kipalestina ambaye alikuwa anaishi mjini Jerusalem.
Rais wa zamani wa Afrika ya Kusini atolewa katika majina ya magaidi."Yupo huru kuingia Amerika".
Washington, Amerika - Rais, George Bush hivi karibuni ametia sahii ya kutaka rais wazamani wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela kufutwa na kuondolewa katika majina ya watu wanajulikana kama magaidi.
Kufutwa kwa rais wazamani wa Afrika ya Kusini katika majina ya watu wanaojulikana kama magaidi kutamwezesha bwana, Nelson Mandela kutembelea Amerika bila kupata ruhusa ya ofisi kutoka ofisi ya mambo ya nje ya nchi ya Amerika.
Kuwekwa kwa jina la rais wa zamani wa Afrika ya Kusini, kulikuja baada ya chama cha kutete haki za wengi nchini Afrika ya Kusini ANC, wakati wanachama na viongozi wa chama hiki walipokuwa wanapinga ubaguzi wa rangi nchini Afrika ya Kusini dhidi ya makaburu.
Picha ya hapo juu wanonekana rais wa zamani wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela na mke
wake bi Winnie wakati Nelson Mandela alipokuwa anawasalimia wanchi kwa mara ya kwanza mara baada ya kuachiwa huru kutoka jela, ambapo alitumikia kifungo cha miaka 27 kwa ajil;i ya kupinga ubaguzi warangi nchini Afrika ya Kusini.
Picha ya chini anaonekana rais George Bush akiwa anaongea na waandishi wa habari.
Waachiwa baada ya kutumikia kifungo kwa kosa la kuwa na madawa ya kulevya.
Akkra, Ghana - Wasichana wawili raia wa Uingereza waliachiwa huru, baada ya kutumika kifungo cha miezi tisa kwa kosa la kutaka kupitisha madawa ya kulevya nchini Ghana kwa kutumia kichakato au (kompyuta) ndogo. Msemaji wa serikali, bwana John Allotey alisema yakuwa wasichana hawa waliachiwa huru na hakuweza kueleza kwa undani zaidi.
Wasichana hawa wakikamatwa kwenye kiwanja cha ndege cha jijini Akkra julai 2007 wakiwa na madawa aina ya kokeini kilo 6 ndani ya (michakato)- kompyuta zao.
Picha hapo juu ni picha ya moja ya madawa ya kulevya ambayo yamekuwa yakisadikiwa kupitia nchi nyingi za Afrika hasa nchi za Afrika ya Magharibi.
Washukiwa wa ugaidi uliyo fanyika nchini Uispania waachiwa huru.
Madrid,Spain - Mahakama kuu ya Uispainia imewachia huru hivi karibuni watu walioshukiwa kuhusika na ulipuaji wa kigaidi uliofanyaka nchini Uispania mwaka 2004, ambapo zaid ya watu wasiopungua 191 walipoteza maisha.
Watu hawa wanne, ni kati ya watu 21 ambao wakikamatwa kwa kushukiwa kuhusika na ugaidi huo.
Kuachiwa kwa watu hao kuliambatana na kuachiwa kwa Rabie Osman Sayed Ahmed ambaye alikuwa anashukiwa kuhusika na katika kusaidia ugaidi ambo ulipoteza maisha ya watu na kujeruhi watu wasiopungua 1,800.
Pichani hapo juu anaonekana bwana Ahamed wakati alipo kuwa ndani ya mahabusu ya mahaka kabla kusikia kesi yake.