Wednesday, March 31, 2010

Mahakama yataka kesi ifunguliwe upya zidi ya rais wa Pakistan.

Wauaji wa kujitolea muhanga watishia amani Urusi.

Moscow, Urusi - 31/03/09. Wauaji wa kujitolea muhanga wamejilipua na kuwauwa watu wapatao 12 akiwepo mkuuwa kituo kimoja cha usalama.
Mauaji hayo ambayo ni ya pili kwa siku mbili zinazo fuatana yameleta mshituko mkubwa nchini Urusi.
Milipuko miwili tofauti ambayo ilitokea katika mji wa Kizlyar imeleta wasiwasi mkubwa kwa wananchi wa maeneo hayo.
Waziri mkuu wa Urusi, Vladimir Putin alisema, " serikali itapambana na kundi ambalo linahusika na mauaji hayo bila kusita." Picha hapo juu wanaonekana rais wa Urusi, Dimirti Medved na waziri mkuu wa Urusi Vladimir Putin wakijadialiana kwa undani kuhusu usalama wa nchi.

Mahakama yataka kesi ifunguliwe upya zidi ya rais wa Pakistan.
Kabul, Pakistan - 31/03/09. Idara inayo shughulikia kukabiliana na rushwa nchini Pakistan, imeiagiza serikali Swisi kufungua kesi ya kuchunga rushwa zidi ya rais wa Pakistan.
Kesi hiyo zidi ya rais Asif Ali Zardari imeombwa kufunguliwa upya, kutokana na matumizi ya pesa zipatazo 13 million.
Uamuzi huo unakuja baada ya mahakama kuu kutoa kizuizi mwezi Desemba mwaka jana zidi ya rais.
Picha hapo juu, anaonekana rais Asif Ali Zardar ambaye tangu achukue kiti cha urais nchini Pakistan.

Friday, March 26, 2010

Kanisa Katoliki " Vyombo vya habari vinachafua jina la Kanisa."

Kanisa Katoliki "Vyombo vya habari vinanchafua jina la Kanisa." Vatican, Vatican City - 26/03/2010. Msaidi wa Papa Benedikt XVI amelaumu vyombo vya habari kwa kujaribu kuharibu jina na kuchafua Kanisa Katoliki na uongozi wake. Akiongea baada ya habari kutolewa ya kuwa Papa Benedict wakati akiwa Kadinali alifutilia mbali malalamiko yaliyoletwa ya kuwa baadhi ya mapadri walikuwa wananyanyasa waumini kijinsia "yanalengo la kuaribu Kanisa na uongozi wake." Kanisa Katoliki limekuwa na wakati mgumu baada ya waumini na wanafunzi waliosoma katika shule za Kanisa hilo kulalamika ya kuwa walinyanyaswa kijinsia wakati wakiwa masomoni katika shule hizo. Picha hpo juu anaonekana Papa Benedikt VXI, akiwasalimia waumini waliokuja kusali na kuomba Mungu kwa pamoja katika moja ya sikuku za Kikristu ndani ya la jiji Vatican. Nchi za Kiaarabu kuchanga pesa kuwasaidia Wapalestina. Sirte, Libya - 26/03/2010. Mawaziri wa mabo ya nchi za nje wa nchi za Kiarabu wamekubaliana kutoa na kuchangisha kiasi cha $500million kwaajili ya kuwasaidia Wapalestina wanao ishi Jerusalem. Mawaziri hao wanaokutana kabla ya mkutano mkuu wa wakuuwa nchi za Kiarabu, umesema "mchango huyo ni kwaajili ya kukabiliana na ujenzi ambao unaendelea katika eneo hilo la Jeruusalemu. Picha hapo juu wanaonekana mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za Kiaarabu wakiwa katika kikao katika mti wa Sitre. Iyad Alawi ashinda uchaguzi wa Irak.

Baghdad, Irak 26/03/2010. Kamati inyosimamia uchaguzi nchini Irak imetangaza chama cha Irakiya Coalition kimeshinda katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni.
Chama hicho kinacho ongozwa na aliyekuwa waziri mkuu wa zamani wa Irak, Ayad Allawi, kimepata viti 91 katika bunge la Irak na chama cha waziri mkuu wa sasa ANour al Malik kimeshinda viti 89.
Hata hivyo ili kuunda serikali Ayad Allawi, itambidi atafute chama shiriki jambo ambalo wataalamu wa siasa ya Irak wanasema " itabidi afanye kazi ya ziada, kwa kufuatia historia ya uongozi wake wa nyuma."
Picha hapo juu, anaonekana Ayad Allawi akiongea wakati wa kampeni za uchaguzi.

Tuesday, March 23, 2010

Baraka Obama atia saini muswada mpya wa bima ya afya kwa Waameika.

Baraka Obama atia saini muswada mpya bima ya afya kwa Waamerika.

Washington, Amerika - 23/03/2010. Rais wa Amerika amesaini muswada wa bima ya afya na kufanyiwa mabadiliko ambayo itawawezesha Waamerika wapatao million 32 watapata matibabu bila matatizo.
Rais Baraka Obama amesaini muswada huo kuwa sheria mbele ya baadhi ya wananchi na viongozi wa serikali.
Baraka Obama alisema " Nimesaini muswada kuwa sheria na afya ya kila mwananchi kila mwanchi wa Amerika itathaminiwa kwa usawa."
Picha hapo juu anaonekana rais Baraka Obama akisaini muswada wa wa bima ya afya kwa wote hivi karibuni.
Serikali ya Izrael kuendelea na ujenzi wake.
Washington, Amerika - 23/03/2010. Waziri mkuu wa Izrael ameliambia balaza la wa Izrael na Amerika ya kuwa serikali yake itaendelea na ujenzi wa nyumba na makazi kwa ajili ya watu wake.
Akiongea, waziri mkuu Benyamini Netanyahu alisema "kila mtu anajua, Amerika Ulaya na Wapalestina wanajua ya kuwa ujenzi wa makazi ni moja ya makubaliano ya kuleta amani." Na ujenzi wa Jerusalem ni sawa na ujenzi wa Telavivi, hivyo ujenzi hautazuia kuwepo kwa mataifa mawili ya Waizrael na Wapalestina."
Picha hao juu anaonekana, waziri mkuu wa Izrael Benyamin Netanyahu, akiongea na wajumbe wa AIPAC.
Uingereza ya mrudisha nyumbani balozi wa Izrael.
London, Uingereza - 23/03/2010 .Serikali ya Uingereza imemrudisha nyumbani mmoja wa balozi wa Izrael nchini Uingereza kutokana na mauaji ya kiongozi wa kundi la Hamas katika nchi za muungano wa nchi za Kiarau United Arab Emarate, (UAE).
Akiliambia bunge, waziri wa mambo ya nchi za nje David Miliband alisema "Tunayo sababu ya kuamini ya kuwa pasport za Uingereza zilitumika kusafiria kuingia na kutoka katika nchi za UAE."
"Kitendo hicho kimeishichia hadhi taifa."
Mvutano huo unakuja baada ya kuuwawa kwa kiiongozi wa HamasMahmoud al Mabhouh katika nchi za muungano wa Kiarabu na kuleta mgogoro wa kidlomasia.
Picha hapo juu ni ya waziri wa mambo ya nje wa Uingereza, ambaye ametangaza kurudishwa kwa balozi wa Izrael.

Monday, March 22, 2010

Serikali ya rais Obama ya weka historia.

Serikali ya rais Obama ya weka historia

Washington Amerika - 22/03/2010. Bunge la Amerika limepiga kura kukubali kuanzishwa kwa bima ya afya kwa wanchi wa Amerika, amabo wengi wao walikuwa wanishi bila kuwa na bima za afya.
Katika upigaji huo wa kura wabunge wa cham cah Demokrasi waliwashinda wabunge wa chama cha Republikan kwa kupiga kura zipatazo 219 kwa 212. Wabunge wapatao thelathin na nne wa
chama cha demokras walipinga mswada huo.
Kupita kwa kura hiyo, ambako kulikuwa kunaleta mvutano wa kisiasa kati ya vya hivyo viwili, kutamrahisishia rais Baraka Obama, kuendelea na shughuli nyingine za kitaifa na za kimataifa.
Rais Baraka Obama, anatarajiwa kusaini mswada huo wa bima ya afya kwa wote muda simrefu.
Picha hapo juu anonekana rais wa Amerika, Baraka Obama akiongea kuhusu swala zima la afya kwa wote, huku kushoto ni makamu wa rais Joe Biden akisikiliza kwa makini.
Picha ya pili wanaonekana waganga na wauguzi wakiwa mbele ya bunge kuunga mkono wa mswada wa bima ya afya kwa wote kabla ya kupigwa kura hiyo ya bima kwa wote.

Sunday, March 21, 2010

Waziri mkuu wa Irak ataka kura zihesabiwe upya.

Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa atemelea Gaza.

Gaza, Palestina - 21/03/2010. Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon amefanya ziara katika maeneo ambayo wanaishi Wapalestina hivi karibuni na kudai ni lazima kuwepo na matifa mawili kati ya Waizrael na Wapalestina. Akiongea, katibu huyo wa umoja wa mataifa alisema"kitendo cha Izrael kuzuia misaada kupelekwa kwa Wapalestina si cha haki, kwani kinasababisha maafa makubwa." "Umoja wa mataifa utafanya kila jitihada kuhakikisha wanchi wa Palestina wana kuwa na taifa lao" na kuagiza kuachiwa kwa askari wa Izrael Gilat Shilad aliyekamtwa mwaka 2006. Picha hpo juu anaonekana katibu mkuu wa umoja wa mataifa katikati akiwa anaangalia hali halisi ya Gaza na vitongoji vyake hivi karibuni. Ayatollah azilaumu nchi za Amerika na Izrael.
Tehran, Iran - 21/03/2010. Kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamemei
amezilaumu Amerika na Izrael kwa kutaka kuleta machafuko na kuondoa serikali ya Kiislaam ya nchi hiyo. Akiongea katika kusherekea sikukuu ya Nowruz, alisema " Iran ilikuwa katika hali ngumu hata watu kumwaga damu, kwa sababu ya upinzani uliokuwa ukisaidiwa na nchi hizo." Adui walitaka kuigawa nchi yetu na kutak kuleta vita, lakini taifa zima lilisima imara," aliongezea. Picha hao juu anaonekana kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, ndiye kiiongozi mkuu mwenye mwenye madaraka ya juu zaidi. Waziri mkuu wa Irak ataka kura kuhesabiwa upya.
Baghdad, Irak, 21/03/2010. Waziri mkuu wa Irak ameagiza kamati inayo shughulikia na kusimamia uchaguzi nchini Irak kuhesabu upya kura. Akiongea waziri mkuu Nouri al Marik, alisema "ni muhimu kufanya hivyo, ili kuleta amani ya kisiasa." Matokea ya uchaguzi ambayo mpaka sasa hayajamalizika kuhesabiwa, yanaonesha chama cha waziri mkuu Nouri al Malik kipo nyuma, ya cha cha mpinzani wake Iyad Alawi. Picha hapo juu anaonekana, waziri mkuu wa Irak, Nouri al Malik akiongea kuhusu swala la uhesabuji wa kura upya. Rais wa Sudan,atakiwa kusafisha jina lake kabla ya uchaguzi.
Kartoum, Sudan - 21/03/2010.
Kiongozi mmoja wa chama cha upinzani cha sudan People's Liberation Movement(SPLM) nchini Sudan, amesisitiza yakuwa rais wa sasa wa Sudani lazima akajibu mashitaka yanayo mkabili katika mahakama ya kimataifa ya Hague iliyopo nchini Uhollanzi.
Akiongea kwa nyakati tofauti, na kukiwa kumebakia siku chache kabla ya uchaguzi wa kuchagua wabunge, Edward Lino, alisema " Hatukumwambia au kushirikiana wakati anafanya hayo makosa na hatukukubaliana naye kwa hilo, hivyo nilazima asafishe jina lake kabla ya kugombe kiti cha urais tena."
Edward Lino aliyaongea hayo wakati wa mkutano wa kuchangia pesa za kujenga upya maeneo yaliyo alibiwa vibaya kutokana na vita.
Picha hapo juu anaonekana rai wa Sudan, Omar al Bashir, ambaye amekuwa akishitumiwa na jumuiya ya kimataifa kutokana na hali mbaya ya Darfur.

Saturday, March 20, 2010

Pope aomba msamaha kwa niaba ya Kanisa.

Tiger Woods,apata mthiani mwingine.

Orlando, Amerika - 20/03/2010. Mcheza gofu na bingwa wa mashinado makubwa ya mchezo huo Tiger Woods na wanasheria wake wanajaribu kuzuia visanamu vya mwan gofu huyo visiuzwe. Kwa mujibi habari zilizo patikana, zinansema, visanamu hivyo vya kimapenzi, vinamleta wakati mgumu Tiger Woods, kwani ni muda ameweza kuweka sawa unyumba wake, baada ya kuyumba kwa muda. Hata hivyo kampuni ambayo inafanya mpango wa kuuza visanamu hiivyo Pipedream ahija eleza lolote kutokana na swala hilo. Picha hapo ni ya Tiger Woods,ambaye alikuwa na matatizo ya kifamili siku za nyuma na sasa ameyamaliza baada ya kuomba msamaha kwa mke wake, famili kwa ujumla na washabiki wake. Pope aomba msamaha kwa niaba ya Kanisa.
Rome, Itali - 20/03/2010. Kiongozi mkuu wa Kainsa Takatifu la Katoliki duniani Papa Denedikt VXI, ameomba msamaha kwa niaba ya Kanisa kwa wanchi wa Irish kutokana na vitendo vilivyo fanywa ndani ya Kanisa kati ya mwaka 1930 hadi miaka ya karibuni.
Katika waraka uliosomwa kwa wanchi wa Irish na Wakristu wote, ulisema "Naomba msamah kwa yote yaliyofanywa na Kanisa kwa kipindi chote hasa katika Kanisa Katoliki na waumini wake, kwa wale wote waliotenda hayo wanaweza kuikimbia sheria lakini Mungu huwa hakimbiwi."
Aliwataka wote wale waliohusika katika kitendo cha kuhaibisah Kanisa wa jitokeze mbele ya sheria wenyewe.
Picha hapo juu nanonekana, Pope Benedict VXI akiwaslimia waumini waliokuja kufanya maombi pamoja na Papa hivi karibuni Vatican.

Thursday, March 18, 2010

Zuma ashinda kura za maoni

Zuma ashinda kura za maoni. Cape Town, Afrika ya Kusini -18/03/1020. Rais wa Afrika ya Kusini ameshinda kura za maoni ambazo zilikuwa zimepigwa hivi karibuni, baada ya vyama vya upinzani kudai kura hizo zipigwe. Vyama vya Congre of people na Democratic Alliance ndivyo viliongoza kwa kutakura za maoni zipigwe. Kura za maoni zilizo pigwa 241 zili kubali uongozi rais Jakob Zuma, na 81 zilipinga uongozi wake. Kura hizo ni za kwanza tangu Afrika ya Kusini kutoka katika serikali ya kibaguzi mwaka 1994. Picha hpo juu anaonekana rais wa Afrika ya Kusini Jakob Zuma, katikati akiwa anashiriki katika mila na utamaduni wa kabila lake la Zulu ambapo huwa anashiriki kikamilifu bila kuficha. Anyongwa kwa makosa ya kifedha. Pyongyang, Korea ya kaskaziani - 18/03/2010. Serikali ya Korea ya Kaskazini ilimuhukumu kifo na kumyonga afiasa mmoja aneye shughulika na mswala ya fedha na uchumi baada kubainika alikuwa anakwenda kinyume na sheria. Afisa huyo Pak Nam-ki, aliuwawa kwa kupigwa risasi. Hata hivyohabari kutoka Korea ya Kusini zinamsema , kuuwawa kwa bwana Pak kunakuja baada ya kubainika alikuwa anapingana na sera za serikali ya mapinduni ya Korea ya Kusini. Picha hapo juu, ni ya bendera ya Korea ya Kaskazini, nchi ambayo imekuwa ikilaumiwa kwa kukiuka haki za binadamu kila wakati. Kitendawili cha Iran jibu bado kwa Amerika na Urusi.

Moscow, Urusi - 18/03/2010. Waziri wa mabo ya nje wa Amerika, Bi Hillary Clinton, amekutana na waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergey Lavrov, na kuitaka serikali ya Urusi kusimamisha kwa muda kuisaidia Iran kujenga mtambo wa kinyuklia wa Buchehr.
Akiongea bi Haillary Cinton, alisema " Ikiwa Iran itaonyesha ya kuwa ina nia ya kushirikiana kujenga mtambo ambayo aitazalisha siraha za kivita."
Hata hivyo, waziri wa mambo ya nje wa Urusi,Sergy Lavrov, alisema " Ujenzi wa mitambo ya kunyuklia nhcini Iran, utakuwa chini ya uangalizi wa jumuia ya kimataifa."
Kwa mujibu wa mkataba uliopo kati ya Iran na Urusi, utaghalimu kiasi cha million 700 pound.
Picha hapo juu anaonekana Bi Hillary Clinton, akiongea na waandishi wa habari jijini Moscow.

Tuesday, March 16, 2010

Sony yaingia mkataba tena na ( Michael Jackson) Jackson Estate.

Sony yaingia mkataba tena na (Michael Jackson) Jackson Estate. New York, Amerika - 16/02/2010.Kampuni ya msiki ya Sony, imetiliana mkataba na Michael Jackson estate ili kuimiliki albamu kumi za marehemu Michael Jackson. Mkataba huo wenye thamani ya $250 million ambao ni wa miaka saba. Kwamujibu wa wachinguzi wa mabo ya muziki wanasema Sony itaweza pata faida kubwa hasa wakati wa kuazimisha siku ya kukumbuka ya kifao cha Michael Jackson. Picha hapo juu ni ya Michael Jackson akifanya mavitu ya kujiandaa na maonyesho, enzi za uhai wake.

Sunday, March 14, 2010

Rais wa Zimbabwe aunga mkono chama cha Consevertive.

Rais wa Zimbabwe aunga mkono cham cha Consevertive.

Harare, Zimbabwe - 14/03/2010. Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe, ameunga mkono mabadiliko ya uongozi wa kisiasa nchini Uingereza kwa kusema "ni vizuri uongozi wa chama cha Conservative kinachoongozwa na David Cameron kushinda uchaguzi ujao, kwani tunaweza kushirikiana na kuelewana nao, kuliko Labour ambao viongozi wake ni waaoga kukutana na sisi."
Rais Mugabe , alikuwa akijibu maswali baada ya ziara ya rais wa Afrika ya Kusini Jakob Zuma aliyoifanya hivi karibuni nchni Uingereza na kuongelea swala la kuondolewa vikwazo kwa serikali ya Zimbabwe.
Hapo juu anaonekana rais wa
Somalia kupata msaada wa kijeshi.
Moghadishu, Somalia - 14/03/2010. Serikali ya Somalia inajiandaa kijeshi kukabiliana na makundi ya kijeshi yaliyopo nchini humo ambayo yame uteka mji mkuu wa Mogadishu.
Kwa mujibu wa habari zilizo tolewa na mmoja wa mkuu wa majeshi ya Somali alisema " Misaada ya kijeshi itapatikana na mingi kutoka Amerika"
Hata hivyo serikali ya Amerika ilikanusha habari hizo
Washington imekuwa ina tafuta ni njia gani itaweza kuleta amani katika eneo hilo ambapo inaminika kundi la Alqaeda lina wafuasi wake.
Picha hapo juu ni baadhi ya wapiganaji wakiwa katika doria jiji Mogadishu.
Pesa yetu itabaki katika mzunguko wa kawida.
Beijing, China - 14/03/2010. Serikali ya China imesema yakuwa lawama zinazo tolewa na baadhi ya nchi kuhusu hali ya kibiashara na mzunguko wa fadha wa China ni wa bure kwani nchi hizo zinataka hali nzima iwe kwa faida ya mataifa yao kibiashara na kiuchumi.
Akiongea katika mkutano waziri mkuu wa China, Wen Jiabao, kuhusu mvutano uliotokea kati ya Beijing na Washingtone siku ya Alhamisi kuhusu swala zima la biashara na mzunguko wa fedha kwa kusema"China itaweka mzunguko wa pesa zake katika hali ya kawaida, ijapokuwa Amerika imedai mabadiliko yafanyike"
Picha hapo juu anaonekan waziri mkuu wa China, Wen Jiabao akiwasalimia walioudhulia mkutano jijini Beijing.

Saturday, March 13, 2010

Kanisa Katoliki lakumbwa na kashfa nyingine nchini Ujeruman

India na Urussi kushirikiana katika kuendeleza nguvu za kinyuklia. New Delhi, India - 13/03/2010. Serikali ya India na Urussi zimetilia sahihi mkataba wa kuanzisha ujenzi wa mitambo ya nguvu za nyuklia nchini India. Mkataba huo ulifanyika jiji Delhi wakati waziri mkuu wa Urussi, Vladimir Putin alpo tembela nchini India. Akiongea kuhusu mkataba huo waziri mkuu wa Urussi, Vladimir Putin alisema" tunajenga uhusiano na India hasa katika sekta ya Nyuklia." Naye waziri mkuu wa India Manmohan Singh, alisema " uhusianowetu na Urussi ni wa uhakika katika nyanja tifauti." Picha hapo juu wanaonekana waziri mkuu wa Urusi, Vladimir Putin kushoto akiongea na waziri mkuu wa India Manmoham Singh kulia wakati walipo kutana jijini Delhi hivi karibuni. Kanisa Katoliki lakumbwa na kashfa nyingine nchini Ujeruman. Munich, Ujeruman -13/03/2010. Askofu mkuu wa Kanisa Katoliki nchni Ujerumani ameomba masamahaa kwa niaba ya kanisa kutokana na matukio na matendo yaliyo tokea miaka ya nyuma. Askofu,Robert Zollitsch,aliyasema" Kanisa lita yafanyia uchunguzi madai yote, litawapatia huduma za kiushauri wale wote walioathirika na matukio hayo." Kuomba msamaha huo kunakuja baada ya Kanisa Katoliki kukumbwa na kashfa shutuma kubwa kufuatia malalamiko yaliyo letwa na watu ambao waliathilika na matukio hayo yaliyo tokea ndani ya Kanisa Katoliki. Picha hapo juu anaonekana, Askofu Mkuu Robert Zolliisch akiongea kuhusu matukio yaliyo toke ndani ya kanisa.

Thursday, March 11, 2010

Kupinga kuvaa hijab haku mkomboi mwananke

Kupinga kuvaa hijab haku mkomboi mwanamke. Strasbourg, Ufaransa - 11/02/2010. Kiongozi mwandamizi wa shirika la kutetet haki za binadamu katika bara la Ulaya, Thomsas Hammarberg amesema " sheria za kutaka kuwazuia wakina mama kuvaa hijab za aina yoyote katika baadhi ya nchi za ulaya ni kukandamiza haki za wanawake na zinaweza kuleta athatari siku za baadaye." Aliyaongea haya wakati wa siku ya wanawake duniani. Akiongezea Thomsas Hammerberg, alisema "kuwazuia wanawake hao kuvaa hijab hakutaleta ukombozi wa wanawake na kunaenda kinyume na maadili ya demokrasi na hasa swala zima la uhuru wa mtu binafsi kuingiliwa katika maaamuzi yake yanayo mfaa. Picha hapo juu wanaonekana, baadhi ya wanawake waliopa katika bara la Ulaya wamevalia hijabu amabzo zinataka kupigwa marufuku.