Wednesday, August 27, 2008

Zambia yakumbwa na msiba mkubwa, rais Levy Mwanawasa hatupo naye tena"Ni pigo kwa taifa asema rais wa zamani Kenneth Kaunda"

Lebanoni yafungua mashitaka dhidi ya serikali ya Libya"Rais ashutumiwa"

Beiruti,Lebanoni-27/08/08.Serikali ya Lebanoni, imemfungulia mashitaka rais wa Libya,Muammar Gaddafi kwa kudai ya kuwa serikali ya Libya ilihusika katika upoteaji wa kiongozi wa dhehebu la Kishia, Sheikh Moussa Sadri.
Kupotea kwa Sheikh Moussa Sadri, kulitokea miaka 30 iliyo pita wakati kiongozi huyo alipo tembelea Libya mnamo mwaka 1978.
Hata hivyo serikali ya Libya imekua ikikataa kuhusika na kupotea kwa kiongozi huyo wa dhehebu la Kishia, na kusema alipanda ndege kuelekea mjini Rome.
Picha ya hapo juu ni ya rais Muammar Gaddafi,anaye shutumiwa na serikali ya Lebanoi ya kuwa serikali yake ilihusika katika kupotea kwa Sheik Sadri.
Chini ni picha ya Sheikh Sadri, aliyepotea miaka 30 iliyo potea akiwa safarini nje ya Lebanoni.
Wateka nyara wajisalimisha, baada ya majadiriano ya muda mrefu.
Kufra,Libya- 27/08/08.Watu walioteka nyara ndege ya shirika la ndege la Sudan, wamejisalimisha kwa serikali ya Libya, baada ya muda mrefu wa majadiriano.
Ndege hiyo aina ya boeng 737 ambayo ilikuwa imechukuwa abiria 95 kutoka mji moja wa Nyala Darfur.
Kwa mujibu wa mmoja ya wasemaji wa wateka nyara hawa, walidai wapelekwe Ufaransa.
Hata hivyo ndege hiyo haikuweza kufika ufaransa kutokana na huaba wa nafuta na kulazimika kutua Kufra baada ya kukataliwa kuingia nchini Misri.
Picha hapo juu ni ya moja ya ndege iliyo tekwanyara ikiwa imetua mjini Kufra kusini mwa nchi ya Libya.
Picha ya tatu inaonyesha ramani ya eneo ambolo ndege ya imetua ili kujza mafuta mjini Kufra.
Zambia yakumbwa na msiba mkubwa,rais, Levy Mwanawasa hatupo naye tena"Nipigo kwa taifa asema rais wa zamani Kenneth Kaunda"
Lusaka, Zambia- 20/08/08. Wananchi wa Zambia wapo katika msiba mkubwa uliyoikumba nchi hiyo, baada ya kifo cha rais wa nchi hiiyo Dr Levy Mwanawasa.
Rais Levy Mwanawasa, alifariki dunia mjini Paris, baada ya kuugua kwa muda mrefu kutokana na ogonjwa wa kupooza uliomkuta wakati akiwa katika mkutano wa viongozi wa Afrika uliofanyika nchini Misri mapema mwezi wezi wa sita (Juni)
Rais Levy Mwanawasa alichaguliwa kuwa rais wa Zambia mnamo mwaka 2002, kama rais wa tatu wa Zambia tangu kupata uhuru 1964.
Nae, rais wa zamani wa Zambia, Kenneth Kaunda, alisema ni pigo kwa taifa zima.
Picha hapo juu ni ya rais, Levy Mwanawasa wakati wa uhai wake akihutubia taifa katika moja ya sherehe za kitaifa nchini Zambia.
Picha ya pili wanaonekana ndugu, jamaa na mke wa rais Levy Mwanawas, bi Maureen, akiwa ameshikiliwa wakati wa mwili wa marehemu mume wake ulipo kuwa ukiagwa na wanchi wa Zambia.
Picha ya tatu wanaonekan maelfu ya wananchi wa Zambia wakielekea kutoa heshima zao za mwisho kwa aliyekuwa raisi wao Dr Levy Mwanawasa.
Picha ya hapo juu wanaonekana askari wakiwa wamebeba jeneza ambapo mwili wa marehemu rais Levy Mwanawasa umo ndani tayari kwa wananchi wa Zambia kutoa heshima zao za mwisho.
Mola aiweke roho ya marehemu rais. Levy Mwanawasa mahali pema peponi. Amina.
Amerika na Libya zarudisha uhusiano, baada ya mvutano wa ajali ya Lockerbie.
Tripol,Libya-22/08/08. Kaya/Familia za watu waliopoteza maisha wakati wa ajali ya ndege iliyo tekwa nyara na watu wanaoshutumiwa kupata misaada ya mafunzo kutoka kwa serikali ya Libya, wameshutumu kurudiwa kwa uhusiano kati ya serikali ya Libya na serikali ya Amerika ni kinyume.
Haya yalisemwa na mmoja wa wasemaji ya watu walio potelewa na ndugu zao katika ajali hii, bwana, Bert Ammerman ambaye kaka yake alipoteza maisha yake,kwa kusema haelewi ni kwanini serikali yake inashirikaana nchi ambayo imehusika katika ajali hii ya Lockerbie.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Amerika nchi ambayo ilikuwa adui mkubwa wa Libya miaaka ya nyuma.
Picha ya pili ni ya mabaki ya ndege ambayo ilipoteza maisha ya watu pale ilipo anguka mjini Lockerbie Scotland.
Picha ya mwisho ni ya bendera ya Libya nchi ambayo imerudisha uhusiano na Amerika hivi karibuni.
Meli zaidi zazidi tekwa nyara pwani ya Somalia.
Mogadishu,Somalia-22/08/08. Zaid ya meli zisizo pungua 4 zimetekwa katika ukanda wa pwani wa unao zunguka nchi ya Somalia.
Kwa mujibu wa shirika moja linalo shughulika maswala ya meli , lililopo mjini Kuala Lumpur(IMB) International Maritime Bureau's, limelipoti yakuwa , kumekuwa na ongewzeko la utekaji nyara wa meli hasa zinapo karibia maeneo ya pwani ya Somalia.
Moja ya meli zilizo tekwa ni kutoka nchi za Japan,Ujerumani, Iran na Malasyia.
Picha hapo juu ni moja ya meli ikiwa katikati ya maji huku imebeba mizigo, lakini meli hizo huwa zinakuwa katika hali ya hatari hasa zifikapo maeneo ya pwani ya Somalia.
Picha ya pili ni ya picha ya meli ya Malasyia ikiwa imetekwa nyara na waharamia katika pwani ya Somalia.
Wanachama wa Muktada Al Sadri waandamana kupinga kukaa kwa muda mrefu kwa wanajeshi ya Amerika na washirki wake.
Bagdad,Iraq -22/08/08.Maelfu ya watu wameandamana mjini Bagdad na kusini mwa mji wa Kufa, kupinga kuwepo kwa muda mrefu kwa jeshi la Amerika nchini humo.
Maandamano hayo yalikuwa yakiongozwa na viongozi, wanachama , wadau na Waumini wa dhehebu la Shia ambao kiongozi wa ni Muqktada Al Sadri.
Mmoja wa kiongozi alisema yakuwa hawataki nchi yao kuwa koloni la Amerika.
Maandamano hayo yalikuja baada ya waziri wa mambo ya nje wa Amerika bi Condoleeza Rice kuwasili nchini Iraq ili kujadili hali halisi ya maswala ya usalama na ushirikianao zaidi.
Picha hapo juu ni Muktada Al Sadri, ambaye amekuwa mstari wa mbele kupinga kuwepo kwa majeshi ya wageni wakiongozwa na Amerika.
Chini ni picha ya wanachama wapenzi na wadu wanao pinga kuwepo kwa jeshi la Amerika na washiriki wake.

Monday, August 18, 2008

Pervez Musharraf ang'atuka madarakani" Asema hii ni kwamanufaa ya taifa".

Pervez Musharraf anga'tuka madarakani''Asema hii ni kwamanufaa ya taifa".

Islamabad, Pakistan-18/08/08. Rais wa Pakistan, Pervez Musharraf, ametangaza kujiuzulu rasmi cheo chake cha Urais wa Pakistan.
Akihututubia kupitia runinga ya taifa rais Musharraf, alisema anaipenda nchi yake na watu wake , na katika kipindi chote cha uongozi wake,alijitahidi kwa hali na mali kulinda na kujenga heshima ya nchi yake.
Uamuzi huu wa kujiuzulu kwa rais Musharraf kumekuja, kufuatia kashfa zilizo kuwa zikimuandama, kutoka kwa wapinzani wenzake wa kisiasa,wakiongozwa na viongozi aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo miaka ya nyuma bwana Nawazir Sharif na Asif Al Zardari.
Picha hapo juu anaonekana wanachama na wapinzani wa rais Pervez Musharraf wakishangilia kwa furaha, hukum mmoja wao akipiga risasi juu, baada ya kusikia habar yakuwa rais Pervez Musharaf anajiuzulu cheo chake cha Urais.
Picha ya pili anaonekana rais Pervez Musharaf , akihutubia taifa kwa njia ya runinga ya kua anangatuka kutoka madarakani.
Picha ya mwisho anaonekana , Gen Pervez Musharraf, akiwa katika mavazi yake ya kijeshi, kabla ya kutangaza rasmi yakuwa anajiuzulu rasmi kuvaa magwanda, na tayari kuwa raia wa kawaida ili kuiongoza nchi yake.
Ukraini ya jiweka tayari kupokea msada wa kiulinzi"Ofisi ya mambo ya nje ya nchi yasema hayo"
Kiev, Ukraini-16/08/08. Serikali ya mjini Kiev,imesema yakuwa ipo tayari kuongea na nchi yoyote ya Ulaya kuhusiana na swala na ushirikiano wa maswala ya kijeshi na ulinzi wa nchi hiyo.
Haya yaliongelewa na ofisi ya waziri wa mambo ya nje ya wa Ukrain.
Kwa mujibu wa mmoja ya wachunguzi wa mambo ya ulinzi ya Ukrain,alisema uamuzi wa Ukrain umekuja baada ya kuona hali halisi iliyo tokea nchini Georgia.
Hata hivyo serikali ya Moscow ilipka kura kujitoa kushirikiana na Ukrain katika maswala ya kiulinzi baada ya Ukraini kuomba kuwa mwanachama wa NATO. Picha hapo juu ni bendera ya Urusi, nchi ambayo imekuwa na mvutano mkubwa na serikali za Umjoa wa Ulaya na Amerika mara baada ya kuishambulia kivita Georgia hivi karibuni.
Picha ya pili ni ya alma ya NATO, umoja ambao nchi nyingi ambazo zilikuwa chini ya jumuia ya Urusi (USSR) zinataka kujiunga na umoja huu.
Picha ya mwisho wanaonekana rais wa Urusi kulia akisalimia na rais wa Ukraine Victor Yushchenko walipo kutana pamema mwaka huu.

Thursday, August 14, 2008

Nigeria yakabidhi rasmi eneo la Abakassi kwa Wakameroon"Ndoto yatimia"

Wajumbe wa upinzani na serikali wakubaliana kwa pamoja nchini Zimbabwe "Wataka haadi itimizwe".

Harare, Zimbabwe- 14/08/08. Mkutanao wa mazungumzo yakulea suruhisho la kisiasa nchi Zimbabwe yanaendelea kati ya rais Robert Mugabe na viongozi wa chama cha upinzani cha MDC, kinacho ongozwa na Morgan Tsvangirai zimnefikia katika hali ja juu zaidi.
Kwa mijibu ya wajumbe waliokuwepo kwenye mkutano huo,walisema yakuwa wajumbe wa kambi zote mbili walikubaliana na ule mkataba wa Lancaster, ambapo makubaliano yaliwekwa kati ya serikali ya Uingereza na Zimbabwe mwaka 1979, yakuwa serikali ya Uingereza itasaidiana serikali ya Zimbabwe katika swala la ardhi, yakuwa lazima utimizwe.
Kwa mujibu wa msemaji wa MDC,alisema haya yote ni kuakikisha yakuwa kila Mzimbabwe ana kuwa na imani na viongozi wao ya kuwa wanajali maslahi ya wananchi wa nchi.
Picha ya hapo juu ni ya moja ya shamba ambalo halijalimwa kitu tangu mgogoro wa kisiasa na ardhi ulipo anza nchni Zimbabwe.
Picha ya pili wanaonekan rais Robert Mugabe na kiongozi wa MDC-Democratic Movement Change, Morgan Tsvangirai wakiwa katika taswila tofauti kutetea hoja zao kwa wamnanchi wakati wa kampeni za uchaguzi uliofanyka mapema mwa mka huu wa 2008.
Picha ya tatu inaonyesha ni jinsi gani ardhi ya Zimbabwe, ilivyo na rutuba,hapo linaonekana moja ya zao lililopandwa shambani likiwa limestawi vizuri.
Picha ya mwisho,anaonekana , rais wa Afrika ya Kusini, Thabo Mbeki akikijibu maswali toka kwa waandishi wa habari, mara baada ya kutoka kwenye mkutano unao kutanisha viongozi wa Zimbabwe, ili kujadili njia za kufika muafaka kumaliza tatizo la kisisasa lililopo nchini humo.
Haya ni maendeleo ya jumuia ya Afrika Mashariki"Rais Paul Kagame".
Kigali, Rwanda-13/08/08. Rais wa Rwanda, Paul Kagame amekaribisha na kukubaliana na waziri mku wa Kenya , Raila Odinga yakuwa hipo haja kupunguza vituo vya kupimia uzito wa mizigo kutokea bandari ya Mombasa kutoka 13 hadi 2 itakapo fikia mwisho wa mwaka 2008.
Akiongea haya rais Kagame alisema hii ni moja ya mambo ya maendeleo ambayo yanahitajika yafanyike na viongozi wa Afrika ya Mashariki ili kuleta maendeleo katika eneo la Afrika ya mashariki.
Jumuia ya nchi za Afrika ya mashariki unazijumuisha nchi za Uganda Burundi Tanzania Rwanda na Kenya.
Picha ya hapo juu anaonekana rais Paul Kagame akiongea na wajumbe waliohudhulia katika walsha ya maendeleo na biashara katika eneo zima la Afrika Mashariki mjini Kigali.
Picha ya pili ni ya waziri mkuu wa Kenya, Raila Odinga, akiwa anasikiliza kwa makini katika mkuno ulio wakutanisha viongozi wa jumuia ya Afrika Mashariki.
Rais wa Tanzania azindua ujenzi wa kiwanda cha aina yake"Katani kutoa umeme"
Tanga, Tanzania-14/08/08. Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete, imefungua rasmi ujenzi kiwanda kitakacho toa nguvu za umeme kwa kutumia mabaki ambayo yanatokana na zao la katani.
Ujenzi huo wakiwanda cha aina yake, umeghalamiwa na UNIDO-United National Industrial Develepment Organasation na kampuni ya kusindika zao la katani.
Kiwamnda hicho kikikamilika kitawezesha kutoa nguvu za nishati ya umeme kwa kiwanda hicho na mwingine utauzwa kwa shirika la umeme la taifa.
Na wakati huo hu serikali ay Norway imetoa jumla ya dola za Kimarekani million 56 kwa visiwa cha Zanzibar, kwa ajili ya kutandaza waya zitakazo peleka umeme viziwani humo.
Umeme huu utachukuliwa kutoka katika mji wa Tanga, haya ni kwa mujibu wa watalaamu na wasimamizi wa mpango huu.
Picha ya hapo juu anaonekana rais, Jakaya Kikwete akiongea hivi karibuni kuhusu maendeleo ya nchi yake, wakati alipo kutana na waandishi wa habari.
Picha ya pili nina onyesha shamba la mkonge,zao ambalo linatarajiwa kutumika katika uzalishaji wa umeme nchini Tanzania.
Nigeria yakabidhi rasmi eneo la Abakassi kwa Wakameroon."Ndoto yatimia"
Abakassi, Kameroon-14/08/08. Serikali ya Nigeria imekabidhi rasmi kwa serikali ya Kameroon eneo lijulikanalo kama Abakassi, lililopo kwenye eneo la ghuba ambayo inautajiri wa mafuta na gesi ya asili.
Kameroon ilipeleka kesi hii ya madai ya ardhi mwaka 1994 kwenywe mahakama ya kimataifa iliyopo mjini Hague
Kukabidhiwa kwa eneo hili, kumekuja baada ya mahakama ya ya kimataifa kutoa uamuzi ya kuwa eneo hili ni la nchi ya Kameroon mnamo mwaka 2002 kufuatia makubaliano ya Uingereza na Ujerumani ya mwaka 1913 nchi ambazo zilitalawa eneo hili.
Kufuatia uamuzi huu wa mahakama ya kimataifa, serikali ya Nigeria na serikali ya Kameroon, zilitiliana sahii mkataba uliojulikana kama (Green Tree ) mjini Newyork mwaka 2006, ambao ulikubalika ya kuwa Nigeria ilikabidhi eneo hili kwa Kamaroon.
Kukabidhiwa kwa eneo hili,kumepokelewa kwa hisia tofauti, na mwannchi mmoja alisikika akisema hatimaye ndoto imetimilika.
Picha ya hopo juu ni ya ramani ya eneo la Abakassi ambalo limekabidhiwa kwa serikali ya Kameroon.
Picha ya pili wanaonekana viongozi wa serikali wa pande zote mbili wakikumbatiana mara baada ya kumaliza kukabidhiana hati za makubaliano yakuwa eneo la Abakassi kuanzia sasa ni la wa Kamereoon.
Mwana wa Mfalme atoa onyo," wakulima wadogo wadogo hatarini".
London,Uingereza- 14/08/08.Mwana wa Mfalme wa na mfalme mtarajiwa wa Uingereza, Charles Philiip, amesema ya kuwa ulimaji wa kutumia mbegu zinazotokana na madawa, au kutengenezwa katika maaabara, zitaleta maafa makubwa katika jamii na mazingira kwa ujumla.
Akiongezea maafa ya ukulima wa aina hii,Mwana wa Mfalme, alisema yakuwa itadidimiza saana wakulima wadogo wadogo, hasa waliopo kwenye dunia ya tatu.
Picha hapo juu anaonekana mwana wa mfalme wa Uingereza na mfalme mtarajiwa Charles Philip, akisalimia wanachi hivi karibuni wakati wa ziara ya kikazi.
Syria na Lebanon za rudisha uhusuano wa karibu.
Damascus, Syria - 12/08/08. Serikali za Syria na Lebanon, zimekubaliana kimsingi kushirikiana na hasa katika matumizi ya mipaka ya nchi hizo mbili.
Makubaliano hayo yalifikiwa, baada ya rais wa Lebanon kutembelea kikazi nchini Syria.
Kufuatia dhiara hiyo marais wote wawili, rais wa Syria Bashar AL Assad na rais wa Lebanon Michel Sleiman, wamekubaliana kuendeleza uhusiano wa nchi hizo mbili.
Uhusiano wa nchi hizi mbili,uliingia doa tangu miaka 1975 wakati wa vita vya wenye kwa wenyewe vilipo anza.
Picha ya hapo juu ni ya bendera ya Lebanon nchi ambayo imekuwa katika hali ya mvutano wa kisiasa kwa muda mrefu.
Picha ya pili wanaonekana rais wa Lebanon, Michel Sleiman akikagua gwaride pamoja na mwenyeji wake rais Assad.
Picha ya chini ni ya bendera ya Syria, nchi ambayo imekuwa haina uhusiano mzuri na Lebanon, kwa muda wa kipindi kirefu, hadi hivi sasa wakati viongozi wa nchi hizi mbili walipo kubalina kurudisha uhusiano wao nchi hizi mbili.

Wednesday, August 13, 2008

Urusi yasimamisha vita dhidi ya Georgia"Tumetimiza matakwa yetu serikali yadai"

Bingwa wa musiki wa soulo,atutoka" Wanamuziki wapigwa na mshituko".

Tennessee,Amerika - 13/08/08. Mwanamusiki bingwa wa musiki wa soulo, Isaak Heyis, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 65.
Mwanamusiki huyo alifariki dunia kutokana na ugonjwa wa kupooza, kwa mujibu wa mganga wake.
Mganga huyu, Mr Steve Shular,alisema Isaak Hayes, aliaanza kuugua mapema mwaka 2006.
Isaak Heyes, alishinda zawadi ya Oscar mwaka 1971 na mwaka 2002, alijumuishwa katika kundi la wanasanaa maarufu duniani lijulikanalo kama (US Rock and Roll Hall of Fame).
Mwanamusiki huyu ambaye alioa mara nne ameacha watoto 12.
Kufuatia kifo chake, wanamuziki wengi wamepigwa na mshituko mkubwa saana, hasa kwa mwanamusiki Gloria Gaynor na alisema ya kuwa jumuia nzima ya wanamuziki wa soul ilikuwa inamjua kwa umairi wake.
Mazishi ya marehemu Isaak Heyis yatafanyika Tennessee, misa ya kumwaga na kumwombea itafanyika katika kanisa la Hope Presbyterian kwenye kitongoji cha Cordova.
Picha hapo juu anaonekana marehemu Isaak Heyis, akiimba na kutumwiza wapenzi wake enzi ya uahai wake.
Picha ya pili anaonekana, marehemu Isaak Heyis, akiwa ameshikilia zawadi ya kujulikana kama mmoja ya wana sanaa maarufu duniani wakati wa enzi za uhai wake.
Mafua ya ndege yaibuka magharibi mwa Afrika"FAO ipo mbioni kukabili janga hili".
Lagos,Nigeria - 12/08/08. Wanasayansi nchini Nigeria, wamesema yakuwa wamegundua ya kuwa kumekuwepo na ugonjwa wa mafua ya ndege nchini humo.
Kwea mujibu wa wanasayansi, ugonjwa wa mafua ya ndege,umegunduliwa kuwepo katika majimbo ya Katsina na Kano.
Kwa kufuatia mfumuko huo wa ugonjwa wa mafua ya ndege,(FAO) Food and Agriculture Organisation, limesema ya kuwa,mpaka sasa ni vigumu kujua ni kwa kiasi gani ugonjwa huu umesambaa na umeibuka vipi katika Afrika, hata hivyo FAO imesema ipo mbioni kukabilina na janga hili.
Chini ni picha ya mkulima mmoja wakitembelea ndani ya shamba lake huku amefunika pua yake.
Picha ya chini,Mbuni ni ndege mkubwa kulikono wote , akiwa amekufa baada ya kukumbwa na ugonjwa wa mafua ya ndege.
Tawi la Al Qaeda kaskazini mwa Afrika la sema Mauritania ijiandae" Baada ya mapinduzi".
Nouakchott,Mauritania - 12/08/08. Kikundi ambacho ni tawi la kundi kubwa la Al-Qaeda, kilichopoo nchini Algeria, kimesema yakuwa mapinduzi yaliyo fanyika nchini Mauritania ni kinyume na yamesadidiwa na nchi za Ulaya Magharibi na Amerika.
Mauritania, nchi ambayo ilikuwa koloni la Kifaransa,imekuwa katika hali ya utata tangu ilipo pata uhuru.
Mauritani ni nchi yenye utajiri wa mafuta, dhahabu na chuma.
Mapinduzi hayo baridi, yalimtoa madarakani rais Sidi Mohamed Ould Cheikh Abdallah.
Picha hapo juu wanaonekan viongozi vinara wa kundi la Al-Qaeda, Osama Bin Laden kushoto na msaidizi wake, Imar Al Zawahiri walipo onekana kwa mara ya mwisho miaka ya nyuma, na kundi lao Al Qaeda limekuwa likisumbua vichwa vya jumuia ya kimataifa kwa muda mrefu.Picha ya chini ni ya bendera ya Mauritania,nchi ambayo wananchi wake wametakiwa kijiandaa na mapambano ya Al Qaeda baada ya mapinduzi yalioyo mngo'a rais Sidi Mohamed Ould Cheikh Abdallah.
Musharraf na wapinzani wavutana "Wapinzani wadai Musharraf ang'olewa".
Islamabad,Pakistan - 12/08/08. Viongozi wa cham cha upinzani nchini Pakistan, wamesema yakuwa inabidi rais, Pervez Musharraf, atolewe madarakani, kwa kushindwa kuwajibika ipasavyo.
Wakiyaongea hay mbele ya waandishi wa habari, alisema ya kuwa rais, Musharraf anatakiwa aonolewe madarakani kwa kukiuka sheria ya nchi na kushindwa kudhibiti mgogoro wa kisiasa ulipo nchini humo na ina bidi bunge ilfanye hivyo.
Hata hivyo, kwa upande waserikali, walikanusha , na kusema yakuwa haitawezekana kwa rais Pervez Musharraf, kutolewa madarakani n a nikitu ambacho hakitatoke.
Picha hapo juu, wanaonekana viongozi wa vyama vya upinzani Muslimu League N party bwana Nawazir Sharif kulia na kushoto ni, kiongozi wa Pakistani Peoples Party Asif Ali Zardari , wakiongea na wandishi wa habari kwa kutaka rais Musharraf atolewe ofisini.
Picha ya pili, anaonekana rais, Pervez Musharraf akisalimiana na baadhi ya watu wakati alipo tembelea katika moja maeneo yanafanyiwa ukarabati.
Picha ya chini, wanaonekana baadhi ya watu na wanachama wambao wanapendelea rais, Musharraf aendelee kuwa rais wa nchi yao.
Urusi yasimamisha vita dhidi ya Georgia"Tumetimiza matakwa yetu serikali yadai"
Moscow, Urusi - 12/08/08. Serilikali ya Urusi, ilitangaza rasmi ya kuwa itasimamisha mapigano ya kivita dhidi ya nchi ya Georgia.
Akiongea haya rais wa Urusi, Dmitri Medvedev, alisema yakuwa ameamuru majeshi kusimamisha mapigano, kwani Urusi, imeweza kutimiza matakwa yake, ya kuzikomboa yaye maeneo ambayo yalikuwa yamechkuliwa na wanajeshi wa Georgia.
Maeneo ambayo yalikuwa yanashikiliwa na wanajeshi wa Georgia, yanajulikana kama Ossetia na Abakhazia.
Na Wakati huo rais wa Urusi akitangaza haya, rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy alikuwa mbioni kujadili na viongozi wa pande zote ili kuleta amani katika eneo hilo.
Picha ya juu, anaonekana rais wa Urusi, Dmitri Medvedev,akiongea hivi karibuni kwenye katika moja ya mikutano iliyofanyika nchini humo.
Picha ya pili wanaonekana wanajeshi wakipigana wakati wa mapambano ambayo yamechukua muda wa siku tano.
Picha ya tatu inaonekana helkopta ya Urusi, ikitua katika moja maeneo ambayo vita vilikuwa vinaendea kabla ya kusimamishwa kwa vita dhidi ya nchi hizi mbili.
Chini anaonekana rais wa Georgia, Mikhael Saakhashvili,akijisugua kichwa, wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu hali halisi ya vita vya nchi yake dhidi ya Urusi.

Thursday, August 7, 2008

Mtuhumiwa aponyoka mikononi mwa polisi."Msako waendelea"

Rwanda yataka viongozi wa Ufaransa wafikishwe mahakamani "Yataja majina 33 ya wahusika".

Kigali, Rwanda - 07/08/08. Serikali ya Rwanda, imetangaza ya kuwa serikali ya Ufaransa,ina husika moja kwa moja katika mauji ya alaiki ya watu wasiopungua laki 800,000 yaliyo tokea 1994.
Katika maelezo yake, serikali ya Rwanda imewataja maafisa 33 wa ngazi za juu wa jeshi na wanasiasa wa Ufaransa waliohusika katika mauaji hayo.
Katika majina hayo wamo rais wa zamani wa Ufaransa Francois Mitterrand na waziri mkuu wa zamani wa Ufaransa bwana Dominique de Villepin ambaye serikali ya Rwanda inadai afikishwe kwenye vyombo vya sheria ili kujibu mashitaka.
Hata hivyo serikali ya Ufaransa imekanusha madai hayo.
Picha ya hapo juu, ni ya bendera Rwanda, nchi ambayo ikikumbwa na mauaji yaliyo shangaza dunia nzima.
Picha ya pili ni ya mabaki ya watu walio poteza maisha yao, kutokana na vita vya kikabila kati ya Watutsi na Wahutu, ambapo serikali ya Rwanda inasema ya kuwa serikali ya Ufaransa ilihusika katika mauaji hayo.
Picha ya chini ni bendera ya Ufaransa,nchi ambayo imekuwa ikilaumiwa na Rwanda kwa kushindwa kuzuia mauaji ya alaiki ya mwaka 1994
Mamia waombeleza na kukumbuka milipuko iliyo poteza maisha," Afrika Mashariki".
Dar es Salaam, Tanzania - 07/08/08 .Mamia ya wanachi nchini Tanzania, wamakusanyika leo kuadhimisha miaka kumi ya kumbukumbu ya matukio ya kutisha, wakati mabomu yalipo lipuliwa katika ofisi za kibalozi za Amerika, zilizopo nchini Tanzania na Kenya.
Mabomu hayo ambayo ya lilipuliwa na kundi la kigaidi la Al Qaeda na kupoteza maisha ya watu wapatao 220 na wengine kupata vilema vya maisha.
Katika kuadhimisha siku hiyo,viongozi wa serikali na wakidini walikusanyika na kumba kwa pamoja na kusisitiza amani na utulivu duniani kote ndiyo njia bora kwa maisha ya mwanadamu.
Picha hapo juu, ni bendera ya Amerika, nchi ambayo imekuwa ikiongoza katika mstari wa mbele kupamabana na kundi la Al Qaeda na washirikimwake na kuaidai kulitokomeza kabisa.
Picha ya pili ni ya jengo la moja ya ofisi za balozi za Amerika zilizopo mjini Dar es Salaam, ambapo liliharibiwa vibaya na mabomu.
Picha ya tatu, lina onekana jengo la ofisi za kibalozi nchni Kenya, ambalo nalo lili polomoshwa kabisa kutokana na mlipuko wa bomu.
Jeshi la twaa madaraka, mgogoro wa kisiasa ndiyo chanzo,"Mapinduzi baridi".
Nouakchott, Mauritania - 07/08/08.Viongozi wa jeshi nchini Mauritania wameipindua serikali iliyo kuwa ikiongozwa na rais, Sidi Mohamed Ould Cheikh Abdallahi.
Mapinduzi hayo ambyo hayakumwaga damu yaliongozwa na viongozi wa jeshi kwa kudai yakuwa kwa kushindwa kuongoza nchi, kwa kufuatia mgogoro wa kisiasa, baada ya ya baadhi ya wabunge wapatao 48 kujitoa katika chama tawala na kupiga kura ya maoni ya kuto mwamini rais huyo baada ya kubadiri baraza la mawaziri.
Mapinduzi haya yaliyo fanyika nchni Maurutania, yamelaniwa vikali na nchini nyingi duniani, zikiongozwa na Umoja wa mataifa.
Picha hapo juu wanaonekana viongozi wa kijeshi wakiongozwa na Ould Abdel Aziz, akiongea na vyombo vya habari muda mchache baada ya mapinduzi ya kumtoa madarakani rais wa Mauritania, Sidi Mohamed Ould Cheikh Abdallahi.
Picha ya pili ni ya rais wa zamani wa Mauritania Sidi Mohamed Ould Chikh Abdillahi, ambaye ametolewa madaraka na jeshi la nchi yake.
Picha chini wanaonekana wanajeshi, wakiwa wanalinda mbele ya ofisi za shirika la utangazaji na radio za Mauritania.
Mtuhumiwa aponyoka mikononi mwa polisi,Msako waendelea"
Nairobi, Kenya - 4/08/08. Serikali ya Kenya inafanya msako mkubwa wa kumkamata mtuhumiwa aliyehusika katika milipuko ya mabomu yaliyo tokea katika balozo za Amerika nchini Tanzania na Kenya.
Mtuhumiwa huyo anaye jukilkana kwa jina la Fazul Abdullah Mohammed, amabye inasemekana aliponyoka katika nyayo zapolisi wakati walipo kuwa wakimfuatilia ili kumkamata.
Kwa mujibu wa masemaji wa polisi, Fazul Abdallah Mohammed, alikuwa akiishi sehemu za Malindi kabla ya kutoroka kabla ya vyombo vya dola kumtia nguvuni.
Picha hapo juu, ni ya bendera ya Kenya, nchi ambayo imekuwa katika halingumu ,kukabiliana na ugaidi.
Picha ya pili ni picha ya Fazul Abdallah Mohammed, amaye anasakwa na vyombo vya dola vya Kenya na jumuia ya kimataifa.
Picha ya tatu wanaonekana polisi wakikagua moja ya magari, katika jitihada za kumsaka Fazul Abdallah Mohammed.
Iran bado ya weka kitendawili kwa Amerika na jumuiya ya Ulaya.
Tehran, Iran - 4/08/08 . Serikali ya mjini teherani, imetangaza hivi karibuni ya kuwa imefanya majaribio ya siraha zake ambazo zinaweza kuzamisha meli na chombo chochote kinacho safiri katika maji au bahari, kwa karibu umbali wa miili 200.
Majaribio haya, yamekuja baada ya jumuiya ya Ulaya na Amerika, zinapanga upya kwa pamoja kuweka vikwazo zaidi dhidi ya serikali ya Tehrani.
Na ikiwa njia hii ya Harmuz itafungwa basi, huenda bei ya mafuta ikapanda kwa kiasi kikubwa, kwani 40% ya mafuta yanapita katika ukanda huo.
Hapo juu zinaonekana, baadhi ya siraha ambazo serikali ya Iran imekuwa ikizijaribu hivi karibuni.
Picha pili ya hapo juu, anaonekana rais wa Iran, Mahamoud Ahamadinejad akihutubia mbele ya bunge la Iran hivi karibuni.
Picha ya chini, ni sehemu moja ya mitambo ambayo vinu vya kuendeshea uzalishaji wa nguvu za kinyuklia vimekuwa vikitakiwa na serikali ya Amerika na Jumuiya ya Ulaya vifungwe, lakini nchi ya Iran, imakataa kabisa kufunga mitambo hiyo.