Wednesday, November 26, 2008

Maendeleo ya China yawa kitendawili kwa dunia"Usili ndiyo kikwazo"

Wairak wavutana kuongezewa muda kwa jeshi la Amerika.

Baghdad,Irak- 25/11/08. Mjadara mkali ambao unaendelea kukubaliana kwa wanchi wa Irak, kukubali kubakia kwa jeshi la Amerika na washirika wake kwa kipindi cha miaka mitatu, umefikia njia panda, baada ya mvutano mkubwa ulio tokea katika bunge la Irak, ili kukubaliana mswada huo.
Amerika yenye wanajeshi wapatao, 150,000, wapo nchini Irak.
Kufuatia mvutano huo, bunge limekubali kwa pamoja ya kuwa kura ya maoni huenda ikatumika ikiwa bunge litashindwa kukubaliana kupitisha muswada huo.
Bunge hilo, linalo jumuisha makundi makubwa ya yaliyo gawanyika kidini ,Suni,Shia na Kurdi.
Picha hapo juu anaonekana, waziri mkuu wa Irak, Nuri Kamal al Maliki, akiongea hivi karibuni kusisitiza lazima kuwepo na uhusiani kati ya Wairak.
Picha ya pili anaonekana,mwanajeshi mmoja wa jeshi Ameria akiwa amesimama nyuma ya muhimiri, huku akitizama usalama wa jamii japo wamekuwa na wakati mgumu wa kuleta usalama wa raia nchini Irak.
Picha ya tatu wanaonekana wananchi wa Irak, wakiandamana hivi karibuni siku ya tarehe 21/11/08, karibuni kupinga kuendelea kuwepo kwa jeshi la Amerika nchini Irak.
Maendeleo ya China yawa kitendawili kwa dunia"Usili ndiyo kikwazo"
Washington,Amerika - 23/11/08.Chifu Marshal wa maswala ya ulinzi nchini Amerika, Angus Houston, amesema kuwa maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia yanayo fanyika kisili nchini China yanaleta hali ya kutokuwa na usawa.
Chifu Marshal, Houston, alisema mpaka sasa China ajaeleza ni kwanini iliamua kuvunja kwa kuaribu mtamdao wa seteliti uliopo kwenye anga la dunia.
Akiongezea katika mazungumzo haya,alisema matumizi ya, China yamepanda kutoka pesa ya Kiamerika $ 59billion hadi $ 93.5billion na hii ni ongezeko la asilimia, 17.1% na huenda ikafikia 139billion.
Picha ya hapo juu ni bendera ya China, nchi ambayo ina leta vichwa kuuma kwa jumuia ya kimayaifa kutokana na usili wake.
Picha ya pili, ni ya bendera ya jumuia ya Ulaya, jumuia ambayo kwanjia moja kukua kwa teknolojia nchini China, kutathili kwa kiasi fulani jumuia hiyo kwa mujibu wa wachunguzi wa mambo.
Picha ya tatu, ni ya bendera ya Amerika nchi ambayo ina zidi kuwa na wasiwasi na usili wa China.
Serikali ya Zimbabwe bado yatoa joto ya jiwe kwa jumuia ya kimataifa.
Harare, Zimbabwe - 24/11/08.Serikali ya Zimbabwe imewazui kuingia nchini Zimbabwe kwa kuwanyima visa, viongozi wa zamani wa kimatifa ambao walitaka kwenda kuangali na kutathmini hali halisi ya kijamii nchini humo.
Viongozi hao ambao walizuiliwa kuingia Zimbabwe ni, Kiffi Anan aliyakuwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Jimmy Carter ambaye alikuwa rais wa Amerika wa 39, na Bi Gracia Machelle.
Picha hapo juu anaonekana, rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, akisikiliza kwa makini katika moja ya mikutano ya kuleta suruhisho la kisiasa nchini Zimbabwe.
Picha ya pili wanaonekana, viongozi ambao wamezuiliwa kuingia nchini Zimbabwe kwa kunyimwa viza, kutoka kulia ni Jimmy Carter, Koffi Anan na bi, Gracia Machelle.
Chama kipya cha kisiasa nchini Afrika Kusini chaleta mtikiso wa kisiasa.
Johannesburg,Afrika ya Kusini - 22/11/08.Mwenyekiti wa chama kipya cha siasa nchni Afrika ya Kusini " Congress of the People" Mosiuoa Lekote, amesema kwamba chama hiki kipya kinamwelekeo unao faa kuindeleza nchi, kuwa kipo tayari kuilinda katiba kwa kushirikiana na vyama vingine.
Mwenyeki, Mosiuoa Leketo ni mmoja ya viongozi wa zamani wa chama tawala ANC - African National Congress,ambaye pia ni mmoja ya viongozi waliopigania kupinga utawala wa watu wachache wa makaburu , ambao walileta siasa za kibaguzi za kuwabagua watu waliowengi kwa rangi za miili yao.
Picha hapo juu ni ya mwasisi wa chama kipya cha Congress of the People, bwana Mosiuoa Leketo, akiwa amezungukwa na wananchi wanao kubaliana naye kimsingi.
Picha ya pili, wanaonekana, baadhi ya wanachama wa chama cha ANC - African National Congress, wakiandamana, na mmoja wao akichana kadi kuonyesha ya kuwa hayumo tena katika chama hicho.

Thursday, November 20, 2008

Syria na Uingereza zafanya mazungumzo ya kiserikali.

Umoja wa mataifa wa pitisha azimio la kupeleka majeshi ya kulinda amani Kongo. Goma, Kongo-20/11/08. Umoja wa mataifa umekubaliana kwa kwapoja kupeleka majeshi ya jumuia hiyo wa wanajeshi wapatao 3100. Uamuzi huo wa kutuma majeshi ya umoja wa matifa umekuja sambamba na uamuzi wa jeshi la upinzani linalo pinga na serikali ya Kongo na linaongozwa na Laurant Nkunda, kusimamisha mapigano. Akiongea hayo, balozi wa Uingereza kwenye umoja wa mataifa, John Sawers, alisema nchi 15 zimekubaliana kwa pamoja kutoa mchango wake. Picha hapo juu wanaonekana wananchi wakiwa wamezingirwa na moshi katika moja ya kambi ya kikimbizi , mmoja ya watu walio kimbia vita alisema "hii yote imeletwa na vita vilivyo tokea hapa nchini kwetu (Kongo ) na kuleta maafa makubwa kwa jamii yetu. Syria na Uingereza zafanya mazungumzo ya kiserikali. Damascus,Syria-19/11/08. Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza David Miliband,amefanya ziara ya kiserikali nchini Syria na kuongea na rais Bashar al Assad. Ziara hii ni ya kwanza ya kiongozi wa serikali ya Uingereza tangu mwaka 2000. Kukutana kwa viongozi hawa huenda kukarudisha uhusiano wa serikali hizi ambao umekuwa na mvutano kwa kipindi kilefu. Picha hapo juu wanaonekana, rais wa Syria, Bashar al Assad, akiongea na waziri wa mambo ya nje wa Uingereza David Miliband, walipo kutana hivi karibuni mjini Damascus. Jaji atoa amri washitakiwe waachiwe huru"Hakuna ushaidi ". Guantanamo Bay, Kuba-20/11/08.Jaji Richard Leon,ameagiza ya kuwa washitakiwa watano wanao tokea Algeria na wanaoshikiliwa katika jela ya Guantanamo Bay waachiliwe kwani kukamatwa kwao ni kinyume cha sheria. Jaji, Richard Leon, alisema ya kuwa hakuna ushahidi kalimi wa kuwahusisha watu hao watano, yakuwa walikuwa na mpango wa kwenda Afghanistani ili kupigana na jeshi la Amerika na washiriki wake. Watu hao watano walikamatwa Bosnia Hercegovina mwaka 2001, tangu mwaka huo wamekuwa chini ya ulinzi katika jela ya Gwantanamo Bay.

Matumaini ya kumpata, Baraka Obama, mwingine bara la Ulaya yapo"Asema mbuge"

Matumaini ya kumpata, Baraka Obama mwingine bara la Ulaya yapo"Asema mbunge".

Paris,Ufaransa-16/11/08. Kuchaguliwa kwa Baraka Obama kuwa rais wa Amerika, kumeleta hisia tofauti kati ya wakazi wa ishio katika bara la Ulaya.
Akichangia na kuelezea haya mbuge wa pekee mwafrika katika bunge la Italia, bwana Jean-Leonard Tauadi, alisema ya kuwa kuchaguliwa kwa, Baraka Obama ni mwamko na matumaini ya kuwa hakuna kinacho shindikana kwa kuzingatia hayo, basi ipo siki yaliyo tokea Amerika ya tatokea hapa Ulaya,japo si kwa kizazi chetu, ni matumaini kizazi cha wajukuu wetu kita yaona haya.
Picha ya hapo juu ni ya bendela ya Amerika , nchi ambayo katika historia ya nchi hiyo tangu kuundwa, wamemchagua rais mwenye asili ya Kiafrika.
Picha ya ya pili wanaonekana baadhi ya watu jijini Ufaransa, wakiangalia kwa makini muda mfupi kabla ya matokea ya uchaguzi wa rais kutangazwa.
Picha ya tatu ni ya bendera ya nchi wanachama wa Ulaya, ambapo wakazi wake wamekuwa na hisia tofauti kuhusu matokeo ya ya uchaguzi nchi Amerika yalivyo leta jasho jembamba kwa jamii tofauti.
Mwana wa Malkia wa Uingereza asherekea siku ya kuzaliwa kwake.
London,Uingereza-13/11/08.Malkia wa Uingereza, Malkia Elizabeth II, ameaandaa sherehe ya mwanae wa Prince Charles, ambaye amefikisha miaka 60 tangu kuzaliwa.
Sherehe hizo zilizofanyika kwenye makazi ya Malkia Backingham Palece, ziliuzuriwa na ndugu, jamamaa na marafiki wa familia ya Malkia.
Picha hapo juu anaonekana, Malkia Elizabeth II kushoto akiongea na mwanae Prince Charles kulia, wakielekea kwenye ukumbi uliofanyika sherehe ya kuzaliwa kwa Prince Charles.
Picha ya pili, anaonekana, Prince Charles ya kuwa yeye ni mtu wa watu, huwa wakati mwingine anakutana na marafiki zake na kupata moja moto moja baridi.
Picha ya tatu, ya wanaonekana, kushoto ni Prince Charles na mkewe Camilla Parker.

Monday, November 10, 2008

Mama Afrika,MIRIAM MAKEBA,atutoka, atuko naye tena"MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI, AMINA

Mama Afrika, MIRIAM MAKEBA, atutoka, atuko naye tena"MUNGU AILAZE ROHO YAKE MAHALI PEMA PEPONI, AMINA".

Naples,Itali-10/11/08. Mama Afrika,Miriam Makeba amefariki dunia, baada ya kupata mstuko wa ugonjwa wa moyo wakati akiwa na tumbwiza jukwaani.
Mama Afrika, Miriam Makeba,alianguka jukwaani na baadaye kukimbizwa hospitali, lakini jitihada za waganga hazikufaniukiwa kurudisha uzima wa Mama Afrika.
Mama Afrika, Miriam Makeba alizaliwa mwezi wa, Marchi 4/1932, mjini Johannesburg ni Shantytown.
Mama Afrika, Miriam Makeba, aliishi ukibizini kwa muda wa miaka 31, kupinga utawala wa kibaguzi wa wazungu wachache.
Kwa kutumia nyimbo zake mama, Miriam Makeba, alitumia nyimbo zake kwa kueleza matatizo yanayo wakabili Waafika wenzake, hasa wananchini Afrika ya Kusini, kulisababisha kuzuiliwa kwake kurudi nchini Afrika ya Kusini kuuzuria mazisha ya marehemu mama yake.
Mama Afrika Miriam Makeba,alirudi nchini Afrika ya Kusini mwaka 1990, baada ya kuachiliwa kwa rais wa kwanza wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandele Madiba.
Picha ya kwanza hapo juu, anaonekana mama Afrika Miriam Makeba, akitumbwiza enzi ya uai wake huku akiwa amevalia vazi murua la kiafrika.
Picha ya pili anaonekana, Mama Afrika, Miriam Makeba, akionyesha umairi wake, wa mwanamke wa Kiafrika anavyo fanya vitu vyake, hasa anapo cheza muziki ama ngoma za kiasili.
Picha ya tatu wanaonekana, mama Afrika, Miriam Makeba na Huge Masekela wakifanya vitu vyao mbele ya wapenzi wamuziki walio kuja kukongwa roho zao.
Picha ya nne,anaonekana mama Afrika, Miriam Makeba, akifanya vitu vyake enzi za ujana wake.
Picha ya mwisho anaonekana mama Afrika, Miriam Makeba akisikiliza kwa makini na huku akitafakali na alikuwa akitoa majibu yenye mafundisho na kumbukumbu kwa vizazi vipya.
MOLA - MUNGU AILAZE ROHO YAKE KWA AMANI PEPONI AMINA.
Rais mteule, Baraka Obama wa Amerika, atembelea Ikulu"Michelle Obama, akagua na kuangalia nyumba yake tayari kwa maisha mapya".
Washington DC ,Amerika - 10/11/08. Rais mteule wa Amerika, Baraka Obama na mkewe, Michelle Obama, wametembela Ikulu kikazi kuangalia na kuongea na rais wa sasa wa Amerika George Bush, kuhusu maswala ya kiuchumi ya nchi na maswala ya kimataifa.
Wakati rais, Baraka Obama anaongea na rais, George Bush, Bi Laura Bush atakuwa anamwonye bi, Michelle Obama mazingira ya ndani na nje Ikulu.
Picha hapo juu wanaonekana rais wa sasa George Bush, akiwa na rais mteule Baraka Obama, wakitembelea kwa pamoja mazingira ya Ikulu, kabla ya kuanza mazungumzo.
Picha ya pili, wanaonekana marais, George Bush na mke wake Laura kwa pamoja na rais mtarajiwa Baraka Obama na mke wake Michelle Obama, wakipiga picha kwa pamoja, kabla ya kuanza kazungumzo.
Picha yatatu wanaonekana, rais mteule, Baraka Obama na mke wake Michelle Obama, wakisalimiana rais, George Bush na mkewe Laura Bush,baada ya kuwasili Ikulu.
Picha ya nne, wanaonekana rais mtarajiwa wa Amerika, Baraka Obama na mkewe wakishuka kwenye gari, tayari kuanza mazungumzo na rais wa sasa, George Bush na mke wake Laura Bush.
Picha ya mwisho, wanaonekana rais mtarajiwa, Baraka Obama na mke wake Michelle Obama, wakiangalia kwa makini matokeo ya uchaguzi, ambayo Baraka Obama, alichaguliwa kuwa rais wa kwanza mwafrika kushinda uchaguzi na kuwa rais wa Amerika.
Afisa wa ngazi za juu wa serikali ya Rwanda, akamtwa nchini Ujerumani ( Rwanda na Ufaransa moshi wafuka .......)
Frankfurt,Ujerumani-10/11/08. Serikali ya Rwanda imelaani vikali kitendo cha kukamatwa kwa afisa wa ngazi za juu wa serikali bi Rose Kabuye, alipo kuwa kikazi ziarani nchini Ujerumani.
Bi, Rose Kabuye alikamatwa alipo wasili kwenya kiwanja cha ndege Frankfurt siku ya jumapili 09/11/08.
Kukamatwa kwake kumekuja, baada ya serikali ya Ufaransa, kufungua kesi mwaka 2006, zidi yake ambayo ina mshutumu kuhusika na mauaji ya rais wa zamani wa Rwanda.
Rais ,Juvenal Habyalimana alifariki dunia baadaya ndege aliyo kuwa akisafiria kuangushwa.
Picha hapo juu anaonekana bi, Rose Kabuye kulia, akiwa na rais wa Rwanda Paul Kagame hivu karibuni.
Wapiganaji wanao pigana na serikali ya Somali wateka nyara masista.
Nairobi,Kenya- 10/11/08. Wafanyakazi wa shirika la msalaba mwekundu kutoka Kenya na mastista wa wa kanisa Katholik wametekwa nyara na wapiganaji wanao pigana na serikali ya Somalia.
Kwa mujibu wa msemaji wa shirika la msalaba mwekundu, alisema yakuwa masista na wafanyakazi wa shirika lao walitekwa nyara wakiwa kwenye nyumba zao.
Tukio hilo lilitokea wakati wapiganaji hao, walipiga risasi na na kutupa mabomu ya mkono katika kituo cha polisi kabla ya kufanya utekaji nyara huo.
Masista hao Caterina Giraodo mwenye umri wa miaka 67 na Maria Teresa Olivero mwenye umri wa miaka 60.
Picha hapo juu linaonekana gari lililo beba wafanyakazi wa shirika la msalaba mwekundu na masista likiongozwa na kundi moja la wapiganaji wanao pigana na serikali.
Watuhumiwa wa mauaji ya Bali wa hukumu yao yakamilishwa.
Jakarta, Indonesia-09/11/08. Washitakiwa watatu ambao walihukumiwa kwa kunyongwa baada ya kukutwa na hatia ya kuhusika katika kulipua majumba mawili ya starehe(Disco), mwaka 2002, kwa mabomu na kusababisha mauaji ya watu wasio pungua 202 mjini Jakarta.
Watuhumiwa hao, Imam Samudra, Amrozi bin Nurhasyim na Mukhlas,au kwa jina jingine Ali Ghufron, waliuwawa kwa kupigwa risasi kwenye saa 12:15 asubuhi katika gereza la Nusu Kampangan,alisema msemaji wa serikali Indonesia Jasman Panjaitan.
Kuthibitishwa kwa vifo vyao, kuliidhinishwa na serikali kwa kutumia vipimo vya kitaalaamu.
Picha hapo juu wanaonekana baazi ya wananchi wakiwa wamebeba mwili wa mmoja ya watuhumiwa walio uwawa kwa kupigwa risasi baada kukutwa na hatia ya mauaji.
Picha ya pili wanaonekana wananchi wakiwa wameshika picha za za mmoja ya watuhumiwa wakati walipo andamana kuelekea kuwafanyia mazishi.
Picha ya tatu, anaonekana mmoja ya mtuhumiwa akipelekwa kupewa hukumu zidi yake na baazi ya maofisa wa serikali.
Picha ya mwisho ni za watuhumiwa ambao walihukumiwa, kuuwawa kwa kupigwa risasi.

Sunday, November 9, 2008

Mgogoro wa mashariki ya kati( Palestina na Izrael) bado kitendawili"Niwakati mgumu asema bi,Condeleeza Rice"

Bara la Afrika lajianda na mapokezi ya Papa Benedict XVI mwaka 2009.

Vatican City, Vatican,09/11/08. Papa Benedict XVI, anatarajiwa kufanya ziara katika bara la Afrika mapema mwakani. Kwa mujibu wa msemaji wa Vatican, Papa Benedict XVI,atafanya ziara hii ikiwa moja ya maandalizi ya mkutano na maaskofu kutoka bara la Afrika, utakao fanyika mwezi wa Oktoba 2009. Kwa mijibu wa msemaji huyo, alisema yakuwa Papa, atafanya ziara katika nchi za Angola na Kamerooni. Kamerooni itaandaa mkutano utakao wajumuisha viongozi Afrika wa kanisa Katoliki. Picha hapo juu ni ya Papa Benedict XVI,ambaye anatarajiwa kufanya ziara katika bara la Afrika mapema mwaka wa 2009.

Mgogo wa mashatiki ya kati(Palestina na Izrael) bado kitendawili"Niwakati mgumu asema Condelleza Rice". Sharm el Sheikh, Misri- 09/11/08. Katibu mkuu wa umoja wa mataifa amesisitiza na kuziagiza jumuia ya Ulaya, Urusi na Amerika na kwa kushirikiana na Umoja wa mataifa,zijitahidi kutatua mgogoro wa mashariki ya kati, ambao ni kati ya Palestina na Izrael. Akisisitiza hayo, waziri wa mambo ya nje wa Amerika, bi ,Condeleezza Rice, amesema ya kuwa makubaliano ya kutimiza mkataba wa kuwa na Palestina huru yamekuwa magumu kwa kuzingatia kwa sasa nchini Israel kunatarajiwa kufanyika uchaguzi mwezi wa februari, na kufanya makubaliliano hayo kuwa finyu kwa sasa. Bi Rice, aliongezea kwa kusema yakuwa, serikali mpya inayo kuja ya rais baraka Obama, itakabidhiwa kazi hii. Picha hapo juu anaonekana waziri wa mambo ya nje wa Amerika Condeleeza Rice kushoto akiwa na badhi ya viongozi waliokuja kuuzuria mkutano wa kutafuta kutatua mgogoro wa mashariki ya kati mjini Shrm el Sheikh. Rais wa zamani wa Sudan afariki dunia. Khartoum, Sudan-5/11/08. Aliyekuwa rais wa Sudana Ahmed al Mighani amefariki dunia, akiwa nchini Misri. Rais Ahmed al Mighani,alichaguliwa kuwa rais wa Sudani mwaka 1986 hadi alipo tolewa madaraka na na jeshi lili ongozwa na rais wa sasa, Omar El Bashir mwaka 1989. Akiongeaha yaha kuthibitisha kifao chake, msemaji wa serikali ya Sudani, alisema yakuwa,mija ya watu wakwanza kutoa rambi rambi ni rais wa sasa wa Sudan Omar el Bashir. Picha hapo juu ni bendera ya Sudani, nchi ambayo rais Ahmed al Mighani, aliiongoza kwa muda wa miaka minne kabla ya kutolewa madarakani kwa nguvu za kijeshi.
Muammar Qaddafi ailaumu Amerika" Ziarani Belarus".
Minsk,Belarus-5/11/08.Kiongozi wa Libya ,Muammar el Qaddafi, ame ilaumu Amerika kwa kutumia uwezo wake visivyo wakati alipo kutana na viongozi wa Belarus.
Qaddafi, alisema ya kuwa, Libya zimakuwa zikipewa mzigo wa lawama zisizo na msingi, na hii yote inatokana na kutokuwa na usawa.
Alizidi kwa kusema yakuwa Amerika na washiriki wake wamekuwa wanakiuka haki za binadamu.
Kusisitiza hayo mwenyeji wake, rais wa Belarus,Aleksandr Kukashenko, alisema inatokana na baadhi ya sheria za Umoja wa matifa zinakiukwa na nchi wana chama hasa nchi zenye nguvu.
Mtoto wa Osama bin Laden, aomba hifazi za kikimbizi Uispania.
Madrid, Uispania - 7/11/08. Mwana wakiume wa kiongozi wa kundi kubwa linalo husishwa na ugaidi duniani Al Qaeda Osama bi Laden ameomba hifazi ya kikimbizi nchi Uispania.
Mwana huyo, anaye julikana kwa jina la Omar Osama bin Laden mwenye miaka 27, aliomba hifazi hiyo hivi karinbuni kwa mujibu wa serikali ya Uispania.
MWana huyo ambaye ameoa mwanamke wa kiingereeza, aliwekwa kwenye nyumba za kufikia wakimbizi zilizopo kwenye kiwanja cha ndege cha Barajan International Airport.
Hata hivyo kwa mujibu wa mmoja wa msemaji wa serikali, alisema ya kuwa mtoto huyu wa Osama bin Laden, amesha kataliwa ukimbizi ,a muda wowote ata rudishwa alikotokea.
Picha hapo juu ni ya mtoto wa Osama bin Laden, kwa jina Omar Osama bin Laden kulia akiwa na mkewe Jane Felix Browneau Zaina Muhammad Al Sabah, mapema walipo kuwa wakiongea na waandishi wa habari.

Thursday, November 6, 2008

Demokrasi yaleta historia.

Demokrasi yaleta historia nchini Amerika, Baraka Obama, mwafrika wa kwanza kuwa rais wa Amerika.

Illinois,Amerika-5/11/08. Mgombea urais kupitia chama cha Demokrat nchini Amerika , Baraka Obama amechaguliwa kwa kura nyingi kuwa rais wa nchi hiyo, kwa kumshinda mpinzani wake John McCain wa chama cha Republikan
Kuchaguliwa kwa Baraka Obama kuwa rais wa Amerika, kume weka historia ya nchi hiyo, kwa kuwa rais wa kwanza mwenye asili ya Kiafrika kuwa rais.
Baraka Obama mwenye miaka 47, atakuwa rais wa 44 wa Amerika.
Ushindi wa Baraka Obama, kumeleta hisia tofauti duniani, na amepongezwa na viongozi karibu wote wa dunia.
Picha hapo juu, wanaonekana rais, Baraka Obama akiwa na makamu wake Joe Bidenn wakiwa wanawapungia mikono kuonyesha ishara ya shukurani na kwa wananchi kuwaamini na kuwachagua kuongoza nchini.
Picha ya pili, ni picha ya rais Baraka Obama.
Picha ya tatu, wanaonekana rais, Baraka Obama na mkewe Michelle Obama, wakipiga kura siku ya tarehe 4/11/08,, siku ambayo historia iliwekwa kwa, Baraka Obama, kuchaguliwa kuwa rais.
Picha ya nne,anaonekana rais mpya wa Amerika, Baraka Obama enzi ya utoto wake , akiwa anaendesha baiskeli wakati wa utoto wake, na sasa ameshika uskani wa kuendesha uongozi wa Amerika.
Picha ya tano rais Baraka Obama,akimsikiliza makamu wa rais Joe Biden,hii inaonyesha ya kuwa katika uongozi kusikilizana ndiyo chanzo cha uongozi bora.
Picha ya sita anaonekana rais, Baraka Omaba, akiwa na bibi (nyanya) wakati alipo kwenda kumsalimia kijijini Kogelo alipo zaliwa baba yake nchi Kenya.
Picha ya mwisho, anaonekana rais mpya wa Amerika, Baraka Obama, akiwa na familia yake,toka kulia ni mke wake, Michelle Obama, Malia Ann Obama, na Natasha ( Sacha) Obama, wakiwaamkia wananchi waliokuja kushangilia kwa pamoja kuchaguliwa kwa bwana baraka Obama kuwa rais wa Amerika.