Thursday, January 31, 2013

Izrael yaishambulia Syria.

Harakati za uchaguzi zaanza rasmi nchini Kenya.

Nairobi, Kenya - 31/01/2013. Viongozi wa siasa nchini Kenya wameanza kampeni za uchaguzi kupitia vyama vyao tayari kujiandaa kwa uchaguzi mkuu utakao fanyika Machi 4/ 2013.
Harakati kubwa za uchaguzi zitakuwa ni katika kinyang'anyiro cha kiti cha urais ambapo kamati ya uchaguzi imeyapitisha majina ya  waziri mkuu Raila Odinga na Uhuru Kenyatta  kuwa baadhi ya wagombea wa kiti cha urais.
Uchaguzi wa viongozi hao umekuja baada ya rais wa sasa Mwai Kibaki kumaliza muda wake kama rais wa Kenya.
Odinga amemchagua makamu wa rais Kalonzo Musyoka kuwa makamu wake na Uhuru Kenyatta amemchagua waziri wa elimu William Ruto kuwa makamu wake.
Wakiongea kwa nyakati tofauti Raila Odinga na Uhuru Kenyatta walisema " tunatumaini uchaguzi utakuwa wa haki na yale yaliyo tokea 2007/2008 hayatatokea tena."

Izrael yaishambulia Syria.

Damascus, Syria - 31/01/2013. Serikali ya Syria imetishia kuchukua hatua kali dhizi ya Izrael.
Tishio hilo la serikali ya Syria limekuja baada ya ndege za kijeshi za Izrael kufanya mashambulizi ndani ya Syria.
Kwa mujibu wa serikali ya Syria, ndege nne za kijeshi za Izrael zimefanya mashambulizi karibu na jiji la Damascus na kuua watu wawili na watano kujeruhiwa.
Kufuatia mashambulizi hayo, jumuiya ya nchi za kiarabu limelaani kitendo hicho kwa kusema ni kinyume  na sheria za kimataifa na kuizaraurisha jumuiya hiyo.
Hata hivyo habari kutoka Washington zimethibitisha yakuwa ndege za Izrael zimeshambulia msafara wa kijeshi nchini Syria.
Nayo Iran imeunga mkono serikali ya Syria kwa kudai ya kuwa ipo bega kwa bega na serikali ya Syria na  ipo tayari kutoa msaada wa kila hali kwa Syria.
Hata hivyo serikali ya Izrael haijathibitisha mashambulizi hayo.

Wednesday, January 30, 2013

Seneta John Kerry kuchukua kiti cha Hillary Clinton.

 Seneta John Kerry kuchukua kiti cha Hillary Clinton.


Washington, Marekani - 30/01/2013. Wabunge wa seneta la Marekani wamepiga kura kwa wingi na kupitisha jina la Seneta John Kerry kwa wingi wa kura 94-3 na kumpa nafasi ya kuwa waziri wa mambo ya nje wa Marekani.
John Kerry 69, ambaye alisha wahi kugombea kiti cha urais kupitia chama cha demokrasi cha Marekani anachukua nafasi ya bibi Hillary Clinton ambaye alishikilia nyazifa hiyo kwa miaka minne iliyo pita.

Rais wa Misri awasili nchini Ujerumani.

 Bonn, Ujerumani - 30/01/2013. Rais wa Misri Mohammed Mosri amefanya ziara ya kikazi nchini Ujerumani katika harakati za kutaka kuijenga nchi yake kiuchumi na kutafuta uvumbuzi wa changamoto ya  kisiasa iliyopo nchini mwake.
Akiongea baada ya kumkaribisha mgeni wake, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel  alisema " wanachi wa  Misri wanatakiwa kukaa katika meza ili kusuruhisha changamoto ya kisiasa iliyopo nchini humo.
Naserikali ya Ujerumani itachangia kwa hali na mali mpaka wananchi wa Mirsi wanapata demokrasi kamili.
Rais Mohammed Mosri amefanya ziara hiyo siku chache baada ya kutangaza hali ya tahadhali ili kurudisha usalama na amani nchini Misri. na kudai yakuwa hakutakuwa na serikali mpya hadi hapo kipindi cha uchaguzi wa wa wabunge kitakapo fika.

Tuesday, January 29, 2013

Iran yafanikwa kutuma nyani mwezini.

Hali ya amani nchini Misri yazidi kuwa tete.

 Ismailia, Misri - 29/01/2013. Waelfu ya wakazi wa mji wa Ismalia  wamekiuka amri ya serikali iliyo wataka kukaa majumbani kwao ili serikali iweze kukabiliana na vurugu zinazo endelea nchi Misri.
Wakazi hao wa mji wa Ismailia na mji wa Suez Kanal walipinga na kuvunja amri hiyo huku wakidai ya kuwa wanacho taka ni haki zao kwani " wamesha tuonea vya kutosha wameua watoto zetu, wake zetu na hali inazidi kuwa mbaya kila kukicha"
Navyo vyama vya upinzani nchini humo vipepinga vikali hatua hizo za serikali za kuweka dharula yakiusalama katika miji hiyo. 
Rais wa Misri Mohammed Musri alitangaza hali ya dharula ya liusalama katika miji yote ambapo vurugu zinaendelea.
Nchi ya Misri imekuwa na wakati mgumu kiamani tangu kufanyaka maandamano ya liyo mtoa rais Husni Mubaraka.

Waethiopia wapigwa sindano za kuzuia kuzaa kwa wingi  chini Izrael.


 Jerusalemu, Izrael - 29/01/2013. Waziri wa afya wa Izrael amekubali ya kuwa serikali ya Izrael imekuwa ikiwachoma sindano za uzazi wa majira wageni wa Kiithiopia ikiwa ni katika harakati za kudhibiti ongezeko la wahamiaji.
 Kukubali huku kwa serikali ya Izrael kumekuja baada ya gazeti la Haaretz kuandika habari hizo kufuatia maelezo na malalamiko yaliyo tolewa na shirika la kufuatilia haki za binadamu likujulikanalo kama Association for Civil Right in Izrael (ACRI) kuitaka sererikali isimamishe mara moja zoezi hilo, kwa kudai ya kuwa wakinamama wanako pigwa sindano hizo hawajui madhara yake hya hapo baadaye.
Sindano hiyo inayo julikana kwa jina la Depo-Provera imekuwa ikitumika kuwadunga wakina mama wa Kiithiopia na wakina mama wanao tumia dawa hiyo huwa wanatakiwa kupiga sindano hiyo kila baada ya miezi mitatu.
Kwa mujibu wa wachunguzi wa kisayansi dawa hiyo aina ya Depo- Provera huwa inaleta madhara ya  kuumwa na kichwa, kupoteza nywele, mzunguko wa kike kutokuwa wa kawaida, kupungukiwa uzito  na ngozi kuwa na madhara.

 Iran yafanikwa kutuma nyani mwezini. 

  Tehran, Iran - 29/01/2013. Wana sayansi wa Iran wamefanikwa kutuma nyani mwezini ikiwa ni moja ya matayarisho ya kutuma binadamu kwenda mwezini ifikipo 2019.
Msemaji wa kisayansi wa Iran alisema " hii ni atuha muhimu katika maendeleo ya kisanyansi nchini Iran na kila tukifanyacho ni kwaa ajili ya matumizi ya Wairan na binadamu wate kwa ujumla na tunashukuru nyani huyo amewasili bila matatizo yoyote."
Kufuatia kitende hicho, baadhi ya mashirika ya kimataifa yametilia wasiwasi kwa kudai ya kuwa ni kitendo kilicho kiuka sheria za kimataifa.
Marekani na washiriki wake wamekuwa wakitilia mashaka kuhusu mpango mzima wa Iran katika maswala ya kinyuklia kwa kudai "Iran inampango wa kutengeneza bomu la nyuklia."

Malkia wa Netherlands kujiudhulu wadhifa wake.

 The Hague, Netherlands - 29/01/2012. Wananchi na wazalendo waishio Netherlands wamepatwa na mishituko  yenye mawazo na maoni tofauti baada ya Malkia Beatrix kutangaza kuachia nyazifa zake za kwa mwanaye Prinsi William-Alexander.
Akiongea kupitia luninga ya taifa huku wananchi, wazalendo na wakazi wanao ishi nchini Netherlands, Malkia Beatrix  ambaye anatimiza miaka 75 siku ya Alkhamisi 31/01/2013 alisema " Nawashukuru kwa kuwa pamoja nami katika kila hali, na leo imefikia wakati wa kuachia kizazi kipya kuiendeleza nchi."
Napenda kuwatangazia ya kuwa tarehe 30/4/2013 mwanangu William-Alexander atachukua kiti cha kifalme.
Netherlands imekuwa na utamaduni wa wafalme kujiudhuru tofauti na nchi nyingine zenye uongozi wa kifalme.







Tuesday, January 22, 2013

Baraka Hussein Obama achukua ofisi kwa mara ya pili.

Washington Marekani - 22/01/2013. Wananchi na wakazi wa Marekani kwa mara nyingine tena walikusanyika ili kushuhudia kuapishwa kwa Baraka Hussein Obama kuchukua kiti cha urais kwa mara ya pili baada yab kushinda uchaguzi mkuu uliyofanyika Marekani mwaka jana.
Baraka Hussein Obama mara baada ya kuapishwa kuwa rais wa Marekani kwa mara ya pili alihutubia taifa  na kusema"Safari yetu haijakamilika mpaka hapo mama zetu, wake zetu, mabinti wentu wataka;po kuwa na haki sawa katika jamii na pia haki kwa kila mtu inatimizwa na kulifanya taifa hili la Marekani kuwa taifa lenye kutoa nafasi kwa kila mtu aishiye nadani ya nchi hii."
Kabla ya kuapishwa mbele ya kadamnasi ya Wamarekani rais Baraka Obama aliapishwa katika Ikulu kwani kisheria siku ya kushika ofisi iliangukia siku jumapili na ikabidi aapishwe ili kukamilisha sheria ya nchi.

Wajerumani na Wafaransa wakumbuka siku mkataba wa ushirikiano kwa nchi zao.


Berlin, Ujerumani - 22/01/1213.Wananchi wa Ufaransa na Ujerumani wanasherekea mkataba uliyowekwa na  uliyo wekwa kati ya viongozi wa nchi hiyo miaka 50 iliyopita.
Mkataba huo unao julikana kama mkataba wa Elysee ambapo ulisainiwa kati ya  rais wa Ufaransa Charles de Gaulle na Kansela wa Ujerumani Konrad Adenauer siku ya tarehe 22 Januari 1963.
Wakiongea katika kuadhimisha sherehe hiyo  viongozi wa Ufaransa na  Ujerumani walisisitiza kuendeleza uhusiano huo na kuhakikisha ya kuwa wanajenga msingi imara kwa kizazi kijapo cha nchi hizo.