Wednesday, May 30, 2012

Charles Tayrol ahukumiwa kukaa jela miaka 50.

Charles Tayrol ahukumiwa kukaa jela miaka 50.



Hague, Uhollanzi - 30/05/2012. Mahakama ya kimataifa inayo shughulikia na kutetea haki za binadamu imetoa hukumu ya kwenda jela  miaka 50  kwa aliye kuwa rais wa Liberia.
Charles Taylor 64, ambaye alikutwa na hatia ya kuhusika katika makosa 11 katika kuwasaidia wapiganaji wa kivita nchi Sierra Leone wakati vita vililivyo piganwa kwa muda mrefu nchi Sierra Leone atatumikia kifungo chake nchini Uingereza
Jaji Richard Lussick akisoma hukumu hiyo alisema " mahakama inakuhukumu kwenda jela miaka 50 kutokana na makosa uliyofanya katika kusaidia ukiukwaji wa haki za ubinadamu.
Hata hivyo baada ya hukumu hiyo kutolewa, wanasheria anaye mwakilisha Charles Taylor amekata rufaa zidi ya hukumu hiyo.

Rufaa wa mwanzilishi wa Wikileaks yakataliwa.

London, Uingereza - 30/05/2012. Mahakama kuu ya Uingereza imikataa rufaa iliyokuwa imeombwa na ya kutaka  mwanzilishi wa Wiki Leak asipelekwe nchi Swiden ili kujibu mashitaka yanayo mkabili.
Rufaa hiyo iliyo katwa na  Julian Assange kwa kupitia wakili wake ilikataliwa na mahakama  ya rufaa
 kwa kusema ni  "azima haki za kisheria kutimizwa."
Kufuatia uamuzi huo wa mahakama, Julian Assange atapelekwa nchi Swiden ambapo anakesi inayo mkabili kujibu baada ya mwanamke mmoja kufungua kesi ya "kuwa Julian Assange alimbaka" jambo ambalo Assange anakanusha kwa kudai  "kesi hiyo imetengenezwa katika mazingira ya kisiasa"
Julian Assange ni mwanzilishi wa mtandao wa WikiLeaks ambao ulichapisha habari za siri za kimataifa na shughuli nyingine za kidiplomasia za Marekani na nchi nyingine tofauti.

 Chama cha Republikan cha pata mgombea urais wa Marekani.

Texas, Marekani - 30/05/2012. Mgombea wa kiti cha urai wa Marekani amepita  bila kikwazo katika baada ya wa wajumbe wa jimbo la Texas kumpa barakan zao.
Mitt Romney ambaye sasa atakuwa mgombea wa kiti cha urais kupitia chama cha Republikan alisema " chama chetu kimeungana kwa nia ya kuweka miaka mitatu iliyo pita ya kindotondoto na ugumu uliyo kuwepo na kuwa tayari kuinua maisha ya Mmarekani kwa kuhakikisha kila mtu anachangia katika kujenga nchi."
Mitt Romney alipitishwa kwa kura 155, ambazo  zimemwezesha kuwa mgombea pekee  wa    chama cha Republikan cha Marekani katika uchaguzi wa urais utakao fanyika hivi karibuni nchini humo.

Rais wa Somalia anusurika na mashambulizi.

Mogadishu, Somalia - 30/05/2012. Kundi la Alshabab limekubali kuhusika na mashambulizi yaliyo fanywa kwenye msafara wa rais wa Somalia nje ya mji wa Mogadishu.
Mtandao ambao unatumiwa na kundi hilo umeto habari na kusema " tumefanya mashambulizi ya msafara kwa na Sharif Sheikh Ahmed ameokolewa na jeshi la umoja wa Afrika kwakutumia  siraha za kigeni."
Mashambulizi hayo ya rais wa Somalia yalitokea wakati alipo kuwa ziarani katika mji wa Afgoye ambo baadhi ya maaskari walinzi wa rais waliumia vibaya.

Sunday, May 27, 2012

Mshukiwa wa kusambaza siri za Kanisa akamatwa.

Matamshi ya Christine Lagard yawasumbua wa Wagiriki.


London, Uingereza -27/05/2012. Mkuu wa shirika la fedha duniani International Monetary Fund (IMF) Christine Lagard ameshutumiwa na kulaumiwa na wanasiasa wa Ugiriki kutokana na kauli aliyo toa kuhusu nchi hiyo katika maswala ulipaji wa kodi za mapato na kutimiza masharti yaliyowekwa na nchi wanachama wa jumuiya ya Ulaya.
Kiongozi wa chama cha Kisoshaliti Eangelos Venizolos alisema  "matamshi ya mkuu huyo kuhusu Ugiriki ni kuwatukana Wagiri.
"Wagiriki tunalipa kodi na hakuna raia wa Ugiriki asiyelipa kodi."
Shutuma hizo zilikuja baada ya Christine Lagard kuseme " mimi ninawasiwasi na Wanchi waliopo  Kusini mwa Jangwa la Sahara barani Afrika kwani wao wanaitaji msaada kuliko wananchi wa Ugiriki"
Matamshi hayo ya mkuu huyo wa shirika hilo la fedha duniani IMF yamekuja  wakati wananchi wa Ugiriki wana wakati mgumu wa kiuchumi huku wakiwa wanajiaandaa na uchaguzi wa serikali itayo takiwa kutimiza masharti ya jumuiya  ya nchi za Ulaya katika kufanya marekebisho ya kiuchumi.


Mshukiwa wa kusambaza siri za Kanisa Katoliki akamatwa.

Vatikan, Vatikan City - 27/05/2012. Ofisi ya makao makuu ya Kanisa Katoliki imetangaza ya kuwa aliyekuwa msaidizi wa Papa Benedikt XVI amekamatwa.
Habari kutoka ofisi ya Kanisa hilo zilisema £Paolo Gabriele 46, alikamatwa mapema wiki hii siku ya Jumatano, baada ya mafaili yenye maelezo ya ambayo yanayo husu Papa Benedikt VXI na shughuli nyingine za kikanisa kukutwa nyumbani kwake."
Mtuhumiwa huyo ambaye alishawahi kufanya kazi katika ofisi za Papa Benedikt XVI mwaka 2006, na wakati huo alikuwa na uwezo wa kuona shughuli zote alizo kuwa anafanya Papa.
Kukamatwa huko kwa Paolo kumekuja baada ya habari za siri za kiofisi za Kanisa Katoliki Vatikani kusaambaa katika vyombo vya habari hivi karibuni.

Nchi za Ulaya Magharibi za agizwa kuondoa vikwazo zidi ya Zimbabwe. 

Harare, Zimbabwe - 27/05/2012. Mkuu wa  maswala ya haki za binadamu  wa umoja wa Mataifa amezitaka nchi za jumuiya ya Ulaya Magharibi, kuondoa vikwazo vilivyo wekwa zidi ya Zimbabwe.
Mkuu huyo Navi Pillay alisema hayo wakati akiwa ziarani nchini Zimbabwe na kudai " vikwazo vilivyo wekwa vinazidi kuwaumiza watu masikini na vinafanya jamii kubwa ya Wazimbwe kushindwa kuimarisha miradi mbalimbali na serkali  inakuwa na wakati mgumu  katika  ajira na kuinua maisha ya watu wenye kuishi maisha ya hali chini."
Zimbabwe iliwekewa vikwazo na nchi za Ulaya Magharibi mwaka 2008, kufuatia matokeo ya uchaguzi wa urais kwa madai ya kuwa  wakati wa kampeni za uchaguzi, wadau na wale wanao muunga mkono rais Robert Mugabe walishiriki katika ukiukwaji wa haki za binadamu.

Viongozi wa makundi ya Kiislaam waungana nchini Mali na kuunda serikali yao.

Azawad, Mali - 27/05/2012. Makundi mawili makubwa ambayo yanapingana na serikali kuu ya  Mali yametangaza kuungana na kuunda serikali ya Kiislam nchini Mali.
Makundi hayo ya kabila la Tuareg la National Movement for the Liberation of Azawad (NMLA) na Ansar Dine  yanayo shikilia  upande wa Mali ya Kaskazini, yalikubaliana kunda serikali hiyo ya Kiislam, baada ya viongozi wa makumndi hayo kukutana.
Kiongozi wa Tuareg  Alghabass Ag Intilla alisema " nimesaini mkataba na kukubali ushirikiano ili kuunda serikali itakayo ongozwa katika maadili ya Kiislam, na tutakuwa nchi huru ya Kiislam."
Makubaliano hayo ya viongozi wa makundi hayo mawili alikutana katika mji wa Gao na kusini mkataba hu.
Nchi ya Mali imekuwa na mvutano wa kisiasa na wakijamii kwa muda sasa tangu mapinduzi yalipo tikea nchi humu hivi karibuni.


Friday, May 25, 2012

Rufaa ya Uhuru Kenyatta na wenzake yakataliwa na mahakama ya Uhollanzi. 

Rufaa ya Uhuru Kenyatta na wenzake yakataliwa na mahakama ya Uhollanzi. 


Nairobi, Kenya - 25/05/2012. Rufaa ya kesi inayo wakabili baadhi ya wanasiasa wa Kenya wanao shukiwa kuhusika na vurugu na mauaji yaliyo tokea nchini Kenya 2008 imekataliwa  na mahakama ya kimataifa inayo shughulikia utetezi wa haki za binadamu iliyopo nchi Uhollanzi.
Rufaa hiyo iliyo kuwa inatafuta uhalali wa mahakam hiyo ya Uhollanzi ilitupiliwa mbali, na kuweka uwezekano wa wanasiasa hao wa kutoka nchi Kenya kushitakiwa.
Watuhumiwa hao ni Uhuru Muigai Kenyatta, ambaye ametangaza kugombea kiti cha urais wakati wa uchaguzi 2013, William Rutto, Francis Muthauri, Joshua Arap Sang wana shutumiwa kwa kuhusika kwa njia moja au nyingine katika ghasi na vurugu zilizo sababisha maisha ya watu 1,200 kupoteza maisha na 600.000 kukosa makazi baada ya mali na makazi yako kuharibiwa kutokana na vurugu hizo.

Serikali yaombwa kuchunguza chanzo cha kifo cha Rashid Yakini.

Lagos, Nigeria - 25/05/2012. aliyekuwa  timu kaptaini wa timu ya taifa ya Nigeria ameiomba serikali ya Nigeria ifanya uchunguzi nini chanzo cha kifo cha aliyekuwa mchezaji maarufu na maili wa timu ya taifa wanchi hiyo Rashid Yakin 49.
Kamptan Segun Odegbami alisema " walimchukuwa kwa wiki tatu na wamemrudisha akiwa marehemu, lazima tujiulize alikuwa wapi katika kipindi chote hiki.
" Hakuna mtu yoyote anasema kwamba aliuwawa, na hakuna maelezo yoyote juu ya kifo chake, haiwezekani mchezaji maarufu wa bara la Afrika afariki bila hata uchunguzuzi wa kifo chake usifanyike?
"Naamini hata huko alipo kwenye kaburi lake, anaomba ukweli wa kifo chake ufahamike na tunacho weza kufanya ni kumwombe kwa  Mola aipumzishe roho yake pema pepono." alimalizia kaptain Segun Odegbami.
Marehemu Rashid Yakini alifariki Mei, 04/ 2012 na alikuwa  mfungaji namba tatu bora  katika mashindano ya kombe la Afrika kwa kufunga magoli 13 na mfungaji bora katika timu ya taifa ya Nigeria kwa miaka mingi kwa kufunga magoli 37. 

Mkutano wa Baghdad kuhusu Iran na nykilia waisha bila muaafaka. 


Baghdad, Irak - 25/05/2012. Mkutano wa uliyokuwa ukifanyika nchini Irak, ili kuzungumzia swala na nyuklia la nchi ya Iran limekwisha bila kufikia muafaka.
Waziri wa mambo ya nje ya nchi wanachama wa nchi za jumuiya ya Ulaya Catherine Ashton akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo alisema " mkutano umekwenda vizuri japo kuwa kuna baadhi ya maswala ambayo yanabidi yaafikiwe kutoka pande zote mbili."
Hata hivyo kwa mujibu  wa habari kutoka mwakilishi wa Iran katika mkutano huo Saeed Jalili alisema " swala la kuitaka Iran kusimamisha uzalishaji wa kinyuklia halita wezekana kwani Iran ina haki ya kufanya uzalisha huo kwa kufuata sheria za kimataifa na Iran inafanya uzalishaji wake kwa matumizi ya kisayansi na siyo kwa ajili ya kutengeneza siraha za kinyuklia."
Mkutano huo uliyofanyika nchi Irak, ulikuwa na mazumuni ya kuendeleza ushawishi wa kuitaka Iran isimamishe uzakishaji wake wa nyuklia, jambo ambalo Iran imekuwa ikilipinga kila kunapo kuwepo na mkutano wa kuzungumzia swala hilo.
Kikao kingine cha kujadili Iran na mradi wake wa kinyuklia unatarajiwa kufanyika nchi Urusi kama ilivyo pendekezwa kabla ya kuisha mkutano hu.

Rais wa Ufaransa afanya ziara ya ghafla nchi Afghanistan.

Kabul, Afghanistan - 25/05/2012. Rais wa Ufaransa amefanya ziara ya ghafla nchini Afghanistani na kufanya mazungumzo na wanajeshi wa jeshi la Ufaransa.
Rais Francois Hollandes alitangaza kwa kusema "  uamuzi wa kutoa jeshi letu nchi Afghanistan ni uamuzi wa nchi na washiriki wetu wa NATO wanalielewa hili bila utata na serikali ya Afghanistan inakubaliana na si bila kipingamizi chochote..
Na majeshi ya Ufaransa yatakuwa yamesha ondoka nchini Afghanistani ifikapo  mwisho wa mwaka huu."
Katika ziara hiyo rais Francois Hollandes amefanya mazungumzo na rais wa Afghanistan Hamid Karzai  ili kujadili ni kwa jinsi gani Ufaransa itasaidia katika kuijenga Afghanistan baada ya kuongoka kwa majeshi ya NATO mwaka 2014 kama ilivyo tangazwa wakati wa kikao cha viongozi wa NATO kilicho fanyika Marekani hivi karibuni.

Kifungo cha Muuguzi cha sababisha Marekani kusimamisha msaada wa fedha kwa Pakistani.


Washington, Marekani - 25/05/2012. Kamati ya bunge la Marekani linalo shughulikia maswala ya utoaji misaada imepiga kura na kuamua kusimamisha msaada wa kipesa inayo pelekwa Pakistan.
Uamuzi huo umekuja baada ya hukumu ya kwenda jela kwa miaka 33 aliyo pewa muuguzi  Shakil Afridi kwa kutoa habari za kisayansi DNA zilizo wezesha kuuwawa kwa kiongozi wa kundi la Al Qaeda Osama bin Laden mwezi Mei 2011.
Mbunge Richard Durbin alisema " Pakistan wanatakiwa watambue hatuna mzaha katika swala la ulinzi  nchi yetu na maslahi yetu, kwani ni kitu cha kushangaza kuona kuwa mtu aliye saidia katika kujua wapi alipo Osama bin Laden anaitwa msaliti."
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Hillary Clinton alisema " kitendo cha kumfunga  Muuguzi Shakil Afridi ni cha kinyume cha sheria na tuta zidisha hoja ya kutaka aachiwe huru, kwa Marekani hatuoni haki ya kufungwa kwake."
Marakani hua inatoa msaada wa kiasi cha $ dola za Kimarakani millioni 33, ikiwa ni moja ya fedha zinazo saidia kati shughuli mbalimbali za kujenga nchi ya Pakistani kiuchumi na kijamii.

Thursday, May 24, 2012

Ugiriki yatakiwa kukamilisha matakwa ya nchi za Umoja wa Ulaya.

Rais wa zamani wa Tunisia huenda akahukumiwa adhabu ya kifo.



Tunisia, Tunis - 24/05/2012. Mwanasheria wa kijeshi ameiomba mahakama kumpa adhabu ya kifo aliyekuwa rais wa Tunisia aliyepinduliwa kutokana na maanamano ya wananchi mwaka 2011.
Mwanasheria huyo aliiomba mahakama kutoa adhabu kali ya kifo kwa  Ben Ali kwa  kusababisha mauaji ya watu 300 katika mji wa Kasserine, Tala, Kairouan na Tajrouine.
Zine al Abidine Beni Ali ambaye alikimbilia nchi Saud Arabia, January/14/2011 na kuachia madaraka, amesha hukumiwa kwenda jela, wakati hayupo nchini Tunisia kwa makoso ya kula rushwa na kutumia mali ya umma vibaya.
Ben Ali ambaye alitawala Tunisia kwa muda wa miaka 23 anashutumiwa kwa kuongoza nchi vibaya, kula rushwa na kuonea wanchi kwa kutumia  vyombo vya dola.

Ugiriki yatakiwa kukamilisha matakwa ya nchi za Umoja wa Ulaya.


Brussels, Ubeligiji - 24/05/2012. Viongozi wa nchi wanachama wa jumuiya ya Ulaya wamemaliza mkutano wao na kusisitiza ya kuwa Ugiriki lazima ikamilishe matakwa mkataba wa mabadiriko ya kiuchumi.
Rasi wa jumuiya ya Ulaya Herman Van Rompuy alisema " tunataka Ugiriki kubakia kuwa nchi mwanachama wa jumuiya ya Ulaya.
"Natunategemea ya kuwa baada ya uchaguzi nchi Ugiriki, serikali itakayo chaguliwa itafanya uamuzi bora ili iweze kusaidiwa kuinua uchumi wa nchi hiyo."
Mkutano huo wa viongozi wa nchi wanachama wa nchi za jumuiya ya Ulaya wamekutana ili kujadili hai halisi ya kiuchumi za nchi wanachama ili kuweka mkakati wa kujikwamua na myumbo wa uchumi uliopo kwa sasa.

Iran yatishia kujitoa katika mazungumzo na nchi za 5+1.

Baghdad, Irak - 24/05/2012. Serikali ya Iran imetishia kujitoa katika mazungumzo yanayo endelea kati yake na nchi za Marekani, Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, China na Urusi yanayo fanyika nchi Irak- Baghdad.
Kwa mujibu wa habari zinasema " nchi hizo tano ambazo ni wanchama wa kamati ya usalama ya umoja wa mataifa zimeshindwa kufikiana na matakwa ya Iran, kwani Iran inadai yakuwa mswada ulio pendekezwa hauna mabadiliko."
Hata hivyo Catherine Ashton waziri wa mambo ya kigeni wa jumuiya ya Ulaya aliongea na mwakilishi wa Iran katika majadiliano ya kinyuklia Saeed Jalili na Catherine Ashton alipo ulizwa nini kiliongelewa katika mkutano huo hakutoa jibu.
Mvutano kati ya Iran na  mradi wake wa kinyuklia na nchi za Ulaya Magharibi umepelekea Iran kuwekewa vikwazo na huku Iran ikidai yakuwa in haki ya kuendelea na mradi wake wa kinyuklia.

anchi wa Izrael wataka wakimbizi wa Kiafrika warudishwe kwao.

Tel-Aviv, Izrael - 24/05/2012. Maelfu ya wananchi nchi Izrael wamenadamana  kupinga kiterndo cha kuongezeka wakimbizi wa Kiafrika nchi humo.
Maandamano hayo ambayo yaliongozwa na  Michael Ben Ari ambaye ni mbuge kupitaia chama cha National  Union Part na Ben-Guir na Baruch Marzel ambao ni waandishi wa habari wenye msimamo mkali wa kisiasa wa upande wa kulia.
Waandamani hao walishika mabango yakupinga na kuilaumu serikali ya Benyamin Tetanyahu kwa kudai ya kuwa haifanyi lolote katika kuwaondoa wakimbizi nchini humo.
Izrael imekuwa na wakimbizi kutoka Sudan ya Kusini ambao wengi wao wameishi kwa muda mrefu nchini Izrael.

Ndege aina ya drone kutumika katika kuzuia ghasia.

Texas, Marekani - 24/05/2012. Polisi nchini Marekani wataweza kutumia ndege aina ya drone katika kutuliza ghasia.
Randy McDaniel ambaye ni mmoja wa  maafiasa wa polisi Texas alisema " hii itasaidia kuimarisha usalama hasa wakati wa vurugu."
Catherine Crump ambaye ni mfanayakazi wa American Civil Liberties Union alisema 2 halitakuwa jambo la busara ikiwa  ndege hizo zitaanza kutumika, kwani zinaweze leta madhara makubwa tofauti na polisi wa kawaida ambao huwa wapo katika matukio."
Ndege hizo aina ya drone zitakuwa na uwezo wa kubebe mabomu ya machozi na risasi zenye raba ambazo maranyingi utumika katika kuzuia ghasia.

Wednesday, May 23, 2012

Muuguzi aliye husika katika kifo cha Osama bin Laden afungwa jela miaka 33.

Urusi yazidi kujimarisha kiulinzi.


Moscow, Urusi - 23/-5/2012. Urusi imefanikiwa kurusha siraha ( bomu) linalo julikana kama intercontinental ballistic missile ambayo inauwezo wa kupambana na kubomoa siraha ya ina yoyote.
Habari kutoka wizara ya ulinzi ya Urusi zilisema " majaribio hayo yalifanyika kwenye eneo la Plesetsk."
Jaribio hilo la Urusi limekuja wakati Marekani inajadili mpango wa kuweka mitambo yake ya kiulinzi katika bara la Ulaya, jambo ambalo Urusi bado haijahafikiana na Marekani katika swala hilo.
Hata hivyo Marekani imekuwa ikisisitiza ya kuwa mitambo hiyo ya kiulinzi ni kwa ajili ya kuzilinda nchi wanacham wa NATO.

eshi la JM ya Kongo lapata wakati mgumu wa kulinda nchi.
Kinshasa, Jamuhuri ya Kidemokrasi Kongo - 23/05/2012. Jeshi la Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, limelaumiwa kwa kutotimiza kiapo cha kulinda wanchi kikamilifu.
Moja wa msemaji wa shirika linalo toa msaada kwa wakimbizi ( hakutoa jina) alisema " wanajeshi wa JM ya Kongo wanakuwa na wakati mgumu kutokana na kukusa mishahara na hata mishahara yenyewe ni midogo jambo jambo ambalo linawafanya kushindwa kutimiza swala la ulinzi wa raia na nchi.
"Vifaa vya kijeshi ambavyo wanatumia ni duni kulinganisha na vya kundi la upinzani linalo ongozwa na Bosco Ntaganda na wenzake ambao wanapingana na serikali ya Kinshasa inayongozwa na rais Joseph Kabila. 

Swala la Irani kuwa na nguvu za kinyuklia wa bado mvutano.

Baghdad, Iraq - 23/05/2012. Mkutano uliyo wakutanisha viongozi wa jumuiya ya kimataifa kutoka Ujerumani, China, Uingereza Urussi na Marekani wamekutana na viongozi wa Iran illikujadili kiundani kuhusu swala Iran kuwa na nyuklia.
Waziiri ambaye anashughurikia maswala ya nje ya nchi za jumjuiya ya Ulaya Catherine Ashton aliwakilisha muswada kwa viongozi wa Iran.
Hata hivyo shirika la habari la Iran IRNA limesema " muswada ambao umeletwa na Catherine Ashton hauna mageni na hauangalii faida za pande zote mbili na lazima ieleweke ya kuwa  pande zote mbili zifikie makubaliano ambayo yanafaida kwa nchi zote."
Iran imekuwa ikivutana na jumuiya ya kimataifa katika swala la haki ya nchi hiyo kuwa na uwezo wa nguvu za kinyuklia.

Muuguzi aliye husika katika kifo cha Osama bin Laden afungwa jela miaka 33.

Peshawar, Pakistan - 23/05/2012. Muuguzi ambaye alitoa uchunguzi wa kisayansi -DNA za aliyekuwa kiongozi mkuu wa kundi la Al Qaeda amehukumiwa kwend jela miaka 33.
Shakeel Afridi amakutwa na hatia ya kuhusika katika kufanya uhaini kwa kutoa habari za kisayansi ambazo nikinyume na sheria ya Pakistan
Mwezi January waziri wa ulinzi wa Marakani Leon Panetta alisibitisha kwa kusema " Afridi amekuwa mfanyakazi wa idara ya upelelezi ya Marekani CIA   kwa kutoa habari za kisayansi DNA ili kumjua na kumtambua aliyekuwa kiongozi wa kundi la Al Qaeda Osama bin Laden."
Shakeer Afridi alikuwa muuguzi wa kuheshimiwa na likamatwa wiki mbili baada ya kifo cha Osama bin Laden kufanywa na jeshi maalumu la Marekani.

Wamisri  wapiga kura  kumchagua rais wa nchi.

Kairo, Misri - 23/05/2012. Wananchi wa Misri wapiga kura leo ili kumchagua rais atakayeongoza nchi hiyo.
Uchaguzi huo wa rais wa Misri unafanyika kwa mara ya kwanza kushiriisha vyama vingi au uchaguzi wa kidemokrasia tangu kuangushwa kwa rais Husni Mubarak ambaye litawala Misri kwa miaka 30.
Viongozi wanaogombania uongozi wanatoka katika chama kinachojulikana Muslimu brothorhood, na viongozi ambao walikuwa wakati wa utawala wa rais Husni Mubarak.
Hamdy Abdel Salman ambaye ni mmoja ya mwakilishi wa Morsi alisme "  hadi kufikia sasa kila kitu kipo sawa japo kuwa watu walikuwa wanalalamika kuwepo kwa mistari mirefu."
Wanchi wa Misri anapiga kura  ili kupata kiongozi atakeye iongoza Misri kwa kufata misingi ya kidemokrasi baada ya miezi 15 kupita bila kuwa na serikali ya kudumu.

Monday, May 21, 2012

Ikulu ya Mali yavamiwa na rais ajeruhiwa vibaya na waandamanaji.

Waafghanistan kukabidhiwa ulinzi na usalama wa nchi yao na NATO 2014.

Chikago, Marekani - 21/05/2012.Viongozi wa nchi wanajumuiya wa nchi za  North Atlantic Treaty Organisation NATO, wamekubaliana kwa pamoja ya kuondoa majeshi ya NATO kuanzia 2013 nchi Afghanistan.
Viongozi hao ambao walikutana nchi Marekani Chikago, na kukubaliana ya kuwa uondokaji wa wanajeshi wa NATO utaanza taratibu naifikapo 2014 majeshi yote yatakuwa yamesha ondoka nchi Afghanistan.
Rais Baraka Obama ambaye alikuwa mwenyeji wa mkutano huo, alisema " nchi za jumuiya ya NATO 27  kuanzia mwaka 2014 swala la usalama wa Afghanistan litakuwa mikoni mwa jeshi Afghanistan, tutatoa misaada ya kimavunzo ili jeshi hilo liweze kuimarika vyema katika kulinda nchi ya Afghanistan."
Uamuzi huo wa viongozi wa wakuu wa NATO utafikisha kileleni vita vilivyo chukua miaka kumu katika kupambana chimbuko la ugaidi lililo kuwa na mizizi nchini Afghanistan. 

Ikulu ya Mali yavamiwa na rais ajeruhiwa vibaya na waandamanaji.

Bamako, Mali - 21/05/2012. Waandamanaji wamevamia Ikulu  ya rais wa  Mali na kumjeruhi vibaya rais wa mpito wa nchi hiyo.
Dioncounda Traore ambaye alikutwa na waandamanaji hao wakati akiwa ofisini na kupigwa hadi kupoteza fahamu na huku waandamanaji wakisema "hatukutaki kuwa rais na hatutaki matwakwa ya ECOWAS."
Msemaji wa hospitali aliyo lazwa rais huyo wa mali  Sekou Yuttara alisema "Dioncounda Traore aliletwa hapa hospitali akiwa hajitambuhi na ameumia vibaya." 
Diocounda Traore alichaguliwa kuongoza nchi katika kipindi cha mpito ili kuunda serikali baada ya makubaliano ya jeshi la Mali ambalo  jeshi lilifanya  mapinduzi ya kumng'oa madarakani rais  Amadou Toumani Toure wezi Machi 2012.

Mazishi ya aliyetumiwa kuangusha ndege ya Pan Am 103 yafanyika leo Trpol.

Tripol, Libya - 21/05/2012. Aliye kuwa mtuhumiwa na kukutwa na hatia  na mahakama ya kuingusha ndege ya Pan AM 103 amefanywa mazishi yake leo baada ya kufariki dunia jana.
Abdel Basset al Megrahi 60, alifariki duni kutokana na ugonjwa wa kansa ambao ulikuwa ukimsumbua kwa muda mrefu tangu akiwa gerezani nchini Scotland.
Abdle Nassar kaka wa marehemu Abdel Basset Megrahi alisema " hali ya ndugu yangu ilianza kuwa mbaya baaday ya kufanyika mapinduzi ya kuing'oa serikali ya Muammar Gaddafi, kwani dawa alizo kuwa nazo ziilibiwa baada ya kuvamiwa na hadi kifo cha Megrahi hakukuwa na mganga wa kumwangalia."
Watu wapatao 100 waliudhuria katika mazishi, na hapakuwepo na viongozi wa serikali ya mpito. 
Abdel Besset Megrahi alizaliwa mwaka 1952 na alisoma Marekani na kuishi Uingereza mapema miaka ya 1970.

Wakuu wa serikali ya Iran wakutana na Mkuu wa usimamizi wa maswala ya Kinyuklia duniani.

Tehran, Iran - 21/05/2012. Mkuu wa shirika linalo simamia maswala ya kiatomiki na nyuklia duniani International Atomic Energy Agency IAEA amewasili nchini Iran.
Yukiya Amano aliwasili nchini Iran na kufanya mazungumzo na mkuu wa maswala ya kinyuklia ya Iran Fereydoun Abbas Daveni.
Baada ya  mkutano huo Fereydoun Abbas Daveni alisema "tumefanya mazungumzo yenye uwazi ambao hauna kutiliana mashaka na kufanikisha maendeleo."
Yukiya Amano pia alikutana Saeed Jalili  msemaji mkuu wa maswala ya kinyukia ya Iran na waziri wa mambo ya nje  Ali Akbar Salehi.
Mkuu huyo wa shirika la kusimamia maswala ya kinyuklia ya kimataifa ametembelea Iran kabla ya mkutano utakao fanyika baghdad Irak kati ya Iran na wawakilishi wa jumuiya za kimataifa ili kujadili mpango mzima wa nyuklia ya Iran.

Sunday, May 20, 2012

Mshutumiwa wa mlipuko wa ndege ya Pan Am 103 afariki dunia.

Mshutumiwa wa mlipuko wa ndege ya Pan Am 103 afariki dunia.


Tripol, Libya - 20/05/2012. Raia wa  Libya ambaye alidai ya kuwa hakuwa na makosa ya kuhusika na mlipuko wa ndege ya shirika la Pan Am 103 mwaka 1988 amefariki dunia.
Abdelbeset Ali Mohmed al Megrahi 60, ye alikutwa na hatia na kuhukumiwa kwenda jela  miaka 27 kwa kosa la kuhusika katika ulipuaji wa ndege iliyo kuwa imebeba watu 270 ambapo watu wote walio kuwepo kwenye ndege hiyo walifariki dunia.
Abdulhakimu  ndugu wa  marehemu alisema " Abdelset A.M. Megrahi alifariki saa saba mchana 13:00 kwa saa za Libya."
Abdelbeset Ali Mohamed al Megrahi alihukumiwa kwenda jela mwaka 2001 nchini Scotland na baadaye aliachiwa huru   mwaka 2009 baada ya wauguzi kugundua ya kuwa alikuwa na ugonjwa wa kansa na kuruhusiwa kurudi nchini mwake Libya ambapo ilisadikiwa angeishi miezi mitatu, lakini aliweza kuishi miaka mitatu zaidi.

Vatikani yakumbwa na mtetemo wa uvumi wa habari.

Vatikan, Vatikn City - 20/05/2012. Papa Benedikt XVI ameteua  kamati maalumu ili kuchunguza kashfa za rushwa na matumizi  mabaya ya mzunguko wa pesa ambazo zimeenea hivi karibuni.
Kamati hiyo ambayo itashughulikia kiundani na kupata majibu ilikujua kama upo ukweli wa habari hizo.
Msemaji  wa Vatican Padri Federico Lombard alisema " kusambazwa ka habari hizo kumevunja sheria ya  na hipo haja kufuatilia ili sheria zichukuliwe."
Habari hizo pia  zina aminika kuelezea maisha ya binafsi ya Papa Benedikt VXI.

Mamia wapambana na polisi nchi Marekani.

Chicago, Marekani - 20/05/2012. Mamia ya watu waandamanaji katika jiji la Chicago wamepambana na polisi ambao walikuwa wanawazuia wasielekee kwenye eneo ambalo wakuu wa NATO wanafanya mkutana ili kujadili hali halisi ya shirikisho hilo.
 Kwa mujibu wa habari kutoka kwenye mkutano huo zinasema " moja ya swala muhimu ambalo litajadiliwa ni Afghanistan, "ambapo badhi ya nchi wanachama wa NATO wamesha tangaza kutoa majeshi yao nchini humo.
Katibu mkuu wa NATO Anders Fogh Rasmussen alisema " namatumaini ya kuwa swala la kuisaidia Afghanistan katika kulinda usalama wake litatiliwa mkazo na nchi za NATO, jambo ambalo litakuwa na faida kwa NATO na Waafghanistan."
Kwenye mkutano huo, rais wa Ufaransa Franois Hollande' atakuwa anaudhuria mkutano huo kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa rais wa Ufaransa siku chache zilizo pita.

Chama cha Repabrikan cha Marekani chapitisha nguvu za kivita kwa Iran.

Washington, Marekani - 20/05/2012. Bunge la chama cha Republikan nchini Marekani limepiga kura na kupitisha muswaada wa kuishambulia Iran kama ikionekana usalama wa kinyuklia kwa Marekani.
Kura hizo zilizo pigwa 229 - 120 ambazo ziliunga mkono mswaadahuo.
Kwa mujibu wa katiba ya Mareakani katika maswala ya kiulinzi inasema " sheria  ya uamuzi wa ulinzi na usalama wa taifa itatumika kama ikihitajika katika kulinda usalama ikiwemo matumizi ya nguvu ya kijeshi."
Uamuzi wa bunge hilo umekuja wakati Marakani na Iran wanavutana katika mswala ya Iran kuwa na nyuklia.

Umoja wa Matifa waiwekea vikwazo Guinea Bissau.

New York, Marekani - 20/05/2012. Kamati ya usalama ya Umoja wa Matifa imeiwekea  vikwazo  serikali ya kijeshi Guinea Bissau baada ya kuchelewa kurudisha madaraka katika serikali ya kiraia.
Vikwazo hivyo ambavyo vimewekwa kwa viongozi wa kijeshi kutoweza kusafiri na kuhusishwa katika maswala ya kimataifa kama serikali.
Kamati hii iliamua kwa pamoja kwa kuiwekea Guinea Bissau  vikwazo vya kutoweza kununua siraha na matumizi ya aina yoyote ya kipesa.
Uamuzi huo umekuja kufuatia mapinduzi ya ambayo yamekuwa yakiikumba Guinea Bissau tangu mwaka 1974 tangu kupata uhuru kutoka kwa Wareno.

Saturday, May 19, 2012

Baraka Obama atanga mabilioni ya dola kwa kilimo barani Afrika.

Chelsea ya twaa ubingwa wa kombe la Ulaya kwa mara ya kwanza.

Munich, Ujerumani - 19/05/2012. Chelsea imechukua ubingwa wa kombe vilabu bingwa vya Ulaya kwa mara ya kwanza baada ya kuishinda timu ya Bayern Munich kwa penati 4-3 baada ya dakika 120 kumalizika kwa kila timu kufunga goli 1- 1.
Bayern Munich ilikuwa ya kwanza kupata goli lake kwa kupitia Tomas Muller katika dakika ya 83 na Didier Drogba alisawazisha katika dakika 88, jambo ambalo lilifanya mchezo huo kuisha 1-1 kwenye dakika 90 na baadaye mchezo huo kuendelea kwa kuongezwa dakika 30 za ziada ambapo zilikwisha  1-1 na mchezo huo kuamuliwa kwa penati na Chelsea kuchukua ubingwa wa kombe la Ulaya kwa msimu wa 2012-13.

 Wakuu wa nchi za G-8 wakubaliana Uguriki kubaki ndani ya jumuiya ya Ulaya.

Camp Davis, Marekani - 19/05/2012. Viongozi wa nchi za G-8 wamekutana nchini Marekani  na wamekubaliana kwa pamoja Ugiriki inatakiwa kubakia ndani ya jumuiya ya Ulaya.
Viongozi hao kutoka Marekani, Ujerumani, Japan, Uingereza, Urusi, Ufaransa, Canada na Itali walisema kwa pamoja " tunakubaliana kwa pamoja Greek ibaki katika jumuiya ya Ulaya wakati hali ya kiuchumi ya nchi hiyo kuwekwa sawa."
Viongozi hao ambao wapo nchini Marekani wamezungumzia pia maswala ya Korea ya Kaskazini na Iran, nchi ambazo zinavutana nazo katika maswala ya kinyuklia.

Mabomu nchini Syria yakutwa na mashaka ya kidemokrasia.

Deir az Zor, Syria - 19/05/2012. Mlipuko mkubwa ulitokea baada ya gari moja iliyokuwa imepakiwa mabomu kulipuka  karibu na maenao ya ofisi za usalama wa kijeshi.
Mlipuko huo ambao ulisababisha vifo vya watu wapatao  tisa na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa vibaya na kuharibu majengo pamoja na magari yaliyokuwa karibu.
Habari kutoka shirika la habari la serikali zilisema "mashambulizi hayo ni moja ya mbinu za wapinzani wa serikali wakisaidiwa na Al Qaeda."
Syria imekuwa ikikumbwa na milipuko ya mabomu tangu kuanza kwa mageuzi ya kidemokrasia amboyo yamekuwa yakileta misimamo tofauti kati ya serikali na wapinzani wake.

Rais Malawi kuingalia upya sheria ya kupinga ushoga.

 
Lilongwe, Malawi - 19/05/2012. Rais wa Malawi ametangaza yakuwa serikali yake itaiangalia upya sheria ya kupinga ushoga iliyopoyo pitishwa mwaka 1994.
Joyce Banda alisema baadhi ya sheria zilizopo  zinatakiwa kuangaliwa upya ikiwemo ile iliyo pitishwa kuhusu ushoga."
Pia rais Banda aliongezea kwa kusema " niwakati mgumu uliopo kwa serikali, kwani naogopa yakuwa kuwasili kwa rais wa Sudan Omar al Bashir  mwezi Julai kwenye mkutano wa nchi za Afrika kunaweza kuleta uhasama na nchi wahisani"
Rais Joyce Banda alichukua madaraka kufuatia kifo cha rais Mbingu wa Mutharika, na tangu kuingia madarakani nchi wahisani wameaanza kuendelea kutoa misaada, baada ya kuisimamisha kutokana na kupishana misimamo na nchi wahisani ikiwepo Uingereza.

Baraka Obama atanga mabilioni ya dola kwa kilimo barani Afrika. 

Washington, Marekani - 19/05/2012. Rais wa Marekani ametangaza yakuwa serikali ya Marekani itatoa kisa kikubwa cha pesa katika bara la Afrika ili kusaidia kilimo.
Baraka Obama " nijambo la kiiutu kusaidia bara la Afrika, a hakuna sababu kubwa inayo lifanya Afrika ishindwe kujilisha yenyewe.
"Serikali ya Marekani itatoa kiasi cha  dola za Kimalekani $3billion ambazo zitawezesha kuinua na kuimarisha kilimo bora na kuinua maisha ya wakazi wa Afrika."
Rais Baraka Obama, aliyatangaza hayo kabla ya kuanza kwa mkutano wa wakuu wa nchi G-8 ambao Obama atakuwa mwenyeji wa mkutano huo
Katika mkutano huo, viongozi wa nchi za Tanzania, Benin, Ghana na Ethiopia wamealikwa kushiriki katika mkutano huo.

Thabo Mbeki kujaribu kusuruhisha Wasudani.

Khartoun, Sudan - 19/05/2012.  Aliyekuwa rais wa Afrika ya Kusini amewasili nchini Sudan ili kujaribu kuleta usuruhishi wa kisiasa uliyopo kati ya Sudani Khartoum na Sudani ya Kusini.
Thabo Mbeki anatarajiwa kukutana na rais wa Sudan Omar al Bashir, wakati mapigano kati ya jeshi la Khartoum na Juba.
Sudan ya Kusini na Sudan - Khartoum zimekuwa zikivutana katika swala la mpaka ambao unazikutatisha nchi hizo mbili, ambapo inaaminika kwenye eneo hilo kuna malighafi za asili ambazo ni kiini cha uchumi wa kila upande wa nchi.

Wednesday, May 16, 2012

Charles Taylor adai mashahidi zidi yake walilipwa pesa

Charles Taylor adai walio toa ushahidi zidi yake walilipwa pesa.

Hague, Uhollanzi - 16/05/2012. Aliye kuwa rais wa Liberia na ambaye amekutwa na hatia ya kukiuka haki za binadamu na koti ya kutetea haki za binadamu amelaumu ya kuwa mashahidi walio kuja kutoa ushahidi zidi yake walipwa pesa.
Charles Taylor  64, alisema " Napenda kusema ya kuwa mashahidi walio kuja kutoa ushahidi zidi yangu walipewa pesa/kununuliwa na hata kutishiwa kushitakiwa ikiwa watakataa kuja kutoa ushahidi.
"Sikuwa na hatarisha maisha ya jamii kama inavyo daiwa, bali nilichokuwa najua ya kuwa ikiwa hakuna amani Sierra Leone, basi hata Liberia hakuta kuwa na amani.
"Mimi napinga na kulaani vitendo vyote vya kinyama, na ningependa uamuzi utakao tolewa na majiji uwe wa haki kuzingatia kiapo cha kazi zenu kwani mimi sasa ni mtu mzima na watoto naitwa babu. Vilevile ningependa kutoa masikitiko yangu kwa wale wote walio pata shida wakati wa vita. alisema Charles Taylor
"Japokuwa nipo hapa  inashangaza ya kuwa  viongozi wa nchi za Magharibi ambao wanauzia siraha makundi yanayo pigana kila sehemu na hasa bara la Afrika hakuna hata mmoja wao ambaye amesha wahi kushitakiwa au kushutumiwa kuhusika na vita na huu ndo ukweli wenyewe."
Wakili wa mahakama hiyo aliomba mahakama impe kifungo cha miaka 80 bwana Charlea Taylor
 wakati wa  kuhumu yake  mnomo tarehe 30 mwezi Mei 2012, atatumika kifungo chake nchi Uingereza kutokana  na makubaliano ya awali.
Hata hivyo mwana sheria anaye mwakilisha Charles Taylor alisema upo uwezekano wa kukata rufaa zidi ya adhabu ya kifungo itakapo tolewa.

Jeshi la Umoja wa Ulaya  la fanya mashambulizi nchi Somalia.

Haradhere, Somalia - 16/05/2012. Jeshi la nchi za jumuiya ya Ulaya limefanya mashambulizi kwa ndani ya Somalia kwa mara kwanza tangu kuanza ulinzi katika eneo hilo.
Jeshi hilo ambalo lilisafirishwa na helikopta hadi bandari Haradhere, ambayo inaamini kuwa kitovu cha maharamia ambao huvamia meli zinazo pita katika maeneo ya bahari  karibu na Somalia.
Bile Hussein ambaye ni msemajiwa wa  moja ya makundi ambayo yanashughurika na uharamia alisema " boti zao zenye mwendo wa kasi zilishambuliwa, pia baadhi ya maeneo yatu na vifaa vimeharibiwa vibaya na jeshi hilo la umoja wa Ulaya."
Serikali mpito ya Somalia   nayo ilithibitisha mashambyulizi hayo kwa kusema "mashambulizi hayo yalitokea kwa ushirikiano wa pamoja kati ya jeshi la Somalia na jeshi la umoja wa Ulaya."
maharamia waliopo nchi Somalia wamekuwa wakiziteka nyara meli zinazo pita katika maeneo yaliyopo karibu na bahari ya Somalia, nakusababisha hali ya uslama kuwa mashakani, jambo ambalo lili ifanya jumuiya ya kimataifa kuamua kuweka ulinzi katika maeneo hayo.

Serikali ya China ya chukuzwa na Serikali ya Uingereza.

Beijing, China - 16/05/2012.  Serikali ya China imelaani kitendo cha waziri mkuu wa Uingereza kukutana kiongozi wa kidini wa  Watibeti Dalai Lama.
Habari kutoka ofisi ya mambo ya nje ya China zilisema " kitendo hicho si cha busara na kinaingilia mambo ya ndani ya China na hakitaleta maantiki."
Nazo habari kutoka ofisi ya waziri mkuu wa Uingereza zinasema " waziri mkuu kukutana na Dalai Lama lilikuwa jambo muhimu, lakini wasingependa  swala hilo lilete kutoelewana kati ya China na Uingereza."
Dalai Lama ambaye alikimbia kutoka Tibeti 1959 na kufanya makazi yake Dharamsla India, baada ya jaribio la kutaka kuingausha serikali ya China kushindwa

Mji wa Mombasa wastushwa kwa mlipuko wa bomu.

Mombasa, Kenya - 16/05/2012. Wakazi wa mji wa  Mombasa nchini Kenya walistuliwa na mlipuko wa bomu uliotokea katika bar moja na kusababisha kifo cha mtu mmoja na wengine watano kujeruhiwa vibaya.
Mashambulizi hayo ya bomu yalitokea katika bar ya Bella Vista Club, baada ya watu wenye sirjha kuzuiliwa kuingia ndani na ndipo walipo rusha bomu ndani ya  bar hiyo.
Mkuu wa Polisi Mombasa Aggrey Adoli alismema " watu waliofanya mashambulizi, kwanza walianza kufyatua risasi na kumjeruhi mmoja wa walinzi na baadaye kurusha bomu."
Kenya imekuwa ikishambuliwa na mabomu kwa muda sasa  tangu jeshi la nchi hiyo kuingia nchini Somalia ili kupambana na kundi la Al Shabab ambalo linasadikiwa kushirikiana na kundi la Al Qaeda.

Tuesday, May 15, 2012

Francois Hollande aanza kazi yake urais rasmi leo nchi Ufaransa.

Francois Hollande aanza kazi yake urais rasmi leo nchi Ufaransa.

Paris, Ufaransa - 15/05/2012. Raia wa Ufaransa wapemepata rais mpya kutoka chama cha mrengo wa kushoto  cha Sosialisti tangu miaka 17 iliyo pita.
Francois Hollande ambaye alishinda uchaguzi wa rais hivi karibuni nchini Ufaransa aliapishwa rasmi leo kuwa rais wa Ufaransa baada ya Nicolas Sarkozy aliyekuwa rais kushindwa katika kura za kugombea kiti hicho cha urais wa Ufaransa kwa mara ya pili.
Rais Froncois Hollande alisema haya baada ya kuapishwa " ukurasa mpya umefunguliwa, ningependa kuwaapa huu ujumbe ya kuwa Wafaransa kuweni na imani, sisi ni taifa kubwa na huwa siku zote tuna pambana na kushinda magumu yanayo tukabili, na nahaidi ya kuwa  nitailinda na kuongoza kwa maadili bora ya ukweli, haki na usawa kwa kila Mfaransa."
Ushindi wa Francois Hollande umekuja baada ya kampeni yake kubwa ya kuhaidi kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi nchini Ufaransa kama akichaguliwa kuwa rais wa nchi hiyo.


Luis Moreno Ocampo bado amsaka  Bosco Ntaganda na wenzake.

Hague, Uhollanzi - 15/05/2012. Mahakama ya kimataifa inayoshughulikia kesi za mauji na unyanyasaji wa haki za binadamu ipo mbioni kuhakikisha viongozi wa makundi ya kijeshi yaliyopo JD Kongo  wakamatwe.
Mwanasheria mkuu wa mahakama hiyo Luis Moreno Ocampo alisema " kuna baru ya kutaka Bosco Ntaganda na Sylvestre Mudacumura wakamatwe ili waje wajibu mashitaka ya kuhusika na ubakaji, unyanyasaji na mauji, watu hawa ni hatari saana."
Maoni hayo ya Ocampo yamekuja baada ya habari kupatikana ya mkuwa jeshi la umoja wa mataifa lilipo nchini JD ya Kongo kushambuliwa na na wanachi kwa madai jeshi hilo linashindwa kuwalinda kutokana na mashambulizi yanayo fanywa na makundi ya kijeshi yanayo pingana na serikali ya JD Kongo.
Viongozi hao wakijeshi waliopo nchini JD Kongo wamekuwa wanashutumiwa kwa kuhusika katika uchafuzi wa amani kwa kusababisha mauaji na ubakaji ambao uamekuwa yakitokea kwa muda mrefu sasa.


Muuaji wa mwanasayansi wa Iran anyongwa.


Tehran, Iran - 15/05/2012. Raia wa Iran aliyekutwa na hatia ya kumuua raia mwenzake ambaye alikuwa mwanasayansi wa mambo ya kinyuklia amenyongwa.
Habari kutoka shirika la habari la Iran zilisema "Majid Jamali Fashi ambaye alikutwa na hatia ya kumuua mwanasayansi  Profesa Massoud Ali Mohamed kwa kumtegea bomu mwaka 2010 alinyongwa hivi karibuni.
"Mtuhumiwa huyo ambaye pia alikutwa na hatia ya kuwa jasusi aliyetumiwa na idara ya upelelezi wa Izrael (MOSSAD) na inaamikiwa alipewa kiasi cha dola za Kimarekani $ 120,000 baada ya kukamilisha mauaji hayo."
Hata hivyo Izreal haikutoa maelezo yoyote kuhusu kuhusu huusiano uliopo kati ya Majid Jamali Fashi na MOSSAD kwa kusema "Izrael huwa aijadili au kuongelea maswala ya usalama kinyume na sheria."
Mauaji ya wanasayansi wanao shughuliklia maswala ya kinyuklia yameistusha serikali ya Iran na kutupia lawama  Marekani na Izrael kuwa ndizo nchi zinazo panga mipango ya mauaji ya wanasayansi wake.
Hata hivyo Marekani na Izrael zimekanusha kuhusika na mipango hiyo kwa kudai ni uzushi ambao usiyo na msingi.