Friday, October 26, 2012

Silvio Berluscon haukumiwa kwenda jela.

 Silvio Berluscon haukumiwa kwenda jela.

 Milan, Itali - 26/07/2012. Aliyekuwa waziri mkuu wa Itali amehukumiwa  kwenda jela na kuzuiliwa  kushiriki katika maswala ya kiofisi baada ya kukutwa na hatia ya kukiuka kodi za malipo.
Hukumu hiyo imetolewa baada ya kukutwa kuhusika katika biashara kinyume na sheria.
Silvio Berlusconi ambaye alikuwa waziri mkuu wa Itali, amehukumiwa kwa mara ya kwanza, japo hapo awali alishafunguliwa kesi tofauti zidi yake.
Baada ya hukumu hiyo, Berlusconi alisema "hukumu haina maana na haikufuata haki"
Hata hivyo Silvio Berlusconi  amekata rufaa baada ya hukumu hiyo.

Rais wa Marekani apiga kura mapema.
 
Chicago, Marekani - 26/10/2012. Rais wa Marekani amepiga katika mji wake Chicago ikiwa ni moja ya kampeni za kutaka wapiga kura wajitokeze kwa wingi.
Rais  Baraka Obama, alipiga kura huku kura za maoni zikiwa zimesimama katikati baada ya mpinzani wake  Mitt Romney kujivuta juu katika kura za maoni zilizo tolewa hivi karibuni.
Upigwaji wa kura hizo ni moja ya mpangilio ya uchaguzi uliyopo nchini Marekani.
Mara baada ya kumaliza kupiga kura Baraka Obama, aliendelea na ziara ya kampeni ya kutaka raia wa Marekani kumpigia kura hasa katika  miji ya Ohio Virginia  na Florida.



Sunday, September 9, 2012

Mtoto wa Muammar Gaddafi kuondoka nchini Niger.

Mtoto wa Muammar Gaddafi kuondoka nchini Niger.


Niamey, Niger - 09/09/2012. Mtoto wa aliyekuwa rais wa Libya Muammar Gaddafi anatarajiwa ,kuondoka nchini Niger.
Saadi Gaddafi mtoto ambaye alikimbilia nchini Niger baada ya serikali ya baba yake Muammar Gaddafi kuangushwa na baadaye kuuwawa.
Kwa mujibu wa habari zinasema " Waziri wa mambo ya nje wa Bazoum Mohamed ameshatoa rukhusa kwa Saadi Gaddafi kuondoka nchini Niger."
Habari zilizo patikana zimedai ya kuwa huenda Saadi akaamia nchini Afrika ya Kusini, japo hadi sasa hakuna  habari za huakika kutoka katika serikali ya Afrika ya Kusini.


Moscow yaonya mashabulizi zidi ya Iran.
Moscow, Urusi - 09/09/2012. Waziri wa mambo ya nje wa Urusi ametoa onyo ya kuwa kitendo chochote cha kuishambulia Iran kijeshi kitaleta madhara makubwa.
Akiongela swala hilo makamu wa waziri wa mambo ya ndani y Urusi  Sergey Ryabkov alisema "tunapenda kuonya ya kuwa mashambulizi ya kijeshi zidi ya Iran yataleta maafa makubwa ambayo yatavuka mipaka ya nchi za Mashariki ya Kati,  na napenda kusisitiza suala la Iran na nguvu zakinyuklia nivizuri kujadiliwa katika meza kuliko kutumia nguvu za kijeshi."
Mazungumzo hayo yamekuja huku nchi za Ulaya na Marekani zikiwa zimezidisha jitihada za kutaka Iran iwekewe vikwazo vya kiuchumi ambavyo vitaifanya nchi hiyo kuachana na mradi wake wa kinyuklia.

Friday, August 24, 2012

 Mauaji yatokea Kusini Mashariki mwa Kenya.
 

Nairobi, Kenya - 24/07/2012. Watu 48 wameuwawa na wengine kujeruhiwa ikisadikiwa kuwa ni kulipa kisasi kati vijiji viwili vinavyo pakana.
Mauaji hayo yaliyotokea katika eneo la  Reketa katika kijiji cha Tarassa Kusini Mashariki  maili 300 mwa mji wa Nairobi. na kuleta mstuko mkubwa tangu mauaji yaliyotokea miaka minne iliyopita wakati na baada ya uchaguzi mkuu nchi Kenya.
Msemaji wa polisi Chifu  Joseph Kitur alisema " watu walifariki kwa kukatwa na mapanga na wengine kuchomwa moto na pia nyumba zao kuchomwa moto jambo ambalo mpaka sasa bado tunalifanyia uchunguzi nini hasa kilifanyika hapo awali na kufikia kufanyika muaji ya kinyama kama haya."
Hata hivyo mkazi mmoja wa eneo hilo alisema hii mauaji haya yote yametokana na mvyutano wa mifugo kati ya wakazi wa vijiji vya Orma na Pokomo.

Angela Merkel na Antonis Samaras wakutana kujadili hali ya Ugiriki.
 
Berlin, Ujerumani - 24/08/2012.  Waziri mkuu  wa Ugiriki amekutana na Khansela wa Ujerumani katikaharakati za kutaka kujua ni kwa kiasi nchi ya Ugiriki inavyo fuata masharti ya kuimarisha uchumi.
Waziri Mkuu Antonis Samara na  Khansela Angela Markel walikutana na kujadili ni kwa kisi gani nchi za Jumuiya ya Ulaya zitashirikiana katika kuhakikisha Ugiriki inarudisha uimara wa uchumi wake.
Antonis Samara akiongea alisema " tunataka kuwahakikishia wenzetu tutafanya kila njia kuhakikisha uchumi wa Ugiriki unakuwa na tunachoomba ni muda zaidi."
Naye  Khansela Angela  Merkel alisema" naimani Ugiriki itatimiza yote yanayo takiwa ili kukuimarisha uchumi wa nchi hiyo na kutokana kwa kufuatia  makubaliano iliyo yafanya na nchi za jumuiya  Ulaya na ukizingatia Ugiriki ni nchi ambayo kwa upande wangu ni mwanachama wa nchi za jumuiya ya Ulaya na ningependa ieleweke kuwa naunga mkono nchi ya Ugiriki kubaki kuwa mwanachama wa nchi za jumuiya  Ulaya .
Nchi ya Ugiriki imekuwa nawakati mgumu katika haarakati za kutaka kuinua uchumi wake baada  ya kupewa mkopo wa pesa kutoka nchi za jumuiya za Ulaya na kutakiwa kufanya mrekebisho ya kiuchumi jambo ambalo limekuwa likileta msuguano kati ya serikali na wanchi wake.
  
Aliyefanya mauaji nchini Norway haukumiwa miaka 21 jela.

Oslo, Norway - 24/08/2012. Mahakama nchini Norway imemuhukumu kwenda jela mshitakiwa aliyehusika katika mauaji ya watu 77 na kufanya ushambulizi kutumia mabomu katika jiji la Olso.
Anders Breivik ambaye aliwavamia vijana waliokuwa katika kisiwa cha Utoya kwa ajili ya  mkutano wa kuhamasisha siasa na kuanza kuwapiga risasi amehukumiwa miaka 21 jela baada ya kukutwa na hatia ya kufanya makosa hayo.
Akiongea baada ya hukumu, mshitakiwa Anders Breivik alisema " nasikitika kwa wale wanachama wenzangu kwa kushindwa kufanya mauaji zaidi wakati ule."
Anders Breivik ambaye alidai ya kuwa ni mwanachama wa Temple Knight na alifanya mauuaji hayo kwani alikuwa anapinga kuwepo kwa wageni na kukua kwa dini ya Kiislaaam nchi Norway na Ulaya.. 


Tuesday, August 21, 2012

Waziri mkuu wa Ethiopia aaga dunia.

Waziri mkuu wa Ethiopia aaga dunia.

Addis Ababa, Ethiopia - 21/08/2012. Wananchi wa Ethiopia wameaanza maombelezi baada  ya waziri mkuu wa nchi hiyo Meles Zanawi kufariki nchini Belgium kwa matibabu.
Msemaji wa serikali   Simon Bereket  akiongea baada ya habari za kifo cha Meles Zanawi alisema " makamu wa waziri mkuu Hailemariam Desalegn ataogoza hadi hapo uchaguzi mwingne mwaka  2015."
Waziri mkuu Meles Zanawi  alifariki dunia alipokuwa katika matibabu nchini Belgium na alichukua madaraka ya uongozi baada mapinduzi yaliyopelekea kuangushwa kwa Haile Mariam mwaka 1991.

 Sergie Lavrov aonya mashambulizi zidi ya serikali ya Syria.

Moscow, Urussi - 21/08/2012. Urussi imeonya na kusema kitendo chochote cha kufanya mashambulizi nchini Syria hakitakubalika.
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Urussi Sergie Lavrov aalionya kwa kusema " haitakiwi kuingilia maswala ya ndani ya nchi huru yoyote ikiwemo Syria, na nikinyume na sheria za kimatafa na nimekuwa nasisitiza hilo kila wakati na naonya ya kuwa kitendo chochote cha kuishambuli Syria kitaleta maafa katika jamii nzima ya maeneo hayo."
Waziri Sergie Lavrov aliyasema hayo baada ya kauli ya rais Baraka Obama kudai kuwa upo uwezekano wa nguvu za kijeshi kutumika ikiwa serikali ya Syiria itatumia siraha za sumu zidi ya wapinzani wanaopigana vita na serikali ya rais Bashar al Assad.

Waliotenda makosa ya jinai kunyongwa hivi karibuni asema rais wa Gambia.

Banjul, Gambia - 21/08/2012. Rais wa Gambia ametangaza kuwa watu wote waliukumiwa kunyonwa nchini humu watapata adhabu hiyo ufika mwezi wa Septemba.
Rais Yahya Jammen akiongea katika siku kuu ya kuadhimisha mwisho wa mfungo wa mwezi wa Ramadhani alisema." ningependa kuthibitisha  ya kuwa wale watu waliohukumiwa vifo baada ya kukutwa na makosa kama ya uuaji, ubebajiwa wa madawa ya kulevya, ushoga, na makosa mengine ya jinai basi adhabu zao zitatekelezwa kwa mujibu wa sheria za nchi inavyo eleza.
""Serikali inabidi kuonyesha makali yake kwa wale wote ambao wanakiuka sheria na kuvuruga amani ya nchi  kwa njia moja au nyingine."
Rais Jammen ambaye alichukuwa madaraka mwaka 1994 baada yamapinduzi ya kijeshi na amekuwa akilaumiwa kwa kuongoza nchi kwa vitisho jambo ambalo serikali yake imekuwa ikilikana.

Monday, August 20, 2012

Machimbo ya madini yafunguliwa baada ya mauaji.

Uchaguzi wa rais wa Somalia wakwama.

Mogadishu, Somalia - 20/8/2012. Uchaguzi wa kumchagua rais wa Somalia umesimapishwa kwa mdai yakuwa wananchi wa Somalia hawakuwa tayari kwa upigaji wa kura.
Uchagu huo ambao ulikiwa kufanyaka leo 20/08/2012 umeesimamishwa kwa madai ya kuwa kuna baadhi ya matakwa ya uchaguzi lazima  yatekelezwe kwanza.
Serikali ya mpito iliyopo  ambayo iliteuliwa kwa msaada wa nchi za Ulaya Magharibi inamaliza leo mnuda wake rasmi kisheria.
Kufuatia umuzi huo, uongozi wa nchi ya Somalia utasimamiwa na viongozi 225 walioteuliwa kwa baraka za viongozi wakiasili na kuapishwa rasmi leo.
Somalia nchi ambayo tangu mwaka 1991 imekuwa ikikumbwa na mvurugiko wa amani na kusabisha vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Machimbo ya madini yafunguliwa baada ya mauaji. 

Johannesburg, Africa ya Kusini - 20/08/2012. Machimbo ya madini ya platinum yaliyopo nchini Africay Kusini yamefunguliwa baada ya kufungwa kutokana na vurugu kati ya polisi na wafanyakazi jambo ambalo lilipekea watu 44 kuuwa kutokana na kupigwa risasi. 
Kampuni inayosima mchimbo hayo Lonmin ilisema" machimbo ya Marikana yamefunguliwa na theruthi moja ya wafanyakazi 28,000 wa machimbo hayo wamerudi kazini."
Machimbo hayo ambayo yamekuwa katika habari baada ya mauaji yaliyotokea kati ya polisi na wafanyakazi wa machimbo hayo kutupiana risasi. 
Kufuatia mauaji hayo rais Jacob Zuma ameteua kamati maalumu ili kuchunguza chanzo cha muaji hayo ambayo yametokea tangu serikal ya kibagu ya Afrika ya Kusini kung'olewa.


Izrael kutumia ujumbe wa siku kwa kutoa tahadhali.

Jerusalem, Izrael - 20/08/2012. Serikali ya Izrael imekamilisha na kufanikiwa kutuma ujumbe kwa kupitia simu za mkono kuwajulisha wanachi wake ikiwa kama kunashambulizi lolote la kijeshi.
Zoezi hili ambalo lilifanyika kwa mudawa siku tano nakjuisha hivi karibuni limefanyika huku kukiwa kuna hali ya utata ya kati ya Izrael na Iran nchi ambazo zimekuwa zikilumbana kwa vitisho vya kivita jambo ambalo serikali ya Marekani ikiingilia kati ili kuituliza Izrael baada  ya kutilia mashaka ya kuwa huenda serikali ya Izrael kaamua kufanya mashambulizi bila kushauriana na washiriki wake.
Lakhadar Brahim adai kazi ni kubwa juu ya amani ya Syria.

Algies, Algeria - 20/08/2012.  Mkuu mpya ambaye ameteuliwa kusimamia uletwaji wa amani nchi Syria amesisitiza yakuwa kazi kubwa iliyopo ni kuhakikisha amani inarudi nchini  Syria.
Lakhdar Brahimi ambaye ni raia wa Algeria alisema "kwa sasa nchini Syria kuna vita vya wenyewe kwa wenyewe na inahitaji kazi ya ziada ilikuweza kusimisha vita hivyo kwa jirani anamuua jirani yake na wakati mwingine kaka namuua kaka yake."
Hata hivyo waziri wa mambo wa mambo ya nje wa Syria amekanusha madai ya  Lakhdar Brahim
na kusema "serikali ya Syria ina pambana na magaidi ambao wanasaidiwa na nchi zenye kutaka serekali ya iondoke madarakani na kuweka vibaraka wao ambao watatumikia."
Lakhdar Brahim amechukua nafasi ya Kofi Annani ambaye amejiudhulu katika kazi hiyo ya kusimamia kuleta amani nchini Syria.

Nchi za Amerika ya Kusini zaunga mkono uamizi wa Ekwado kwa Julian Assange.

Quito, Ekuado - 20/08/2012. Mawaziri wa mabo ya nchi za nje wa serikali za Amerika  ya Kusini wameagiza kuanzishwa kwa mazungumzo kati ya serikali ya Ekuado na Uingereza ilikutataua mzozo uliotokea kati ya nchi hizo mbili juu mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks Juliane Asange.
Mawaziri hao kwa pamoja walikubaliana na kuiunga mkono Ekuado kwa uamuzi wake wakumpa hifadhi ya kiutu Julian Assange ambaye anakabiliwa na shutuma za ubakaji nchi Swedeni, jambo ambalo anakusha.
Julian Assange ambaye aliongea kwa mara ya kwanza huku akiwa kasimama katika dirisha la ubalozi wa Ekuado iliyopo jiji London Ungereza ambapo alikimbilia kwa madai upo mpango ukiopo wa kumrudisha nchini Swedeni ni wa kutaka apelekwe nchini Marekani ambapo anadai amefunguliwa mashitaka kwa kutoa habari za kisiri za Marekani katika mtandao wake wa Wikileaks.

Friday, August 17, 2012

Bingwa wa Marathon 2012Londoon apokelewa kwa shangwe nchini.


Bingwa wa Marathon 2012Londoon apokelewa kwa shangwe nchini.

Kampala, Uganda - 16/08/2012. Mwanariadha aliyeshinda mbio za Marathon za michezo ya Olympics London alikalibishwa kwa shangwe na kupewa heshima ya kupata kuonana rais Yoweri Museven.
Stephen Kiprotich aliyeshinda medali ya dhahabu katika mashindo ya michezo Olympics iliyofanyika London, alikaribishwa na rais Yoweri Museven katika chakula ambacho aliandaa kwa ajili ya mwanariadha huyo kwenye Ikulu ya rais ya Entebe.
Rais Yoweri Museven akimkaribisha Kiprotich, alisema' "ningependa kumpongeza kwa ushindi huu, na wale wote ambao wamehusika katika kumsaidia Stephen Kiprotich kuiletea ushindi Uganda."
Stephen Kiprotich  alipewa $800,000 na rais Museven na ameiwezesha Uganda kupata medali ya dhahabu baada ya miaka 40 ambapo marehemu Akii-Bua aliipatia Uganda medali ya dhahabu katika mchezo wa mbio za kuruka viunzi 400 meta.

Wednesday, August 1, 2012

Sweden yaweka ngumu kwenda ubalozi wa Ekuado.
London, Uingereza - 31/07/2012. Serikali ya Sweden imekata ombi la serikali ya Ekuado la kutaka serikali hiyo kuja kumuhoji mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks ambaye yupo ukimbizini kwenye ubalozi wa Ekuado uliopo London.
Julian Assange ambaye ndiye mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks alikimbilia katika ubalozi wa Ekuado baada ya siku zake za rufaa kukaribia kuisha, jambo ambalo linge mfanya arudi jela na huenda angesafirishwa nchi Sweden ili kujibu mashitaka yanayo mkabili ya uubakaji, jambo ambalo Assange analikataa na kulikanusha.
Assange aliamua kuomba ukimbizi ubalozi wa Ekuado uliopo London, baada ya kuhisi ya kuwa kama angerudishwa Sweden, basi angepelekwa nchi Marekani ili kujibu mashitaka ya kuchapisha nyaraka za siri za nchi ya Marekani.

Rais w Syria atakiwa kuachia madaraka.

Tunis - Tunisia - 31/07/2012.Waziri wa ulinzi wa Marekani amemtaka rais wa Syria kuachia madaraka kama anataka kuilinda familia yake.
Leon Panetta alisema " Marekani na jumuiya ya kimataifa hawatavumilia, na inabidi Asad atoke madarakani kwa kuiokoa nchi yake."
"Pia hatutafanya makosa kama tuliyo yafanya nchini Irak, na nia yetu n kuleta amani na uimara wa eneo zima kwa ujumla."
Agizo la waziri Panetta liomekuja wakati akiwa ziarani nchini Tunisia na huku vita kati ya jeshi la serikali la Syria lililo chini ya rais Asad linapambana vikali na jeshi la upinza linalo pata misaada toka nchi za nje.

Wednesday, July 25, 2012

Wananchi Ghana waanza maombelezi baada ya kifo cha rais.

Wananchi  Ghana waanza maombelezi baada ya kifo cha rais.


Akkra, Ghana - 25/07/2012. Wananchi na wakazi waishio nchi Ghana, wameanza maombelezi bada ya rais wa nchi hiyo kufariki baada ya kuugua kwa  muda fupi.
Hayati rais John Atta Mills 68 ambaye alichaguliwa kuwa rais wa Ghana kwa kumshinda mpinzani wake Nana Akufo-Addo kwa kiasi kidogo cha kura mwaka 2008.
Kufuatia kifo cha rais Attap-Mill, makamu wake wa urais John Dramani Mahama ameapishwa kuwa rais wa Ghana kuanzia sasa mpaka hapo uchaguzi wa rais mpya utakapo anza mwisho wa mwaka huu.

Kesi zidi ya makamu wa rais wa Irak yaharishwa.

Baghdad, Irak 25/07/2012. Kesi inayo mkabili makamu wa rais wa Irak na ambaye yupo ukimbizi nchi Uturuki imeharishwa.
Kesi hiyo ambayo inamkabili aliyekuwa makamu wa rais  Tariq al-Hashimi ilihairishwa baaada ya rais wa Irak Jalala Talabani kukataliwa kutoa ushahidi mbele ya mahakama.
Makamu wa rais Hashimi anakabiliwa na kesi ya kuhusika katika mauaji na mateso ambayo amekanusha.

Nchi zajumuiya ya  Ulaya hakuna mafikiano juu ya Hezbollah

Brussels, Ubeligiji - 25/07/2012. Jumuiya ya nchi za Ulaya imelikataa ombi la Izrael la kutak kundi la Hezbollah llilipo Lebanoni kuingizwa katika makundi yanayo husika na ugaidi.
Waziri wa mambo ya nje ya nchi wa Cyprus Erato Kozakou-Marcoullis ambaye nchi yake ndiyo inayoshikilia urais wa nchi za jumiya ya ulaya alisema "kwa sasa hakuna makubaliano ya kuliunganisha kundi la Hezbollah kama kundi la kigaidi."
Waziri Kozakou-Marcoullis aliyasema hayo baada ya Izrael kuzitaka nchi za jumuiya ya Ulaya kuliunganisha kundi la Hezbollah kuwa moja ya makundi ya kigaidi.
Izrael imeilaumu kundi la Hezbollah kwa kuhusika na bomu lililo lipuliwa nchini Bulgaria na kusabababisha vifo vya raia wa Izrael na wengine kujeruhiwa wakati wakiwa matembezini nchi humo.

Saturday, July 21, 2012

Mkuu wa polisi wa Afrika ya Kusini kutolewa jela.

Mkuu wa polisi wa Afrika ya Kusini kutolewa jela.


Johannesburg, Africa ya Kusini - 21/07/2012. Aliyeuwa mkuu wa polisi nchini Afrika ya Kusini na ambaye anatumikia kifungo, anatarajiwa kutolewa hivi karibuni kutoka jela.

Waziri wa magereza wa Afrika ya Kusini Sibusiso Ndebele alisema "Jack Selebi ataachiwa kutaokana na kuwa na matatizo ya figo na mtatizo mengine ya kiafya.
Jackie Selebi 62 alihukumiwa kwenda jela baada ya kukutwa na hatia ya kuopea rushwa mwaka 2010 nakuhumiwa kifungo cha jela miaka 15.
Mahakama ya kimataifa yataka rais wa zamani wa Chad akamatwe.

Brussells, Ubeligiji -21/07/2012. Mahakama ya kimataifa inayoshughulikia makosa ya ukiukwaji wahaki za binadamu ya Ubeligiji, imetaka aliyekuwa rais wa Chad akamatwe ili ajibu mashitaka ya kukiuka haki za binadamu.
Hissene Habre ambaye alikuwa rais waChad, anashitakiwa kwa makosa ya kukiuka haki za binadamu wakati wa utawala wake katika ya miaka ya 1982 - 1990.
Kesi zidi ya Hissene Hebre ilifunguliwa na raia wa Ubeligiji mwenye asili ya Chad kwa madai ya kuwa wakati wa utawala wa  Hissene Hebre watu wapatao 40,000 waliteswa na hata wengine kupoteza maisha.
Hissene Hebre yupo ukimbizini nchi Senegal ambako alikimbilia baada ya utawala wake kuondolewa.
Izrael ya ombeleza vifo vya watu walo fariki na mlipuko wa basi

Burgas, Bulgaria - 21/07/2012. Polisi nchini Bulgaria bado wanatafuta muhusika katika tukio la kulipua basi lililo kuwa limewabeba abiria wa Kiizrael.
Akiongea na waandishi wa habari, waziri wa mambo ya ndani wa  Bulgaria Tsvetan Tsvetanov alisema "hadi sasa tumetambua ya kuwa aliyelipua basi hakuwa raia wa Kibulgaria na uchunguzi bado unaendelea."
Jiji la Burgas lilikumbwa na mshituko mkubwa baada ya basi lililo beba abiria wa Kiizrael kulipuka na kusababisha vifo na majeruhi walokuwa katika matembezi jiji humo.
Kufuatia mlipuko huo serikali ya Izrael imezilaumu Iran na washiki wake kwa kuhusika na mlipuko huo, jambo ambalo Iran imekanusha.

Friday, July 13, 2012

Venezuela yapelek mafuta nchi Syria.

Venezuela yapelek mafuta nchi Syria.


Karakas, Venezuela - 13/07/2012.  Serikali ya Venezeula imepeleka mafuta nchini Syria kufuatia viwazo vilivyo wekewa nchi hiyo.
Uamuzi wa serikali ya Venezuela kupeleka mafuta nchini humo umekuja kutokana na uhusiano uliyopo kati ya nchi hizo mbili.
Habari kutoka serikali ya  Venezuela zinasema  "mafuta yatazidi kupelekwa nchini Syri kma kawaida."
Serikali Venezuela imetumia meli zake za kusafirisha mafuta kufuatia mashirika ya meli na bima za nchi za Ulaya na Marekani kukataa kuzidhamini meli za mafuta zinazo peleka mafuta nchi Syria baada ya vikwazo kuwekwa kwa serikali ya rais Bashar al Assad.

Ruksa kutailiwa kufuatia imani za dini nchini Ujerumani.

Berlin, Ujerumani - 13/07/2012.  Kansela wa Ujerumani ameunga mkono jamii za Kiyaudi na za Kiislaamu zinazo taka kitendo cha kutahiriwa kiendelee katika jamii zao.
Mseamji wa Kansela Angela Merkel, Steffen Seibert alisema " kutailiwa kwa watoto wa kiume ni kitendo ambacho kinakwenda sambamba na imani ya dini hizo na hakuna adhabu itakayo tolewa.
"Na ieleweke serikali inaruhusu haki ya kiimani na Wayahudi na Waislaam ni Wajeruamani hivyo wanahaki sawa na Wajerumani wangine."
Kuungwa mkuno huko kwa kitendo cha kutailiwa kumekuja baaada ya dakitari mmoja kutokutwa na hatia ya kusababisha maumvu kwa mtoto aliye mtairi, ambapo idaiwa mtoto huyo alikutwa na matatizo ya kiafya kutokana kutailiwa huko.
Hata hivyo kitendo cha kutailiwa kimekuwa kinaleta mvutano katika jamii nchi Ujerumani huku wengine wakipinga na wengine wakiunga mkono.

Marekani yaongeza nguvu za kijeshi kanda za Ghuba

Washington, Marekani - 13/07/2012.  Serikali ya Marekani kimeongezea siraha na nguvu za kijeshi katika nchi zenye makao yake ya kijeshi zilizopo katika nchi za Ghuba.
Kwa mujibu wa habari zilizo tolewa zinasema " uamuzi wa serikali ya Marekani kuogeza nguvu zake za kijeshi katika eneo hilo jimekuja katika harakati za kutaka kuizuia Iran isiweze kuzuia ghuba ya Hormuz kama ilivyo tangaza hapo awali."
Iran ambayo imewekewa vikwazo na Marekani na nchi washiriki wake ilitangaza hapo awali yakuwa itafunga njia ya Hormuz ambayo inatumika kusafirisha mafuta kutoka katika nchi zilizopo maeneo hayo.

Sunday, July 8, 2012

George Bush ashiriki ujenzi wa Zahanati nchi Zambia

Roger Federer akata ndoto ya Waingereza.

London, Uingereza - 08/07/2012. Roger Federer amekata ndoto ya Waingereza baada ya kushinda kwa mara ya saba kombe la tenisi la Wimbledon kwa upande wa wanaume.
Roger Feder ameweka kibindoni makombe makubwa 17 (Grand Slam) na kuwa sawa na mchezaji maarufu wa mchezo huo Peter Sampras katika ushindi wa kombe la Wimbledon.
Ushindi huo wa Roger Federer alipata baada ya kumshinda Andy Murry kwa seti 4-6, 7-5, 6-4 jambo ambalo limezima ndoto ya wapenzi wa mchezo wa tenis nchi Uingereza ya kuwa huenda mwaka 2012 ungekuwa wao kwa mchezji  Mwingereza kushinda kombeli hili ambalo kwa mara ya mwisho mchezaji wa Uingereza alishinda mwaka 1936.

George Bush ashiriki ujenzi wa Zahanati nchi Zambia
Lusaka, Zambia- 08/07/2012. Aliyekuwa rais wa Marekani alifanya ziara nchi Zambia na  Botswana ili kuimarisha ufahamu wa ugonjwa wa saratani ( Kansa).
Akiwa nchi Zambia, George Bush, alishiriki katika ujenzi wa  zahanati itakayo toa matibabu ya ugonjwa wa kansa ( saratani) katika mji wa Kabwe na baadaye alizungumza na viongozi wa serikali na viongozi wa maswala ya afya ya Zambia.
George Bush ambaye alisha wahi kufanya ziara barani Afrika, amekuwa akitoa kipao mbele katka harakati za kupambana na magonjwa yanayo tisha ikiwemo ukimwi na malaria katika bara la Afrika tangu alipo kuwa rais wa Marekani na hadi sasa.

Jeshila Bosco Ntaganda lazidi kuteka miji nchi JM-Kongo.


Rutshuru, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo - 08/07/2012. Jeshi la upinzani wa serikali ya JD-Kongo limeteka nyara mjiwa Rutshuru uliyopo km 70 Kusini mwa mji wa Goma baada ya jeshi la serikali kuzidiwa nguvu.
Jeshi hilo la upinzani wa serikali ya Komgo linalo ongozwa na  Generali Bosco Ntaganda,lili chukuwa mji huo muhimu baada ya mapigano makali na jeshi la serikali na baadhi ya wanajeshi wake kukimbilia nchi Uganda.
Wakati huo huo mwanajeshi wa kulinda amani wa umoja wa mataifa kutoka India aliuwawa katika harakati za jeshi laupinzani wa serikali lilipo fanya mashambuli katika mji wa Bunagana.

Rais wa Misri atengua uamuzi wa jeshi la Misri.

Kairo, Misri - 08/07/2012. Rais wa Misri ametengua uamuzi wa jeshi la nchi hiyo kwa kuamuru baraza la bunge la nchi hiyo kurudi bungeni mara moja na kuanza kazi yake ya bunge.
Rais Mohamed Musri alitoa mri hiyo kwa kuvunja amri ya koti kuu ya nchi yakuwa bunge  lazima lirudi kazini mpaka hapo uchguzi mpya utakapo fanyika.
Amri hiyo ya kuvunjwa kwa bunge nchi Mirsi ilitolewa na jeshi wakati lilipo kuwa limeshikilia madaraka baada ya kuangushwa kwa utawala wa rais Hosni Mubarak.
Kufuatia kuvunjwa kwa amri hiyo na rais Mohamed Musri, wakuu wa jeshi nchi Mosri wameitisha kikao cha dharula ili kujadili uamuzi huo wa rais. 

Rais wa Syria aishutumu Marekani.

Damascus, Syria - 08/07/2012. Rais wa Syria ameishutumu Marakani kwa kusababisha vurugu nchi Syria ambazo zinaleta myumbo wa kisiasa, kijamii na kiuchumi.
Rais Bashar al Assad akiongea  alisema " Marekani kwa kusaidiana na Katar na Saudi Arabia wana saidia magaidi  ambao ndiyo chanzo cha vurugu nchini Syria.
" Pia majirani zetu Uturuki wanawapa magaidi hawa waliopo Syria kila msaada wanao uhitaji, na kama hali hii ikiendelea basi magaidi watakuwepo na wapo tayari kushirikiana na Marekani.
"Tumekamata wapiganaji wengiwa kundi la Al Qaeda waliotokea nchini Tunisia na Libya na Marakani inahusika pia katika mauaji ya raia wa Syria."
Wakati huohuo jeshi la Syria limeaanza mazoezi ya kijeshi ili kujua kwa kiasi gani jeshi la nchi hiyo lipo tayari  ikiwa vita vikubwa  vitaanza katika nchi hiyo.

Saturday, July 7, 2012

Afghanistan kuwa mwanachama huria wa NATO.

Serena Williams ashinda Wimbledon kwa mara ya Tano.

London, Uingereza - 07/07/2012. Serena Willliams ameshinda tena kwa mara ya tano kombe la mashindano ya tennis ya Wimbledon.
Serena alimshinda Agnieszka  Rwadwanska kwa 6-1, 5-7, 6-2 na katika mchezo ambao ulikuwa wa vuta ni kuvute.
Ushindi huu Serena Williams wa mara ya tano katika kombe la tennis la Wimbledon  umekamilisha hatua ambayo dada yake Venus alisha wahi kushinda kombe hilo.
Serena Williams ameshinda kombe hilo mwaka 2002,2003,2009, 2010, 2012  na kuwa mmoja ya wacheza tennis kwa upande wa wanawake kushinda kombe tennis la Wimbledon  hilo mara nyingi

Rais wa Afrika ya Kusini achorwa magazetini na sehemu za siri.

Johannesburg, Afrika ya Kusini - 07/07/2012.  Chama tawala nchi Afrika ya Kusini kimelaani kitendo cha mchoraji wa vikatuni wa gazeti la Gurdian na Mail wa Afrika ya Kusini kumchora rais wa nchi hiyo na kuonyesha sehemu zake za siri.
Jonathan Shapiro alichora kikatuni ambacho kinamwonesha rais Jacob Zuma sehemu zake za siri, jambo ambalo limepingwa vikali na serikali ya Afrika ya Kusini.
Kuchorwa huku kwa rais Jacob Zuma kumekuja baada ya siku za nyuma baada ya msaani mmoja kuandaa maonyesho ya sanaa za uchoraji ambapo zilikuwepo picha za zinazo onyesha sehemu za siri  za rais Jacob Zuma.

Jeshi la Iran la tangaza kugundua miali siraha.

Tehran, Iran - 07/07/2012. Jeshi la Iran limetangaza ya kuwa limetengeneza miali siraha ambayo inaweza kuongoza mitambo yake ya kivita.
Waziri wa Ulinzi wa Iran Brigedia General Ahmad Vahidi akiongea na waandishi wa habari alsema " miaali siraha ambayo tumeitengeneza itatusaidia katika kutuongoza kujua adui yupo wapi,kuongoza katika kushambulia siraha ya angani na siraha za aina nyingine.
"Miali siraha hii ni ya kisasa na inauwezo mkubwa na kwa jina ni Dehlavieh na itasaidia katika kuimarisha ulinzi wetu.
Kitendo cha Iran kutangaza kugundua miali siraha hii kumekuja siku chache baada ya jeshi la nchi hii kufanya mazoezi ya kijeshi na kurusha makombora katika harakati za kujua uwezo wa jeshi na nguvu za jeshi hilo.  

Tumbaku bado haijafa thamani yake nchi Marekani.

Kentuck, Marekani - 07/07/2012. Ukulima wa zao la tumbaku umeongezeka nchi Marekani kufuatia mahitaji makubwa ya uvutaji wa sigara.
Katika mji wa Kentuck, wakulima wa mashamba hayo wamekuwa wakiongeza ukulima huo, baada ya faida kuonekana kutokana na mahitaji ya sigara kuongezeka katika bara la Afrika na  Asia.
Hata hivyo wakati mahitaji ya uvutaji wa sigara yakiongezeka katika nchi za Afrika na Asia, barani Ulaya na Marekani uvutajiwa wa sigara umekuwa ukipigwa vita na vyama, mashirika yasiyo ya kiserikali na serikali zenyewe ili kuweza kupunguza vifo vinavyo sababishwa na uvutajiwa wa sigara.

Walibya wapiga kura ya vyama vingi kwa mara ya kwanza.

Tripol, Libya - 07/07/2012. Wanachi wa Libya wamepiga kura kwa mara ya kwanza katika uchaguzi uliyo husisha vyama vingi tangu kuangushwa kwa utawala wa Muammar Gaddafi.
Zaidi ya watu million 2 walijiandikisha kupiga kura ili kuwachagua wabunge 200 ambao wata unda bunge ambalo litakuwa naserikali ambayo itachukua madaraka kutoka katika serikali ya mpito.
Walibya ambao wamepiga kura kuwachagua wabunge wao nakimekuwa ni kitendo ambacho hakijawahi kufanyika zaidi ya miaka 40 iliyo pita tangu Muaamar Gaddafi achukue madaraka.

Afghanistan kuwa mwanachama huria wa NATO.

Kabul, Afghanistan - 07/07/2012. Afghanistan inatarajiwa kuwa mwanachama huria wa nchi za NATO.
Maelezo hayo yalitokewa na waziri wa mambo ya nje ya nchi wa Marekani baada ya kukutana na rais wa Afghanistan.
Hillary Clinton akiongea na waandishi wa habari alisema " uamuzi wa kuikaribisha Afghanistani katika NATO ni moja ya majukumu ya kudumisha uhusiano wa muda mrefu ambao utasaidia katika kujenga serikali ya mpito kuelekea kujenga demokrasi ya kweli na serikali imara ya  Waafghanistan."
Maelezo hayo ya waziri wa mabo ya nje wa Marekani Bi Hillary Clinton yamekuja wakati Marekani na washiriki wake katika NATO wakiwa katika harakati za kuondoz majeshi yao nchi Afghaniztani ifikapo mwaka 2014.
Nchi nyingine ambazo ni wanachama huria wa  NATO ni Pakistan, Izrael, Misri, Japan, Jodan, Korea ya Kusini, Australia na New Zealand

Thursday, July 5, 2012

Urusi yakanusha kuwa rais wa Syria kuchukua ukibizi.

Ligi kuu ya Uingereza kuanza kutumia teknolojia ya goli line.

London, Uingereza - 05/07/2012. Shirikisho la Soka Duaniani FFA limekubaliana kwa pamoja yakuwa teknolojia inayo julikana kama Hawk eye ya kutumia mtandao katika kuhakikisha mpira umevuka mstari wa goli inatumika.
 Kufuatia uamuzi huo wa FIFA, chama cha mpira nchi Uingereza kimeamua kuanzia msimu wa ligi wa mwaka 2012/13 teknologia hiyo itaanza kutumika.
Uamuzi wa kutumia teknolojia hiyo umekuja baada yamechi kati ya Uingereza na Ukraine kuleta matata ya umuzi wakati Ukraine ilipo pata goli lakini waamuzi wa mechi hiyo hawakona kama goli lilikuwa limeingia.

Urusi yakanusha kuwa rais wa Syria kuchukua ukibizi.

Moscow, Urusi - 05/07/2012. Serikali ya Urusi imekanusha uvumi iliyokuwa umevuma ya kuwa rais wa Syria  Bashar al Assad anampango wa kuchukua ukimbizi nchini humo.
Waziri wa mambo y kigeni wa Urusi Sergei Lavrov alisema " hakuna kitu kama hicho na wanaovumisha habari hizo wana njama zao binafsi na inaelekea wanaupungufu wa uelewa wa hali halisi."
Uvumi huo ya kuwa Urusi inampango wa kumpa rais wa Syria ukimbizi umekuja baada ya China na Urusi kuwa kinara katika kutetea serikali ya rais Bashar al - Assad ambayo inapingwa na nchi za Ulaya Magharibi na Marekani.

Wikileaks yachapisha habari za siri za Syria na washiriki wake.

London, Uingereza - 05/07/2012. Wikileaks imetoa mafaili yenye habari za nchi ya Syria na jinsi ilivyo jihusisha na nchi nyingine kisiasa, kiuchumi na kibiashara tangu mwaka 2006 hadi 2012.
Msemaji wa Wikileaks Sarah Harrison akiwakilisha maelezo ya Julian Assange aliseme " maelezo yaliyopo kwenye mafaili hayo yataleta aibu kwa serikali ya Syria na wale wanaojiita wapinzani wa Syria.
"Na itasaidia kuelewe ni kwa kiasi gani ukweli uliyopo na  ni kwanini vita vimetokea nchi Syria.
Wikileaks imelipa jina tukio hil kama " The Syria Files" na kudai ya kuwa kuna mafaili  zaidi ambayo yatafuta ikiwa ni mpango wake wakuchapisha habari hizo ambao ulianza 2010.

Tuesday, July 3, 2012

Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat watoa majibu nusu.

Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat watoa majibu nusu.

Paris, Ufaransa - 03/07/2012. Uchunguzi wa kisayansi uliyofanywa kuhusu kifo cha aliyekuwa kiongozi na rais wa Wapalestina umetoa majibu nusu tangu kuanza kwa uchunguzi huo.
Rais Yasir Arafat ambaye alifariki dunia nchini Ufaransa ambapo alipelekwa kwa ajili yamatibabu baada ya kuugua wakati akiwa amefungiwa  kutoka katika mji wa Ramallah na serikali Izrael.
Dr Francois Bochud ambaye ni mtaalamu wa Radiophysique iliyopo nchini Switzerland alisema " naweza kusema tumekuta aina ya gesi inayo julikana kama polonium-210 ambayo inaweza kuwa chanzo ca kifo chake na tunaweza kupata jibu sahihi ikiwa baadhi ya viungo vya marehemu Yasir Arafat vitapatikana kwa  uchunguzi zaidi."
Uchunguzi wa kifo cha Yasir Arafat ulikuja baada ya mkewe Suha Arafat  kuruhusu uchunguzi kuendelea na kutoa ruhusa ya kuwa mwili wa Yasir Araf ufukuliwe kwa uchunguzi zaidi  na kuiomba serikali ya Wapalestina kushirikiana naye.

Iran yadia kupata ufahamu wa ndege ya Marekani waliyo iteka.

Tehran, Iran - 07/03/2012.  Jeshi la Iran limedai ya kuwa limepata uwezo wa kuisoma ndege inayo endeshwa kwa kutumia mtandao (Drone) ambao utasaidi jeshi hilo kiutaalamu.
Brigadia Generali Amir -Ali Hajizadeh aliema " ndege ya Marekani RQ - 170 ambayo tumeikamata itasaidia saana kwani tulicopata ni kitu ambacho maadui zatu hawakuta tukijue."
Maelezo hayo ya mkuu huyo wa jeshi la Iran yamekuja wakati jeshi la nchi hiyo likuwa katika mazoezi ya kijeshi ambayo yameanza hivi karibuni.

Ofisi na nyumba za Nikolas Sarkozy za vamiwa na polisi.

Paris, Ufaransa - 03/07/2012. Ofisi na nyumba anayoishi aliyekuwa rais wa Ufaransa Nikolas Sarkozy zimevamiwa na polisi katika haraki za kufanya uchunguzi zidi ya rais huyo wakati wa kampeni za uchaguzi.
Polisi hao ambao waliaandamana na wapelelezi waiiingia katika ofisi hizo na nyumbani kwa rais huyo na kuchukua baadhi ya mafaili na vitu vingine ambavyo vinashukiwa kuhusika katika uchunguzi huo.
Hata hivyo Nikolas Sarkozy amekanusha kuhusuka na tuhuma hizo na wala hakuhusika.
Uchnguzi huo umekuja ikiwa ni katika harakati za kutafuta ukweli kama kuna kitendo cha rushwa kilitendeka wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2007.


Rais wa Syria hatuta jenga huhasama na Uturuki kamwe.

Iran yazidi kujimarisha kijeshi.

Tehran, Iran - 03/07/2012. Jeshi la mapinduzi la Iran lmeanza mazoezi yake ya kijeshi siku chache kabla ya kuanza rasmi ka vikwazo kwa mafuta ya Iran katika nchi za jumuiya ya nchi za Ulaya.
Katika mzoezzi hayo jeshi la Iran limejaribu siraha zinazo julikana kam ShababMeteor) 1,2,3, Khalij Fars (Persian Gulf), Tondar(Lightning), Fateh (Victor),  Zelzal (Quake) na Qiam(Uprising).
Mazoezi hayo yaklijeshi ya Iran, yanafuati yale yaliyofanywa  mwezi wa Februari ambayo yalijlikana kama Val Farj.
Iran imekuwa ikivutana na nchi za Ulaya gharibi na Marekani kuhusu mradi wake wa kuendeleza nguvu za kinyuklia jambo ambalo hadi sasa halijapagtiwa ufumbuzi.

Kashfa zasabisha mkuu wa beni ya Barclays kujiudhulu uongozi wake.

London, Uingereza - 03/07/2012. Mkuu wa benki kubwa ya tatu nchi Uingereza Barclays, amejiudhulu uongozi wake kufuatia kashfa za benki hiyo kukiuka maadili ya kibenki.
Mkuu huyo Bob Diiamond imembidi ajiuzuru uongozi wake baada ya banki ya Barclays kukutwa na hatia ya kuwalipisha riba wateja wake kinyume na maadili ya kibenki jambo ambalo limeleta msituko mkubwa katika jamiii nzima ya mfumo wa benki unavyo endeshwa nchini Uingeereza.
Kujiudhulu huko kwa mkuu huyo waa benki kumekuja bada ya waziri mkuu wa Uingereza David Cameron kusema" nitaunda tume kupitia bunge ili kuchunguza uarifi huu uliyo tokea katika benki, kwa watu wanataka kujua ukweli na lazima tujifunze hali hi isije klutokea tena."

Rais wa Syria hatuta jenga huhasama na Uturuki kamwe.

Damascus, Syria - 03/07/2012. Rais wa Syria amesikitishwa na kitendo cha kuangushwa ndege ya jeshi la Uturuki wakati ilipo ingia anga za Syria.
Rais Bashar Al Assad alisema " tulijua ni ndege ya Uturuki baada ya kuiangusha, na naomba nieleweke kama tungejua ni ndege ya kijeshi ya Uturuki tusinge iangusha kamwe.
"Na hatutaruhusu uhasama kujengeka kati yetu na Uturuki kwani watu wapande zote mbili wataathirika kijamii na kiuchumi, na sisi hatutaweka jeshi letu karibu na mpaka na Uturuki japo serikali ya waziri mkuu Tayyip Erdogan imeweka jeshi lake mpakani na Syria."
Kuongea kwa rais Bashar al Asssad, kuhusu kuangushwa kwa ndege ya kijeshi ya Uturuki, huku hali kati ya nchi hizo mbili zikiwa katika utata.


Kampuni ya madawa ya Uingereza yapigwa faini.

Massachusetts, Marekani - 03/07/2012. Kampuni ya madawa ya Uingereza imepigwa faini baada ya kujulikana  kuepuka kwa makusudi kutoa maelezo ya dawa zake kwa watumiaji nchini Mareakani.
GlaxoSmithKline, imekubali kulipa kiasa cha dola za Kimarekani $3billion, baada ya kukutwa  na hatia na mahakama iliyopo Massachusetts.
Mwanasheria mwandamizi  wa serikali James M Cole alisema " hatutakubali wala kuachia afya za watu kuchezewa au kufanyiwa mchezo wa kirushwa,na kuanzia sasa hii ni onyo kwa makampuni mengine ya madawa."
Faini hiyo imekuja baada ya dawa zilizo tolewa na GlaxoSmithKline kwa ajili ya watu waliochini ya miaka 18 na kutumiwa kwa wagonjwa waliozidi umri wa miaka 18.