Thursday, February 28, 2013

Papa Benedikt ajiudhuru rasmi uongozi wake wa Kanisa Katoliki.

Papa Benedikt ajiudhuru rasmi uongozi wake wa Kanisa Katoliki.

Vatican City, Vatican - 28/02/2013.Papa Benedikt wa XVI amewaaga rasmi waumini wa Kanisa Katoliki duniani kwa misa maaalumu aliyo iongoza.
Papa Benedikti 85, ambaye amongoza Kanisa Katoliki kwa muda wa miaka nane alitangaza kujiudhuru wadhifa wake huo mwanzoni mwa mwezi huu kutokana na hali ya afya yake kuto mruhusu kuendelea na kazi hiyo ya kuliongoza Kanisa Katoliki lenye waumini wapatao 1.2 billion.
Akihutubia waumini waliokuja kuudhuria misa ya kumuaga, Papa Benedikti alisema "nawatakiwa baraka za Mungu ziwe nanyi na nawashukuruni sana na tuzidi kuendalea katika njia apendayo Mungu."
Papa Benedikti ambaye alizaliwa na kubatizwa kwa jina la Joseph Ratzinger amekuwa Papa wa kwanza  kujiudhuru madaraka yake tangu ilipotokea miaka 600 iliyopita. 

Marekani kutoa kifedha kwa wapinzani wa serikali ya Syria.

 Washington, Marekani - 28/02/2013. Serikali ya Marekani imetangaza kuongeza msaaada wa kifedha kwa kundi linalo pingana na serikali ya Syria.
Akiongea katika mkutano uliofanyika nchi Itali Roma ambao ulijulikana kama mkutano wa marafiki wa Syria. waziri wa mambo ya nje ya nchi wa Marekani John Kerry alisema " kiasi cha dola za Kimarekani $60millioni zitatolewa kwa kundi Syria National Coalition (SNC) ."
"Pesa hizo zitakuwa kwa ajili ya misaada ya kiutu" aliongezea waziri John Kerry.
John Kerry yupo katika ziara za kikazi baada ya kuapishwa kuchukua wadhifa wa waziri wa mambo ya nje ya nchi ya Marekani .
Hadi kufikia sasa maelfu ya Wasyria wamekubwa na hali mbaya kiuchumi na kijamii tangu kuanza vita  vya kutaka kuun'goa utawala wa rais Bashar al Assad.

Tuesday, February 12, 2013

Korea ya Kaskazini yaitikisa dunia kwa kufanikiwa jaribio la nyuklia.

 Pyong Yang, Korea ya Kaskazini - 12/03/2013. Serikali ya Korea ya Kaskazini imetangaza kufanikiwa  katika jaribio la kulipua bomu la kinyuklia.
Kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya Korea ya Kaskazini zimesema " tumefanikiwa katika jaribio la kinyuklia  ambalo lilifanyika chini ya ardhi na tumetumia teknolojia ya kisasa na yenye ujazo mdogo."
Jaribio hili ni la tatu, na kiongozi wa Korea ya Kaskazini amesema "majaribio mengine kama hayo yatafuata."
Idara ya sayansi na nyuklia ya umoja wa mataifa iliyopo Vienna imesibitisha  kuwepo kwa mlipuko mkubwa  kuliko ile wa kwanza 2009 ambao ulifanywa na serikali ya Korea ya Kaskazini.
Kufuatia kufanikiwa kwa serikali ya Korea ya Kaskazini, kamati ya usalama ya umoja wa mataifa imeitisha mkutano wa dharula mjini New York ili kujadili kitendo hicho cha Korea ya Kaskazini.

John Kerry akaribishwa  kitendawili cha Iran.

 Washington, Marekani - 12/03/2013. Waziri wa mambo ya nje wa Marekani ameitaka Iran  kusimamisha mpango wake wa kuendelea kuzalisha nyuklia.
John Kerry ambaye amechukua nafasi iliyo achwa wazi na Hillary Clinton alisema " jumuia ya kimataifa ipo tiyari ikiwa Iran itakuwa tayari kwa mazungumzo."
Mazungumzo hayo ya John Kerry yamekuja baada ya Marekani kuona Iran inazidi kuwa kichwa ngumu kwa jumuiya ya kimataifa katika mpango wake wa kuendelea na miradi ya kinyuklia na kudai nikwaaajili ya matumizi ya kisayansi na siyo kwa vita.

Monday, February 11, 2013

 Papa Benedikti XVI atangaza kujiudhulu.


Vatican, Vatican City - 11/02/2013.Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani ametangaza kujiudhulu wazifa wake kutokana na hali ya kiafya kuto mruhusu kuendelea na kazi za kiinjili.
Akitangaza kuhusu habari hizi,  Federico Lombardi ambaye ni msemaji wa Vatican alisema Papa Benedikti wa XVI atajiudhulu  wadhifa wake kama mkuu wa kanisa Katoliki duniani  tarehe 28/02/2013.
Papa Benedikti mwenye miaka 85, ambaye alitawazwa kuwa mkuu wa kanisa Katoliki April 19, 2005 amekuwa ni kiongozi wa kanisa Katoliki wa 265.
Kufuatia kujiudhulu huko kwa Papa Benedikti, Makadinali watakutana katika ya mwezi Machi ili kumchagua kiongozi mpya wa kanisa hilo.
  
Libya yavutana na ICC juu ya washitakiwa kutoka nchini Libya


 Tripol, Libya - 11/03/2013. Mahakama ya Kimataifa inayoshughulikia makosa ya jinai (ICC) imeitaka serikali ya Libya kumkabidhisha mikonino mwa mahakama hiyo aliyekuwa mkuu wa upelelezi wa Libya wakati wa utawala wa rais Muammar Gaddafi.
Abdullah Senussi  ambaye alikamatwa nchini Mauritania mwezi Machi mwaka jana, hadi sasa yupo mikononi mwa serikali ya Libya, na anakabiliwa na mashitaka ya kukiuka haki za binadamu wakati akiwa kama mkuu wa upelelezi wa Libya.
Kwa mujibu wa habari kutoka makao makuu ya koti (ICC) iliyopo Hague nchini Netherlands, zinasema " serikali ya Libya inatakiwa kumkabidhi haraka iwezekanavyo Abdulah Senussi mikononi mwa ICC kabla sheria haijachukua mkondo wake"
Kesi zidi ya Senussi imekuwa inaleta mvutano kati ya ICC na serikali ya Libya jambo ambalo limeifanya ICC kutishia kutumia mbinu mbadala baada ya serikali ya Libya kuzidi ng'ang'ania azma yake ya kumzuia mtuhumiwa huyo.
  
Wagombea urais Kenya wawekwa kiti moto kupitia Luninga.

Nairobi, Kenya - 11/02/2013. Wananchi na kaaazi wa Kenya watapata kwa mara ya kwanza fursa ya kuwa ona wanasiasa  wanaogombania urais wakijadili na kuongea sera zao za kisiasa na kiuchumi kwa kutangazwa moja kwa moja kupitia luninga na redio za kitaifa.
Mdaharo huo wa kisiasa ambao utachukua  muda wa masaa mawili, utawakutanisha wanasiasa  ambao ni viongozi wa vyama  wanagombania kiti cha urais kupitia vyama hivyo ili kuelezea wananchi  wa Kenya ni kwa kiasi watainua maisha ya Wakenya kiiuchumi na kijamii.
Wananchi nchini Kenya watapiga kura 4 mwezi Machi 2013, ili kumchagua rais na wabunge. 


Sunday, February 10, 2013

Muuaji wa kujitolea muhanga afa nchini Mali

Muuaji wa kujitolea muhanga afa nchini Mali

Gao, Mali - 10/02/2013. Mapigano ya kivita kati ya wapiganaji wa makundi ya Kiislam na majeshi ya serikali chini ya usaidizi wa jeshi la Ufaransa yameendelea katika eneo la Kaskazini  mwa  Mali.
Habari kutoka kwa msemaji wa kijeshi zinasema " mapigano hayo yaliaanza karibu na kituo cha polisi na baadaye muuaji wa kujitolea  kujilipua karibu na kizuizi kilicho wekwa barabarani."
Mji wa Gao ambao hapo awali ulikuwa umerudishwa mikononi mwa jeshi la serikali unaelekea kuwa kituo cha waasi hao wa Kiislam kwani inaaminika bado wapo katika baadhi ya vijiji vilivyopo kwenye mji huo.  

Wairan wapo imara asema rais Mahmoud Ahmadinejad.

Tehran, Iran - 10/02/2013.Rais wa Iran amesisitiza ya kuwa Wairan hawata tikiswa na mtu yoyote na lolote wanalo fanya ni kwaa ajili ya kuendeleza nchi yao na si kwaa ya kutishia nchi nyingine.
Rais Mahmoud Ahmedinejad aliyasema hayo wakati akuhutubia maelfu waliokusanyika  katika bustani ya  Azadi ili kuadhimisha miaka 34 tangu mapinduzi ya kuuong'oa utawala wa uliokuwa unakubalika na serikali za Magharibi.
"Leo maadui wanafanya kila njia ili kuzuia taifa la Iran kufanya maendeleo ya kisayansi kwa kutumia kila njia  ,kalini hadi sasa wameshindwa na tutazidi kuendeleza uwekezaji wa kisanyansi ili kizazi cha  Wairan wajao wawe na msingi imara." Aliongezea rais Ahmadinejed
Iran imekuwa na mvutano na serikali za magharibi kuhusu mpango wa mradi wake wa kinyuklia., jmabo ambalo serikali za magharibi zi na shukia ya kua Iran inampango wa kutengeneza siraha za kinyuklia na huku serikali ya Iran ikipinga shukuma hizo.



Sunday, February 3, 2013

Majeshi ya Ufaransa kuondoka nchini Mali.

 Wapinzani nchini Misri walia na rais Mosri.

 Kairo, Misri - 03/02/2013. Polisi nchini Misri wamekuwa na kashfa nyingine tena, baada ya kuonekana katika picha za luninga wakimpiga mmoja ya waandamanaji wakiwa "uchi" bila nguo.
Kufuatia tukio hilo vyama vya upinzani nchini Misri vimedai rais Mohamed Mosri ashitakiwe, kwani tangu achukue madaraka zaidi ya watu 60 wamekwisha uwawa kufaatia ghasia zinazo endelea nchi humo.
Mmoja wa kiongozi wa vyama vya upinzani akisikika akisema " kitendo kilicho fanywa na polisi kimekiuka haki za binadamu na tunataka rais atolewe madarakani kwani yale tuliyo yakataa wakati wa utawala wa Husni Mubaraka Mosri ndiyo anayayenda."
Hali ya amani nchini Misri imekuwa ya kuyumba saana tangu kuingia serikali mpya ya  Mohammed Mosri  chini ya chama cha Muslim Brotherhood, jambo ambalo lilimfanya rais Mosri kutangaza hali ya tahadhali katika baadhi ya miji mikuu nchini  Misri, kitu ambacho kiliwafanya wanachama wa vyama vya upinzani kupinga na kuanzaa maaandamano kupinga tahadhali hiyo.

Majeshi ya Ufaransa kuondoka nchini Mali.

 Bamako, Mali - 03/02/2013. Rais wa Ufaransa Francois Hollande amewaahakikishia Wamali ya kuwa jeshi la Ufaransa lipo nchini Mali ili kusaidia kurudisha amani nchini humo.
Akiongea na wahandishi wa habari rais Hollande alisema " jeshi la Ufaransa lipo kwa ajili ya kurudisha amani  na pindipo kazi hiyo itakapo kamilika, jeshi hilo litarejea nyumbani."
Wakati akiongea na waandishi wa habari rais Hollande, majeshi ya Ufaransa kwa kushirikiana na majeshi ya Mali yamezidisha mashambulizi zidi ya waaasi wa kundi linaloshirikiana na Al Qaeda na kulifanya kundi hilo kutokomea kabisa na kuachia mji wa Timbuktu ambao ulikuwa chini ya waaasi hao.
Rais Hollande alifanya ziara ya kiserikali nchini Mali ikiwa ni jitihada ya Ufaransa kuonyesha kuunga mkono serikali ya Mali na kuwapa moyo wanajeshi wa Ufaransa waliopo nchini Mali.