Saturday, October 30, 2010

Mizigo inayo sadikiwa kuwa na bomu yapatikana

Mizigo inayo sadikiwa kuwa na bomu yapatikana. Dubai, UAE - 30/10/2010. Makachero wa UAE na makachero wa kimataifa wa nchi za Uingereza na Amerika wamefanikiwa kuukamata mizigo ambao inasadikiwa ilikuwa ndani ya ndege tayari kuelekea Amerika. Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema "mizigo hiyo ilikuwa imetokea nchini Yamen. Mizigo hiyo likutwa na aina fulani ya unga PETN ambao unasadikiwa ungetumika kuleta madhara." Picha hao juu inaonekana moja ya ndege ya kubebea mzigo ikiwa inafanyiwa ukaguzi mara ya habari kupatikana ya kuwa kuna moja ya ndege za kubebea mizigo imebeba mzigo wenye bomu.

Makampuni ya ulinzi ya watu binafsi yaongezewa muda kukaa nchini Afghanistan.
Kabul,Afghanistan - 30/10/2010. Serikali ya Afghanistani imekubali kuongeza muda wa kuwepo kwa makampuni ya ulinzi ya kibinafsi.
Kwa mujibu wa habari za apo hawali makampuni yote wa kiulinzi yaliyopo nchini Afghanistani yalitakiwa kuondoka ifikapo mwisho wa Desemba 2010 lakini yameongezewa muda hadi kufikia mwezi Machi 2011.
Uamuzi wa kufuta mkataba na makampuni ya kiulinzi yaliyopo nchini Afghanistan ulitolewa serikali na kutangazwa rasmi na rais Karzai.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Afghanistan Hamid Karzai akiwa mazungukwa na walinzi ambao baadhi yao wameajiliwa na makampuini ya ulinzi ya watu binafsi.
Picha ya pili anaonekana mmoja wa walinzi wa makampuni ya ulinzi ya watu binafsi akikatiza katika shamba moja nchini Afghanistan wakati wa akiwa kazini.
Aliyekuwa rais wa Argentina azikwa kijijini kwao
Santa Cruz,Argentina - 30/10/2010. Aliyekuwa rais wa Argentina Nestor Kirchner azikwa nyumbani kwao alikozaliwa Rio Gallegos.
Rais huyo ambaye alikuwa mume wa rais wa sasa Bi Cristina Kirchner, alikuwa kiongozi aliye simamia na kufanya kazi bila kuchoka ili kuleta maendeleo ya Argentina.
Picha hapo juu anaonekana marehemu Nestor Kirchner ambaye alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 60.
Picha ya pili wanaonekana rais wa Argentina Bi Cristina Kirchner kushoto akiwa na marehemu mume wake Nestor Kirchner enzi za uhai wake.
Picha ya tatu wanaonekana baadhi ya Waargentina wakisindikiza gari lililo mbeba marehemu Nestor Kirchner kuelekea kijiji kwao kwa mazishi.

Tuesday, October 26, 2010

Tarik Aziz ahukumiwa kifo na mahakama kuu nchini Irak.

Tarik Aziz ahukumiwa kifo na mahakama kuu nchini Irak.

Baghdad, Irak 26/10/2010. Mahakama kuu nchini Irak imemuhukumu adhabu ya kifo aliyekuwa waziri wa mambo ya nchi za nje na naibu waziri mkuu wakati wa utawala wa rais Saddam Hussein.
Hukumu hiyo ilitolewa kwa Tarik Aziz ambaye alikuwa msemaji mkuu wa serikali ya Irak katika shughuli zote za kimataifa.
Tarik Aziz 74, alikuwa mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu wakati wa utawala wa rais Saddam Hussein kutoka katika madhehebu ya Kikrisru
Picha hapo juu anaonekanaTarik Aziz enzi zake kama waziri wa mambo ya nchi za nje wa Irak akihutubia moja ya mkuutano mkuu wa umoja wa Mataifa.
Picha ya pili anaonekana Tarik Aziz akikaribishwa na hayati Papa John Paul II wakati alipo kwenda kumtembe Vatikani kwa mazungumzo.

Sunday, October 24, 2010

China huenda ikatumia kura yake ya veto.

China huenda ikatumia kura yake ya veto.

New York Amerika - 24/10/2010. Umoja wa Matifa umesema huenda China ikaweka kizuizi kufuatia repoti inayo sema ya kuwa risasi zilizo tumika kuwashambulia wanajeshi wa Umoja wa Mataifa ni za Kichina. Habari hizi zilipatikana wakati kamati ya usalama ya Umoja wa Mataifa inakutana kujadili vikwazo zidi ya serikali ya Sudan. Akiongea mwakilishi wa China kwenye Umoja wa Mataifa Zhao Baogang alisema " hii repoti haina ukweli na hawaitambui na nilazima uchunguzi ufanyike kwa makini." Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wanajeshi wa Umoja wa Mataifa ambao wamekuwa wakishambuliwa mara kadhaa wakati kufanya doria. Umoja wa Mataifa wasimamisha zawadi kwa rais wa Ekuetioa Guinea.
New York, Amerika - 24/10/2010. Umoja wa Matifa umesimamisha zawadi yenye thamani ya $ 300,000 iliyo tarajiwa kutolewa kwa jina rais wa Ekuetoria Gunea, Obiang Nguema Mbasogo.
Kwa mujibu wa habari kutoka idara ya Umoja wa Matifa - UNESCO zinasema "uamuzi wa kusimamisha zawadi hiyo kunatokana na maombi amyayo yameletwa kupinga kuwepo kwa zawadi hiyo kutokana na rais Obiang na serikili yake walivyo itawalawa nchi na kuweka katika hali ya kimaskini." Picha hapo juu anaonekana rais wa Ekuetoria Guinea Obiang Nguema Mbasogo akiwa katika moja ya mikutano ya kimataifa.
Wikileaks yatoa nyaraka za siri kuhusu vita vya Irak.
London, Uingereza, 24/10/2010. Shirika moja la habari WikLeaks limetoa hadharani nyaraka za siri ambazo zinaelezea kiundani hali na matokeo ambayo yalitokea na hali halisi ilivyo nchini Irak tangu kunza kwa vita hadi hivi sasa.
Nyaraka hizo za siri zinaeleza "mauaji mengi ya raia yalitokea kinyume na habari zilizotolewa na serikali ya Iraq na washiriki wake."
Pia katika repoti hizo zinaeleza " baadhi ya wanawake wajawazito waliuwawa wakati walipokuwa wakikimbiziwa hosptali na ikiwa kulitokea mauaji ya liyo vunja sheria za vita wafiwa walipewa fidia ya kiasi cha $10,000."
Picha hapo juu inaonesha sehemu ambayo mauaji yalitokea kwa wingi.

Friday, October 15, 2010

Venezuela ya saini mkataba na Urussi kujenga mitambo ya nguvu za kinyuklia.

Michezo ya 19 ya jumuia ya Madola yamalizika nchini India.

New Delhi, India 15/10/2010. Mashindano ya 19 ya nchi za jumuia ya Madola yamemalizika rasmi leo nchini India.
Katika mashindano hayo Australia ambayo imeondoka na medali nyingi za dhahabu zipatazo 74, ikifatiwa na Uingereza.
Akiongea wakati wa kufunga mashindano hayo rais wa michezo hiyo Mike Fennell alisema "michezo yote imekwisha vizuri na kila aliyeshiriki alifurahi japo kulikuwa na matatizo ya hapa na pale."
Picha hapo juu anaonekana mmoja ya watumbijazi akifanya vitu vyake wakati wa kufunga mashindano ya nchi ya jumuia ya Madola ya liyo fanyika nchini India
Picha ya pili wanaonekana washiriki na wanamichezo walioshiriki mashindano ya nchi wanachama wa jumuia ya Madola wakiwa uwanjani tayari kwa ufungaji wa michezo ya hiyo.
Venezuela ya saini mkataba na Urussi kujenga mitambo ya nguvu za kinyuklia
Moscow, Urussi - 15/10/2010.Serikali ya Venezuela imetiliana sahii mkataba na serikali ya Urussi kujenga mtambo wa nguvu za kinyuklia nchini Venezuela.
Mkataba huo uilisainiwa na waziri wa mambo ya nje wa Venezuela Nikolaus Maduro na rais wa mambo ya kinyuklia wa Urussi Sergie Kiriyenko.
Makataba huo kati ya serikali ya Urussi na Venezuela ulishuhudiwa na viongozi wa serikali zote mbili Hugo Chavez wa Venezuela na Dmitry Medvedev.
Mara ya kusaini mkataba, rais wa Urusi alisema "Venezuela ni mshiriki mkubwa wa Urussi katika nyanja za kimaendeleo."
Picha hapo juu anaonekana rais wa Venezuela Hugo Chavez kushoto akiwa na rais wa Urussi Dmitry Medvedev kulia mara baada ya kumaliza mazungumzo ya kiserikali.
Barabara ndefu duniani ya kamilika kuchimbwa
Milima ya Alps , Uswis 15/10/2010. Uchimbaji wa barabara chini ya milima ya Alps ambayo itakuwa barabara ndefu duniani kupita ndani ya mlima imemalizika.
Uchimbaji huo amabo ulianza miaka 15 iliyopita ulimalizika leo kwa kuunganisha barabara hiyo na barabara ambayo iliyopo Gottard Base.
Barabara hiyo itaunganisha kusini na kaskazini mwa Ulaya kiusafiri hasa ule wa mizigo mikubwa.
Picha hapo juu anaonekana mmoja ya wafanyakazi akiwa kazini kuanza ujenzi wa reli itakayo tumika kubebea mizigo.

Thursday, October 14, 2010

Kazi ya uokoaji yamalizika salama nchini Chile

Kazi ya uokoaji yamalizika salama nchini Chile.

Atacama, Chile 14/10/2010. Waokoaji wamefanikisha kazi ya kuwaokoa wafanyakzi 33 waliokuwa wamekwama kutoka katika migodi iliyopo kwenye jangwa la Atacama baada ya kukwama ndani ya machimbo ya migodi kwa zaidi ya miezi miwili .
Akiongea mara ya kumalizika uokoaji rais wa Chile Sebastian Pinera, alisema "kwama ra nyingine tena tumekuwa tumezaliwa upya na sisi Wachile tumeuonyesha ulimwengu ya kuwa tuko pamoja katika kila hali."
Akiongea mmoja wa waokolewa Luis Urzua alisema " tulikuwa na imani na tulikuwa tunapigania kwa ajili ya familia zetu na tumefanikiwa kutoka tukiwa hai kutokana na ushirikiano tuliokuwa nao kwa wakti wote tulipo kuwa chini ya ardhi."
Pia shughuli za uokoaji zilishuhudiwa na rais wa Bolivia Evo Morares ambaye alikuja kumuunga mkono rais mwenzake wa Chile na kumpokea mmoja wa watu waliokuwa wamekwama chini ya ardhi alikuwa ni raia wa Bolivia.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Bolivia Evo Morares akiongea huku akimtizama rais wa Chile Sebastian Pinera wakati alipo kwenda kumuunga mkono shughuli za uokoaji zilipo anza.
Picha ya pili anaonekana rais wa Chile Sebastian Pinera, akitangaza rasmi kuanza shughuli za uokoaji huku akitazamwa na wananchi ambao walikuwa wanangoja kwa hamu kuwaona ngugu zao wakiwa hai.
Picha ya tatu anaonekana rais wa Chile akikumbatiana na Florencio Avalos ambaye alikuwa wa kwanza kuokolewa kutoka kwenya migodi iliyo bomoka na kuwazuia wasiweze kutoka yeye pamoja na wenzake.
Picha ya nne, anaonekana Carlos Mamani Soliz akiwa amepiga magoti kushukuru Mungu, mara baada ya kukombolewa kutoka ndani ya machimbo ya migodi ambayo ilibomoka wakati walipokuwa kazini.
Rais wa Iran afanya ziara ya kiserikali nchini Lebanon.
Beiruti, Lebanon-14/10/2010. Rais wa Iran amewahutubia maelfu ya Walebanoni kwa nyakati tofauti tangu kuanza kwa ziara yake ya kiseikali nchini humo. Rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad katika hotuba zake aliwasifu wananchi wa Lebanon kwa kusema "ujasiri wane wa kutokukubali kuonewa na ndiyo imekuwa changamoto katika eneo zima la Mashariki ya Kati."
Pia rais huyo aliongezea kwa kusema "Iran itasimama bega kwa bega na Lebanon ikiwa kutatokea matatizo yaina yoyote."
Hata hivyo serikali ya Amerika na Izrael zimekiaani kitendo cha rais wa Iran kufanya ziara nchini Lebanon kwa kusema "sijambo muafaka."
Mahmoud Ahamadinejad yupo nchini Lebanon katika kuendeleza na kukuza ushirikiano wa Karibu na nchi hiyo ambapo nchi hizo mbili zilitiliana sahii mikataba ya ushirikiano kibiashara, kilimo na katika nyanja mafuta.
Picha ya kwanza ni ya rais wa Iran Mahmoud Ahmadinejad akiwa mbele ya bendera za Iran na Lebanon.
Picha ya pili wanaonekana watu waliokuja kumsikiliza rais wa Iran wakati alipo kuwa akihutubia katika moja ya mikutano wakati wa ziara yake nchini Lebanon.
Mamia waandamana kupinga kuteuliwa Kim Jong-Un
Seoul, Korea ya Kusini - 14/01/2010. Mamia ya watu wameandamana katika jiji la Seoul kupinga kitendo cha kiongozi wa serikali ya Korea ya Kaskazini kumteua mtoto wake kushika madaraka yake.
Katika maandamano hayo mmoja wa waandamanaji amabye mwanaye alitekwa mwaka 1971 alisema "dunia imeshangazwa na kitendo cha kiongozi wa Korea ya Kaskazini kupanga kumrisisha mwanae madaraka kinyume na demokrasi.
Picha hapo juu anaonekana mmoja ya watu waliokimbia kutoka Korea ya Kaskazini akiwa ameshikiria kitu mkononi kutopia picha iliyo chorwa ya Kim Jong-Un,ambaye inaaminika tachukua madaraka kutoka kwa babayake Kim Jong Il.
Viongozi wakutana kupata majibu ya chanzo cha kifo cha raia wa Uingereza.
London Uingereza - 14/10/2010. Waziri Mkuu wa Uingereza amekutana na Mkuu wa Majeshi wa Amerika anayesimamia vita vya Afghanistan ili kupata muafaka kuhusu kifo cha raia mmoja wa Uingereza.
Waziri Mkuu David Cameron alikutana na Kamanda David Petraeus katika ofisi ya waziri mkuu zilizopo jijini London.
Kifo cha Mwingereza Linda Norgrove 36 kilitokea wakati wa harakati za kutaka kumkomboa kutoka mikononi mwa wateka nyara waliomteke. Natokea kuuwawa kwa Mwingereza huyo kumekuwa na habari tofauti kuhusu kifo chake.
Picha hpo juu anaonekana marehemu bi Linda Norgrove ambaye alipoteza maisha wakati wa jitihada za kutaka kumwokoa.

Monday, October 11, 2010

Swala la amani kati ya Waizrael na Wapalestina laingia sura mpya.

Swala la amani kati ya Waizrael na Wapalestina la chukua sura mpya.

Jerusalem, Israel - 11/10/2010. Waziri mkuu wa Izrael amewataka viongozi wa Kipalestina kukubali na kutambua ya kuwa Izrael in taifa la Mayahudi.
Binyamin Netanyahu, aliyasema hayo wakati alipo kuwa aki hutubia bunge la Izrael Knesset
Waziri mkuu Netanyahu alisema "kulitambua taifa la Izrael ni nguzo muhimu katika swala zima la mazungumzo ya amani."
Hata hivyo msemaji wa serikali ya Wapalestina alisema "Wapalestina hawakubaliani masharti hayo na wanataka ili mazungumzo yaendelee ni lazima serikali ya Izrael isimamishe ujenzi wa nyumba zake katika maeneo inayo yakali."
Picha hapo juu ni ya bendera ya Izrael ambao viongozi wa serikali wanataka Wapalestina walitambue Taifa la Waizrael.
Picha ya pili ni ya bendera ya Wapalestina, ambapo wanataka Izrael isimamishe ujenzi ili mazungumzo ya amani yaendelee.
Serikali ya Hungari kukataifisha kampuni iliyo husika na janga la sumu.
Budapest Hunguri - 11/10/2010. Polisi nchini Hungari wamemkamata na kuweka kizuizini mkuu wa kampuni ya kuzalisha vyuma kwa kosa la kupasuka kwa bwawa lenya maji yaliyo changanyika na sumu hivi karibuni.
Msemaji wa serikali Anna Nagy aliema " Zoltan Bakony ambaye ni mkuuwa kampuni hiyo alikamatwa hivi karibuni."
Akiongea mbele za waandishi wa habari ,waziri mkuuwa Hungari Viktor Orban alisema "kampuni hiyo inatakiwa kuwa chini ya serikali kwa kutokana na matatizo yaliyo tokea ya kuaribu mazingira na makazi wa wana vijiji."
Kufuatia mafuriko hayo watu wapatao saba walipoteza maisha yao na wengi zaidi ya 150 kujeruhiwa vibaya.
Bwawa hilo lililo pasuka lipo km 160 magharibi mwa mji wa Budapest lilifianya mji mzima kuwa na rangi nyekundu sumu ambayo huenda ikaleta madhara makubwa kiafya katika jamii.
Mgogoro wa China na Japan mawaziri wakutana.
Hanoi, Vietnam - 11/01/2010. Mawaziri wa ulinzi wa serikali za China na Japan wamekutana kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwa mzozo baada ya serikali ya Japan kumkamata rais wa China Zhan Qixiong.
Mzozo huo ulizidi kuwa mkubwa mara baada ya serikali ya Japan kukataa kumwanchia huru raia huyo wa China ambaye alikuwa kiongozi wakati meli ya uvuvi ya China inlipo gongana na boti ya ulinzi ya Kijapan.
Msemaji wa serikali ya China Liang Guanglie alisema " mazungumzo ya maafisa hao wawili wa serikali zote yaliendelea viziri na kuna matumaini ya kuwa mgogoro huu utakwisha hivi karibuni."
Picha hapo juu hapo juu inaonekana meli ya uvuvi ya Kichina ambayo ilikuwa chanzo cha mgogoro kati ya China na Japan.

Thursday, October 7, 2010

Askofu Dasmond Tutu astaafu kazi za kiofisi.

Askofu Desmond Tutu astaafu kazi zote za kiofisi.

Cape Town, Afrika ya Kusini - 07/10/2010. Askofu, kiongozi, mtetezi, mpigania haki za binandamu na mmoja wa vionngozi walio pinga ubaguzi wa rangi nicni Afrika ya Kusini wakati wa serikali ya kibaguzi ya makaburu wa Afrika ya Kusini ametangaza kujiudhulu kazi zote za kiofisi.
Askofu Desmond Tutu aliyasema hayo wakati akiazimisha siku ya kuzaliwa kwake leo ambapo anatimiza miaka 79.
Askofu Desmond Tutu alisema "Kuanzia sasa nitakuwa karibu na mke wangu, familia yangu kwa muda wote na kupumzika huku nikiangalia michezo, na wakati huo nikitoa husia kwa wanangun wajukuu na vijukuu."
Picha hapo juu anaonekana, Askofu Desmond Tutu akiwa anaongoza maombi kabla ya kufikiwa wakati wa kustaafu kazi zake zote za kiofisi.

Sunday, October 3, 2010

Mashindano ya Jumuia ya Madola ya funguliwa.

Mashindano ya Jumuia ya Madola ya funguliwa. New Dheli, India - 03/10/2010. Wananchi wa India wamewakaribisha wanamichezo mbalimbali ili kushiriki mashindano ya nchi wanachama wa jumuia ya nchi zilizo kuwa koloni la Uingereza ambayo yanajulikana kama mashindano ya nchi za jumuia ya madola. Mashindano hayo ya 19th yameanza rasmi baada ya habari za wasiwasi kuenea ya kuwa itakuwa vigumu kwa mashindano hayo kufanyika kutoakana na maandalizi yaliyo tiliwa mashaka. Picha hapo juu wanaoneka wanamichezo wakishiriki wakati wa ufunguzi huku wakiongozwa na maonyesho yalioandaliwa kwa ajili ya ufunguzi.

Wajerumani kushangilia kumbukumbu ya muungano.
Berlin, Ujeruman - 03/10/2010.Wananchi wa Ujerumani wameshangilia siku ya kuungana Ujerumani ya Mashariki na Ujerumani ya Magharibi ambapo ziliungana 1990.
Muungano huo ulipokelewa kwa shangwe na wananchi wa Ujerumani na Ulaya kwa ujumla na umekuwa ukikumbukwa na kusherekewa kila mwaka.
Picha hapo juu anaonekana Kanselar wa Ujerumani Angela Merkel na viongozi wengine wakiangali kwa pamoja mazingira mapya baada ya muungano huo kutokea miaka 20 iliyo pita
China kuisaidia Greek kuinua Uchumi wake.
Athens, Greece - 03/10/2010. Serikali ya China imesema itaisaidia kikamilifu serikali ya Greek katika kujenga uchumi wake uliyo yumba.
Waziri mkuu wa China Wen Jiabao alisema " China itashiriki kikamilifu katika kuisaidia Greek kujijenga upya kiuchumi ili kupunguza deni ambalo ni mzigo kwa serikali kwa kuongeza ushirikiano wa karibu na kukuza biashara kati ya nchi hizi mbil."
Picha hapo juu ni ya bendera za China nchi ambayo itashirikiana kikamilifu na serikali ya Greek ili kuinua uchumi wa nchi hiyo.
Na picha inayo fuata chini ni ya Greek nchi ambayo inakabiliwa na tatizo la kiuchumi na kwa sasa itashirikiana na China kikamilifu ili kuinia uchumi wake.

Friday, October 1, 2010

Rwanda na Uganda zakanusha madai ya repoti ya Umoja wa Mataifa.

Denzel Washington kutangaza siku yamshindi wa Nobel nchini Oslo. Oslo, Norway - 01/10/2010. Mcheza simema maarufu duniani atakuwa mtangazaji wakati wa kutoa zawadi ya Nobel Price itakayo fanyika mwaka huo Oslo. Denzel Washington ambaye amekuwa maarufu kwa kucheza sinema zenya kusisimua hisia katika jamii alisema "niheshima iliyoje kuwa mmoja wapo ya watu watakao kuwepo na kushiriki kwenye sherehe hiyo." Picha hapo juu anaonekana Denzel Washington akiwa ameshikilia zawadi aliyo shinda kuwa mshindi bora katika kucheza sinema nzuri na kusisimua. Rwanda na Uganda zakanusha madai ya repoti ya Umoja wa Mataifa.

Kigali, Rwanda - 01/10/2010. Serikali ya Rwanda na serikali ya Uganda zimepinga vikali repoti iliyo tolewa na Umoja wa Mataifa kwa kuzihusisha nchi hizo mbili katika vita na mauaji yaliyo tokea katika Demokrasi Jamuhuri ya Kongo.
Kwa mujibu wa reporti hiyo yenye kurasa 617 ilisema "majeshi ya Rwanda na Uganda yaliwauwa raia wengi wakati wa vita na hasa katika kipindi cha miaka ya 90 hadi mwisho wa miaka hiyo." Katika repoti hiyo pia nchi nyingine ambazo zilitajwa ni Burundi, Kongo na Zimbabwe.
Akiongea wakati wa kutangaza repoti hiyo kamishana wa kutetea haki za binadamu Navi Pillay alisema "katika kila jamii ya wananchi wa DR Kongo basi yupo mtu mmoja ambaye ameathirika kutokana na vita hivyo."
Picha hapo juu zinaonekana picha za bendera za Rwanda juu na ya chini ni ya Uganda nchi ambazo zinashutumiwa katika repori ya umoja wa Mataifa.
Rais wa zamani wa Pakistani aanzisha chama kipya cha siasa.
London, Uingereza - 01/10/2010. Rais wa zamani wa Pakistan na aliyekuwa amiri jeshi mkuu ameanzisha chama cha siasa.
Pervez Musharraf, alitangaza mbele ya wandishi wa habari alisema "chama hicho kitajulikana kama All Pakistan Muslim League na kitashirki katika uchaguzi ujao utakao fanyika mwaka 2013."
Aliongeza kwa kusema "ninaogopa kwani Pakistan uenda ikagawanyika kama hakutakuwa na mabadiliko ya uongozi."
Vilevile alitumia fursa hii kuomba msamaha kwa makosa yaliyo tokea wakati wa uongozi wake.
Picha hapo juu anaonekana aliyekuwa rais wa zamani wa Pakistani, Pervez Musharraf akiwasalimia wanachi waliokuja kusikiliza kuzinduliwa kwa chama kitakacho ongozwa naye.
Sherehe ya miaka 50 ya uhuru yaingia dosari nchini Nigeria.
Abuja, Nigeria - 01/10/2010. Watu wapatao wanane wamepoteza maisha yao na wengine kujeruhiwa baada ya gali kulipuka katikati ya jiji la Abuja.
Mlipuko huo uliokea wakati wanachi wanajipanga kuanza kushangilia miaka 50 ya uhuru wa Nigeria.
Mlipuko huo ulitokea mbele ya viongozi wa nchi ambalo walikuja kusherehekea sikuku hiyo.
Picha hapo juu yanaonekana baadhi ya magari ambayo yamearibiwa kutokana na mlipuko na kupoteza maisha na kusababisha majeruhi.