Tuesday, July 28, 2009

China na Amerika zakutana kujadili ushirikiano wa kiuchumi.

Unene wa mwili ni hali ya hatari kwa mtu na matumizi ya serikali.

Chicago, Amerika - 28/07/09. Swala la kunenepa kwa watu kupita kiasi hasa katika nchi za Magharibi, zimekuwa zinaleta vichwa kuuma kwa watu na jamii nzima ya maeneo haya.
Kwa mujibu wa wachunguzi wa wa mambo ya afya ya watu, zinasema ya kuwa unene wa mwili ni hali ya hatari kwa binadamu mwenyewe na serikali za nchi hizo kwa kutumia pesa nyingi katika matibabu yanayo sababishwa na unene wa mwili.
Akiongea haya, Dr Thomas Frieden, alisema hipo haja ya watu kwa kusaidiana na serikali kupambana na hali hii.
Picha hapo juu, anaonekana mmoja ya watu, ambao unene umekuwa ukiwa tatizo kwa jamii.
Picha ya pili, wanaonekana, baadhi ya watu wa nchi za Magharibi, ambao wanakabiliwa na hali ya kuongezeka kwa watu kuwa wanene kupita kiasi, na kutetetlesha hali ya afya zao.
Utumiaji wa simu ya mikono huku ukiendesha gari, ni hatari kwa watumiaji wa barabara.
Virginia, Amerika - 28/07/09. Wataalamu wa mambo ya usalama barabarani, wamesema yakuwa kuna ya asilimia kubwa kwa dereva anaye endesha gari wakati anaandika teksti kwa kutumia simu ya mkono kupata ajali, au kusababisha ajali kwa madereva wengine wanaotumia barabara wakati huo.
Kwa mujibu wa wataalamu kutoka chuo cha usafiri cha Virginia, zimesema kugonga ao kugongana na gari jingine kuanaweza kutokea wakati wowote wakati dereva anaandika teksti kwa kutumua simu ya mkono huku akiwa anaendesha gari.
Wachunguzi hao walisema, hata upokeaji wa simu kwa kutumia mkono kuhu uanendesha gari, kunaleta hatari pia.
Picha hapo juu, ni moja ya picha za video zinaonyesha kwa kiasi gani dereva, anapo endesha gari, huku huku akituma teksti anaweza sababisha ajali barabarani.
China na Amerika zakutana kujadili ushirikiano wa kiuchumi.
Washington,Amerika - 28/07/09. Rais wa Amerika, Baraka Obama, ameukaribisha uhusiano wa Amerika na China na kutaka uwe wa faida kwa nchini zote mbili na wanachi wake.
Rais , Obama aliyaongea hayo wakati alipo kuwa anawakaribisha viongozi wa China wakiongozwa na makamu wa waziri mkuu wa China, Wang Quishan.
Ujumbe huo kutoka China, upo nchini Amerika, kujadili ni jinsi gani nchi hizi mbili zitashirikiana kiuchumi.
Picha hapo juu, anaonekana rais, Obama, akiongea mbele ya wajumbe wa China na Amerika kabla ya kuanza mjadiliano ya kiuchumi.
Picha ya pili,rais , Baraka Obama, akimkaribisha, makamu wa waziri mkuu wa China, Wang Qishan, na kulia ni waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, Bi Hillary Clinton.
Picha ya tatu, wanaonekana wajumbe na viongozi kutoka China,wakimsikiliza rais wa Amerika, Baraka Obama wakati wa ufunguzi wa mazungumzo ya kiuchumi wa nchi hizo mbili, (Amerika na China)
Sijawahi kula nyama ya mtu, adai rais wa zamani wa Liberia.
Hague,Nederland - 28/07/09. Rais wa zamani wa Liberia , Charles Taylor, amekanu sha shutuma zakuwa alikuwa anatafuta na kula nyama za watu, na kuesam nu upuuzi mtupu.
Akiongea kwa msisitizo , rais huyo wa zamani wa Liberia, Charles Talor, aliambia koti ya kuwa watakuwa ni wagonjwa kama wakiamini ushaidi unaotolewa juu yake yakuwa alikuwa ana kula nyama za watu, inafanya mtu aweze kutapika.
Rais huyo wa zamani wa Liberia, anakabiliwa na makosa ya kukiuka haki za binandamu,na ya kivita zidi ya nchi ya Sierra Leone.
Picha hpo juu anaonekana, rais wa zamani wa Liberia , Charles Taylor, akiwa mahakani, huku akiandika pointi na huku akisikiliza shutuma zidi yake.
Machafuko yaleta hali ya wasiwasi nchini Nigeria.
Kano , Nigeria - 28/07/09. Hali ya usalama nchini Nigeria imeingia katika hali ya utata, hasa katika eneo la jimbo la Kano, lililopo kaskazini mwa Nigeria.
Kufuatia machafuko hayo amboyo bado yanaendelea chini humo katika jimbo la Kano,yamesababisha baadhi ya watu kupoteza maisha yao.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema watu wapatao 100, wamesha poteza maisha mpaka sasa.
Ghasia hizo ambazo zinakuja baada ya wakazi wa eneo hilo la Kano, hawakubaliani na mpango wa elimu ya kisasa, kwa madai yakuwa haiendani na matakwa ya jamii hii, na wanataka elimu iwe inaendana na dini yao ya Uislaam.
Kufuatia mvutano huo, watu walikwenda kuvamia kituo cha polisi,kwa madai ya kuwa kuna mmoja ya mwenzao amekamatwa, na hivyo polisi kujibu mashambulizi na kuteta maafa makubwa.
Picha hapo juu, wanaonekana baadhi ya watu wakiwa chini ya ulinzi, mara baada ya kutiwa chini ya ulinzi.

Tuesday, July 21, 2009

Taliban watumia mbinu mpya katika kutengeneza nyenzo zao za kivita.

Swala la Rio Tinto, serikali mbili kukutana kuliongea.

Sydney, Australia - 22/07/09. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Australia Stephen Smith, amesema atakutana na waziri wa mambo ya nchi za nje wa China Yang Jienchi,ili kuzungumzia mgogoro uliopo kati ya serikali hizi mbili, kufuatia China kumkamata mkubwa anayesimamia kampuni ya Rio Tinto, Stern Hu, ambaye ni rai wa Australia.
Stern Hu, alikamatwa July 5/2009 na serikali ya China, kwa madai ya upelelezi na kutaka kutoa rushwa kwa baadhi ya wafanyakazi ili aweze kuapata siri ya mikataba inavyotolewa .
China imekuwa ikifanya biashara na Australia,na hasa katika usambazaji wa vyuma, ambapo kampuni ya Rio Tinto, ndiyo kampuni mama katika uchimbaji na usambazaji.
Picha hapo, juu ni moja ya mitambo ya Rio Tinto, kampuni ambayo ni maarufu kwa uchimbaji wa madini kutoka ardhini.
Picha ya pili ni ya Stern Hu, ambaye kwa sasa yupo kizuizini nchini China kwa kudaiwa kuhusika na makosa ya jinai.
Nchini wanachama wa EU wapewa ruhusa kuweka akiba ya gas asilia.
Brussel, Ubeligiji - 22/07/09. Muungano wa Ulaya, umeziagizia nchi wanachama kuanza kuweka akiba ya gas ya asili, endapo kutatokea kutokuelewa tena na Urussi.
Kwa mujibu wa kamati inayo shughulikia maswala hayo imesema yakuwa kila nchi mwanachama, inatakiwa kuwa na gas ya asili ya kutosha ifikapo mwaka 2014, na gasi hiyo iwe na uwezo wa kutumika kwa muda wa miezi hadi miwili (Siku 60).
Mgogoro wa gas kutoka Urussi, umekuwa ukizisumbua nchi nyingi za Muungano wa Ulaya,kwa muda mrefu na kusababisha baadhi ya nchi kutiliana mkataba na Uturuki, ili kujengwa mabomba mapya yatakayo wezesha gas kutoka Caspian na Mashariki ya Kati,ili kupunguza kuitegemea Urussi katika upatikanaji wa gas.
Picha hapo juu,ni ya nembo ya nchi wanachama wa Muungano wa Ulaya, ambapo nchi wana chama wamekuwa wakipata msukosuko wa kupata gasi, pindipo panapotokea mtafaruki.
Picha ya pili ni moja ya mitambo ianayo tumika kuhifadhi gas, ambapo kuanzia sasa mitambo hiyo itabidi iongezewe uwezo wa kuhifadhi gasi hiyo.
Taliban, watumia mbinu mpya katika kutengeneza nyenzo zao za kivita.
Gardez ,Afghanistan - 22/07/09. Wapinaji wa kundi la taliban, wameshambulia maeneo ya yaliyopo majengo na ofisi za serikali kwenye miji tofatuini ncini Afghanistan.
Maeneo hayo ambayo yameshambuliwa yapo katika miji ya, Gardez na Jalalabad,wakati nchi hiyo inajiandaa mna uchaguzi wa rais utakao fanyika mwisho wa mwaka huu.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, watu watun sita waliova nguo za kike, huku wakiwa na siraha na mabomu, walishambulia maeneo hayo tofauti ya serikali.
Kundi la Talibani limekuwa likitumia mbinu za kisasa kutengeneza mabobu yake, kwa mujibu wa wataalamu wa mambo ya kijeshi.
Hata hivyo , walinzi wa serikali waliweza kuwaua watu watatu, na wengine watatu waliweza kukumbia.
Picha hapo juu, wanaonekana, baadhi ya wanajeshi wakiimgia katika helkopta tayari kwenda mstari wa mbele kupambana na kundi la Talibani.
Picha ya pili, ni anaonekana mmoja ya mwanajeshi akikimbia, kukwepa bomu, ambalo lililipuka karibu yake.
Vijana wamiminika katika hospitali na zahanati kufanyiwa operesheni(Kutailiwa).
Bloemfontein, Afrika ya Kusini - 22/07/09.Kutokana na kuthibitishwa ya kuwa wanaume waliotailiwa wana nafasi kubwa ya kutoambukizwa ugonjwa wa ukimwi,vijana walio wengi nchini Afrika ya Kusini, wanamiminika katika zahanati tofauti ili kufanyikwa operesheni hiyo ndogo( Kutailiwa)
Kwa mujibu wa mmoja wa madokta ambao wanashughulikia operesheni hizo Dr, Diono Rech, alisema amekuwa anafanya operasheni hizo hadi kufikia 50 kwa wiki.
Picha hapo juu, wanaonekana, baadhi ya vijana wakiwa katika zahanati moja, tayari kufanyiwa opereshieni au ( Kutailiwa).
Kansa ya mapafu yajadiliwa kiundani na wataalamu jijini New York.
New York, Amerika - 22/07.09. Wanasayanchi nchini Amerika, wamesema ni hivi karibuni, walipo kutana jijini, New Yor, kwatafanikiwa vipi kutibu kansa ya mapafu,kwa kutumia vyombo ya kitaalamu zaidi.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana kutoka katika mahaabara inayo shughulikia uchunguzi na matibabu ya kansa, iliyopo jijini New York,zilisema muda si mrefu wataalamu wataamua ni njia ipi iliyo bora zaidi katika kutibu ugonjwa huo.
Picha hapo juu, ni ya mapafu, ambapo wataalamu wana sema muda si mrefu waataanza kutumia vidonge kuanza kutibu mapafu yaliyo kuwa na kansa.
Mamiliona washuhudia kupatwa kwa jua barani Asia.
Bangkok , Thailand - 22/07/07. watu wapatap millioni katika bara la Asia, wamekusanyika katika sehu maalumu zilizo tayarishwa kwaajili ya kuangalia kupatwa kwa jua katika karne hii.
Kwa mujibu wa wataalamu wa mambo ya kijiografia, wamesema ya kuwa, maeneo tofauti katika bara la Asia, Japan, India ,na China,wataweza kuona kitend hicho ambacho hutokea kwa mara moja katika kila bara
Picha hapo juu, ni ya jua linaonekana kuzibwa kabisa , na kuleta giza kwa muda katika eneo ambalo lilitakiwa jua liwe linawaka.
Picha pili hapo juu wanaonekana, baadhi ya wanafunzi, wa wanaosomea maswala ya sayansi, wakiangali kupatwa kwa jua katika jimbo la Bihar nchini India.

Sunday, July 19, 2009

Ndugu,jamaa, marafiki na viongozi washerekea siku ya kuzaliwa Nelson Mandela.

Ndugu, jamaa, marafiki, na viongozi washerekea siku ya kuzaliwa Nelson Mandela.

Johannesburg, Afrika ya Kusini - 18/07/09. Maelfu ya watu wamesherekea siku ys kuzaliwa kwa aliye kuwa rais wa kwanza mwafika, mpigani uhuru, haki na usawa kwa wanchi wa Afrika ya kusini, Nelson Mandela,ambapo ametimiza miaka 91 tangu kuzaliwa.
Moja kati ya watu walioudhulia sherehe hizo ni rais wa sasa wa Afrika ya Kusini Jacob Zuma.
Nelson Mandela, ameweza kuleta mabadiliko na kuwa changa moto kwa watu wengi, bila kujali rangi zao na wapi wanatokea.
Picha hapo juuwanaonekana, rais wa sasa wa Afrika ya Kusini, Jacob Zuma, akiwana rais wa kwanza mwafrika wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela, kabla ya kupata maakuli kushangilia siku ya kuzaliwa kwa Nelson Mandela.
Picha ya pili, anaonekana, rais wa kwanza wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela, akitabasamu mbele ya watu walio kuja kusherekea siku ya kuzaliwa kwake.
Picha za mwanajeshi aliyetekwa nyara zasambazwa kwenye mitandao.
Paktika, Afghanistan - 16/07/09. Mwanajeshi wa Amerika aliye potea waktai akiwa mstari wa mbele siku ya tarehe 30/juni/2009, ameonekana kwen picha za video na kwenye mitaandao huku akiongea ni kwajinsi hali anayotarajia, na kwa kiasi gani ana wakumbuka watu wote wa famial yake.
Video ya mwanajeshi huyo, mwenye umri wa miaka 23, ilionyeshwa kwa dakika 28 siku ya jumamosi, huku akiwa amekatwa nywele zake za kichwani.
Pentagon, imesema ya kuwa mwanajeshi huyo, Bowe Bergdahl, wa Kentchum Idaho,juhudi za kumtafuta mahali alipo fishwa kama mateka bado zinaendelea, na jeshi la limesambaza vikaratasi katika eneo ambalo alikamatwa mwanajeshi huyo na kutaka mtu yoyote atakaye saidia kupatikana kwa mwnajeshi huyo, atapewa zawadi.
Na wakati huo huo , makao makuu ya jeshi la Amerika , limesema kitendo cha kundi ambalo limemkamata mwanajeshi huyo, kusambaza video zake ,ni kinyume na sheria za kimataifa.
Picha hapo juu ni ya mwanajeshi aliye tekwa nyara, Bowe Bergdahl, amnaonekana akila chakula alicho pewa na kundi ambalo lime mteka nyara.

Thursday, July 16, 2009

Kifo cha rais wa Palestina chaleta kitendawili kati ya viongozi wa Wapalestina.

Iran na Amerika bado kupeana majibu.

Washingtone, Amerika - 16/07/09. Serikali ya Amerika imesema ya kuwa utafika wakati mpango wa mazungumzo na Iran hautakuwa na maana tena, kwa kuzingati Iran imesha pewa hadi kufikia mwezi wa Septemba, iwe imesha toa jibu kama itakuwa tayari kuongea na Amerika, kupitia Umoja wa Mataifa.
Hayo yaliongewa na waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, Hilary Clinton, jana wakati akiongelea mipango ya serikali ya Amerika katika maswala mambo ya nje, na kudai ya kuwa Iran haitakiwa kuwa na nguvu za kijeshi za kinyuklia, bali wanaweza kuwa na nyuklia kwa ajili ya uzalishaji na maendeleo ya jamii.
Wakati huo huo, mkuu wa idara ya nyuklia wa Iran Gholama Reza Aghazadeh, amejihuzuru nyazifa yake wiki tatu zilizo pita.
Kwa mujibu wa shirka la habari ISNA, limesema ya kuwa hakuna habari kamili zilizo sababisha kujihuzuru kwake.
Picha hapo juu ni ya waziri wa mambo ya nje wa Amerika, ambaye amesema yakuwa serikali ya Amerika, itafika wakati hatua za mazungumzo hazitafaa tena.
Picha ya pili ni mkuu wa nyklia wa Iran, ambaye aneng'atuka madarakani.
Kifo cha rais wa Palestina chaleta kitendawili kati ya viongozi wa Wapalestina.
Tunis, Tunisia - 16/07/09. Kiongozi wa mkuu wa kundi la Wapigania Ukombozi wa Wapalestina (PLO) Palestina Liberation Organasation Farouk Kaddoumi, ameongea na vyombo
vya habari na kudai ya kuwa ripoti aliyotoa anaisimamia na yoyote aneye ona siyo kweli, basi aje na ushahidi mwingine wa kutosha.
Farouk Kaddoumi,alikuwa anasisitiza hivyo, kuhusu yeye kuandika ripoti ya kuwa kuna baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wa Wapalestina walishiki katika mauaji ya aliyekuwa rais wa Wapalestina, hayati, Yasir Arafat.
Hata hivyo, baada ya habari hizi kupatikana, baadhi ya vyama vilivyo tajwa vimekanusha habari hizo.
Farouk Kaddoumi, ambaye no mmoja wa viongozi waanzilishi wa PLO, aishie Tunisia.
Picha hapo juu, ni ya hayati rais, wa Palestina, Yasir Arafat, ambaye aliga dunia miaka mitano iliyo pita nchini Ufaransa, wakati alipo pelekwa matibabu.
Picha ya pili ni ya, Farouk Kaddoumi, ambaye ametoa ripoti ambazo zinateta kitendawili kwa Wapalestina.

Wednesday, July 15, 2009

Rais, Muammar Gaddafi,NAM, ipataiwe kiti cha kudumu cha Usalama UN.

Wairan na Walmania wakumbwa na msiba.

Qazvin, Iran - 15/07/09. Ndege ya shirika la ndege la Caspian imedondoka na kuuwa watu wote waliokuwemo kwenye ndege hiyo.
Kwa muibu wa msemaji wa serikali wa Iran,Mohammed Reza Montezer Khorasan, alisema ndege hiyo ambayo ilikuwa imebeba watu wapatao 168 kutoka Iran Tehran na kuelekea jijini Yerevan Almenia, ilianguka karibu na mji wa Qazvin siku ya leo jumajatano, na kuwaauwa watu wote waliokuwemo kwenye ndege hiyo, wafanyakazi 15 na abiria 153.
Chanzo cha ajali bado kinachunguzwa, alimaliza msemaji huyo wa serikali.
Picha hapo juu, anaonekana, mmoja wa mama aliyepoteza ndugu zake katika ajali hii, akiwa analia kwa uchungu uku akisaidiwa na ndugu wengine.
Picha ya pili ni shirika la ndege la Caspiana Airline, ambapo moja ya ndege yake imeanguka na kupoteza maisha ya watu wapatao 168.
Picha ya tatu, wanaonekana wafanyakazi wa shirika la kutoa huduma ya kwanza wa Iran, wakiwa wamebeba baadhi ya mabaki ya miili ya watu waliopata ajali na ndege.
Picha ya mwisho, inaonekana,moja ya enjini ya ndege, ikiwa imeharibika vibaya ,ka kutupwa mbala na eneo ambalo ndege iliangukia.
Vita vya Gaza, habari tata za aanza kusikika hazarani?" Izrael".
Jerusalem,Izrael, - 15/07/09. Baada ya miezi sita kupita tangu, kusimama kwa vita kati ya kundi la Hamas na Izrael, baadhi ya wanajeshi wa Izrael, wamekuwa wakieleza matukio tofauti yaliyotokea wakati wa vita hivyo, ambavyo vilialibu vibaya eneo zima la Ukanda wa Gaza.
Wanajeshi hao, walisema ya kuwa matimizi ya siraha zenye gasi ya kunguza, zilitumika kwa nyakati fulani, na kudai kuna wakati mwingine waliamuliwa kuchukua hatua ambazo haziendani na maadili ya kijeshi.
Hata, hivyo , msemaji wa jeshi la Israel,Leutenant Colonel, Avital Leibovich, alikanusha madai hayo. na kusema madai hayo siya ukweli na hayana ushahidi wala tarehe ya matukio.
Picha hapo juu, ni ya moja ya tanki la kijeshi la Izrael likiwa mstari wa mbele katka maeneo ya Ukanda wa Gaza.
Rais,Muammar Gaddifi,NAM ipatiwe kiti cha kudumu cha usalama wa UN.
Sharm el Sheikh, Misri - 15/07/09. Rasi wa Libya, Muammar Gaddadfi, ameshutumu, Balaza la Usalama la Umoja wa mataifa ni kama chombo cha kutishia, ambacho kinatumika kwa baadhi ya nchi zenye viti vya kudumu katika kamati hiyo,na kunyima usawa katika maamuzi muhimu ya dunia, hasa kwa nchi masikini. aliyasema haya katika mkutano wa viongozi wa nchi zisizofungamana na upande wowote unaofanyika nchini Misri (Non Aligned Movement)
Akiongezea , rais Muammar Gaddafi, alisema wakati umefika wa NAM, kuwa na kiti katika kamati hiyo ya usalama ya umoja wa Mataifa , kwani tumekuwa tunajaziwa siraha na sasa zina kuwa mzigo kwa nchi wanachama wa NAM.
NAM, ambayo ni jumuia ya nchi zitokazo, Afrika, Asia na Latin Amerika.
Picha hapo, ni ya rais wa Libya, Moammar Gaddafi, ambaye amateaka NAM, ipatiwe kiti, katika balaza la Usalama la Umoja wa mataifa.
Kiongozi wa Al Qaeda namba mbili achomoza tena katika mitandao.
Islamabad/Pakistan - 15/07/09. Kiongozi namba mbili wa kundi la Al Qaeda's Ayman al Zawahiri, amewataka wafuasi wa kundi lake na wa Pakistani kupigana na Amerika na washirika wake waliopo nchini Pakistani, kwa kudai wamekuja kuwatawala na kuchukua nchi ya Pakistani.
Ujumbe huo wa Ayman al Zawahiri, uliwekwa kwenye mitandano siku ya jumanne wiki hii.
Hamasa hiyo kutoka kwa kiongozi wa Al Qaeda namba mbili, zimekuja wakati majeshi ya Pakistani, Amerika na washiriki wake, wakizidisha mashambulizi zidi ya kundi la Taliban na washiriki wake hivi karibuni katika eneo la maporomoko na mabonde ya Swat. Picha hapo juu ,ni ya Al Qaeda, Ayman al Zawahiri, akiongea kwa ujumbe wake katika moja ya mitandao ya kisasa.
Picha ya pili, wanaonekana, wanajeshi wa Pakistani, wakiwa katika doria, kulinda maeneo yao ili yasishambuliwe na Taliban na washiriki wake.

Tuesday, July 14, 2009

Rais wa zamani wa Liberia akanusha mashitaka zidi yake.

Muungano wa Ulaya wapata rais mpya. Brussels, Ubeligiji - 14/07/09.Mbuge wa Poland, Jerzy Buzek, amechaguliwa kuwa rais wa bunge la muungano wa Ulaya, baada ya kuchaguliwa kwa kura nyingi zaid ya 555 kati ya kura 644 zilizo pigwa katika uchaguzi wa rais wa bunge la muungano wa Ulaya. Mbunge, Jerzy Buzek, ambaye ni mbuge wa mlango wa kati kimsimamo, amechaguliwa, ikiwa nchi yake ina miaka minne tangu kujiunga na muungano wa Ulaya. Picha hapo juu, anaonekana, rais wa sasa wa muungano wa Ulaya, akiongea mara baada ya kuchaguliwa kwake.

Rais wa Liberia atuhumiwa na kwa kuhusika kusaidia vita.
Monrovia ,Liberia - 14/07/09. Rais wa sasa wa Liberia,Ellen - Sirleaf, amekumbwa na wakati mgumu, baada ya kamati inayo simamia hali halisi ya uharibifu wa vita nchini Liberia, umeomba rais wa Liberia asimamishwe uongozi wake kwa kuhusika na kundi moja ambalo, lilikuwa likipigana miaka 20 iliyo pita nchini Liberia.
Kamati,inayo shughulika mapatana, mariziano na kusameheana,inasema yakuwa katika watu ambao wametajwa ni rais wa sasa wa Liberia, Ellen - Sirleaf, kwa kuhusika kwa karibu na uongozi wa rais wa zamani Charles Tayrol, ambaye yupo Hague, kujibu mashitaka yana yo mkabili zidi yake.
Hata hivyo, msemaji wa rais , Ellen Serleaf, Cyrus Badio, amesema yakuwa rais ,bado anatafakali ripoti hiyo na ataongea hapo baadaye.
Rais wa zamani wa Liberia, akanusha mashitaka zidi yake.

Hague, Holland - 14/07/09. Rais wa zamani wa Liberia, Charles Taylor ametoa ushahidi wake leo zidi ya makosa 11, ambayo yanamkabili.

Akiongea, mbele ya jaji, rais huyo wa zamani wa Liberia,Charles Taylor,alisema ya kuwa makosa zidi yake ni ya , uzushi,uongo ulio jaa fununu za ajabu,uvumi, na hayana ukweli ndani yake na wale wanao zania ya kuwa yeye alihusika,katika mauaji na machafuko ya liyotokea nchini Sierra Leone.

Machafuko na mauaji hayo yaliyo tokea mwaka 1991 - 2001, yalipoteza maisha ya watu wapatao 200,000. Hata hivyo kesi hii bado inaendelea. Picha hapo juu, anaonekana, rais wa zamani wa Liberia Charles Tayrol kushoto, akiwa mahakamani kutoa ushahidi wake.

Sunday, July 12, 2009

Rais wa Amerika , Baraka Obama, Barani Afrika.

Rais , Baraka Obama, awasili barani Afrika kwa mara ya kwanza akiwa rais wa Amerika.

Akkra Ghana - 11/07/09 . Rais wa Amerika, Baraka Obama, amefanya ziara ya siku moja ya kiserikali nchini Ghana, ikiwa ni kuonyesha ya kuwa serikali yale inatilia mkazo uhusiano Amerika na Afrika.
Katika ziara hiyo, rais Obama, alisema viongozi wa Afrika, wana jukumu kubwa la kujenga na kuendeleza nchi zao kwa misingi uongozi bora kwani wa Afrika ndiyo watakao jenga Afrika.
Picha hapo juu, anaonekana, rais Baraka Obama, akipokea heshima kutoka kwa jeshi la Ghana, kabla ya kuanza rasmi mazungumzo na viongozi wa serikali ya Ghana.
Picha ya pili,anaonekana, rais Baraka Obama, akiongoea mara baada ya kuwasili nchini Ghana.
Picha ya tatu, rais Baraka Obama, mtoto wake Sasha na mtunza jumba la Cape Coast Castle, akiwapa maelezo kwa undani jinsi gani watumwa walivyo kuwa wakitolewa katika jumba la Cape Coast Castle, na kupitia kwenye mlango ambao wanatokea, mlango ambao watumwa alikuwa wakitolewa tayari kwa kusafirishwa kwenda Amerika na kwingine duniani, kuwa watumwa.
Picha ya nne, anaonekana , rais Baraka Obama, akiwa na mwenyeji wake, rais wa Ghana, John Atta Mills, wakielekea kwenye ofisi za Ikulu ya Ghana, tayari kwa mazungumzo.
Picha ya pili, anaonekana, rais Baraka Obama, akiongea na viongozi na wananchi wa Ghana.
Picha ya tano wanaonekana, rais Baraka Omba na mke wake, Michelle Obama, wakiwa waslimia wauguzi na wagonjwa wa hospitali kuu ya jijini Akkra.

Thursday, July 9, 2009

Majina ya walioanzisha vurugu nchini Kenya yakabidhiwa kwa ICC.

Mgomo waleta kichwa kuuma kwa wapenzi wa soka duniani.

Cape Town, Afrika ya Kusini - 09/07/09. Maelfu ya wafanyakazi wanaofanya kazi katika ujenzi wa viwanja vya mpira wa miguu, ambavyo vitatumika katika kuchezea fainali za mpira wa miguu za kombe la dunia 2010 nchini Afrika ya Kusini, wameanza mgomo wao leo, kwa kudai waongezwe malipo ya kipato chao (mshahara) kufikia (asilimia) 13%.
Akiongea na waandishi wa habari, mmoja ya wafanyakazi wa viwanja hivyo 10 vya mpira wa miguu,Martin Baloyi, alisema hayo huku akiwa amelala katika vyuma vya kujengea,yakuwa wanataka wapate pesa ambazo ni haki kwao.
Kwa kipindi cha miezi miwili sasa vyama vya wafanyakazi viwili na South Africa Federation of Civil Engineering Contractors, vimekuwa katika majadiliano bila kufukia muafaka. Vyama hivyo vinavyo wakilisha wafanyakzi wapatao 70,000,, vimedai yakuwa wafanyakazi wamekuwa wakipata malipo ya $ 1.75, kwa saa na vyama hivyo vinataka kipato hichao lazima kiongezwe.
Kufuatia mgomo huu, hali ya ukamilishwaji wa viwanja hivyo kwa ajiliya mshindao hayo, huenda ukaleta kichwa kuuma kwa serikali ya Afrika ya Kusini.
Picha ya kwanza, wanaonekana wafanyakazi wa ujenziwa moja ya kiwanja jijini Cape Town, wakiandamana kudai kipato kiongezeke.
Picha ya pili juu, wanaonekana baadhi ya wafanyakazi wa kujenga moja ya kiwanja cha mpira wakiwa wamekaa chini baada ya kuanza mgomo,huku nyuma yao ni kiwanja cha mpira wa miguu kikiwa hakijakamilika ujenzi wake.
Majina ya lioanzisha vurugu nchini Kenya, yakabidhiwa kwa ICC.
Hague, Uhollanzi - 09/07/09. Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan, amekabidhi majina ya watu waliohusika katika vurugu wakati na baada ya uchaguzi wa Kenya, uliofanyika mwaka 2007.
Kwa mujibu wa habari, zinasema Kofi Annan, alimkabidhi mwanasheria wa mahakama inayo shughulikia makosa ya ukiukwaji wa haki za binadamu, bwana, Moreno Ocampo.
Hata hivyo, swala hilo halikuwafurahisha baadhi ya viongozi wa Kenya, kwani walikuwa wanadai yakuwa kesi za watu hao ingebidi zisikilizwe nchini Kenya, lakini baadhi ya viongozi wengine walisema,ikiwa kesi hizo sitasikilizwa nchi Kenya, huenda kukakiukwa baadhi ya sheria na kutakuwa hakuna njia bora ya kuwalinda mashahidi.
Hapo juu,anaonekna Kofi Annan, akiwa amefunga mkono, huku akiangali juu.
G8, zahaidi kushirikiana kupunguza uzalishaji wa hewa chafu duniani.
Laquila, Itali - 09/07/09. Viongozi wa nchi tajiri duniani, G8 wanaendelea kukutana nchini Itali, kujadili ni jinsi gani, zitashirikiana kupunguza uzalishaji wa hewa chafu inayozalishwa na viwanda vikubwa, mitambo mikubwa na teknoloji zinazo atarisha mazingira na viumbe vyake kwa ujumla.
Wakiongea kwa nyakati tofauti, wakiongozwa na rais, Baraka Obama, walihaidi kupunguza hewa chafu kwa kiasi cha (digree) nyuzi 2 celsius mpaka itakapo fika 2050.
Akiongea kusisitiza hayo rais Amerika , Baraka Obama, alisema ya kuwa viongozi wa sasa wana deni kubwa ambalo itawabidi washirikiane ili kulinda hali ya hewa isichafuliwe zaidi na hewa chafu inayo tokana kukua kwa maendeleo ya nchi tajiri, na akashauri ni lazima nchi tajiri ziangalie na kubuni mbinu mpya za kuleta maendeleo bila kuharibu mazingira kwani hakuna wa kulaumiwa, hili ni jukumu la kila nchi na watu wake.
Picha hapo juu wanaonekana viongozi wa G8, wakiwa pamoja baada ya mkutano wao kwanza kuisha.
Hali ya usalama wa Irak,bado mthiani kwa serikali ya Irak.
Tal Afar,Iraq - 09/07/09.Watu wapatao 33wamefariki dunia kwa mlipuko wa mabomu, baada ya mauaji ya kujitolea muhanga kulipuka sehemu tofauti, na kuacha zaidi ya watu 70, wamejeruhiwa vibaya.
Kwa mujibu , wa msemaji wa polisi,Kanali, Khaled Omar, mashambulizi hayo, yametoke karibu na ofisi za mahakama.
Wakati huo huo, kwa mujibu wa habari zilizotolewa na serikali, zina sema zaidi ya watu 437, wamepoteza maisha tangu kutangazwa kwa jeshi la Amerika, kulipa madaraka jeshi la Iraq.
Picha hapo juu, anaonekana kijana, mmoja ambaye ameumia vibaya baada ya kuwa katika eneo bomu lililolipuka.

Tuesday, July 7, 2009

Dunia nzima yamuaga Michael Jackson kwa huzuni. Mungu ailaze roho yake peponi.Amina

Dunia nzima, yamuaga,Michael Jackson kwa huzuni. Mungu ailaze roho yake peponi. Amina.

Los Angeles, Amerika - 0 7/07/09.Maelfu waliuzuria misa na maombi ya mwisho ya kumuaga mfalme wa musiki wa Pop Michael Jackson,ambaye alifariki siku 25/05/09.
Katika maombi hayo yaliuzuriwa, ndugu, marafiki,viongozi wa dini zote,waumini na wapenzi wa hayati mfalme wa musiki wa POP, Michael Jackson.
Picha hapo juu picha, zilizo pigwa wakati wa misa ya mwisho kukumuaga Michael Jackson, zinajieleza zenyewe, ni kwa jinsi gani tulivyo mpenda, Michael Jackson, wa kubwa kwa watoto.
Mfalme wa musiki, Michael Jackson, dunia nzima tutakukosa,umetwachia kumbukumbu ya milele kwa musiki wako na staili ya uchezajiwa wako, ulikuwa Michael Jackson,utabaki Michael Jackson, milele..
Michael Jackoson, Mungu ailaze roho yako peponi. Amina.