Tuesday, January 20, 2009

Baraka Hussein Obama,aapishwa rasmi kuwa rais wa 44 wa Amerika."Amerika ya pata rais wa kwanza Mwafrika ( Mweusi), ukurasa mpya umefunguliwa.

Baraka Hussein Obama, aapishwa rasmi kuwa rais wa 44 wa Amerika. "Amerika ya pata rais wa kwanza Mwafrika (Mweusi) na ukurasa mpya umefunguliwa, na ndoto imetimia.

Washington,Amerika. 20/01/09 - Baraka Hussein Obama, ameapishwa rasmi kuwa Rais wa 44 wa Amerika.
Rais, Baraka Hussein Obama, ambaye alishinda uchaguzi kwa kura nyingi zidi ya mpinzani wake kutoka chama cha upinzani cha Republikan bwana, Jonny MacCain.
Kuapishwa kwa na kukabiziwa ofisi, kumeleta msisimko mkubwa kwa jumuia ya kimataifa, kwa kuzingatia ya kuwa ni rais wa kwanza mweusi - Afrikan Amerikan, na kutimiza zile ndoto za viongozi waliopita.
Akiongea katika hutuba yake ya kwanza, baadada ya kuapishwa, rais Baraka Hussein Obama, aliiakikishia jumuia ya mataifa ya kuwa Amerika, ipo kwa kuleta amani na utulivu, na Amerika ni rafiki wa kila nchi na wananchi wake, na kuhaidi kuleta mabadiliko ndani ya Amerika na kwa jumuia ya kimataifa.
Picha ya hapo juu anaonekana rais mpya wa Amerika, Baraka Husseina Obama, akihutubia taifa mara baada ya kuapishwa kuwa rais wa 44 wa Amerika.
Picha ya pili, wanaonekana baba na mama yake rais, mwafrika wa kwanza ( mweusi), Baraka Hussein Obama kuwa rais wa Amerika tangu taifa la Amerika kuundwa wakiwa wamepiga picha ya pamoja wakati wa ujana wao.
Picha ya tatu,anaonekana, rais mpya wa Amerika rais, Baraka Hussein Obama, akiwa na baba yake, Hussein Obama, wakati wa utoto wa rais Baraka Obama.
Picha ya nne, wanaonekana, wananchi wakiwa wameshikilia, kitambaa kikubwa, kilicho andikwa, hatimaye tumeshinda, (Tumevuka).
Picha ya tano anaonekana, rais wa zamani wa amerika, George Bush, akiwa ndani ya helkopta tayari kuondoka, kuelekea nyumbani, baada ya kazi ngumu ya miaka minane ya kuongoza nchi.
Picha ya sita, wanaonekana, rais mpya wa Amerika, Baraka Hussein Obama kushoto, mke wa rais wa zamani wa Amerika, Laura Bush kati kushoto, rais wazamani wa Amerika George .W. Bush, kati kulia na mke wa rais mpya wa Amerika Michelle Obama, walipo piga picha ya mwisho, kabla ya rais wa zamani wa Amerika, George Bush, kuondoka rasmi Ikulu ya Amerika.
Picha ya saba, wanaonekana, rais wa zamani wa Amerika George Bush na rais mpya wa Amerika Baraka Hussein Obama, wakikumbatiana mara baada ya rais,Baraka Hussein Obama, kuapishwa kuwa rais wa 44 wa Amerika.
Picha ya nane, ni mikono ya bwana na bibi Baraka Hussein Obama, wakila kiapo mbele ya Mungu,na wananchi wa Amerika huku wakiwa wameshikilia Biblia, na Biblia hii ilitumiwa na rais wa kumi na sita wa Amerika, Abraham Linconi.
Picha ya tisa, anaonekana rais mpya wa Amerika, Baraka Hussein Obama,akila kiapo kuwa rais wa Amerika, huku mke wake akiwa ameshikilia Biblia.
Picha ya kumi, wanaonekana, rais mpya wa Amerika, Baraka Obama, na familia yake wakiwasalimia wananchi baada ya kuapishwa kuwa rais.
Picha ya kumi na moja,anaonekana, mke wa rais mpya wa Amerika, akisalimia huku ameshikilia Biblia, ambayo mume wake,ameitumia kuapa mbela ya Mungu, ili kuwa rais wa Amerika.
Picha ya kumi na mbili, wanaonekana, rais mpya wa Amerika, Baraka Obama, na John Kerry wakiwa wanaongea mara baada ya Baraka Obama, kumaliza kuongea katika mkutanao wa kumuunga mkono, John Kerry wakati alipokuwa anaaanza kampeni ya kutaka kugombea urais mwaka 2004.
Picha ya kumi na tatu anaonekana, Baraka Obama, enzi ya toto wake, akiwa ameshikilia, fimbo ya kupigia mpira, kuonyesha ni jinsi gani alivyo kuwa tayari kupambana na kushinda.
Picha ya kumi nanne, Barka Obama, akionyesha ni jinsi gani,anaweza tawala hata kwenye maji,hii inaonekanakwenye picha hapo chini, akiwa amezungukwa na maji ya bahari.
Picha ya mwisho, anaonekana, Baraka Obama, na mama yake, Stanley Anna Dunham, wakiwa pamoja katika sehemu moja ya kuchezea watoto.

Tuesday, January 13, 2009

Guantanamo bay,kufungwa, Obama akichukua ofisi.

Ethiopia ya ondoa majeshi yake nchini Somalia,"Wasiwasi wazidi". Addis Ababa,Ethiopia-13/01/09. Serikali ya Ethiopia, imetangaza rasmi, jeshi lake lililo kuwa linasaidia kulinda usalama nchini Somalia, limeanza rasmi kuondoka nchini Somalia kuelekea nyumbani. Kufuatia kuondoka kwa jeshi la Ethiopia,hali ya usalama nchini Somalia imekuwa katika hali ya wasiwasi kwa mujibu wa mmoja wa makzi wa mji wa Mogadishu Hata hivyo, kuna habari ya kuwa umoja wa Mataifa, upombioni kupitisha mswada wa kupeleka jeshi la kimataifa ili kulinda amani,kwani kuondoka kwa jeshi la Ethiopia, kumeacha majeshi ya Burundi na Uganda kuwa majeshi pekee ambayo yanasaidia kulinda amani kwa serikali ya Somalia. Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza awa na kazi ngumu na mgogoro wa Mashariki ya Kati.

London,Uingereza-13/01/09.Vita vinavyo endelea katia ya Izrael na Palestina,vimeleta utata na kazi kuwa ngumu kwa aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Tony Brair, ambaye anashughulikia swala la kuleta amani katia ya Waizrael na Wapalestina.
Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza, Tony Brair,ambaye anashughulikia kuinua maendeleo ya Wapalestina kwa ujumla waishio wa Gaza na West Bank, amekuwa akikumbana na wakati mgumu kwa kuzingatia vita vinavyo endelea kati ya kati ya Izrael na Palestina.aliyaongea haya Mustafa Barghouti amabye ni mmoja ya viongozi wa serikali ya Wapalestina.
Picha ya pili anaonekana Tony Brair,akiwa anasikiliza kwa makini waswali anayo ulizwa kuhusu mgogoro kati ya Izrael na Palestina katika moja ya mikutano na waandishi wa habari.
Picha ya pili wanaonekana , Tony Brair na rais wa Wapalestina, Mahamoud Abbas walipo kutana hivi karibuni kujadiri maendeleo ya Wapalestina.
Guantanamo Bay kufungwa, Obama akianza kazi.
Washington, Amerika-13/01/09.Rais mchaguliwa wa Amerika, Baraka Obama,atatia sahii kufungwa mara moja kwa gereza la Guantanamo Bay, mara baada ya kuapishwa kuwa rais wa Amerika, Gantanamo Bay, imekuwa jela ya kuwafungia watuhumiwa wanao shukiwa kuhusika na ugaidi.
Baraka Obama, ataapishwa kuwa rais, siku ya jumanne 20/01/09.
Picha hapo juu anaonekna , rais mtarajiwa wa Amerika, Baraka Obama, akiongea katika moja ya mikutano, na amekuwa akisisitiza kufungwa kwa gereza la Guantanamo Bay, kwani linailetea sura mbaya Amerika.
Picha ya pili wanaonekana watuhumiwa ( wafungwa) wakiwa ndani ya jela ya Guantanamo Bay, ambamo wengi wa wafungwa hawa wamekaa muda mrefu katika jela hiyo bila kuhukumiwa.
Picha ya tatu, wanaonakana, wanajeshi wa Amerika, wakiwa wana wachunga baadhi ya watuhumiwa wanao shutumiwa kuhusika na ugaidi.
Simu ya waziri mkuu ya fanya kura kutopigwa "jibu ni mgogoro wa Izrael na Palestina".
Jerusalem,Israel-13/01/09. Waziri Mkuu wa Izrael, Ehud Olmert, amesema yakuwa alimpigia simu rais George Bush, kuomba Amerika isipige kura kupitisha kura ya kutaka kusimamisha mapigano kati ya Izrael na Palestina.
Kufuatia hatiua hiyo, waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika,Condoeezza Rice, aliacha kupiga kura na kutoka katika kikao cha kamati ya usalama ya umoja wa mataifa.
Picha hapo juu, wanaonekana, Condoleezza Rice akisalimiana na waziri mkuu wa Israel Ehud Olmert, mapema walipo kutana nchini Izrael, kujadiri mgogoro wa Izrael na Palestina.
Picha ya pili, wanaonekana wajumbe wa kamati ya usalama ya umoja wa Mataifa, wakiwa katika moja ya kikao ili kujadili maswala ya kiusalama yanayo ikabili swala la Mashariki ya Kati.
Picha ya tatu, anaonekana,Condoleezza Rice, akiwa katika kikao cha kamati ya usalama ya umoja wa Mataifa, wiki iliyo pita kujadili swala la amani ya Mashariki ya Kati.
Mkutano wa nchi za Kiaarabu,utakao fanyika Doha, wawa na mvutano.
Doha, Katar-13/01/09. Serikali ya Misri,imekataa kukubaliana na jumuia ya nchi za Kiaarabu kutumia mkutano unao tarajiwa kufanyika mjini Doha,tarehe 18/01/09,kujadiri swala la vita vinavyoendelea katia ya Israel na Palestina.
Kikao hicho, hicho cha jumuia ya Kiaarabu, ambao unatarajia kuzungumzia maswala ya kiuchumi, huenda ukakumbwa na mvutano mkubwa, kati ya nchi wanachama wa jumuia hiyo.
Picha hapo juu ni ya nchi ya Misri, nchi ambayo ina shughulika, swala la kuleta amani kati ya Waizrael na Wapalestina kwa Muda mrefu,bila mafanikio ya kusimamisha vita hivi milelel.
Picha ya pili ni ya Katibu wa jumuia ya Kiaarabu, Amr Moussa akiongea na waandishi wa habari, mara baada ya kumaliza kikao kuhusu swala la mgogoro wa mashariki ya kati nadi ya UN- Umoja wa Mataifa

Thursday, January 8, 2009

Mashoga wafungwa miaka kwa kuwa mashoga.

Vyombo vya habari vya nchi za Magharibi zachafua jina la letu"China ya dai"

Beijing,China-08/01/09.Waziri wa mambo ya nje ya China Quin Gang, ameziliaumu nchi za Magharibi kwa kutumia vyombo vya habari kuharibu jina la nchi yake China.
Akisisitiza ya kuwa nchi kama Zimbabwe na Jamuhuri ya Kongo (DRC) ya kuwa zina fanya biashara na China kinyume cha sheria katika ununuzi wa siraha, hii siyo kweli.
Waziri, Quin Gang, alisema kwa mtu au shirika lolote likichunguza kwa undani, wataona yakuwa yote wanayo sema siyo ya kweli.
Picha ya hapo juu, ni ya bendera ya China, nchi ambayo inasema vyombo vya habari ya Magharibi vina chafua jina la nchi ya China.
Picha ya pili ni ya moja ya vyombo vya habari,ambavyo vinadaiwa kuchafua jina la China, kwa kutangaza mambo yasiyo ya kweli.
Mashoga wafungwa miaka kwa kuwa mashoga.
Dakar, Senegal-08/01/09- Watu tisa wamehukumiwa kwenda jela miaka minane, baadada ya kukutwa na hatia ya kuhusika na maswala ya ushoga.Kwa mujibu wa mwanasheria wa watuhumiwa hao,Diadji Diouf.
Picha hapo juu ni ya bendera ya nchi ya Senegal,nchi ambayo ushoga ni kinyume na sheria ya nchi.Picha ya pili ni ya bendera ya jumuiya ya mashoga.
Picha ya tatu wanaonekana mashoga wakibusiana,kuwepo kwa mashoga katika nchi nyingi za Afrika ni kinyume na sheria, lakini mashoga waishio Ulaya, wamekuwa wanapata haki sawa kama binadamu wengine.
Jumuiya ya Ulaya na Urusi bado kukubalina kuhusu swala la gasi.
Brussel,Belgium-08/01/09.Jumuiya ya Ulaya imekuwa na mazungumzo na kampuni ya mafuta ya Urusi Gazprom, ambayo imefunga usambazaji wa gasi katika nchi za jumia ya Ulaya.
Ufungaji wa usambazaji wa gas, umekuja baada ya Urusi kudai ya kuwa Ukrein imefungua bomba linali sambaza gas Ulaya, na kusamba za gasi hiyo nchini Ukrein.
Mvutano huo wa gasi, umekuja baada ya serikali ya Ukrein kushindwa kukubaliana kimsingi juu ya bei ya gasi.
Picha hapo juu ni moja ya mitambo ya kusambazia gasi,ikikaguliwa na mmoja ya wafanyakazi, hasa kwa kipindi hiki cha baridi katika nchi za Ulaya.
Picha ya pili ni ya bendera ya Urusi nchi ambayo ndiyo msambazaji mkuu wa gasi katika nchi nyingi za Ulaya.
Picha ya tatu, ni ya bendera nchi za jumuiya ya Ulaya, nchi hutegemea gasi kwa matumizi kutoka Urusi.
UN- Umoja wa Mataifa wanyanyua mikono juu, kutokuendelea kutoa misaada Gaza."Hadi hapo hali ya usalama itakapo kuwepo"
Gaza, Ukanda wa Gaza-08/01/09.Shirika la kutoa misaada la Umoja wa Mataifa, limesimamisha misaada yake yote kuelekea eneo la Gaza.
Uamuzi huuo umekuja baada ya mmoja ya wafanyakazi wake kushambuliwa na kupoteza maisha wakati jeshi la Isreal lilipo shambulia msafara wa misaada ya vyakula na madawa vilivyokuwa vikielekea Gaza.
Picha hapo juu linaonekana moja ya gari la kubebea wagonjwa likiwa njiani kuwapeleka majeruhi ambao wamajeruhiwa katika vita vinavyo endelea kati ya Israel na Palestina katika eneo la Gaza.
Picha ya pili, linaonekana lori likiwa limebeba shehena kuelekea Gaza, lakini hata hivyo magari hayao yamekuwa yakukutwa na misukosuko na mengine kutokufika yanapo takiwa kupeleka misaada.
Picha ya tatu, zinaonekana baadhi ya majengo yakiwa yamezunguka mosho unaotoka katikati, baadaya ya eneo hilo kushambuliwa na jeshi la Israel.

Wednesday, January 7, 2009

Ghana yapata rais mpya

Ghana yapata rais mpya.

Accra Ghana -7/01/09. John Atta Mills, mwenye miaka 64, ameapishwa kuwa rais wa Ghana, baada ya kushinda uchaguzi wa urais zidi ya mpinzani wake Nana Akufo Addo.
Rais John Atta Mills,ambaye aligombea urais kwa kupitia chama cha NDC - National Demokratik Kongresi, aliweza kushinda kura kwa kupata asilimia 50.23% zidi ya mpinzani wake Nana Akufo Addo aliyepata asilimia 49.77%.
Picha hapo juu anaonekana rais mpya wa Ghana, John Atta Mills, akiapa mbele ya Mungu na wananchi wa Ghana, ili kuwa rais wa Ghana.
Picha ya pili, anaonekana, rais mpya wa Ghana John Atta Mills, akiangalia kwa makini, wakati wa uchaguzi ukindelea kabla ya matokeo kutoka yakuwa, John Atta Mills ameshinda uchaguzi wa rais.
Picha ya tatu, anaonekana rais, John Atta Mills, akiwasalimia wanchama na wapenzi waliompigia kura kuwa rais.
UN - Umoja Wamataifa washikwa kigugumizi kutatua mgogoro wa Israel na Palestina.
Gaza,Ukanda wa Gaza - 4/01/09.Vita vinavyo endelea kati ya Israel na Kundi la Hamas, zimefikia hatua ya kugonisha vichwa jumuiya za kimataifa.
Kwa mujibu wa wachunguzi wa maswala ya kisiasa katika eneo hili la mashariki ya kati,wanasema yakuwa mvutano uliopo kati ya Wapalestina na Israel,umefikia kiwango cha kuzifanya nchi za jumuiya za kimataifa kushindwa kuamua,kwa kwa kuzingatia uhusiano uliopo kati ya nchi hizi zikiongozwa na Amerika.
Hali hii imefika kutoangalia haki za binadamu kwa pande zote mbili , Israel na Wapalstina na jumuiaya ya kimataifa inaangalia huku wakitupiana maneno nani aanze kusimamisha vita.
Kwa upande wa Israel, inasema ni lazima Hamas isimamishe kabisa kutumia roket kwa kubomu ndani ya Israel,na wakati uhuo huo, Palestina chini ya Hamas na Fatah,zinadai lazima Israel, iondoke katika maeneo inayo yakalia kwa nguvu.
Picha hap juu, ianaonyesha moshi ulio jaa moto ukilipuka baada ya jeshi la Israel,kutupa mabomu yake ndani ya maene ya liyopo Gaza.
Picha ya pili wanonekana wanachama wa Hamas na na Wapalestina kwa ujumla wakiandamana kupinga kitendo cha Israel kuvamia Gaza.
Picha ya tatu, wanaonekana wanajeshi wa Israel wakimsaidia askari mwenzao, baada ya ku jeruhiwa katika mapambano na Hamas.
Picha ya nne , linaonekana jengo likilipuka baada ya kushambuliwa na mabomu kutoka kwenye helkopta za kijeshi za Israel.