Sunday, November 27, 2016

Rais Fidel Castro hatupo naye tena

Rais wa kwanza wa Kuba aaga dunia.


Havana, Kuba - 26/11/2016. Fidel Castro 90 rais wa kwanza wa Kuba na mwana mapinduzi amaefariki dunia.
Akitangaza kupitia luninga ya nchi hiyo, rais was sasa wa Kuba Raul Castro, alisema kuwa "rais wetu wa kwanza na kiongozi na mwanamapinduzi Komrade Fidel Castro amefariki leo 25/11/2016."
Kufuatia kifo cha rais Castro, Kuba itakuwa katika maombelezo ya siku tisa. Mazishi ya rais huyo wa Kuba yanatarajiwa kuudhuliwa na viongozi mbalimbali wa dunia.
Fidel Castro alikuwa mpinzani wa siasa za kibepari na alikuwa akipenda kusema "Uwanamapinduzi ni ni mapambano mpaka kufa ya wakati uliyo pita na wakati ujao."
"Wanaongea kushindwa kwa ujamaaa, lakini yapo wapi mafanikio ya siasa za kibepari katika bara la Afrika Asia na Latin Amerika?
" Sikubaliani na ubepari, ni mbaya auvutii na unatenganisha unaleta vita vitna na mashindano yasiyo na tija katika jamii."
Marehemu rais mstaafu wa Kuba Fidel Castro alizaliwa mwaka 31/08/1926 mjini Biran Kuba.

Wednesday, November 9, 2016

Donald John Trump ashangaza ulimwengu wa Siasa, Achaguliwa kuwa rais wa Marekani

Donaldo John Trump achaguliwa kuwa rais wa 45 wa Marekani

New York, Marekani - 09/10/2016.  Donald John Trump, amechaguliwa kuwa rais wa 45 Marekani baada ya kupata vit vya kura 289 zidi ya mpinzani wake Hillary Clinton aliyepata viti vya kura 218.

Donald Trump akiongea mbele ya wapenzi na washabiki wake walikuwa katika hotel yake inayo julikana kama The Trump alisema. " Hillary Clinton amenipigia simu na kutupongeza na ninampongeza kwa jitihada zake wakati wa harakati wa uchaguzi huu."

"Ushindi wa leo, ni harakati na hazikuwa kampeni za uchaguzi, hivyo hizi harakati ndio sasa zimeanza kazi."

Vilevile rais mteule Donald Trup, aliwaomba watu wote kuwa wamoja na kwa kusema kuwa wale waliomchagua na wasionipigia kura wote wawe kitu kimoja na kuwa atakuwa rais wa Wamarekani wote.  "Nawaomba wote walio umia kutokana na uchaguzi tuwe wamoja ili kujenga Marekani mpya."

Rais mteule, Donald Trump, alikumbana na vikwazo vya kila namna katika kampeni za kuwania urais wa Marekani, kwa kudaiwa kuwa mbaguzi, msemaji wa vitu na mambo ambayo si yakiutu an pia kudaiwa kuwa alikuwa anadhalilisha wanawake.

Ushindi wa Donald Trup unatafsiliwa kuwa ni jibu kwa wanasiasa kwamba wabadirike kwa kuwa wa watu wamechoka na siasa zisizo eleweka na haadi wazizotimiza.

Friday, October 28, 2016

Tony Blair ateta lake juu ya Brexit



London Uingereza - 28/10/2016. Waziri wa zamaniwa Uingereza Tony Blair, ameongelea wasiwasi wake kuhusu madhara ambayo huenda yakatokea baada ya Uingereza kuanza rasmi mazungumzo ya kujitoa katika jumuiya ya muungano wa nchi za umoja wa Ulaya.

Akiongea na BBC 4 radio, Blair alisema "Ikiwa tutatoka katika jumuiya ya Ulaya, basi madhara yake yatakuwa makubwa kijamii na kiuchumi."
Blair aliyasema hayo kwa kusisitiza kuwa watu 48% ya wakipiga kura walipiga kura ya kubaki ndani ya Umoja wa Ulaya na kwani walijua umuhimu wake.

"Wananchi wanatakiwa wapewe nafasi ya kuliangalia hili suala kwa undani, ikibidi kuwepo na kura ya nyingine kuhusu Uingereza kuwa mwanachama wa Umoja wa Ulaya."

Hata hivyo Maria Caulfield, mbunge wa chama tawala cha Conservative na mmoja wa viongozi wanao shughulikia Uingereza kujitoa katika muungano wa umoja wa Ulaya amesema " Blair anatakiwa  kutoa mawazo ya kuijenga Uingereza iliyo amua kuwa nje ya jumuiya ya nchi za Ulaya na siyo vinginevyo"

"Blair anapinga demaokrasi, wanachi walishaamua na matakwa yao lazima sisi kama viongozi tuyatekeleze." Alisisitiza  Caulfield.

Maoni hayo ya Tony Blair yamekuja kufuatatia maswali mengi yanayo ulizwa kuhusu nafasi ya Uingereza baada ya kujitoa rasmi katika muungano wa jumuiya ya nchi za Ulaya na kushuka kwa thamani ya fedha ya Uingereza tangu Waingereza kupiga kura ya kukataa kuwa jumuiya ya Ulaya.

 

Sunday, March 20, 2016

Rais Jakaya Kikwete


Mwandishi wa Habari na Mtangazaji, Rukundo L Kibatala, anakuletea makala fupi ya historia ya Uongozi wa Rais Mstaafu wa Tanzania ndugu Jakaya M Kikwete.

Wednesday, March 9, 2016

Iran yarusha makombora.


Tehran, Iran 09/03/2016. Jeshi la Iran limefanikiwa kurusha makombora mawili  (Ballist missiles)  Urushaji wa makombora hayo yaliyo pewa majina ya Qadr -H na Qadr F ulifanyika kaskazini mwa nchi hiyo katika eneo lijulikanao Alborz Mashariki. Makombora hayo yanauwezo wa kushambulia umbali wa kilomita 1500 hadi 2000.

Kamanda wa kitengo cha usalama wa anga wa Iran, Brigedia, Amirali Hajizadeh amesema kuwa. "Kombora aina ya Qadr H linuwezo wa kushambulia umbali wa kilomita 1700 na jingine Qadr F linaweza haribu na kuchakaza kabisa kitu chochote kilichopo umbali wa kilomita 2000."

Tamko la Iran kuhusu kurusha makombora yake, limekuja baada ya msemaji  wa serikala ya Marekani Mark Toner kukosoa kitendo hicho nakusema " Kufuatia kitendo hicho cha Iran, Marekani italifikisha suala hilo katika balaza la usalama la umoja wa mataifa."

Hata hivyo waziri wa mambo ya nje wa Iran Javad Zarif, amesema kuwa " Iran haitaji ruhusa yoyote katika masuala yake ya kiulinzi wa nchi, na tulisha sema kuwa hatuta ulizia wala  omba ruhusa katika kushughulikia masuala yetu ya kiulinzi."

Iran nchi ambayo ilikuwa imewekewa  vikwazo vya kiuchumi kwa muda mrefu na Marekani na washiriki wake, imekuwa kwa miaka mingi ikijitengenezea mitambo ya kiulinzi ya kijeshi na pia kuhakikishia jumuia ya kimataifa kuwa utengenezaji wa zana za kiulinzi  ni harakati za kujiimarisha katika suala la ulinzi wa nchi.




Wednesday, March 2, 2016

Osama bin Laden alitaka mirathi yake itumike kundeleza mapambano. 


Aliyekuwa kiongozi wa kundi la Al Qaeda, Osama bin Laden, alikuwa ameandika kuwa mirathi yake  ya kifedha zipatazo $29 millioni, kwa kiasi kikubwa zitumike takika kusaidia kuendeleza "Jihad" mapambano,  na kiasi kidogo kigawiwe kwa ndugu wa familia, ijapokuwa mpaka hazijulikani hizo fedha zipo wapi.

Zikiwa zimeandikwa kwa mkono wa Osama bin Laden, habari hizi, zimetolewa na serikali ya Marekani wiki hii, baada ya kuruhusu mafaili yaliyo kamatwa na kikosi maalumu cha kijeshi cha Marekani wakati walipo kuvamia makazi na  maficho  ya Osama bin Laden yaliyo kuwepo kwenye mji wa Abbottabad  Pakistan siku ya 1. Mai 2011 na kufanikiwa kumua.

"Nivyema kwa jamii kufahamu nini kiongozi wa Al Qaeda alipanga"  Alisema Brian Hale Mkurugenzi wa mambo ya jamii kutoka idara ya upelelezi ya taifa ya Marekani huku akiwa anaonyesha makaratasi yaliyo chukuliwa kutoka katika makazi wa Osama bin Laden

Karatasi hiyo ambayo inaonyesha nini kiongozi wa Al Qaeda alitaka kifanyike katika mirathi yake, ni moja ya makatasi 100 ambayo yameruhusiwa kuwekwa hadharani, baada ya kamati ya ulinzi na usalama kuyapitia kwa uangalifu.



Sunday, February 28, 2016

Urusi yazidi kujiimarisha kijeshi.


Urusi yazidi kujiimarisha kijeshi.

Urusi imeonyesha rasmi gari mpya  aina ya Batmobile ambayo itatumika katika mapambano ya kivita na vurugu za aina yoyote. Gari hiyo ambayo hapo awali ilijulikana kama  Punisher, inasemekana ni jibu kwa gari la kijeshi la Kimarekani Humvee.


Akiongea wakati wa kukagua gari hii mpya ya kijeshi, rais wa Urusi, Vladmir Putin alisema "nawashukuru kwa jitihada  na hii inahakikishia kuwa Urusi ipo tiyari kujibu mashambulizi ya aina yoyote pindipo tutakapo shambuliwa."

Kwa mujibu wa shirikala la habari la Urusi RT, gari hii mpya ya Kirusi, inauwezo wa kuchua watu kumi na ndani gari hii ina muundo wa V ambao inatoa kinga kubwa kwa watumiaji wa gari hii pindipo wakishambuliwa au gari kushambuliwa na bomu na vilevile hili gari lina mitambo ya kurushia mizinga.

Uzinduzi wa gari hili, unatarajiwa kuleta vichwa kuuma kwa Marekani na washiriki wake, kwani Urusi tangu iingilie vita vya Syria, nguvu zake za kijeshi zimefanya kuwepo na mabadiriko makubwa ya kivita kati ya serikali ya Syria inayo ungwa mkono na Urusi na wapinzani wa serikali wanao ungwa mkono na nchi za magharibi.

Thursday, February 4, 2016

Shirika la utangazaji la RT la Urusi lawa tishio.

Shirika la utangazaji la RT la Urusi lawa tishio.


Shirika la utafiti wa masuala ya kiusalama la Marekani CEPA, limemlaumu George Galloway mtangazaji na mwanasiasa mkongwe wa Uingereza ya kuwa kipindi chake  Sputnik kinacho tangazwa katika luninga ya Kirusi - RT kuwa kinahatarisha na kuzidharaulisha serikali za nchi za Magaharibi na NATO.

CEPA Center for European Policy Analysis yenye makao ya ke makuu jijini Washington, limesema kutokana na kuwepo na RT  inayo tangaza kiingereza, kipindi cha Sputnik, kimekuwa kikitumika kama sehemu ya kukuza na kundesha  juhudi za Urusi dunia kwa kuponda mipango na mikakati ya Marekani na washirika wake.

Ripoti ya hiyo ambayo ilitolewa January 2016, iliandaliwa ili kufanya utafiti ni kwa jinsi gani amshirika ya habari yanavyo fanya kazi na shirika la utangazaji wa luninga RT likanonekana kuwa linazidi kukua na kuwa tishio kwa mashirika ta utangazaji ya nchi za Ulaya Mgharibi na Marekani.