Sunday, February 28, 2016

Urusi yazidi kujiimarisha kijeshi.


Urusi yazidi kujiimarisha kijeshi.

Urusi imeonyesha rasmi gari mpya  aina ya Batmobile ambayo itatumika katika mapambano ya kivita na vurugu za aina yoyote. Gari hiyo ambayo hapo awali ilijulikana kama  Punisher, inasemekana ni jibu kwa gari la kijeshi la Kimarekani Humvee.


Akiongea wakati wa kukagua gari hii mpya ya kijeshi, rais wa Urusi, Vladmir Putin alisema "nawashukuru kwa jitihada  na hii inahakikishia kuwa Urusi ipo tiyari kujibu mashambulizi ya aina yoyote pindipo tutakapo shambuliwa."

Kwa mujibu wa shirikala la habari la Urusi RT, gari hii mpya ya Kirusi, inauwezo wa kuchua watu kumi na ndani gari hii ina muundo wa V ambao inatoa kinga kubwa kwa watumiaji wa gari hii pindipo wakishambuliwa au gari kushambuliwa na bomu na vilevile hili gari lina mitambo ya kurushia mizinga.

Uzinduzi wa gari hili, unatarajiwa kuleta vichwa kuuma kwa Marekani na washiriki wake, kwani Urusi tangu iingilie vita vya Syria, nguvu zake za kijeshi zimefanya kuwepo na mabadiriko makubwa ya kivita kati ya serikali ya Syria inayo ungwa mkono na Urusi na wapinzani wa serikali wanao ungwa mkono na nchi za magharibi.

Thursday, February 4, 2016

Shirika la utangazaji la RT la Urusi lawa tishio.

Shirika la utangazaji la RT la Urusi lawa tishio.


Shirika la utafiti wa masuala ya kiusalama la Marekani CEPA, limemlaumu George Galloway mtangazaji na mwanasiasa mkongwe wa Uingereza ya kuwa kipindi chake  Sputnik kinacho tangazwa katika luninga ya Kirusi - RT kuwa kinahatarisha na kuzidharaulisha serikali za nchi za Magaharibi na NATO.

CEPA Center for European Policy Analysis yenye makao ya ke makuu jijini Washington, limesema kutokana na kuwepo na RT  inayo tangaza kiingereza, kipindi cha Sputnik, kimekuwa kikitumika kama sehemu ya kukuza na kundesha  juhudi za Urusi dunia kwa kuponda mipango na mikakati ya Marekani na washirika wake.

Ripoti ya hiyo ambayo ilitolewa January 2016, iliandaliwa ili kufanya utafiti ni kwa jinsi gani amshirika ya habari yanavyo fanya kazi na shirika la utangazaji wa luninga RT likanonekana kuwa linazidi kukua na kuwa tishio kwa mashirika ta utangazaji ya nchi za Ulaya Mgharibi na Marekani.