Saturday, December 31, 2011

Kwaheri 2011 kwa mafundisho, karibu 2012 kwa wema barani Afrika.

 Kwaheri 2011 kwa mafundisho, karibu 2012 kwa wema barani Afrika.


 
Mwaka 2011 utakumbukwa na Waafrika kama mwaka ambao ulikuja na majonzi na furaha ya  kihistoria, hasa kwa kizazi cha tatu cha bara la Afrika.
Kizazi cha tatu cha Afrika, ni wale wote waliozaliwa miaka ya 70 hadi miaka ya 90 tangu Afrika ipate uhuru kutoka kwa wakoloni na mwaka 2011 na chini ya uongozi wa demokrasi wameongozwa na kubadika kuliko walivyo tarajia.
 Kizazi hiki cha tatu cha Waafrika  waliozaliwa miaka ya 70 na hadi 90  wameweza kuona mabadiliko ya kijamii, kisayansi, kiuchumi na siasa ambayo wengi hawakutarajia kuyaona kwa muda mfupi wa maisha walioishi kulinganisha na baba mama, mababu na mabibi waliopigania uhuru.
Mwaka 2011 mengi yametokea, hasa kubwa katika swala la kisiasa chini ya kiongozi demokrasi na kuleta mauaji na machafuko katika bara la Afrika tangu uhuru.
 Kizazi hiki cha tatu ambacho wengi wana miaka kati 45 na 20 chini ya kiongozi demokrasi ambaye amewafanya kujitambua yakuwa wanahitaji mabadiliko na kuanza kuyatekeleza kwa njia tofauti.
Yaliyofanyika kimabadiliko chini ya kiongozi demokrasi  yameonekana na sehemu ya matokeo yake yameaanza onekana na mengi matokeo yapo njiani yanakuja.
Jambo ambalo lapaswa kukumbukwa na kizazi cha tatu cha Afrika tangu uhuru ni kwamba swala la uangalifu na umakini utazamwe kwa undani ni kwa jinsi gani kiongozi demokrasi anavyo ongoza katika kuleta mageuzi.
Na vile vile ieleweke ya kuwa  binadamu ameumbwa kuwa na tofauti, na kama hizo tofatuti zikifanyiwa kazi kwa lengo moja mazuri yatafanyika na kuleta haki na amani.
Kwani naimani yakuwa kizazi cha tatu cha bara la Afrika tangu uhuru kina lengo la kuleta maendeleo katika bara la Afrika.
Na kwa viongozi waliopo ningependa kuwakumbusha yakuwa kuongoza ni mthiani mkubwa ambao ipo siku watapata majibu yao kama walifauru au walishindwa.
Ikumbukwe kuwa  wazazi wetu, mababu na mabibi walipo kuwa wanapigania uhuru walikuwa wanajua wafanyalo, hivyo basi kizazi cha tatu cha Afrika chini ya kiongozi demokrasi umakini unatakiwa ili kufikia malengo yaliyo kusudiwa.
Yaliyo tokea mwaka 2011 chini ya kiongozi demokrasi yameleta matokeo ambayo lazima kuyatafakari kwani mtutu wa bunduki na nchi ya mkuki siyo chanzo cha haki sawa kwa wote.
Hivyo basi  mabaya yaliyo tokea mwaka 2011 yawe ni fundisho na yasirudiwe  na tuanze  mwaka 2012 kwa malengo mazuri.
Kwaheri 2011 kwa mafundisho na karibu 2012 kwa wema barani Afrika.
Mungu Ibariki Afrika.
Mungu wabari wale wote wapendao Haki na Amani duniani.
Kwaniaba ya launite.blogspot.com tunawatakia heri ya mwaka mpya 2012 na Mungu atubariki wote. Amina
Mhariri.






Marekani na na nchi za UAE zakubaliana kikataba ya kiulinzi.

  Marekani na na nchi za UAE zakubaliana kikataba ya kiulinzi.


Washington, Marekani - 31/12/2011. Serikali ya Marekani na umoja wa shirikisho wa nchi za Kiarabu United Arab Emarates zimekubaliana kuwekwa mitambo ya kiulinzi katika nchi za UAE.
Makubaliano hayo ambayo yalisainiwa 25/12/2011,  yatiwezesha Marekani kuweka mitambo yake ya ulinzi katika nchini hizo.
Msemaji wa serikali George Little alisema "mkataba huo ambao utagharimu kiasi cha dola za Kimarekani $3.48billion na itasidia kuimarisha ulinzi katika nchi hizo."
Mkataba huu utawezesha kuwekwa kwa mitambo ya kuzuia mabomu, mitambo ya mashabulizi 96, rada na mitambo mingine ya kiulinzi.
Marekani na umoja wa shirikisho wa nchi za Kiarabu zimekuwa na uhusiano wa karibu kwa muda mrefu jambo ambalo limeziwesha nchi hizi mbili kushirikiana katika maswala ya kiuchumi na kiulinzi.

 Jeshi la  Ethiopia laingia nchini Somalia.

 Beledweyne, Somalia - 31/12/201Jeshi la Ethiopia limefanikiwa kushikiria mji wa Beledweyne kutoka mikononi mwa kundi la Al-Shabab.
Kundi la Al Shabab limedai kuyaondoa majeshi yake katika eneo hilo baada ya kuzingirwa na jeshi la Ethiopia.
Kwa mujibu wa wanchi waliona  wanajeshi wa Ethiopia walisema  " tumeona magari ya kijeshi yakizunguka zunguka hapa mjini tangu jana."
Habari kutoka jeshi la Ethiopia zinasema "jeshi la Ethiopia limeamua kuisaidia Somalia baaday ya serikali hiyo ya Somalia kuomba msaada."
Wakati huo huo habari kutoka ofisi ya  waziri mkuu wa Somalia zinasema " serikali ya Somalia imetangaza ukombozi na kuhaidi kupambana na kundi la Al-Shabab kwa kila hali na tutaomba kila msaada kwa nchi majirani ili tuweze kulinada nchi yetu na kuliangamiza kundi la Al-Shabab."
Kundi la Al-Shabab limekuwa likipambana na serikali ya Somalia kwa muda mrefu jambo ambalo limeifanya serikali kushindwa kufanya shuighuli zake za kusaidia wananchi na kuijenga nchini.

Kim Jong Un ateuliwa rasmi kuwa kiongozi wa Korea ya Kaskszini.

 Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 31/12/2011. Mtoto wa aliyekuwa kiongozi wa Korea ya Kaskazini Kim Jong Il ambaye amefariki dunia siku chache zilizo pita ameteulia kushika madaraka ya baba yake.
Kim Jong Un ambaye aliongoza mazishi ya baba yake na kuhusishwa na maswala ya serikali kabla ya baba yake Kim Jong Il kufariki ameteuliwa rasmi kuwa kiongozi wa chama tawala cha wafanyakazi ana ambacho ndoyo kinacho ongoza nchini hiyo.
Kuteuliwa huko kwa Kim Jong Un atakuwa kiongozi wa jeshi na kuwa na madaraka ya juu katika nchi hiyo.
Kwa mujibu wachunguzi wa mambo ya kisiasa na maswala ya ulinzi wanadai huenda  mrithi huyo akawa mgumu  kushirikiana naye kwa kuzingatia ya kuwa amezungukwa na watu waliokuwa wanafanya kazi na baba yake.

Friday, December 30, 2011

Rais Hugo Chavez atilia wasiwasi Marekani kuhusu kuugua ugonjwa wa tarasini-kansa.


Marekani yaiuzia Saudi Arabia ndege za kijeshi.

Riadhi, Saudu Arabia - 30/12/2011. Marekani imeiuzia serikali ya Saudi Arabia ndege za kivita  zenye thamani ya dola za Kimarekani 30 billion.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani  Josh Earnest alisema "makubaliano hayo yatawezesha kupatikana kwa kazi wa watu 50,000 ."
Ndege hizo aina ya  Jet F-15s  ziliuzwa ikiwa ni moja ya makubaliano ya kibiashara kati ya Saudi Arabia na Marekani.
Andre Shapiro ambaye ni mmoja ya maofisa wa Ikulu ya Marekani alisema " kuuzwa kwa ndege hizo nchini Saudi Arabia ni kutoa onyo kwamba Marekani itafanya kila njia kuleta amani katika eneo la Mashariki ya Kati na itasaidia nchi hiyo kuwa imara..
Habari za kuuzwa kwa ndage hizo zimepatika baada ya rais Baraka Obama kuyasema hayo katika mji wa Hawaii ambapo yupo huku huko kwa mapumziko.

Rais Hugo Chavez atilia wasiwasi Marekani kuhusu kuugua ugonjwa wa tarasini-kansa.

Karakas, Venezuela - 30/12/2011. Rais wa Venezuela ametilia wasiwasi ya kuwa Marekani inashiriki katika kuwaambukiza ugonjwa wa saratani viongozi wanaonekana kupingana na mwenendo wa nchi Ya Marekani.

Rais Hugo Chavez  57 alisema " nisingependa kusababisha mfarakano lakini inawezekani Marekani ina husika katika kuwaambukiza ugonjwa wa saratani - kansa viongozi wa Amerika ya Kusini ambao tunapingana na nyendo za kibepari za Marekani." 
" Ikiwa Marekani inafanya kitendo hiki itakuwa ni cha kushangaza, na kitajulikana tu, kwani 1946-48 walifanya majaribio kwa watu wa Guatemala na matokeo yake watu walipata magonjwa ya siri, na haya yalikuja julikana miaka 50 baadaye."
"Nimeamua kusema hivyo ili kuweka mfahamo wangu wazi na nasema haya kutumia uhuru wangu niliyo nao," aliongezea rais Hugo Chavez.
Hata hivyo serikali ya Marekani imekanusha maoni hayo, msemaji wa serikali  Victor Nuland alisema "maoni kama hayo ni ya kushangaza,  haya na msingi wowote na siyo ya kuthaminika." 
Matamshi hayo ya rais Hugo Chavez yamekuja baada ya rais wa Argentina Cristina Fernandez Kirchner 58 kujulikana ya kuwa anaugonjwa wa tarasini - kansa, huku rais wa Paruguayi Fernando Lugo 60, rais wa Brazil Dilma Rousseff 64 na rais mstaaf Luiz Inacio Lula da Silva kutibiwa  ugonjwa wa tarasini - kansa.
Rais Hugo Chavez aliyaongea hayo kwa kuangalia mfululizo wa kuugua ugonjwa wa tarasni - kansa kwa viongozi hawa wanao pingana na Marekani na kudai ya kuwa rais mstaafu wa Kuba amekuwa akimwonya juu ya mwenendo wa vyakula  anavyo kula kwani vinachangi katika kuambukizwa ugonjwa wa tarasani - kansa.

Wafanyakazi wa shirika la waganga wasio na mipaka wauwawa nchini Somalia.

Mogadishu, Somalia - 30/12/2011. Mtu  mmoja amewashambulia  na kuwauwa wahudumu wanaotoa misaada wa shirika la waganga aliopo nchini  Somalia.
Mauaji hayo yalitokea kwenye ofisi za waganga hao wasiti na mipaka Medicins Sans Frontieress wahudumu.
Waziri wa mambo ya ndani wa Somalia Abdisamad Moalin Mahamud alisema " mtu huyo ambaye aliwauwa wafanyakazi wa shirika baada ya kufukuzwa kazi kutoka shirika hilo."
"Mtu huyo aliye fanya kitendo hiki ni mtu ambaye amekuwa anafanya kazi kwa muda mrefu katika mashirika ya misaada." aliongezea waziri Abdisamad.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema "watu ambao wamepoteza maisha yao ni rais wa Belgium Philippe Havet 53 na Andrias Karel Keiluhu  44 raia wa Indonesia."
Kufuatia mauaji hayo serikali imeaanza uchunguzi wake na kuimarisha usalama zaidi kwa wafanyakazi wa shirika hilo la waganga wasio na mipaka  waliopo nchini humo.

Alqaeda yatuma wapiganaji nchini Libya.

Tripol, Libya - 30/12/2011. Kiongozi wa kundi la Alqaeda ametangaza ya kuwa ametuma mmoja wa wapiganaji wa kundi hili nchini Libya ili kuunda kikundi imara.
Kwa kujibu wa habari kutoka kwa kundi hili zimasema " Ayman al Zawahiri amemtuma mpiganaki huyo ambaye hapo awali alikuwa  amekamatwa  na kuwekwa chini ya ulinzi nchini Uingereza."
Mpiganaji huyo aliingia nchini Libya mwezi wa tano baada ya kiongozi huyo wa Libya kuona ya kuwa Muammar Ghaddafi amesha poteza uwezo wa kuongoza nchi."
Hadi sasa inaaminika yakuwa mpiganaji huyo ameshawakusanya wapiganaji 200 kwa mujibu wa wachunguuzi  wa mambo ya usalama.

Thursday, December 29, 2011

Iran na Marekani zavutana kwa maneno juu ya ghuba ya Strait Hormoz

Maharamia wa Kisomali wateka meli nyingine tena.

Mogadishu, Somalia - 29/12/2011. Maharamia wa Kisomalia wameteka nyara meli ya mizigo na wafanyakazi 18 karibu na pwani ua Oman.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana kutoka ofisi za mkurugenzi wa meli ya India zinasema "meli hiyo Turkey-bound Enrico levoli  wenye wafanyakazi kutoka India 7, Itali 6, na watano kutoka Uikraine ipo njiani kuelekea pwani ya Somalia na meli hiyo ilikuwa imebeba caustic soda kutokea Iran kwenda Uturuki."
Utekwaji wa nyara huo umekuja wakati inaaminika ya kuwa maharamia hao wamekuwa nawakati mgumu wa kuteka nyara meli kutokana na ulinzi unao tolewa na majeshi ya majini ya nchi za Ulaya.
Handi kufikia sasa inaaminika kuna  idadi wa watu 200 bado wanashikiliwa na maharamia baadaya kuteka meli walizo kuwa wakifanya kazi.

Hamid Karzai aweka masharti ya kufunguliwa ofisi za Taliban nchini Katar.

Kabul, Afghanistan - 29/12/2011. Rais wa Afghanistan amekubali kufunguliwa ofisi za kundi la Taliban nchini Katar ikiwa zitakuwa kwa mazumuni ya kuleta mafanikio ya mazungumzo ya amani.
Rasi Hamid Karzai alisema "Kama Marakani inasisitiza kufunguliwa kwa  ofisi za Taliban tutakubaliana ufunguzi wa ofisi hiyo nchini Katar kwa malengo ya kuwa itatumika katika kujenga uhusiano wa kuleta amani kati yetu japo inasikitisha."
Msukumo huo wa kuleta mazungumzo ya amani na kundi la Taliban umekuwa na mvutano hasa baada ya kujulikana ya kuwa ifikapo 2014 jeshi la Marekani litaondoka rasmi nchini Agahanistan.
Hata hivyo serikali ya Afghanistan imekuwa na wakati mgumu wa kufanya mazungumzo na kundi la Taliban kutokana na historia ya kundi hilo.

 Korea ya Kaskazini kumaliza rasmi leo msiba wa kiongozi wao Kim Jong Il. 



Pyongyang, Kora ya Kaskazini - 29/12/2011. Maelfu ya wanchi wa Korea ya Kaskazini  wameshuhudia mwili wa aliyekuwa kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong Il ukipitishwa kwenda kwenye maziko.
Mwili wa Kim Jong Il 69, ulipitishwa kwenye gari aina ya remozini na kuongozwa na mwanae Kim Jong Un huku wanajeshi wakiwa wamejipanga barabarani kumwaaga kwa mara ya mwisho.
Seo Ju-rim mmoja wa wanajeshi walioudhuria mazishi yaho alisema " kwa kuangalia kuanguka kwa barafu kunanifanya nimkumbuke kiongozi wetu mpenda nchi ambaye alikuwa anaongoza kwa upendo na ameicha nchi yetu ikiwa na nguvu zaidi."
Wasemaji wa maswala ya hali ya Korea ya Kaskazini waliopo nchini Korea ya Kusini walisema " mazishi ya Kim Jong Il yanafanana na  mazishi alioyo fanyiwa baba yake Kim Il Sung mwaka 1994.
Kufuatia kifo cha Kim Jong Il, mtoto wake Kim Jong Un 28, amekabidhiwa kiti cha baba yake kuiongozi nchi hiyo.
Iran na Marekani zavutana kwa maneno juu ya ghuba ya Strait Hormoz.

Tehran, Iran 29/12/2011. Makamu wa rais wa Iran ametishia ya kuwa Iran itafunga ghuba ya Strat Hormuz ikiwa vikwazo vya kiuchumi zidi ya Irani vitaendelea.
Makamu wa rais Mohamed Reza Rahimi alisema " hakuna mafuta yatakayo ruhusiwa kupita katika eneo la Strait Hormuz, na siyo  niya yetu kufanya hivyo, lakini ipo haja ya kufanya hivyo ili tuweze kutuma ujumbe kwa wale wanao fikiria kufanya hivyo na wao waone ugumu wa vikwazo na waache kuweka vikwazo."
Hata hivyo msemaji wa jeshi la Marekani  Navy 5th  Rebecca Rebarich alisema " hatutaweza kukubali hali hiyo itokee ya kuzuiwa mafuta yasipite kwenye eneo la Strait Hormuz na tupo tayari kulinda eneo hilo ili kuhakikisha mafuta yanapita bila shida."
Malumbano hayo yamekuja wakati Iran inafanya mazoezi ya kivita karibu na eneo hilo.

Mahakama nchini Urusi  yakataa kukifungia kitabu cha Hare Krishna.

Tomsk, Urusi 29/12/2011- Mahakama nchini Urusi imekataa kukifungia kitabu cha dini ya Hare Krishna, baada ya madaya yakuwa kitabu hicho kinapotosha maadili ya watu.
Uamuzi huo wa mahakama ulipokelewa na kushukuriwa na ofisi ya waziri wamabo ya nje wa India kwa  kusema " swala kama ili nyeti limeamuliwa  kwa kufuata misingi yeti na nifuraha." 
Akiomba kufugiwa kwa kitabu hicho mwanasheria wa serikali alidai "kitabu hicho likicho tafsiliwa kwa Kirusi 'Bhagavad Gita kinapotosha na kutangaza maadili mabaya kwa wale wasio waumini na vina itikadi kali."
Hata vivyo mahakama ilkataa maombi ya mwanasheria huyo.
Kesi hiyo iliyo anza mwezi wa June mwaka huu.

India na Japan wakubaliana kubadalishana pesa.


New Delhi, India - 29/12/2011. Serikali za India na Japani zimetiliana sahii mkataba wa kibiashara na kukubaliana kukubadilishana fedha za nchi hizo.
Mkataba huo ambao utaziwezesha nchi hzo kubadilishana kiasi cha dola 15billion.
Waziri mkuu wa Japan Yoshihiko Noda alisema " mkataba huu utasidia kuimarisha uchumi wanchi hizi mbili."
Naye waziri mkuu wa India Manmohan Singh alisema " nimefurahi kutaokana na kukubaliana na waziri mkuu Noda."
Kufuatia makubaliano hayo Japan itaweza kuiazima India pesa ili iweze kulinda thamani ya  peas ya India  ijulikanayo kama Repee.

Mjumbe wa nchi za Kiarabu aliyepo Syria atoa maono ya mwanzo kuhusu hali ilivyo. 
Homs,Syria -29/12/2011. Mmoja wa wajumbe wanaoakagua hali ilivyo nchini Syria kutokana na vurugu za kisiasa na ambaye raia wa Sudan  ameongelea hali ilivyo hadi sasa nchini Syria.
Jenerali Mohamed Ahmed Mustafa al Dabi alisema "ingawa sehemu nyingine zilikuwa za kuoesha yakuwa kulikuwa na machafuko, lakini tulivyo fika maeneo mengi hayukuonekana kutisha na hali ilikuwa shwali na hatukuona vifaru vya jeshi ili tuliona gari za jeshi, na ningependa mkubuke ya kuwa hii ilikuwa siku ya kwaza  tangu tuanze uangalizi wetu."
Hata hivyo maoni ya Jenerali Dabi yalitiliwa wasiwasi na  nchi za Magharibi kwa kusema ya kuwa maoni ya ke ni ya mwazo tu."
Nazo habari kutoka ofisi za umoja wa nchi za Kiarabu zilisema, "maoni ya Jenerali Mohamed Mustafa Dabi yanathaminika kwani ni muhimu kwa kuzingatia yeye nimwanajeshi na mwana diplomasia vilevile."
Syria imetembelewa na wakaguzi 50 wa nchi za jumuiya ya Kiarabu, ili kutathmini hali halisi ya matatizo ya kisiasa yanayo endelea nchini humo.

Monday, December 26, 2011

Miaka 20 yatimia tangu kuvunjika kwa USSR.

Wapiganaji walio saidia kumng'oa Gaddafi wadai wapo tayari kwenda Syria kwa mapigano.

Tripol, Libya - 26/12/2011. Kiongozi wa kundi lililoshiriki kumtoa madarakani Muammar Gaddafi amewahimiza wananchi wa Syria kufanya mapinduzi.
Mohamed Alhuraizi alisema " tupo tiyari kuwasaidia ndugu zetu wa Syria, vijana wapo tayari  kupigana kuikomboa Syria, kwani kwa uwezo wa Mola tutashinda kwa kufuata nia ya Che Guevara ya kupigania haki  amani na uhuru tnataka kuwasaidia ndugu zetu na nafikiri ni wajibu wetu."

Pakistani na China kushirikiana kiukaribu zaidi.


Isamabad, Pakistan - 26/12/2011.  Serikali ya Pakistan na China zimehaidi kushirikaiana kikamilifu ilikudumisha uhusiano uliopo.
Hayo yaliongelewa na rasi wa Pakistani  Asif Ali Zardari na mgeni wake mwakilishi wa serikali ya China kamishna Dai Bingguo.
Kukutana huko kumekuja katika kuadhimisha miaka 60 ya ushirikiano wa China na Pakistani.
Beijing na Islamabad zilitiliana sahii mkataba wa kibiashara wa $1.6 billion ambapo nchini hizi mbili zitaweza kubadilishana kibisahara na kupunguza kutegemea mzunguko wa pesa.
Uhusiano wa China na Pakistan umekuwa wa karibu saana na hata kufikia kufanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi katika mji wa Jhelum uliopo Pakistan.

Brazil yakuwa kiuchumi na kuipita Uingereza.


Rio de Janairo Brazil - 26/12/201. Kitengo kinacho shughulikia maswala ya uchunguzi wa uchumi duniani Centre Economics and Business Research CEBR kimetangaza matokeo ya maendeleo ya kiuchumi duniani.
CEBR imeripoti " Brazil imekuwa nchi ya sita kiuchumi na kuipita nchi ya Uingereza kutonaka kukua uchumi kwa 7.5% sambamba na mipango mbinu ya uzalishaji wa bidhaa zinazo tumika na kuuza vitu vyake hasa nchini China na kuagizia vitu vichache kutoka nje ya nchi (Brazil)."
Kitengo hicho kimetabiri ya kuwa huenda Urusi ikakuwa kiuchumi ifikapo mwaka 2020 kwani kwa sasa  ni ya tisa na nchi za Ulaya huenda zikadondoka kiuchumi ifikapo 2020.

Syria yahaidi kushirikiana na wajumbe wa jumuiaya ya nchi za Kiarabu waliopo nchini humo.


Damascus, Syria - 26/12/2012. Wajumbe wa umoja wa nchi za Kiarabu wamehakikishiwa kupata ushirikiano wa kila aina kutaka serikali ya Syria.
Habari kutoka serikali ya Syria zinasema " serikali itashirikiana kikamilifu katika kuahakikisha ya kuwa mipango yote iliyo pendekezwa na umoja huo zinafuatwa."
Mkurugenzi wa maswala ya unangalizi wa Mashariki ya Kati Haisham Jaber alisema "habari zinazo tolewa na vyombo vya habari zinaelezea vifo vya watu , lakini havielezei ya kuwa pia makundi ya upinzani ya wanajeshi ambao wanapigana na serikali, na nibora kutenganisha kati wa wanajeshi wapinzani na raia na hii ndiyo inaweza kuwa chanzo cha ugumu wa kazi kwa wajumbe wa jumuiya  ya Kiarabu waliopo nchini Syria."
Wajumbe hao ambao waliwasili nchini Syria, wamekuwa na wakati ngumu, kutokana na hali ya mvutano wa kisiasa na misimamo na malengo ya vyama vya upinzani vinavyo pinga serikali ya Syria iliyopo chini ya rais Bashar al Assad.

Miaka 20 yatimia tangu kuvunjika kwa USSR.


Moscow, Urusi - 26/12/2011.  Wanchi waliokuwa katika shirikisho la nchi za  United Soviet Socialist Repiblic USSR wanaadhimisha miaka 20 tangu kuvunjika kwa shirikisho hilo.
Shirikisho hilo ambalo liliundwa 1922 lilivunjika  chini ya uongozi rais Mikhail Gorbachev na nchi zote ambazo zilikuwa katika shirika hilo kuwa nchi huru na kuanza kujijenga ka nchi.
Hata hivyo waziri mkuu wa sasa wa Urusi Vladmir Putin alisema "kuvunjika kwa shirikisho hilo ni moja ya makosa ya kihistoria ya karne ishirini na ishirini na moja." Waziri mkuu Putini aliyasema haya wakati alipo kuwa rais wa Urusi.
Hata hivyo wachunguzi wa mambo ya kisiasa wanadai kuvunjika kwa USSR, hakukuwa kama mapinduzi, bali ilikuwa ni utengano wa amani ambao matokeo yake yanaonekana mpaka sasa.



Papa Benedikt aongoza misa ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo.

Papa Benedikt VXI aongoza misa ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo. 




Vatican, Vatican City - 26/12/2011. Papa Benedikt wa XVI ameongoza misa ya Kristmas katika kanisa la Mtakatifu Peter Basilika wakati wa  kusherekea siku ya kumbukumbu ya  kuzaliwa kwa Jesu Kristo mjini .
Papa Benedikt alisema " waumini lazima tufanye mabadilko makubwa ya kiimani na kujua umuhimu wa siku kuu ya Krismas, kwan siku hizi sikukuu ya Krismas imekuwa siku ya biashara na kusahahu ya kuwa sisi binadamu tunatakiwa tukumbuke ya kuwa ni siku ambayo tuliletewa mkombozi ili aje kutukomboa kutonaka na dhambi zetu, na inapaswa kutafakari ukarimu huo."
"Tumwombe Mungu atuzidishie mapenzi na tupendane kusaidiana, kwani machafuko ugomvi na mvurugo wa amani katika jamii vina sababishwa na kutokuwa karibu na Mungu na wale wote waletao hayo wajue ya kuwa jesu Kristo atawashinda tu. Aliongeza Papa Benedikt.
Misa hiyo iliyo ongozwa na Papa Benedikt wa VXI ilikuwa moja ya misa na sara zilizo fanyika duniani kote ili kusherekea kuzaliwa Jesu Kristo. 

Urusi ya mteua mkuu mpya wa maswala ya sayansi ulinzi jeshi
na upelelezi.


Moscow, Urusi - 26/12/2011. Serikali ya Urusi imemteua mkuu mpya wa maswala ya upelelezi wa kiulinzi jeshi  ili kuchua nafasi iliyo achwa wazi na aliyekuwa kiongozi wa sekta hiyo.
Habari kutoka ofisi ya wizara ya ulinzi zilisema "Maja Jenerali Igor Sergu 64 alichaguliwa  kuchukua nafasi hiyo baada ya Kanali Generali Alexander Shlyakhtuvo kujiudhuru kutokana na sababu kibafsi ikiwa ni moja ya maandalizi ya kulitaya kazi kutokana na umri."
Meja Generali Igor Sergun atashughulikia  maswala ya ulinzi wa kisayansi jeshi na kusimamia mambo yote yanayo husu sekta ya  ukachelo wa kiulinzi jeshi.

Waziri wa mambo ya nje wa Izrael adai rais wa Wapelestina siyo mtu wa kuleta amani.


Jerusalem, Izrael - 26/12/2011. Waziri wa mambo ya nje wa Izrael awahutubia watu waliohudhuria mkutano mjini Jerusalem na kudai  ya kuwa mapatano na Wapalestina ni kitendawili.
Waziri Avigdor Liebrman alisema " rais wa Wapalestina siyo mtu wa kukaanaye ukaongea maswala ya amani na hihi imetokea mara kwa mara na yoyote anayesema ya kuwa matatizo kati ya Waizrael na Wapalestina yatakwisha hivi karibuni anawaongoza wengine vibaya na visivyo kwani hali hii inaonekana itachukua miaka na lazima tujiandae ili kuweza kutafuta ufumbuzi wake kiuchumi, kijamii, kiushirikianao na bila kusahahu swala la ulinzi na usalama."
 "Na haiwezekani kuanza kuweka msingi wa nyumba wakati bado tetemeko la ardhi lina tikisa ardhi?"Aliukiza waziri Lieberman.
Jambo muhimu kati Waizrael na Wapalestina ni kutafuta njia ya kutatua ugomvi uliopo na siyo kusimamisha ugomvi." aliongezea Lierbman. 
Mgogoro wa Wapalestina na Waizrael na Wapalestina  imekuwa kitendawili kwa jumuia ya kimataifa kwa miaka mingi na hadi sasa bado utatafutiwa ufumbuzi.

Kiongozi wa kundi la JEM nchini Sudani auwawa na jeshi la Sudani.



Kordofan, Sudan - 26/12/2011. Jeshi la Sudani limetangaza ya kuwa limefanikiwa kumuua aliyekuwa kiongozi wa kundi la upianzani la  Justice Equality Movement JEM na baadhi ya wapiganaji wake 30.
Kwa mujibu wa habari kutoka jeshi la Sudani zinasema " mashambulizi hayo yalifanyika mapema alfajiri wakati ndege za kijeshi zilipo fanya mashambulizi kwenye aneo ambalo alikuwepo Khalil Ibrahim na badhi wa piganaji wake."
 Waziri wa habari wa Sudani allisema "tungependa kundi hilo lijiunge kwenye meza ya makubaliano ya amani kwani milango bado ipo wazi na itakuwa jambo la busara kama kundi hilo litaamua hivyo."
Mashambulizi hayo yamekuja baada ya kundi la JEM kudai yakuwa lilikuwa linakaribia kuingia jijini Khartoum tayari kujianda kuuangusha utawala wa  rais Omar al Bashir wa Sudan.
Kundi la JEM limekuwa likilaumiwa kwa kufanya au kuhusika na mashambulizi mara kwa mara nchini Sudan

Mchezajiwa Kriket nchini Pakistan aanza kampeni za uchaguzi.


Karachi, Pakistani - 26/12/2011. Mamia ya waru walikusanyika kusikia hotuba ya aliyekuwa mchezaji maarufu wa mchezo wa kriketi na ambaye kwa sasa ni mwanasiasa maarufu nchini Pakistani.
Imran Khan, ambaye amefanya mkutano huo zikiwa zimebakia siku chache za kuanza uchaguzi wa wabunge alisema "Pakistani inatakiwa kufuata maadili ya Uislaam, ambapo kila mwanachi apate haki sawa kielimu, afyaa na huduma nyingine zote za jamii na bila kusahau haki itendeke kwenye vyomb vya sheria."
"Nafahamu yote hayo yapo, lakini kwa sasa hayo yote ayatekelezwi ipoasavyo, na kama nchi za Ulaya UK zingekubali kutekeleza Uislaam zingekuwa nchi bora kuliko sisi. Aliongezea Khan.
Katika hotuba yake hiyo, Imran Khan  alihaidi kupambana na rushwa na kuongeza ya kuwa matatizo yaliyopo nchini Pakistani yanaweza tatuliwa ikiwa



Saturday, December 24, 2011

Uhuusiano wa Uturuki na Ufaransa wazidi kuwa na mvutano.

 
Hali ya kisiasa nchini Kongo JK yazidi kuleta utata.


Kinshasa, Kongo JK - 24/12/2011. Maafisa usalama nchini Kongo JK wamepambana na waadau na wale wanao muunga mkono kiongozi wa upinzani wa nchini hiyo Etienne Tshisekedi.
Mapambano hayo yametokea wakati wa maandalizi ya kumwapisha kiongozi huyo, kwa kudai Etienne Tshisekedi ndiye mshindi rasmi na anatakiwa ahapishwe awe rais.
Hata hivyo kwa mujubu wa habari zilizo patikana zinasema "Etienne Tshisekedi aliapishwa katika makazi yake."
Matokeo ya uchaguzi nchini Kongo JK yameteta mvutano kufuatia ripoti za jumuiya za kimataifa ya kuwa uchaguzi huo ulikuwa na matatizo.
Katika uchaguzi huo rais wa sasa wa Joseph Kabila alitamkwa kama mshindi kwa kupata kura 49% za kura na  mpinzani wake Etienne Tshesekedi kupata 32%.
Joseph Kabila aliapishwa hivi karibuni kuwa rais wa Kongo JK na ataongoza nchi hiyo kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Uhuusiano wa Uturuki na Ufaransa wazidi kuwa na mvutano.

 Ankara, Uturuki - 24/12/2011. Serikali ya Uturuki imeishambulia kwa maneno serikali ya Ufaransa na kudai pia kuwa Ufaransa kuhusika na mauaji ya kimbari nchini Algeria.
Uamuzi huu wa serikali ya Uturuki kufanya hivyo, umekuja baada ya bunge la Ufaransa kupiga kura kutambua ya kuwa mauaji ya Armenia yaliyo fanyika nchini Uturuki ni ya kimbari.
Waziri mkuu wa Uturuki Recep yayyip Erdogan alisema "mauaji yaliyo fanywa na Ufaransa  nchini Algeria kuwanzia mwaka 1945 ni ya kimbari na yatambulike hivyo pia."
Ikiwa rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy ahajui kuhusu mauaji hayo ya kimbari, ni bora amuulize
baba yake Paul Sarkozy ambaye alikuwa mwanajeshi aliyepigana nchini Algeria 1940."Aliongezea waziri mkuu Reccep Erdogan.
Mvutano kati ya Ankara na Paris ulizidi kuwa mbaya baada ya kura hiyo na serikali ya Ututuki kutangaza kufunga mahusiano na Ufaransa.

Kuba kuachia wafungwa wa kisiasa.
 
  
Havana , Kuba - 24/12/2011. Rais wa Kuba amatangaza msamaha kwa wafungwa wapatao 3000 wakiwemo wafungwa  86 kutoka nchi za kigeni  25.
Rais Raul Castro alitangaza hayo wakati alipo kuwa akihutubia baraza la sheria la nchi hiyo na hii itakuwa mara ya kwanza kwa rais Raul kutoa msamaha tangu kuchukua madaraka kutoka kwa kaka yake Fidel Castro.
Kwa mujibu wa wachunguzi wa mabo ya kigeni ya Kuba walisema " uamuzi wa serikali ya Kuba kutoa msamaha kwa wafungwa hao ni katika mpango wa kujiaanda na ziara ya Papa Benedikt XVI ambayo anatarajiwa kuifanya hapo mwakana."
Uamuzi huu wa kuachia wafungwa wa kisiasa na wengine nchini Kuba kumekuja wakati nchi nyingi za Ulaya ya Magharibi na Amerika bado zinawasiwasi na serikali ya Kuba kutokana na msimamo wake wa kisiasa.

Maafisa usalama wa Nigeria wapambana na kundi la Boko Haram.
 Abuja, Nigeria - 24/12/2011. Watu wapatao 61 wamepoteza maisha na makazi kuharibiwa kutokana na mashambulizi yanayo endelea kati ya jeshi serikali na kundi la Boko Harama.
Mashambulizi hayo ambayo yameaanza baada ya milipuko ya mabomu katika jimbo la Borno na Yobe na kuleta huharibifu mkubwa.
Kwa mujibu wa habari kutoka heneo hilo simasema " mashambulizi hayo yamesababisha vifo vya  wakuu wawili wa polisi wakati wapambano hayo."
Kundi la Boko Haram limekuwa likipambana na serikali ya Nigeria kutokana nambishano wa tofauti wa siasa.
Na kutokana na vurugu za kisiasa nchini Nigeria watu wapatao 450 wameshapoteza maisha yao.




Thursday, December 22, 2011

Jiji la Dar-es- Salaam nchini Tanzania la kumbwa na mafuriko.


Jiji la Dar-es- Salaam nchini Tanzania la kumbwa na mafuriko. 

Dar-es- Saalam, Tanzania - 22/12/2011.  Jiji la Dar -es- Salaam nchini Tanzania limekubwa na mafuriko makubwa baada ya mvua kubwa kunyesha na kusababisha maafa makubwa ya kijamiii na kimazingiia 
Kwa mujibu wa habari kutoka  serikalini zilisema "watu wapatao kumi na mbili wamefariki dunia na watu walio wengi wamepoteza makazi yao."
 Mkuu wa polisi wa jiji la Dar -es- Salaam Suleiman Kova alisema " maeneo yaliyo kumbwa na mafuriko ni Tabata, Buguruni, Kinondoni Mkwajuni, Jangwani, Kigogo na maeneo ya Mikocheni.
pia mafuriko hayo yalibomoa barabara na kuvunja madaraja."
Kitengo kinacho shughulikia hali ya hewa kimetoa maelezo yakuwa mvua hizi hazijawahi kunyesha kiasi hiki tangu 1956 ambapo zilifikia kina cha 216 cha ujazo wa maji ardhini na pia kusababishwa na upepo unao enendelea.

Sweden yata waandishi  wa habari kutoka Sweden  waliopo Ethiopia waachiwe




Adis Abeba, Ethiopia - 22/12/2011. Mahakama jijini Adis Ababe imewakuta na hatia waandishi wa habari kutoka Sweeden na kosa la uhaini kwa kuwakamata katika kundi la wapiganaji wanao pinga serikali la Ogaden.
Johan Persso na Martin Schibbye walikamatwa mwezi wa Julai wakati jeshi la serikali ya Ethiopia lilipo kuwa likipambana ba kundi la Ogaden na baadaye kushitakiwa kwa kukutwa  makosa ya kuingia nchini Ethiopia kiyume na sheria na kutoa msaada wa kundi la kigaidi.
Waaandishi wa habari hao wanatarajiwa kuhukumiwa vihi karibuni kabla mwisho wa mwaka na wanaweza kukaa jela miaka 18.
Hata hivyo serikali ya Sweden imeitaka serikali ya Ethiopia kuawachia waandishi wa habari hao, kwani walikuwa wanafanya kazi zao bila makosa.

Rais wa Urusi atangaza mpango mpya wa mfumo wa siasa nchini Urussi.



Moscow, Urussi - 22/12/2011. Rais wa Urussi ametangaza na kupendekeza  mabadiliko ya mfumo wa kisiasa nchi Urussi.
Rais Dmitry Medvedv alisema " serikali ya Urussi haitakubali machafuko yanayo letwa na watu wenye itikadi kali kwa kutumia mlango wa neno demokrasia na hatuta ruhusu watu wanamna hiyo kuwa na nafasi."
"Nchi inataka mabadiliko ya kisiasa yenye demokrasi bora na siyo vurugu, hii inahitajika ili kufungua ukurasa mpya ambapo kila raia wa Urussi atakuwa na haki sawa na kila chama  kitapata nafasi katika demokrasi itakayo wafaa raia wa Urussi."Alimalizia rais Medvedev.
Hotuba hiyo ya rais Dimitry Medvedev, imekuja siku chache baada ya uchaguzi wa wabunge uliyo fanyika nchini humo na kuleta wasiwasi mkubwa kufuatia matokeo ya uchaguzi huo na watu kuandamana.


Jiji la Baghda nchini Irak  lashutushwa  milipuko ya mabomu iliyo leta maafa.


Baghdad, Irak - 22/12/2011. Jiji la Baghdad limekumbwa na milipuko ya mabomu ambayo yamesababisha  maafa makubwa na kuleta hali ya wasiwasi kwa wakazi wa jiji hilo.
Kwa mujibu wa mashahidi walisema " kunametokea milipuko  zaidi ya kumi na mbili tofauti katika jiji hilo."
Habari kutoka wizara ya ndani ya Irak zinasema " watu wapatao 63 wamefariki dunia na wengine 176 kujeruhiwa vibaya kutoka na milipuko hiyo iliyo tokea sehemu tofauti ndini ya jiji la Baghdad."
Milipuko hiyo imetokea siku chache baada ya jeshi la Marekani kuaanza kuondoka nchini Irak na wakati huo huo kukiwa na mvutano wa siasa katia ya waziri mkuu Nour al Marik Shia na makamu wa rais Tarik al Hashim Sunni  ambaye yupo  ukimbizini katika eneo linalo ongozwa na Kurdish.


Monday, December 19, 2011

Kiongozi wa Korea ya Kaskazini afariki dunia.

Kiongozi wa Korea ya Kaskazini afariki dunia.


Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 19/12/2011.  Kiongozi wa Korea ya Kaskazini amefariki dunia siku ya Jumamosi wakati akiwa njiani kutoka katika jiji la Pyongyang.
Kim Jong-Il  69 alifariki kwa kugonjwa wa moyo kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya nchi hiyo.
Mtangazaji wa luninga ya taifa ya Korea ya Kaskazini alisema " tumepoteza kiongozi mpendwa wa chama na nchi  na ni uchungu kwa taifa ziama."
Kwa mujibu wa habari kutoka Korea ya Kaskazini zinasema, mtoto wake wa kiume Kim Jong-Un 28 ndiye aliyechaguliwa kushika nafasi ya baba yake.
Kim Jong Il alichukua uongozi wa Korea ya Kaskazini  mwaka 1994 baada ya baba yake Kim Il Sung
kufariki dunina.
Kufuatia  kifo cha kiongozi huyo, nchi za Magharibi zimetoa matazamo tofauti na kutaka uongozi mpya kujitaidi kushirikiana na jumuiya ya kimataifa.
Syria yakubali kusaini mkataba wa makubaliano na jumuiya Kiarabu.



Kairo, Misri - 19/12/2011. Serikali ya Syria imekubali kutia saini mkataba wa makubaliano jumuiya ya nchi za Kiarabu ambao utaruhusu waangalizi wa jumuia hiyo kuingia nchi Syria ili kuangalia hali halisi ya kisiasa nchini humo.
Makubaliano hayo ambayo yalitiwa saini na waziri msaidizi wa mambo ya nje wa  Faisal al Maqgad na latubu msaidizi wa jumuiya ya nchi za Kiarabu Ahmed Ben Helli jijini Kairo nchi Misri.
Waziri wa mabo ya nje wa Syiria Walid Muallem alisema " Syria imesaini makubaliano hay baada ya kuona yana manufaa kwa nchi na hayaingilii mambo ya ndani ya nchi."
Makataba wa makubaliano hayo umekuja siku chache kabla ya jumuiya nchi za Kiarabu kuamua kupeleka swaka la Syria katika balaza la usakama la Umoja wa Mataifa.

Friday, December 16, 2011

Luis Moreno Ocampo atatizwa na vifo vya Muammar Gaddafi na mwanae

Rais wa zamani wa Ufaransa Jacques Chirac ahukumiwa miaka miwili.

Paris, Ufaransa - 16/12/2011. Mahakama nchini Ufaransa imemuhukumu aliyekuwa raia wa Ufaransa kifungo cha miaka miwili baada ya kukutwa na kosa la kuhusika katika njama za rushwa na kuwepo na matumizi yasiyo elewaka.
Jacques Chirac amehukumiwa kifungo cha nje cha miaka miwili, na kuwa kiongozi wa pili kufuatia kesi ya Philippe Petain iliyo tokea wakati wa vita pili vya dunia.
Hukumu hiyo ilitolewa bila Jacques Chirac kuwepo mahakamani kutokana na hali yake ya kifya kutoruhusu kuwepo mahakamani.
Luis Moreno Ocampo atatitwa na vifo vya Gaddafi na mwanae.
Ze Hague, Uhollanzi - 16/12/2011. Mwanasheria mkuu wa mahakama ya inayo shughulika na kesi za jinai na kutetea haki za binadamu ya Uhollanzi amedai ya kuwa mauaji ya rais wa Libya Muammar Gaddafi na mwanaye, yalikiuka haki za binadamu na kuna kesi ya kujibu kwa wale walio husika na mauaji hayo.
Luis Moreno Ocampo alisema " kutokana na jinsi walivyo uwawa Gaddafi an mwanaye, kuna leta
wasiwasi ya kuwa mauaji hayo yalifanyika kwa kuvunja sheria na kuna haja ya kuchunguzwa."
Nimetuma barua kwa serikali ya mpito ya Libya na kutaka waaanze uchunguzi na kama wakishindwa kufanya hivyo basi itabidi tufanye uchunguzi wetu wenyewe." aliongezea Ocampo.
Tamko hilo la Ocampo limefuatia ombi la mtoto wa Muammar Gaddafi Aisha Gaddafi, kutaka kifo cha baba yake kichunguzwe.
Urussi yajiunga na shirika la bishara la Kimataifa.
Geneve, Uswisi - 16/12/2011. Shirika la biashara la Kimataifa World Trade Organization - WTO ilimepitisha na kukubali kujiunga uanachama kwa nchi ya Urussi kwenye shirika hilo.
Olesugun Aganga waziri wa biashara wa Nigeria na ambaye nimwenyekiti wa kikao cha nane cha shirika hilo aliwatangazia wajumbe kwenye kikao hicho ya kuwa Urussi kuanzia sasa itakuwa mwanachama wa shirika hilo.
Kufuatia kujiunga huko kwa Urussi kwa shirika hilo, " Urussi itakuwa inanunu vitu kutoka nchi za jumuiya ya Ulaya kwa bei nafuu na kuweza kuuza mafuta na gasi bila matatizo yoyote kwa nchi hizo."
Waziri mkuu wa Urussi, Vladimir Putin alisema " kufikiwa makubaliano hayo ni matokeo ya mazungumzo yaliyo chukua muda na washiriki wenzetu."
Urussi imekuwa mwana chama wa WTO kufuatia mazungumzo yaliyo chukua miaka 18.

Wednesday, December 14, 2011

Rais Baraka Obama awakaribisha wanajeshi kutoka Irak.

Palestina yakubaliwa kujiunga na UNESCO
Paris, Ufaransa - 14/12/2011. Serikali ya Wapalestina imeongezwa kuwa mwanachama wa UNESCO -UN Education, Scientific and Cultural Organasation, katika sherehe iliyo fanyika nchini Ufaransa baada ya bendera ya Wapalestina kupandishwa juu sambamba na bendera ta umoja wa mataifa kama ishara ya kujiunga na shirika hilo.
Rais wa Wapalestina Mahmoud Abbas alisema " hii ni historia na tunatumaini yakuwa Wapalestina watakuwa wanachama wa mashirika mengi muda si mrefu."
Kukubaliwa huko kwa Wapalestina kujiunga na UNESCO kumekuja huku viongozi wa nchi hiyo wakiwa katika kampeni ya kutaka Wapalestina watambulike rasmi katika baraza la umoja wa mataifa kama taifa huru.
Pakistani yazidi kuiwekea ngumu Marekani kusafirisha vifaa nchini Afghanistan.
Islamabad, Pakistan - 14/12/2011. Serikali ya Pakistan imetangaza ya kuwa vikwazo na vizuizi zidi ya vifa vya kijeshi na vya ujenzi vitaendelea hadi hapo hali ya mapatano itakapo fikiwa.
Waziri mkuu wa Pakistani Yousuf Gilani alisema "kwa sasa kuna kuto kuaminiana kati ya Marekani na Pakistani jambo ambalo linaleta wasiwasi kwa pande zote na ikiwa hali itazidi kuwambaya basi itabidi tufunge mawasiliano ya anga."
Uhusiano wa Marekani na Pakistani uliingia dosari baada ya askari 24 wa Pakistani kuuwawa kutokana na shambulizi yaliyo fanywa na jeshi la Marekani.
Rais Baraka Obama awakaribisha wanajeshi kutoka Irak.
Karolina
, Marekani - 14/12/2011. Rais wa Marekani amewakaribisha nyumbani wanajeshi waliokuwa wamebakia nchi Irak, ili kumalizia ujenzi wa kiulinzi nchini humo.
Baraka OBama alisema "ningependa kusema ya kuwa tumefikia mwisho wa vita vya Irak na karibuni nyumbani na Irak sasa ipo chini ya Wairak na hongereni kwa kazi nzuri kwa kuiweka Irak katika hali ya kuweza kujijenga."
Naningependa kuwahakikishia ya kuwa ifikapo mwisho wa mwezi huu Desemba wanajeshi wote wa Marekani watakuwa nyumbani." Aliongezea rasi Obama.
Kuwasili huko kwa wanajeshi hao kunafikia tamati baada ya vita vya kuingoa serikali ya aliye kuwa rais wa Irak Sadaam Hussein mwaka 2003.

Saturday, December 10, 2011

Papa Benedikt kufanya ziara nchini Kuba.

Zawadi ya Nobel ya amani ya mwaka 2011 yatolewa rasmi kwa watunukiwa.
Oslo, Norway - 10/12/201. Rais wa Liberia na wenzake wawili ambao walichaguliwa kutunukiwa zawadi ya amani ya Nobel wamekabidhiwa rasmi katika jiji la Oslo nchini Norway.
Ellen Johnson Sirrleaf Leymah Gbowee na Tawakul Karman walitunukiwa rasmi zawadi mbele ya wageni rasmi na wageni waalikwa ili kuja kushuhudia kutolewa kwa zawadi hiyo.
Mwenyekiti wa kamati inayo simamia utoaji wa zawadi hiyo Thorbjoern Jaglang alisema " wana mama hawa watatu wameonyesha mfano mzuri kwa jamii ya kuwa wakina mama wakipewa nafasi wanaweza kufanikisha kuleta amani duniani."
Wakina mama hao waliteuliwa mapema mwaka huu kutokana na mchango wao katika harakati za kupigania amani na utulivu kwenye nchi zao.
Kroatia yakubaliwa kujiunga na nchi wanachama wa jumuiya ya Ulaya.
Zagreb, Kroatia - 10/12/2011. Serikali ya Kroatia imetia sahii mkataba wa kuwa nchi ya 28 kujiunga na jumuiya ya nchi za Ulaya.
Sahii hiyo iliwekwa 09/12/2011, masaa machache baada kumalizika mkutano wa viongozi wa nchi hiyo walipo kutana kujadili mbinu za kudhibiti matumizi ya nchi wanachama wa jumuiya hiyo ya Ulaya.
Rais wa jumuia ya Ulaya Herman Van Rompuy alisema "Kroatia imeonyesha unadni wake na kutaka nchi hiyo iwe mwanachama wa kweli wa nchi za jumuiya ya Ulaya na tunaikaribisha."
Rais wa Kroatia Ivo Josipovic alisema " leo Kroatia imeingia ndani ya jumuiya ya Ulaya ili cha muhimu ni kwamba jumuiya ya Ulaya imefunguliwa milango na Wakroatia."
Uanachama huo wa Kroatia utaanza kamili ifikapo mwakani meizi ya kati ya mwaka.
Papa Benedikt XVI kufanya ziara nchini Kuba.
Vatican, Vatican City - 10/12/2011. Papa Benedikt XVI atatembela nchi ya Kuba hapo mwani kwa mujibu wa ofisi inayo shughulikia safari za Papa.
Kwa mujibu wa habari hizo zinasema "ziara ya Papa nchi Kuba itambatana na kuazimishwa kwa miaka 400 ya Mtakatifu Virgin wa Caridad del Cobre na itazidi kuongeza na kukuza imani ya Wakuba ambo wengi ni watu wa imani."
Hata hivyo tarehe ya Papa kuanza ziara nchini Kuba itatangazwa siku chache kabla ya kuanza ziara hiyo.
Ziara hiyo ya Papa Benedikt XVI inafuatia ziara ya marehemu Papa Benedikt aliyo ifanya nchini Kuba mwaka 1998.
Hali si shwali nchi JKD na Joseph Kabila atangazwa kushinda uchaguzi wa urais.
Kinshasa
- JKD Kongo- 10/12/2011. Vurugu zimedizi kuongezeka nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya rais wa sasa Joseph Kabila kutangazwa kama mshindi wa uchaguzi huo.
Akiongea kupitia TV na kuelezea matokeo ya uchaguzi huo, waziri wa mawasiliano Ngoy Mulunda alisema, " mpaka sasa rais Joseph Kabila amesha pata 48% ya matokeo ya uchaguzi, ila bado tunasubiri uamuzi wa mwisho wa mahakama kuu kutoa uamuzi wake."
Mgombe mpinzani wa kiti hicho cha urais, Etienne Tsheked alisema "sisi wapinzani hatuta kubaliana na matokeo yoyote kwani shughuli zote za upigaji kura haukuwa wa kihalari."
Uchaguzi wa JKD Kongo ulifanyika 28-28/12/2011 ili kumchagua rais atakaye ongoza nchi hiyo kwa kipindi kingine cha miaka mitano.