Monday, September 28, 2009

Miaka ya 1980s,dunia ingepatwa na mstuko mkubwa.

Miaka ya 1980s,dunia ingepatwa na mstuko mkubwa.

Havana, Kuba 28/09/09.Miaka ya 1980s, ambapo Amerika na Kuba, zilikuwa katika hali ya hatari karibu kupigana kivita,hakukuzaniwa ya kuwa hali hii,ilifikia hadi rais, wazamani wa Kuba ,Fidel Catro kuimba Urussi, kuisaidia Cuba ,kuishambulia Amerika kwa bomu la nyuklia, pindipo vita vitaanza.
Lakini kutokana na ushauri wa wataalamu wa Urussi, walimweleza ya kuwa ikiwa bomu hilo litatumika, basi hata wanachi wa Kuba wanaweza kiathirika pia.
Miaka ya 1980s, ilikuwa maka ya hatari hasa kati ya Amerika na Kuba pamoja na Urussi,na kupelekea aliyekuwa rais wa Amerika, Ronald Regan, kuizinisha mpango wa kujihami kisiraha,kwa kujihami na Urussi.
Hata hivyo,hali haikufikiwa ya kutokea vita, japo kuwa rais, Ronald Regan, alishambulia Urussi kwa maneno makali na kuiita Muungano wa nchi za Urussi ni wa kishetan.
Picha hapo juu, ni ya rais , mataafu wa Kuba ,Fidel Castro, ambaye alikuwa adui wa viongoziwa Amerika kwa muda mrefu kwa msimamo wake.
Picha ya pili, anaonekana, hayati, rais wa Amerika, Ronald Regan, ambaye wakati wa utawala wake Amerika na Kuba zilikuwa almanusla kupigana.
Tushirikiane kuepuka kutegemea nchi za Ulaya na Amerika,"marais wawakumbusha marais/viongozi wenzao".
Margarita, Venezuela - 28/09/09. Rais wa Venezuela, Hugo Chavez ,amewataka viongozi wa Afrika na Amerika ya Kusini, kushirikiana kikamilifu ili kuepuka kuzitegemea nchi za Ulaya na Amerika.
Akiongea katika mkutano huo, rais Cahvez, alisema kushirikiana kwa nchi za dunia ya tatu, kutasaidia nchi hizo kiuchumi na kuinua maisha ya watu wake.
Rais, Chavez,alisisitiza ya kuwa huu ndiyo mwazo wa kujikomboa kwa nchi za Afrika kwa kushirikiana na nchi za Amerika ya Kusini,kwani nchi hizi zina kila kitu, na kama zikishirikiana vizuri, basi karne ya 21, itakuwa ni ya kuinua uchumi wa nchi hizi.
Naye rais, wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva, alisema hakuna matatizo yasiyo kuwa na majibu, hivyo basi ni muhimu kwa viongozi kukakana kutafakari na jibu litapatikana, ili kukabili hali halisi ya Afrika na Amerika ya Kusini
Kwa kuunga mkono, hoja hizo, rais wa Libya , Muammar Gaddafi, alisema inabidi kuundwa NATO ya Kusini, kwani nchi zenye nguvu, zimekuwa zikitumia nguvu zao vibaya,kwa kupoteza nafasi ya kutusaidia ,bali kututumia kama wanyama na kuaribu ardhi yetu.
Hivyo umefikia wakati wa kupigania kujikomboa kwa kila hali.
Picha hapo juu, anaonekana, rais wa Venezuela, Hugo Chavez,akiongea mbele ya viongozi/marais wa Afrika na Amerika ya Kusini, wakati wakikao cha wakuu wanchi hizo.
Picha ya pili ni ya rais wa, Brazil, Lula Da Silva,ambaye alisisitiza utafakari wa kutatua matatizo.
Picha ya tatu, ni rais wa Libya, Muammar Gaddafi,ambaye alitaka nchi za Afrika na Amerika ya Kusini, kuanza kujikomboa kwa kila hali.
Hali ya usalama na amani wa Guinea mashakani
Konakry,Guinea - 28/09/09. Watu kadhaa wameuwawa na wengine kujeruhiwa baada ya polisi kupamabana na waandamanaji wanaopinga uamuzi wa mkuu wa jeshi, kugombea kiti cha urais
Mkuu huyo wa majeshi,Moussa Dadis Camara, ambaye amechukua madaraka kwa mapinduzi , baada ya kifo cha rais wa nchi hiyo Lansana Contee, ambaye alitawala tangu mwaka 1984.
Kwa mujibu wa mashaidi waliokuwepo kwenye maandamano hayo, ambayo yalianzia karibu na kiwanja cha mpira cha Konakry,walisema polisi walitumia gasi za kutoa machozi na kufyatua risasi kuelekea kwa waandamanaji.
nchi ya Guinea , imekuwa ikitawaliwa na kiongozi ambaoyealikuwa mwanajeshi na wanajeshi lilikuwa nyuma yake.
Picha hapo juu, anaonekana moja ya mwanadamanaji, akiwa chini ya ulinzi wa maafande tayari kumpeleka mung'anda.

Bi, Angel Markel, kuongoza usukani tena nchini Ujerumani.

Ndugu wawili ,Wakijerumani ndiyo waanzilishi wa makampuni za viatu maarufu duniani.

Furth, Ujerumani - 28/09/09.Kampuni ya viatu ya adidas na Puma, zimetimiza miaka 60 tangu zianzishwe nchini Ujerumani na watoto wa baba mmoja Adi Dassler na Rudolf Dassler.
Jina la Adidas,linatokana na jina la Adi Dassler.
Puma ilianzishwa mwaka 1948, na adidas mwaka 1949,ilianzishwa rasmi kama kampuni ya viatu
Hata hivyo, kufuatia kutokuelewana kwa ndugu hawa, ndipo kulipelekea kuanzishwa kwa kampuni mbili za Puma na adidas, kampuni ambazo ndizo zinazo uza viatu kwa wingi duniani.
Mamba atumiwa na mafia kama utimizi masharti yao.
Rome Itali - 28/09/09. Serikali ya Itali imesema ya kuwa, kundi la mamafia waliopo nchini Itali wamekuwa wakitumia mamba ili kuweza kufanya biashara zao.
Mmoja wa mamafaia hao, Antoni Cristofaro,alikutwa na mamba mwenye uzito kilogram 40,kwenye bustani iliyopo nyumbani kwake Napeles.
Kwa mujibu wa wataalamu wa mswala ya wanyama,walisema mamba huyo, anauwezo wa kuvunja mbavu za mtu kwa mng'ato mmoja tu.
Hata hivyo bado uchunguzi unaendelea ni kwa jinsi gani mamba huyo aliweza kutumiwa.
Picha hapo juu, anaonekana mmoja wa mamba, ambao wamekuwa wanatumiwa kutishia watu ili kufuata masharti ya mamafia.
Rais wa Ufaransa ashitakiwa na waziri mkuu wa zamani.
Paris,Ufaransa - 28/09/09.Waziri mkuu wa zamani wa Ufaransa, Dominique Villepin, amefungua kesi zidi ya rais wa sasa wa Ufaransa,Nikolas Sarkozy.
Mwanasheria wa waziri huyo wa zamani,alisema yakuwa,rais Sarkozy, alihusika katika kashfa ya kuaribu jina la bwana, Villepin inakwenda kinyume na sheria.
Hata, hivyo, kesi ambayo rais,wa Ufaransa anashitakiwa, hataweza kufikishwa mahamani kutokana sheria ya nchi ya kuwa rais, hawezi kufikishwa mahakamani hadi hapo, atakapo toka ofisini kama rais.
Picha hpo juu, wanaonekana,rais wa Ufaransa, Nikolas Sarkozy kushoto, akiongea na Dominique Villepin siku za nyuma walipokuwa bungeni.
Picha ya pili, ni aliyejuwa waziri mkuu wa zamani wa Ufaransa,Dominique Villepin, ambaye uhusiano na Nikolas Sarkozy umekuwa utatani.
Bi, Angel Markel ,kuongoza usukani tena nchini Ujerumani.
Berlin,Ujerumani - 28/09/09. Kansella wa Ujerumani, Bi, Angel Markel na chama chake CDU- Christian Demokrat Union wamshinda uchaguzi mkuu uliofanykia mapema jana jumapili, kuvishinda vyama vingine kwa kupata kura nyingi kwa asilimia 33.8,wakati vyama vya SD - Social Demokrat kilipata asilimia 23 na vyana vingine vilipata asilimia chini ya 20.
Akiongea mbele ya wanachama na adau wake , Bi,Angel Markel, alisema yakuwa wamefanikiwa kwa kiasi kushinda lakini bado kuna kazi ya kujenga serikali mpya na kutatua matatizo ya nchi. Kufuatia, ushindi huo, mama Angel Markel, atatakiwa kuunda ya mseto kwa kushirikiana na vyama vingine.
Picha hapo,wanaonekana, Bi, Angel Markel kulia akiwa na mume wake,wakiangalia kwa tabasamu wanachama na wadau waliokuja kusikiliza matokeao ambayo yamempa ushindi mkubwa chini ya chama chake cha CDU.
Iran yaichanganya jumuia ya kimataifa.
Tehran,Iran - 28/09/09.Serikali ya Iran, imejaribu makombora yake ya masafa marefu aina Shabab 3 yenye uwezo ya kwenda km , 2000 namakombora mafupi aina ya shabab 1 na shabab 2 ambayo yanaweza kwenda umbali wa km 300-700.
Makombora shabab 3 yenye uwezo wa kwenda zaidi ya km 2000, yameleta wasiwasi kwa nchi jirani, kwani makombora hayo yanuwezo wakupiga Izrael , baadhi nchi ulaya, nchi za jumuia ya Kiaraabu.
Uzinduzi wa makombora hayo ulipokelewa kwa shangwe nchi Iran, wakuu wa jeshi wamesema hii ni kwaajili ya ulinzi wa Iran.
Kufuatia majaribio hayo ya makombora,jumuia ya kimataifa imelaani kitendo hicho na kudai kinatishia aman katika eneo zima.
Picha hapo juu,linaonekana kombora,likianza kuruka kuelekea hewani kwa majribio.

Thursday, September 24, 2009

Nchi zenye nguvu za kubaliana kupunguza siraha zake za nyuklia.

Nchi zenye nguvu za kukubaliana kupunguza siraha zake za nyuklia.

UN, Amerika - 24/09/09. Kamati ya ulinzi na usalama ya umoja wa Matifa,umekubaliana kwa pamoja kupunguza nguvu za siraha za nyuklia duniani chini ya rais wa Amerika Baraka Obama.
Hii ni mara ya kwanza kwa rais wa Amerika kusimamia mkutano wa kamati ya usalama ya umoja wa mataifa.
Akiongea hayo,mwenyekiti aliye simamia kikao hicho, rais wa Amerika , Baraka Obama, alisema yakuwa kwa kipindi cha miezi 12 inayo fuata, kutakuwa na kazi ngumu kutekeleza yale yote yaliyokubaliaka na viongozi wote wa dunia hasa kwanchi zile zenya siraha za nyuklia.
Kwa mujibu wa (IAEA) shirika linalo shughulikia maswala ya nyuklia.zina sema, nchi ambazo zina siraha za nyuklia, Urussi, Amerika, Ufaransa, Uingereza, Izrael, India na Pakistan.
Picha hapo ujuu, anaonekana, rais wa Amerika, Baraka Obama, akisikiliza kwa makini, wakati wa kikao cha kuzungumzia kupunguza nguvu za siraha nyuklia duniani.
Picha ya pili,inaonyesha ni kwa kiasi gani, siraha za nyuklia, zitakavyo athiri mazingira na kuleta madhara kwa jamii pindipo zikitumika.
Picha ya tatu, ni alama ya nguvu za nyuklia, nguvu amabzo zikitumika vibaya dunia huenda ikawa historia.
Wapalestina lazima wakubali taifa la Waizrael" Asema waziri mkuu Binyamin Netanyahu"mbele ya UN.
Umoja wa Mataifa, Amerika - 24/09/09. Waziri mkuu wa Izrael, Binyamin Netanyahu, ameuambia yakuwa serikali yake, na Waizrael wote nanacho taka ni kwa Wapalestina kukubali kuwepo kwa taifa la Izrael, ambao wataishi kama majirani.
Hata, hivyo, waziri mkuu huyo wa Izrael, alisema ile hoja yakuwa mauaji ya Waizrael ya Holokosti haya kufanyaika ni aibu kwa wote amabo wanasema hayo, kwani ushaidi ndiyo huu" Hapo alikuwa akionyesha baadhi ya karatasi ambazo zilikuwa zimetumika au kuandaliwa na watu wa kundi la NAZI.
Vilevile, alilaumu, kamati la umoja wa mataifa inaloshughulikia haki za binadamu, kwa kutoa uamuzi kwa upendeleo.
Waziri mkuu, Binyamin Netanyahu,alimaliza kwa kusema,kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu, amani itakuwepo.
Picha hapo juu, ni picha ya waziri mkuu wa Izrael, Binyamini Netanyahu,ambaye alihutubia umoja wa mataifa leo.
Rais wa Iran, azilaumu nchi tajiri na zenye nguvu.
UN, Amerika - 24/09/09. Rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad, ameilaumu nchi tajiri na zenye nguvu kwa kusababisha vita, umwagaji wa damu, kukuza ugaidi na kutishia amani, kwenye eneo la Mashariki ya Kati na Afghanistan.
Rais huyo wa Iran, alisema yakuwa, nchi hizi za Ulaya, zimekuwa zikitangaza kuwa lazima kuwe na demokras katika kila nchi, lakini zinakiuka misingi kamili ya maana ya demokrasi, na imefikia wakati kwa dunia kuyaeleza kiuwazi,pia kutokueleweka kwa misimamo ya nchi hizi za Ulaya zenye nguvu, kwa kuuleza vingine na kutenda vingine kinyume na waliosema bali kukaripia nchi nyingine na kuzitisha.
Akizungumzia, swala la nyuklia, rais wa Iran, alisema kunahaja ya kuangamiza siraha za kibaiolojia na siraha za kikemikali,na kuruhusu kuwepo na teknolojia inayo tokana na nyuklia kwa matumizi ya ya maendeleo ya sayansi. Picha hapo juu, anaonekana, rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad, akihutubia mkutano wa 64 wa umoja wa mataifa mapema jana.

Wednesday, September 23, 2009

Viongozi wa dunia tukubali kuwajibika"Asema rais ,Baraka Obama"

Viongozi wa dunia tukubali kuwajibika" Asema rais, Baraka Obama" Umoja wa Mataifa,Amerika - 23/09/09.Rais wa Amerika, Baraka Obama, amewataka viongozi wa dunia, kukubali kuwa tayari na kukabiliana na mageuzi ya dunia ya sasa,kwani ina mapambano makubwa sana. Akiongea, rais Obama,alisema, nilazima kila kiongozi awajibike,kwani Amerika pekee yake haitaweza kutatua matatizo ya dunia nzima,ambayo yanasababishwa na matatizo yanayo ikabili dunia, na hatimayake kunapelekea kuwepo na watu wenyer itikadi kali na baadeye wanakuwa magaidi, wauwaji , wavurugaji wa amani na umasikini kuongezeka na hata kuharibu hali ya hewa na mazingira yake. Rais , Obama, alisema tangu kuchukua ofisi,yeye pamoja na uongozi wake wamejitahidi kupambana na ukweli wa hali halisi inayo ikabili dunia ya leo. Hii ndiyo hali halisi ambayo tunakabiliwa nayo. Kuhusu, hali ya amani ya Mashariki ya Kati, rais, Obama, alisema yakuwa uongozi wake utajitahidi kwa hali mali kuhakikisha amani inapatikana kati ya Wapalestina na Waizrael. Kwani wakatai umefika kukuzungumza bila kuwekeana vikwazo wala masharti, kwani wanaoumia ni wanachi wa Izrael na Wapalestina na siyo wanasiasa, "akijionyeshe yeye mwenyewe". Picha hapo juu, anaonekana rais , wa Amerika, Baraka Obama, akiwahutubia viongozi walioudhulia mkutano wa 64 wa umoja wa Mataifa jijini New York Amerika, ili kujadili hali ya dunia nzima inavyobadirika kimazingira na swala la kuwepo amani duniani kote. Rais wa Libya Muammar Gaddafi, ashambulia umoja wa matifa, "Adai mabadiliko ya kikatiba ya UN". UN,Amerika - 23/09/09. Rais wa Libya, Muammar Gaddafi, amelishambuli umoja wa Matifa kwa kusema ya kuwa linakwenda kinyume na katiba ya umoja huo. Akisisitiza, kwa undani, rais Gaddafi, alisema ya kuwa kamati ya usalama ya umoja wa matifa, haitakiwi kuwa baadhi ya nchi wanachama tu, bali kila nchi mwanachama lazima ihusishwe, kama hakutafanywa hivyo,ni kukiuka katiba ya umoja huu. Rais, Gaddafi, alisema yakuwa nchi ambazo zina viti vya kudumu, katika kamati ya usalama ya umoja wa mataifa , zina nyanyasa nchi ndogo na masikini,kwa kutumia kura zake za veto,na kwani katiba ya umoja huo,inasema ya kuwa nchi zote ni sawa ndogo hadi nchi kubwa. Akiongezea, rais Gaddafi, alisema yakuwa,inabidi umoja huu uundwe upya kikatiba ambayio itaipa kila nci hakisawa. Kuhuusu swala la amani mashariki ya kati,rais Gaddafi,alisema yakuwa Waarabu na Waizrael hawana uadui, bali ni mgongano wa kisiasa unao sababisha kutokuwepo na amani. Kwa kumalizia, rais wa Libya, Muammar Gaddafi, alisema yakuwa swala la kuleta amani duniani ni la kila kiongozi kuwajibika kikamilifu. Picha hapo juu, anaonekanana raia wa Libya, Muammar Gaddafi, awaaga viongozi wa nchi waliokuwa wakimsikiliza hotuba yake iliyo chukua saa moja na dakika 27,kuelezea kiundani wa UN. Lazima tutumize malengo tuliyo yaweka kwenye karne ya 21"Asema katibu mkuu" Umoja wa Mataifa,Amerika - 23/09/09.Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa,Ban Ki moon,amefungua rasmi, baraza kuu la mkutano wa umoja wa mataifa la 64, na kusisitiza viongozi wa nchi zote kuungana kutimiza agizo la kupambana mabadiliko ya hali ya hewa na kuleta amani duniani, ili kufikia malengo ya karne ya 21. Katibu huyo, Ban Ki moon,ameagiza pia viongozi waasimamishe umwagikaji wa damu, huko mashariki ya Kati na Afghanistan,kupamabana na umasikini,kulinda haki za wanawake,kudumisha demokrasi,na kupunguza nguvu za nyuklia na bila kusahahu Somalia na Sudan. Picha hapo juu, anaonekanana, katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki moon,akihutubia wakuu wa nchi walioudhulia mkutanao wa Umoja wa Mataifa wa 64, jijini New York.

Tuesday, September 22, 2009

Amerika na Venezuela, kisa cha uhasama chawekwa hazarani.

Umoja wa Mataifa waanza kwa vishindo kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.

UN, Amerika - 22/09/09. Viongozi mbalimbali duniani, wamekutana leo kwenya ukumbi wa umoja wa mataifa kwa ajili ya kuangali upya ni jinsi gani wataifanya dunia kuawa sehemu ya amani na salama kwa viumbe wote.
Mkutano huo ambao uliitishwa na katibu mkuu wa UN,Ban Ki- moo,ilikuwahimiza viongozi hao kupambana na hali ya mabadiliko ya hali ya hewa duniani,hali ambayo katibu huyo alisema ipo haja ya kuishughulikia haraka kabla hali haijawa mbaya.
Akikubaliana na hoja hiyo , rais wa Amerika, Baraka Obama,alisema ipo jhaja viongozi wote wa dunia, kushirikiana kikamilifu ili kukabiliana na hali hii ya hatari, ambayo ikifanikiwa kutushinda basi hatutaweza tena kuikabili.
Picha hapo juu, anaonekana, rais wa Amerika, Baraka Obama, akihutubia viongozi, walioudhulia mkutana kujadili hali ya hewa duniani inavyo badilika kuelekea pabaya.
Picha ya pili anaonekana,katibu wa UN, Ban Ki moon, akimkaribisha, rais wa Amerika, Baraka Obama kuhutubia viongozi walilio udhulia mkutano kujadili hali mabadiliko ya hali ya hewa duniani.
Picha ya tatu, wanaonekana viongozi wa mbalimbali wakiwa wameka katika ukumbu wa mkutanao wa UN, huku wakimsikiliza rais, Baraka Obama.
Rais , Obama, awataka viongozi wa Izrael na Palestina kufanya uamuzi wa busara.
New York, Amerika - 22/09/09.Rais wa Amerika, Baraka Obama, amewataka viongozi wa Izrael na Palestina kufanya uamuzi wa busara na kwa makini ili kuleta amani.
Rais, Baraka Obama,aliyasema hayo wakati alipo kutana na viongozi hao, waziri mkuu wa Izrael, Binyamin Netanyahu na rais wa Wapalestina, Mahmoud Abbas, jijini New York, kujadili kwa undali hali ya amani kati ya Waizrael na Wapalestina.
Picha hapo juu, wanaonekana, rais wa Amerika, wa pili kutoka kushoto,waziri mkuu wa Izrael, Binyamin Netanyahu, kushoto,na rais wa Palestina, Mahmoud Abbas, kulia wakati walipo kutana leo jiji New York.
Amerika na Venezuela, kisa cha uhasama chawekwa hazarani.
Caracas, Venezuela - 22/09/09. Rais wa zamani wa Amerika, Jimmy Carter, Washington walijua yakuwa kulikuwa kuna mpango wa kuipindua serikali ya rais wa Veneuela, Hugo Chavez, mwaka 2002, na huenda ilishiriki kwa njia moja ama nyingine.
Jimmy Carter, alisema yakuwa hakuna shaka, mwaka 2002, serikali ya Amerika, ilikuwa inahabari kamili yampango huo, na ndiyo sababu, serikali ya rais, Hugo Chavez, ililaumu serikali ya Amerika na kuwa maadui wakubwa na serikali ya Amerika, iliyo kuwa ikiongozwa, rais George Bush.
Hata hivyo seriali ya Amerika, chini ya rais, George Bush, ilikanusha kuhusika na wala hawakuwa na habari za kutaka kuipindua serikali ya Venezuela.
Picha hapo juu, wanaonekana , rais wa zamani wa Amerika , Jimmy Carter kushoto,akiongea na rais wa Venezuela, Hugo Chavez,wakati walipo kutana hivi karibuni.
Usalama na amani wa Afghanistan bado kupatiwa jibu kamili.
Kabul, Afghanistan - 22/09/09.Kamando mkuu wa majeshi ya NATO, Stanley Mc Chrystal, amesema ya kuwa habari zilizo patikana katika vyombo vya habari, kuhusu hali halisi ya Afghanistan na usalama wake kwa raia utakuwa na wakati mgumu, kama hakutaongezwa na wanajeshi kupambana na kundi la Taliban, kwa umakini ni wa ukweli.
Kamando huyo,Stanley Mac Chrystal,aliilaumu serikali ya Taliban kwa kushindwa kudhibiti rushwa iliyo shamili nchini humo, na kwa sababu ya hali hiyo, inawafanya wananchi kutokuwa na imani na serikali.
Kamando, MC Chrystal, alisema yakuwa kuma hakutachukuliwa uamuzi wa busara, basi itafika wakati Taliban watakuwa ni wagumu kupambana nao.
Picha hapo, anaonekana, Gnl,Stanley McChrystal, akikagua maeneo ya kivita hivi karibuni.
Picha ya pili, linaonekana, jeneza la moja ya mwanajeshi wa jeshi la Amerika, akirudishwa nyumbani, mara baada ya kupoteza maisha wakati alipo kuwa katika mapambano na kundi la Taliban.
Izrael kuhaidi mbele ya Urussi, hakuna mashambulizi zidi ya Iran.
Moscow, Urussi - 22/09/09. Rais wa Izrael, Shimon Peres, ameihakikishia serikali ya Urussi, ya kuwa serikali ya Izrael,haitaishambulia Iran.
Uhakika huo ulitolewa mbele ya rais wa Urussi, Dmitry Medvedev, wakati alipo kutana na rais wa Izrael, ambaye alikuwa ziarani nchini Urussi.
Kwa kuongezea hayo,rais wa Urussi, Dmitry Medvedev,alisema yakuwa kitendo chochote cha kuishambulia Iran, kutakuwa ni kibaya na huenda kikaleta hali ya mashaka katika eneo zima la mashariki ya Kati.

Saturday, September 19, 2009

Rais wa zamani wa Amerika aweka ukweli bayana.

Mitambo ya nyuklia ya Izrael yataikiwa ichunguzwe " Umoja wa Matifa wasema".

Viena Austria - 19/09/09. Shirika la Kimataifa linalo shughulikia ukaguzi wa siraha za nyuklia, limeitaka serikali ya Izrael, kuwaruhusu wachunguzi wa IAEA (International Atomic Egenegy Agency), kuchunguza mitambo yake na kuitaka nchi hiyo iingie kwenye mkataba wa na shirika hilo la la umoja wa mataifa.
Kwa mujibu habari kutoka umoja wa matifa, zinasema yakuwa kura zilipigwa siku ya ijumaa na kwa mara ya kwanza,mswada huo ulipata ushindi, wajumbe kutoka nchi za Kiaarabu walionesha furaha zao, kwa kuzingatia walikuwa wanajaribu kusukuma mswada huu upite kwa muda wa miaka 18.
Hata hivyo serikali ya Izrael,hakukubaliana na mswada huo.
Wakati huo huo,kuna habari yakuwa Iran inauwezo wa kutengeneza siraha zenye uwezo wa kinyukli, hii ni kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na wachunguzi wa Umoja wa Matifa.
Kwamujibu wa UN, ni nchi tatu, ambazo hazina mkataba na IAEA, India, Pakistan na Izrael.
Picha hapo juu, ni alama ya shirka la kimatifa linalo shughulikia ukaguzi wa nyuklia na madhara yake, ambalo limekuwa na wakati mgumu kutatua mgogoro wa nguvu za nyukili duniani.
Picha ya pili, ni ya moja ya ndege za kivita za Izrael, ambazo zina uwezo wa kisasa wa kivita.
Picha ya tatu, inaonesha makombora yakitoka ardhini,hili ni moja ya mazoezi ya kijeshi ya jeshi la Iran, nchi ambayo imekuwa na mvutano na IAEA, kuhusu swala na nyuklia.
Amerika bado kupata jibu la kitendawili cha Izrael na Palestina.
Tel Aviv,Izrael - 19/09/09. Mjumbe wa serikali ya Amerika, ambaye anashughulika swala la kuleta amani kati ya Wapalestina na Waizrael, George Mitchell, ameshindwa kupata uhakika ya kuwa Izrael itasimamisha utanuzi wa ujenzi wa makazi,na kujua ni kwa jinsi gani, mazungumzo ya amani yata rudi kuzumgumzwa tena.
Kushindwa huko, kwa mjumbe huyo wa Amerika, George Michell, kuweka mikakati mipya ya kuwakutanisha viongozi wa upande wa Wapalestina na Izrael.
Kwa mujibu wa serikali ya Palestina, haitaweza kuendelea na mazungumzo, hadi hapo serikali ya Izrael, itakapo simamisha utanuzi ujenzi wa makao mapya katika eneo la West bank na Mashariki ya Jerusalem.
Picha hapo juu,anaonekana, mjimbe wa Amerika, George Mitchell,kushoto akiongea na waziri mkuu wa Izrael,Binyamin Netanyahu, kabla ya mjumbe huyo wa Amerika kurudi nyumbani.
Meli zenye takataka za sumu, kutafutwa baharini"Zimezamishwa makusudi"
Rome, Itali - 19/09/09.Serikali ya Itali imeanza uchungu wa kina,baada ya habari kuvuma ya kuwa kuna meli zenya uchafu na takataka za sumu zimekuwa zikizamishwa kwenye bahari ya pwani ya Kalabrian kwa makusudi na mamafia.
Kwa mujibu wa habari hizo , inasemekana kuana zaidi ya meli 32, ambazo zimezamishwa.
Akijibu swali hili, mkuu wa mazingira ya eneo la Kalabrian,Silvestero Greco,alisema yakuwa, habari hizi,zilitolewa na aliyekuwa mmoja ya mamafia hao Francesco Fonti, ambaye alikubali yakuwa yeye, alisha wahi kuhusika katika uzamishaji wa meli moja yenye takataka za sumu.
Picha hapo juu, ni nchi ya Itali,nchi ambayo, uchunguzi unafanywa kwa udani kujua meli zilizamishwa wapi na lini, ili kuopoa mazingira.
Picha ya pili, mkuu wa mazingi wa eneo la Kalibrian,Silvestero Groco,ambaye anajukumu kubwa la kuhakikisha maingira yakuwa ya usalama kwa binadamu na viumbe wengine.
Rais wa zamani wa Amerika aweka ukweli bayana.
Washington, Amerika - 19/09/09.Rais wa zamani wa Amerika,Jimmy Carter, amesema yakuwa wale wote, ambao wana kuongea vibaya kumpinga rais wa Amerika, Baraka Obama, wana fanya hivyo kutokana na chuki za kibaguzi,kwa kuzingatia , rais Obama ni abaasili ya Afrika ( Mweusi).
Jimmy Carter, aliyasema hayo, baada ya baadhi ya wananchi wa Amerika wenye msimamo mkali,kupinga kwa kashfa mipango ya rais, Baraka Obama ya kuinua hali za maisha na afya kwa wanchi wote wa Amerika.
Kufuatia, matamshihayo, pia rais, Baraka Obama, alikubaliana na mawazo hayo,kwa kusema ya kuwa anafahamu fika kuana, baadhi ya watu na viongozi wanapinga au wanampinga kuleta mabadiliko kutokana na rangi yake, na wengine wanakubaliana naye,hivyo ukweli ni kwamba kuja haja ya kuwepo na mabadiliko ya kimaisha, hasa kiafya kwa Waamerika wote, hiyo ndiyo moja ya melengo yake.
Picha hapo, anaonekana,rais wa zamani wa Amerika, ambaye huwa asiti kusema ukweli pindipo akiona baadhi ya viongozi wanakwenda kinyume na maadili mazuri ya uongozi
Venezuela ya ikaribisha China.
Caracas, Venezuela - 19/09/09. Serikali ya Venezuela imetiliana imtetangaza ya kuwa imetiliana mkataba wa $US dolla 16 billion na serikalia ya China,mkataba ambao utaiwezesha serikali ya China, kuchimba na kutoa mfuta katika jimbo la Orinoco.
Mkataba huo,ulio sainiwa jiji Beijing, unahusisha pia makubaliana ya kuwa serikali ya China,itasaidia ukarabati wa na ujenzi wa barabara na nyumba.
Picha hapo, juu anaonekana , akimpiga busu,mmoja ya wanafunzi wakati alipo kwenda kutembelea eneo ambalo,China imepata mkataba wa kuchimba mafuta.

Thursday, September 17, 2009

Ofisi za ulinzi za Umoja wa Afrika nchini Somalia zashambuliwa.

Hatujengi tena mitambo ya kurusha makombora ulaya ya kati, "asema rais Baraka Obama.

Washington, Amerika - 17/09/09. Rais wa Amerika, Baraka Obama, amefuta mpango wa serikali ya Amerika kujenga mitambo ya kurushia makombora ya kijilinda na mashambuli ya kijeshi ya aina yoyote katika nchi za Poand na Czech.
Akiongea hayo, rais, Baraka Obama, alisema ya kuwa vitisho vya vilivyo kuwa vimewekwa na serikali iliyo pita, havikuwa na usahihi ya kuwa Iran, inaweza shambulia masrahi ya Amerika yaliyopo katika nchi za Ulaya, ambazo ni wananachama wa NATO.
Hata hivyo, rais, Baraka Obama, alisema yakuwa mitambo mipya ya makombora ina ya SM3 itajengwa katika meli za kijeshi na baadaye kuwekwa katika moja ya nchi za NATO.
Kwa kusisitiza hayo, waziri wa ulinzi wa Amerika. Robert Gate, alisema yakuwa, serikali ya rais, Obama bado inalitilia maanani swala la Iran kuwa na mitambo ya kinyuklia, na hivyo hakuna haja ya kuwa na shaka,kwani mitambo mipya itakuwa na uwezo wa kila aina kupambana na kila shambulizi.
Kufuatia uamuzi wa serikali ya Amerika, kufuta mpango wa kujenga mitambo ya kurusha makombora katika nchi za Poland na Czech,nchi hizo zimesema zimesikitishwa na uamuzi huo wa serikali ya Amerika.
Picha hapo juu, anaonekana, rais wa Amerika, Baraka Obama,ambaye amefuta mpango wa serikali ya Amerika kujenga mitambo ya kurushia makombora ulaya ya kati.
Picha ya pili ni ya baadhi ya makombora, yakiwa yapo tayari kwa mashambulizi wakati wowote,lakini kwa sasa mitambo ya makombora hayo hayatajengwa tena ulaya ya kati.
Ofisi za ulinzi za Umoja wa Afrika nchini Somalia zashambuliwa.
Mogadishu, Somalia - 17/09/09.Mabomu yamelipuka katika ofisi za makao makuu ya jeshi la Umoja wa nchi za Afrika zilizopo nchini Somalia kwaaajili ya kulinda amani.
Kufuatia mlipuko huo, watu wapatao 11, wamepoteza maisha, wakiwemo wanajeshi 6, wa jeshi la Umoja wa nchi za Afrika na wengine 18 kujeruhiwa vibaya.
Akiongea kuthibitisha ya kuwa kundi la Al Shabab,mmoja wa msemaji wa kundi hilo alisema yakuwa kundi lao ndiyo lililo fanya mashambulizi hayo, kwani wanahabari ya kuwa baada ya mwezi wa Ramadhan kuisha,jeshi la umoja wa nchi za Afrika unapanga kulishambulia kundi hilo, wamelipa kisasi cha kuuwawa mmoja wa kiongozi wao Ali Saleh Nabhan, ambaye aliuwawa na jeshi la Amerika siku mbili zilizo pita, baada ya kutafutwa kwa muda mrefu, kwa kuhusika na mashambulizi ya hotel na ndege ya Izrael nchi Kenya.
Picha hapo juu,linaonekana, moja gari la jeshi la Umoja wa Afrika, ambalo lipo katika mzunguko kwa ajili ya ulinzi katika moja ya mitaa ya mji wa Somalia
Picha ya pili wanonekana wapiganaji wa kundi la Al Shabab, wakiwa mazoezi,kundi hili limekuwa linapingana na serikali ya Somalia kwa muda mrefu sasa.
Waathirika wa uchafu na sumu kupata fidia, kampuni ya mafuta yakutwa na hatia.
Abidjan, Ivory Coast - 17/09/09. Kampuni ya kuuza mafuta, ya Trafigura imekubali kulipa fidia kwa watu na jamii nzima iliyo athirika na uzembe wa makusudi kwa kutupa takataka za mabaki ya sumu katika ufukwe wa bahari ya Ivory Coast.
Kwa mujibu wa habari kutoka UN,Umoja wa Matifa,zinasema ya kuwa kuna ushaidi kamili ya kuwa kutokana na kumwaga uchafu huo katika ufukwe wa bahari wa Ivory Coast,watu wengi wameathirika kiafya na hata wengine kupoteza maishayao,kwani uchafu huo ulikuwa nasumu.
Uchafu huo ulimwagwa na meli ya shirika la Probo Kaola, baada ya kukusanya uchafu uliotokana na mafuta yaliyo chujwa kutoka kwenye viwanda vya kuchujia mafuta hayo vilivyopo nchi za ulaya.
Picha hapo juu, wanaonekana baadhi ya wataalamu wa mazingira wakimwaga dawa kuua sumu iliyo mwagwa na meli ya Probo Kaola katika ufukwe wa Ivory Coast.
Picha ya pili, anaonekana mama mmoja, ambaye aliathirika kutokana na sumu,iliyo mwagwa na meli ya Pobo Kaola.
Hamid Karzai avilaumu vyombo vya habari
Kabul, Afghanistan - 17/09/09. Rais wa Afghanistan, Hamid Karzai, ambaye anagombania tena kiti cha urais huo kwa mara ya pili, amezilaumu baadhi ya vyombo vya habari kwa kutoa habari zinazo haribu ukweli wa hali halisi ya uchaguzi wa Afghanistan.
Hamid karzai, aliyasema hayo leo, wakati alipo kuwa akingea na waandishi wa habari, kufatia ripoti iliyo tolewa na wasimamizi wa uchaguzi kutoka jumuia ya umoja wa Ulaya, ya kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, baadhi ya kura zipatazo million 1.5 zimekuwa na utata.
Hata hivyo, Hamid Karzai, aliwataka wanachi wa Afghanistan kuwa wavumilivu, kungoja matoke ya mwisho, kwani atashirikiana kikamilifu katika kuchunguza kama kulikua kuna ukiukwaji wa kupiga kura.
Picha hapo juu, anaonekana, Hamid Karzai,ambaye anaongoza kwa kupata kura nyingi katika uchaguzi uliofanyika nchini Afghanistan, lakini haliya ya ukiukwaji wa kupiga kura bado hakujamwakikishia ushindi kamili.
Hatimaye bunge la umoja wa Ulaya lapata rais.
Brussels, Ubelgiji - 17/09/09. Umpja wa Ulaya, umemchagua tena, Jose Manuel Barroso, kuwa rais wa umoja huo, kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Katika uchaguzi huo, Jose Emanuel barroso, alipata kura 382,ambazo zilitakiwa kuzidi nusu ya idadi ya wabunge, kura 219 zilimkataa, na wabunge 117, hawakupiga kura.
Matokeo ya uchaguzi huu, kumemaliza utata, uliokuwa umezingira umoja huu kwa muda wa miezi sasa.
Akiongea mara baada ya kuchaguliwa, Jose Emanuel Barroso, alisema ya kuwa atahakikisha ya kuwa umoja wa wa Ulaya unadumisha demokrasi.
Picha hapo juu, anaonekana, Jose Emanuel Barroso,ambaye amechaguliwa kuwa rais mpya wa umoja wa Ulaya kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Japan yapata waziri mkuu mpya.
Tokyo,Japan - 17/09/09.Wanchi wa Japan, wamepata waziri mkuu mpya,Yukio Hatoyama, ambaye ameshinda uchaguzi uliofanyika mwezi uliopita.
Akihutubia mbele ya wabunge, waziri mkuu,Hatoyama, alisema atadumisha uhusiano uliopo kati ya Japan na Amerika, na vilevile kuendeleza uhusiano bora na nchi majirani zake hasa China.
Picha hapo juua anaonekana, waziei mkuu mpya wa Janap, Yukio Hatoyama,akiongea mbela ya wabunge mara baada ya kuapishwa kuwa waziri mkuu.

Tuesday, September 15, 2009

Mwandishi wa habari aliyetikisa dunia atoka jela.

Mwandishi wa habari aliyetikisa dunia atoka jela.

Baghdad, Irak,- 15/09/09. Mwandishi wa habari, Muntadhar Al Zeidi, ambaye aliukumiwa kwenda jela kwa mwaka mmoja baada ya kumtupia kiatu aliyekuwa rais wa Amerika, George Bush, ameachili huru , baada ya kumaliza kutumikia kifungo chake.
Akiongea na vyombo vya habari, Muntadhar, alisema ya kuwa alishindwa kujizuia kumrushia kiatu aliye kuwa rais wa Amerika, George Bush,kwani alikuwa anawakilisha wale wote aliopoteza maisha, na kuumia kutokana na vita vya uvamizi wa Amerika kwa nchi ya Iraq,ambapo kila alipo kuwa akimaliza kazi alikuwa anapata ndoto za ajabu kwa kuona mateso ya watu wa ambao alikikuwa anawasaidi wakati akiwa kazini kwenye kuripoti matukio ya kivita, na ndiyo maana akaamua ya kuwa njia moja ya kumuuga na kumwonyesha rais Busha ya kukwa uvamizi wake umeleta maafa makubwa kwa wanachi wa Irak, ni kumtupia viatu na kumtukana.
Vilevile, Muntadhar, alisema baada ya muda atajtaja majina ya wale wote walio hisika katika kumtesa wakati alipo kamatwa na alipo kuwa jela.
Mwandishi wa habari huyo, alisema ya kuwa aliteswa vibaya sana, na madai yaliyo tolewa na waziri mkuu, hayakuwa ya kweli ,na kudai ya kuwa kuna watu wengi ambao hawana hatia wapo jela bila kufikishwa mahakamani.
Na mwisho, Muntadhar al Zeidi, alihaidi yakuwa atajitolea kusaidia wale wote waliopata matatizo kutokana na vita japo hali ya usalama wake upo mashakani, kwani kuana makundi yanampango wa kumua.
Picha hapo juu,anaonekana,akirusha kiatu kuelakea alipo kuwa rais wa zamani wa Amerika, George Bush,kabla ya kukamatwa na walinzi, ili asileta maafa zaidi.
Picha ya pili, wanaonekana, rais wa Amerika George Bush, kushoto na waziri mkuu wa Irak, Nouri al Maliki,wakati walipo kuwa pamoja kuongea na waandishi wa habari, kabla ya mashambulizi ya viatu yaliyo fanywa na Muntadhar al Zeidi.
Picha ya tatu, anaonekana , Muntadhar al Zeidi , akiongea na waandishi wa habari, mara baada ya kumaliza kifungo chake.
Venezuela yazidi jiimarisha kijeshi.
Moscow, Urussi, 15/09/09. Serikali ya Urussi , imekubali kuikopa serikali ya Venezuela, zana zakivita zenye thamani ya dola za Kiameria billion 2.
Zana hizo za kivita, ambazo zitakuwa mizinga ya kutungulia ndege,vifaru na siraha nyingine za kiteknologia ya kisasa.
Makubaliano hayo yalifanyikia wakati wa viongozi wa serikali hizi mbili walipo kutana jijini Moscow wiki mbili zilizo pita.
Kufuatia, Venezuela, kupata siraha hizo kutoka Urussi, serikali ya Amerika, imesema kuongezeka kwa matumizi ya kununua zana za kivita kwa Venezulam kunaweza kuleta hali ya wasiwasi kwa nchi majirani.
Picha hapo juu, zinaonekana, moja ya zana za kijeshi za Kirussi, ambazo Venezuela, itakuwa mmiliki wa baadhi ya zana hizo.
Adhabu ya kuzini ni kupigwa mawe hadi ufe, bunge lapitisha sheria mpya.
Aceh, Indonesia - 15/09/09. Jimbo la Aceh, ambalo ni sehemu ya Indonesia, limepitisha sheria ya kupigwa mawe hadi kufa, ikiwa mtu amakutwa na hatia ya kuzini.
Kwa mujibu wa habari kutoka katika bunge la jimbo hilo,ambalo wakazi wake wengi ni waumini wa dini ya Kiislaam,sheria hiyo itakayo julikana kama "Qanun jinayat"ita wakuta wale wote wanao kwenda kinyume na dini,ikiwepo mashoga, na wele wanao anza kufanya mapenzi kabla ya wakati.
Sherii hii itachukua mkondo wake kutokana na kosa lilitendwa, kwa kupigwa viboko 100, kwenda jela miaka mingi na kupigwa mawe hadi kufa na sheria hiyo itaanza kufanya kazi siku ya 31 tangu kupitishwa kwake.
Hata hivyo mashirika ya kutetea haki za binadamu, wamepinga vikali sheria hiyo na kudai imekwenda kinyume na haki za binadamu.
Picha hapo, juu wanaonekana baadhi ya wananchi wa jinbo la Aceh, wakiowa mbele ya bunge kupinga kupitishwa kwa sheria ya Kwanum Jinayati.
Rais, Baraka Obama, mabenki lazima yafatiliwe kiungalifu.
Washingtone, Amerika - 15/09/09. Rais wa Amerika, Baraka Obama, amesema ya kuwa hali ya uchumi wa Amerika una ananza kukua, kazi zinaanza kupatikana kwa wanachi wa Amerika.
Rais, Obama , alisema yakuwa, kukua kwa uchumi wa Amerika, ni kukua kwa uchumi wa dunia nzima, na kuporomoka kwa uchumi wa Amerika, kuliathiri uchumu dunia nzima,hivyo chini ya uongozi wake hataruhusu tena kutokuwajibika kwa wafanyakazi katika sekta ya fadha, ambo ndiyo chanzo cha mporomoko wa uchumi uliotokea kwa kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
Rais Baraka Obama, aliliomba bunge la Kongresi kupitisha miswaada yote aliyo ipendekeza.
Picha hapo juu, ni ya rais wa Amerika Baraka Obama, ambaye toka, achukue madaraka kama rais wa Amerika, amekuwa na kibarua kigumu cha kuinua uchumi wa Amerika, ili kuwezesha nchi hiyo kurudi katika hali yake ya kawaida ya kuongoza dunia.
Helkopta ya kijeshi yafanya mashambulizi ya ghafla.
Mogadishu,Somalia - 15/09/09. Wapiganaji wawili wa kundi la Al Shabab, wameuwawa, baada ya helkopta ya kijeshi kuwashambulia wapiganaji hao walio kuwa ndani ya gari.
Kwa mujibu wa watu walio ona tukio hilo walisema yakuwa wanajeshi kutoka kwente helkopta walishambuli gari hilo karibu na kitongoji cha Barawe.
Na baadhi ya watu wamesema helkopta hiyo ilikuwa ya Kiamerika.
Nalo kundi la Al Shabab, limekubali ya kuwa kumekuwa na mashambulizi yaliyo fanywa kwa wapiganaji wake, lakini halikutoa maelezo kamili.
Hata hivyo, msemaji wa serikali ya Amerika, hakuweza kukana wala kukubali wakati alipo ulizwa kuhusu mashambuli hayo.
Picha hapo juu, kwenye ramani, sehemu ya ramani yenye rangi udongo mwekundu ni ya ramani ya nchi ya Somalia nchi ambayo imekuwa katika hali ya utata wa kiusalama kwa muda mrefu sasa