Wednesday, May 28, 2008

Aman ya Lebanon"Uongozi mpya utaleta utulivu?" Siniora arudi ofisini.

Oliver Kahn ,nyota ya makipa ya Ujerumani, ameliaga rasmi lango la milingoti mitatu maeneo yake.

Munchen, Ujerumani - Aliyekuwa golikipa namba moja wa timu ya bayen Munchen, naaliyewahi kuwa golikipa namba moja wa timu ya taifa ya Ujerumani, Oliver Kahn, hivi karibuni alicheza mechi yake ya mwisho na timu yake ambayo amechezea kwa kipindi zaidi ya muongo mmoja.
Oriver Kahn, ambaye alianza kudakia timu ya Karlsruher SC,wakati akiwa na miaka 18 na baadaye msimu wa 1993-94, kuamia Bayen Munchen.
Kahn alilikuwa na wakati mgumu na wakati wafuraha wakati wote alipokuwa kipa namba moja wa Buyen Munchen na timu ya taifa ya Ujerumani.
Picha ya kwamza hapo juu anaonekana kipa Oliver Kahn, akifanya vitu vyake kumnyima kaptain wa timu ya Kamerooni Rigobert Song, kufunga goli wakati wa mashindano ya kombe la dunia yaliyo fanyika Japan -Korea ya Kusini mwaka 2002.
Picha ya pili anaonekana Oliver Kahn,akiangalia bila matumaini jinsi gani nyavu zinavyo cheza, baada ya Ronaldo kufanya vitu vyake 2002 kwenye kombe la dunia lililo fanyika Japan - Korea ya Kusini.
Picha nyingine ya kati anaonekana, Oliver Kahn akitoka nje baada ya kufanya vitu vyake kulinda lango la timu yake Buyen Munchen.
Picha ya nne, anaonekana Oliver Kahn, akitokwa na damu kwenye kipaji cha uso baada ya kugongwa na kitu kisicho julikana,.
Picha ya chini anonekana Oliver Kahn, akiokoa mpira usielekeendani ya lango lake 1999, wakati timu yake Bayen Munchen ilipo pambana na Man United katika fainali za klabu bingwa za Ulaya mwaka 1999 na pembeni wanaonekana mshambuliaji wa Man United, Andy Cole na beki wa Bayen Munchen Sammy Kofour wakiangalia kwa makini.
Jimmy Carter "Amerika ifikilie kuongea na Iran" mabomu ya nyuklia "Carter", ayakadilia idadi yake duniani.
London, Uingereza - Rais wa zamani wa Amerika, bwana Jimmy Carter, amesema ya kuwa itabidi rais atakaye chaguliwa kuiongoza Amerika , kuongea moja kwa kwa na serikali ya Iran, ili kuishawishi kuacha mpango wake wa kuendelea na ujenzi wa mitambo ya nyuklia.
Akiongea haya, nchini Uingereza, bwana Carter alisema yakuwa nchi kama Amerika, Uingereza , Ufaransa, Urusi na Israel, ambazo zina mabomu ya nguvu za kinyuklia.
Aliongezea yakuwa Amerika ina siraha za nyuklia zisizo pungua 12,000, na nchi nyingine kama Ufaransa,Uingereza zina zaidi ya mamia na Israel ina zaidi ya 150 ya siraha hizo.
Picha hapo juu, anaonekana bwana, Jimmy Carter, alipo kuwa amepokea zawadi za nishani ya amani.
Picha nyingine anaonekana bwana, Jimmy Carter, akisaidia kujenga jamii hivi karibuni, ikiwa ni moja ya kazi anayo ifanya kusaidia kuinua maisha ya watu walio na kipato cha chini.
Kiongozi mpya wa bunge la Iran, aonya IAE, baada ya ripoti kutolewa.
Teheran, Iran - Bunge la Iran, limemteua aliyekuwa kiongozi wa Iran katika mazungumzo ya kinyuklia bwana Ali Larijani kuwa kiongozi wa bunge la Iran ( Spika wa Bunge).
Baada ya uteuzi huu, bwana, Ali Larijani alionya ya kuwa nchi yake Iran, itafikilia tena kushirikiana na shirika la kuchunguza nguvu za nyuklia duniani (IAE) International Atomic Energy.
Bwana, Ali Larijani ,alisema haya baada ya ripoti ya shirika hilo la IAE kutoa ripoti yake na kudai ya kuwa Iran haijashirikiana kikamilifu na shirika hilo.
Picha hapo juu ni picha ya bwana, Ali Larijani muda mfupi kabla ya kuchaguliwa kwake kuwa spika wa bunge la Iran.
Picha ya pili ni picha ya bwana Ali Larijani, enzi hizo alipokuwa akiongelea jinsi gani nchi yake Iran na swala la nyuklia mbele ya jopo la wataalamu wamaswala ya nyuklia mjini Viena.
Siasa yaingia kindumbwendubwe, waziri mkuu atakiwa ajiudhuru.
Jerusalem, Israel - Waziri wa ulinzi wa Israel, bwana Ehud Barak, amemtaka waziri mkuu wa sasa wa Israel bwana Ehud Olmert kujihudhuru kutoka serikalini kama waziri mkuu kufuatia kashfa za kupokea rushwa.
Waziri huyu wa ulinzi bwana Ehud Barak, alisema ya kuwa waziri mkuu bwana, Ehud Olmert hawezi kuongoza serikali kwani kashfa za rushwa zitakuwa zinamzonga kila wakati. Hata hivyo waziri Olmert, alisema ya kuwa pesa hizo zilitolewa kama kama mkopo kwakwe, na hivyo ikiwa atakutwa na makosa basi atajihuzuru.
Picha hapo juu ni picha ya waziri mkuu wa sasa wa Israel bwana Ehud Olmert.
Picha ya chini ni picha ya waziri wa ulinzi wa Israel bwana, Ehud barak, ambye anataka bwana Olmert kujihuzuru.
Amani ya Lebanon, "Uongozi mpya utaleta atulivu?" Siniora arudi ofisini.
Beiruti, Lebanon - Waziri mkuu wazamini wa Lebanon, bwana Fuad Siniora, ataendelea tena kuliongoza bunge la nchi hiyo.
Uteuzi huo, umefanywa na rais mpya wa Lebanon bwana, Michel Sleiman, na aliyekuwa kiongozi wa jeshi, bwana Michel Sleiman.
Hata hivyo kundi la Hezbollah, halikufurahishwa na uteuzi huo, lakini limesema yakuwa watashirikiana na serikali ya sasa, ili kuleta amani na utulivu nchini humo.
Bwana, Fuad Siniora, ambaye anapendelea serikali ya Lebanon, ishirikiane na nchi za Ulaya Magharibi.
Pichani hapo juu ni picha ya bwana, Fuad Siniora ambaye amechaguliwa kuliongoza serikali mpya la Lebanon.
Pichani hapo juu ni picha ya rais wa sasa wa Lebanon, bwana Michel Sleiman.
Japan kufuata mkondo wa China, "Afrika soko la marighafi kwa dunia".
Yokohama, Japan - Serikali ya Japan, imetangaza ya kuwa itatoa zaidi ya $ 4billion kwa nchi za Afrika, ili ziweze kujijenga kiuchumi na kijamii kwa kipindi cha miaka mitano itakayo fuata.
Akiongea haya kiongozi wa Japan, Yasuo Fukuda, alisema ya kuwa pesa hizo zitatolewa kwa njia ya mikopo yenye riba nafuu, ili kuinua maendeleo ya bara la Afrika.
Hata hivyo, viongozi wa Afrika, walionyesha sononeko lao kuhusu, bei za bidhaa za Afrika kukuso soko katika nchi za Magharibi, hata kukabiliana na vikwazo vya kibiashara ambavyo vimewekwa na nchi hizi za magharibi.
Picha hapo juu, ni picha ya bendera ya Japan, ambayo ina taka kuingia Afrika kibiashara, ili kushindana na nchi kama China, ambayo imejijenga kiuchumi na kibiashara na nchi zilizopo barani Afrika.
Picha ya chini ni picha za viongozi na marais wa Afrika, ambao wapo Japani katika mkutanao wa kibiashara na serikali ya Japan.
Rais Muammar Gaddafi, azishutumu nchi za magharibi" Wazamisha mashua na watu hupoteza maisha".
Tripol, Libya - Kiongozi na rais wa Libya,bwana Muammar Gaddafi , amelaani kitendo cha kuwazamisha kwa makusudi baharini, Waafrika ambao hutumia njia ya bahari kufika Ulaya.
Rasi Gaddafi, alisema hay hivi karibuni na kudai nchi za Ulaya zimekuwa zikifanya hivyo kwa makusudi, na hivyo vita dhidi ya Waafrika katika bahari ya Mediteranian ni kwaajili ya kujilinda na nchi za Ulaya zinafanya kila njia kuzuia watu Waafrika wasifike ulaya kwa kudai kuwa bashua zao zimezama.
Rais, Gaddafi, hakutaja ni nchi gani, wakati alipo kuwa akiongea na wakati wa mkutano wa kibiashara
Pichani hapo juu ni picha ya rais Muammar Gaddafi,ambaye ni rais wa Libya.

Thursday, May 22, 2008

Jeshi kupunguzwa hivi karibuni kutoka mstari wa mbele nchini Irak " Jemedari Mkuu"

Hatimaye ndoto ya kocha Alex Ferguson ya timia,"Man - United Bingwa wa Ulaya 2008-9".

Moscow, Urusi - Chini ya Kocha mkuu na mzoefu wa soka, timu ya Manchester United ya Uingereza, imeshinda tena na kulibeba kombe la vilabu bingwa vya Ulaya katika kindumbwendumbwe kilicho fanyika nchini Urusi ndani ya jiji la Moscow , kwenye uwanja wa Luzhniki , kati ya timu ya Manchester United na timu ya Chelsea FC, ambayo pia ni ya kutoka nchini Uingereza.
Ushindi huu,ulipatikana baaday ya dakika 90 kumalizika kwa goli 1 kwa 1, na hata dakika za nyongeza kutokuzalizasha goli, na hivyo kuamuliwa kwa kupiga gozi la ng'ombe mbele ya matuta kumi na mbili, na kamptaini wa timu ya Chelsea FC , John Terry, kupeperusha gozi la mwisho la tano,na hatimayake kwenda kwenye matuta ya ziada na ndipo,Nikolaus Arnelka mchezaji huyo, gozi lake kushindwa kuvuka tuta la manchester na kuishia mikononi mwa golikipa namba moja wa Holland na Manchester, Edwin van der Sar.Na ndoto ya Chelsea FC kuondoka mikono mitupu ndini ya uwanja wa Luzhniki.
Timu ya Man United ilibebe kombe la ubingwa wa Ulaya chini ya kocha Alex Ferguson mwaka, 1998-1999, na sasa 2008 - 2009.
Picha hapo juu anaonekan kocha mkuu wa Man United, bwana Alex Ferguson,akiwapungia wapenzi wa timu yake baada ya kunyakua kombe la ligi ya Uingereza hivi karibuni.
Picha ya pili anaonekana kocha Alex Ferguson, akinyanyua kombe la ubingwa wa Ulaya kwa mara ya pili.
Picha ya tatu wanaonekana wachezaji wa Man United, wakishangilia ubingwa wa kombe la Ulaya 2008-9 ndani ya jiji la Moscow.
Picha ya nne, ni kombe ambalo huwa linagombaniwa kila mwaka, msimu wa 2008-9 limebebwa na Man United.
Picha ya tano,anaonekana bila matumaini golikipa wa wa Man United, Edwin van der Sar, akiangalia mpira bila matumaini uliopigwa na na John Terry, lakini uligonga mlingiti wa goli na kuikosesha Chelsea FC ubingwa wa Ulaya msimi wa 2008-9.
Picha ya sita anaonekana, mchezaji na kaptain John Terry, akiwa amekaa chini,kwa uchungu uku amewshikilia mguu wake wa kushoto ambao uliteleza na kunfanya apeperushe penati ya ushindi dhidi ya timu ya Man United.
Picha ya mwisho, anaonekana mchezaji wa siku nyingi wa timu ya Man United Poul School, akiwa ameinama mkao wa kondoo anaye taka kupigana na kondoo mwenzake, lakini siyo hivyo bali inaonyesha ni jinsi gani mechi ya fainali kati ya timu yake Man United na Chelsea ilivyoi kuwa ngumu, kwana kukaa kwa kwa mtindo huu, siyo kupenda bali inaonyesha yakuwa ubingwa huu wa Ulaya wameufanyia kazi kubwa na hata damu zilimwagika.
Poul School aliumia baada ya kugongana na mcheza wa Chelsea na wa timu ya taifa ya Ufaransa, Claude Makelele wakati walipo ruka juu kuwania mpira.
Wapiganaji Tuereg na wanajeshi wa serilika wapigana nchini Mali " Tuereg kudai madaraka".
Bamako,Mali - Zaidi ya watu wasiopungua 32 wamepoteza maisha wakati wanajeshi wa wapiganaji kundi la Tuereg.
Mapambano hayo amboyo yapo kaskazini mashariki mwa nchi ya Mali, yalipoteza maisha ya wanajeshi 15 na wapiganaji 17.
Wapiganaji hawa wa kundi la Tuareg, alivamia moja ya kitua cha jeshi kilichopo kaskazinimashariki mwa nchi ya Mali na ndipo mapigano yalipo anza kati ya kundi la Taureg na jeshi la serikali.
Kundi hili ambalo linadai kutaka kujitawala kimadaraka katika eneo lao, limekuwa likipigana na jeshi kwa kipindi kilefu sasa
Picha hapo juu, nanaonekana rais wa Mali bwana Amadou Toure, ambaye anaonekana akikagua shamba moja nchini mali kuangali hali ya ukame ilivyo asili kilimo nchini humo.
Chini ni picha za wapiganaji wa Tuereg, ambao wanapingana na serikali ya Mali inayo ongozwa na rais Amadour Toure.
Jeshi kupungunzwa hivi karibuni kutoka mstari wa mbele nchini Irak" Jemedari Mkuu"
Washington, USA - Jemedari mkuu wa jeshi la Amerika nchini Irak , bwana David Petraeus amesema hivi karibuni ya kuwa kuna mpango wa kupunguza idadi ya wanajeshi waliopo nchini Irak.
Jemedar huyo,bwana David Petraeus, alisema haya mbele ya kamati ya huduma za jeshi, ingawaje hakutaja yakuwa ni idadi ya wanajeshi wangapi watapunguzwa kutoka mstari wa mbele nchini Irak.
Picha hapo juu, anaonekana Jemedari, David Petraeus, akiwa na wanajeshi wapiganaji nchini Irak hivi karibuni.
Chini ni picha ya Jemedari, David Petraeus, akinyanyuka baada ya kumaliza kuongea na kamati jeshi la Ulinzi la Amerika.
Je mazungumzo kati ya Israel na Siria, ni chanzo cha amani mashariki ya kati?
Ankara,Uturuki - Mazungumzo kati ya serikali ya Israel na Siria yamemalizika hivi karibuni, na kuonyesha matumaini ya kuleta amani katika eneo la mashariki ya kati.
Mazungumzo haya ambayo yamechukua karibu siku tatu, yamekuwa yakifanyika, chini ya mpatanishi kutoka Uturuki bwana Ali Babacan , ambaye ni waziri wa mambo ya nchi za nje ya Uturuki.
Kwa mujibu wa wachunguzi wa hali ya kiusalama na kisiasa kwenye maeneo ya mashariki ya kati, wamesema ya kuwa huu ni mwanzo, ijapo kuwa mazungumzo hay yalifanyika kupitia ngazi za chini za serikali hizi.
Hata hivyo, msimamizi wa mapatano haya bwana , Ali Babacan, waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uturuki, alisema ya kuwa mazungumzo haya ni chanzo cha kuleta matumaini ya amani kwenye maeneo haya ya mashariki ya kati.
Picha ya hapo juu ni picha ya rais wa Siria, bwana Bashar Assad.
Picha ya kati ni picha ya msimamizi wa mazungumzo ya bwana Ali Babacan, ambaye ni msimamizi wa mapatano kati ya Siria na Israel.

Monday, May 19, 2008

Wageni wakiona cha mtema kuni Afrika ya Kusini"Wamekuja kuchukua kazi zetu" Wadai wazawa.

Jela ya mkabili Willy Snipes," Sitarudia tena kosa kama hili" Snipes.

Florida, USA - Msanii maarufu na nyota ya kucheza sinema duniani, Willy Snipes, amehukumiwa kwenda jela hivi karibuni kwa muda wa miaka mitatu na mahakama ya Ocala, mjini Florida, kutokana na kosa la kukosa kulipa kodi ya mapato katika kipindi cha miaka ya 1999 hadi 2001.
Akitoa hukumu hii, jaji William Terrel Hodges, nimuhimu kutoa hukumu kama hii , kuonyesha ya kuwa siyo vizuri kutolipa kodi ya mapatato kwa serikali, na akaagiza ya kuwa maasifa wa jela atakayo tumikia kifungu wampe taarifa ni lini ataanza kutumikia kifungo chake.
Hata hivyo Willy Snipe, yupo nje kwa dhamana hadi hapo rufani yake itakapo sikilizwa tena. Willy Snipes, alisema alikuwa anasikitika sana kwa kosa hili na ya kuwa hatarudi tena kosa kama hili.
Hata hivyo, mwana sheria mtetezi wa Willy Snipes , alisema ya kuwa , mteja wake anadaiwa kiasi kisicho pungua US dollal 400,000, na kwa kesi hiyo hastahili kutumika kifungo cha jela.
Navilevile wanasheria huyo aliendelea kwa kuongeza ya kuwa kuna baadhi ya wasanii na wacheza sinema,mfano , Marc Anthony na Meya wa jiji la Washington Mario Barry waliachiwa kwa kosa la kukwepa kulipa kodi ya mapato , na vilevile mwana musiki, Willie Nelson, aliachiwa huru kwa kosa kama hilo lakutokulipa kodi ya mapato ya thamani ya US dollal 17 million.
Picha hapo juu anaonekana, Willy Snipes akiwa na mcheza sinema mwingine Ving Rhames, wakati wa kicheza sinema ijulikanayo kama Mirax's Undisputeed.
Picha ya kati anaonekana Willy Snipes, akiwapungia wapenzi wake walio kuja kusikiliza kesi yake, na kupewa hukumo ya kukaa jela miaka mitatu.
Picha ya mwisho, anaonekana, Willy Snipes, akiwa ameinama na kufikilia nini la kufanya hapo baadaye.
Hali hii ni kawaida nchini Somalia," Maisha halisi mjini Mogadishu".
Nairobi, Kenya - Mazungumzo kati ya wawakilishi wa serikali ya Somalia, kikundi kikubwa kinacho pingana na serikali ya Mogadishu na kinacho julikana kama Alliance for the Re liberation of Somali (ARS) yanaendela nchini Kenya, huku baadhi ya viongozi wa ARS, wakisema ya kuwa mazungumzo haya hayataleta ufumbuzi wowote.
Mmoja wa viongozi hawa, alisema, itakuwa ni vigumu kufika muafaka,hadi hapo wanajeshi wa Ethiopia watakapo angamizwa ama kujitoa wenyewe nchini Somali. Machafuko na mapigano ya vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini , Somali yamechukua miaka mingi sasa zaidimya miongo miwili.
Pichani hapo juu ni picha ya mmoja ya wapiganaji wa jeshi la Serikali, akiburutwa mitaani na anaonekana mwana dada akipiga picha ya mpiganaji huyu, kwa kutumia simu yake ya mkononi.
Picha chini pi picha ya moja ya magari ya jeshi la serikali na mshirika wake Ethiopia, likipiga doria mjini Mogadishu hivi karibuni.
Tbilisi na Moscow, hali ya uhusiano wa kijirani wao ni tete.
Moscow, Urusi - Serikali ya Urusi , imesema hivi karibuni imemkamata mmoja wa wapelelezi kutoka nchini Georgia, ambaye inasemekana anahusika na kuleta mtafaruku katika eneo hilo.
Kutokana na habari zilizo patikana kutoka kwa shirika la habari na wakala wake FSB , zimesema ya kuwa usalama wa taifa wa Urussi, wamemkamata raia mmoja wa Georgia, ambaye alikuwa akiishi kusini mwa Urusi kwenye jimbo la Checheyna, inadaiwa raia huyu alikuwa mmoja wa wapiganaji walio pata mavunzo ya kijeshi.
Hata hivvyo, serikali ya Georgia ilikanusha madai haya, na kudai madai haya ya Urusi ni ya kuleta huasama na Tbilisi
Tsvangirai asitisha safari ya kurudi nyumbani, "MDC ya dai kuna njama ya mauaji".
Harare, Zimbabwe - Chama (MDC) Movemet Democratic Change, kinacho ongozwa na Morgan Tsvagirai, kimedai yakuwa kimepata habari nyeti ya kuwa mwenyekiti wa chama hicho, bwana, Tsvangarai maisha yake yapo hatarini pindipo atakapo rudi nchini Zimbabwe kuanza kampeni ya kugombania kinyang'anyiro cha urais dhidi ya rais wa sasa wa Zimbabwe , bwana Robert Mugabe.
Bwana Morgan Tsvangirai, alitakiwa kurudi siku ya jumamosi nchini Zimbabwe, lakini ilibidi asimamishe safari hiyo, baada ya chama chake MDC, kusema ya kuwa kuna njama za kutaka kumuua, kwa kutumia mashushu.
Bwana, Morgan Tsvangirai ambaye yupo nchin Afrika ya kusini kwa sasa,hakuweza kuhudhulia moja ya vikao vya kampeni ya uchaguzi unao fuata hivi karibuni.
Marudiano hayo ya duru la uchaguzi, yanatarajiwa kufanyaika mezi wa sita - juni 27
Pichani hapo ni picha ya rais wa sasa wa Zimbabwe, bwana Robert Mugabe, ambaye atagombea kwa mara nyingine kuiongoza Zimbabwe.
Picha ya chini, ni picha ya bwana Morgan Tsvangirai, ambaye alishinda duru ya kwanza ya uchaguzi, lakino hakufika kiwango kinachotakiwa kuwa raisi wa nchi hii Zimbabwe.
Viongozi wa wapiganaji wa JEM, wa Sudani wafukuzwa nchini Misri.
Kairo, Misri - Serikali ya Misri hivi karibuni, imewafukuza nchini humo viongozi wa chama cha upinzani wa chama JEM (Justice and Equality Movoment) cha Sudani Darfur.
Hata hivyo serikalai ya Misri haikutoa sababu gani zimewafanya wawa fukuze viongozi hawa na wapiganaji wa JEM
Viongozi hawa na wapiganaji bwana Ahmed Tugd , Ahmed Sharif na Mohmed Ali, walikamatwa hivi karibuni na kutakiwa kuondoka nchini humo.
Picha hapo juu, ni picha ya bendera ya Misri.
Wageni wakiona cha mtemakuni Afrika ya Kusini,"Wamekuja kuchukua kazi zetu" Wadai wazawa.
Johannesburg, Afrikia ya Kusini - Zaidi ya wahamiji wasio pungua 20, wamepoteza maisha yao hivi karibuni nchini Afrika ya Kusini, kutokana vurugu na machafuko yanayo endelea kati ya wanchi wazawa wa Afrika ya Kusini na wageni walio amia.
Vurugu hizi zimeanza kutokana na mtazamo wa wazawa wa Afrika ya Kusini ya kuwa hawa wahamiaji wanakuja kuchukua kazi zao.
Watu ambao wamekubwa na mikasa hii, ni hasa wananchi wanaotokea nchi za
Zimbabwe,Mozambiki, Malawi, na Zambia.
Raia mmoja wa Malawi, alisema ya kuwa amepoteza mali zake zote, alizofanyia kazi kwa kipindi kirefu na sasa hana kitu tena, na hajui atafanya nini ili kuweza kumudu maisha yake ya baadaye, na akadai yakuwa wazawa hawa walikuwa wakisema hawa makwerekwere, lazima waondoke warudi kwao,alimalizia raia huyu wa Malawi.
Kutokana na mikasa hii, wahamiaji wengi, wamekuwa wa kikimbilia katika vituo vya polisi ili kuokoa maisha yao, na wengine kukimbia kwa wasamalia wema.
Pichani anaonekana mmoja wa wazawa wa Afrika ya Kusini, akiwa ameshikilia bakora, tayari kufanya vitu vyake kwa wageni, huku moto ukiwa unawaka kwenye taveni au ( kioski), na inasadikiwa ya kuwa taveni hii na mali zilizopo ni mali ya mmoja wa wageni hawa.
Mume wa marehemu Bhuto, afutiwa kesi na mahakama," Kesi haikuwa na ushaidi kamili"Hakimu.
Islmabad, Pakistan - Mahakama ya nchini Pakistan, imetupilia mbali kesi iliyokuwa inamkabili ya mwenyekiti wa chama PPP ( Pakistan People's Part) bwana Asif Ali Zardari.
Mwenyekiti huyu bwana, Asif Ali Zardari, alikuwa akikabiliwa na kesi ya kuhusika na uingizaji wa madawa ya kulevya au (Mihadarati).
Kesi hii ambayo imechukua zaidi ya miaka mingi, akisema haya, jaji Ejaz Hussain Awan, alisema yakuwa kesi hii akuwa na ushaidi kamili.
Pichani hapo juu, ni picha ya bwana Asif Ali Zardari, akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.

Monday, May 12, 2008

Tetemeko la ardhi la sababisha vifo na maafa makubwa nchini China.

Alex Ferguson,anyakua ubingwa kwa mara ya 10, Giggs avunja rekodi.

Manchestar, Uingereza - Timu ya mpira wa miguu ya Uingereza Manchester United , imenyakua ubingwa wa Uingereza kwa mara nyingine tena.
Chini ya uongozi na kocha mkuu, bwana Alex Ferguson, timu hiyo imeweza kunyakuwa kikombe hiki mara 10.
Wakati huo huo , mchezaji nyota na mahili wa mchezo wa soka, katita timu ya Manchester Unaited , Ryan Giggs, amesawazisha rekodi ya ufungaji wa magoli 758, katika timu hii, ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Bobby Charton.
Giggs alifunga goli la kusawazisha rekodi ya Bobby Charton na goli hilo lili hakisha ubingwa kwa timu ya Mancheter United wa msimu wa 2008-2009.
Ryan Giggs ni moja ya mchezaji wa muda mrefu wa timu ya Manchester United tangu enzi ya miaka ya mwanzo ya 90.
Picha hapo juu, anaonekana, kocha mkuu wa Manchester United, bwana Alex Ferguson,akinyanyua kombe la ubinga wa ligi ya Uingereza kwa mara ya kumi.
Picha ya kati ni mchezaji, Ryan Giggs,akinyanyua kombe kwa mara nyingine chini ya uopngozi wa kocha wake wa muda mrefu,Alex Ferguson, baada ya kufunga goli lililo wazamisha matumaini Wigan Atlet ya kuwa waweza kuwasimamisha Man United.
Picha ya chini , ni picha za mcheza Ryan Giggs, akiwa anaonyesha vitu vyake kwa mbinu tofauti za kutikisa nyavu na kuchezea kabumbu.
Familia ya rais Bush, yawa mfano bora kwa jamii, mtoto wao afunga pingu zamaisha.
Texas, USA - Famili ya rais wa Amerika bwana George Bush, siku ya tarehe 10/05/2008, walikuwa na furaha isiyo kifani , baada ya kushuhudia mtotao wa wa kike Jenna Bush akifunga pingu za maisha ya rafiki yake wa muda mrefu bwana Henry Hager.
Harusi hiyo iliyo fanyika mjini Texas, iliudhuriwa na watu wapatao 200,wakiwemo wazazi wa pande zote mbili, familia ya rais, George Bush na familia ya bwana, John Hager.
Picha hapo juu ni picha ya bi Jenna Bush akisema kwa bwana Henry Hager ya kuwa mimi sasa ni wako wa milele, na huku bwana Henry, anaonekana akisema bi Jenna, sasa wewe ni wangu wakufa nakuzikana, na kati yao ni mchungaji, Kirbyjon Caldwell, anashuhudi hayo waili hawa kuwa kitu kimoja.
Picha ya kati wanaoneka Bi Jenna na bwana Henry Hager, wakiwa kitu kimoja baada ya harusi yao.
Chini pichani, anaonekana baba mzazi wa Jenna, rais George Bush,akiwa na tabasamu la furaha huku amenshikilia malaika(mtoto) wake Jenna, kwani kazi nzuri walioifanya ya kumlea kwa maadili mema mtoto wa Jenna, na sasa anaenda anza maisha yake na mume wake bwana Henry.
Hatutafanya jambo lolote la kumpa nguvu rais "Nawaz Sharif".
Islamabad, Pakistan - Mgogoro wa kisiasa nchini Pakistani huenda ukaanza tena baada ya aliyekuwa waziri mkuu wa zamani wa nchi hiyo, bwana Nawaz Sharif, kutangaza ya kuwa chama chake kitajitoa serikalini kutokana na kucheleweshwa kwa kurudishwa kazini aliye kuwa jaji mkuu wa Pakistani aliye simamishwa kazi na rais Pevez Musharaf, mapema mwaka jana.
hata hivyo wachunguzi wa maswala ya kisiasa ya Pakistan, wanasema ya kuwa mwana Zardari, ananagalia kwa makini swala hili kwani,hapendi hili swala likaja likaleta mgongano wa kisisa tena.
Hata hivyo , bwana Sharif , alisema ya kuwa chama chake hakitafanya aina yoyote ya vitendo ambavyo vitamwongezea nguvu rais Musharaf,
Picha hapo juu ni picha ya bwana,Nawaz Sharif akiwapunguia mikono wanachama wenzake wakati wakampeni uchaguni uliopita.
Chini ni picha ya pamoja kati ya bwana Sharif na bwana Zardari, wakiwa pamoja hapo mwanzoni, na sasa wanapishana katika kumaamuzi ya kisiasa.
Tetemeko la ardhi la sababisha vifo na maafa makubwa, nchini China.
Beijing, China - Inasadikiwa zaidi ya watu wapatao 5000, wameuwawa kutokana na tetemeko la ardhi, lili tokea kusini mashariki mwa China.
Tetemeko hilo lenye nguvu za 7,8, lilitoke katika mji wa Chengdu uliopo umbali wa km 92 kutoka makao makuu ya jimbo la Sichuan
Hata hivyo huenda idadi ya vifo vikaongezeka kutokana na maafa haya ya liyo letwa na tetemeko hili,hii ni kwa mujibu wa msemaji wa serikali.
Kwa mujibu wa wanasayasi tetemeko hilo lilitoke muda wa saa (1448) kwa masaa ya China siku leo ya jumatatu.
Ili mkukabiliana na hali hii serikali ya China, imetoa misaada na jeshi ili kuwasaidia wananchi walopatwa na janga hili.
Picha juu wanaonekana baadhi ya watu wakiwasaidia majerui walio umia kutoka na tetemeko hili la ardhi.
Chini pichani wanaonekana baadhi ya wananchi wakiwa hawana na kufanya, wakiangalia njinsi gani tetemeko lilivyo haribu na kuteketeza mali na makazi yao.
Korea ya kusini kuanza kuonyesha ushirikiano"msemaji wa serikali".
Washington, USA - Serikali ya Amerika , imesema ya kuwa, serikali ya Korea ya Kaskazini, imekabidhi nyaraka zilizo na maelezo kuhusu hali ya kinyuklia ya Kora ya Kaskazini.
Akisema haya , msemaji wa serikali ya Amerika, alisema ya kuwa hii ndiyo mwanzo wa kuonyesha ya kuwa serikali ya Pyongyang, inaanza kuonyesha ushirikiano na kuweka uwazi kuhusu hali ya kinyuklia ya nchi hiyo.
Picha hapo juu ni bendera ya Korea ya Kaskazini,nchi hii ya korea imekuwa na uhasama mkubwa na Amerika kwa kipindi kilefu tangu kumalizika kwa vita ya Korea miaka ya hamsini
Picha ya kati ni jeshi la Kora ya Kaskazini, likiwa linakula kwata,mbele ya viongozi wa seriikalimwakati wa kuadhimisha shererhe za kitaifa nchini humo.
Picha ya chini wanaonekana wawakilishi wa serikali ya Amerika, wakiwa wameshikilia, masanduku yenye nyaraka za maelezo kuhusu hali ya nguvu za kinyuklia, tayari kuzipeleka Amerika kwa uchunguzi zaidi.
Hali ya kisiasa katika Afrika, Uchaguzi wa Swazland mashakani"Wapinzani".
Mbabane, Swazland - Wakati matayarisho ya uchaguzi wa kuchagua wabunge nchini Swazland,
yapo njiani, kunauwezakano mkubwa wa uchaguzi huo kususiwa na baadhiya viongozi wa siasa nchini humo hapo muda wa uchaguzi utakapo fikia mwezi wa Septemba.
Swazland ni nchi pekee katika Afrika, ambayo Ufalme ni moja ya nguzo muhimu katika seriakali.
Kwa mjibu wa msemaji mmoja wa mambo ya kisiasa nchini Swazland, prof Quambukusa Magagula,alisema ya kuwa mfumo wa siasa nchini Swazland, ahurusu mfumu wa vyama vingi vya kisisa kwa madai mfumo huu unaleta badhi ya matatizo katika jamii. Hapo juu ni picha ya bendera ya Swazland, nchi pekee katika Afrika yenye Mfalme anaye ongozo changia katika kuongoza nchi.
Chini ni picha ya Mfalme Muswati III, akiwa amevalia mavazi ya kijeshi na kutoa heshima(Salute) kwa wanajeshi walipopita mbele yake wakati wa sherehe za kitaifa nchini Swazland hivi karibuni.
Picha ya chini kapisa, anaonekana Mfalme Muswati III, akiwa amesimama tayari kuwapokea mashujaa wa Kiswaz, wakati wa sherehe za kimila, ambazo hufanyaka kila mwaka nchi Swazland.
Afrika kukumbwa na njaa,Benki ya Maendeleo ya Afriaka yaonya.
Maputo, Mozambiki - Benki ya Maendeleo katika Afrika, imeonya ya kuwa hali huenda ikawa mbaya zaidi kwa upande wa lishe, baada ya kupanda kwa bei ya vyakula zaidi ya mara mbili.
Benki ya Maendelo ya Afrika katika ripoti yake aliyo tolewa kabla ya kuanza kikao hicho mjini Maputo,ilisema yakuwa hii ina tokana na uduni wa kimaendeleo ulizo nazo nchi nyingi za bara la Afrika.
Na kuagiza ni lazima hatua za haraka zichukuliwe mapema kabla hali haijawa mbaya zaidi.
Kikao hiki ambacho kitafanyika mijini Maputo, kwa muda wa siku mbili, kiligusia vile vile upandaji wa mafuta ya kundeshea mitambo na mgari, ni sababu moja wapo ya bei ya vyakula kupanda mara dufu.
Picha hapo juu ni picha ya zao la ndizi,zao ambalo muhimu saana katika lishe barani Afrika.
Picha nyingine hapo chini, ni picha ya shamba la mahindi, zao hili limekuwa likipata shida kuku,hasa kutokana na ukosefu wa mvua,na zao hili ndiyo chakula kikubwa katika nchi nyngi za Afrika.