Sunday, July 31, 2011

Rwanda nchi ya kwanza duniani kuwa na wabunge wengi wanawake.

Rwanda nchi ya kwanza duniani kuwa na wabunge wengi wanawake.
Kigali, Rwanda - 31/07/2011. Nchi ya Rwanda imekuwa nchi ya kwanza duniani kwa kuwa na wabunge wanawake katika bunge la nchi hiyo.
Bunge hili lenye ambalo lina viti 80 na 45 kati ya viti hivyo vinashikiliwa na wanawake.
Rwanda nchi ambayo mwaka 1994 ilikumbwa na mauaji wa kikabila, imekuwa ikichukuliwa kama mfano bora kwa kujaribu kuwapa wanawake nafasi sawa na wamume katika kujenga uchumi wa nchi hiyo.
Viongozi wa zamani wa Tanzania waonya mvurugano bungeni.
Dar es Salaam, Tanzania - 31/07/2011. Viongozi wastaafu wa serikali ya Tanzania wamelilaumu bunge lilipo katika kipindi hiki ya kuwa halifanyi kazi inayo takiwa kama bunge.
Viongozi hao Joseph .S. Warioba na Salim .A. Salim, ambao walishawahi kuwa mawaziri wakuu wakati wa utalwala wa aliyekuwa rais wa kwanza wa Tanzania hayati Mwalimu Julias K Nyerere kwa pamoja walisema, " bunge la sasa hivi lililopo bungeni halifanyi kazi yake na limekosa mwelekeo wa kutetea wananchi na kupanga malengo ya kujenga na kuinua uchumi wa nchi, lakini matokeo yake wabunge wote wanaaangalia maslahi yao ya kisiasa na vyama vyao. Na ule utaifa, uzalendo wa kupenda, kulinda na kujenga nchi umekwisha kwa viongozi wetu walipo madarakani na wanchi kukusa imani.
Viongozi hao pia walitaka tabia hiyo ikome, kwani kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi siyo mwanzo wa kureta fujo na kuondoa amani, bali watumie mfumo huu kuuimarisha umoja na kujenga nchi japo wanatofautiana kiitikadi, kwa kuzingatia nchi hiyo ipo katika hali isiyo nzuri kwa kukosa umeme na kupanda kwa hali ya maisha.
Na walisitiza kuwepo na mwamko mpya wa uzalendo na utaifa ambao rais wa kwanza wa nchi hiyo hayati Julias K Nyererer aliujengea misingi bora.
Maonyo ya viongozi hao yamekuja baada ya bunge la nchi hiyo kuwa na vurugu kati ya wabunge wa vyama vya upinzani na wabunge wa chama tawala katika miswaaada mbalimbali inayoletwa bungeni humo.
Namibia yagundua kuwepo na mafuta nchini humo.
Windhook,
Namibia - 31/07/2011. Serikali ya Namibia imetangaza hivi karibuni ya kuwa imegundua kuwepo kwa mafuta kwenye eneo lililopo Kusini mwa pwani ya nchi hiyo.
Waziri wa nishati na madini Isak Katali alisema " kugunduliwa kwa mafuta hayo ambayo yatakapo anza kuchimbwa yatasaidia kuinua uchumi wa Namibia na maisha ya watu wote kwa ujumla."
Kunaaaminika ya kuwa kuna zaidi ya magalloni billioni 13 ambayo yataifanya Namibia kuwa nchi ya tano katika uchimbaji wa mafuta katika bara la Afrika baada ya zile za Libya, Nigeria, Algeria na Angola.

Umoja wa Afrika watoa tahadhali za mashambulizi zidi ya Al-Shabab.

Umoja wa Afrika watoa tahadhali za mashambulizi zidi ya Al-Shabab.
Mogadishu,
Somalia - 31/07/2011. Kamati ya usalama ya umoja wa Afrika umetangaza ya kuwa kundi la Al-Shabab linalo pingana na serikali ya Somalia lina panga kufanya mashambulizi wakati wa mwezi mtukufu wa mwezi wa Ramadhani.
Habari kutoka kamati hiyo zinasema " kundi la Al-Shabab limepanga kufanya mashambulizi wakati wa mwezi wa Ramadhani baada ya kupata siriha kutoka kwa kundi washiriki lililopo nchini Yameni."
Vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Somalia vimekuwa vikileta matatizo kwa wanchi wa Somalia na hata nchi ambazo zimepakana na nchi hiyo.
Hata hivyo serikali ya Somalia imekuwa ikipambana na kundi hilo ambalo lina sababisha kuwepo kwa ugumu kwa mashirika ya kimataifa yanayo toa misaada ya vyakula nchini Somali kushindwa kusambaza chakula katika maeneo ambayo yamekumbwa na ukame nchini humo.

Friday, July 29, 2011

Rubani alaumiwa kwa kusababisha ajali ndege

Rubani alaumiwa kwa kusababisha ajali ndege.
Paris, Ufaransa - 29/07/2011.Rubani aliyekuwa akirusha ndege ya shirika la Ufaransa amelaumiwa kwa kusababisha kuanguka kwa ndege iliyopoteza maisha ya watu 228.
Ndege hiyo ambayo ilianguka wakati ilipokuwa ikifanya safari zake za kaiwada kueleka Ufaransa iliaangu kutoka umbali wa mita 40,000 na kutumbukia katika bahari ya Atlantiki mwaka 2009.
Ripoti ilitolewa baada ya kufanyika kwa uchunguzi na BEA inasema " rubani hakuwa amepata mafunzo mazuri ya kurusha ndege hasa kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.
Kuafuatia ripoti hiyo, shirika la ndege la Ufaransa limehaidi kuongeza mafunzo zaidi ya rubani wake ili kuepuka ajali kama hiyo kutokea tena.
Kiiongozi wa kundi la kijeshi la upinzani nchini Libya auwawa.
Benghazi,
Libya - 29/07/2011. Mkuu wa majeshi ya upinzani yanayo mpinga Muammar Gaddafi ameuwawa kwa kupigwa risasi yeye pamoja wasaidizi wake wawili.
Abdel Fattah Younes, ambaye alikuwa mmoja wa wanajeshi waliongoza mapinduzi ambayo yalimweka madarakani Muammar Maddafi 1969, na baadaye kuongoza kama waziri wa mambo ndani hadi hapo alipo jitoa kutoka kwenye serikali ya Muamar Gaddafi na kujiunga na kundi linalo mpinga lenye makao yake makuu Benghazi.
Hata hivyo kifo chake bado kinaleta utata na huenda kikaleta mvutano ndani ya kundi hilo la upinzani.

Thursday, July 28, 2011

Muungano wa mashoga watambulika na umoja wa mataifa.

Serikali ya Eritria yakabiliwa na shutuma.
Addis Abeba, Ethiopia-28/07/2011. Serikali ya Eritria imeshutumiwa kwa kutaka kushambualia kikao cha viongozi wakuu wa Afrika kilicho fanyika mapema mwanzoni mwa mwaka huu.
Kwa mujibu wa habari hizo zinasema, " serikali ya Eritria kwa kushirikiana na vikundi vya kigaidi walipanga kuulipua mkutano huo pamoja na sehemu muhimu za jiji la Adis Abeba."
Hata hivyo serikali ya Eritria ilikataa na kusema "haina ushirikiano wowote na makundi ya kigaidi na kudai ya kuwa hiyo ni mbinu za kutaka kuichafua serikali Eritria ," kwani serikali ya Ethiopia ndiyo iliyo ahidi kwa kupitaia waziri wake mkuu ya kuwa itavisadia vikundi vinavyo pingana na serikali ya Eritria."Habari kutoka ofisi ya mambo ya nje ya Erirtia zilisisitiza.
Muungano wa mashoga watambulika na umoja wa mataifa.
New York,
Marekani- 28/07/2011. Umoja wa mataifa umetangaza kutambu muungano wawakilisha mashoga na wale wote ambao wanapendelea kufanya mapenzi kwa watu wa jinsia moja.
Habari kutoka shirika la kutetea haki za binadamu limesema " uamuzi huo wa umoja wa mataifa ni mzuri kwani unaonyesha ni jinsi gani jumuia ya kimataifa inaamini binadamu wote wanaihitaji kupewa haki sawa."
Uamuzi huo wa kutambulika kimataifa kwa muungano wa wawakilishi wa mashoga umekuja wakati bado nchi nyingi hasa Afrika hazitambui haki za mashoga hao.

Wednesday, July 27, 2011

Serikali ya Uingereza yaitambua rasmi baraza la mpito la waasi nchini Libya.

Serikali ya Uingereza yaitambua rasmi baraza la mpito la waasi nchini Libya.
London, Uingereza -27/07/2011. Serikali ya Uingereza imefunga ofisi zote za ubalozi wa serikali ya Libya na kuwafukuza wafanyakazi wote ambao wanawakilisha serikali ya Muammar Gaddafi.
Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza William Hague aliyasema hayo wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kwa kusema " kuanzia sasa hatuta itambua serikali ya Muammar Gaddafi na uhusiano uliopo wa kidiplomasia na serikali yake tumeufuta."
William Hague aliongezea kwa kusema " tunalitambua rasmi kundi la Walibya wanaoongoza serikali ya mpito kama wawakilishi wa wa Walibya na tutashirikiano nao kikamilifu."
Kufuatia kuvunjika uhusiano wa kidiplomasia serikali ya Uingereza na ya Muammar Gaddafi, serikali ya Uingereza itazifilisi mali zote za serikali ya Libya na kutumika katika kulisaidia kundi linalo pingana na serikali ya Gaddafi.
Wakati huo huo, serikali ya Libya imesema haitafanya mazungumzo yoyote mpaka hapo NATO itakaposimamisha mashambuliz yake nchini humo.
Rais wa zamani wa Misri agoma kula.
Kairo, Misri - 27/07/2011. Aliyekuwa rais wa Misri , amekuwa na matatizo ya kiafya na anakataa kula, wakati kesi zidi yake ikiwa inatayarishwa ili kujibu mashitaka ya kutoa ruhusa kwa polisi kuwauwa na kuwajeruhi waandamanaji waliokuwa kipinga serikali yake mapema mwanzoni mwa mwaka huu.
Kwa mujibu wa habari zinasema " Hosni Mubara anakunywa maji na mwili wake umeanza kukonda na uzito kupungua.
Hosni Mubaraka ambaye ameitawala Misri kwa muda wa miaka 29 kabla ya kutolewa madarakani kwa nguvu za maandamano ya wananchi yaliyo tokea mapema mwaka huu ambapo baadhi ya watu walipoteza maiasha wengine kuumia na maafafa makubwa ya kijamii kutokea.
NATO yaingia kutatua mzozo kati ya Wakosovo na Waserbia.
Brussels,
Ubeligiji - 27/07/2011. Jeshi la nchi za magharibi la NATO limeamua kuingilia kati kutatua mgogoro uliotokea wakugombania mpaka kati ya Wakosovo na Waserbia.
Uamuzi huo wa NATO umekuja baada ya serikali ya Wakosovo kuwekea vikwazo bidhaa zote za Waserbia kupitia nchi humo jambo ambalo limesababisha serikali ya Serbia kutokubaliana nalo.
Jumuiya ya Ulaya imelaani kitendo hicho na kuzitaka pande zote kukaa kwenye meza ya mazungumzo na kulimaliza tatizo hilo mara moja.

Tuesday, July 26, 2011

Baraka Obama awasihii viongozi wenzake kukubalia

Baraka Obama awasihii viongozi wenzake kukubaliana.
Washington, Marekani - 26/07/2011. Rais wa Marekani amelitangazia taifa na kuonya ya kuwa kama hakutawa na makubaliano itahatarisha uchumi na maisha ya jamii kwa ujumla.
Rais Baraka Obama alisema " hali hii siyo nzuri kwa kuendelea kulumbana kwani hakutasaidia na matokeo yake yatalitia taifala Mareani katika hatari ya kuporomoka kiuchumi na maisha ya wanchi wa Marekani, kwani hali hii haijawahi kutokea hadi kulipelekea taifa kufikia hali hii."
Rais Obama alihutubia taifa baada ya kutofikia makubaliano kati ya chama chake cha demokrasi kilichopo madarakani na chama cha wapinzani cha repablikani ambacho inapinga miswada ya ambayo inatolewa na serikali.
Umoja wa mataifa waongeza nguvu kupambana na baa la njaa.
Rome
, Itali -26/07/2011. Shirika lainalo shughulikia maswala ya chakula duniani , limepitisha mswaada wa kuanza kusambaza chakula kwa kutumia usafiri wa ndege kati nchi ambazo zimekumbwa na ukama katika eneo la Afrika ya Mashariki.
Habari zinasema " kazi hiyo ya kuanza kusambaza chakula katika maeeneoa hayo itaanza mapema hivi karibuni ili kukabili baaa hilo la njaa na kwa kuzingatia watoto ndiyo walioathirika kwa kiasi kikubwa." Lilisema shirika hilo.
Uamuzi huo umekuja baada ya mkutano uliofanyika nchi Itali ambao ulikuwa na mazumuni ya kupanga mbinu za kupambana na baaa hilo.
Nchi ambazo zinakabiliwa na baaa hilo ni Djibouti, Ethiopia, Kenya, Somalia, Sudan na Uganda.

Sunday, July 24, 2011

Mshitakiwa wa mauaji ya Norway atubu kwa madai.

Mshitakiwa wa mauaji ya Norway atubu kwa madai.
Oslo,
Norway -24/07/2011. Mshitakiwa ambaye anashikiliwa na polisi kwa makosa ya kuhusika na mauaji kwa kuwapiga sirasi zaidi ya watu 90 na wengine kupoteza maisha kutokana na tukio hilo,anataraijwa kufikishwa mahakani ili kujibu mashitaka zidi yake.
Anders Breivik, ambaye amekubali kuhusika na mauaji hayo ametoa maelezo kupitia mwanasheria wake kwa kusema " nimeamua kufanya jambo hili ili kuleta mageuzi katika jamii ya nzima ya wanachi wa Norway."
Mshitakiwa huo ambaye inaaminika ni mkristu mwenye imani kali na ni mwanchama wa kundi la watu wenye itikadi kali ambao wanapinga kuwepo kwa wageni nchini humo na hasa wale ambao ni waumini wa dini ya Kislaamu na pia inasemekana alisema alikuwa amepanga kufanya kitendo hicho cha mauaji kwa toka siku za nyumu.
Wakati huo huo maelfu ya Wanorway wafanya misa na ibada za maombelezi kuwaombea wale wote walifariki kutokana na mauaji ya mlipuko wa mabomu na mauaji ya kupigwarisasi yaliyo tokea nchini humo.

Saturday, July 23, 2011

Wanorway wapatwa mistuko na mauaji ya mabomu na ya risasi.

Wanorway wapatwa mistuko na mauaji ya mabomu na ya risasi.
Aslo, Norway-23/07/2011. Wanachi wa Norway bado wapo katika mshituko mkubwa baada ya milipuko ya mabomu na mtu mmoja aliyeva nguo za polisi kuwaua watu waliokuwepo katika kisiwa cha Utoya nchi humo.
Mauaji hao ambayo yametokea kwa kufuatana, mabomu yalisababisha mauaji ya watu 7 na katika kisiwa cha Utoya watu zaidi ya 84 waliuwawa na wengine kujeruhiwa vibaya na mtu huyo aliyevaaa kama askari polisi wakati wakiudhulia mkutano wa umoja wa vijana wa chama cha Labour.
Polisi wamemkamata mtu mmoja raia wa Norway Anders Berring Breivik 32 kwa mahijiano zaidi kufuatia matukio hao.
Viongozi wa serikali tofauti duniani wametuma salamu za rambirambi kwa serikali ya Norway kufuatia mauaji hayo ya kutisha yaliyo wakuta wanchi wa Norway.
Muammar Gaddafi bado mthiani kwa wapinzani na NATO.
Tripoli, Libya -23/07/2011. Milipuko mikubwa ya mabomu imesikika katika jiji la Tripoli huku mamia wakiakiandamana kumuunga mkono Muammar Gaddafi.
Mamia ya waandamanaji walikusanyika mbele ya bendera kubwa yanye picha ya kiongozi huo na kusema wanamuunga mkono mpaka mwisho.
Kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya Libya zinasema " mabomu hayo yalishambulia maeno ya hotel za kitalii."
Wakati huo, kundi la upinzani linalo mpinga Muammar Gaddafi linamsema " tumefanikiwa kumkamata mmoja wa viongozi wa kijeshi generali Abdul Nabi Zayed ambaye ni mafaniko makubwa kwetu kwani alikuwa mmoja ya viongozi ambao walikuwa nawapanga mbinu za kimashambulizi zidi yetu, na vilevile tunakaribia kuukamata mji wa Zliten na pia baadhi ya wapiganaji wetu wameweza kuingia ndani ya jiji la Tripol."
Mapigano yanayo endela kati ya wapinzani wa Gaddafi na serikali yake yamesha chukua zaidi ya miezi mitatu na kusababisha maafa makubwa kijamii na kimazingira.
Mashambulizi ya jeshi la NATO yamekuwa yakifanyika ili kumlazimisha Muammar Gaddafi aachie madaraka.
Wapalestina wahaidi kudai utaifa wao Septemba mwaka huu.
Istambul. Uturuki - 23/07/2011. Rais wa serikali ya Wapalestina ameliambia baraza la washiriki walioshirikia katika mkutano uliofanyika nchini Uturuki ya kuwa serikali yake imeamua na kuongoza nia ya Wapalestina kutaka kutambulika kama taifa huru ifikapo mwezi Septemba.
Rais Mahmoud Abbas alisema " tunaenda umoja wa mataifa kudai haki ya kuwa taifa huru baada ya serikali ya Izrael kutulazimisha kufanya hivyo kwa kuendelea na kitendo cha kujenga makazi katika eneo letu."
Na tumekutana ili kuandaa mikakati kamili ya kudai haki zetu katika baraza kuu la umoja wa mataifa." Alisema raia Abbas.
Mgogoro wa Wapalestina na Waizrael ni wa muda mrefu, ambao bado unaleta kichwa kuuma kwa jumuia ya kimataifa, na hasa inapofikia makubaliano ya mpaka kuwa wapi kufuatia makubaliano ya mwaka 1967.

Friday, July 22, 2011

Mabomu yalipuka na kuleta maafa nchini Norway.

Mabomu yalipuka na kuleta maafa nchini Norway.
Aslo, Norway 22/07/2011. Jiji la Olso limekutwa na mshituko baada ya mabomu kulipuka katika ofisi za serikali na kusababisha maafa makubwa kwa jamii na raia.
Waziri mkuu wa Norway Jens Stoltenberg ambaye inasemekana hakuwepo katika ofisini wakati wa milipuko hiyo yupo salama.
Hata hivyo waziri mkuu ambaye alitakiwa kuhudhulia mkutano wa umoja wa vijana wa chama cha Labour ambao ulikuwa unafanyika katika kisiwa kilichopo nje kidogo ya mji wa Aslo mbapo kulitokea mashambulizi ya risasi katika kambi hiyo, baada ya mtu mmoja kuvaa nguo kama polisi kuanza kushambulia katika kambi hiyo na kuleta maafa makubwa na kupoteza maisha ya vijana waliokuwa kwenye mkutano huo..
Hadi kufikia sasa hakuna kundi ambalo limedai kuhusika na mashambulizi hayo na idadi ya watu waliopoteza maisha na kujeruhiwa katika matukio hayo mawili bado haijajulikana na polisi wanaendelea na uchunguzi.
Ugiriki yapata mkopo kwa mara yapili.
Brussels, Ubeligiji-22/02/2011. Viongozi wa nchi zinazo tumia sarafu ya Euro wamekubaliana kwa pamoja kuta mkopo kwa serikali ya Ugiriki ili iweze kujikwamua kiuchumi ambao ulikwa unaelekea kuporomoka.
Mkutano huo ulio washirikisha viongozi na wafanyabiasha wa sekta binafsi walifikia makubaliano na kuamua kuikopesha Ugiriki kiasi cha euro 109 billion ambazo ilikuwa inazihitaji ili kuinua na kuimarisha uchumi wake.
Kwamujibu wa habari zinasema , "kwenye mkutano huo viongozi wa serikali waliwashawishi viongozi wa mabenki kukubali kupokea hasara ili kuiokoa Ugiriki kiuchumi."
Ugiriki imebidi ipewe mkopo kwa mara pili baada ya mkopo wa kwaza kutotoshereza kuimarisha uinuaji wa uchumi wa nchi hiyo.
Kundi la Al Shabab lapinga kusambazwa kwa chakula nchini Somalia.
Mogadishu
, Somalia -22/07/2011. Kundi la la Al Shabab linalo pingana na serikali ya Somalia, limekataaa kuruhusu mashirika ya kimataifa yanayo toa msaaada wa chakula kuingia katika maeneo linalo miliki na kudai ya kuwa hakuna njaa ya kutisha kama inavyo tangazwa.
Habari kutoka kwa kundi hilo zimesema " hatutaruhusu kwa kundi lolote kuingia katika maeneo yetu kwa sababu za kusambaza chakula, kwani madi hayo siyo ya kweli na wala hakuna shida ya njaa kama inavyotangazwa."
Al Shabab kundi ambalo hapo awali lilikubali kutoa ruhusa kwa mashirika ya kimataifa kusambaza chakula katika maeneo inayo yashikilia, imeamua kubadisha uamuzi huo ambao hadi sasa unawashangaza wahudumu na wahisani wanao sambaza na kutoa msaada wa vyakula katika nchi ya Somalia ambayo imekumbwa na ukame na kufikia kutangazwa na umoja wa mataifa kuwa nchi hiyo imekumbwa na baaa la njaa la kihistoria katika kipindi cha miaka 60.

Sitaongea na wapinzani hadi siku ya kiama asema Muammar Gaddafi.

Mtuhumiwa wa vita akamatwa na kuwasilishwa Uhollanzi.
Hague, Uhollanzi- 22/07/2011. Kiongozi wa kivita vilivyotokea Kroatia kati ya 1991-199 amewasilishwa nchini Uhollanzi ili kujibu mashitaka ambayo yanamkabili kuhusika katika vita na mauaji.
Goran Hadzic, ambaye atakuwa mtuhumiwa wa mwisho katika kesi hii alikamatwa karibu na misitu Fruska Gorakilomota 65 kaskazini mwa jiji la Belgrade.
Kabla ya kuondoka Goran Hadzic aliruhusiwa kuonana na ndugu na jamaa zake akiwepo mama yake mzazi.
Kukamatwa huko kwa Goran Hadzic kunatarajiwa kurahisisha kwa Belgredi kusukuma mpango wa nchi hiyo kujiunga na umoja wa Ulaya.
Umoja wa mataifa kichwa kuuma zidi ya Morokko na Sahara Magharibi
New York - Marekani 22/07/2011. Kikao kilicho itishwa na umoja wa mataifa ili kujadili hali ya maelewano kati ya Morokko na Sahara ya Magharibi kimekwisha bila kufikia muafaka.
Msimamizi wa mkutano huo, ambao ulifanyika jijini New York Christopher Ross alisema " kila upande bado unashikilia msimamo wake jambo ambalo limefanya majadiliano kuwa magumu."
"Hata hivyo pande zote mbili zimekubaliana kushiriki katika mazungumzo yayote ya hapo baadaye."
Mgogoro wa Morokko na Sahara ya Magharibi umekuwa wa muda mrefu, jaambo ambalo umoja wa mataifa bado inalitafuatia ufumbuzi.
Sitaongea na wapinzani hadi siku ya kiama asema Muammar Gaddafi.
Tripoli, Libya - 22/07/2011. Kiongozi wa Libya amewahutubia wanachi na wale wote wanaomuunga mkono ya kuwa hatafanya mazungumzo na kundi la wapinzani wa serikali yake hatasiku moja mpaka siku ya kiama.
Muammar Gaddafi ambaye amatawala Libya kuwa muda mrefu alisema " siwezi kufanya mazungumzo na kundi lolote linalao pingana na serikali yetu na haitawahi kutokea hadi siku ya kiama."
Wakisikiliza ujumbe wa kiongozi wao Muammar Gaddafi,mamia ya wakazi wa Tripoli ambao walikusanyika kumsikiliza huku wakishangilia kwa kupeperusha bendera za kijani na huku wakiwa wamebeba mabango na maandishi kwenye nguo zao zilioandika kumuunga mkoni Muammar Gaddafi, licha ya mashambulizi yanayo endelea na jeshi la NOTO nchini humo.
Kwa mujibu wa habari kutoka kwa wataalamu wa maswala ya siasa za Libya wamasema " yaelekea hotuna za Muammar Gaddafi zinaleta ugumu kwa kundo la wapinzani kila siku."

Thursday, July 21, 2011

Mahakama ya Uingereza yaruhusu kesi ya rais wa Kenya kuendelea.

Mahakama ya Uingereza yaruhusu kesi ya rais wa Kenya kuendea.
London, Uingereza - 21/07/2011. Mahakam kuu nchi Uingereza imekubaliana na maombi raia wa Kenya kuishitaki serikali ya Uingereza kwa kuhusika na mauaji na mateso wakati wa kundi la Mau Mau lilipo kuwa lipinga ukoloni.
Jaji katika mahakama hiyo Richard McCombe ambaye alitoa uamizi huo alisema " Washitaki wanaweza kuendelea na kesi hii, kwani ushaidi wa kisheria upo kwa serikali ya Uingereza kujibu mashitaka haya."
Katika kesi hiyo, serikali ya Uingereza imekuwa ikijitaihidi kupinga kuendelea na kesi hiyo, kwa madai yakuwa hilo ni" jukumu la serikali ya Kenya."
Wawakilishi katika kufungua kesi hiyo Ndiku Mutwiwa Mutua, Paulo Muoko Nzili, Mbugua Wa Nyingi na Jane Muthoni Mara ambao wapo na umri kati ya miaka 70 na 80, wanadai ya kuwa serikali ya kikoloni ya Uingereza iliwatesa na kuwapiga na baadhi ya jamaa zao walipoteza maisha kutokana na mateso hayo.
Kesi hiyo inatarajiwa kuanza mapema mwaka 2012.

Wednesday, July 20, 2011

Wanchi wa Malawi waandamana.

Ukame wa Somalia watangazwa kimataifa.
Mogadishu, Somalia- 20/07/2011. Umoja wa Mataifa umetangaza ya kuwa Somalia imekua na baa la njaa kimataifa kwa kipindi cha miaka 60 iliyo pita.
Kwa mijibu wa habari kutoka ofisi za umoja wa mataifa zinazo shughulikia chakula zimesema, "Somalia imekuwa na ukame wa kutisha na kuhatarisha maisha ya kila kiumbe hai."
Hata hivyo mashirika ya kutoa misaada ya kibinadamu yamezilaaumu nchi tajiri dunia kwa kutokulipa kipao mbele swala la njaa iliyopo Somali na Afrika ya mashariki kwa ujumla.
Wanchi wa Malawi waandamana.
Lilongwe, Malawi - 20/07/2011. Mamia ya wanchi wa Malwi wamepambana na polisi wa kuzuia ghasia ambao wanadai rais wa nchi hiyo kujitoa madarakani kutokana na kuanguka kwa uchumi na haki za binadamu.
Habari zinasema"raia hao walichoma matairi ya magari na kuharibu baadi ya maeneo."
Msemaji wa polisi, Willie Mwaluka alisema " polisi wapo katika tahadhali kwani hali inaelekea kuwa mbaya na tunajitahidi kutuliza ghasia na kulinda usalama wa raia."
Serikali ya Malawi imekuwa na matatizo ya kiuchumi na Uingereza kusimamisha mchango wake wa kiasi cha £341milion ambazo zimekuwa zikisaidia katika nyanja tofauti nchini humo.
Akiongea katika radio ya taifa, rais wa Malawi Bingu wa Mutharika alisema " wakati nchi zinazo endelea zinasaidiwa kifedha ili kuinua uchumi wake na shirika la fedha, sisi nchi masikini tunaambiwa tupunguze thamani ya fedha zetu hili si jambo jema kwa jumuia ya kimataifa."
Serikali ya Malawi imekuwa na mvutano na shirika la fedha la kimataifa katika swala la kifedha.
Wapinzani wa Gaddafi wakubaliana na Ufaransa
Paris, Ufaransa - 20/07/2011.Serikali ya Ufaransa itangaza ya kuwa kiongozi wa Libya mUammar Gaddafi anaweza kukua nchini Libya ikiwa atakubali kuachia madaraka.
Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa, Alain Juppe alisema " jumuiya ya nguvu za nje zipo tayari kuruhusu Muammar Gaddafi anendelee kuishi nchini Libya, ikiwa atakubali kuachaia madaraka, na kuwepo kwa amani nchi Libya kupo mikononi mwa Gaddafi na tupo kuwahakikisha ya kuwa Libya ina kuwa huru kutoka mikononi mwa Gaddafi."
Maelezo haya yamekuja baada ya viongozi wa kundi la upinzani linalo pingana na serikali ya Muammar Gaddafi kufanya mazungumzo na serikali ya Ufaransa ambayo inawasaidia kwa hali na mali ili kumuondoa Gaddafi madarakani..
Waziri mkuu wa Uingereza awekwa kiti moto na bunge.
London,Uingereza. 20/07/2011. Waziri mkuu wa Uingereza amekuwa na wakati mgumu kujitete ili kutotikisa uamini wake kwa raia wa Wauingereza na wanachama wa chama chake kutoka na kumwajili mmoja wa aliyekuwa mhariri wa gazeti la News of the world.
David Cameron ambaye amekatisha ziara yake katika bara la Afrika, na kuja kuliongelea swala kumwajili Andy Coulson, kwa kusema " nisingeweza kumwajili Andy kama ningejua hali hii na kwa hilo naweza kuomba radhi kama ikibidi."
Unaishi, kujifunza na kuamini na kwa minajili hiyo ninawajibu kuwajibika ili kutatua swala hili" alisema David Cameron.
Hata hivyo kiongozi wa chama cha upinzani Ed Miliband alisema " David Cameron amefanya makosa katika uamuzi wake."
Kiti moto hicho ambacho alikuwa nacho waziri mkuu wa Uingereza, kimekuja baadaya mmiliki wa gazeti la news of the world ambalo limefutwa, Rupert Mudorch na mtoto wake kumaliza kufanywiwa mahojiano na kamati ya bunge kuhusu gazeti kuhusika na kurekodi simu za watu binafsi kinyume cha sheria.

Friday, July 15, 2011

Kenya yakubali kufungua kambi nyingine ya wakimbizi.

Serikali ya Muammar Gaddafi bado kitendawili kwa NATO na washiriki wake.
Istambul, Uturuki - 15/07/2011. Serikali ya Amerika imejiunga na nchi nyingine kulitambua kundi la wapinzani wanao pingana na serikali ya Libya inayo ongozwa na Muammar Gaddafi katika mkutano uliofanyika nchini Uturuki jijini Istambul.
Katika mkutano huo ambao umewakutanisha viongozi wa nchi mbalimbali umetamka ya kuwa serikali ya Muammar Gaddafi na watu wake wakaribu wanaotawala hawatambuliki na niwakati wake kuachia madaraka kwa wanchi wa Libya.
Uingereza nchi ambayo ipo mstari wambele katika jitihada za kumngoa madarakani Muammar Gaddafi, imeatangaza kuongeaza misaada ya kijeshi katika jeshi la NATO linalo fanya mashambulizi nchini Libya kwa muda wa miezi minne hadi sasa.
Msemaji wa serikali ya Libya inayo ongozwa na Muammar Gaddaf amekanusha kauli hiyo ya mkutano wa Istambuli kwa kusema " usemi huo wa mkutano wa Uturuki nchini Istambuli hatuutambui na tutapigana hadi kufa kwa kulinda mafuta yetu zidi ya jeshi la NATO, tuta ua tupo tayari kufa kwa mafuta yetu."
Kwa mujibu wa habari kutoka kwenye mkutano huo zinasema " lengo la mkutano huo ni kuangalia kiundani nakutathmini ni kwa jinsi gani Libya itakuwa mara baada ya kuondoka kwa Muammar Gaddaf na serikali yake na vilevile kupanga mikakati mipya ya kumngoa Muammar Gaddaf madarakani.
Bunge la Itali lakubali mbano wa matumizi.
Rome, Italy - 15/07/2011. Bunge nchi Italy limepiga kura nakupitisha mbano wa matumizi na umakini katika kodi za mapato kwa kipindi cha miaka mitatu.
Mbano huo utakao kuwa wa kiasi cha dola za Kimarekani 67 billioni ulipita kwa kura 314 zidi ya zile zilizo pinga 280.
Kwa mujibu wa habari toka serikalini zinasema " serikali imeamua kufanya hivyo ili kulinda uchumi wa nchi hiyo na kufikia malengo yake ifikapo 2014."
Serikali ya Itali imefuata mlolongo wa nchi wanachama wa jumuiya ya Ulaya ambazo ziliamua kuchukua hatua kama hiyo ili kunusuru kuporomoka kwa uchumi wa nchi zao.
Ushindi huo wa kura katika bunge kumezidi kumpa uzima wa kisiasa waziri mkuu wa Italli Silvio Berlusconi ambaye anakumbwa na misukosuko katika uongozi wake hasa kutoka upande wa wapinzani wa serikali yake.
Kenya yakubali kufungua kambi nyingine ya wakimbizi.
Nairobi, Kenya - 15/07/2011. Serikali ya Kenya imekubali kufungua kambi ya ukimbizi iliyopo mpakani kwenye eneo la Ifo II Dabaab, kwa ajili kuwapokea wanchi wa Somalia ambao wanakimbia ukame ulioikumba nchi hiyo na hali ya usalama wa maisha yao kuwa mashakani kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyo chukua zaidi ya miaka 15.
Waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga, alikubali kufunguliwa kwa kambi hiyo mara baada ya kutembelea kambi moja ambayo imewapokea wakimbizi wapatao 100,00o kutoka Somalia.
Raila Odinga, alisema, " ingawaje tunafikilia na kujali usalama wa raia Kenya, lakini hatuwezi kuacha ndugu zetu wateseke, na niwajibu wetu kutoa misaada wa hali na mali."
Msemaji wa shirika la kuhudumia wakimbizi duniani, Fafa Attidzah alisema " tunafuraha na kuishukuru serikali ya Kenya kwa kukubali kufungua kambi nyingine ambayo itatuwezesha kuwapokea wananchi wa Somalia na kuwapa huduma za kibinadamu."
Kambi hiyo ya Ifo II iliyopo Dabaab inatarajiwa kupokea zaidi ya wakimbizi 300000.

Thursday, July 14, 2011

Serikali ya Sudani ya Kusini inawakati mguu kukuza sekta ya afya.

Serikali ya Sudani ya Kusini inawakati mguu kukuza sekta ya afya.
Juba,Sudan ya Kusini - 14/07/2011. Wananchi wa Sudani ya Kusini ambao wanasherekea kuzaliwa upya kama taifa huru tangu tarehe 09/ Julai/ 2011 na kujulikana kamataifa kama nchi huru na umoja wa mataifa kuitambua nchi hiyo na kuipa uanachama namba 193 katika umoja mataifa, imegundulika ya kuwa serikali itakuwa na wakati mgumu wakujenga muundo mbinu wa kiafya na nyanja zake.
Habari zilizo patikana zinasema, "miundo mbinu ya kiafya katika hospitali zilizopo nchini humo zinaupungufu mkubwa wa nyenzo za kufanyia kazi na hii nikatika maeneo yote hadi kwenye kambi za jeshi."
"Wafanyakazi wa hospitali hizo ambao wanapokea zaidi ya wagonjwa 200 kwa siku, wana fanya kazi katika mazingira mangumu." Habari zimesema.
Sudani ya Kusini ni nchi ambayo imeundwa baada ya wanchi wa nchi hiyo kupiga kura ya maoni na kuunga mkono kugawanyika kwa nchi ya Sudan.
Serikali ya India ya wasaka waliohusika na milipuko jijini Mumbai.
Mumbai, India - 14/07/2011. Polisi nchini India bado wanaendelea kufanya uchunguzi ili kujua ni kundi gani ambalo limehusika katika mashambulizi ya mabomu yaliyo tokea jiji humo.
Waziri wa mambo ya ndani Palaniappan Chidambaram alisema " milipuko hiyo ambayo imetokea inaashiria ya kuwa ilikuwa ni mpango wa magaidi ili kutishia wanchi wa India ambao hawata tishika kamwe."
Milipuko hiyo ambayo imetokea jijini Mumbai imekuwa ikidhaniwa yakuwa kuna makundi ambayo yanahusika, japo mpaka sasa hakuna kundi ambalo limekubali au kutangaza kuhusika na milipuko hiyo ambayo imeleta maafa makubwa kupoteza maisha ya watu zaidi ya 21 na wengine kujeruhiwa vibaya.
Mashambulizi hayo ni ya pili tangu yale yaliyo tokea mwaka 2008, ambapo kundi la kigaidi kutoka Pakistan Lashkra-e- Taiba lililaumiwa kwa kuhusika namilipuko hiyo na kuzika nchi ya India na Pakistani katika wakati mgumu wa kidipromasia
Dawa ya ukimwi yaleta matumaini mazuri.
New
York, Marekani - 14.07/2011. Shirika linalo shughulikia maswala ya afya la umoja wa mataifa WHO limetoa habari yakuwa dawa zinazo tumiwa na ugonjwa wa ukimwi zinapunguaza kwa kiasi fulani maambukizo ya ugonjwa huo.
Shirika la afya limetoa habari hizo kufuatia uchunguzi uliofanyika nchini Kenya, Uganda na Botswana na kusema " 62% zinaonyesha watu waliotumia dawa hizo walipunguza kwa kiasi maambukizi ya ugonjwa ukimwi kwa wapenzi wao."
Mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Margaret Chan alisema " WHO inaendelea kudumisha kazi yake ya kutoa dawa za ukimwi ili kupunguza ugonjwa huo hasa katika nchi hambazo hazina uwezo kiuchumi."
Wachunguzi wa mambo ya kiafya wamelifurahi matokeo hayo ya matumizi ya dawa hizo.

Sunday, July 3, 2011

Hezbollah yalia na Izrael katika mauaji ya Rafik Hariri.

Ugiriki yapata mkopo.
Athens, Ugiriki -03/07/2011. Serikali ya Ugiriki imepatiwa mkopo wa pesa za dola ya Kimarekani zipatazo Billlion 18 kutoka kwenye jumuya ya Ulaya.
Wakipitisha muswada huo, mawaziri wa fedha wa jumuya hiyo walikubaliana kwa pamoja kuipa Ugiriki fedha hizo baadaya serikali ya Ugiriki kukubali kufanya mabadiliko katika sera zake za kuijenga nchi hiyo kiuchumi.
Vilevile jumuya Ulaya imewaagiza viongozi wa siasa wa Ugiriki kushirikiana kikamilifu ili kuinua hali ya uchumi wa nchi hiyo.
Hezbollah yalia na Izrael katika mauaji ya Rafik Hariri.
Beirut, Lebanon -03/07/2011. Kiongozi wa kundi la Hezbollah ameilaumu Izrael kwa kuhusika na mauaji aliyekuwa waziri mkuu wa Lebanon Rafik Hariri mwaka 2005.
Hassan Nasrallah alisema " tunajua Izrael imehusika katika mauaji na hii kesi iliyopo nikwaaajili ya kuleta mvurugano wa kisiasa nchini Lebanon na tunaomba kati hiyo ifanye uchunguzi wake kwa upande wa Izrael pi
na siyo kuleta mvurugano kati ya Walebanon.
Rafik Hariri aliuwawa baada ya mlipuko wa mabomu kulipuka katika eneo alilo kuwepo na tangu kipindi hicho cha kifo chake, serikali ya Lebanon imekuwa ikitafuta kwanundani nani aliye husika na kifo chake.
Ethiopia yakumbwa na ukame mkubwa.
London,
Uingereza -03/07/2011. Serikali ya Uingereza imehaidi kutoa msaada wa pesa kiasi cha paundi million 38 kwa serikali ya Ethiopia ili kusaidia kununua chakula, baada ya nchi hiyo kukumbwa na ukame mkubwa.
Waziri wa ushirikiano wa kimataifa wa Uingereza Andrew Mitchell alisema " msaada hun wa pesa utaambatana na mpango wa shirika la chakula duniani katika kukuza kuwepo kwa lishe bora kwa watoto wapatao 329,000."
Ethiopia nchi mojawapo katika bara la Afrika ambayo imekumbwa na ukame wa hali ya juu kwa kipindi cha miaka 60 iliyopita.Hata hivyo nchi hiyo ilikumbwa na ukame kwenye miaka ya themani ambapo dunia nzima ilishikwa na mstuko mkubwa.
Kwamujibu wa habari kutoka shirika la umoja wa mataifa zinasema "nchi nyingine ambazo zinakabiliwa na hatari hiyo ya ukame ni Somalia, Djibouti na Kenya."

Thailand yapata waziri mkuu mpya mwanamke kwa mara ya kwanza.

Thailand yapata waziri mkuu mpya mwanamke kwa mara ya kwanza.
Bangkok, Thailand- 03/07/2011. Waziri mkuu wa Thailand amempongeza mpinzani wake bi Yingluck Shinawatra ambaye ni kiongozi wa chama cha Pheu Thai Party kwa kushinda kura nyingi katika uchaguzi uliyofanyika nchini humo.
Waziri mkuu Abhisit Vejjajiva akitoa pongezi zake alisema " napenda kumpongeza kiongozi wa Pheu Thai Party na nawatakia mafanikio mema katika kuunda serikali mpya na nitampa ushirikiano mkubwa kwani amekuwa kiongozi wa kwanza mwanamke kushika kiti hicho na naimani ataleta ushirikiano mkubwa."
Akiongea baada ya huku matokeo hayo bi Yingluck Shinawatra alisema " swala kubwa ni kuinua uchumi wanchi na kunakazi kubwa ambayo inatukabili wana Thailand na kwa ushirikiano tutafanikiwa."
Bi Yingluck Shinawatra, ambaye ni dada ya aliyekuwa waziri mkuu wa zamani Thaksin Shinawatraaliye ondolewa madarakani mwaka 2006.
Umoja wa Afrika wapinga amri kukamatwa kwa Muammar Gaddaf
Moscow,
Urusi- 03/07/2011. Rais wa Afriak ya Kusini yupo nchini Urusi katika ziara rasmi ili kujadili na kufanya mazungumzo na viongozi wa serikali ya Urusi na kundi linalo shughulikia swala la kuleta amani nchi Libya.
Rais Jacob Zuma, ambaye atawakilisha Umoja wa nchi za Afrika, anatarajiwa kuelezea msimamo wa umoja huo na maamuzi yaliyo fikiwa wakati wa kikao kilicho amalizika hivi karibuni nchini Ekwetaria Guinea.
Hata hivyo kikao hicho hakikubali na kupinga swala la mahakama ya kimataifa ya Hague iliyopo nchi Uhollanzi kwa kutoa amri ya kukamatwa kwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddaf kutoka na kudai mahakama hiyo imekuwa "inaaangali makosa yanayo fanyika katika bara la Afrika na kufumbia macho yale yanayo fanywa na nchi za Ulaya Magharibi hasa huko Iraq, Pakistan na Afghanistan na kudai yakuwa Mureno Ocampo analeta mzahaa katika kutimiza na kuangalia haki" alisema Jean Ping ambaye ni mwenyekiti wa umoja huo wa Afrika.

Friday, July 1, 2011

Majina ya washukiwa ya mauaji Rafik Harir yatajwa.

Dominique Strauss-Kahn apata unafuu wa katika kesi yake.
New York, Marekani - 01/07/2011.Mahakama ya jijini New York imemwondolea aliyekuwa mkuu wa shirika la fedha duniani IMF-Intarnational Monitary Fund Dominique Strauss-Kahn, sheria ya kumtaka akae katika nyumba yake bila kutoka wakati kesi yake ikiendelea.
Jaji anayesikiliza kesi hiyo alisisitiza wakati wa kusoma uamuzi huo alisema " kuachiwa huko hakuna maana kesi imefungwa, bali kesi bado inaendelea na haruhusiwi kutoka nje ya nchi."
Hata hivyo hata habari kutoka ofisi ya mwanasheria anayeshughulikia kesi hito zinansema, " uamuzi huo umekuja baadaya ya uchunguzi kuonyesha wasiwasi juu ya kesi yenyewe hasa kutoka kwa mshitaki wa kesi hiyo."
Dominique Strauss-Kahn anakabiliwa na kesi ya kutaka kumbaka mmoja ya wafanyakazi wa hotel aliyokuwa amefikia wiki chache zilizo pita akiwa ziarani kikazi Marekani,
Dominique Strauss-Kahn kama atakutwa na hatia anaweza kuhukumiwa kifungo cha miaka 25 jela.
Rais wa Sudan Omar al bashir ziarani nchini China.
Beijing, China - 01/07/2011. Serikali ya China na serikali ya Sudani zimakubaliana kushirikiana kwa ukaribu zaidi katika sekta ya kiuchumi kufuatia ziara ya rais wa Sudan Omar al- Bashir.
Rasi wa China Hu Jintao ambaye alikuwa mwenyeji wa rais wa Sudan Omar al-Bashir alisema " nifuraha kumkaribisha rais wa Sudan na hii inaonyesha kukua kwa urafiki kati ya nchi hizi mbili China na Sudan na kutaongeza kubadilishana maarifa katika kukuza uchumi kati ya nchi hizi."
Rais Omar al Bashir, ambaye alifunguliwa mashitaka na mahakama ya inayo tetea haki za binadamu, atazungumzia pia hali halisi ya bara la Afrika na mgawanyo wa Sudan unaotarajiwa kutokea July 9.
China imekuwa nchi ambayo inashirikiana kiukaribu na Sudani katika sekta ya kibiashara hasa kwenye uzalishaji wa mafuta.
Majina ya washukiwa ya mauaji Rafik Harir yatajwa.
Beirut. Lebanon-01/07/2011. Waziri wa mambo ya ndani wa Lebabon amethibitisha rasmi majina ya watu wanao shukiwa katika mauaji ya aliyekuwa wazairi mkuu wa Lebanon Rafik Harir na watu wengi 22 mwaka 2005.
Waziri Marwan Charbel alisema ya kuwa , "mwanasheria mkuu wa Lebanon, ametoa kibali cha kukamatwa kwa washikiwa ambao ni Mustafa Bedreddine, Salaim Ayyash amabye anaulaia wa Marekani, Assad Subra na Hussein Anaissi."
Kwa mujibu wa habari zilizo patina zinasema washutumiwa hao hawajulikani wapo wapi na hivyo kesi dihi yao itakuwa wazi mpka hao watakapo kamatwa.
Hata hivyo kundi Hezbollah limekanusha madai hayo na kiongozi wakundi hilo amedaia yakuwa yoyote atakaye karibu "kuwakamata watu hao atakata mikono yao."
Nayo serikali ya Marekani inefurahishwa na kitendo hicho cha kujulikana kwa wahusika wa mauaji ya aliye kuwa waziri mkuu wa Lebanon Rafik Hariri na kusisi tiza ya kuwa haki lazima itendeke.