Friday, January 25, 2008

Suharto afariki dunia, alikuwa kipenzi cha nchi za magharibi wakati fulani.

Afrika kuionyesha dunia ya kuwa soka iko damuni, soka ni furaha kama ngoma zetu.

Accra Ghana - Mashindano ya kombe la mataifa ya Kiafrika yamenza hivi karibuni nchini Ghana, huku kila nchi mshiriki wa mashindano haya ikiwa na matumaini makubwa ya kutwaa ubingwa huu wa mwaka 2008.
Hii itakuwa ni kwa mara ya 26 mashindano haya yana chezwa kutafuta ni nani gwiji wa soka katika bara la Afrika.
Kwa kawaida mashindano haya huwa yanachezwa kila baada ya miaka miwili, hivyo basi bingwa huwa anawakilisha bara la Afrika katika mashindano ya mabingwa wa mabara yote sita ya dunia na bingwa wa soka wa dunia.
Hivyo roho za wapenzi wa soka zipo juju kutaka kujua kama nchi zao zitaweza nyakua ubingwa huu.
Pichani hapo juu wanaonekana mamia ya watu walio hudhuria siku ya ufunguzi wa mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika mjini Accra 2008.
Kama tunavyo jua Afrika, mpira wa miguu siyo tu huwa pekeyake bali husindikizwa na burudani kwa ujumla, hapo juu anaonekana mmoja wa shabiki wa soka akipiga ngoma, kusindikiza wachezaji waliopo uwanjani wacheze vizuri kama wana cheza ngoma. Picha ya tatu mpaka ya sita, wanaonekana washabiki wa kiwa na shahuku kubwa kwa kufanya vitu vyao, ili kuwapa moyo wapenzi na wachezaji kwa ujumla.
Suharto afariki dunia, alikuwa kipenzi cha nchi za magharibi wakati fulani.
Jakarta, Indonesia - Aliyekuwa rais wa zamani wa Indonesia,bwana Haji Muhammad Suharto, amefariki dunia, baada ya kupata matatizo ya kiafya kwa muda mrefu.
Bwana Suharto, ambaye ameongoza Indonesia kwa miaaka isiyo pungua therasini (30), inasadikiwa alitawala kwa kutumia mkono wa chuma na hasa wakati wa vita baridi kati ya Komunisimu na Ubepari au kati ya NATO na USSR.
Bwana Suharto alikuwa akipendwa saana na kupata misaada kutoka nchi za ulaya magharibi na Amerika.
Bwana Suharto amefariki dunia, akiwa na umri wa miaka 86, huku alikuwa anashitakiwa kwa makosa mengi ya haki za binadamu.Lakini kutokana sheria za za Indonesia, pindipo mtu anapo aga dunia,basi kesi yake huwa inasimamishwa.
Pichani juu ni picha ya hayati Haji Muhammad Suharto, enzi hizo alipokuwa rais wa Indonesia. Picha nyingine anaoneka hayati rais Suharto, alipokuwa rais wa Indonesia akiongea na rais wa zamani wa Amerika bwana Billy Clinton.
Na picha ya chini anonekana hayati,rais wa zamani wa wa Indonesia, akisalimiana na rais wa zamani wa Afrika ya Kusini bwana,Nelson Mandela walipokutana.
Wapalestina waonja raha ya kuwa huru,kiongozi mwasisi afariki dunia.
Gaza, Palestina - Raia wa Kipalestina wapatao makumi kwa mamia, walivuka mpaka na kuingia nchini Misri kwa wingi kwa mara ya kwanza, baada ya kundi la HAMAS kuvunja ukuta ulio kuwa umejengwa kuwazuia Wapalestina waishio katika mji wa Gaza.
Kuvunjwa kwa ukuta huo kuliwawezesha wanchi wa Palestina kuingia nchini Misri, na kujipatia mahitaji muhimu ambayo walikuwa wanaya kosa kwa muda mrefu.
Hali hii imekuwa ikilalamikiwa na Israel, na kuiagiza serikali ya Misri kuweka usalama zaidi ili kundi la HAMAS, lisipitishe siraha.
Wakati huo huo aliyekuwa mmoja wa wanachama na mwanzilishi wa PFLP- Popular Front for the Liberation of Palestine bwana George Habash amefariki dunia siku nya jumamosi 26-01-2008, kwa ugonjwa wa moyo.
Bwana,Habash ambaye alikuwa mtu wa karibu wa kiongozi wa PLO - Palestine Liberation Organasation, hayati Yasir Arafat.
Hayati George Habash alikuwa akiishi nchini Jordan, na atakumbukwa kwa mbinu zake za kuongoza utekwaji wa ndege,na utekwaji nyara kwa wapinzani wa Palestina.
Pichani juu wanaonekana waplestina wakivuka mpka na kuingia nchini Misri,na picha ya chini linaonekana katapira,likisaidia kubomoa kabisa ukuta ili wananchi wa Palestina waweze kuvuka bila matatizo.
Uchaguzi mkuu wa Zimbabwe kuwa machi 29," Wapinzani wanamashaka"
Harare, Zimbabwe - Wapinzani wa chama cha upinzani cha MDC nchini Zimbabwe wanao ongozwa na bwana Morgan Tsvsngirai, wamelalamikia hatua ya serikali kuamua kuweka tarehe ya uchaguzi mkuu wa nchi tarehe 29 mwezi wa machi.
Msemaji wa MDC, alisema kutangazwa kwa tarehe hiyo ni kinyume, na hii inahashiria ya kuwa serikali na ZANU-PF, wanakiuka baadhi ya makubaliono, hasa kwa wasuruhishi wa mgogoro huu wa kisiasa kutoka Afrika ya Kusini wakiongozwa na rais Thabo Mbeki.
Viongozi wa MDC,wameomba uchguzi huu usogezwe mpaka mwezi wa juni. Picha hapo juu anaonekana bwana Morgan Tsvangirai, akiutubia wananchi katika moja ya kampeni za kuimarisha chama cha MDC.
Picha chini, wanonekana vijana wanachama wa MDC wakiandamana hivi karibuni mjini Harare.
Wapiganaji (MEND) wa mwalika George Clooney, kujionea mwenyewe hali ya Niger Delta.
Niger Delta,Nigeria - Wapiganaji wa nao pigania haki zao katiaka ukanda wa mafuta wa Niger Delta, wamemwalika mcheza sinema, mwana amani na mtetezi wa haki za binadamu bwana George Clooney kutembelea eneo la Niger Delta.
Eneo la Niger Delta, ni eneo ambalo linatoa mafuta kwa wingi nchini Nigeria, limekuwa katika hali ya mashaka kila kukicha.
George Clooney mwenye miaka 46, amekuwa akijitahidi na kuiomba dunia kusiammisha vita vya Darfur, na mwalikoko huu wa watu wa Niger Delta,kumeonyesha ni jinsi gani bwan Clooney alivyo muhimu katika harakati za kuleta amani.
Wachunguzi wa mambo wamedai ya kuwa kama hali iliyopo Niger Delta, atafanyiwa kazi sasa, basi huenda ikawa na ubaya zidi kwa binadamu, kulikono hali hilivyo sasa Darfur.
Pichani anaonekana bwana George Clooney aliongea na waandishi wa habari kuhusu hali mbaya inayao sababishwa na vita hasa katika bara la Afrika.
Picha ya chnini wanaonekana wapiganajiwa wa Niger Delta(Emanicipation of the Niger Delta) mwakiwa na siraha tayari kupamabana na yoyote wanaye ona anakwenda kinyume na matakwa yao.
Makubaliano ya amani ya mjini Goma,kuwa ni mwanzo wa kuisha vita?
Kivu,Jamuhuri ya Kongo - Wapiganaji wa jeshi linalo ongozwa na Mej Laurant Nkunda, wametia mkataba wa amani hivi karibuni na serikali ya Kinshasa.
Makubaliano haya yaliyo fanyika mjini Goma, makao makuu ya Kivu Kaskazini. yalihudhuliwa na rais wa Kongo Kinshasa bwana joseph Kabila.
Kutiwa mkataba huu wa makubaliano, unakuja baada ya mazungumzo yaliyo chukua zaidi aya wiki mbili.
Kuweko kwa makubalianao haya, huenda kukumaliza mapambano ambayo yameshukua zaidi ya miaka kumi.
Kutokana na machafuko haya, inadadikiwa ya kuwa zaidi ya watu wasiopungua 1,500,hufa kila siku, kwa kukosa mahitaji ya muhimu.
Picha ni hapo juu ni picha ya kiongozi wa kundi la jeshi la wapinzani wa serikali ya Kongo Kinshasa Mej Laurant Nkunda.
Picha chini ni picha ya wapiganaji wa jeshi ka serikali wakiwa mstari wa mbele kupambana na wapinzani wa serikali hivi karibuni.
Singa singa, wadai ya kuwa haki zao za kidini zimevunjwa"Hii ni kinyume cha katiba"
Paris,Ufaransa - Wananchi wa jamihii ya Singa singa waishio nchini Ufaransa, walianadamana hivi karibuni, kupinga kuzuiliwa kuvaa vilemba vyao vya kichwani kwenye maeneo ya serikali na kwenye mashule.
Wakiongea, mmoja wa viongozi wa jamihii ya Singa singa, alisema ya kuwa kuzuiliwa kuvaa vilemba vyao, kunaingilia na kuvuruga imani ya dini yao. Kwani hata katiba inaruhusu kila mtu anayo haki kuabudu na kuomba Mungu bila kuingiliwa nakuzuiliwa kutekeleza amri za dini.
Hapa juu, wanaonekana wananchi wa jamii ya aina ya Singa singa, wakiandamana kupinga kuzuiliwa kuvaa vilemba vyao, na huku wakiwa wameshikiria picha ya kiongozi (rais ) wa Ufaransa.

Sunday, January 20, 2008

Putin na Kremlin wazidi kutanua misuri ya kiuchumi barani Ulaya.

London, Uingereza - Mchezaji wa zamani wa timu ya Real Madrid , Man United na aliyekuwa kaptain wa timu ya taifa ya Uingereza, David Beckham, amejiunga na timu ya Arsenal kwa ajili ya kuijiweka fiti.
David Beckham, ambaye kwa sasa anachezea timu ya LA Galxy ya Amerika, yupo nchini Uingereza, baada ya ligi ya Amerika kuisha kipindi chake cha 2007.
Kufanya mazoezi na timu ya Arsenal, kutamsaidia David Beckham, kuwa fit pindipo ataitwa kujiunga na timu ya taifa ya Uingereza, ambayo ina kocha mpya bwana Fabio Kapello.
Picha hapo juu anaonekana, David Beckham, Kolo Ture, na wachezaji wengine wakielekea mazoezini.
Chini pichani anaonekana David Beckham, akipasha viungo moto tayari kula ufundi wa kisoka kutoka kwa Wenger .
Thabo Mbeki,awasili Zimbabwe , ''Kitendawili bado kuteguka?''
Harare, Zimbabwe - Rais wa Afrika ya Kusini bwana Thabo Mbeki, amewasili nchini Zimbabwe, ilikujaribu kuzungumza na viongozi wa serikali na viongozi wa vyama vya upinzani.
Hata hivyo viongozi wa chama cha upinzani wamepanga maandamano makubwa yatakayo fanyika hivi karibuni kudai mabadiliko ya katiba.
Ziara ya rais,Mbeki ni moja ya harakati za kutaka kusuruhisha mgogoro wa kisiasa uliopo kati ya chama cha ZANU-PF,na wapinzani.
Ufaransa yaiwekea ngumu Rwanda,mtuhumiwa hatasafirishwa"Mahakama"
Paris, Ufaransa - Mahakama ya serikali ya Ufaransa, imesimamisha kuhamishwa kwa mtuhumuiwa ambaye inasadikiwa alihusika katika mauaji ya watu wengi, wakati wa vita vya wenyewe kwa wenye nchini Rwanda.
Mtuhumiwa huyu,bwana Dominique Ntawukuriryayo, anashutumiwa kwa kuhusika na mauaji ya watu jamii ya tutsi wapatao 25,00 wakati wa mauaji yaliyo stua dunia 1994.
Akiongea kwa niaba ya mtuhumiwa, mwanasheria anaye mwakilisha bwana Dominique, bwana Thiery Mausis, alisema uhamuzi huu umekuja baada ya kugundulikaya kuwa kuna baadhi ya sheria zilikiukwa.
Pichani ni rais wa Rwanda, bwana Poul Kagame, ambaye aliongoza kuleta utulivu nchini Rwanda, kuhakikisha kila aliye husika katika mauaji ya watu wasio na hatia, lazima wakumbane na vyombo vya sheria kujibu mashtaka.
Putin na Kremlin wazidi kutanua misuri ya kiuchumi barani Ulaya.
Sofia,Bulgaria - Serikali ya Urusi na Serikali ya Bulgaria zimetiliana makubaliano ya kuwa serikali ya Urusi itajenga mabomba ya kupitisha gasi nchini Bulgaria.
Kujengwa kwa mabomba haya kutaiwezesha Urusi, kuwa ndiyo nchi pekee kwenye bara la Ulaya itakayo kuwa na uwezo mkubwa wa kusambaza gasi.
Wakati huo huo huo,serikali ya Urusi ,imeseamaya kuwa serikali ya Uingereza inapoteza ukweli wa hali halisi,wa matukio yaliyo tokea kati ya London na Moscow.
Hali hii inatokana na serikali ya Urusi kufunga ofisi za muhimu ambazo zilikuwa zinatumiwa na mashirika na watu binafsi kuweza kufanya kazi na Uingereza.
Pichani wanaonekana viongozi wa Urusi na Bulgaria wakiwa pamoja wakati wakijiandaa kuongea na waandishi wa habari baada ya kukubaliana kimikataba.
China kuwa mkombozi wa uhaba wa lishe kwa wananchi.
Harare,Zimbabwe - Serikali ya China imehaidi kuisaidia serikali ya Zimbabwe,ili iweze kujinyakua kwenye hali ya uhaba wa chakula kwa kuipatia kiasi cha toni 5000 za chakula..
Ahadi hii ilitolewa na makamu msaidizi wa balozi wa China nchini Zimbabwe bwana Ma Deyun.
Akiongea,wakati alipo kutana na viongozi wa serikali ya Zimbabwe,kaimu balozi huyu bwana, Ma Deyun, alisema nchi hizi mbili zitaongeza ushirikiano wa kijamii na kibiashara kwenye msimu wa mwaka 2008.
2007, biashara kati ya China na Zimbabwe, ili ongezeka kwa kiasi kikibwa, na kwa mwaka 2008, huusianao wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili utagharimu kiasi cha $500million.
Serikali ya China,imekuwa ikijenga uhusiano na serikali nyingi za Afrika.
Hapo juu ni picha ya bendera ya Zimbabwe na chini ni picha ya bendera ya China.

Sunday, January 13, 2008

Hatuta pindishwa na kupigishwa magoti na nchi za Ulaya"Ayatollah"

Hatuta pindishwa na kupigishwa magoti na nchi za Ulaya"Ayatollah"
Teheran, Iran - Kiongozi mkuu wa Iran, bwana Ayatollah Ali Khamenei, amesema ya kuwa Amerika haitaweza kamwe kuizuia Iran maendeleo yake ya kupata nguvu za kinyuklia.
Kiongozi huyo alisema yakuwa Amerika na washiriki wake wasiwaze kabisa ya kuwa Iran, itapindishwa na kupigishwa magoti, kataika mradi huu wa nguvu za nyuklia.
Na ametaka swala hili liachiwe chombo kinacho simamia maswala haya kifanya kazi yake kama kawaida na siyo kukipangia.
Hadi hivi sasa, Iran imekuwa inasisitiza ya kuwa, mitambo ya nyuklia iliyo nayo ni kwaajili ya matumizi ya umeme na siyo kwa ajili ya kutengeneza siraha za kinyuklia.
Pichani anaonekana kiongozi mkuu wa Iran,Ayatollah Ali Kamenei akiongea hivi karibuni miji Teheren.
Hatumo tena kwenye mazungumzo"Hali ya usalama siyo nzuri kwetu"
Kivu, DRC - Kiongozi wa kijeshi , na aneye ongoza mapambano ya kutete jamii watutsi chini Kongo, Gen,Laurent Nkunda, amesema ya kuwa wamesimamisha mazungumzo na serikali ya Kinshasa kwa sababu za kiusalama.
Akiongea ,msemaji wa kundi la Gen Laurent Nkunda, bwana Jean Desire Muiti,alisema ya kuwa wamechukua uhamuzi huu , baada ya mmoja ya wa mmsemaji wa kikindi hicho bi Milindi kutishiwa kukamatwa.
Akiongezea, bwana Jean Desire Muiti, alisema ,ilibidi wajumbe waingilie kumuokoa , bi Milindi asikamatwe na kikosi cha askari wapatao kumi, amabo ni kikisi maalumu cha serikali ya Kinshasa, inayo ongozwa na rais Joseph Kabila.
Picha ya hapo juu anaonekana Gen Laurent Nkunda, akiongea na waandishi habari hapo siku za nyuma.
Picha nyingine anaonekana,mmoja ya wajumbe wa mukutano akiwa amekaaa hajui la kufanya,baada ya mkutano kuvunjika.
Senegel, yapotelewa na mmoja ya viongozi wake"Alikuwa na ushauri mzuri"
Dakar, Senegel - Aliyekuwa kiongozi wa chama cha tajiri na chenye nguvu, kijulinakacho kama Islamic Brotherhood, bwana Bara Falilou,amefariki dunia hivi karibuni.
Bwana Bara Falilou aliyekuwa na miaka 92, alikuwa ni mjukuu wa mwanzilishi wa chama hiki Islamic Brotherhood amabcho kilianzishwa mnamo mwaka 1883.
Chama hiki Islamic Brotherhood, kimekuwa muhimili wa ushauri wa serikali ya Senegel.
Mmoja ya watu walio huzuria maombelezi ya kifo cha bwana, Bara Falilou, ni rais wa Senegel, bwana Abdoulaye Wade.
Kutokana na kifo cha bwana Bara Falilou, serikali ilitangaza maombelezo ya siku tatu
Pichani anonekana marehemu Bara Falilou, alipokuwa akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa viongozi waserikali.
Picha ya chini ni picha ya mwanzilishi wa chama cha Islamic Brotherhood, bwana Ahmadou Bamba.
Askari wa Irak, awaua askari wenzake kwa makusudi"Wakuu wa jeshi"
Mosul, Irak - Askari mmoja wa Irak, aliwapiga risasi askari wawili wa jeshi la Amerika na kuwajeruhi wengine.
Tukio hili ni laina yake tangu Amerika, ivamie Irak mwaka 2003.
Askari huyo aliwapiga risasi askari wa amerika mmnamo tarehe 26/12, walisema wakuu wa jeshi ya kuwa tukio hilo lilitokea wakati askari hawa walipopo kuwa wakila doria moja ya vitongoji vya mji wa Mosul.
Hata hivyo wakuu wa vikosi hivi walisema mauaji haya yalifanyika kwa makusudi na askari huyu, anasemekana alijipenyeza na kujiunga na jeshi, na anatokea kwenye jamii ya Wasunni.
Pichani wanaonekana wanajeshi wa jeshi la shirikisho la Irak wakiwa tayari kuanza doria, na nyuma yao ni helikopta ikiondoka baada ya kuwashusha.
Kesi ya rais wa zamani wa Liberia yaingia awamu mpya"Ushahidi waanza kutolewa"
Hague, Netherland - Kesi ya aliyekuwa rais wa zamani wa Liberia,bwana Charles Taylor mwenye miaka 59, imeingia kataika hatua za mwanzo, baada ya mmoja wa mashahidi kuelezea mahakama,uhusianao uliokuwepo kati ya bwana Charles Taylor na baadhi ya viongozi wa vita vya wenyewe kwawenye, nchini Liberia na Sierra Leone.
Maelezo haya yalitolewa na mmoja wa aliyekuwa mkuu wa ulinzi wa bwana Taylor,bwana Varmuyan Sherif.
Bwan Sherif, alisema yakuwa alitumwa na ,bwana Taylor, kwenda kuonana na mmoja wa kiongozi wa kikundi cha kivita bwana Sam Bockarie .
Kikundi cha bwana Bockarie ndicho kinasadikiwa kuhusika katika vita vya Sierra Leone.
Hata hivyo mwanasheria kwa upande wa bwana Taylor,amesema ya kwamba, bwana Sherif alikuwa na matatizo ya akili wakati wote alipo kuwa akifanya kazi wakati ule.
Pichani hapo juu wanaonekana dada wa bwana Charles Taylor,bi Ann Payne Tayrol na Thelma Tayrol wakisikiliza na kuangalia kwenye runinga njinsi gani kesi ya kaka yao inavyo kwenda.
Picha ya pili anaonekana bwana Tayrol, alipokuwa mahakamani kusikiliza kesi yake.
Na picha nyingine ni ya bwana Sam Bockarie,amabye anasadikiwa kuwa ndiye aliyeongoza vita vya Sierrra Leone.

Wednesday, January 2, 2008

Je unajua mwanasiasa wa Afrika anaishi kwa mashaka? " Na mashaka haya ni chanzo cha matatizo haya.

Je unajua mwanasiasa wa Afrika,anaishi kwa mashaka "Namashaka haya ndiyo chanzo cha matatizo"

Nairobi, Kenya - Afrika na Demokrasi, Kenya yawa mfano wa nchi za Afrika na jumuia ya kimataifa. Wakati dunia nzima inashanga nini kimeikumba taifa la Kenya, lakini ukweli ni kwamba hali hii imekuwa inatokea karibu nchi zote, hasa ufikapo wakati wa uchaguzi.
Demokrasi ambayo Wafrika wengi waliipokea, haikuwa kama ilivyo tarajiwa, kwani wakati wa mageuzi yalipoanza vuguvugu lake, siyo Waafrika wengi walijua ya kuwa hali hii itakuwa kinyume na matarajio yao.
Waafrika wengi walitarajia maendeleo ya jamii na ya kiuchumi, na walitarajia yakuwa, kuja kwa vyama vingi au kwa mageuzi ya kisiasa yangeleta neema, kwa kila jamii.
Lakini ukweli ni kwamba sivyo ulivyo, kwani hakuna hata mwanasiasa mmoja ambaye aliweza kuueza ukweli kuhusu hali halisi ya mageuzi .
Bali wale wanasiasa ambao walikuwa wapo kabla ya mageuzi,, walishikwa na wasiwasi, na kuanza kupanga mikakati ya kukabiliana na mageuzi haya, nawakati huo huo chimbuko la wanasiasa ambao hawakupata nafasi ya kushiriki katika serikali ya awali, iliwabidi waanzishe vyama vya upinzani ambavyo vitakabiliana na chama tawala, si kwa kujenga bali kwa kulumbana na kusahahu kupanga mipango ya kujenga nchi kwa pamoja.
Jambo jingine ambalo naomba ni wafahamishe ndugu zangu, yakuwa mwanasiasa ni binadamu wa kawaida tu, ambaye ni mfanyakazi kama wewe au mimi, bali tofauti tulio nayo ni katika utendaji wa kazi, ni kwamba mwanasiasa anakuwa na mkataba wa muda fulani, kuongoza jamii kwa kipindi fulani, kufuatia katiba ya nchi iliyo wekwa na kipindi hiki kinaweza kuwa miaka mitano au zaidi, lakini tukae tukijua hii nikazi ya muda tu kwa mwanasiasa huyu.
Kama tunavyo jua wanasiasa wengi wa Afrika hawana huakika wa maisha baadaye pindipo watokapo madarakani, au chama chao kushindwa na chama pinzani, kutokana na hali hii, hujikusanyia kipato na kutumia fursa hii ya madaraka walio nayo kwa kufanya kila njia kujiandaa na hali ya baadaye pindipo hali ikienda kinyume,na wakati huo huo kupanga mikakati ya kubaki madarakani,
Kwani hadi hivi sasa karibu nchi zote za Afrika ambazo zimefanya uchaguzi wa kushindanisha vyama vingi, zimekumbwa na matatizo karibu yanayo fanana,na yale yaliyo tokea nchini Kenya, hasa kwa matokeo ya uchaguzi kuwa na mashaka mengi na mauaji ya kutisha ambayo jumui za kimataifa huwa hazijui ama hazifuatilii kuindani hali hizo.
Hii inategemea ni kwa kiasi gani chama kilicho shinda kinakubalika vipi kwenye jumuia ya kimataifa, hata kama chama hicho kimeshinda kwa mashaka makubwa.
Hali ya jumuia ya kimataifa kutofatilia malalamiko haya, yamekuwa ndiyo chanzo cha jeuri anayoendelea sehemu zote katika Afrika,kwani hadi hivi sasa kuna nchi zimefanya uchaguzi, na mauaji yametokea hakuna hata kiongozi mmoja wa serikali ambaye ameulizwa au kushitakiwa.
Hii siyo tu,inaonekana ya kuwa Waafrika bado tunawakati mgumu wa kukabiliana na hali hii, bali pia kuna baadhi ya viongozi ambao wanagombania kuongoza nchi hizi hawana mapenzi na watu wao wala kizazi kijacho cha nchi hizi.
Viongozi hawa wamekuwa wakigombania kuongoza nchi kwa kutumia mbinu za kila namna na hasa ukabila, dini na hali ya ufukara, kwa kuwarubuni wananchi yakuwa watasawazisha matatizo hayo, na kuwapa matumaini makubwa.
Lakini wanapo ingia madarakani wanakuta hali sivyo walivyo haidi, na kushindwa kuwaelezea wanchi ukweli ya kuwa hali sivyo ilivyo kama walivyo haidi.
Ukweli ni kwamba uchumi na siasa ni sawa na baba na mama, kwani baba anapokuwa hatekelezi majukumu yake, basi mama hataangaika pekeyake kujenga nyumba, na kama mama hataonyesha mapenzi kwa baba na kushirikiana kumsaidia baba kujenga nyumba, basi hali huwa mbaya kifamilia.
Hivyo basi uchumi wa Afrika kiasilia ni mwingi hauna mfano wa kulingana, lakini jinsi ya kuboresha uchuni huu ndiyo mashaka makubwa,kwani nchi nyingi za Afrika katika bajeti ya kila mwaka haziweki fungu la fedha la kuhimiza au kusaidia watu kugungua nyezo bora za kujenga na nyezo kusaidia au kurahisisha kazi za kila siku.
Fedha nyingi hupotea bila kujulikana matumizi yake na wala hazijulikani zimewekwa kwenye mabenki gani?
Bali utasikia kila kiongozi wa Afrika, anasema ya kuwa hatuna fedha za kusaidia kuboresha maisha ya wanainchi, lakini wakati huo huo utaona ya kuwa matumizi ya wanasiasa ya nakuwa makubwa kupindukia, nampaka kuwashangaza wana nchi na jumuia za kimataifa.
Vile vile jumuia za kimataifa zina changia kwa kiasi kikubwa kuleta hali hii,kwani baadhi ya mikataba inayo wekwa huwa haina manufaa kwa pande zote mbili, na 10% huwa ndiyo kiungo cha kumbana mwanasiasa wa Afrika.
10% na mambo mengine ya kiundani ambayo jumuia ya kimatifa inajua kuhusu viongozi hawa wa Afrika, ambao wapo madarakani, huwa ndiyo siraha kubwa ya kuwabana wasiwe na sauti wanapo kuja kukubaliana kuhusu mikataba na kutetea haki za wanachi wao,hivyo huwafanya viongozi hawa kuwa wazee wa ndiyo ndiyo kwa kila wanacho ambiwa.
Demokrasi na Afrika ni kitu kigeni saana, kwani wananchiwalio wengi wa Afrika, wanaishi kwa kila kukicha na kukizama hawajui nini la kesho, bali wale wachache, alio jaaliwa kupata homa ya demokrasi, basi hutumia kuwaambukiza Waafrika wenzao na matokeo yake ni kama yalio tokea nchini Kenya hivi karibuni.
Ikiwa kama mwananchi hawana matumaini na serikali na serikali haisemi ukweli kuhusu hali halisi, basi wananchi wanakuwa wanageuzwa geuzwa kama pia kwa kufuata wapi kunatoka maneno matamu, nakusahau ya kuwa wanacho hitaji siyo maneno matamu bali ni maendeleo ya kijamiii na kiuchumi, lakini hali ya rushwa na udanganyifu inapo fikia kiwango cha kuwa ndiyo njia ya kipato kwa mwananchi basi, ndipo kila mtu ujiangalia nafsi yake na kusahahu mwingine na kuangalia atamsaidia vipi ndugu yake, ili aweze kupambana na maisha ya lila siku, na ndugu yake akipata basi ataangalia ndugu yake, na ndugu yake kwa ndugu yake na itakuwa hivyo, mpaka yatapo tokea mabadiliko ya uongozi, na huyu kiongozi atakaye ingia atafatialia mtindo huu, na kiongozi mwingine akifatilia mtindi huu, basi nchi huishia kugawanyika kimakabila au kidini.
Na hii ni sumu moja kubwa ya kuua jamii fulani na kuinua jamii fulani, na hatimayake ikifikia tamati ni punje moja ya baruti itawasha mbunga nzima, kwani mbuga nzima ilikuwa majani yake yalikuwa yamekauka tayari.
Swali la kujiuliza je wakati mbuga nzima ina kauka jumuia ya kimataifa ilikuwa haioni?
Ukweli ni kwamba jumuia ya kimataifa ilikuwa inaona, kwani kila usikiapo maoni ya wanasiasa na wa tafsili wa mambo wanazungumzia ya kuwa hali hii ilikuwepo tangu zamani.
Je, hawakujua yakuwa mbuga inapo kauka ni chembe moja ya baruti ikiwaka iataunguza mbuga mzima?
Ukweli ni kwamba walijua, nasema haya kutokana na historia ya wanadamu, ya kuwa huwa anavumulia kwa kiasi fulani lakini uvumulivu ukishindwa basi, ni uadui hufuata na huasama.
Hivyo basi hali ya nchi ya Kenya, ilikuwa inajulikana kwa kiasi kikubwa ya kuwa yapo mataba na matatizo ya ukabila, lakini kwa sababu fulani na manufaa ya liyokuwa yanapatikana kutokana na hali hii, zilifanya jumuia ya kimataifa,kupuuzia, kutofatialia kuindani madhara yatakayo kuja baadaye au kujiuliza je siku ikifikia uvumilivu huu ukaisha kutakuwa nini?
Sasa leo hii, dunia nzima inalia na Wananchi wa Kenya, hasa Afrika,maisha ya watu yanapotea kiunyama.
Viongozi wa siasa,dini na watu tofauti wanajaribu kuomba na kusisitiza utulivu nchini Kenya, lakini inakuwa vigumu kwani nusu ya mbuga imesha kauka na baruti imewaka na kuleta moto ambao kuuzima kunaitaji jitihada zaidi kulikoni ilivyo tarajiwa
Hii ni fundisho jingine kwa jumia ya kimataifa, kwani tujue ya kuwa dunia na walimwengu wa leo tunategemeana kwa kiasi kikubwa sana, japo wapo watu wasioamini hili.
Matatizo ya nchi moja ni matatizo ya dunia nzima kwa ujumla, hivyo naombatushirikiane kutimiza amri za Dini zote Zina himiza tuwe na Upendo.
Kwani kwa wale Wakritu, kama wanakumbuka,"Bwana Yesu Kristu, alisema amri mpya na wapa pendaneni kama nilivyo wapenda mimi, kwani mtu hawezi kumpenda Mungu wakati haumooni, na wakati huo huo unamchukia jirani yako mbaye unamuona. Hivyo basi fumbo hili tukilitimiza basi dunia nzima itakuwa na amani japo kwa dakika moja.
Mungu Ibariki Afrika, Mungu tunaomba Hekima na Upendo utushushie Afrika
Picha juu inaonyesha ramani jinsi gani nchi ya Kenya ilivyo gawanyika kikabila.
Picha nyingine anaonekana polisi anamwangalia rais jinsi alivyo pata madhara kutokana na vurugu hizo.
Picha, anaonekana mwanajeshi wa Kenya akiwa ameshika bunduki juu, huku wananchi wakiwa wanamwangalia kwa hasira.
Matokea ya uchaguzi nchini Kenya yameleta hali isiyo tabilika, wanaonekana wananchi wenye hasira wakiwa na kila aina ya zana tayari kupamba wao kwa wao.
Siku zote panapo tokea vita au vurugu wanao dhurika zaidi ,ni wakina mama na watoto, pichani wanaonekana wakina mama wakiangalia kwa kiasi gani mali na makazi yao yalivyo haribiwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe.