Mauaji yatokea Kusini Mashariki mwa Kenya.
Mauaji hayo yaliyotokea katika eneo la Reketa katika kijiji cha Tarassa Kusini Mashariki maili 300 mwa mji wa Nairobi. na kuleta mstuko mkubwa tangu mauaji yaliyotokea miaka minne iliyopita wakati na baada ya uchaguzi mkuu nchi Kenya.
Msemaji wa polisi Chifu Joseph Kitur alisema " watu walifariki kwa kukatwa na mapanga na wengine kuchomwa moto na pia nyumba zao kuchomwa moto jambo ambalo mpaka sasa bado tunalifanyia uchunguzi nini hasa kilifanyika hapo awali na kufikia kufanyika muaji ya kinyama kama haya."
Hata hivyo mkazi mmoja wa eneo hilo alisema hii mauaji haya yote yametokana na mvyutano wa mifugo kati ya wakazi wa vijiji vya Orma na Pokomo.
Angela Merkel na Antonis Samaras wakutana kujadili hali ya Ugiriki.
Berlin, Ujerumani - 24/08/2012. Waziri mkuu wa Ugiriki amekutana na Khansela wa Ujerumani katikaharakati za kutaka kujua ni kwa kiasi nchi ya Ugiriki inavyo fuata masharti ya kuimarisha uchumi.
Waziri Mkuu Antonis Samara na Khansela Angela Markel walikutana na kujadili ni kwa kisi gani nchi za Jumuiya ya Ulaya zitashirikiana katika kuhakikisha Ugiriki inarudisha uimara wa uchumi wake.
Antonis Samara akiongea alisema " tunataka kuwahakikishia wenzetu tutafanya kila njia kuhakikisha uchumi wa Ugiriki unakuwa na tunachoomba ni muda zaidi."
Naye Khansela Angela Merkel alisema" naimani Ugiriki itatimiza yote yanayo takiwa ili kukuimarisha uchumi wa nchi hiyo na kutokana kwa kufuatia makubaliano iliyo yafanya na nchi za jumuiya Ulaya na ukizingatia Ugiriki ni nchi ambayo kwa upande wangu ni mwanachama wa nchi za jumuiya ya Ulaya na ningependa ieleweke kuwa naunga mkono nchi ya Ugiriki kubaki kuwa mwanachama wa nchi za jumuiya Ulaya .
Nchi ya Ugiriki imekuwa nawakati mgumu katika haarakati za kutaka kuinua uchumi wake baada ya kupewa mkopo wa pesa kutoka nchi za jumuiya za Ulaya na kutakiwa kufanya mrekebisho ya kiuchumi jambo ambalo limekuwa likileta msuguano kati ya serikali na wanchi wake.
Aliyefanya mauaji nchini Norway haukumiwa miaka 21 jela.
Oslo, Norway - 24/08/2012. Mahakama nchini Norway imemuhukumu kwenda jela mshitakiwa aliyehusika katika mauaji ya watu 77 na kufanya ushambulizi kutumia mabomu katika jiji la Olso.
Anders Breivik ambaye aliwavamia vijana waliokuwa katika kisiwa cha Utoya kwa ajili ya mkutano wa kuhamasisha siasa na kuanza kuwapiga risasi amehukumiwa miaka 21 jela baada ya kukutwa na hatia ya kufanya makosa hayo.
Akiongea baada ya hukumu, mshitakiwa Anders Breivik alisema " nasikitika kwa wale wanachama wenzangu kwa kushindwa kufanya mauaji zaidi wakati ule."
Anders Breivik ambaye alidai ya kuwa ni mwanachama wa Temple Knight na alifanya mauuaji hayo kwani alikuwa anapinga kuwepo kwa wageni na kukua kwa dini ya Kiislaaam nchi Norway na Ulaya..