Sunday, December 30, 2007

Kijana wa miaka 19 apewa kazi ya kufuata nyayo za mama Bhutto.

Alex Ferguson awapiga faini wachezaji wake kwa kukuso maadili mema kwa jamii.

Manchester, Uingereza - Kocha mkuu wa timu ya Man United, bwana Alex Ferguson, amepiga marufuku shereha zote hasa wakati wa Kri-Max, zinazo husisha klabu na wachezaji bila viongozi kuwepo.
Akiongea na wachezaji wake , kocha Alex Ferguson, alionya na kusema hatavumilia tena kitendo hicho na anawapiga faini wachezaji wote walio kuwepo kwenye sherehe hiyo.
Onyo hilo limekuja baada ya kujulina yakuwa wachezaji hawa walikwenda kwenye sherehe hiyo bila wake zao, wala marafiki zao wa kike,bali waliandaliwa wadada wapatao 100, kuwapoza na kuwastaresha.
Katika sherehe hizo, wachezaji walilewa na kufanya vitu vya ajabu, na mmmoja ya wachezaji wa timu hiyo, anachutumiwa kwa kumjamii mwanadada wakati wamelewa.
Pichani anaonekana kocha Alex Ferguson akiongea na vijana wake,na picha nyingine wanaonekana baadhi ya wachezaji nyota wa timu hiyo walio sadikiwa kuwepo kwenye sherhe hiyo.
Mwamuzi wa zamani wa soka (The Sheriff) Upara apewa ulinzi .
Rome, Itali - Mwamuzi wa zamani na maarufu duniani katika mchezo wa soka, au mpira wa miguu, bwana Pierluigi Collina ameongezewa ulinzi na polisi baada ya kupata tishio.
Hali ya vitisho imekuwa ikizidi, na zimekuwa zikiongezeka kwa kupita mtandao wake.
Bwana Collina, ambaye amechaguliwa kuwa msimamizi wa wamuzi wa soka nchini Itali, ndiye anaye husika na upangaji wa wamuzi wa mechi zote za ligi daraja la kwanza na lapili nchini Itali.
Mwamuzi huyu wa zamani wa soka, au gozi la ng'ombe, bwana Collina au The Sheriff) mwenye upara, alikuwa maarufu kwa kujua kazi yake ya uamuzi wa soka, naalikuwa anaheshimika na wachezaji wote wa soka duniani.
Picha ya kwanza, anaonekana bwana Collina, akiwa amevalia mavazi ya kawaida baada ya kuacha kazi ya urefa miaka ya karibuni.
Picha ya pili anaonekana Pierluigi Collina, pamoja na wachezaji maarufu duniani walipo kuwa wakicheza mechi kwa ajili ya michango wa umoja wa Mataifa kusaidia Maendeleo.UNDP - Unated Nations Development Programme.
Picha ya tatu, anaonekana the Sharrif, Collina akimpa onyo mchezaji wa timu ya taifa ya Ujerumani Klose, baada ya kufanya manyago uwanjani.
Mchezaji anapo kosa maadili ya mchezo wa soka, basi kwa the Sheriff ( Upara) Collina alikuwa hana simile hata kiduchu, kadi nyekundu hukuonyesha, Fabian Barthez ahamini macho yake.
Naikiwa mchezaji hujisahahu, basi The Upara ( Sheriff) humkumbusha kwa kumuelekeza ya kuwa hii ni soka, na lazima ufate maadili yake.Hivyo anaonekana akimkumbusha mchezaji wa Argentina Gabriel Batistuta ya kuwa nakuona mwenendo wako uwanjani hivyo kaa chonjo.
Wapenzi wa sadamu wasema watamkumbuka daima kiongozi wao, yupo miyooni mwao daima"Ni mwaka sasa watimia"
Awja, Iraq - Mamia wa wapenzi na wanchi walio kuwa wakimenda Saddam Hussein kama kiongozi wa nchini Iraq, walifanya maombelezi ya kumkumbuka kiongozi wao ambaye alinyongwa kwa kutumia kitanzi, 30/12/2006.Baada ya kukutwa na kosa la kukiuka haki za kibinadamu.
Maombelezi hayo yaliongozwa na viongozi wa jamii ya Kisuni pamoja na viongozi wa makabila,yaliuzuliwa na wanafunzi na watu wengine alipozikwa hayati Saddam Hussseni kwenye mjiwa Awja. Huku wakiombelza kwa kusoma Koran, mmoja wa ndugu wa familia ya hayati rais Saddam Hussein, bwana Ghalib Hammud,alisema yakuwa kiongozi hwao wapo pamoja naye kiroho na watamkumbuka kila mwaka.
Picha ya kwanza anaonekana kijana akiombeleza mbele ya picha na kaburi la rais Saddam Hussein.
Pichani anonekana enzi zake rais wa Iraq, Saddam Hussein akihutubia wananchi wa Iraq.
Picha ya pili wanaoneka mabwana wawili walimvisha kitanzi, Saddam Hussein, tayari kuaga dunia.
Picha ya tatu wanaonekana wanfunzi wa shule ya msingi wakiombeleza mbele ya kabuei la hayati rais Saddam Hussein.
Picha ya mwisho anaonekana rais Saddam Hussein, akisikiliza hukumu yake toka kwa jaji.
Dunia nzima yalia na mama asilia, Tsunami bado kuwa tukio la kutisha.
Java, Indonesia - Tukio kubwa ambalo walimwengu mzima ulisikitika na kushangaazwa kwa unyonge paka leo hii na jibu lake bado ni kitendawili kwa wana sayansi,dini na wahenga ni lile tikio la watu zaidi ya nusu million kupoteza maisha kwa kipindi kifupi, kwa ajili ya mgivu za mama asilia amabye alipewa jina la Tsunami.
Hivi karibuni wakazi wa maeneo ambayao yalikumwa na tsunami ya 26/12/2004 na duniani kote, na kuleta maafa makubwa kwa binadamu na mazimgira yake yaliadhimishwa.
Tukio hili la tsunami, lilikumba karibu kila jamii hapa duniani, hapo pichani juu wanaonekana wanachi wakitafuta sehemu ya kujificha kuepuka madhara ya maji yanayo kuja kutoka baharini.
Picha ya pili chini ni siku chache baada ya tsunami kuleta madhara, na picha nyingine wanaonekana wakina mama wakilia kwa uchungu baada ya kuona madhara ya tsunami.Pcha ya chini wanoneka baadhi ya watu waliokuwepo kwenye ufukwe wa bahari,hawamini wanacho kiona kwani ilikuwa ghafla bahari imepandisha maji kwanguvi hadi kwenye nyumba zao.
Kijana wa miaka 19, apewa kazi ya kufuata nyayo za mama Bhotto.
Rawalpindi, Pakistani - Chama cha - PPP ( Pakistani Peoples Party) kilicho kuwa kikiongozwa na marahemu bi Benazir Bhutto, kimefanya uteuzi wake mpya wa uongozi.
Katika mkutano huo ambao ulikuwa namadhumuni kumchagua kiongozi wa chama hiki (PPP) na kuangalia ni jinsi gani watashiriki katika uchaguzi
Kwa pamoja uongizi wa chama cha PPP, umepitisha bila kipingamizi ya kuwa mtoto wa marehemu bi, Bhutto kuwa kiongozi wa chama cha Pakistani People Party na kukubali kushiriki katika uchaguzi ujao, na kuomba vyama vyote vya upinzani kushiriki katika uchaguzi huo.
Akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari, bwana wa bi Bhutto, bwana Zardari, alisema ya kuwa mtoto wao wa kiume, bwana Bilawal Bhutto Zardari,ndiye atakeye kuwa kiongozi wa chama hicho.
Bilawal Bhutto,mwenye miaka 19, ambaye bado nimwanafunzi wa chuo cha Oxford nchini Uingereza,amesema yakuwa kwa sasa,baba yake ndiye atakaye kuwa akiongoza chama hiki katika shughulizake za kila siku, mpaka hapo atakapo kuwa tayari kukiongoza chama hicho. Bilawal alizaliwa mwezi mmoja kabla ya marehemu mama yake kuchaguliwa kuwa waziri mkuu wa Pakistani mwaka 1988, alipewa jina hili lenye maana ya kuwa hakuna wa kulingana naye.
Pichani anaoneka , mume wa marehemu bi, Bhuotto ,bwana Asif Ali Zardari, akiongea na waandishi wa habari,na picha nyingine anaonekana bwana Bilawal ambaye ndiye kiongozi mkuu wa chama cha PPP.
Balozi wa Tanzania ajeruhiwa vibaya na majambazi na kuporwa vitu.
Pretoria, Afrika ya Kusini - Aliyekuwa balozi wa Tanzania nchini Afrika ya Kusini, bwana Emannuel Mwambulukutu, amjeruhiwa vibaya na majambazi waliovamia ubalozi wakati wa sherehe za kumuaga balozi huyo na familia yake.
Tukio hilo lilitokea mida ya saa mbili usiku wa tarehe 29, na hali ya balozi Mwambulukutu,inasemekana ya kuwa bado siyo nzuri.
Hata hivyo polisi wamesema ya kuwa wamemkamata mtu mmoja ambaye anashukiwa mmoja ya watu walio kuja kuvamia na kuleta maafa makubwa kwenye ofisi za ubalozi.
Pichani anaonekana balozi Mwambulukutu, akiwa kazini.
Uchaguzi wa Kenya, matokeo yaleta utata, Mwai Kibaki awa rais tena wa Kenya.
Nairobi, Kenya - Matokeo ya uchaguzi nchini Kenya, hatimayake yamepatikana, rais Mwai Kibaki, apita tena kuwa rais wa Kenya kwa kipindi kingine cha miaka mitano. Rais Kibaki inasemekana amemshinda mpinzani wake mkuu bwana Raila Odinga kwa kiasi kidogo cha kura zote zilizopigwa.
Matokeo haya ya uchaguzi yalimpa bwana Kibaki kura zipatazo 4,584,721 zidi ya bwana Odinga.
Bwana Mwai Kibaki, aliapishwa kuwa rais wa Kenya, mara tu ya kutangazwa mshindi, nainadadikika ni kati ya dakika sitini baada ya matokeo, bwana Kibaki akikabidhiwa ofisi kama rais wa Kenya.
Hadi kufikia leo jiono hali ilikuwa ya hatari, na vyombo vya habari vyote vimefungwa na hakuna matangazo ya yaina yoyote ya luninga, hii ni kwa ajili ya manufaa kwa taifa msemaji mmoja wa serikali alisema.
Pichani, anaonekana bwana Mwai Kibaki, akipokea biblia,tayari kula kiapo kama rais wa Kenya.
Chini ni picha ya bwana Raila Odinga, akiongea na waandishi wa habari kuhusu hali halisi ya uchaguzi nchini Kenya, nakudai kuwa bwana Mwai Kibaki na chama chake wameiba kura, na kutaka kura ziridiwe kuhesabiwa.
Chini anaonekana rais, Mwai Kibaki akiongea baada ya kuapishwa kuwa rais.

Friday, December 28, 2007

Bi, Benazir Bhutto, aaga dunia kwa imani aliyokuwa akiitetea

Bi, Benazir Bhutto,aaga dunia kwa imani aliyokuwa akiitetea.

Rawalpindi, Pakistan - Aliyekuwa waziri mkuu wa zamani wa Pakistan na kiongozi wa chama cha (PPP) Pakistani Peoples Party, bi Benazir Bhutto, amefariki dunia tarehe 27/12/07, kutokana na majeraha ya risasi yaliyo mpata kwenye shingo na begani.
Tukio hili lilitoke wakati bi, Bhutto alipo maliza kuhutubia mkutano wakampeni ya uchaguzim kwenye mji wa Rawalpindi.
Inaaminika bi, Bhutto alikumbwa na janga hili, baada ya mlipuko mkubwa wa bomu kutokea karibu na gari yake aliyokuwemo ndani, nandipo mjitolea muhanga mmoja alipo fyatua risasi na kumpiga bi Bhutto, na yeye mjitolea muhanga kujiua kwa kujilipua na bomu.
Bi, Bhutto alikimbizwa hospitali, lakini titihada za madakitari kuokoa maisha yake hazikifanikiwa.Bi, Bhutto alikuwa kiongozi wa upinzani ambaye alikuwa anatarajiwa yeye na chama chake kushinda kwenye uchaguzi utakaofanyika mapema januari, picha nyingine anaonekan bi, Bhutto akishuka ngazi kutoka jukwaani baada ya kumaliza mkutano
Pichani anaonekana bi,Benazir Bhutto akiwaaga wapenzi na wanachama wake baadaya kumaliza kampeni za uchaguzi.
Hapo kati anaonekana bi, Bhutto akiwa na Malkia Elizabeth wa Uingereza, alipombelea Malkia wakati akiwa kama waziri mkuu wa Pakistani.
Pichani ni Wapenzi na Wanachama wakilia kwa uchungu baada ya kupata habari ya kuwa bi Bhutto ametutoka.
Pichani linaonekana jeneza la bi, Bhutto likipokelewa kutoka hospitali tayari kwa kuelekea nyumbani kwao kwa mazishi.Mola aiweke roho yake peponi "Amin."
Uchaguzi nchini Kenya,demokrasi yatafutwa kwa kila njia."Mungu Ibariki Afrika"
Nairobi, Kenya - Harakati za uchaguzi nchini Kenya zimefika tamati huku wagombea wote wa vyama vilivyo shiriki vikiwa na matumaini makubwa ya kushinda.
Hata hivyo hali ya viti ya ubunge vimekuwa na mageuzi makubwa, kwani kwa asilimia kubwa ,wale wote waliokuwa wapo kwenye serikali ya rais Kibaki wameshindwa kupita tena, na hii ina ashiria ya kuwa hata kama rais Kibaki ata shinda kiti cha urais, basi atakuwa nawakati mgumu kimaamuzi.
Kutokana na wachunguzi wa mambo ya kisiasa, wansema ya kuwa uchaguzi wa Kenya umekuwa na vitisho vingi na vurugu za kila namna kutoka kambi zote za upinzani, nahata kufikia baadhi ya watu kupoteza maisha au kujeruhiwa.
Hadi sasa bado kura zinahesabiwa na wanchi wa Kenya wanasubiri kwa hamu kuona kama kura zao zimelenga walipo chagua.
Pichani anaonekana bwana Laira Oginda, akiwa na wanachama wenzake kuelekea kwenye kampeni za uchaguzi.
Chini inaonyesha jinsi gani, uchaguzi nchini Kenya unavyokuwa wa hatari, mpaka mapanga huhusishwa katika uchaguzi.
Pichani anaonekana mama Yoyo akipiga kura yake, je safari hii watakumbukwa?
Picha chini anaonekana bwana Mwai Kibaki akimsalimia mmoja ya wazee wakati wa kampeni.
Kitendawili cha mafuta, bado kupatiwa jibu na rais mpya wa Nigeria.
Lagos, Nigeria - Kulikuwa na mshtuko mkubwa ndani ya jiji la Lagos, baada ya moto mkubwa ukiambatana na moshi mzito na mweusi, huku kelele za watu zikisikika, karibu na bomba moja la kupitishia mafuta ya aina ya petrol,haya ni maneno ya mmoja ya watu walioshudia tukio hili.
Mlipuko huu ulio chukua upna wa mita zipazo nusu uwanjwa wa mpira, ulijeruhi watu wengi nawengine kupoteza maisha yao baada ya kuungua vibaya na moto huu.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, watu hawa walio ungua na kufariki dunia walikuwa wana chukua mafuta kutoka kwenye bomba hilo, amablo linasadikiwa lilitobolewa kwa makusudi.
Hata hivyo baadhi ya watu walisikika wakisema, hii inatokana na ukame na upungufu wa bidhaa hii,amabyo nchi yao no ya saba dunia katika utoaji wa bidha hii ( mafuta).
Hili sio tukio la kwanza, kwani Wanchi wa Nigeria wamekuwa wakipoteza maisha kutokana na matukio haya ya kuchukua mafuta kutoka kwenye mabomba yaliyo toboka.
Pichani juu wanaonekana polisi wakiangali magalono amabyo hutumiwa kichukulia mafuta haya,picha nyingine anaonakana rais mstahafu wa Nigeria bwana Obasanjo akishuka kutoka kwenye gali, naambaye alimkabidhi kibarua kizito rais wa sasa wa Nigeria bwana Amuru Yar Adua ambaye picha yake ipo chini ya Obasanjo.
Picha ya mwisho inaonjesha moja ya mitaa, ambapo mafuta yanapo tokea au kuchimbwa, lakini hali ya wazawa bado kitendawili.
Wafaransa waota joto la jiwe la jela ya Afrika"Kazi ngumu Pilato asema"
Ndjamena, Chad - Serikali ya Chad imewahukumu wafaransa sita kwenda jela miaka nane na kazi ngumu , kwa kosa la kukutwa na hatia ya kutaka kusafirisha watoto kinyume cha sheria.
Hukumu hiyo ilitolewa siku ya jumatano zidi ya wafaransa hao, hata hivyo siku ya ijumaa serikali ya Ufaransa imeiomba serikali Chad ya kuwa wafaransa hao waruhusiwe kwenda kutumikia kifungo chao nchini Ufaransa.
Hata hivyo serikali ya Chad bado inafikiria ombi hilo.Tukio hilo la kutaka kusafirishwa kwa watoto hao lilileta mtafaruku mkubwa saana kati ya jamii ya Wafaransa na Wachad. Picha juu anaonekana rais wa Chad, bwana Idriss Deby akiongea na watoto alipo kwenda kuwatembelea.
Picha ya kati anaonekana Eric Breteau, mwanzilishi wa Merikebu ya NOA,akiwa na wafanyakazi wenzake ndani ya lupango nchini Chad.
Picha ya mwisho chini anaonekana mmoja wa watuhumiwa akielekea kwa Pilato kula kigungo.
Ebola kukung'utwa kabisa ifikapo 2008"Wizara ya Afya Uganda"
Kampala, Uganda - Serikali ya Uganda, iko katika hatua za mwisho kupmabana na ugonjwa wa Ebola.
Akiongea hivi karibuni kwa niaba ya wizara ya Afya, bwana Sam Okware, alisema ya kuwa idadi ya watu wenye kukumbwa na virusi hivi, imepungua hasa kwenye maeneo amabyo yalikuwa yamekumbwa na ugonjwa huu.
Hadi hivi sasa hatujapata habari za kifo kuhusiana na ugonjwa huu, bado tunachunguza kwa makini kujua kama kweli tumefanikiwa kukabiliana na ugonjwa huu, hivyo hadi kufikia januari 12, tutapata huhakika kamili , alimalizia kwa kusema haya.
Picha juu ni bendera ya Uganda yenye ngede mzuri, na picha nyingine inaonyesha mandhari ya milima iliyopo sehemu ambazo zilivamiwa na ugonjwa ebola, na wanao taabika hasa ni watoto amabo wanonekana wakingojea jebu kwa kinga.

Monday, December 24, 2007

The, Hugo Chavez, kuwa mkombozi wa watekwa nyara nchini Kolombia?

Kizuri hukumbukwa siku zote, wapenzi kukongwa na kumbukumbu.

Stocklohm, Sweden - Lile kundi maharufu la muziki duniani, hasa katika miaka ya "arobaini saba" the ABBA GROUP, watafungua jumba lao la kumbukumbu mjini Stockholm ufikapo mwaka 2009.
Jumba hilo la kumbukumbu, litakuwa na vyombo vya muziki walivyo tumia enzi zao, nguo na picha mbalimbali walizopiga na washabiki(wapenzi wao) wakati walipo kuwa pamoja na kutikisa roho za walimwengu na kwakukonga mioyo kwa nyimbo zao Fernando, money nakadhalika. Kundi hili la ABBA, lilikuwa ni Bjorn Ulvaeus, Benny Anderson, Agnetha Faltskog na Anni Frid Lyngstad.
Akiongea haya, afisa anaye simamia mradi huu, Ulf Westeman na mkewe bi Ewa Wigenhem Westen, alisema, watu watakao tembelea jumba hili la kumbukumbu za ABBA, wataru kutumia studio kujaribu kumba na kujikumbusha enzi hizo.
Pichani wanaonkana kundi la ABBA, wakiwa wamekula pozi enzi zao, picha nyingine wanaoneka the ABBA, wakiwa na mmoja ya washabiki wao.
Picha ya chini wanoneka the ABBA GROUP wakifanya vitu vyao miaaaaaaka hiiyo ya 47.
Mama Afrika, achaguliwa bila kupingwa, mama bado ni nguzo ya chama."ANC"
Polokwane, Afrika ya Kusini -Mama mwana mapinduzi, mpigania haki za binadamu ,na mmoja wa kiongozi aliyeongoza kupinga ubaguzi wa rangi usidumu milele nchini Afrika ya Kusini bi Winnie Madigizela Mandela, amerudi tena katika ngazi za juu za za uongozi za chama cha ANC, ambacho ndiyo chama tawala nchini Afrika ya Kusini.
Bi, Winnie Madigizela Mandela, alishinda kura zipatazo 2,845 za wanachama waliopiga kura amabo walikuwa 3,603.
Hata hivyo bi Winnie, alisikika tena , baada ya kutaka kusuhurisha mgogoro uliopo katai ya kambi ya rais Thabo Mbeki, mwenyekiti wa sasa wa ANC, bwana Jacob Zuma.
Pichani anaonekana bi Winnie Mandela akihutubia hivi karibuni, na chini nim picha ya bi Winnie enzi hizo za kampeni, kupinga ubaguzi wa rangi.
The Hugo Chavez , kuwa mkombozi wa watekwa nyara nchini Kolombia?
Havana, Kuba - Rais wa Venezuela,bwana Hugo Chavez, ameseama ya kuwa ule mpango wa kusimamia kuachiwa kwa mateka waliotekwa na jeshi la upinzani la Kolombia FARC hutakamilika hivi karibuni.
Akizungumza baada ya kuudhulia mkutano mjini Havana rais Hugo Chavez, alisema mpango huu hupo njiani na karibuni mateka wote wataachiwa.
Aliongeza ya kuwa mpango huu ni mgumu, kwani wapo baadhi ya viongozi wa serikali hapendi kufanikiwa kwa kuachiwa kwao, na wapo vile vile majeshi ya serikali ambayo yapo tayali kuvuruga mpango huu.
Ikiwa mopango huu ukifanikiwa, basi utazidi kuleta kindumbwembwe kati ya serikali ya Kolombia na Venezuela.
Picha hapo juu ni picha ya kuchora ya rais Hugo Chavez na picha ya kati anaonekana rais Hugo Chavez alipo kuwa akuhutubia umoja wa Mataifa hivi karibuni.
Picha ya mwisho anaonekana rais Chavez wakati wa kampeni ya kuhimiza watu wakubaliane na mabadiliko ya kisasa na kiuchumi nchini Venezuela.
Hezbollah kuzuia maoni ya rais Bush?Hali bado ya utata nchini humo.
Beiruti, Lebanon - Kikindi cha Hezbollah, kimepinga kabisa mawazo yaliyo tolewa na rais wa Amerika bwana Georgr Bush.
Hii inakuja baada ya Lebanon, kukaa kwa kipindi kilefu bila kuwa na serikali kamili itakayo kuwa chini ya rais ambaye mpaka sasa hajachaguliwa kutokana na mivutano ya kisisa kati ya makundi yanayo kubalika na Alaya na Amerika na yale yanayo sadikika ya kubalika na Syria.
Akiongea haya, kiongozi msaidizi wa kundi la Hezbollah, Sheikh Naim Kassem, ya kuwa mambo yote yaliyo zungumzwa na rais Bush, hayatakubalika na kutimizwa.
Pichani ni picha ya rais Bush, amabye anatarajiwa kutembela Mashatiki ya kati hivi karibuni.
Hapo juu ni picha ya bendera ya kundi la Hezbollah, ambalo lina nafasi kubwa kinguvu nchini Lebanoni.
Nguvu zaidi kwa jeshi la AU, Somali bado kasheshe kwa wote.
Mogadishu,Somalia - Katika harakati za kuleta amani na utulivu chini Somali,jeshi la AU ( African Union) limepata nguvu, baada ya nchi ya Burundi kutuma wanajeshi wasiopungua 100.
Kuwasili kwa wanajeshi hawa 100 wa Burundi,ambao walikutana na mashambulizi ya vita kati ya jeshi la serikali na wapinzani wa serikali ya Somalia
AU inawanajeshi wasiopungua 1,600 wengi wao ya wanajeshi wanatoka nchini Uganda,hata hivyo Au inatakiwa kuwa na wanajeshi 8,000 ili kukabiliana na hali mbaya iliyopo nchini Somalia.
Pichani anaonekana mmoja ya mwannchi wa Somalia, akiwa hospitali huku hali yake kiafya ikiwa dhofu li hali na huku akiwa na majeraha kungoja matibabu.
Pichanyingine anaonekana askari wa jeshi la AU, akila doria karibu na ufukwe wa pwani wa bahari ya India nchini Somalia.
Irani yawa joto ya jiwe, kwa mashushu wa nje na ndani ya nchi.
Tehrani, Iran - Ufualiaji wa kujua wapi mmoja ya wafanyakazi wa FBI, bwana Robert Levinson, umefika hatua ya kukatisha tamaa.
Akiongea hivi karibuni , mke wa bwana Bob, alisema imekuwa vigumu kujua yupo wapi?Kwani hapa nilipo nina machungu na majonzi.
Bwana Robert Levinson, aingia nchini Irani kibiashara, namara ya mwisho alionekana kwenye maeneo ya Kish Island kwenye Ghuba ya Persia.
Na hivi karibubi serikali ya Irani, ilimfungulia mashitaka aliyekuwa msamaji wa serikali ya Iran kuhusu maswala ya Nuklia, bwana Hossein Moussa, kwa kuwa mpelelezina kutoa habari kwa serikali za nje.
Pichani wanaonekana mke wa bwana Robert Levinson na mtoto wake wakongea na waandishi wa habari hivi karibuni miji Terhani,
Hapo juu ni picha ya bwana Houssen Moussa, amabye inasadikiwa alikuwa mpelelezi wa serikali za nje.
Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza, awa muumini"Mungu mkubwa"
Vatican City,Vatican - Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza bwana Tony Blair, amebatizwa tena na kuwa muhumini wa jumuia ya kanisa la Katoriki.
Bwana Blair, ambaye alikuwa hapendelei kuongelea hadharani maswala ya imani na dini yake wakati wa uongozi wake wauwaziri mkuu wa Uingereza.
Hata hivyo bwana Blair, amabye alikuwa ni muumini wa kanisa la Uingereza Agrikani.
Bwana Blair na familia yake walikuwa wanonekana manr kwa mara kuhudhulia misa za kanisa la Katoriki.
Akitangaza, mbele ya waumini wengine, Kardinal Cormac Murphy O Connor, ambaye ndiye kiongozi wa Katoriki wa Wales na Uingereza, alisema tunamkaribisha bwana Tony Blair na familia yake katika familia ya Kikataoriki.
Sala pamoja na maombi yetu yapo pamoja na familia yake.
Pichani anaonekanabwana Tony Blair, akiaga wakati alipo kuwa namalizia kipindi chake cha Uwaziri mkuu wa Uingereza.
Picha nyingine anaonekana bwabna Tony Blair, akiwa na Papa Benedict XVI, mapema mwaka huu.
Shutuma za rushwa bado moto, uchaguzi moto,kusafiri marufuku"Uingereza"
London, Uingereza - Serikali ya Uingereza, imeweka vikwazo vya usafiri kwa mawaziri wa serikali ya Kenya ianyaongozwa na rais Mwai Kibaki nawatu wake wote waliopo karibu na uongozi wake kwa tuhuma za rushwa.
Ofisi ya ubalozi wa Uingereza iliyopo nchni Kenya , imeagiza mashirika yote ya ndege ya yaendayo Ulaya kutowachukuwa viongozi hawa, wakiwemo mawaziri watatu na waziri za zamani wa fedha bwana David Mwiraira na bwana Nicholas Biwott.
Hata hivyo serikali ya Uingereza, imesema vikwazo hivi haviingiliani na hali ya uchaguzi utakaofanyika hivi karibuni.
Hata hivyo msemaji wa serikali bwana Alfred Mutua, alikataa kuongele swala hili, alipo ulizwa na wahandishi wa habari.
Pichani anaonekana aliyekuwa waziri wa zamani wa faranga wa Kenya bwana, Davd Mwiraira, ambaye ndege za UK, kawekewa ngumu,
Ndege aina ya Jet kununuliwa, Uganda yawa na jet mbili za rais?
Kampala, Uganda - Serikali ya Uganda imepitisha bajeti ya kununu ndege aina ya jet kwa ajili ya matumizi ya rais.
Akiongea kuhusu swala hili , kiongozi aliyesimamia uamuzi huu bi Mary Karooro Ukurut,alisema ndege hii itagahalimu kiasi US $dolla 48million.
NDege hii aina ya jet ni ya pili kununuliwa na serikali ya Uganda, baada ile ya kwanza iliyo nunuliwa US$35millionmwaka 2000, kwajili ya matumizi ya rais,nawakati huhu serikali ilikuwa inatafuta mikopo kutoka mashirika ya fedha ya kimataifa, hii ilileta mvutano mkubwa .
Hasa baada ya IMF kuuliza ya kuwa,inakuwaje nchi za kimasikini kukua ndenge za gharama, wakati bado zinadai zifutiwe maden?
Hapo juu, anaonekana rais Yoweri Kaguta Musen, akiongea hivi karibuni kwenye moja ya mikutano nchini Uganda.
Picha nyingine inaonekana picha ya jet, ambayo iatanunuliwa na serikali ya Uganda kwa ajili ya matumizi ya rais.