Wednesday, April 16, 2008

Tuache kutumia pesa za Amerika, US $ dollar,tuanzishe benki zetu,rais wa Iran.

Nyota ya sinema ya big mama, atimiza miaka 43 ya kuzaliwa.

Holly Wood, Los Angels - Masani maarufu duniani Lawrance Martin, leo ametimiza miaka 43 tangu kulzaliwa.
Martin Lawrance, ambaye alizaliwa tarehe 16/4/1965, nchini Ujerumani Frankfrut,ametokea kuwa msanii maarufu ambaye amecheza sinema nyingi, na vilele amecheza sinema na wasanii kama,Willy Smith na wasinii wengi duniani anasifika kwa kuchekesha saana hasa hawapo jukwaani.
Pichani anaonekana akiwa anafanya vitu vyake kwenye sinema ya big momma.
Picha nyingine anaoneka,Martin Lawrence,akiwasalimia baadhi ya washabiki wake.
Hapo juu anaonekan Martin Lawrence, akiwa ametana shati.
Vatican haitaruhusu vitendo vingine vya aibu kutokea"Pope"
New York, Amerika - Pope Benedict, amewasili nchini Amerika kwa ziara rasmi,ili kuimarisha uhusiano kati ya serikali ya Amerika na Vatikani.
Kufanyika kwa ziara hii ya Pope Benedict kumetonesha donda kwa baadhi ya watu ambao, wanadai yakuwa,baadhi ya watumishi wa kanisa hili la Katoliki kutuhumiwa kuwalawiti baadhi ya waumini wao.
Pope Benedict , alihaidi atahakikisha ya kuwa Vaticani haita ruhusu tena hali hii kutokea.
Hata hivyo,Pope Benedict, atarajiwa kuzungumzia swala hili na swala la Iraki,pindipo watakapo kutana na rais wa Amerika bwana George Bush.
Na wakati huo huo, Pope Benedict, atasherekea siku yake ya kuzaliwa kwenywe Ikuru ya Amerika, sherehe hizi zimeandaliwa na George Bush,na inatarajiwa kuhudhuriwa na watu wasiopungua 9,000
Picha anaonekana,Pope Benedict, akisalimia baadhi ya waumini waliokuja kuudhulia misa hivi karibuni.
Chini ni picha za Pope Benedict tangu alipo kuwa kijana na mpaka anatimiza miaka mwaka 81 leo.
Urusi yataka zidi kutanua misuri yake, Georgia yawa na homa.
Moscow, Urusi - Serilakai ya Urusi imetangaza ya kuwa itaanzisha uhusiano na majimbo ya Kusini mwa Ossetai ,na Abkhazia, yaliyopo Georgia.
Uhusiano huu na majimbo haya utakuwa wa kiuchuni, kijamii na pamoja na kisayansi mbinu.
Hata hivyo serikali ya Georgia, imesikitishwa na kitendo hicho, kwani imedai inakwenda kinyume cha sheria za kimataifa alisema waziri wa mambo ya nje ya Georgia bwana David Bakradze.
Pichani zinaonekana baadhi ya nguvu za serikali ya Urusi, zikionekana amabzo zinaipa homa nchi ya Georgia.
Hapa anaonekana rais wa Georgia,ametangaza ya kuwa atahakikisha yakuwa hali hii aita endelea.
Tuache kutumia pesa za Amerika, US dollar, tuanzishe benki zetu,
Teheran,Irani - Rais wa Iran, bwana Mohmoud Ahamadinejad amewataka wanachama wa OPEC, waache kutumia ($dollar), pesa inayo tumika nchini Amerika katika kufanya biashara.
Akiongezea, ameagiza ya kuwa lazima waanzishe benki itakayo milikiwa na wanachama na pesa zao.
Mvutano kati ya serikali ya Iran na Amerika umekuwa wamuda mrefu, na Iran kuungana na baadhi ya nchi kama, Venezuela, na Syiria,zinazo pingana na sera za serikali ya Amerika.
Wakati huo huo, serikali ya China imaeanza mazungumzo na serikali ya Irani na kwa kuongoza mazungumzo kuhusu swala zima la kuwepo kwa nyuklia na mitambo yake nchini Irani.
Mazungumzo haya yamekuja , baada ya serikali ya Iran kutangaza ya kuwa imewekeza zaidi viini vya nyuklia vipatavyo 6,000.
China ni nchi ambayo inafanya biashara na Iran, japo baadhi ya nchi za magharibi zimeweka vikwazo kwa serikali ya Irani.
Baadhi ya wananchi wa Irani wakiwa wameshikilia bango lenye picha za maris ambao wanapinga sera za nje za serikali ya Amerika.
Pichani hapo juu, wanaonekana marais wa Venezuela bwana Hugo Chavez na Iran bwana Mahmoud Ahamadinejad wakionyesha ushirikiano wao ulivyo komaa.
Picha nyingine wanaonekana rais wa Syiria bwana, Bashar al Assad na rais wa Irani, Mohamoud Ahamadnejad walipokutana hivi karibuni.
Picha nyingine wanaokena baadhi ya wajumbe wa serikali ya China na Iran walipo tia saini baadhi ya mikataba ya kibiashara hivi karibuni.
Ajali ya ndege, nchini Jamuhuri ya Kongo, yaleta wasiwasi kuhusu ubora wa ndege .
Goma, Jamuhuri ya Kongo - Serikali ya Jamuhuri ya Kongo, imetangaza ya kuwa ajali ya ndege iliyo tokea mjini Goma,imesababisha zaidi vifo vya watu wasiopungua 40 kupoteza maisha yao.
Ndege hiyo ambayo inasemekana ya kuwa ilipata itilafu kwenya tairi lake moja, ambolo inaaminika ndiyo chamzo cha ajalihiyo.
Kutokana na ajari hii, kutokea hivi karibuni, kuna leta wasiwasi kuhusu hali nzima ya usalama wa ndege hizi, kwani kampuni inayo miliki ndege hizi ijulikanayo kama Hewa Bora, ni moja ya kampuni ambayo imefungiwa na mashirika ya kimataifa kwa ndege zake kutumika kwenye anga za kimataifa.
Pichani hapo juu wanaonekana baadhi wenye huruma wakiwa katika harakati za kuwaokoa watu ambao wamo ndani ya ndege hii iliyo pata ajali.
Picha nyingine, inaonekana sehemu ya ndege hii ambayo imepata ajali, na kuuwa zaidi ya watu wasiopungua 40.

Sunday, April 13, 2008

Kenya yaweka rekodi ya dunia kwenye karne ya 21, kwa kuwa na baraza kubwa la mawaziri.

Je wapenzi wa Nou Camp kukusa uhondo wa Kibrazil na kuhamia Itali?

Milan , Itali -Aliyekuwa mchezaji bora wa dunia Ronadinho kwa upande wa soka, (kabumbu) ambayeni mchezaji wa timu ya taifa ya Brazil na Barcelona, amekubali kimsingi kuamia timu ya AC Milan ya Itali, kwa mujibu wa wakala wake, ambaye ni kaka ya mchezaji huyu bwana Robert de Assis.
Ronadinho mwenye miaka 28, amekuwa na wakati mgumu kwenye uwanja wa Nou Camp, kutokana ma maumivu ya liyo mkumba kwa kipindi kisicho pungua miezi michache iliyopita.
Picha hapo juu anaonekana Ronadinho akiwa unjanjani anafanya vitu vyake.
Ron akama anavyo julikana kwa mavitu ya kuchezea mpira kama kwa wake wanao jua kula samaki mwenye miiba mingi mdomoni , anaonekana akiwa ndani ya jezi ya Basca.
Picha nyingine wanaonekana manyota wa soka wa dunia Zinedin Zidane kushoto na Ronadinho kulia wakigombania gombe la gozo wakati timu hizo zilipo kutana.
Kenya yaweka rekodi ya dunia kwenye karne ya 21,kwa kuwa na baraza kubwa la mawaziri.
Nairobi, Kenya - Mgogoro wa kisiasa nchini Kenya, umefikia tamati baada ya rais Mwai Kibaki kutangaza baraza jipya la mawaziri wapatao 40.
Kiongozi wa chama pinzani bwana Raila Odinga, amechukua nafasi ya waziri mkuu, wizara ambayo imeanzishwa ili kugawana madaraka.
Baraza hili litajumuisha vyama vya upinzani , hata hivyo baraza hili limepokelewa kwa hisia tofauti na wananchi wa Kenya.
Pichani hapo juu wanaonekana waziri mkuu mpya , Raila Odinga na rais Mwai Kibaki wakipongezana baada ya kutangaza baraza la mawaziri.
Picha nyingine anaonekana rais Mwai Kibaki akitangaza baraza la mawaziri mbele ya waandishi wa habari.
Waziri wa zamani wa Itali kurudi madarakani?
Rome, Itali - Wananchi wa Itali wameanza na kupiga kura kuwachagua kuchagua wabunge wa bunge la Itali.
Uchaguzi huu unafanyika wakati viongozi wa wanao tazamiwa kuchuana vikali ni aliye kuwa waziri mkuu wa zamani wa Itali bwana Silvio Berlusconi na Veltroni.
Hata hivyo wachunguzi wa maswala ya kisiasa wanasema huenda bwana Berlusconi akarudi madarakani ikiwa chama chake kitaongoza.
Pichani anaonekana Veltroni akihutubia wakati wakampeni za uchaguzi.
Picha nyingine anaonekana waziri mkuu wa zamani wa Itali akiwa anongea na waandishi wa habari hivi karibuni.
Serikali ya Libya yatoa msamahaa kwa wapinzani walio taka kumtoa Muhamar Gaddaf miaka ya 1995.
Tripol, Libya - Serikali ya Libya imewaachia zaidi ya watu wapatao 90, ambao wengi wao ni wanachama wa Islamic Group, chama ambacho kinapingana na serikali inayo ongozwa na rais Muhamar Gaddaf.
Kuachiwa huko kumesaidiwa na chama kisicho cha kiserikali kinacho ongozwa kaka wa rais wa Libya.
Chama hiki ambacho kiliibuka mwaka 1995, kikiwa na madhumini ya kumtoa madarakani rais wa Libya Muhamar Gaddafi.
Pichani wanaonekana baadhi ya wafungwa ambao wame achiwa hivi karibuni.
Wanachi wa Rwanda wakumbuka siku ya mauaji ya vita vya wenyewe vya kikabila vilivyo tokea 1994.
Kigali, Rwanda - Wananchi wa Rwanda wameadhimisha hivi karibuni, kukumbuka vifo vya watu wapatao milion moja ambao walipoteza maisha yao wakati wa vita vya kikabila vilivyo zuka nchini Rwanda 1994.
Vita hivyo vya kikabila kati ya watu jamiii ya kihutu na kitutsi, wakati vita hivyo idadi kubwa ya waru jamii ya kitutsi kuuwa kinyama kwa kukwatwa na mapanga na siraha nyingine za jadi.
Vita hivi ambavyo vilichukua miezi mitatu na siku kadhaa, na vilikwisha baada ya kikosi cha jeshi la upinzani ( RPF ) Rwandise Patriotic Front kikiongozwa na rais wa sasa bwana Poul Kagame, kushinda na kukiondoa madaraka chama na MRND, kilicho kuwa kikiongozwa na hayati rais , Juvenail Habyalimana.
Pichani wanaonekana baadhi ya watuhumiwa waliohusika na mauaji vita wakiwa wamevalia magwanda ya serikali na kujenga nchi kwa kufanya kazi ya kilimo.
Picha nyingine hapo chini, anaonekana mmoja wa watuhumiwa akiwa anasikiliza makosa kwenye koti ya ijulikanayo kama Gachacha.
Picha nyingine, hapo nchini ni picha linaonekana moja ya fuvu la watu waliopoteza maisha yao wakati wa vita vya wenyewe vya kikabila nchini Rwanda.
Janga la njaa, laleta msuko suko na kiongozi wa nchi apigwa chini na bunge.
Port Au Prince, Haiti - Bunge la nchi ya Haiti limepiga kura na kukubaliana kwa pamoja ya kuwa waziri mkuu bwana Jacque Edouard Alexis kuondolewa madarakani.
Hii ina kuja baada ya kuzuka kwa huaba wa lishe au chakula na kuongezeka kwa huaba wa kazi.
Kufuatia hali hii ya kiuchumi kuwa mbaya, ilisababisha raia wa Haiti kuandamana na kupambana na wanajeshi wa wa jeshi la kumoja wa mataifa.
Pichani hapo wanaoneka wanainchi wa Haiti, wakiwa wamekaa chini kwa shahuku kubwa kwa kutaka kujua nini jeshi hili litafanya kuwapatia lishe na Kazi.
Lakini wanajeshi wa umoja wa Mataifa wapo nchi Haiti kwa ajili ya kulinda usalama.
Hali ya utata kuzuka na kuwacha watu kuwa na butwaa baada ya bomu kulipuka msikitini.
Teheran, Iran - Kusini mwa Iran kwenye mji ujulikanao Shiraz, kumetokea mlipuko wa bomu ndani ya msikiti na kusababisha vifo vya watu 11.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, alisema ya kuwa, mlipuko huo umetokana na bomu la kutengenezwa kihuria au mabomu ya kutengenezwa nyumbani.
Hata hivyo kunahabari ya kuwa huenda vifo vya watu vikaongezeka.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya watu wakiwa wameshikwa na mshangaokuhusu tukio hili kutokea ndani ya msikiti.
Picha chini, linaonekana gari la kubeba wagonjwa likitoka kwenya sehemu ya tukio hili.
Wanaume watakiwa kufanyiwa kujitokeza zaidi kwa kuwa tayari kutairiwa.
Nairobi, Kenya - Katika kupambana na ugonjwa hatari wa ukimwi nchini Kenya, serikali ya nchi hiyo imeandaa mikakati ya kujaribu kupunguza kuenea kwa ugonjwa wa ukimwi kwa kutoa mafunzo ya kitaaluma kwa watumishi wake wate wanaohusika na kujua ni jinsi gani ya kutairi na kujaribu kuwaelimisha wananchi njia bora ya kujikinga na ugonjwa huu.
Picha hapo juu anaonekana baadhi ya wananchi wa Kenya wakiwa wamashikiria mabango kuhimiza serikali yao kuwapatia dawa wagonjwa walio athirika na ugonjwa wa ukimwi.
imepitishwa kisheria kutairiwa kwa wanaume, ikiwa ni njia moja wapo ya kupambana na ugonjwa.

Thursday, April 3, 2008

Waziri mkuu wa zamani wa Kosovo,hanahatia, mahakama ya mwachia huru.

Bi, Naomi awa matatani na polisi uwanja wa ndege mjini London.

London,Uingereza - Mwana dada, Naomi Campbell amekamatwa na polisi kwenye kiwanja cha ndege Heathrow.
Bi, Naomi, amekamatwa na polisi,baada ya kukorofishishana na polisi wakiwanja cha ndege.
Bi, Naomi aligombana na polisi, baada ya kupishana lugha na na polisi hawa kuhusu mizigo yake kwenye termimal 5.
Pichani za hapo juu anaonekana bi Naomi, akiwa amepozi wakati wa moja ya maonyesho ya sanii.
Umoja wa mataifa upo kwa ajili yakuleta amani na utuilivu duniani kote"asema katibu mkuu"
Bucharest, Romania - Katibu mkuu wa umoja wa mataifa bwana, Ban Ki moo, amesema ya kuwa umoja huu haupingi Uislam.
Bwana Ki moo, aliyaongea haya kwenye kikao cha NATO kinacho fanyika mjini Bucharest, na kupinga maneno ambayo ya meongewa na kiongozi na mbili wa Alqaida, bwana Ayman Al- Zawahir, ambaye amedai yakuwa umoja huu wa mataifa unashiriki katika kupiga vita Uislamu.
Aliongezea yakuwa umoja huu upo kwa ajili ya kuleta amani na utulivu duniani kote.
Bwana Ki moo, amealikwa katika kikao hiki kuongea na viongozi wa NATO, kuhusu maswala ya amani duniani,kwanai NATO , ni shirikisho lenye nguvu duniani.
Picha hapo juu anaonekana bwana, Ban Ki moo, akongea na waziri mkuuwa Uingereza kuhusu maswala fulani, huku akonyesha kwa vitendo kutumia mkono wake.
Chini ni picha ya kiongozi namba mbili wa kundi la Aqaida, bwana Ayman Al Zawahiri, akiongea kupitia mtandao.
Waziri mkuu wa zamani wa Kosovo, hanahatia, mahakama ya mwachia huru.
The Hague, Holland - Mmoja ya watuhumiwa wa vita vya Kosovo,bwana Ramush Haradinaj,ameachiliwa huru baada ya kesi dhidi yake kukusa ushaidi kamili.
Bwana, Ramush Haradinaj, ambaye alishawahi kuwa waziri mkuu wa Kosovo, aliachiwa huru , baada ya baadhi ya mashahidi kushindwa kutoa ushahidi dhidi yake kwa kuhusika katika viata vya wenyewekwa wenyewe ambavyo vilifanyika nchin Kosovo 1998.
Akiongea mbele ya koti , jaji Alphonss Orie, alisema ya kuwa imekuwa ni vigumu kumtia hatiani mtuhumiwa kwani ushahidi haukuwa wakutosha.
Kabla ya hapo wakili wa mahakama hiyo waliomba mahakama imuhukumu bwana Ramush Haradinaj kifungo cha miaka 25 jela, laki hata hivyo kutokana na ukosefu wa ushahidi imekuwa ni vigumu , alimalizia mmoja ya wanasheria wa mahakama hiyo.
Picha hapo juu kulia ni picha ya bwana Ramush Haradinaj, akitabasamu baada ya jaji kusema yakuwa hakuna ushahidi na hivyo hayupo hataiani.
Picha ya pili naonekana bwana Ramush Haradinaj,akiingia mahakamani wakati wa mwazo wa kuanza kesi dhidi yake.
Mtetezi wa haki za binadamu awekwa ndani na Pilato kwa kuongea.
Beijing, China - Mmoja wa watetezi wa haki za binadamu nchini China bwana Hu Jia, amehukumiwa kwenda jela kwa kipindi cha miaka mitatatu na nusu, kwa kosa la kuongea mambo amabyo serikali ya China haikufurahishwa nayo.
Bwana Hu Jia, amekutwa na hatia baada ya habari alizo ongea na waandishi wa habari, kuonekana kwenye (internet) au mtandao.
Bwana Hu Jia ,amekuwa mtetezi wa haki za binadamu nchini China ,na amekuwa akiongelea hasa swala la wagojwa wa ukimwi na matatizo yanayo wakuta wagonjwa hao nchini China.
Hata hivyo shirika la kuteteta haki za binadamu na mataifa ya magharibi yameiomba serikali ya Chnia kumwachia huru, bwana Hi Jia, kwani wanakiuka haki zabinadamu na haki za kila mtu kueleza au kutoa maoni yake.
Pichani hapo juu ni picha ya bwana Hu Jia kabala yakukamatwa kwake. Na picha nyingine anaonekana bwana Hu Jia alipo kuwa amewekwa kifungo cha ndani siku za nyuma
Imani za dini inapogongana na sheria alizo weka binadamu nani mkweli?
New-York, Umoja wa mataifa - Katibu mkuu wa umoja wa mataifa bwana Ba Ki- moo, siku ya ijumaa ya 28/3/ 2008, ameonya na kulani kitendo cha mmoja wa wabunge na kiongozi wa chama cha siasa bwana Geert Wilders kwa kitendo chake chakutaka kuonyesha picha za sinema ambazo zinahusisha Uislam.
Bwana, Ban Kim-moo, alisema yakuwa hali hii inahatarisha na inaleta mgongano wa kiimani katika jamiii. Na alieleza ya kuwa anafahamu ni kwa jinsi gani, serikali ya Holland ,inavyo jitahidi kuzuia sinema hii isionyeshwe.
Katibu mkuu huyu alisema hakuna sheria ambayo inayo ruhusu mtu kueleza maoni yake ambayo yanaweza leta maafa katika jamii, na hivyo lazima tuwe wangalifu na sheria hizi.
Bwana Geert Wilders, ametengeneza picha ya sinema ijulikanayo kama FITNA, ambayo imeleta mzozo mkubwa katika jamii ya wananchi wa Holland na Jamii ya waumini wa dini ya Kiislaam duniani.
Pichani hapo juu wanaonekana baadhi ya wananchi wakianadamana kupinga kuonyeshwa picha ya sinema ijulikanayo kama FITNA.
Picha ya pili anaonakana katibu mkuu wa umoja wa mataifa bwana Ban Ki moo, akiongea na wandishi wa habari hivi karibuni.
Picha ya tatu , ni picha ya bwana Geert Wilders, ambaye picha yake ya sinema ijulikanayo kama FITNA inagonganisha vichwa vaya watu.

Ufaransa yaanza mikakati ya kutaka kuachiwa kwa bi, Ingrid Betencourt's

WTA, Miami yaonyesha ya kuwa Serena bado kiboko kwa kila anaye kuja.

Miami, Amerika - Mwana dada Serena Williams, ameweza kuendelea kwenya mashindano ya tenis kwa upande wa wanawake (WTA) baada ya kufika nusu fainali.
Bi, Serena Williams, ambaye kufika kwake nusu fainali kumekuja baada ya kumnyanyasa bi Justine Henin.
Bi Serena, alishinda kwa pointi 6-2, 6-0, kwenye mpambano wa kukata na choka uliofanyika mjini Miami.
Bi, Justine Henin na bi Serena Williams wamekuwa wapinzani wa jadi tangu walipo anza kukutana kiprofecheni miaka isiyo pungua mitano iliyo pita.
Waziri mkuu ajiuzuru kwa kufuatwa na kashfa za mafaranga.
Dublin, Irland(Irish) - Waziri mkuu wa Irland ( Irish) bwana Bertie Ahern , amaetangaza ya kuwa atajiuzuru wadhifa wake ifikapo mwezi wa mei tarehe 6, baadha ya kudhuka kwa kashfa juu yake.
Bwana, Bertie Ahern mwenye umri wa miaka 56, anashutumiwa kwa kuchukua pesa kutoka kwa baadhi ya wafanyabishara kwa vipindi tofauti kati ta miaka ya 1989 na 1992.
Lakini bwana Bertie Ahern, amekanusha kashfa hii na kudai yakuwa hana hatia wa wasiwasi wa swala hili.
Hata hivyo, waziri Bertie Ahern, anasifika kwa kuinua uchumi wa kisiwa hiki cha Irish.
Pichani hapo juu anaonekana bwana Bertie Ahern akitangaza tarehe ya kujiudhuru kwake.
Picha ya chini anaonekana waziri, Bertie Ahern akwaaga baadhi ya watu aliokuja kusikiliza yale aliyo yasema.
Mambo si shwali tena nchini Somalia, wapinzani wateka baadhi ya maeneo.
Mogadishu, Somalia - Mapigano mapya yamezuka tena nchini Somalia, na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 19, mapigano hayo ambayo yamesababisha hali ya wasiwasi kurudi tena jiji Mogadishu.
Mapambano haya yaliongozwa na kundi la Islamic Courts Union, amablo pia limedai ya kuwa limeteka mji wa Baidoa na kuteka vifaa vingi vya kijeshi kutoka kwenye kundi la wanajeshi wa serikali.
Pichani wanaonekana baadhi ya wananchi wakiwa hawajui la kufanya , mmoja wa wapiganaji akiwa ameshikilia bunduki tayari kwa lolote litakalo tokea.
Wazimbabwe tuwepamoja kujenga nchi yetu, tuachane na siasa," Mfanya biashara aomba".
Harare, Zimbabwe - Baadhi wa wakazi wa jamii ya ulaya au wazungu ambao ni wazaliwa wa nchi ya Zimbabwe wamekuwa na maoni tofauti kuhusu hali halisi ya uchaguzi nchini humo.
Mmoja wa wakazi hawa bwana Mercer, ambaye ni mfanyabiashara, alisema ya kuwa inabidi sisi kama Wazimbabwe tuungana kujenga nchi yetu, na maswala ya siasa yasituvuluge vichwa vyetu, kwani siasa ndio chombo pekee ambacho siku zote kinaleta migogoro kataika jamii, na matatokeo yake hivi leo ni vikwazo kila kukicha , na juu ya vikwazo hivi ni vigumu kwetu kufanya biashara na ndio maana hatuagizi, wala hakuna wateja, kutokana na migogoro ya siasa.
Hivyo Wazimbabwe tujenge nchi yetu na kuwa pamoja.
Ufaransa yaanza mikakati ya kutaka kuachiwa kwa bi, Ingrid Betancourt's.
Bogota, Kolombia - Serikali ya Ufaransa na washiriki wake Spain na Uswisi wanafanaya mkakati wa kutaka kuachiwa kwa mwana siasa na mwanaharakati wa kutetea haki za binadamu, bi Ingrid Batancourt's, ambaye ameshikiliwa na wanajeshi wa kundi la FARC.
Kundi hili la FARC, linapingana na serikali ya Kolombia kwa kipindi kisicho pungua miongo miwili.
Bi Ingrid Betancourt's ambaye ana uraia wa Ufaransa na Kolombia, na alisha wahi kuwa mgombea wa Urais kipindi cha nyuma kabla ya kukamatwa kwake na waaasi wa FARC.
Kutokana na habari kutoka kwa ndugu na familia , zinasema yakuwa bi, Betancourt's anamatatizo ya kiafya na huenda yakahatarisha maisha yake.
Picha hapo juu anaonekana mama wa bi Ingrid Betancourt's , akiongea kwa uchungu na majonzi kuhusu hali ya afya ya mwanae bi Ingrid.
Picha nyingine anaonekana, bi Ingrid Betancourt's akiwa kwenye kambi ya wapinzani wa FARC , ambao wanamchikilia hadi sasa.
Picha ya chini anaonekana na mtoto wa bi, Ingrid Betancourt's, Lorenzo akiongea na waandishi wa habari kuhusu hali ya kiafya ya mama yake, ambaye amashikiliwa na waasi wa FARC.
Waumini wa dini ya Bodee, watafikishwa mbele ya Pilato kujibu mashitaka.
Beijing, China - Zaidi ya watu wasiopungua 1000, watafikishwa mahakamani katika jimbo la Tibeti, mapema mwezi wa mei mwaka huu. .
Mmsemaji mmoja wa serikali ya Beijing, amesema ya kuwa , watuhumiwa hawa wana husika na machafuku ya kisiasa na kijamii katika jimbo la Tibeti.
Mmsemaji huyo alisema ya kuwa machafuko haya yalikuwa yamepangwa na waumini wa dini ya Mabodee ambao wanaongozwa na Dalai Lama.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya waumini wa dini ya Bodee, wakiwa wanasoma vitabu vya dini yao.
Mvutano kati ya NATO na Urusi bado kitendawili, wapewa matumaini hapo baadaeye.
Bucharest, Romania - Shirikisho la Umoja wa Kijeshi la nchi za Ulaya (NATO) limekubaliana kwa pamoja ya kuwa nchi za Georgia na Ukreini kusubiri kuwa mwanachama wa shirikisho la NATO.
Hali ya uamuzi huu inakuja baada ya kuwekewa ngumu na nchi ya Rusia ( Urusi), kwani nchi hii ina ona ya kuwa nchi hizi kuwa mwanachama wa shirikisho hili litahatarisha usalama wa nchi ya Urusi, kwa kuzingatia nchi hizi zipo karibu na Urusi.
Hata hivyo baadhi ya wajumbe wa NATO wamesema nchi hizi zisiwe na wasiwasi ipo siku zitajiunga na shirikisho hili.
Vile vile Rusia ( Urusi) ina pinga mpango wa Amerika kuweka mizinga ya ke karibu na mipaka ya Urusi, ama nchi ambayo ipo karibu na nchi hii ya Urusi.
Picha hapo juu wanaonekana viongozi vinara wa NATO, waziri mkuu wa Uingereza bwa Gordon Brawn na rais wa Amerika bwana George Bush.