Saturday, August 29, 2009

AQ Khan ruhusa kutembea,kizuizi cha ondolewa.

Matuzi ya madawa tofatuti ndiyo chanzo cha kifo cha mfalme wa musiki wa pop.

Los Angeles,Amerika - 29/08/09. Wachunguzi wa kisayansi ambao walikuwa wanachunguza kifo cha aliyekuwa mfalme wa musiki wa pop, Michael Jackson, wamesema yakuwa kifo chake kilisababishwa na madawa ambayo alikuwa amemeza kwa ajili ya matibabu.
Baada ya uchunguzi wa mfalme huyo wa musiki wa pop, hayati Michael Jackson,kufanyika, alikutwa na na madawa ya aina ya midazolam,diazepam, au Valium; lidocaine,alocal anesthetic;na ephedrine.
Hata hivyo polisi , L.A .P.D., imesema bado wanaendelea na uchunguzi zaidi.
Picha hapo juu ni ya hayati, Michael Jackson, aliyekuwa binngwa na mfalme wa musiki wa pop,akiwa punguia mikono wapenzi wa muziki walio kuja kumuona enzi ya uhai wake.
Picha ya pili, anaonekana hayati, Michael Jackson, mfalme wa muziki wa pop, akitumbwiza jukwaani.
Meli ya siraha kutoka Korea ya Kaskazini ya kamatwa.
Dubai,UAE,- 29/08/09. Serikali ya Muungano wa nchi za Kiaraab, imesema ya kuwa imeikamata meli ya mizigo ambayo ilikuwa imebeba siraha kutoka Korea ya Kaskazini.
Habari kutoka serikali ya UAE zimesema, meli hiyo ya mizigo ilikuwa imebeba siraha zilizo kuwa zikielekea Iran.
Kwa mujibu wa habari hizo, ambazo zilipelekwa umoja wa Mataifa,na baadaye barua kutumwa Korea ya Kaskazini na Iran, zilisema UAE, ilikamata meli hiyo, kutekeleza sheria ya umoja wa mataifa wa kuiwekea vikwazo Korea ya Kaskazini.
Meli hiyo, ilikamatwa tarehe 14/08/09, ikiwa na siraha tofauti zilizobebwa na meli ya shirka la meli la Australia ANL.
Picha hapo juu, ni ya meli iliyo kamatwa na serikali ya UAE, ikiwa na siraha kutoka Korea ya Kaskazini.
AQ Khan ruhusa kutembea, kizuizi cha ondolewa.
Lahore,Pakistan - 29/08/09. Mwana sayansi ambaye anadaiwa ndiye kiini cha nchi ya Pakistan kupata sayansi ya utengenezaji wa nguvu za kinyuklia Abdul Qadeer Khan, amepewa ruhusa ya kuwa rais huru na mahakama.
Ruhusa hiyo ilitolea baada ya, AQ Khan kukata rufaa kwa kudai ya kuwa ilikuwa ni kinyume cha sheria ya yeye kuzuhiliwa kuwa huru kama mwanchi mwingine wa Pakistan.
AQ Khan,aliwekwa kizuizini na serikali ya aliye kuwa rais wa Pakistan, Pervez Musharaf, baada ya ushaidi kuonyeha alihusika katika biashara ya kuuza utaalaamu wa sayansi ya nuklia kinyume cha sheria kwa nchi za Libya, Iran na Korea ya Kaskazini.
Picha hapo juu,ni ya AQ Khan, ambaya ameruhusiwa kuwa huru.
Rais, Jakob Zuma, asisitiza uhusiano na ushirikiano wa serikali ya Zimbabwe.
Harare, Zimbabwe - 29/08/09. Rais wa Afrika ya Kusini, Jakob Zuma, amewataka viongozi wa serikali ya Zimbabwe kushirikiana ili kujenga nchi yao.
Rais , Zuma , alisema ya kuwa umefika wakati wa viongozi wa serikali ya Zimbabwe kuweka siasa pembeni, kufikiria na kufikiria ni kwa jinsi gani watainua uchumi wa nchi na kutimiza yale walio kubaliana wakati walipo saini mkataba mapema mwezi february..
Picha hapo juu wanaonekana, rais wa Zimbabwe Robert Mugabe kushoto, akiwa na rais wa Afrika ya Kusini Jakob Zuma wakati walipo kutana mjini Harare.
Korea ya Kusini na Kaskazini zafanya mazungumzo ya karibu.

Seoul, Korea ya Kusini - 29/08/09. Viongozi wa serikali za Korea ya Kusini na ya Kaskazini wamekutana hivi karibuni ili kujadili hali halisi ya maeneo ya nchi zao

Mazungumzo hayo , ambayo yanafanyika karibu na mlima wa Kumgang,yanalenga hasa ni jinsi gani nchi hizi zitashirikiana katika kuungani familia zilizo tengana tangu mwaka 1950, baada ya vita kuisha kati ya nci hizo.

Kwa mujibu wa habari, kuna watu wapatao 600,000 kutoka Korea ya Kusini waliopo Korea Kaskazini,ambao hawajawahi kuonana na ndugu zao tangu miaka ya 1950.

Picha hapo juu, wanaonekana viongozi wa Korea ya Kaskazinia na Kusini wakisaliamiana wakati viongozi hao walipo kutana kujadili hali halisi ya nchi zao.

Wednesday, August 26, 2009

Edward"Ted" Kennedy, Simba wa utetezi wa haki kwa watu wote, hatuko naye tena.

Edward "Ted" Kennedy, Simba wa utetezi wa haki kwa watu wote, hatuko naye tena.

Massachusetts, Amerika - 26/08/09. Kiongozi wa muda mrefu chama cha Demokratiki cha Amerika, Edward "Ted"Kennedy na ambaye amekuwa Seneta kwa kipindi kirefu amefariki leo kutokana na ugonjwa wa tarasani ya ubongo kwa muda mrefu.
Seneta,Ted Kennedy, alichaguliwa kuwa seneta wa Massachusetts mwaka 1962 kama senate na tangu hapo amekuwa seneta katika kipindi chote hicho.
Hata hivyo, atakumbukwa kwa kutaha haki kwa wa Amerika wote.
Hata hivyo, amehusika kwa ukaribu zaidi katika kampeni uchaguzi wa rais wa sasa Baraka Obama.
Picha hapo juu ni ya seneta, Edward "Ted" Kennedy, akiwa amesimama mbele ya ofisi za seneta, wakati wa uhahi wake.
Picha ya pili, wanaonekana, rais wa sasa wa Amerika, Baraka Obama kushoto , akiwa na hayati seneta Edward "Ted" Kennedy, akisikiliza kwa tabasamu baadhi ya maneno anayo sema, rais , Baraka Obama walipo kuwa pamoja katika moja ya mikutano ya chama cha Demokratik.
Jerusalemu ni ya Izrael, asema waziri mkuu Netanyahu.
London, Uingereza - 26/08/09. Waziri mkuu wa Izrael, Nenyamin Netanyahu, ameanza ziara ya bara la Ulaya , ili kuzungumza na viongozi wa bara Ulaya kuhusu swala zima hali ya Mashariki ya Kati.
Katika, ziara yake hiyo , amekutana na waziri mkuu wa Uingereza, Gordon Brown.
Wakati walipo kutana , waziri mkuu wa Izrael, alisema ya kuwa Jerusale, itakuwa mikononi mwa Izrael na haitakuwa chini ya Wapalstina na swala hili halina mjadara.
Katika ziara yake barani Ulaya, atakutana na kiongozi wa German na viongozi wengine.
Taliban yakili kifo cha kiongozi wao.
Waziristan ya Kusini,Pakistan - 26/08/09. Kundi la Taliban, limekubali ya kuwa kiongozi wao Baitullah Mehsud, amefariki dunia jana siku ya jumapili, kutokana na majeraha aliyo yapata baada ya mashambilizi yaliyo fanywa na ndege mtandao ya Amerika.
Kwa mujibu wa Taliban, Baitullah Mehsud, aliumia siku ya tarehe 05/08, baada ya ndege mtandao kushambulia nyumba ya baba mkwe wake.
Picha hapo juu ni ya , kiongozi wa Taliban eno la Waziristan Kusini, Baitullah Mehsud katikati, akiwa anawalinzi wake nyuma.
China yatoa ruhusa kuuza au kutoa viongo vya mwili kwa hiyari.
Beijing, China - 26/08/09. Serikali ya China, imetoa ruhusa kwa watu ambao kwa matakwa wapo tayari kutoa baadhi ya viongo vyao kwa ajili ya kusaidia watu wengine. Kwa mujibu wa serikali, shirika la msalaba mwekundu la China,kwa kusaidiana na wizara ya afya zitasimamia kwa uangalifu swala zima la hali hiyo.
Kufuatia kutolewa ruhusa hiyo, kutapunguza biaashara haramu ya ununuzi wa viungo vya binadamu ambayo ilikuwa inaanza kushamiri kwa sana.
Picha hapo, ni ya figo, kiungo ambacho huwa kina soko kubwa duniani.
Picha ya pili ni ya moyo, kiungo ambacho, upatikanaji wake umekuwa ni mgumu, lakini ikiwa mtu yoyote kabla ya kufariki, anaweza kutoa rai yake ni wapi moyo wake utumike.
Sigara kushutumiwa kuuwa watu zaidi ya millioni 6.
Washington, Amerika - 26/08/09. Shirika linalo shughulikia kuangalia afya za watu duniani, limesema yakuwa kiasi cha watu wapatao millioni 6, watapoteza maisha yao kutokana magonjwa yanayo sababishwa na uvutaji wa sigara, ifikapo mwisho wa mwaka ujao.
Kwa mujibu wa shirika hilo,(Lung Foundation), limesema yakuwa watu wengi watakao athirika ni wale wanao toka kwenye dunia ya tatu au nchi masikini duniani.
Zikithibitisha,habari kutoka kwenye shirika hilo zilimesema yakuwa uvutaji wa sigara katika nchi Amerika na za Ulaya hasa zile tajiri, uvutaji wa sigara umepungua kwa kiasi, lakini uvutaji wa sigara umeongezeka katika nchi masikini, na hivyo hali ya watu wengi kupoteza maisha kutokana na magonjwa yanayo sababishwa na uvutaji wa sigara kuongezeka.
Picha hapo juu, ni picha ya sigara, zao ambalo linachangia kuinua uchumi kwa kwa kuanzia wakulima na viwandani, lakini kwa upande mwingine, matumizi ya zao hilo kwa wateja wake ni ya kuathiri afya zao.

Monday, August 24, 2009

Wakuu wa majeshi wataka nguvu zaidi ili kupambana na Taliban.

Makundi ya kivita ya Somalia ya ungana kuipinga serikali.

Gedo,Somalia - 24/08/09. Kundi la Hizbu lililopo kusini mwa Somalia,limesema ya kuwa limeungana na kundi la Al-Shabaab. Kujiunga kwa kundi la Hizbu, kulitangazwa na , Sheikh Ahmed Mohamud, ambaye ni makamu wa wa kundi hilo alitangaza hayo wakati alipo kutana na waandishi wa habari hivi karibuni. Kiongozi huyo wa Hizbu, alisema wanaungana na wenzao ili kupambana na wapinga Wasomalia na tutawashinda alimalizia kwa kusema kiongozi huyo wa kundi la Hizbu lililopo mjini Gedo kusini mwa nchi ya Somalia.Picha hapo juu, ni wapiganaji wa kundi la Hizbu,kundi ambali limeungana na kundi la Al- Shabaab kupambana na serikali. Shirika la ujasusi la Amerika na mkuu wake wasimama njia panda.

Washingiton, Amerika - 24/08/09.Shirika la kijasusi la Amerika, huenda lakawa na wakati mgumu kufuatia habari ya kuwa huenda kesi zinazo husiana na mateso ya watu walio daiwa ni magaidi, zikafunguliwa na kuanza kuchunguzwa tena. Kesi hizo zilifutwa wakati wa uongozi wa rais wa zamani wa Amerika, George Bush, lakini tandu uongozi mpya wa rais , Baraka Obama, chini ya mwanasheria mkuu ,Erik H. Holder umekuwa na mtazamo upya katika swala zima la ugaidi. Picha hapo juu, ni alama ya shirika la kijasusi la Amerika, ambalo ndicho kiini cha ulinzi wa serikali ya Amerika. Picha ya pili, ni ya mwanasheria mkuu, wa Amerika, Erik H.Holder, ambaye tangu achukue ofisi, amekuwa na wakati mgumu kujaribu kuweza kurudisha hadhi ya shirika la kijasusi la Amerika.
Wakuu wa majeshi wataka nguvu zaidi ili kupambana na Taliban.
Bargam, Afghanistan - 24/08/09.Wakuu wa majeshi ya Amerika na NATO wamesema ya kuwa hawana majeshi ya kutosha kuweza kupambana na kundi la Taliban hadi kuliangamiza.
Kwa mujibu wa habari zilizo tolewa, zinasema yakuwa mashambulizi ya nayo fanywa na kundi la Taliban yamekuwa yakiongezeka kwa kasi na kufanya jeshi la Amerika na NATO,kupanga mikakati mipya ya kupambana na kundi la Taliban.
Kufuatia hali hiyo, wakuu wa NATO na Amerika wamesema kuna haja kubwa ya kuogeza wanajeshi kutoka katika nchi wanacham wa NATO.
Picha hapo juu, anaonekana,mmoja wa mwanajshi akiwa mstari wa mbele kupambana na kundi la Taliban.

Friday, August 21, 2009

Usain Bolt, hana mpinzani katika mbio za mita 100 na 200.

Usain Bolt, hana mpinzani katika mbio za mita 100 na 200.

Berlinn Ujerumani - 21/08/09. Usain Bolt, mwana riadha wa Jamaika, amevunja rekodi za dunia za mbio za mita 100 na 200 kwa upande wa wanaume.
Usain Bolt,ambaye amekuwa hana mpinzani, aliwashangaza wapenzi wa riadha, na kuwaacha macho yakiwa hawaamini ya kuwa rekodi ya mbio za mita 200 ya sek 19:32, iliyo wekwa na Michael Johnson, baada ya kukumbia mbio hizo za mita 200 kwa sek 19:19.
Picha hapo juu,anaonekana, Usain Bolt, akiwa mbele pekee yake mara baada ya kuvuka mstari wa mwisho, na kuvunja rekodi.
Picha ya pili, anaonekana, Usain Bolt, akiwa mbele ya wakimbiaji wenzake wakati wa fainali za mita 200.
Picha ya tatu, anaonekana, Usain Bolt, akiwa mbele ya tangazo, linalo onyesha ya kuwa ameweka rakodi mpya ya dunia ya mbio za mita 200.
Mtuhumiwa wa Lockerbie awasili nyumbani.
Tripol, Libya -21/08/09. Abdel Basset al Megrahi,ambaye anatuhuniwa kwa kuhusika na mlipuko wa bomu nadni ya ndege ya Pan Am 103, amewasili nyumbani, baada ya kuachiwa huru jana na serikali ya Uingereza, kwa kuzingatia hali ya afya yake.
Bwana, Abdel Basset al Megrahi, alikuwa amehukumiwa kifungo cha maisha, mara baada ya kukutwa na hatia ya kuhusika na ulipuaji wa ndege iliyo kuwa imebeba watu 270, watu wote kupoteza maisha kutokana na mlipuko huo.
Kufuatiwa kuachiwa kwake, baadhi ya viongozi wa kimataifa wamekuwa wakitoa maoni tofauti,kuhusu kuachiwa kwake.
Lakini hata hivyo, Abdel Basset al Megrahi, alipokelewa kwa shwange alipo wasili jijini Tripol.
Picha hapo juu, anaonekana, akiwa ameshikiliwa na baadhi ya watu waliokuja kumpokea.
Picha ya pili, anaonekana A.B. al Megrahi,akipanda ngazi kuingia ndani ya ndege, tayari kuanza safari ya kurudi nyumbani Libya.
Picha ya tatu, A.B.al Megrahi, akishuka kutoka kwenye uwanja wa ndege nchini Libya na wanaonekana mamia wakija kumpokea kwa shangwe.

Thursday, August 20, 2009

Uchaguzi wa Afghanistan, wakamilika jumuia ya kimataifa yangoja matokeo yake
Kabul, Afghanistan - 20/08/09. Wanachi wa Afghanistan, wamemaliza kupiga kura kuwachagua viongozi watakao ongoza nchi kwa kipindi cha miaka mitano mingine.
Kufuatia kumalizika kwa kupigwa kwa kura leo 1700( saa kumi na moja) kwa masaa ya Afghanistan, kura zimeanza kuhesabiwa rasmi. Kumalizika kupiga kura nchini Afghanistan, kumesifiwa na mwakilishi wa serikali ya Amerika, Richard C Holbrooke.
Bwana, Holrbooke, alisema ya kuwa wanchi wa Afghanistan, wameweza kupiga kura bila kuogopa vitisho vya Taliban, na huu ndiyo mwanzo wa kuijenga nchi yao Waafghanistan.
Picha hapo juu ni za wagombea wa kiti cha urais wa Aghanistani, kutoka kushoto,Abdullah Abdullah,Ramadhani Bashardost, Ashraf Ghani na Hamid Karzai.
Picha ya pili, wanaonekana wanchi wa Afghanistan, wakiwa katika mstari tayari kupiga kura kuchagua viongozi wao.
Uingereza yatakiwa kudhibiti biashara ya siraha.
London, Uingereza 20/08/09.Shirika linalo shughulikia usimamizi wa uuzaji wa siraha duniani, limeitaka serikali ya Uingereza, kuchukua hatua upya ya kusimamia reseni na uuzaji wa siraha wa makampuni yanayo uza siraha hizo ambazo zinatikea nchini humo.
Kwa mujibu wa shirika hilo,limesema yakuwa, katika uchunguzi wake, limegundua ya kuwa siraha nyingi zinazo tumika katika mapigano sehemu tofauti zinaalama ya matengenezo kutoka Uingereza.
Shirika hilo pia limeitaka serikali ya Uingereza kujaribu kushirikiana na mashirika ya siyo ya kiserikali ili kudhibiti uuzaji haramu wa siraha hizo.
Hata hivyo serikali ya Uingerza imesema yakuwa inafuata sheria za kimataifa na itazidi kuimarisha udhibiti huo.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Uingereza nchi ambayo imetakiwa kuongeza bidii kudhibiti uuzaji wa siraha zinazo tokea nchini humo.

Wednesday, August 19, 2009

Mmea wa bangi majaribioni kutibu kansa.

Rais wa za zamani wa Zambia, ashukuru Mungu, "Kesi imefutwa" Lusaka, Zambia - 19/08/09. Rais wa zamani wa Zambia, Frederick Chiluba, ameachiwa huru, baada ya kukutwa hana hatia ya kula rushwa wakati wa uongozi wake akiwa rais wa Zambia. Kesi hiyo, ambayo aliyo kuwa inamkabiri rais huyo wa zamani wa Zambia, Fredrick Chiluba ni kuhusika na upotevu wa $500,000 za Amerika Kwa mujibu wa mahakama, wanasheria wa serikali walio fungua kesi hiyo walikosa ushahidi kamili. Rais huyo wa zamani wa Zambia, Fredrick Chiluba, amekuwa akikabiliwa na kesi iliyo chukuwa miaka minane tangu ashitakiwe. Mungu ni mkubwa, ameonyesha ukweli upo wapi na alisikika akisema hayo rais huyo wa zamani wa Zambia. Picha hapo juu, anaonkekana, rais wa zamani wa Zambia, Fredrick Chiluba, akinyanyua mikono juu kumshukuru Mungu, mara ya kusikia kesi iliyo kuwa ikimkabili imetupiliwa mbali na mahakama. Wanaume wabakwa kwa wingi nchini DRC. Goma, DRC - 19/08/09. Hali imezidi kuwa mbaya katika eneo la Goma, baada ya wanaume kuanza kubakwa. Kwa mujibu wa mmoja ya watu waliokumbwa na mkasa huo,Kazungu Ziwa,alisema alivamiwa na kukamatwa na watu wenye mapanga na virungu. Baada ya kuvamiwa alijaribu kupigana nao, lakini alishindwa , na matokeo ya ke wakamtawiti kwa nguvu, na baadaye walimwacha akiwa taabaani. Kwa mujibu wa bwana Ziwa, alisema ya kuwa watu hao, walikuwa ni moja ya makundi wanaopigana katika maeneo hayo. Picha hapo juu, ni moja ya picha za watu ambao walikumbwa na mikasa ya kulawitiwa.

Mmea wa bangi majaribioni kutibu kansa.
London,Uingereza -19/08/09.Mmoja wa wataalamu wanaofatilia tiba ya kansa,Ine Diaz-Laviada, amesema ya kuwa mmea wa bangi unaweza kusaidia kuponyasha ugonjwa wa kansa.
Ine Diaz Laviada, alisisitiza ya kuwa chunguzi wa muda mrefu umeonyesha mmea huu unaweza kutumika kama dawa ya kusaidia kutibu kansa.
Hata hivyo bado uchunguzi unaendelea zaidi.
Picha hapo juu, ni ya mmea wa bangi, mmea ambao huenda hapo baadaye ukasaidia kutibu kansa.
Mwanafunzi mzee kuliko wote, afariki dunia.
Nairobi, Kenya - 19/08/09. Raia wa Kenya, Mzee, Kimani Nganga Maruge aliyekuwa na miaka 90, amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu ugonjwa wa kansa ya tumbo.
Mzee Kimani Nganga Muruge, ambaye aliweka historia,na kuandikwa katika kitabu cha historia, kwa kujiandikisha shule ya msingi huku akiwa na miaka 84,na mzee wa kwanza kuanza shure akiwa na umri mkubwa.
Mzee, Kimani Nganga Magure, aliamua kujiandikisha shule,baada ya kuhisi ya kuwa muhubiri alikuwa anatafsili vibaya na kupoteza maana ya ujumbe kamili.
Mzee, Kimani Nganga Maruge, alikuwa mmoja ya wapigania uhuru wa Kenya miaka ya 1950, chini ya Uongozi wa Mau Mau.
Picha hapo juu, anaonekana katikati mzee Kimani Nganga Maruge,akiwa darasani na yupo tayari kuuliza swali.Mungu ailaza mahari pema peponi roho yake mzee Kimani Nganga Maruge.
Wajenzi wa viwanja kupata tiketi za bure, " Mchezo wa soka Afrika ya Kusini.
Johannesburg, Afrika ya Kusini -19/08/09. Chama cha mpira nchini Afrika ya Kusini, kwa kushirikiana na shirikisho la kandana ulimwenguni FIFA, zimepanga kutoa tiketi zaidi ya 120,000 za bure, ili waler wapenzi wa sika nchini humo, wasio na uwezo wa kulipa waweze kuhudhulia mashindano hayo ya soka yatakayo fanyika nchini humo - ( Afrika ya Kusini).
KWa mujibu wa FIFA, tiketi hizo za bure, zitadhaminiwa na mashirika na makampuni ya Adidas,Coca Cola, kampuni ya Magari ya KIA, Emarates, Hyundai, Sony na Visa.
Kufuatia kutolewa kwa tiketi hizo, wajenzi wote waliohusika katika kujenga viwanja hivyo, watakuwa wa kwanza kupata tiketi hizo.
Picha hapo juu ni ya mmoja ya washibiki wa soka nchini Afrika ya Kusini, ambaye huenda akabahatika kupata tiketi ya bure kuona mpambano wa soka wa kunyanyia kombe la Dunia.

Wednesday, August 12, 2009

Kura ya maoni ya Niger yaleta maswali kwa EU.

Kura ya maoni ya Niger yaleta maswali kwa EU.

Brussels, Ubeligiji - 12/08/09. Muungano wa nchi za Ulaya EU, umesema uhenda ikapunguza kuendela kuisaidia nchi ya Niger, baada ya rais Mamodou Tandja, kubadilisha katiba na kumwezesha kutawala tena kwa kipindi kingine.
Kubadilishwa kwa katiba hiyo ya nchi ya Niger, kumekuwa kukilaumuwa na nchi wanchama wa EU.
Mabadiliko hayo ya katiba, yatamwezesha rais Mamodou, kutawala kwa kipindi kingine cha miaka mitatu.
Picha hapo juu ni ya bendera ya nchi wanachama wa Muungano wa Ulaya, ambao umekuwa ikisaidia nchi ya Niger kwa muda mrefu.
Picha ya pili ni ya rais, Mamodou Tandja,ambaye kura za maoni zilikubali pendekezo lake.
Urusi kuimarisha jeshi lake karibu na mipaka na Georgia.
Sukhumi,Abhakazia - 12/08/09. Waziri kuu wa Urusi, Vladimir Putin, amesema ya kuwa nchi nyingi za Ulaya zinailaumu Georgia kwa kuanzisha vita,na viongozi Georgia hawataki kukubali ya kuwa wao ndiyo waliotoa mri ya kuanza vita.
Waziri mkuu yuho, Vladimir Putin,alisisi tiza kwa kusema yakuwa viongozi wa Georgia hawawezi kukubari kutokana na mkandamizo wanao upata kutoka Amerika.
Ziara hiyo katika jimbo la Abhakazia, ni katika kuangalia na kuwapa pole wale wote walio athirika na vita.
Waziri mkuu, Putin, alisema Urusi itawekeza $ 470, ili kuimarisha ulinzi katika eneo la Abhakazia na kipaka na Georgia.
Picha hpo juu, anaonekana mama , mmoja alimsalimia waziri mkuu, wa Urusi, Vladimir Putin, alipo tembelea Abhakazia.
Rais atoa amri kutafutwa kwa meli iliyo potea.
Moscow, Urusi -12/08/09. Rasi wa Urusi, Dmitry Medvedev, ametoa amri ya kutafutwa kwa moja ya meli ya mizigo iliyo potelea karibu na pwani ya Ufaransa.
Kwa mujibu wa msemaji wa idara ya ulinzi wa bahari wa Urusi,Vladimir Vysotsky,alisema amri hiyo,imekuja mara baada ya juuudi za kutafuta meli hiyo kuleta utata.
Meli hiyo iliyo kuwa na raia wa Urusi, ilipotelea njiani tangu tarehe 4/8/09, njiani kuelekea Algeria.
hata hivyo kuna wasiwasi yakuwa meli hiyo,huenda ikawa imetekwa na na maharamia.
Picha hapo juu ni rais wa Urusi, Dmitry Medvedev , ambaye ameagiza kutafutwa kwa meli iliyopotelea baharini.

Tuesday, August 11, 2009

Daw Aung San Suu Kyi, aongezewa kifungo zaidi.

Yangon Myanmar - 11/08/09. Serikali ya Myanmar,imemuhukumu kifungo cha miezi 18 au mwaka mmoja na nusu, Daw Aung San Suu Kyi, ambaye kiongozi wa National League for Democracy - NLD.
Uamuzi wa kumgunga kifungo cha ndani ulikuja baada ya mahakama kudai ya kuwa , Suu Kyi, alivunja sheri ya ndani na hivyo atatumikia kifungo cha mieizi 18 baada ya kukutana John Yettaw Ambaye ni raia wa Amerika nyumbani kwake.
Picha hapo juu, ni picha ya, Daw Aung San Suu Kyi,akichungulia dirishani, na hivi sasa amehukumiwa kifungo cha ndani cha miezi 18 zaidi.
Picha ya chini, ni moja ya gari la polisi la Myanmar, likiwa na walinzi na baadhi ya watu ndani ya gari hilo tayari kuelekea mahabusu.

Monday, August 10, 2009

Uingereza haitaruhusu watu kuteswa na makachero.

Wepesi wa mawasiliano ya kimtandao kuwepo Afrika. Mombasa, Kenya - 10/08/09.Kampuni ya SEACOM, imewekeza kiasi cha $ 2.6billion katika eneo la Afrika ya Mashariki katika kuinua mawasiliano ya kimtandao. Kwa mujibu wa mtasmini wa mambo ya mawasiliano, David Lerche, alisema ya kuwa Afrika itafaidika kwa kiasi kikubwa zaidi ya mara 10, na kuweza kuwasiliana na mabara mengine kiuraisi zaidi kwa kutumia mtandao, kwani mitambo hiyo itaunganisha bara la Asia na Ulaya na itakuwa na nguvu zaidi. Picha hapo juu wanaonekana, wafanyakazi wa kiwa kazini kuvuta moja ya waya za kupitishia mawasiliano katika mji wa Mombasa nchini Kenya kuelekea ndani ya bahari ya Indi kuelekea katika bara la Asia. Uingereza haitaruhusu watu kuteswa na makachero. London,Uingereza, 10/08/09.Serikali ya Uingereza, imesema yakuwa itakuwa ni vigumu, kwa makachero au majasusi wa nchi kukubali au kukataa ya kuwa habari zilizo patikana, lizipatikana kutoka kwa watu washukiwa wa makundi ya uhaini, baada ya kuteswa kwa kinyume cha sheria za haki za binadamu. Akiongea hayo, waziri wa mambo ya nje wa Uingereza, David Miliband, alisema hayo alipo kuwa akiongea na vyombo habari, na kusema ya kuwa serikali ya Uingereza, hairuhusu wa kutesa watu kwa aajili ya kupata habari na hii ni kinyume na haki za binadamu. Picha hapo juu ni ya waziri wa mambo ya nje wa Uingereza, David Miliband,alipo kuwa akiongea na vyombo vya habari siku ya jumapili wiki hii. Uhusiano wa Venezuela na Kolombia wawa wa wasiwasi. Caracas, Venezuela - 10/08/09. Rais wa Venezuela, Hugo Chavez, amekaripia nchi ya Kolombia kwa kudai yakuwa imetuma wanajeshi kuingia Venezuela. Akisisitiza ,rais Hugo Chavez, alisema ya kuwa hawakuwa askari wa kulinda mpaka, bali walikuwa ni wanajeshi na walivuka Mto wa Orinoco na kuingia hadi ndani ya Venezuela. Na wakati wanjeshi wa Venezuela walipokwenda kwenye eneo hili, walikuta wanajeshi wa Kolombia wamesha ondoka. Venezuela, imekua ikipinga kitendo cha Kolombia kuruhusu, Amerika kuweka kambi zake za kijeshi nchini Kolombia. Na wakti huo huo , Kolombia imekuwa ikiilaumu Venezuela, kwa kuwasaidia waasi wa kundi la FARC, ambalo linapingana na serikali ya Kolombia. Hata hivyo, serikali ya Kolombia imekanusha madai hayo. Picha hapo juu, wnaonekana, rais wa Venzuela, Hugo Chavez, akiongea na vyombo vya habari.

Sunday, August 9, 2009

Viongozi wa siasa nchini Madagaska wakibaliana

Viongozi wa siasa nchini Madagaska wakubaliana kimsingi

Maputo, Mozambiki - 09/08/09. Vyama vya upinzani nchini Madagaska, vimekubaliana kushirikiana kuunda serikali ya mpito kwa kipindi cha miezi 15 chini ya usimamizi wa rais wa zamani wa Mozambiki, Joakim Chissano.
Kwa mujibu, wa msemaji wa UN (Umoja wa Mataifa) Tiebile Drame, pande zote mbili zimekubaliana kimsingi yakua kipindi hicho cha mpito cha miezi 15, kikifikia wanachi wa Madagaska, watajiandaa kupiga kura kwa uchaguzi mkuu.
Picha hapo juu, ni ya rais wa sasa wa Madagasca, Andry Rajoeli,ambaye aliingia madarakani, baada ya kung'olewa madarakani rais, Marc Ravalomanana.
Picha ya pili, ni ya rais wa zamani wa Madagaska, Marc Ravalomanana,ambaye kutolewa kwakwe madarakani watu wapato 100, walifariki dunia.
Picha ya tatu ni ya bendera ya Madagaska, nchi ambayo imekuwa na myumbo wa kisiasa tangu kufanyika mapinduzi yaliyo mng'oa madarakani rais, Marc Ravalomanana.

Wednesday, August 5, 2009

Mahmoud Ahmadinajed, aapishwa tena kuwa rais wa Iran.

Billy Clinton, azuru Korea ya Kaskazini, waandishi wa habari wa achiwa huru.

Los Angeles,Amerika - 05/08/09. Waandishi wa habari wawili raia wa Amerika, Laura Ling na Euna Lee,wameachiwa huru na kuwasili nyumbani kuungana na familia zao, baada ya kukaa jela kwa muda wa miezi minne na siku kadhaa kwa msamahaa wa rais wa Korea ya Kaskazini.
Kuchiwa kwao kumekuja mara baada ya rais wazamani wa Amerika,Billy Clinton kufanya ziara ya ghafla nchini Korea ya Kaskazini, na kuongea na rais Kim Jong Il.
Hata hivyo hakuna habari zozote zilizo elezwa kuwa viongozi hawa waliongea nini.
Picha hapo juu, wanaonekana, rais wa zamani wa Amerika, Billy Clinton kushoto,na rais wa Korea ya Kaskazini, Kim Jong Il, wakati alipo kuwa nchini Korea ya Kaskazini.
Picha ya pili, wanaonekana, Laura na Euna, wakishuka kutoka kwenye ndege, kukanyaga ardhi ya Amerika, baada ya kuachiwa huru kwa msamahaa wa rais wa Korea ya Kaskazini.
Picha ya tatu, wanaonekana, Laura na Euna wakikaribishwa kuingia kwenye ndege na rais wa zamani wa Amerika Billy Clinton.
Mahmoud Ahmadinajed, aapishwa tena kuwa rais wa Iran.
Tehran,Iran - 05/08/09. Mahmoud Ahmadinejad ameapishwa kwa mara ya pili kuwa rais wa Iran.
Akiongea baada ya kuapishwa, rais, Mohmoud Ahmadinejad,alisema ya kuwa atafanya mabadiliko katika serikali yake, kitaifa na kimataifa.
Katika, sherehe ya kuapishwa kwake, kuliudhuliwa na viongozi na mabalozi wa nchi tofauti, lakini baadhi ya viongozi wa vyama pinzani walisusia sherehe hiyo.
Picha hapo juu, anaonekana,rais wa Iran, Mahmoud Ahmadinejad kulia,akikabidhiwa hati za serikali na kiongozi mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei aliyepo kushoto.
Picha ya chini, anaonekana, rais wa Iran,Mahmoud Ahmadinejad,akiongea mara ya baada kuapishwa kwake.

Tuesday, August 4, 2009

Nashukuru kuondoka kwa Eto'o,alikuwa ananipa ndoto zisizo za kawaida.

Nashukuru kuondoka kwa Eto'o, alikuwa ananipa ndoto zisozo za kawaida.

Madrid, Uispania - 04/08/09. Golikipa au mlinzi namba moja wa timu ya taifa ya Uispania Iker Casillas, amesema amefurahi kuondoka kwa mshambuliaji hatari wa timu ya FC Barcelona na timu ya taifa ya Kameroon, Samwel Eto'o.
Akiongea leo hii, Casillas, alisema ya kuwa Eto'o, alikuwa akimfanya aote ndoto zisizo eleweka kila anapo fikilia mechi na timu ya Barcelona.
Akiulizwa na waandishi wa habari, Iker Casillas, kuhusu mshabuliaji ,Zlatan Ibrahimovic, mlinda mlango huyo, alisema Ibrahimovic ni mchezaji mzuri, lakini Eto'o ni hana mfano.
Hapo juu, ni picha tofauti, zinaonyesha ni kwa kiasi gani,mlinzi wa timu ya Madrid, Iker Casillas, alivyokuwa akiteswa na kuteseka kila anapo kutana na mshambualiji wa Barcelona, Samwel Eto'o.
Kwani, Eto'o amekuwa akimpa wakati mgunga mlizi huyo, Iker Casillas na kuona nyavu zilizo chini ya ulinzi wa kipa huyo.