Sunday, January 24, 2010

Evo Morales aapishwa kuwa rais wa Bolivia.

Evo Morales aapishwa kuwa raia wa Bolivia La Pazi, Bolivia - 24/01/2010. Wanachi wa Bolivia kwa maro nyingine tena wameshuhudia kuapishwa kwa raia Evo Morales kuwa rais wa nchi hiyo. Evo Morales, alichaguliwa kufatia uchaguzi uliofanyika mwaka jana. Kwenye sherehe hiyo iliudhuliwa na raiwa Venezuela Hugo Chavez, na rais wa Ekuador Rafael Correa. Picha hapo juu ni rais wa Bolivia, Evo Morales, mara baada ya kuapishwa kuwa rais wa Bolivia baada ya kushinda uchaguzi wa urais Bolivia. Korea ya Kaskazini yatishia kutumia nguvu za kijeshi.

Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 24/01/2010. Serikali ya Korea ya Kaskazini imeonya ya kuwa itakuwa tayari kuishambulia Korea ya Kaskazini kutokana na kauli iliyotolewa na wakuuwa jeshi wa nchini hiyo.
Onyo hilo limekuja baada ya viongozi wa jeshi la Korea ya Kaskazini kudai hawakubaliani na Korea ya Kaskazini kuwa na mitambo ya nyuklia.
Kufuatia maelezo hayo, serikali ya Korea ya Kaskazini, inalichukulia kama tishio la usalama wa nchi na hivyo hii swala lina weza kuleta vita.
Picha hapo juu, ni bendera ya Korea ya Kaskazini, nchi amabyo imekuwa na mvutano na jumuia ya Kimataifa kuhusu swala la nguvu za nyuklia katika nchi hiyo.
NATO kutumia mbwa kunusa mabomu ardhini.

Kandahar, Afghanistan - 24/01/2010. Jeshi la NATO na washirika wake limeanza kutumia mbwa kujaribu kunusa na kutambua yaliyo tegwa ardhini.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana, zinasema yakuwa hadi kufikia hivi sasa kuna mbwa wapatao 20 na idadi hiyo itaongezeka hadi kufikia zaidi ya mbwa 200.

Mbwa hao amabo huenda wakaghalimu $ dola 40,000 kwa mwaka huwa wanafunzwa kwa muda wa miezi mitano.

Picha hapo juu anaonekana mmoja ya mbwa akiwa kazini kunusa wapi mabomu yametegwa.

Thursday, January 14, 2010

Google hatarini kufungwa nchini China.

Kiongozi wa Guinea awasili Bukinafaso kuepuka utata. Conakri, Guinea-14/01/2010. Kiongozi wa kijeshi wa Guinea, Moussa Dadia kamara, amewasili nchini Bukinafaso kwa mujibu wa wizara ya mambo yanchi za nje wa nchini hiyo. Moussa Dadis Kamara, aliwasili Ouagadougou siku ya Jumanne kutokea nchini Moroka ambapo alikuwa kwaajili ya matibabu baada ya kunusulika kuuwawa kwa kupigwa risasi ya kichwa na mmoja ya walinzi wake. Kuwasili kwa Moussa Dadia Kamara nchini Bukinafaso kumekuja baada ya habari yakuwa serikali ya Moroko imekuwa ikitakiwa kumpeleka mkuu huyo wa nchini ya Guinea katika nchi za Ulaya ili ashitakiwe kwa makosa ya mauaji ya raia wakati wa maandamano yaliyo fanyika mwaka jana. Picha hapo juu anaonekana mkuu wa jeshi na kiongozi wa Guinea, Moussa Dadis Kamara, baada ya jeshi ya kuchukua madaraka nchi Guinea japo kulipingwa na wengi. Google hatarini kufungwa nchini China. Beijing,China -14/01/2010.Serikali ya Chini imesema kampuni yoyote inayo taka kufanya biashara nchini humo lazima ifuate sheria za nchi -China. Msemaji wa serikali ya China, Wang Che alisema" ikiwa kampuni ya internet itaenda kinyume na sheria ya serikali basi hatua za kisheria zitachukuliwa na hata kampuni kufungwa." Maelezo hayo yametolewa baada ya kamuni ya mtandao ya Google kulalamika ya kuwa mitandao yake imekuwa ikishabuliwa na kushindwa kutoa huduma nzuri kwa jamii nzima iliyopo China na huenda wakafunga ofisi zao nchini humo. Picha hapo juu in nembo ya Google nchini China, ambapo kampuni hiyo imekuwa ina vutana na serikali ya China katika kutoa huduma za kimtandao kwa wanchini wa nchi hiyo. Viongozi wa dini nchini Yemeni watoa onyo. Sanaa, Yemen-14/01/2010. Viongozi wa kidini nchini Yemen, wamesema yakuwa ikiwa nguvu za kijeshi zitatumika na jeshi la kigeni kuingia nchini mwao, basi litakuwa ni jikumu la kila Myameni kuilinda nchi yao kufautia sheria za dini. Katika barua ambao imesainiwa na vingozi wa kidini wapatao 150 ulisema "itakapo fikia hatua ya nchi za nje kushambulia Yemeni, basi lazima wajue yakuwa vita vitakuwa vita vya jihadi." Kwa mujibu wa wachunguzi wa mambo ya kisiasa nchini Yemeni, wanasema" ikiwa viongozi wa kidini wameingilia swala la hali ya Yemeni, basi huenda kukalete mabadiliko makubwa na mwelekeo mzima wa kuitizama Yemeni." Hata hivyo, Amerika na nchi za Ulaya zimekuwa ziliilaumu Yemeni kwa kuwa kituo kikubwa cha kufunzia wapiganaji wa kundi la Al-Qaeda. Picha hapo juu ni ya jiji la Sanaa, mji mkuu wa Yemen, nchi ambayo imekuwa na mvutano wa kisiasa kwa muda mrefu Wananchi wa Haiti wakumbwa na tetemeko la ardhi.

Port-au-Prince,Haiti -14/01/2010.Maelfu ya watu wamepoteza makazi yao na mamia kupoteza maisha baada ya tetemeko la ardhi lenye nguvu za nyuzi 7.0 kutokea nchini Haiti.
Kwa mujibu wa habari zinasema tetemeko hilo la ardhi limeleta maafa makubwa kwa jamii nzima ya Haiti.
Kufuatia tetemeko hilo la ardhi, umoja wa mataifa na nchi tofauti duniani zimeanza kutoa misaada yakila aina ili kuwasaidia rais wa Haiti.
Picha hapo juu, wanaonekana vijanawakimsaadia mmoja wa watu ambao wameumia kuktokana na tetemeko la ardhi.
Picha ya pili anaonekana mwamama akiwa amezungukwa na vumbi na matofari ya nyumba iliyobomoka wakati akiwa katika eneo analo kaa na kusababisha majeruhi kwa watu waliokuwa karibu na jengo hilo.

Saturday, January 9, 2010

Timu ya taifa ya Togo yashambuliwa kwa risasi nchini Angola.

Timu ya taifa ya Togo yashambuliwa kwa risasi nchini Angola. Kabinda, Angola-09/01/2010. Mashindano ya kutafuta bingwa wa mchezo wa Soka katika bara la Afrika, yaliongia dosali baada ya timu ya taifa ya Togo kushambuliwa kwa risasi na kundi linalo pigania kujitenga na kutete eneola Kabinda. Mashambulizi hayo yalitokea wakati timu ya taifa ya Togo ilipo vuka mpaka wa Kongo na kuingia nchini Angola kwa kutumia usafiri wa basi. Kufuatia mashambulizi hayo, dereva wa basi aliuwawa hapo hapo, kocha msaidizi alipoteza maisha baadaye na baadhi ya wachezaji kujeruhiwa vibaya. Picha hapo juuanaonekana, kaptain wa timu ya taifa ta Togo, Emmanuel Adebayor, akisaidiwa na mmoja wa mchezaji mwenzake mara baada ya kuokolewa na vyombo vya usalama vya serikali yaAngola. Kiongozi wa mkuu wa Iran aagiza atua kali zichukuliwe. Tehran, Iran - 09/01/2010. Kiongozi mkuu wa Iran ameagiza vyombo vya usalama nchini Iran kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya viongozi wa na wanachama wa vyama pinzani vinavyo leta vurugu na kuipinga serikali. Kiongozi huyo Ayatollah Ali Khamenei alizilaumi nchi za kigeni kwa kuchochea vurugu nchini Iran kwa kutumia vyama vya upinzani. Hata hivyo habari kutoka kambi ya vyama vya upinzani zina sema watu wapatao 180, walikamatwa hivi karibuni wakiwepo waandishi wa habari. Akithibitisha kukamatwa kwa watu waliokuwa wakiandamana, wakili wa serikali Abbs Jafari Dolatabadi alisema"kesi dhidi ya watu wote waliokamatwa zitaanza wiki hii." Amani yaingia utata Sudan ya Kusini. Khartoum, Sudan -09/01/2010. Vita vya ukabila vimeanza tena kusini mwa nchi ya Sudan, na kusababisha zaidi ya watu wapatao 139 kupoteza maisha yao. Kwa mujibu wa msemaji wa serikali Sabino Makana, alisema "vita hivyo vilitokea kati ya kabila la Nuer na Dinka wakati walipo kuwa wakigombania mifugo." Habari kutoka ofisi za UN zinasema ya kuwa mapambano hayo yameanza mapema mwaka huu na yanaweza kuhatarisha mkataba wa amani uliokubalika miaka ya nyuma. Picha hapo anaonekana mmoja ya mkazi wa Sudan ya kusini akiwa anachuga mifugo yake, ambayo ilikuwa chanzo cha kuzuka kwa vita vya kikabila katika eneo hilo hivi karibuni. Aliyetaka kuilipua ndege akanusha mashitaka. Detroit, Amerika - 09/01/2010. Raia wa Nigeria, Umar Farouk Abdulmutallab, amekanusha mashitaka yake ambayo yanamkabili kwa kutaka kulipua ndege iliyokuwa imebeba abiria ikitokea Amsterdam. Alikanusha mashitaka hayo wakati alipo tokea mahakamani kusilikiliza mashitaka hayo. Kufuatia kukanusha mashitaka kwa mtuhumiwa huyo kesi hiyo ilihairishwa. Picha hapo juu ni ya mshitakiwa anayeshutumiwa kwa kutaka kulipua ndege iliyokuwa ikitokea Amsterdam kuelekea Amerika.

Tuesday, January 5, 2010

Iceland mashakani kulipa madeni.

Mshitakiwa wa 9/11 akataliwa rufaa. Washington, Amerika - 05.01/2010.Mahakama ya imetupilia mbali rufaa iliyokuwa ime ombwa na mshitakiwa Zakaria Massaoui, anayeshukiwa kuhusika na mashambulizi ya Septemba 11.2001 yaliyo tokea jijini New York na kupoteza maisha ya watu wapatao 3000 na wengine kujeruhiwa vibaya. Kufuatia uamuzi huo wa mahakama, Zakaria Massaoui ambaye ndiye mshitakiwa ataendelea kutumikia kifungo cha maisha. Picha hapo juu ni ya mtuhumiwa wa mauaji ya Septemba 11 2001, ambaye rufaa yake imekataliwa na mahakama.

Iceland mashakani kulipa madeni.
Reykjavik, Iceland - 05/01/2010. Rais wa Iceland amekataa kusaini muswada uliopitishwa na bunge la nchini hiyo ili kulipa madeni ambayo nchi hiyo inadaiwa na Uhollanzi na Uingereza.
Rais wa Iceland Olafur Ragnar Grimsson, alisema "swala hili litaamuliwa na wananchi kwa kupigwa kura ya maoni,"kwani wanchindiyo wakatao amua nini mbeleni watakabiliana nacho.
Hata hivyo viongozi wa Uhollanzi na Uingereza wamesikishwa na uamuzi huo na wameitaka nchi hiyo kulipa deni hili la pesa ambazo Iceland ilipewa wakati wa mporomoko wa masoko ya fedha yaliyo tokea mapema miaka miwili iliyo pita.
Picha hapo juu wanaonekana wanchi wa Iceland, wakiandamana kupinga uamuzi wa serikali yao kutaka kulipa deni ya pesa zilizo kopwa kutoka wa Uhollanzi na Uingereza.
Kachero wa ajitolea muhanga.
Jimbo la Khost Afghanistan - 05/01/2010.Muaji wa kujitolea muhanga aliye sababisha vifo vya makachero wa Amerika CIA na Joradan, ametambuliwa ya kuwa alikuwa kachero aliyekuwa akifanya sehemu mbili tofauti za upererezi.
Kachero huyo raia wa Jordan Hammam Khalil al Balawi, "inasemekana alikuwa amechaguliwa na ofisi ya makachero ya Jordan kufanya kazi nao, ili kujua mbinu za kundi la al Qaeda."
Hammam Khalil al Balawi, alidai "ataweza kutoa habari wapi moja wa viongozi wa al Qaeda
walipo."
Picha hapo juu wanaonekana mwili wa mmoja wa makachero wa Jordan ukiwa umbebwa mara baada ya kuwasili Jordan tayari kwa mazoshi.
Rais Zuma aongeza jiko la tatu.
Kwazulu Natal, 05/01/2010. Afrika ya Kusin - Rais wa Afrika ya Kusini Jokob Zuma, amefunga pingu kwa mara ya nne mapema wiki hii.
Harusi hiyo iliyo fanyika Nkandla, 67 rais Jakob Zuma, amefunga pingu za maisha na bi Tobeka Madiba 37 ambaye tayari anawatoto watatu wa Jakob Zuma.
Sherehe hiyo iliyo udhuliwa na viongozi wa serikali na wa kitamaduni pamoja na wafanya biashara kutoka sehemu tofauti nchini Afrika ya Kusini.
Picha hapo wanaonekana wapendanao walio funga pingu za maisha Tobeka Zuma kushoto na kulia Jakob Zuma wakicheza ngoma ya kiasili ya Kizulu wa wakati wa sherhe yao ya kufunga pingu zamaisha iliyo fanyika siku ya Jumatatu.
Picha ya pili, anaonekana rais wa Afrika ya Kusini Jakob Zuma, wa pili kulia akiwa na wake zake watatu mara baada ya kufunga ndoa na bi Tobela wa pili kulia.

Saturday, January 2, 2010

Yamen kupata misaada kupambana na Al Qaeda

Mwasisi wa chama tawala Tanzania aiaga dunia

Dar es Salaam,Tanzania - 02/01/2010. Wananchi wa Tanzania wameaanza kuombeleza kifao cha aliyekuwa kiongozi imara wakati wa kupigania uhuru hayati Rashid Kawawa.
Rashid Kawawa alifariki dunia katika hospitali ya Muhimbili iliyoko jijini Dar es Salaam Tanzania
Rashidi Kawawa alikuwa mwasisi wa chama tawala cha Tanzania CCM, pia aliwahi kushika nyazifa mbalimbali wakati wa serikali ya hayati Mwalimu Julius Nyerere, na kuwa mmoja wa viongozi walioaminika saana na Mwalimu Julias Nyerere wakati wa uongoziwake.
Picha hapo juu anaonekana hayati Rashid Kawawa akiwa tayari kuchezesha mechi ya mpira wa miguu enzi zake kama mwamuzi wa soka.
Picha ya pili, aanaonekana hayati Rashid Kawawawa tatu kulia, akiwa na viongozi wenzake mara baada ya muungano wa Zanziba na Tanganyika.
Picha ya tatu , anaonekana enzi za uahai wa Rashid Kawawa, akiwa amevalia shati la kijani ambalo ni vazi lasmi la cham tawala CCM.
Picha ya mwisho anaonekana rais wa Tanzania , Jakaya Kikwete, kushoto akiongea na hayati Rashid Kawawa,wakati rais Kikwete alipo kwenda kumtembela nyumbani kwake.
Yemen kupata misaada kupambana na Al Qaeda.
Washington, Amerika - 02/01/2010. Rais wa Amerika, Baraka Obama ameseama yakuwa shambulizi lililo shindwa kufanyika siku ya Krismas kwenye ndege ya shirika la Delta ilyo kuwa ikitokea Amsterdam kuelekea Detroit lilikuwa limepangwa na kundi la Al Qaeda.
Baraka Obama, aliyasema yakuwa mtuhumiwa wa tukio hili raia wa Nigeria, Umar Farouk Abdulmutallab, alipewa mafunzo hayo wakati alipo kuwa nchini Yemen na kuhaidi kuzidisha ulinzi wa usalama wa Amerika na kuhaidi kuongea misaada kwa serikali ya Yemen kwa ajili ya kupambana na kundi la Al Qaeda na washiriki wake.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wanachama wa kundi la Al Qaeda wakiwa katika mkutano nchini Yemeni.
Wafanyakazi wa Blackwater waachiwa huru na mahakama.
Baghdad, Irak - 02/01/2010. Serikali ya Irak, inapanga kufungua kesi dhizi ya kampuni ya ulinzi ya Blackweter ambao waliusika katika mauaji ya raia wa Irak.
Uamuzi wa serikali ya Irak, kutaka kufungua tena kesi hiyo, kumekuja baada ya hakimu wa mahakama Ricardo Urbina, kufuta kesi iliyo kuwa ikiwakabili wafanyakazi wa kampuni ya ulinzi ya Blackwater.
Kwa mijibu wa mshauri wa serikali,Saad al Muttalib, alisema "uamuzi wa mahakama hiyo, umeleta mshangao mkubwa kwa wanchi wa Irak na uhenda ukaleta utata wa ushirikiano wa nchi mbili hizi."
Hata hivyo, wafanyakazi wa kampuni hiyo ya ulinzi Blackwater, "walidai yakuwa walianza
kushwambuliwa na ndipo walijibu mashambulizi hayo"
Kampuni ya Blackwater inashughulika na ulinzi wa aina tofauti duniani.
Picha hapo juu inaonekana moja ya gari ambalo lilimelipuliwa kutokama na hali ya kutokuwa na usalama wakuridhisha.