Thursday, August 28, 2014

Hamas na Izrael wa kubaliana suruhu.

Hamas na Izrael wa kubaliana suruhu.

Gaza/Jerusalem - Makshariki ya Kati - 28/08/2014. Izrael na wapiganaji wa kundi la Palestina wafikia makubaliano ya kusimamisha mapigano.

Wakiongea kwa nyakati tofauti, viongozi wa pande zote mbili walidaikuwa kila upande umepata ushindi.

Akiongea kwa mara ya kwanza tangu kutangazwa kwa makubaliano hayo 26/08/2012 jiji Kairo, waziri mkuu wa Izrael Benjamin Netanyahu alisema '' tumelitia adabu kundi la Hamas, na Izrael haikukubaliana na masharti yaliyo tolewa na kundi la Hamas katika mazungumzo yaliyo fanyika Misri Kairo.''

'' Na hatutafungu bandari au kiwanja cha ndege au kuondoa vizuizi na hatuta kubali au kuruhusu kundi la Hamas kurusha roketi zake ndani ya Izrael.''Aliongezea waziri Netanyahu.

Nalo kundi la Hamas limesema kupitia msemaji wake Sami Abu Zuhri '' Huu ni ushindi kwa Wapalestina wote, na bila kupambana hii hali isingetokea, bado tuendeleza mapambano mpaka Palestina itakapo pata haki yake.''

Vita kati ya Hamas na Izrael vimechukua siku 50, ambapo Wapalestina  2,139 walifariki dunia kutokana na mashambulizi ya kutoka jeshi la Izrael, na kwa upande wa watu 70 walipoteza maisha yao kati yao 64 wanaj
wanajeshi wa Izrael na raia sita.

Kwa mujibu wa habari kutoka katika kikao cha makubaliano, pande zote mbili zimekubaliana kusimamisha mapigano kwa muda wa mwaka.

Tuesday, August 26, 2014

Baba ya gaidi asadikiwa kuwa mpiganaji wa Al-Qaeda.

Nguvu zatumika kwa Rais Salva Kiir na Riek  Machar ili kuleta amani 

Juba, Sudani ya Kusini - 26/08/2014. Rais wa Sudani ya Kusini na kiongozi wa kundi linalo pingana na serikali yake wamesaini  mkataba wa kusimamisha vita vya wao kwa wao na kupewa siku 45 kuunda serikali ya muungano.

Rais Salva Kiir na Riek Machar, walikubali kusaiani makubaliano ya kusimamisha mapigano, baada ya jumuiya ya shirikisho la maeneo ya Afrika Mashariki - IGAD na jumuiya ya kimataifa kutishia kuweka vikwazo kwa yoyote atakaye pinga kusimamisha mapigano.

Akiongea mara baada ya kusainiwa makubaliano ya kusimamisha vita kati ya serikali ya rais Kiir na kundi linalo muunga mkono  Riek Machar, waziri mkuu wa Ethiopia Hailemaria Desalegn alisema ''tumetoa ujumbe kamili kwa viongozi wa Sudani ya Kusini yakuwa kitendo chochote cha kuchelewesha  kutimiza makubaliano ya amani hakitakubaliwa na ikitokea hivyo basi hatua zitachukuliwa.''

Tangu kuanza kwa vita kati ya serikali ya rais Salva Kiir na kundi linalo muunga mkono Riek Machar, maelfu ya watu  wameuwawa na zaidi ya milioni mbili kukimbia makazi yao na kati ya hao 100,000 walikimbilia katika maeneo ya ofisi za umoja wa mataifa zilizopo nchini Sudani ya Kusini na kufanya ndiyo makazi yao.

Mgogoro wa uongozi ulikuwa ndiyo chanzo cha  vita nchini Sudani ya Kusini, baada ya rais Salva Kiir kumfukuza kazi Riek Machar, ambaye alikuwa makamu wake wa urais

Baba ya gaidi asadikiwa kuwa mpiganaji wa Al-Qaeda.

New York,, Marekani - 26/08/2014. Baba mzazi wa mtuhumiwa ambaye aliye mchinja mwandishi wa habari, yupo jela nchini Marekani akisubiri hukumu ya kuhusika katika mauaji, kupanga mauaji na kulipua mabomu.

Adel Abdel Bari 54, ambaye anashitakiwa kwa kuhusika katika milipuko ya mabomu yaliyo tokea nchini Kenya na Tanzania 1998, ambapo ofisi za balozi zilizopo nchini humo zililipuliwa kwa mabomu na kusababisha maafa makubwa  na mauaji ya kutisha.

Habari  za kikachero zimethibitisha  kuwa '' Bari ni baba  wa mpinajii wa kundi la ISIS Abdel Majid Abdel Bari au kwa jina la John, ambaye inasadikiwa ndiye aliye fanya kitendo cha kinyama, kwa kumchinja mwandishi habari James Foley ambaye alikuwa raia wa Marekani''

 '' Bari alikuwa akiongoza katika kuunganisha mawasiliano ya  wapiganaji wa kundi la Al-Qaeda walio  kuwepo nchini Kenya na makao makuu ya Al-Qaeda''

'' Na vile vile inaminika alikuwa mmoja wa kiongozi na mwanajeshi a mwenye  cheo cha juu, na alikuwa karibu saana na Osama bin Laden.''Ziliongeazea habari hizo za kikachero.

Adel A Bari, ambaye hapo mwanzo alishikiliwa na polisi nchini Uingereza kwa muda miaka 14, kwa kushukiwa kuhusika na makosa ya kigaidi, aliachiwa huru baada ya kukosekana ushahidi, lakini baadaye alikamatwa na kupelekwa Marekani kwa kutakiwa kujibu mashitaka kama hayo.

Syria ipo tayari kushirikaiana na Marekani.

Damascus, Syria - 26/08/2014. Serikali ya Syria imesema ipo tayari kushirikiana na Marekani katika kupambana na kundi la kigaidi la ISIS.

Akiongea kuhusu ni nini kifanyike ili kukabiliana na kundi la ISIS, waziri wa mambo ya nchin wa Syria Walid Moallem amesema '' juhudi zozote za kukabiliana na kundi la ISIS zinakaribishwa, na tupo tayari kushirikiana na Marekani kwa kupitia mwamvuli wa umoja wa mataifa wa kupambana na ugaidi duniani.''

Maeleozo ya waziri Moallem, hayakujibiwa na serikali ya Marekani, kwani Marekani ni moja ya nchi inayo pinga kuwepo kwa utawala wa rais Bashar al Assad, ambaye serikali yake imekuwa ikipambana na magaidi wa kundi la ISIS, ambo wamekuwa wakipata misaada kutoka serikali za Magharibi ili kuing'oa madarakani serikali ya rais Bashar al Assad.







Monday, August 25, 2014

Uturuki na Ujerumani za vutana juu ya ukachero.

Iran yatungua ndege aina ya drone ya Izrael

Tehran, Iran - 25/08/2014. Serikali ya Iran imetangaza kuwa imeangusha ndege inayo endeshwa kwa mtandao ''Drone'' ambayo ilikuwa imengia kwenye anga la Iran.

Akiongea kuhusu kuangashwa kwa ndege hiyo aina ya drone,  Brigedia General Ramezan Sharif alisema '' Drone tuliyo iangusha inauwezo wa kuzunguka mduara wa kilomita 800 na kuruka urefu wa km 1,600 kutoka usawa wa bahari.''

''Hii drone tuliyo iangusha ni kutoka Izrael, naikikuwa inaelekea kwenye eneo la mitambo lenye mitambo ya kinyuklia ya Natanz, na bado tunaendelea kuchunguza zaidi nini kilichopo katika drone hii tuliyo idondosha.''

Kutunguliwa kwa drone ya Izreal nchini Iran, kumechukuliwa kama kitendo cha hatari kwa Iran, kwani Izrael ilisha dai kuwa ikibidi itafanya mashambulizi katika kituo cha mitambo ya kinyuklia cha Natanz.

Uturuki  na Ujerumani za vutana juu ya ukachero.

Ankara, Uturuki - 25/08/2014. Serikali ya Uturuki, imeshutumu serikali ya Ujerumani, kwa kitendo cha kukachero mienendo ya serikali ya Uturuki kwa muda miaka 38.

Shutuma hizo zimetolewa kwa mara ya pili, baada ya zile za mwanzo zilizo lipotiwa na gazeti la Ujerumani la Der Spiege, ambalo August 17,  liliripoti kuwa '' Ujerumani imekuwa ikikachero nchi ya Uturuki kwa niaba ya nchi za NATO.''

Akiongela suala hili, waziri wa mambo ya ndani wa Uturuki Efkan Ala,alisema hiki kitendo cha ukachero ni cha hatari kati ya nchi marafiki

Hata hivyo habari zilizo toka ofisi ya mambo ya ndani ya Uturuki  ziliasema ''kitengo cha usalama BND kimekuwa kikifanya shughuli ya ukachero zidi ya Uturuki tangu mwaka 1976, baada ya kuidhinishwa na aaliyekuwa Kansela wa Ujerumani Helmut Schmidt, ambaye alikuwa kiongozi wa SD - Social  Demokratiki.''

Hata hivyo, serikali ya Ujerumani, hakuelezea kuhusu shutuma hizo za kutoka serikali ya Utiruki, bali msemaji wa serikali alisema '' Uturuki ni nchi mwana chama wa NATO, na nchi rafiki wa Ujerumani hii ndivyo mahusiano yaliyopo kati ya nchi hizi mbili.''

Nchini Ujerumani kuna watu zaidi ya millioni 3 wenye asili ya kutoka Uturuki, ambapo umekuwa ndiyo kiungo cha nchi hizi mbili kuwa na ukaribu kwa sana.

Urusi kupeleka tena misaada ya kiutu nchini Ukraine.

Moscow, Urusi - 25/08/2014. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Urusi, ametangaza kuwa, nchi yake itapeleka misaada kwa mara nyingine nchi Ukraini, na kuzitaka nchi nyingine kuunga mkono jitihada hizo za Urusi.

Waziri Sergey Lavrov,aliyasema hayo wakati alipo kuwa akiongelea hali halisi ilivyo nchini Ukraine kwa kusema '' sisi tutaendelea kutoa misaada kwa watu wanao hitaji misaada, hiyo kwani hali iliyopo katika maeneo yaliyo shambuliwa na yanayo zidi kushambuliwa na jeshi la serikali ni mbaya sana.''

''Na msafara wa pili wa misaada unatarajiwa kuondoka wiki hii kwa kupitia njia ile ya mwanza, na tunaomba ushirikiano na kutoka kwa serikali ya Ukraine, kwani serikali ya Ukraine imefunga na kuzuia huduma zote za kibinadamu, jambo ambalo ni kinyume za  haki za binadamu.'' Aliongezea waziri Lavrov

Ni wiki sasa, tangu  Urusi ilipo iliamua kuingiza misaada nchini Ukraine, bila ruhusa kutoka kwa serikali ya Ukraine, jambo ambalo lililalamikiwa na washiriki wanao unga mkono serikali ya Kiev, lakini Urusi ilisisitiza kuwa ilikuwa inafanya hivyo kwa nia ya kusaidia watu waliokumbwa na maafa ya vita vya wenye kwa wenye vinavyo endelea nchini Ukraini.


Saturday, August 23, 2014

Urusi ya fanya kweli kwa mara nyingine

Waziri Mkuu wa Uingereza awekwa njia panda na ISIS na rais Bashar al Assad.


London, Uingereza - 23/08/2014. Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron, amekumbwa na wakati mgumu kutoka kwa baadhi ya wabunge na viongozi wazamani wa serikali wa Uingereza, kwa kutakiwa kuangalia upya uhusiano na serikali ya rais Bashar al Asad katika mkakati wa kupambana na kundi la ISIS.

Wakiongea kwa nyakati tofauti, viongozi hao walisema '' Ili kuweza kukabiliana na wimbi la kundi la ISIS, ipo haja ya kushirikiana na serikali ya Syria, ambayo inauweza kupambana na kundi hilo,kwani itakuwa nivugumu kwa serikali za magharibi kupambana na kundi hilo peke yao.''

Saga hiyo ambayo inamwandama waziri David Cameron,  imekuja baada ya picha za mauaji ya mwandishi wa habari wa Marekani James Foley kusambazwa mitandaoni na kundi la ISIS na kudai kuwa wale wote wanao isaidiia Marekani wajiaandae na malipo kutoka kwa kundi hilo.

Kundi la ISIS ambalo hapo awali lilikuwa linapambana na serikali ya rais Assad, na kuungwa mkono na serikali za Magharibi, lilibadirisha mwelekeo wake nchi Irak, na kuwa mpinzani wa nchi za Magharibi, jambo ambalo limeleta tishio kwa nchi hizo.

Kutokana na uamuzi wa kundi la ISIS kugeuka kupingana na sera za nchi za Magharibi nchini Irak,  limefanya Marekani na washiriki wake kuaanza kulishambulia kijeshi kundi hilo na kulifanya kundi hilo kutangaza vita na nchi za Magharibi.

Hadi kufikia sasa, kuna idadi ya raia 500 wa Uingereza ambao ni wapiganaji wa kundi la ISIS, ambao inahofiwa wakirudi nchi Uingereza wanaweza kuwa watu wahatari kiusalama wa nchi.

Urusi ya fanya kweli kwa mara nyingine.


Moscow, Urusi - 23/08/2014. Serikali ya Urusi, imetangaza kuwa  imefanikiwa kupeleka misaada ya kiuutu nchini Ukraini na magari yaliyobeba misaada hiyo yamerudi salama.

Akiongea baada ya kurudi salama magari hayo, naibu waziri wa misaada na dharula wa Urusi Eduard Chizhikov amesema '' magari 227 aina ya maroli yamerudi salama, baada ya kushusha misaada nchi ya kiutu nchini Ukraini''

Akiongea kuthibitishwa kufika kwa misaada nchini Ukraine, mkuu msaidizi wa umoja wa matifa katika masuala ya haki za kibinadamu na dharula Valerie Amos, amesema ''nimeweza kuongea na wakazi wa Slavyanks ambao wamekimbia kutokana na vita,na kushuhudia misaada waliopata.''

''Kikubwa kinachotakiwa ni kwa jumuiya ya kimataifa na kuangalia upya hali ya utoaji wa misaada ya kiutu, kwani wote tunakubaliaana kuwa kunahaja ya kutoa misaada kwa watu walikumbwa na matatizo ya vita vinavyo endelea nchini Ukraine.'' Aliongezea bi Valerie Amos.

Hata hivyo kitendo cha magari hayo ya kutoka Urusi kuingia bila  ruhusa ya serikali ya Ukraini kimelaumiwa na Marekani na washiriki wake, lakini serikali ya Urusi imesema haitatilia maanani lawama hizo kwani Urusi imefanya jambo la kiutu na ''hakuna kitakacho zuia Urusi kutoa misaada ya kiutuu inapohitajika Urusi kufanya hivyo''

Misaada hiyo ambayo ilipelekwa katika mji wa Lugansk, baada ya serikali ya Urussi kuamua kuingiza misaada hiyo ambayo ilikaa mpakani kwa muda wa wiki ambapo serikali ya Kiev ilikuwa inapinga kuingia kwa misaada hiyo nchi Ukraini, kwa madai inaweza ambatanishwa na siraha kwa ajili ya wapinzani serikali hiyo.




Tuesday, August 19, 2014

Iss yatangaza vita zidi ya Marekani.

Iss yatangaza vita zidi ya Marekani.

Tikrit, Iraq - 19/08/2014. Wapiganaji wa kundi la ISS la Irak wamebakia wakilishirilia mji wa Tirkit, baada ya jeshi la Iraq kushindwa kuendelea na mashambulizi kutokana na kukosa vifaaa vya kijeshi.

Kwa mujibu wa msemaji wa jeshi ambaye hakutaja jina lake alisema '' imebidi tusimamishe mashambulizi yetu, kwani wapiganaji wa ISS wapo na vifaa vya kisasa na pia hatuna vifaa ya kutegua mabomu ambayo yametegwa karibu kila eneo la kuingia mji wa Tikrit.''

Mji wa Tikrit ambao ni makazi na alipo zaliwa na kuzikiwa aliyekuwa rais wa Iraq Saddam Hussein, umekuwa chini ya wapiganaji wa kundi ISS, ambalo lina pingana na serikali ya Irak.

Kundi la ISS limetangaza kuwa ''litafanya mashambulizi kwa Marekani na washiriki wake wakati wowote na mahali popote kuanzia sasa.''
 Kundi la ISS linapambana na jeshi la Irak, jeshi la Wakurdi ambapo yanapata msaada kutoka kwa Marekani na washiriki wake, jambo ambalo limefanya hali ya usalama nchi Irak kuzidi kuwa tete zaidi.

Kenya kuwe ugumu kuingia nchini humo.

Nairobi, Kenya - 19/08/2014. Serikali ya Kenya imetangaza kuwa itasimamisha usafiri wa anga kutoka nchi ambazo zimekumbwa na ugonjwa wa ebola.

Uamuzi huo umekuja baada ya utafiti kufanywa na wataalamu wa afya nchini Kenya  na  kuonekana kuwa kuna hatari ya Kenya kukumbwa na ugonjwa huo kutokana na kuwa kiungo cha ndege nyingi zitokazo na kuingia nchini humo kutoka sehemu tofauti katika bara la Afrika.

Nchi ambazo zitahathirika na kusimamishwa kwa usafiri wa anga ni pamoja na ''Liberia na Nigeria''

Ugonjwa wa ebola umekuwa tishio hasa kwa nchi za Afrika ya Magharibi na kusabibisha vifo vya watu 1000 mpaka sasa, na kufanya shirika la afya dunia WHO kutangaza vita rasmi zidi ya ugonjwa huu.