Wednesday, September 24, 2014

Viongozi wa dunia waambiawa amani huja kwa gharama.

Viongozi wa dunia waambiawa amani huja kwa gharama . 
  
New York, Marekani 24/09/2014. Rais wa Wamarekani, amehutubia mkutano wa viongozi na wakuu wa nchi walio hudhuria katika kikao cha 69 cha umoja wamataifa ambacho kimeanza rasmi wiki hii.
 
Akihutubia rais Baraka Obama alisema " dunia inatakiwa kushirikiana katika kuleta amani na kuilinda, kwani vita vya kupitia mlango wa nyuma vinavyo endelea havita leta suruhu kwa kila upande."
 
"Na inatakiwa kutumia nguvu za kila namna ili kuweza kushinda na kuleta amani, na wakati mwingine  amani inakuja baada ya gharama ya kivita kuwepo."
 
"Inabidi sheria za kimataifa zifuatwe ili amani iwepo, kwani vita vya imani za kidini ndiyo chanzo cha matatizo yote  vita."
 
 "Hivyo inatakiwa ushirikiano wa kweli ili kupata ufumbuzi kwanini imani za kidini zinaleta vita, na mfano halisi ni kati ya Shia na Suni nchini Irak."
 
Rais Obama, alizungumza kuwa Marekani itakuwa mshiriki mkubwa katika kutetea demokrasi na amani popote duniani, na haitaona haya kufanya hivyo, "kwani huo ndiyo msingi uliyo ijenga na ambao unaendelea kuijenga Marekani hadi sasa."
 
"Tunamatatizo yetu kama nchi nyingine, hii nikuonyesha kuwa, licha ya kuwa na matatizo kama nchi, lakini hatuachi kuwa mstari wa mbele katika kutetea demokrasi nza haki za binadamu ndani na nje ya nchi, kwa kupinga ukandamizaji na ubaguzi wa kila namna  na huu ndiyo msimamo wa Marekani"
 
Pia katika hotuba yake, rais Obama, aliilaumu Urusi kwa kuwa muhusika mkuu katika utibuaji wa amani nchini Ukraini, na vile vile akusita kuzishambulia nchi ambazo zinasaidia makundi ya ISI na washiriki wake kifedha na kuzitaka kuacha kufanya hivyo japo akuzitaja majina.
 
Akisitiza rais Obama, alinikuhuu maneno ya kitabu Kitakatifu kwa kuseme "mtendee mema mwenzio kama unavyo taka kutendewa" na kusema wale wanaofanya mabaya wanakwenda kinyume na maagizo ya Mungu.
 
Kwanye hotuba yake Obama alisisitiza pia ni muhimu kwa serikali za nchi zote kupambana na elimu ya itikadi kali, ambayo inaleta mvurugo wa amani, na hata kama ina tolewa na "Wakristo, Wayahudi, Waislaam au Waumini wa dini yoyote." kwani kwa kuachia hii itikadi basi jamii nzima itaaathirika na matokeo yake yanaonekana.
 
Mkutano  wa 69 wa umoja wa mataifa unawakutanisha viongozi wapatao 140 , ambao wanatarajiwa  kuzungumzia na kujadili masuala ya kuongezeka na kukua kwa makundi ya itikadi kali duniani, na jinsi ya kuyadhibiti na pia mbinu za kupambana na magonjwa hatari na hasa ugonjwa wa Ebola ambao umekuwa tishio kwa jamii ya kimataifa.
 
Bwana matata aliyekuwa mwiba kwa Uingereza aachiwa huru. 
 



Amman, Jordan - 24/09/2014. Mahakama ya jijini Jordani, imemuachia huru mtuhumiwa aliye kuwa akishitakiwa kwa kupanga mauaji ya watalii wa raia wa Kiizrael,  Marekani  na pia  raia wa Jordani wakati wa sikuku ya kuanza karne mpya mwaka 2000 katika jiji la Amman.

Abu Qatada, ambaye alikuwa nchi Uingereza kama mkimbizi na baadaye kuwa mpinzani na mkosoaji wa serikali ya Uingereza na siasa zake za nje  kutokana na msimamo wake wa itikadi kali, jambo ambalo lilisababisha asafirishwe kurudi kwao Jordan na kukumbana na   mashitaka yaliyo kuwa ya kimkabili, na hatimaye  mahakama jijini Jordani imemwachia huru baada ya kukumkuta hana hatia.

Akiongea baada ya kuachiwa huru waziri wa mambo ya ndani wa Uingereza  Thereza May amesema " Abu Qatada hataruhusiwa kurudi Uingereza, kwani alikuwa mtu hatari katika jamii ya Kiingereza na ni raia wa Jordan hapa alikuwa amepewa hifadhi ya kikimbizi tu."

Abu Qatada au kwa jina jingine Omar Othman alishutumiwa kwa kuhusika kwa njia moja au nyingine na kundi la Al Qaeda, na pia kuhusika katika kufundisha itikadi kali za kidini, na vile vile kuwashawishi vijana wa Kiingereza kujiunga na kundi la Al Qaeda na kusadikiwa kuwa ni kiongozi wa kundi hilo nchini Uingereza na kuwa mwiba kwa wanasiasa na serikali nzima.

Naye Abu Qatada akiongea baada ya kuachiwa alisema " Nilipewa nafasi ya kujitete na ukweli umeonoekana kuwa sikuwa na makosa, na yote yaliyozungumzwa zidi yangu yalikuwa ya kuzushwa kisiasa."

Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Qatada kuachiwa huru, baada ya ya kesi aliyokuwa akishutumiwa yakuwa alikuwa na mpango wa kushambulia shule ya Kimarekani iliyopo nchini Jordani kutupiliwa mbali na Mahakam kwa kukosekana kwa ushahidi.

Mwaka 2000, mahakama ya jijini Jordani,ilimuhukumu Abu Qatada kwenda jela miaka 15, wakati huo alipo kuwa akiishi ukimbizini nchini Uingereza, baada ya kukubaliwa kuishi nchini huko kama mkimbizi mwaka 1994.







Friday, September 19, 2014

Wascotland waamua kuendelea na Muungano hauheni kwa waziri mkuu David Cameron.



Wascotland waamua kuendelea na Muungano kuwa hauheni kwa waziri mkuu David Cameron.
 
Glasgow, Uingereza - 19/09/2014. Wascotland wame amua kuendelea kuwa sehemu ya muungano wa Uingereza, baada ya matokeo ya kura kutoa jibu lililo kuwa likisubiliwa..
 
Majibu hayo yalitolewa baada ya kura kupigwa kujua nini wananchi wanataka kuhusu muungano, na kura nyingi zilitoa majibu ya kuwa kuendelea kuwa kwenye muungano na tofauti na wale waliopiga kura kujitoa.
 
Akiongea mara baada ya matokeo ya kura, waziri mkuu wa Scotland Alex Salmond na ambaye alikuwa kinara katika kuongoza kampeni ya kujitenga na muungano alisema " Wascotland wameamua kwa wingi  kwa sasa kuendelea kuwa katika muungano, hivyo naomba tushirikiane  na kuwa pamoja katika kuendelea kuijenga Scotland."
 
"Kilicho baki tungoje nini kitafanyika, kama kambi ya kuunga mkono muungano itatekeleza iliyo ahaidi wakati wa kampeni zao."Aliongezea waziri mkuu Solmond.
 
Naye waziri mkuu wa Uingereza, David Cameron akihutubia taifa baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa alisema
 " Ni jambo la kujivunia kuwa Wascotland wamekubali kuendelea kuwa sehemu ya muungano wa Uingereza, na napenda kuwahakikishia kuwa yote tuliyo haidi yatatekelezwa na hii siyo tu kwa Scotland, bali pia kwa Wales, England na Irelandi ya Kaskazini."
 
Kufuatiwa matokeo ya kura za Scotland za kuunga mkono kuendelea kuwa sehemu ya muungano wa Uingereza, mabadiriko makubwa ya kiutawala na kisiasa yana tarajiwa kutokea, kwani nchi zilizomo kwenye muungano wa Uingereza ambazo ni Wales, England na Ireland ya Kaskazini nazo zimetaka zipewe haki sawa kama Scotland.
 
Jambo ambalo serikali ya waziri David Cameron itakuwa na wakati mgumu katika kukamilisha matakwa hao.
 
Hata hivyo wataalamu wa siasa wameeleza kuwa mmatokeo ya kura, yamemsaidia waziri mkuu David Cameron, kwani kama yangekwenda kinyume na matarajio ya serikali yake, basi angekuwa na wakati mgumu kioungozi na historia ya Uingereza inge mnata kuwa David Cameron kama waziri mkuu alishindwa kuulinda muungano.
 
Afrika kuwa na kizazi zaidi kuliko mabara mengine.
 
Washington, Marekani - 19/09/2014. Dunia itakuwa na ongezeko la wingi wa atu ifikapo mwaka 2100, na asilimia kubwa la ongezeko hilo litakuwa katika bara la Afrika.
 
Adria Aftery, ambaye ni mtaalamu wa mahesabu ya ongezeko la watu kutoka chuo kikuu cha Washington alisema " kunauwezekano mkubwa wa ongezeko la watu ifikapo 2100, hasa katika bara la Afrika kwa asilimia 80% kutoka watu billion 3.5 na kuwa na ongezeko la 5.1."
 
"Na hivyo kufikia mwaka 2100 ongezeko la watu litakuwa mara nne zaidi kutoka billioni 1 na kufikia billion 4." Alisisitiza  Profesa Adrian Raftery.
 
"Hadi kufikia sasa idadi ya watu duniani imekuwa ikiongezeka kwa asilimia 1.14 kwa mwaka na hili niongezeko mara mbili katika kipindi cha miaka 40 iliyopita toka mwaka 1959 hadi 1999 kutoka billion 3 hadi kufikia billioni 6." aliongezea Profesa Raftery.
 
Kwa mujibu wa habari kutoka kwa watafiti wa ongezeko la watu duniani, ongezeko kubwa la watu limekuwa kubwa katika bara la Asia, ambapo nchini kama India na China zimekuwa na ongezeko la watu kitaifa.
 
Na katika bara la Afrika, Nigeria imekuwa naongezeko kubwa kitaifa na kukadiriwa huenda nchi hiyo ikawa ya tatu dunia,  itakapo fika katikati ya karne ya 21 na kupita  nchi zilizopo katika mabara ya Amerika kwa ujumla.
 
Julian Assange aichimba na kuiweka wazi Google.
 
London, Uingereza - 19/09/2014. Mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks Julian Assange, ameendelea kufumbua siri, kwa kusemakuwa kampuni mama ya kimmtandao ya Google ni mshiriki mkubwa katika kutoa siri na habari za watu kwa serikali.

Akiongea Julian Assange alisema "Google inafanya kazi pamoja na kitengo cha masuala ya usalama cha GCHQ cha Uingereza  na NSA cha Marekani, na inapata kipato chake kwa asilimia 80%  kwa kufanya kazi ya ushushu kwa kukusanya na kuzigawa habari za watu na shughuli zao za kibinafsi kwa mashirika hayo."

"Na Google ilipata mkataba wa kufanya kazi hiyo mwaka 2002." aliongezea Assange.

Julian Assange, ambaye kwa sasa anishi ukimbizini katika ofisi za kibalozi za nchi ya Ekwado zilizopo nchini Uingereza, amekuwa akisubiriwa nje ya jengo hilo na polisi wa Uingereza,  ili wamkamate na kumpeleka nchini Swiden,  ambapo anatakiwa kujibu mashitaka ya kuhusika na maingiliano bila hiyari na wana dada wawili wakati alipo kuwa nchini Swiden.

Thursday, September 18, 2014

Rais wa Ukraine aililia Marekani kimsaada.

Leo ni siku ya Waingereza wasimama njia panda.

Glasgow, Scotland - 18/09/2014. Wananchi wa Uingereza wapo katika mtazamo tofuti na kutokujua nini kitatokea, kwani leo hii raia wakazi wa Scotland wanapiga kura ili kuamua kama wataendelea kuwa katika muungano wa Uingereza au kujitenga na muungano huo na kuanza kujitawala, jambo ambalo limeleta tumbo joto kwa Waingereza walio wengi.

Kura hizo ambazo zimeaanza kupigwa leo hasubuhi, huku  wanasiasa wa pande zote, wanao unga mkono kujitenga  na wale wanao pinga kujitenga, watakuwa wanasubiria kuona kama kampeni walizo fanya zimeleta matokeo waliyo tarajia.

Matokeo ya kura hizo yatangazwa siku ya Ijumaa 19/09/2014.
Ikiwa wananchi wa Scotland watapiga kura kujitenga, kutavunja muunganao ulidumu  miaka 307, jambo ambalo litaleta mabadiriko makubwa ya kisiasa, kiuchumi,kijamii na pia kiutawala wa kifalme.

Rais wa Ukraine aililia Marekani kimsaada.

Washington, Marekani - 18/09/2014. Rais wa Ukraine, ameitaka Marekani kuipatia nchi yake siraha na vifaa vya kivita ili serikali yake iweze kuzitumia kuleta amani Mashariki mwa Ukraine.

Akihutubia bunge la Kongresi la Marekani, rais Petro Poroshenko alisema "Blangeti na vifaa vya kuangazia usiku wa giza ni muhimu, lakini hata hivyo blanketi haziwezi kusaidia kushinda vita na kuleta amani, hivyo tunaomba mtupe vifaa vya kivita ambavyo vitasaidia kuleta amani."

Akipigiwa makofi na wabunge wa  Kongresi, rais Poroshenko aliongezea "Naiomba Marekani kutupatia msaada ya kiulinzi ambao utaambatana na ushirikiano wa jumuhia ya NATO, kwa Ukraine haitaweza kusimama peke yake katika mapambano haya."

Vile vile katika hotuba yake, rais Porocshenko, aliitupia lawama Urusi kwa kuhusika katika kuvuruga amani nchini Ukraine kwa kuwaunga mkono wapinzani wa serikali yake.

Na pia rais Poroshenko alifananisha hali iliyopo nchini Ukraine ni sawa na ile iliyotokea Georgia, na hivyo Marekani ni muhimu kutoruhusu hali kama hiyo kutokea tena.

Thursday, September 11, 2014

Marekani kufanya mashambuli nchini Syria zidi ya ISI.

Boko Haram yateka mji mzima.

Maiduguri, Nigeria - 11/09/2014. Kundi linalo pingana na sheria za serikali ya Nigeria la Boko Haram limewaweka wakazi wa mji Maiduri roho zao juu kwa kutangaza kuwa mji huo upo chini ya utawala wao.

Kwa mujibu wa habari kutoka kwa wakazi wa mji huo na kuthibitishwa na kundi la Boko zinasema "kundi la Boko Haram, lipo kati ya km 40 kwa 50 kila upande wa mji wa Maiduguri,  na hivyo wamefanikiwa kuuzingira mji wa Maiduguri nawanaweza fanya mashambulizi kutoka kila upande wa mji huo wakati wowote."

Hata hivyo kufuatia tangazo hilo la kundi la Boko Haram, serikali ya Nigeria imekataa kuongelea suala hilo.

Kundi la Boko Haram limekuwa likisumbua na kutibua amani nchini Nigeria kwa kutaka wanachi wa nchi hiyo kufuata sheria za dini ya Kiislaam  na wakikataa wamekuwa wakiuwawa au kuteswa.

Vile vile kundi hilo limekuwa likiwakamata watu kwa nguvu  na kuwaficha na pia kundi hilo katikati ya mwaka huu  lilishutumiwa na jamii ya kimataifa baada ya kuwateka wanafunzi wa kike wapatao 200  siku ya 29/Juni/2014, na ambapo mpaka leo wanafunzi hao hawajulikani walipo, japo kuliwepo haadi za kimataifa ya kuwa wataokolewa muda siyo mrefu tangu wa wanafunzi hao wa kike watekwe.

Ni miaka 13 tangu mashambulizi ya Septemba 11/2001.

New York,  Marekani - 11/09/2014. Wanachi wa Marekani leo wamefanya maombi na sara kwa kuwakumbuka mamia ya wata walio umia na kufariki dunia baada ya mashambulizi ya kigaidi kufanywa  nchini humo miaka 13 iliyo pita.


Mashambulizi hayo ambayo yalifanyika mwaka 11/09/2001 na kundi la kigaidi la Al Qaeda na kusababisha upotevu wa maisha, ajali na uharibifu wa mali, yamefanyiwa kumbukumbu nchini kote.
Huku rais Baraka Obama akiwa mongozi mwa Wamarekani walio omboleza na kusari katika kukumbuka siku hiyo  ya Septemba 11 ambapo   majina ya wale wote walipoteza maisha kutokana na mashambulizi hayo yalisomwa kwa kuwakumbuka.
Hii ndiyo majengo ya Manhatani yanavyo onekaa kabla ya mashambulizi.

Kufuatia mashambulizi hayo yanayo julikana kama Septemba 11, serikali ya Marekani ilitangaza vita zidi ya ugaidi wa kila namna na kuanza kupambana na kundi la Al Qaeda  na washiriki wake na kufanikiwa kumuua kiongozi wa kundi la Al Qaeda,  Osama bin Laden, tarehe  2/05/2011, ambapo alikukuwa mafichoni nchini Pakistan, na mpaka sasa vita zidi ya ugaidi bado inaendelezwa duniani kote na Marekani ikiwa kinarani.


Marekani kufanya mashambuli nchini Syria zidi ya ISI.

Washington, Marekani - 11/09/2014. Rais wa Marekani ametangaza mkakati mpya wa kupambana na kundi la ISI na kuliangamiza bila kuacha kinvuli.

Akilihutubia taifa rais Baraka Obama alisema " nia kubwa hasa ni kuahakikisha kuwa kundi la ISI linapotea na kutokuwepo, na hivyo kila njia itatumika ili azimio hili lifikiwe na hatutasita kuwafanya mashambulizi mahali popote walipo ISI ."

Katika hotuba hiyo, rais Obama aliongea kuwa serikali yake itatoa  wanajeshi wasio pungua 500 ambao watahusikia katika masuala ya ufundishaji kwenye jeshi la Irak,  jeshi la Wakurdi na wapinzani wa serikali ya Syria  ili kuweza kupamana na na kundi la ISI lenye mizizi yake nchini Irak  na hivyo kuliomba bunge la Kongresi la Marekani kukubaliana naye kwa kuunga mkono serikali yake katika mpango wa kuwapa  kutaka kutoa mafunzo ya kijeshi.

Kufuatia hotuba hiyo, Marekani itakuwa na uwezo wa kufanya mashabulizi nchini Syria, ambapo pia kundi la ISI limekuwa likipiga kambi zake katika kutimiza azma yake ya kukuza kundi hilo la ISI.

Hata hivyo serikali ya Syria imeonya  kuwa "kitendo cha kufanya mashambulizi nchini Syria kwa kusingizio cha  kufanya mashambulizi zidi ya kundi la ISI,  halitakubalika na itakuwa ni kitendo cha kuvunja sheria za kimataifa." Alisema waziri wa mambo ya maridhiano na mapatano wa  Syria  Ali Haidar.

Akiongezea Haidari alisema " Syria imeshatangaza kuwa ipo tayari kushirikaiana na jumuiya ya kimataifa katika kupambana na kundi la ISI, na haitakuwa jambo la busara kufanya mashambulizi ndani ya Syria kwa kisingizio cha kuwashambulia wapiganaji wa ISI."

Naye msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Urusi, Alexander Lukashevich, akizungumzia kuhusu uamuzi wa Marekani kuamua kufanya mashambulizi kwenye makazi na vilinge vya wapinzani walioko chini Syria  alisema "ikiwa kitendo hicho kitafanyaka, basi kitakuwa ni kitendo cha utumiaji wa nguvu kinyume cha sheria na itakuwa vyema kushirikiana na serikali ya Syria kabla ya kufaya mashambulizi nchini humo."

Marekani imekuwa ikikuwa ikifanya kila njia ili kupambana na kundi la ISI, wakati huo huo imekuwa ikitaka utawala wa rais wa Syria Bashar al Bashir utolewe.

Wednesday, September 3, 2014

Mgonjwa wa Ebola raia wa Uingereza apona.

Tutawasaka wauaji na kuwaangamiza asema rais Baraka Obama.

 Estonia, Tallinn - 03/09/2014. Rais wa Marekani, amelaani kitenndo cha kuuwawa kinyama kwa raia wa Marekani ambaye alikuwa akishikiliwa na kundi la ISI linalo pambana na serikali ya Irak na sekali ya Syria.

Rais Barak Obama alilaani kitenndo hicho, baada ya  kundi la ISI kusambaza video kwenye mitandao inayo onyesha kuuwawa kinyama kwa raia wa Kimarekani Steven Sotloff ambaye alikuwa akifanya kazi ya uandishi wa habari.

 Akiongea wakati wa ziara yake nchini Estonia,  rais Baraka Obama alisema '' vyovyote kundi la ISI litakavyo fanya, halitafanikiwa, na watambue tutawasaka na kuwaweka kwenye vyombo vya sheria.''

'' Na wakae wakijua hatuwaachia wala kusahahu kwa vitendo wanavyo vyao vya kinyama wanavyo fanyaa''Alisisitiza rais Obama.

Kuuwawa kwa Steven Sotloff kumekuja baada ya raia mwingine wa Marekani James Foley kuwawa kinyama  na kundi ISI mwezi uliyo pita.

Hadi sasa kundi la ISI limefanya mauaji ya kinyama kwa raia  wawili wa Marekani, ambao wote walitekwa nyara wakati walipokuwa wakufanya kazi za uandishi wa habari, napia kudai kuwa siku za mbeleni lita muua raia wa Uingereza walie naye ikiwa mashambulizi ya ndege za kivita yanayo fanyiwa na Marekani, Uingereza na washiriki hayatasimamishwa.

 Rais, Obama alifanya ziara nchini Estonia, ili kuzihakikishia nchini za Baltik kuwa Marekani na washiriki wake chini ya muungano wa kiulinzi wa NATO upo tiyari kuwasaidia muda wowote kwa hali na mali, na hasa kwa sasa ambapo nchi za Baltik zimekuwa na wasiwasi na jirani ya Urusi.

Kundi la Aqaeda kufungua matawi barani India.

 Al Qaeda - 03/09/2014. Kiongozi wa kundi la Al Qaeda ametangaza kuwa kundi lake litafungua matawi katika nchi  zilizopo katika bara la India ili kukuuza uhusiano na wale wanao unga mkono kundi la Al Qaeda.

Akiongea Ayman al Zawahri alisema, ''Burma, Bangladesh, Assam, Gujarat, Ahmedabad, na Kashimir kwani maeneo haya ni muhimu sana na nia yetu ni kuhakikisha ndugu zetu katika Uislaam wanatendewa haki.''

'' Navile vile napenda kuwaeleza ndugu zetu wa waliipo Afghanistan chini ya uongozi wa Mullah Omar ya kuwa tupo  pamoja.'' Zawahri aliongezea.

Akiongea kuhusu kundi la ISI, kiongozi huyo wa Al Qaeda  Ayman Zawahri alisema '' nikitu ambacho hakitakiwi kufanyika kwa Muislaam kumuonea Muislaam mwingine kwa hali na mali, hivyo ISI wafanyavyo wanakwenda kinyume na Maadili ya Uislaam.

Ugomvi kati ya  ISI na Al Qaeda ulitokea mwaka 2013, baada ya kundi ISI kuanza kushambulia nchini Syria na vitendo vingine vya kuufanya mauaji ya kinyama nchini Irak.

Ayman Zawahri, alichukua kiti cha uongozi mwaka 2011, baada ya jeshi la Marekani kufanikiwa kumwua Osama bin Laden nchini Pakistani.

Mgonjwa wa Ebola raia wa Uingereza apona. 

London, Uingereza - 03/09/2012. Muuguzi raia wa Uingereza ambaye alikuwa amekumbwa na ugonjwa wa hatari wa Ebola, ameruhusiwa kutoka hospitali .

William Pooley 29, ambaye alipata ugonjwa wa Ebola wakati alipo kuwa akifanya kazi nchini ya uuguzi nchini Sierra Leone, alikimbiziwa nyumba Uingereza ili kupata matibabu na alipofika alizwa katika hospitali ya Uhuru wa Kifalme iliyopo London hadi alipo ruhusiwa baada ya waganga kuridhika ya kuwa amepona baada ya kutumia dawa aina ya ZMapp..

 Akiongea mara baada ya kutoka hopspitali, William Pooley alisema ''Nina bahati kupona, kwa nimeshuhudia ugonjwa wa Ebola ulivyo waua watu wengi na ukweli nilikuwa na wasiwasi kuwa nitakufa, jambo ambalo hata familia yangu ilikuwa na wasiwasi pia.''

Mganga Michael Jacobs aliyeongoza katika matibabu ya muuguziWilliam Pooley  alisema '' Pooley yupo mzima na ugonjwa aliyokuwa nao, sasa anweza kwenda nyumbani kuendelea na maisha yake kama kawaida.

Ugonjwa wa Ebola umekuwa tishio kubwa hasa katika bara la Afrika kwenye maeneo ya Afrika Magharibi na sehemu kadhaa nchini Jamuhuri ya Kongo, umepoteza maisha ya watu zaidi 3,500 na wengi wao kutoka Liberia, Sierra Leone, Guinea, Nigeria na Senegal na hivyo dawa ya ZMapp huenda ikawa ndo jibu la kutibu na kuangamiza ugonjwa hatari wa Ebola.

Monday, September 1, 2014

Urusi yapata jibu la kitendawili kutoka EU.

Joto la Urusi la iweka NATO mkao wa chonjo.

Brusells, Ubeligiji - 01/09/2014. Muungano wa kijeshi wa kujihami wa NATO, umetangaza rasmi kuunda kikosi maalumu cha kijeshi ndani ya jeshi hilo ili kuweza kupambana na vitisho kutoka Urusi.

Akiongea, katibu mkuu wa muungano wa NATO, Anders Fogh Rasmussen amesema '' NATO imeshaa andaa kikosi cha wanajeshi 4,000 ambao watakuwa na kazi maarumu ya kukabiliana na vitisho kutoka kwa Urusi na vitisho vingine vitakavyo onekana kuhatarisha nchi wanachama wa NATO.''

'' Kikosi hiki kimeundwa baada  yali halisi ya Ukraini, kwani hali hii inatisha, NATO imeona haja ya kuunda kikosi  hiki maalumu, ambacho kitakuwa na uwezo wa kuwa tayari kwa muda wa masaa 48, na hivyo mkutano wakuu wa nchi wanachama utakao fanyika mjini Newport Weles ndiyo utakao idhinisha kikosi hicho.''

Kuundwa kwa kikosi hicho maalumu cha NATO na ambacho  kitakuwa  kikuzunguka katika nchi za Baltik kimakazi,  kumetiliwa mashaka na wataalamu wa masuala ya ulinzi wa kimataifa kwa kudai kuwa  ''kunaweza vuruga makubaliano ya mwaka 1997 ambapo NATO na Urusi zilikubaliana kuwa hakutakuwepo na kambi ya NATO katika maeneo ya nchi za Baltik.''

Habari za ndani za NATO zinasema ''wanajeshi hao 4,000 hawa takuwa ni  sehemu ya wanajeshi 10,000 ambao Uingereza ilipendekeza hapo awali.

Mkutano wa wakuu wa nchi za NATO unatarajiwa kuaanza siku ya Alkhamisi wiki hii ambapo utatawaliwa na hali ya  Afghanistan baada ya NATO kuondoa majeshi yake nchini humo na pia wimbi la vita vya Ukraini

Ujerumani yabadiri mwelekeo wa mambo yake ya kigeni.

Berlin, Ujerumani - 01/09/2014. Ujerumani imekubali kuwa imesha peleka siraha  nchini Irak ilikusaidia serikali ya Wakurdishi katika kupambana na kundi la ISI ambalo limekuwa likipambana na serikali  kuu ya Irak kivita.

Akilihutubia bunge la Ujerumani, Kansela Angela Merkel alisema ''Kundi la ISIS, ni kundi ambalo ni hatari sana, na inabidi kukabiliana nalo kwa hali na mali, nikundi la kigaidi ambalo linatishia, usalama  wa Wajerumani na Ulaya kwa ujumla.''

''Kama kundi hili likiachiwa litafika Ulaya hadi Ujerumani na siraha walizo nao  watazitumia katika kuhatarisha usalama wa raia wa Ulaya kwa kuendeleza ugaidi, na ndomaana Ujerumani imeamua kuisaidiana na serikali ya Wakurdi ili kulitokomeza kundi hili la ISI.''

Siraha ambazo Ujerumani imezipeleka nchini Irak ni, G3 16,000, G36 Raifo, Siraha za kuzua mabomu ya kulipua vifazu 30, roketi 240, na mabomu ya mkono 10,000.

Kansela Angela Merkel, ilielezea uamuzi huo wa serikali, baada ya vyombo vya habari kutangaza kuwa Ujerumani imesha peleka vifaa vya kivita nchi Irak katika jimbo la Wakurdishi ili wazitumie katika kupambana na kundi la ISI.

Uamuzi huo wa serikali ya Kansela Angela Merkel, ulmeshutumiwa na baadhi ya Wajerumani ambao wanapinga kitendo cha Ujerumani kushiriki katika vita au kutoa msaada wa vyombo vya kivita kwa kuamini unakwenda kinyume na maamuzi ya kihistoria ya Wajerumani.

Lakini hata hivyo, Wajerumani wengine wamekuwa wakiunga mkono uamuzi huo wa serikali, kwa kusema kuwa lazima Ujerumani sasa ibadirike na iwe kipao mbele katika masuala ya kigeni.

Urusi yapata jibu la kitendawili kutoka EU.

Moscow, Urusi - 01/09/2014. Viongozi wa China na Urusi wamefungua rasmi ujenzi wa bomba la gesi ambalo litatumika kusafririshia gesi kutoka Urusi kueleke nchini China.

Akifungua ujenzi huo, rais wa Urusi Vladmir Putin,alisema '' hili bomba la kupitishia gesi, likikalimilika lita saidia katika kukuza uchumi wa nchi, hasa kwa nchi za Asia-Pasifiki na kutakuwa na uhakika wa kuuuza zao la gesi bila matatizo.''

'' Makubaliano haya na  China yamekuja kutokana na umakini tunaokuwanao katika masuala ya mahusiano katika masuala ya kigeni, na China ni rafiki mkubwa wa Urusi na  siku zote tumekuwa hatuna vipingamizi kati yetu.''

Bomba ilio ambalo litakuwa na urefu wa  kilomita 3,968 na kupitia Siberia na linatarajiwa kuwa kubwa na lenye urefu kuliko mabomba  yote duniani la litasafirisha gesi yenye ujazo wa meta tillion 4 kwa muda wa miaka 30 na bomba hilo la gesi litamilikiwa na shirika la nishati Gazprom la Urusi.

Kuanza kwa ujenzi wa bomba hili la gesi kuelekea China, kutaifanya Urusi na ambao utakamilika 2018 utaleta unafuu, kwani Urusi  imekuwa ikivutana na nchi za jumuiya ya Ulaya katika suala la zao la gesi, na hasa tangu kuzuka kwa mchafuko wa siasa nchini Ukraini