Abdullah Senoussi ambaye alikuwa mkuu wa maswala ya usalama wakati wa utawala wa rais Muammar gadaffi , alikata rufaa kwa kutaka kesi yake isikilizwe nchini Uhollanzi katika mji wa Hague kwani anahofia kuwa mahakama ya Libya haitakuwa na usawa katika uendeshaji wa kwsi nzima kwa kuzingatia kazi aliyokuwa aliifanya.
Katika uamuzi wake huo, mahakama hiyo imesema kuwa " Libya ipo na uwezo wa kuendesha kesi hiyo baada ya kumaliza kufanya uchunguzi na kwani kesi hiiyo ilisha anzishwa nchini Libya."
Abdullah Sonoussi alishitakiwa mwaka 2011kwa makosa ya mauaji, utesaji na kuhusika katika kupinga kuangushwa kwa serikali ya Muammar Gadaffi 2011.
Rais Xi Jinping ambaye hii ni ziara yake ya kwanza, tangu kuwa rais wa Chinaa alikutana na viongozi wa serikali ya Kuba na kuzungumzia ni kwa jinsi gani nchi hizi mbili zitaendelea kudumisha uhusiano.
Ziara hiyo ya rais wa China kwa nchi Kuba imefanyika, akiwa katika moja ya mpango wa China kutaka kuimarisha uhusiano wakaribu na nchi zilizopo katika nchi za Karibiani.
Mikataba iliyo sainiwa kati ya China na Kuba itahusisha sekta ya kilimo ambapo itaghalimu kiasi cha $115 millioni za Kimarekani na pesa nyingine za Kimarekani $600million zitatumika kwa kununulia madini ya aina ya chuma ya nikele kutoka Kuba na vile vile kujenga bandari nchi Kuba.
Mikataba ya China na Kuba imekuja siku chache baada ya rais wa Urusi Vladmir Putin kumaliza kufanya ziara nchini Kuba na kusaini mikataba katika sekta tofauti za kiuchumi.