Tuesday, October 25, 2011

Mazishi ya Muammar Gaddafi yafanyika jangwani kisili.

Jiji la Nairobi la kubwa na mlipuko wa bomu kwa mara ya pili.

Nairobi, Kenya -25/10/2011. Mlipuko mwingine wa bomu umelipuka katikati ya jiji la Nairobi siku moja baada ya bomu kulipuka ndani ya ukumbi wa starehe.
Mlipuko huo ambao umetokea kwenye kituo cha basi umesababisha watu 12 kuumia na kuleta wasiwasi mkubwa ndani ya jiji la Nairobi
Mkuu wa Polisi Matthew Iteere alisema " Polisi bado wanafanya uchunguzi na kwani mpaka sasa hakuna ushaidi ya kuwa mashambulizi hayo ni ya kundi la Al-Shabab."
Jiji la Nairobi limepata mlipuko wa pili, baada ya ofisi za kibalozi za Kimarekani kutoa onyo kwa rais wake juu ya usalama katika jiji la Nairobia.
Wakati huo huo serikali ya Kenya itashirikiana na serikali ya Ufaransa katika kupambana na kundi la Al-Shabab.
Msemaji wa jeshi la Ufaransa Kanal Thiery Burkhard alisema " tutaoa misaada ya vifaa vya kivita na ndege zetu zitasaidia kuwasafirisha wanajeshi wa Kenya kwenye mpaka na Somalia."
Hata hivyo Kanal Thiery Burkhard alikanusha kauli ya jeshi la Kenya ya kuwa ndege za jeshi la Ufaransa zilifanya mashabulizi nchini Somalia.
Serikali za Izrael na Misri kubadilishana wafungwa.
Tel Aviv, Izrael - 25/10/2011. Serikali ya Izrael na Misri zimekubaliana kubadilishana wafungwa.
Habari kutoka ofisi ya waziri mkuu zimesema " Izreal itawaachia Wamisri 25 ambao ilikuwa inawashikilia nayo serikali ya Misri itamwachia Muizrael ambaye inamshikilia."
Muizrael Ilan Grapel ambaye anashikiliwa nchini Misri anashutumiwa kwa kuwa mpelelezi, na alikamatwa mapema mwaka huu June 12.
Hata hivyo serikali ya Izrael ilikanusha madai yakuwa Ilan Grapel mwenye uraia wa nchi mbili Izrael na Marekani ni mpelezi.
Kubadilishana wafungwa na Misri kumekuja siku chache baada ya serikali ya Izrael kukubali kunadilisha wafungwa na Hamas, kitendo ambacho kilipelekea kuachiwa kwa askari wa Izrael Girad Shalit ambeye alikuwa anashikiliwa na kundi la Hamas.
Mazishi ya Muammar Gaddafi yafanyika jangwani kisili.
Sirte, Libya - 25/10/2011. Aliyekuwa kiongozi na rais wa Libya Muammar Gaddafi ambaye alitolewa madarakani na baadaye kuuwawa amezikwa kwenye jangwa kisili siku chache baada ya kifo chake.
Serikali ya mpito ya Libya imesema " tumeamua kumzika kisili ili kuepuka watu kufanya kaburi lake kama sehemu ya kishujaa au kumbukumbu."
"Vilevile alifanyiwa maombi na kiongozi wa kidini yeye pamoja na mwanaye pamoja na aliyekuwa msaidizi wake."
Mazishi ya Muammar Gaddafi, mwanae na msadizi wake yalifanyika mapema alfajiri 05:00 sehemu ambayo haitakuwa raisi kwa watu kupafahamu na wale wote waliohusika katika mazishi walikula kiapo ya kuwa awatatoa siri ya kuonyesha alipo zikwa kiongozi huo aliye tawala Libya kwa miaka zaidi ya 40.

Monday, October 24, 2011

Bomu la lipuka katika ukumbi wa starehe jijini Nairobi.

Mtoto wa Gaddafi ahaidi kulipiza kisasi.

Al Rai, Syria TV Station - 24/10/2011. Mtoto waaliyekuwa kiongozi wa Libya amehaidi kuendelaza mapambano na serikali ya mpito ya Libya na kulipiza kisasa kwa niaba ya wale wote waliopoteza maisha katika kipindi cha miezi 8 ya harakakati za kuung'oa utawala wa baba yake marehemu Muammar Gaddafi.
Saif al-Islam aliseme kupitia TV iliyopo nchini Syria " tutaendelea kupambana, mimi ni Mlibya nipo Libya tayari kupambana na kulipiza kisasi na tutahakikisha tulalinda mali asili ya Libya zidi ya wavamizi na waasi wa nchi."
Mtoto huyo wa marehemu kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi ambaye aliuwawa wakati hivi karibuni, inasemekana ameteuliwa kuwa kiongozi kushika madaraka aliyo yaacha baba yake ya chama cha kitabu cha kijani, na vile vile kuungwa mkono na viongozi wa kabila la kwao ambao wamehaidi kupambana bega kwa bega na Saif Al-Islam zidi ya serikali ya mpito.
Mpaka sasa hivi haijulikani mahali Saif Al-Islam alipo, japo inasadikiwa ya kuwa yupo katika maeneo ya jangwa ndani ya Libya.
Wakati huohuo, shirika la kutetea haki za binadamu, limedai uchunguzi zaidi unabidi ufanyike baada yakujulikana ya kuwa wafuasi wa kiongozi wa zamani wa Muammar Gaddafi waliuwawa wakati jeshi la upinzani lilipo ingia mjini Sitre.
Maiti za watu hao wapatao 53 zilipatikana ndani ya hotel na huku mikono yao ikiwa imefungwa.
Habari zinasema wengi ya watu walio uwawa walikuwa wafanyakazi wa serikali ya Muammar Gaddafi.
Shirika hili limedai haya nimauaji ya kiana nainaelekea kulikuwa na ukiukwaji wa haki za kibinadamu.
Bomu la lipuka katika ukumbi wa starehe jijini Nairobi.
Nairobi, Kenya - 24/10/2011. Watu kumi na mbili wameumia vibaya baada ya bomu kulipuka ndani ya ukumbi wa kuchezea musiki jijini Nairobi.
Msemaji wa Polisi wa Kenya Charles Owini alisema " mpaka sasa bado tunafanya uchunguzi na tutatoa habari kamili baada ya uchunguzi wa tukio hilo."
Mlipuko huo umekuja baada ya ofisi za Marekani nchini Kenya "kuwaonya raia wa nchi yake kama wanapanga mpango wa kuja kutembelea wafikilie kwa undani kwani hali ya mashambulizi inaweza tokea wakati wowote."
Kwa mujibu wa habari hizo zilisema ya kuwa mashambulizi yanaweza tokea katika maeneo wanayofikia watalii na kumbi za starehe.

Jeshi la Kenya lazidisha mashabulizi zidi ta Al-Shabab.

Jeshi la Kenya lazidisha mashambulizi zidi ya Al-Shabab.

Nairobi, Kenya -24/10/2010. Ndege za jeshi la Kenya zimefanya mashambulizi katika mji wa Kismayo uliopo nchini Somalia, ikiwa katika moja ya kampeni ya serikali ya Kenya ya kupambana na kundi la Al-Shabab.
Kundi la al Shabab limethibitisha mashambulizi hao na kudai ya kuwa " hakuna maafay mkubwa yaliyo tokea katika kundi lake." Na kudai yakuwa waliwe kushambulia ndege hiyo na haikuweza kurudi tena.
"Na wapiganaji wetu wanajiaandaa tayari kwa kupambana na jeshi la Kenya."alisema msemaji wa Al-Shabab
Naye msemaji wa jeshi la Kenya alisibitisha yakuwa mashambulizi yalifanyika katika enelo la Kismayo na mashambulizi kama hayo huenda yakatokea siku za mbeleni.
Waturuki wakubwa na maafa ya tetemeko la ardhi.
Jimbo la Van, Uturuki - 24/10/2011. Tetemeko la ardhi lililo tokea nchini Uturuki limesababisha vifo vya watu wapatao 300 na wengine kijeruhiwa pamoja na maafa makubwa kijami yenye thamani ya mamilion.
Waziri mkuu wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan amesema " hadi kufikia sasa shughuli za uokoaji zinaendelea japo kuna matatizo kutokana na mazingira kuwa magumu katika uokoaji."
"Naserikali inajitahidi kwa kila hali ili kuweza kuwasaidia wale wote walioathirika na tetemeko hili."
Tetemeko la ardhi lenye nguvu za nyuzi 7.2 lilitokea nchini Uturuki siku ya Jumapili na hadi sasa bado serikali inajitahidi katika kuhakikisha inatoa kila msaada kwa wale wote waliokubwa na janga hilo la tetemeko la ardhi.

Friday, October 21, 2011

Kifo cha Muammar Gaddafi kuchunguzwa na mazishi ya lipangwa kufanyika kisiri.

Kifo cha Muammar Gaddafi kuchunguzwa na mazishi yalipangwa kufanyika kisiri.

Tripol, Libya - 21/10/2011. Uongozi wa serikali ya mpito ya Libya (NTC) ,umesimamisha mazishi ya aliyekuwa rais na kiongozi wa nchi hiyo Muammar Gaddafi, baada ya shirika la kutetea haki za binadamu kutaka uchunguzi ufanywe juu ya kifo cha kiongozi huyo.
Uamuzi wa kutaka uchunguzi ufanyike umekuja baada ya video na picha zilizo onyeshwa kwenye mitandao ya kuwa Muammar gaddafi alikamatwa akiwa mzima, lakini baadaye alionekana amekufa, jambo ambalo linaleta utata katika kifo chake.
Rupert Colville msemaji wa shirika la kutetea haki za binadamu alisema " inasikitisha na ukiangalia kwa ujumla matukio yenyewe kwani yamekwenda kinyume na sheria za haki za binadamu."
Serikali ya mpito ya Libya (NTC) imekubali uchunguzi ufanyike kuhusu kifo cha Muammar Gaddafi, baada ya hapo mwanzo kusema ya kuwa aliuwawa wakati wa mapambano.
Hata hivyo habari kutoka ndani ya serikali ya mpito ya Libya (NTC) zinasema " mazishi ya Muammar Gaddafi yalikuwa yamepangwa kufanyika kwa siri, na inaaminika ya kuwa kulikuwa na mpango wa kumzika baharini, ili kuepusha watu wasifanye kaburi lake kama sehemu ya kumbukumbu na kuabudiwa hapo baadaye jambo ambalo limekuwa likipingwa na baadhi ya viongozi ndani ya (NTC)."
Mwili wa Muammar Gaddafi umehifadhiwa katika mji wa Misrata tayari kwa mazishi.
Mapambano yazidi kati Al-Shabaab na jeshi la Muungano wa Afrika.
Mogadishu, Somalia - 21/10/2011. Uongozi wa Muungano wa Afrika umekanusha ya kuwa miili iliyo kuwa inaburutwa na kundi la Al-shabaab ni ya wanajeshi wanao linda amani nchini Somalia.
Habari za kukanusha tukio hilo limekuja baada ya kundi la Al-Shabaab kudai " yakuwa miili ya watu waliyokuwa wakiburuza ilikuwa ni ya askari wa Umoja wa Afrika ambao waliwauwawa wakati wa mashabulizi kati yao."
Hata hivyo, Muungano wa Afrika umesema " wanajeshi wake kumi wameuwawa na baadhi kujeruhiwa wakati wa mapambano na kundi la Al-Shabaab."
Nchi ya Somalia imekuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe tangu kuangushwa kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Muahamad Siad Barre
Kundi la ETA la Uispania latangaza kusimamisha mashambulizi.
Madrid, Uispania - 21/10/2011. Kundi lilinalo pingana na serikali ya Uispania la ETA limetangaza kusimamisha mashambulizi na kuweka siraha chini.
ETA kundi ambalo limekuwa likilaumiwa kwa kuhusika milipuko ya mabomu na mauji iliyokuwa ikitokea tangu kundi hilo lianza upinzani zidi ya serikali, lili tangaza rasmi ya kuwa linaweka siraha chini na kusimamisha vitendo vyote vya mashambulizi.
Kundi hili ambalo lilikuwa linapigania kujitenga kutoka serikali kuu ya Uispania na kuwa nakutaka kujulikana kana eneo huru la Baskeu (Basque).
Waziri mkuu wa Uispania Jose Luis Rodriguez Zapatero alisema " hii ni furaha kwa wananchi wa
Uispania na nimwanzo wa ushindi katika kukuza demokrasi nchini Uispania."
Suruhisho la amani la Uispania limekuja kutokana na juhudi za kimataifa zikiongozwa na aliye kuwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan na aliyekuwa kiongozi wa chama Sinn Fein cha Ireland ya Kaskazini Gerry Adams.
Wabunge wa chama cha David Cameron wataka kura ya maoni juu Uingereza na Muungano wa nchi za Ulaya.
London, Uingereza - 21/10/2011. Wabunge wa chama cha Konzevativi cha Uingereza amba cho kinatawala kwa katika serikali ya shirikiasho wametishia kujitoa ikiwa waziri mkuu hatabadilisha msimamo wake katika swala juu ya jumuyia ya muungano wa Ulaya.
David Cameron, amekuwa na wakatio mgumo, baada ya wabunge wapatao 70 kutaka bunge kupiga kura ya maoni kuhusu kushiriki kwa Uingereza katika jumuiya ya nchi za Ulaya.
Habari kutoka ofisi ya waziri mkuu numba 10 Westminster jijini London zinasema "wabunge kutoka chama cha Konzevativi wamelazimishwa kwa mujibu wa sheria kupiga kupinga muswada kuhusu Uingereza katika kushiriki kwake kwenye jumuiya ya Ulaya."
Swala la kutaka kupigwa kura kuhusu ushiriki wa Uingereza katika jumuiya ya Ulaya umekuja kutokana na msukumo wa baadhi ya viongozi kudai ya kuwa jumuiya ya Ulaya imekuwa ikilazimisha baadhi ya sheria kutekelezwa nchi Uingereza, jambo ambalo wanahisi kama jumuia hiyo inamadaraka makubwa na kuhatarisha uwezo wakujiamualia mambo kwa Waingereza.

Thursday, October 20, 2011

Aliyekuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi auwawa.

Aliyekuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi 69 auwawa. Picha hapo chini hapo zinaonyesha enzi ya uhai wa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi, akiwa kama kiongozi wa Libya na kukutana baadhi ya viongozi tofauti duniani hadi mwisho wa uhai wake ambapo alitawala Libya kwa miaka 41.

Muammar Gaddafi akiongea jijini Tripol ka mara ya mwisho kabla ya jiji la Tripol kuangushwa.
Sura inayo onekana inaaminika ya kuwa sura ya Muammar Gaddafi akiwa amezingirwa.
Mwili wa Muammar Gaddafi ukionekana baada ya kifo chake.
Muammar Gaddafi akiaga katika mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Muammar Gaddafi akiongea wakati wa mkutano wa umoja wa Mataifa.
Muammar Gaddafi akiwa na baadhi ya viongozi wa jumuia ya nchi za Kiarabu.
Muammar Gaddafi akiwa na viongozi tofauti wa dunia.
Muammar Gaddafi akiwa akisalimiana na rais wa Marekani Baraka Obama.
Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza akiwa na Muammar Gaddafi enzi za uhai wake.
Rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy akisalimiana na Muammar Gaddafi alipo tembelea Ufaransa.
Muammar Gaddafi akisalimiana na Vladimir Putin.
Enzi za uhai wake Muammar Gaddafi alikuwa mgeni wa heshima katika nchi tofauti duniani.
Muammar Gaddafi na waziri Mkuu wa Itali wakiwa wameshikilia bunduki wakati walipo kutana.
Gordon Brown wakati akiwa waziri mkuu wa Uingereza alikutana na Muammar Gaddafi pia.
Nelson Rolihlahla Mandela - Madiba alikuwa rafiki mkubwa wa Muammar Gaddafi.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Condoleeza Rice alitembelea nchi Libya ili kuimarisha ushirikiano na serikali ya Muammar Gaddafi.
Muammar Gaddafi akiwa na rais wa Venezuela Hugo Chavez.
Muammar Gaddafi akiwa na Robert Mugabe, viongozi ambao wamekuwa shubiri kwa nchi za Magharibi.
Muammar Gaddafi alikutana na rais wa Syria Bassad al Assad.
Rais wa Palestina Mahamoud Abbas akikabilishwa na Muammar Gaddafi.
Hayati kiongozi wa Palestina Yasir Arafat alikuwa mshiriki mkuu wa hayati kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi.
Muammar Gaddafi siku alipo tangaza rasmi kuwa kiongozi wa Libya baada ya kuung'oa utawala wa kifalme wa Idris.
Tripol, Libya - 20/10/2011. Kiongozi na rais Muammar Gaddafi wa Libya aliyetolewa madakani kwa nguvu za kijeshi ameuwawa baada ya kukimbia na kukaa mafichoni kwa muda mrefu tangu kuanza kwa vita nchini humo.
Waziri Mkuu wa muda wa serikali ya Libya Mahmoud Jibril alisema " Muammar Gaddafi ameuwawa na ni furaha kwa Walibya wote, kwani tulikuwa tunaingojea siku hii kwa hamu."
Rais wa Marekani Baraka Obama alisema " uhuu ni muda wa Walibya baada ya kuangushwa kwa Muammari Gaddafi na tutakuwa pamoja na Walibya katika kuijenga nchi yao."
Waziri Mkuu wa Uingereza ambaye aliongoza katika kampeni ya kumg'oa Muammar Gaddafi alisema " ni siku ya kukumbukwa na wale wote waliopata kuteswa na waliouwawa Kanali Gaddafi."
Naye Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema " ni historia ya kukumbukwa na kuonya ya kuwa Walibya watakuwa na wakati mgumu katika kujenga nchi yao."
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema ya kuwa Muammar Gaddafi, aliuwawa katika mashambulizi kwenye eneo alilo kuwa ameweka makao yake baada ya kukimbia jijini Tripol kutokana na kuzisiwa nguvu na jeshi la serikali ya mpito kwa masaada wa jeshi la NATO.

Wednesday, October 19, 2011

Misaada kwa nchi za Afrika kusimamishwa miaka michache ijayo.

Vladimir Putin ahaidi kuimarisha uchumi wa Urusi kimataifa.

Moscow, Urusi - 19/10/2011. Waziri mkuu wa Urusi na ambaye anatarajiwa kugombea kiti cha urais chini humo amewahakikishiwa wanachi ya kuwa akichaguliwa atakuwa na jumukumu la kuinua uchumi.
Vladimir Putin alisema "kazi itakayo pewa kipao mbele ni ya kuinua uchumi wa Urusi kimataifa, kuimarisha misingi ya kisiasa na demokrasi."
" Sikufikilia swala la urais, lakini nilipo pendekezwa kuchukua majukumu haya ndipo nilipo jua nina wajibu mkubwa wa kuiinua Urusi kiuchumi na kuifanya kuwa nchi imara, pindipo nitakapo chaguliwa."
Waziri mkuu Vladimir Putin, alipendekezwa kugombea kiti cha urais katika mkutano mkuu wa chama tawala uliyo fanyika hivi karibuni jijini Moscow na kutangazwa rasmi na rais wa sasa Dmtri Medvedev.
Misaada kwa nchi za Afrika kusimamishwa miaka michache ijayo.
London, Uingereza - 19/10/2011. Misaada kwa nchi za Afrika itaanza kufutwa miaka michache ijayo ili nchi hizi ziweze kujitegemea kwa kila kitu katika kuinua uchumi na maendeleo ya wananchi wao.
Waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair aliyasema hayo katika mkutano ya kuwa " kusimamisha misaada hiyo ni nia ya baadaye ili kuzipa nafasi nchi hizo kujijenga kwa kutumia maliasili zao, kwani bila hatua kuchukuliwa nchi hizi hazitapata mwamko wa kujitegemea."
"Vilevie bara la Afrika kwa sasa lina watu wenye uwezo wa kuongoza na kujenga nchi zao kiuchumi kisiasa na kijamii kutokana na kodi na mapato yatakayo patikana katika nchi hizo."
Tony Blair aliyasema hayo wakati alipo kuwa akihutubia mkutano ulio andaliwa na shirika linalo shughulikia utoaji wa misaada kwa nchi za dunia ya tatu.

Tuesday, October 18, 2011

Shirika la Afya la Dunia kumpambana na malaria kwa hali na mali.

Waizrael na Wapalestina wabadilishana wafungwa.

Tel Aviv, Izrael - 18/10/2011. Wanchi wa Izrael wameshangilia kwa hari na raha baada ya askari aliyekuwa amekamatwa na kundi la Hamas kuachiwa huru.
Gilad Shalit, ambaye alikamatwa na kundi la Hamas mwaka 2006, ameachiwa baada ya kufikiwa makubaliano kati ya serikali ya Izrael na kundi la Hamas katika kubadilishana wafungwa.
Baada ya kuachiwa Gilad Shalit alisema " nilijua ipo siku nitaachiwa ingawa sikujua itakuwa lini, na tumaini yakuwa huu utakuwa mwazo wa kuleta amani kati ya Waizrael na Wapalestina."
Kuachiwa kwa Gilad Shalit, kumetokea wakati huo huo serikali ya Izrael imewachia zaidi ya Wapalestina 477 ambao ilikuwa inawashikilia na wengine zaidi ya 600 wataachiwa hapo baadaye kutokana na makubaliano yaliyowe kwa kati ya serikali ya Izrael na kundi la Hamas.
Jambo ambalo limefurahiwa katika Ukanda wa Gaza na West Bank wakati walipokuwa wanawapokea Wapalestina waliochiwa kutoka katika jela za Izrael.
Shirika la Afya la Dunia kupambana na malaria kwa hali na mali
Geneva, Uswisi - 18/10/2011. Idadi ya watu wanao poteza maisha kutokana na ugonjwa wa malaria umepungua kwa asilimia 20, kwa mujibu wa ripoti ya shirika la afya la Umoja wa Mataifa (WHO).
Katika ripoti hiyo WHO imesema "kufanikiwa kupungua kwa kuenea kwa ugonjwa wa malaria kumetokana na ufuatiliaji wa ukaribu katika kupambana na ugonjwa huo na tunamatumaini kuuangamiza kabisa katika baadhi ya nchi ifikapo 2015."
Shirika la afya duniani lilianza kupambana na ugonjwa wa malaria tangu 1955 ambao umepoteza maisha ya watu wengi hasa katika nchi zilizopo Kusini mwa Sahara.
Hillary Clinton afanya ziara ya ghafla nchini Libya.
Tripol, Libya - 18/10/2011. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani amewasili nchini Libya kwa ziara ya kiserikali.
Hillary Clinton aliwasili nchini Libya ili kuongea na viongozi wa serikali ya mpito na kutaka kujua maendeleo yaliyofikiwa tangu kuangushwa kwa Kanali Muammar Gaddafi.
Waziri Hillary Clinton akiwa ziarani Libya alisema "
Nina furaha kusimama hapa kuona wananchi wa Libya wakiwa huru na kwaniaba ya Marekani napenda kuwapa pongezi."
"Ningetumaini kama Gaddafi angekamatwa au kuuwawa na Walibya wakawa huru siku zote."
"Na naimani serikali ya mpito itawaunganisha Walibya wote ili kuijenga upya Libya." Alimalizia kwa kusema waziri Hillary Clinton.
Ziara ya Hillary Clinton nchini Libya imefanyika bila kutangazwa kwenye vyombo vya habari.

Sunday, October 16, 2011

Baraka Obama atuma jeshi kumsaka Joseph Koni.

Malawi ya mpokea rais wa Sudan licha ya kutafutwa na mahakama ya kimataifa. Blantyre, Malawi - 16/10/2011. Rais wa Sudan ambaye anatafutwa na mahakama ya kimataifa inayoshughulikia makosa ya ukikwaji wa haki za binadamu, amewasili nchini Malawi kwa ziara ya kiserikali. Omar Al- Bashir ambaye alishitakiwa katika mahakama ya Uhollanzi, yupo nchini Malawi ili kudumisha uhusiano wa karibu na nchi hiyo. Msemaji wa mahakama ya kutetea haki za binadamu iliyopo nchini Uhollanzi Elise Kepper, alisema "Malawi kamanchi mwanachama wa mahakama hii , ni lazima watimize masharti kwa kumkamata Omar Al Bashi ambaye anatakiwa na mahakama kujibu mashitaka yanayo mkabili." Kesi zidi ya rais, Omar Al Bashir, ilifunguliwa mwaka 2009 na mahakama ya kimataifa ya Hague nchini Uhollanzi kufuatia uchunguzi ulionyesha ya kuwa serikali yake ya Sudani ilihusika katika ukiukwaji wa haki za binadamu katika eneo la Darfur na kutaka akamatwe tayari kufikishwa mahamani ili kujibu mashitaka zidi yake. Baraka Obama atuma jeshi kumsaka Joseph Koni. Kampala, Uganda - 16/10/2011. Rais wa Marekani, Baraka Obama ametuma wanajeshi wapatao 100 ili kusaidiana na jeshi linalo mtamfuta kiongozi wa kundi la Lord's Rasistance Army. Katika barua iliyopatikana ikulu ya Washington ilisema " rais Obama ameruhusu idadi ya wanajeshi wapatao 100, ili kushiriki katika kumsako wa kumsaka Joseph Koni ambaye ni kiongozi wa kundi la LRA." Koni na kundi lake wana pingana na serikali ya Uganda kwa upanda wa kaskazini mwa nchi hiyo na kushutumiwa kuhusika katika vitendo ambavyo vinakihuka haki za binadamu tangu aanzishe vita vya kuipinga serikali tawala ya rais Yoweri Musen kwa miaka 10 sasa. Luis Moreno Ocampo kuchunguza mauaji ya Ivory Coast. Abidjan, Ivory Coast - 16/10/2011. Mkuu wa mashitaka wa mahakama ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu iliyopo nchi Uhollanzi amewasili nchini Ivory Coast tayari kwa kuanza uchunguzi zidi ya ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe. Luis Moreno Ocampo, ameanza kazi hiyo baada ya makahama ya kimataifa kumpa ruhusa kuendelea na uchunguzi ili kujua ukweli kama kulikuwa na ukiukwaji wa haki za binadamu wakati kundi la rais wa sasa Alassane Ouattara lilipo kuwa linapambana na kundi la rais aliyetolewa madarakani kwa nguvu za kijeshi Laurent Gbagbo. Akiongea mara baada ya kuwasili nchini Ivory Coast Luis Moreno Ocampo alisema " katika uchunguzi wetu tuta kutana na makundi yote yaliyo husika katika vita na wale wote walio athirika na vita hivyo ili kupata ukweli zaidi." Kuwasili kwa Moreno Ocampo kumekuja kufuatia ripoti ya shirika la kutete haki za binadamu kuripoti ya kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa makundi ya Gbagbo na Ouwattara yalipo kuwa yanapambana baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa Ivory Coast. Serikali ya Kenya yaamua kupambana kundi la Al Shabaab katika mipaka yake Nairobi, Kenya - 16/10/2011. Jeshi Kenya limeanza msako wa kuwasaka wapiganaji wa kundi la Al Shabaab waliopo mpakani na nchi hiyo. Alfred Mutua ambaye ni msemaji wa serikalialisema," serikali ya Kenya imeamua kufanya hivyo ili kulinda mipaka yake tayari kupambana na kundi la Al Shabaab, kundi ambalo limekuwa likihusika katika utekaji wa nyara wa raia wa kigeni wanao tembelea nchini Kenya, na tunayo haki ya kujilinda na mashambulizi ya aina yoyote na jeshi la Kenya lipo tayari kuwatafuta wale wote waliohusika na ushambulizi na utekaji wa nyara." Matamko ya serikali ya Kenya kupambana na Al Shabaab yamekuja huku kundi hilo likiwa linaendelea kupambana na serikali ya Somalia na kufanya amani kuwa tete nchini Somalia.