Silvio Berluscon haukumiwa kwenda jela.
Hukumu hiyo imetolewa baada ya kukutwa kuhusika katika biashara kinyume na sheria.
Silvio Berlusconi ambaye alikuwa waziri mkuu wa Itali, amehukumiwa kwa mara ya kwanza, japo hapo awali alishafunguliwa kesi tofauti zidi yake.
Baada ya hukumu hiyo, Berlusconi alisema "hukumu haina maana na haikufuata haki"
Hata hivyo Silvio Berlusconi amekata rufaa baada ya hukumu hiyo.
Rais wa Marekani apiga kura mapema.
Chicago, Marekani - 26/10/2012. Rais wa Marekani amepiga katika mji wake Chicago ikiwa ni moja ya kampeni za kutaka wapiga kura wajitokeze kwa wingi.
Rais Baraka Obama, alipiga kura huku kura za maoni zikiwa zimesimama katikati baada ya mpinzani wake Mitt Romney kujivuta juu katika kura za maoni zilizo tolewa hivi karibuni.
Upigwaji wa kura hizo ni moja ya mpangilio ya uchaguzi uliyopo nchini Marekani.
Mara baada ya kumaliza kupiga kura Baraka Obama, aliendelea na ziara ya kampeni ya kutaka raia wa Marekani kumpigia kura hasa katika miji ya Ohio Virginia na Florida.