Tuesday, March 27, 2012

Papa Benedikt XVI awasili nchini Kuba.

Kenya yatangaza kuwa na mafuta katika ardhi yake.

Nairobi, Kenya - 27/03/2012. Serikali ya Kenya imetangaza kugunduliwa kwa mafuta nchini humo katika maeneo ya Kaskazini Magharibi mwa Turkana.
Rais Mwai Kibaki alisema" hii ni habari  jema kwani ni kwa mara ya kwanza Kenya inagundulika ya kuwa ina mafuta"
Ugunduzi wa mafuta hayo umefanywa na kampuni inayo julikana kama Tullo Oil ambayo pia imedai yakuwa mafuta yenye uboara kama haya ya Kenya  yamegunduliwa nchini Uganda.
Uchimbuzi wa mafuta hayo nchini Kenya unatarajiwa kwenda kina cha umbali wa mita 2,700 ifikapo mwezi wa Mei.


Papa Benedikt  XVI awasili nchini Kuba.


Havana, Kuba- 27/03/2012.  Kiongozi wa madhehebu ya Kikatoliki duniani amewasili nchini Kuba kwa ziara ya siku tatu nchini humo.
Papa Benedikt wa Kumi na Sita - XVI, aliwasili nchini Kuba baada ya kumaliza ziara yake nchini Mexico.
Rais wa Kuba Raul Castro katika kumkaribisha  Papa Benedikt alisema " Kuba inatambua umuhimu wa Kanisa Katiliki  nchini Kuba na Wakuba wapo pamoja na Kanisa katika kulinda haki za Wakuba na kwa kushirikiana na Kanisa Wakuba watailinda Kuba."
Papa Benedikt allsema " nawaomba wa Kristu wenzangu kumwamini Mungu na kupingana nakila aina ya njia za shetani kwani ndiyo njia pekee ya kushinda umasikini na ubaya wa ubinadamu."
Katika ziara hiyo Papa Benedikt anatarajiwa kukutana viongozi wa serikali ya Kuba ili kujadili hali halisi ya kiimani nchini humo.

Korea ya Kaskazini bado kitendawili kwa Marekani.


Seoul, Korea ya Kusini - 27/03.2012. Serikali ya Marekani imeitaka serikali ya Korea ya Kaskazini kuachana na mpango wake wa kuendeleza mradi wa kinyuklia.
Onyo ilo lilitolewa  baada ya rais wa Marekani,  Baraka Obama yupo   ziarani nchini Korea ya Kusini na ameuhduria kikao cha viongozi wa dunia ili kujadili udhibiti wa matumizi ya sirha za kinyuklia.
Rais Obama alisema "Korea ya kaskazini  lazima iachane na mradi wa kinyuklia kwani kitendo cha serikali ya Korea ya Kaskazini kuendelea na mpango wake wa kuendeleza  vitisho vya kinyuklia  kwa kujaribu mabomu havita saidia ila vina ifanya Korea ya Kaskazini kutengwa zaidi."
Serikali ya Korea ya Kaskazini imekuwa ikivutana na jumuiya ya kimataifa katika harakati zake za  kinyuklia kwa muda sasa baada ya mazungumzo kukwama miaka michache iliyo pita.

Iran bado yasisitiza yakuwa itajibu mashambulizi.

Tehran, Iran - 27/03/2012. Mmoja wa viongozi wa  ya Iran amedai ya kuwa kitendo chochote  cha kuishabulia Iran kitakuwa cha kujutiwa.
Ayatollah Seyyed Ahmad Khatami alisema " ikiwa Izrael au nchi yoyote kuishambulia Iran, basi wajuwe yakuwa majibu yetu Iran yatakuwa ya kuiwezesha dunia  kutambua ya kuwa tunachosema huwa tunatekeleza.2
"Kwani kumekuwa na vitisho vingi vya kuishambulia Iran, Izrael imekuwa  ikiishawishi jumuiya ya kimataifa kuamini ya kuwa Iran ni adui wa jamii, jambo ambalo si la kweli.
"Iran hajawahi kuishambulia nchi  yoyote na kitendo cha kuishamblia Iran kitakumbwa na majibu ambayo yatafanya jamii isituke na uenda ikawa fundisho kwa wale wote wanao taka kutumia nguvu kwa ajili ya manufaa yao."
Iran imekuwa ikishutumiwa na Mareakani na washiriki wake yakuwa inampango wa kutengeneza siraha za kinyuklia kinyume na sheria, jambo ambalo  Iran imekanusha vikali kwa kudai yakuwa mradi wake wa  nyuklia ni kwa ajili ya maendeleo ya kisayansi.

Thursday, March 22, 2012

Mswada wa Kofi Annan juu ya Syria wakubaliwa na Umoja wa Mataifa.

Mswada wa Kofi Annan juu ya Syria wakubaliwa na Umoja wa Mataifa.

New York, Marekani - 21/03/2012. Kamati ya usalama ya umoja wa Mataifa imepitisha mswada ulio pendekezwa ili kuleta amani nchini Syria.
Mswaada huo ambao ulipendekezwa na aliye kuwa katibu mkuu wa umoja wa Mataifa Kofi Annan
ambaye alipewa jukumu la kusuruhisha mgogoro wa kisiasa uliyopo nchini Syria, ambao umesababisha vurugu na vifo vingi nchini huko.
Mswaada huo ambao unazitaka pande zote mbili, serikali ya Syria na wapinzani kuweka siraha chini ili kutoa njia kwa misaada inayotakiwa kutolewa kwa watu walioathirika na vita na kila pande ikubali kumaliza mgogoro huu kwa kukaa chini ya meza na kuongea."
Mswaada huo pia ulikubaliwa na China na Urussi nchi ambazo hapo mwanzo zilipinga mswaaada uliopendekezwa kabla ya huu mpya uliotolewa na Kofi Annan.

Mwingereza aliyetekwa nyara nchini Somalia ahachiwa huru.

Mogadishu, Somalia - 21/03/2012. Raia wa Uingereza aliyekuwa ameshikiliwa na kundi la maharamia ameachiwa huru.
Judith Tebbut 57 alisema " nafurahi kuwa huru japo ninamajonzi kutokana na kifo cha mume wangu na nashukuru kupata fursa ya kuwa na familia yangu tena.
Nawakati wote nilipo kuwa chini ya maharamia hawakuni nyanyasa, na walikuwa wananiangalia kwa makini, na hasa nilipo umwa walitoa matibabu haraka."
Kundi lililo mteka nyara limedai yakuwa "kunamalipo ya pesa zilitolewa na ndipo wakaamua kumwachia huru Judith."
Judith Tebbutt ambaye alitekwa nyara katika mji wa Lamu ulipo kwenye pwani ya bahari Indi nchi Kenya mapema mwezi Semptemba 2011 wakati wakiwa  katika mapumzikoni nchini Kenya na mume wake kuuwawa wakati wa tukio la kutaka kuwateka nyara wote.
Ofisi ya mabo ya nje ya nchi Uingereza imethibitisha kuachiwa huru kwa Judith Tebbutt na kuhusu swala la kutolewa kiasi cha pesa, msemaji wa serikali alikanusha madai hayo na kusema "cha umuhimu kwa sasa ni kuhakikisha Judith anaelekea nyumbani kwani amechoka na anahitaji kuwa na mapumziko na kujiunga na familia yake.



Tuesday, March 20, 2012

Malkia wa Uingereza atimiza miaka 60 tangu kutawazwa rasmi kuwa Malkia.

Malkia wa Uingereza atimiza miaka 60 tangu kutawazwa rasmi kuwa Malkia. 


London,Uingereza - 20/03/2012. Malkia wa Uingereza amesherekea miaka 60 tangu kutawazwa rasmi kuchukua wadhifa huo.
Malkia Elizabeth II alisema " huu ni ukumbusho wa maisha yetu yanayo ambatana na historia ya nchi yetu ambayo kila mtu anahaki sawa na kuheshimina ni msingi wake mkuu.
Nipata bahati ya kushuhudia mambo memgi ya kihistori yakitokea, na nashukuru familia yangu kwa kuwa na mimi wakati wote kwa hali na mali, na najitolea kuitumikia nchi yangu na watu wake kwa sasa na miaka mingi ijayo."
Malkia Elizabeth wa Uingereza ni Malkia wa pili katika historia ya kifalme ya Uingereza kutimiza miaka 60 ya kuwa mtawala Malki kwa kufuata nyayo za Malkia Viktoria 1897. 

Mauaji yaliyofanywa na mwanajeshi wa Marekani yaundiwa kamati kuchunguzwa 
Washington, Marekani - 20/03/2013. Jeshi la serikali ya Marekani imepanga kuchunguza kiundani ili kutaka kufahamu kiini cha mauaji yaliyo fanywa na mmoja ya wanajeshi wa Kimarekani hivi karibuni nchini Afghanistani.
Gen Ajonh Allen alisema " kamati maalumu itaundwa ili kuchunguza kwa makini mauaji hayo na kutaka kujua kiundani ilikuwaje mshukiwa Staff Sgt. Robet Bale  alifanya mauaji hayo."
Mauaji hayo yaliyo fanywa na mwanajeshi huyo wa Marekani  nchini Afghanistan yameleta vichwa kuuma kwa serikali ya Marekani na kusababisha maamdamano nchini Afghanistan ya kutaka mwanajeshi huo ashitakiwe. 

Kiongozi wa Iran aonya nia ya kuishambulia Iran.

Tehran, Iran - 20/03/2012. Kiongozi mkuu wa serikali ya Iran, ametoa onyo ya kuwa ikiwa nchi yake itashambuliwa nayo serikali ya Iran bila kusita.
ayatollah Ali Khamenei aliseme " tutajibu shambuio lolote lile kwa kiasi tutakavyo shambuliwa na tutafanya hivi kwa kujilinda.
Hatutengenezi mabomu ya nyklia na hatuna mpango huo, na tusingependa kuona Marekani inafanya makosa hayo, kwa kuitishia Iran hakuta vunja Iran."
Kiongozi huyo wa Iran, aliyaongea hayo baada ya rais wa Marekani Baraka Obama, kutoa hotuba ambayo ilikuwa ni kwa ajili ya wanachi wa Iran.
Katika hotuba hiyo rais Obama alisema "Iran imewawekea wananchi wake ukuta wa umeme ili wasiweze kusikika, kuona, kuongea kwa kutofuata haki za binadamu."

Urussi kuafikia mapendekezo ya Kofi Annan juu ya Syria.

Moscow, Urussi - 20/03/2012. Serikali ya Urussi imekubaliana na mpango wa amani uliopendekezwa na aliyekuwa katibu mkuu wa zamani wa umoja wa mataifa Kofi Annan.
Waziri wa mambo ya nje wa Urussi Sergie Lavrov alisema " mpango wa mapendekezo ya Kofi Annan, ili kuleta amani nchini Syria in mzuri na nimuhimu kutekelezwa kama alivyo alivyo pendekeza."
Matamko haya ya Urussi yamekuja wakati Kofi Annan amesha fanya mazungumzo mara mbili na rasi wa Syria Bashar al Assad ili kujadili mbinu za kuleta amani nchini Syria.



Saturday, March 17, 2012

Aliyehusika na mauaji ya Sobibor aaga dunia.

Hugo Chavez arudi nyumbani baada ya matibabu nchini Kuba

Karakas, Venezuela - 17/03/2012. Rais wa Venezuela amewasili nyumbani baada ya kumaliza matibabu ya kansa ambayo ilikuwa ina muathiri afya yake.
Rasi Hugo Chavez akiongea kutoa shukurani kwa wale wote walio mwombea na kuwa naye katika wakati mgumu wa ki afya   alisema "nimerudi nyumbani na nguvu mpya na nipo tayari kuongoza jahazi" 
Hugo Chavez alitolewa uvimbe wakati wamatibabu yake nchini Kuba.
Venezuela nchi ambayo inakalibia kufanya uchaguzi wa rais, Hugo Chavez anatarajiwa kugombea tena kiti cha urais wa Venezuela kwa mara nyingine tena.

Aliyehusika na mauaji ya Sobibor aaga dunia.

Berlin, Ujerumani - 17/03/2012. Askari wa mwisho aliyehusika katika mauji katika kambi ya Sobibor nchini Paland amefariki dunia.
John Demjanjuk 91 ambaye alikutwa na makosa ya kuhusika katika mauaji zaidi ya watu 167,000 wakati akiwa kama mlinzi kati ya mwaka 1942-43.
Habari za kuhusika kwa Demjanjuk kuhusika katika vifo hivyo zilipatikana katika kumbukumbu za mauaji ya Holokost ambayo yalifanya afunguliwe kesi na kukutwa na hatia baadaye alihukumiwa kwenda jela miaka mitano.
Hata hivyo Demjanjuk alikata rufaa na kuruhusiwa kuishi katika nyumba za wazee ambapo ndipo umauti ulimkuta.

Iran ya dai yakuwa Izrael haina uwezo wa kupigana vita zaidi ya wiki.

Tehran, Iran - 17/03/2012. Waziri wa mambo ya nje wa Iran ametahadharisha ya kuwa kitendo cha Izrael kushambulia maeneo yaliyo na mitambo ya kinyuklia ya Iran kitaleta matokeo ambayo hayatasemeka.
Ali Akbar Salehi alisema " kitendo cha Izrael kushabikia vita zidi ya haikisaidii kwani kama vita vikiianza basi Izrael haina uwezo wa kupigana zaid ya wiki moja, hivyo  kila kitisho kinachotolewa tunakichukulia kwa makini na hatuzani kama Izrael ni kitisho kwa Iran."
Iran imekuwa ikisukumwa kusimamisha mradi wake wa kinyuklia na  nchi za Magharibi, jambo ambalo Iran imekuwa ikidai ya kuwa ni haki kwa nchi hiyo kuendelea na mradi huo wa nguvu za kinyuklia kwani ni kwa ajili ya maendeleo ya kisayansi.

Serikali ya Syria yadai Saudi Arabia inawauzia siraha wapinzani.

Damascus, Syria - 17/03/2012. Serikali ya Syria imetangaza ya kuwa siraha zinazo tumiwa na wapinzani wa serikali zinatoka katika nchi za Kiarabu.
Waziri wa habari wa Syria Adnan Mahmoud alisema " Saudi Arabis na Katar ni nchi ambazo zipo mbele katika kuwasaidia wapinzani wa serikali ambo wengi ni maharamia wanatumia siraha hizo kinyume na sheria na hata kuwadhuru raia."
Maelezo hayo yamekuja baada ya bomu kulipuka katika jiji la Damascus na kuuwauwa zaidi ya watu 20 na kuwajeruhi watu wapatao 27.
Serikali ya Syria imekuwa ikidai ya kuwa tangu mwezi wa Machi 2011, Saudi Arabia na washiriki wake wamekuwa wakishiriki katika kuwapa siraha wapinzani wa serikali na kusababisha machafuko nchini Syria.

Wednesday, March 14, 2012

Mahakama ya Hague yamtia hatiani Thomas Lubanga.

Mahakama ya Hague yamtia hatiani Thomas Lubanga.

Hague, Netherlands - 14/03/2012. Mahakama inayo shughurikia  makosa ya ukiukwaji wa haki za binadamu iliyopo jijini Hague imemkuta na hataia aliyekuwa kiongozi wa Union of Congolese Patriots UPC Thomas Lubanga kwa kuwatumia vijana wadogo chini ya miaka 15 kama wanajeshi katika kundi lake.
Lubanga anatarajiwa kuhukumiwa siku za karibuni, kwa mujibu wa wanasheria waliofatilia kesi hii wanasema " huenda akahukumiwa kifungo cha maisha"
Thomas Lubanga, amekuwa kiongozi wa kwanza kukutwa na hatia tangu koti hiyo iliyopo Netherlands Hague kuanzishwa miaka 10 iliyo pita.

Ikulu ya rais wa Somalia yashambuliwa.

Mogadishu, Somalia - 14/03/2012. Watu watatu watano wamefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa baada ya ya bomu kulipuka kwenye Ikuru ya rais yaliyopo  mjini Mogadishu.
Kundi la Al-Shabab limekili kuhusika na "mlipuko huo na kuonya yakuwa milipuko  na mashambulizi mengine yatafuata."
Al Shabab walifukuzwa katika maeneo ya jiji la Mogadishu baadaya ya majeshi ya umoja wa Afrika kwa kusaidiana na majeshi ya Somalia kuzidi nguvu kundi la hilo.

Tuesday, March 13, 2012

Muamar Gaddafi alikuwa mtu wa karibu wa Nicolas Sarkoozy.

Ndizi zilizo iva ni muhimu kwa nguvu za kiume.

Kampala - Uganda - 13/03/2012.  Ndizi zilizo iva au kwa jina jingine "banana" zimetambulika kwa kuongeza nguvu zaa kiume mwilini.
Kama inavyo julikana ndizi zilizo iva zinakusaanya vitamini na vilishe  vya potassium, chuma zinc, cabohydrates,B6,A,C,B1,B2 na E ambavyo uhongeza nguvu.
Mataalaamu wa mambo ya  lishe Geoffrey Babaghirana alisema " ndizi zinasaidia kukuza nguvu za mwili hasa kwa wanaume na kuongeza uwezo wa kimapenzi kutokana na vilishe vinavyo patikana katika zao hilo na vile vile zinajenga ngozi ya mwili kutokana na kuwa na Vitamini C."
Zao la ndizi ni chakula kikuu katika jamii kubwa ya Waganda na sehemu za Tanzania zilizo pakana na Uganda.

Muamar Gaddafi alikuwa mtu wa karibu wa Nicolas Sarkoozy.

Paris, Ufaransa - 13/03/2012. Shirika moja linaloshughurikia uchunguzi wa maswala ya siasa na siri zake limetoa habari kuwa rais wa Libya Muaamar Gaddafi alichangia pesa ili kumsaidia rais wa Ufaransa.
Kwa mijibu wa shirika hilo zinasema "kiasi cha Euro 50 million zilitolewa kwa rais wa sasa wa Ufaransa Nicolas Sarkozy  na rais wa Libya Muammar Gaddafi kabla ya kuangushwa kutoka madarakani."
Hata hivyo rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy alikanusha madai hayo kwa kusema " nafikri mnajua ya kuwa Gaddafi alikuwa akiongea atakalo na hizi habari si za ukweli."
Uhusiano wa rais Sarkozy wa Ufaransa na rais Gaddafi wa Libya ulikuwa wa karibu saana na hasa pale iliposhuhudiwa rais Sarkozy kumwalika Muammar Gaddafi nchini Ufaransa baada ya uchaguzi mkuu wa Ufaransa.

Mashambulizi ya mabomu yatokea Nairobi.

Nairobi, Kenya - 13/03/2012. Mabomu yamelipuka hivi karibuni katika jiji la Nairobi na kusababisha vifo na watu wengine kujeruhiwa.
Msemaji wa polisi Charles Owinom alisema " kulikuwepo na milipuko tofauti ambayo imesababisha vifo vya watu wanne na watu wapatao 40 wamejeruhiwa."
Jeshi la Polisi nchini Kenya limeilaumu kundi la Al-Shabab kwa kuhusika na mashambulizi na kuhaidi ya kuwa mashambulizi hayo hayata tikisa taifa la Kenya.
Mashambuulizi hayo yaliyofanyika hivi karibuni ni mrorongo wa mashambulizi ambayo yamefuatia yale yaliyo tokea mwishoni mwa mwaka  jana na kusababisha maafa kwa jamii.

Wednesday, March 7, 2012

Machifu watanagaza serikali yao nchini Libya.

Iran yakubalia kuendelea mazungumzo juu ya haja na mipangoo ya kinyulia.

Viena, Austria - 07/03/2012. Shirika linalo shughulikia maswala ya  kinyuklia limetangaza ya kuwa mazungumzo yanayo husu swala la Iran na nguvu za kinyuklia huenda yakaanza karibuni.
Marekani, Fransi, Britain, China, Urussi na Ujerumani zimekubali kuanza mazungumzo ambayo yalikuwa yamesimamishwa kutokana na kutokuelewana kati ya nchini hizo na Iran.
Rais wa Marekani Baraka Obama alisema " hii ni faida kwa kila mtu, kwani kutatua swali hili kiamani ni jambo la maana."
Wakati huo huo, serikali ya Iran imetoa ruhusa kwa wakaguzi wa maswala ya kinyuklia wa kimataifa kutembelea eno la kambi ya jeshi ambao linazaniwa kuwa na mitambo ya kinyuklia.
Marekani na waashiriki wake wamekuwa wakishuku ya kuwa Iran inampango wa kutengeneza sirha za kunyukia, jambo ambalo Iran imekataa ya kuwa inampango huo.


Machifu watanagaza serikali yao nchini Libya.
Benghazi, Libya - 07/03/2012. Serikali ya mpito ya Libya imetangaza kupinga kitendo cha viongozi wa Mashiriki ya Benghazi kutangaza kujitawala na kuunda serikali yao.
Kiongozi wa serikali ya mpito Mustafa Abdel Jalil alisema " tutalinda muungano na Libya ni moja, hatupo tayari kuigawa nchi.
"Ningependa kuwatahadharisha ya kuwa wawe waangalifu na wafuasi wa Muamar Gaddafi na serikali itatumia kila nguvu zilizopo kulinda Libya na inashangaza ya kuwa baadhi ya nchi za Kiarabu zimeounga mkono uamuzi huo na nisingependa kuzitaja."
Libya ilizaliwa mwaka 1959 -63 baada ya kuungana kwa majimbo ya kichifu ya Cyrenaica, Tripolitania na Fezzan.


Aliyefanya mauaji nchini Norway afunguliwa kesi ya uhaini namauaji. 
Olso, Norway - 07/03/2012.  Serikali ya Norway imemfungulia mashitaka ya kesi ya uhaini na mauaji kwa raia wanchi hiyo ambaye aliyafanya na kuisitua dunia nzima.
 Anders Behring Breivik 33 amefunguliwa kesi hiyo, baada ya mauaji aliyo yafanya kwa kuua watu 77 kwa kuwapiga risasi katika kituo Utoeya na kuhuusika na kutega mabumu katika jiji la Olso.
Mwanasheria wa serikali Svein Holden  alisema " Anders amefanya makosa ya kihaini ambayo ni ya kihistoria katika nchi yetu."
Kwa mujibu wa habari zilizopo zinasema huenda Anders Behring Breivik akahukumiwa kwenda jela miaka 30 ingawa hapo awali alionekana na ubovu wa akili.


Mwakilishi wa umoja wa Maataifa awasili nchini Syria.
Bab Amr, Syria - 07/03/2012. Mwakillishi wa Umoja wa Mataifa katika kushughulikia haki za binadamu amewasili nchini Syria na kutembelea maeneo yaliyo athirika na mapambano.
Valerie Amos alitembelea Bar Amr baada ya serikali ya  Syria kuhakikisha yakuwa hali ya usalama wake ulikuwa umekamilika.
Waziri wa mambo ya nje wa Syia Walid Muallem alimweleza ya kuwa serikali ya Syria inatoa huduma za chakula n madawa kwa wale wote walio athirika na mashambulizi hayo.
Valerie Amos aliwasili nchini Syria baada ya kukubaliwa kutembelea maeneo yaliyoathirika na vita kati ya majeshi ya serikali na yale yanayo pinga serikali ya Syria.

Sunday, March 4, 2012

Vladmir Putin ashinda uchaguzi wa urais.

Vladmir Putin ashinda uchaguzi wa urais.

Mosccow, Urusi - 04/03/2012. Matokeo ya uchaguzi nchini Urusi yamempa ushindi mkubwa waziri mkuu wa Urusi kwa asilimia kubwa kuliko wapinzani wake.
Vladmir Putin ameshinda uchaguzi huuo kwa zaidi ya asilimia 60% na anayemfuata kwa ushindi amepata 17%.
Huku machozi yakimtoka mbele ya wanachama na watu wapatao 100,000 walio kuwepo kwenye makao makuu ya chama United Russia Vladmir Putin alisema "tumeshinda kama tulivyo haidi na ni ushindi kwa wale wote waitakiayo Urusi mema."
Vladmir Putin alihutubia mkutano huo baada ya mtokeo ya uchaguzi kuonyesha ya kuwa ameshinda uchaguzzi huo kwa asilimia kubwa.


Baraka Obama ataoa onyo kwa serikali ya Iran. 
Washington, Marekani - 04/02/2012. Rais wa Marekani ameoinya Iran kuachana na mpango wake kinyuklia au hatasita kutumia nguvu za kijeshi.
Rais Baraka Obama alisema "viongozi wa Iran lazima watambue hili, itabidi kutumia nguvu za kijeshi ikiwa mbinu zote za kisiasa kuisimamisha Iran kuendelea na mpango wake wa kinyuklia.
Ningeomba Izrael wawe na subira ili jitihada za kidilpomasia kufanya kazi yake, ikiwemo vikwazo vya kiuchumi ambavyo nafikiria vitafanikiwa na swaala la mazungumzo ya kivita tusiliongelee kwa sasa."
Hata hivyo serikali ya Iran imekuwa ikipinga ya kuwa haina nia ya kutengeneza siraha za kinyuklia na kuonya ya kuwa ikiwa kuna shambulizi lolote litafanyika nchini humo , basi Iran itajibu mashambulizi hayo kwa nguvu zote.


Izrael ianuwezo wake wa kujiamualia kuhusu Iran.
Tel Aviv, Izrael - 04/03/2012. Waziri wa mambo ya nje wa Izrael amehaidi yakuwa Izrael itamua niwakati gani kufanya mashambulizi nchi Iran bila kujali washiriki wake.
 Avigdor Lieberman akiongea alisema "kweli Marekani ni nchi yenye nguvu kijeshi na mshiriki wetu mkuu wa karibu lakini Izrael ni nchi iliyo huru na inauamuzi wake yenyewe.
"Na uamuzi juu ya mpango wa kuisimamisha Iran isiendele na nguvu za kinyuklia ni uamuzi utakao faywa na Izrael."
Waziri Lieberman aliyasema hayo wakati wakati waziri mkuu wa Izrael Benyamin Netanyahu akiwa njiani kwenda kuonana na rais wa Marekani Baraka Obama, na swala la nyuklia Iran litakuwa na kipao mbele.


China kuongeza matumizi ya kijeshi.
Beijing, China - 04/03/2012. Serikali ya China imetangaza kuongeza matumizi ya kijeshi ili kuweza kupata uwezo sawa katika kujenga uchumi na ulinzi.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema " serikali ya China imesha panga kuongeza matumizi ya kijeshi kufikia asilimia 11.2%."
China imehaidi kuweka swala la ulinzi mbele na halitaharibu mipango mingine ya kiuchumi kwani fedha
 hizo zitatumika kati mafunzo hya kijeshi kwa ajili ya wanajeshi wa China.