Tuesday, December 31, 2013

Jeshi la serikali la rais Salva Kiir lazidiwa nguvu.

Jeshi la serikali la rais Salva Kiir lazidiwa nguvu.


Bor, Sudani ya Kusini - 31/12/2013. Wapiganaji wanao pingana na  serikali ya Sudan Kusini, wa mekamata  mji wa Bor, baada ya kupambana vikali na  wajeshi wa serikali na kulizidi nguvu.

Akiongea baada ya kuukamata mji huo,  Moses Ruai ambaye ni msemaji wa jeshi la upinzani amesema " Mji wa Bor upo mikononi mwetu, na hivyo makao makuu wa jimbo la Jonglei ni yetu pia."

Wakati mapambano yanaendelea, kiongozi wa upinzani  na ambaye jeshi lake limetwaa mji wa Bor Riek Machar amekataaa kukutana na rais Salva Kiir ili kufanya mazungumzo ya kuleta amani ambayo yalitarajiwa kufanyika jijini Addis Ababa Ethiopia hii karibuni.

Hata hivyo kwa upande wa serikali, waziri wa mambo ya nchi za nje wa Sudan ya Kusini, Barnaba Marial Benjamin, amesema " mpango wa Riek Machar kushirikiana na kugawana madaraka na rais Salva Kiir haupo tena, na hii ni kutokana na kuwa Machar ni kiongozi wa jeshi linalotaka kupindua serikali halali ya wanchi wa Sudan ya Kusini."

Tangu kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe,  kwenye nchi changa ya Sudan ya Kusini na ambayo ilipata uhuru wake 2011, watu wapatao 1000 wamesha poteza maisha yao, wengi kujeruhiwa na mali nyingi kuharibiwa kutokana na vita hivyo.

Urusi ya shutuliwa na milipuko ya mabomu mfululizo.


Urusi ya shutuliwa na milipuko ya mabomu  mfululizo.

Moscow. Urussi - 31/12/2013. Muuaji ya kigaidi yametolea tena kwa mara ya pili katika mji wa Volgograd na kuuwa watu wapatao 14 na wengi 41 kujeruhiwa vibaya ja.

Mauji hayo yalitokea baada ya  bomu kulipuka katika basi la abiria linalo fanya mizinguko ya kuchukua abiria katika mji huo na kuwashitua wananchi wengi wa Urussi ambapo nchi yao ipo mbioni kuandaa mashindano ya michezo ya Olympic Baridi siku chache zijazo.

Mlipuko wa bomu  ndani ya basi umefuatia mlipuko mwingine ambao umetokea siku moja katika kituo cha treni cha mji huo na kusababisha vifo vya watu 18 na wengine zaidi ya 20 kujeruhiwa vibaya baada ya muuaji wa kujitolea muhanga kusimamishwa katika kizuizi cha kuingilia katika kituo hicho.

Kufuatia milipuko hiyo katika mji wa Volgograd, rais wa Urusi Vladimir Putin ameagiza ulinzi uongezwe na kuhaidi kuwa wale wote ambao wanahusika na milipuko hiyo ambayo ina nia ya kutishia wananchi wa Urusi watatiwa nguvuni na sheria itapitisha panga lake kwao.

Friday, December 27, 2013

Rais wa Sudan ya Kusini akubali suruhu.

Rais wa Sudan ya  Kusini akubali suruhu.

Juba, Sudan ya Kusini - 27/12/2013. Rais wa Sudani ya Kusini Salva Kiir  amekubali kusimamishwa mapambano ya kivita kati yake na kundi ambalo linaunga mkono mpinzani wake Riek Machar ambaye alikuwa makamu wake wa urais.

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya  na waziri mkuu wa Ethiopia  Hailemariam Desalegn waliweza  kumshawishi rais Kiir kukubali kusimamishwa kwa vita baada ya kukutana na kujadiliana katika mji mku  wa Juba.

Akiongea  baada ya rais Kiir  kukubali kusimamishwa kwa vita , rais Uhuru Kenyatta amaesema " nimefurahishwa na kitendo cha rais Kiir kukubali kusimamisha vita, kwani nafasi iliyopo ni finyu, na naomba ijulikane kuwa  IGAD haitaruhusu kuona rais aliyechaguliwa kihalali anatolewa madarakani kwa nguvu"

" Na nawaomba Riek Machar na rais Salva Kiir  kuhakikisha amani inarudi nchini Sudani ya Kusini kwani vita siyo suruhu ya kuleta maendeleo ya nchi." Aliongeza  rais Uhuru Kenyatta.

Jitihada za kusimamisha vita nchini Sudan ya Kusini  zinasimamiwa na  (Inter-Government Authority on Develoment -IGAD) ikiwa  na nia ya kusimamia uongozi bora na kuhakikisha kuondoa migogoro ya kisiasa katika nchi zilizopo  Afrika ya Mashariki na Kati.

Mvutano kati ya Udugu wa Kiislam na serikali waiweka amani ya Misri njia panda.


Kairo, Misri -27/12/2013. Waandamaji wanaounga mkono kundi la Undugu wa Kiislaam ( Muslim Brotherhood) wamepambana polisi katika matukio tofauti yaliyo tokea nchi Misri tangu kutangazwa kuwa kudi hilo ni kundi la kigaidi nchi Misri.

Katika maandamano hayo watu watatu wamepoteza maisha jiji Kairo, na wengine kujeruhiwa vibaya wakati polisi wa kuzuia ghasia  walipo pambana na waandamanaji,  na zaidi ya watu 265 wamekamatwa kutokana na vurugu hizo,  

Tangu kutolewa madarakani kwa nguvu kwa rais Mohammed Morsi, hali ya amani na utulivu imechafuka nchini Misri, na hii inatokana na wanachama  wanaounga mkono kundi la Undugu wa Kiislaam kutaka rais Mohammed Morsi arudishwe madarakani na pia wanapinga kitendo cha serikali kukitangaza cha chama cha Udugu wa Kislaamu kuwa cha kigaidi.

Saada al Hariri alia na Hezbollah.

Beiruti, Lebanon - 27/12/2013.  Saad al Hariri ambaye alisha wahi kuwa waziri mkuu wa Lebanoni, amelilaumu kundi la Hezbollah kwa kuhusikia na shambulizi la bomu ambalo limemuua mmoja ya mshauri wake mkuu.

Mohamad Bahaa Chatah 62, aliuwawa baada bomu kulipuka  katikati ya msafara wake wakati  alipo karibia ofisi za majengo ya serikali ambapo alikuwa njiani keelelea kwenye mkutano wa kuipinga Syria uliyokuwa ukiongozwa na Saad al Hariri

Mlipuko huo pia uliharibu majengo na kusababisha baadhi kushika moto na kuungua vibaya.

Akiongea kuhusu mauaji ya Chatah, Saada al Hariri alisema " watu walio muua Chatah ni wale ambao wanataka haki isitendeke kufuatia kuwepo na kesi inayotarajiwa kuanza kwenye koti ya kimataifa mjini  Hague Uholanzi mapema mwezi January 2014."

Mohamad Chatah, alikuwa mkosoaji mkuu wa serikali ya Syria,  amekuwa akipinga na kulaumu kundi la Hezbollah kwa kushirikiana na rais Bashar al Assad katika vita vinavyo endelea nchi Syria.

Kifo cha Chatah kimekuja wiki tatu kabla ya kuanza kesi zidi ya baadhi ya wanachama wa Hezbullah ambao wanasadikiwa kuhusika katika mauaji ya  mwaka 2005 ya waziri mkuu wa Lebanoni  Rafik al Hariri ambaye ni baba wa Saad al Hariri,



Wednesday, December 25, 2013

Rais wa Uruguay awapa zawadi ya kufunga mwaka 2013 wanachi wake.

Rais wa Uruguay awapa zawadi  ya kufunga mwaka 2013 wanachi wake.


Montevideo, Uruguay - 25/12/2013. Rais wa Uruguay amewapa salamu za Kristmas na mwaka mpya wanchi wake wa Uruguay kwa kusaini mkataba wa kuruhusu kilimo cha bangi na matumizi yake  nchini humo.

Akithibitisha kusainiwa kwa muswada huo, Diego Canepa ambaye ni msemaji kutoka ofisi ya rais amesema " rais Jose Mujica ametia sahii kuwa sheria kuruhusiwa kulima na kuuzwa bangi nchini humo siku ya Jumatu, na hii inatokana na wabunge kupiga kura kuunga mkono muswada huo,  na sheria hii itaaanza rasmi kutumika kuanzia April 9 2014."

Rais  Jose Mujica ambaye ndiye mwanzishi wa kampeni ya kuruhusiwa matumizi ya bangi nchini humo kwa kuamini kuwa kuruhusu  kilimo cha zao hilo nchini mwake kutapunguza uharamia na biashara haramu ambayo mara kwa mara umesababisha mauaji na kupunguza amani katika jamii ya Wauruguay.

Hata hivyo shirika la ukimataifa la kupambana na madawa ya kulevya limelaani kupitishwa kwa sheria hiyo na kudai ya kuwa Uruguay imevunja sheria za kimataifa ambapo ni nchi wanachama.

Papa Fransis aomba kuwepo na amani duniani.

Vatican City, Vatican - 25/12/2013.Mkuu wa kanisa Katoliki dunia Papa Faransis ameto wito kwa kila mtu kushiriki katika kulinda na kuleta amani duniani.

Akizungumza katika misa ya kusherekea siku ya kuzaliwa kwa Yesu Kristu, Papa Fransis amesema " amani ni imekuwa ikivurugwa na watu wenye nia mbaya na pia  dunia na mazingira yake yamekuwa yakiharibiwa na watu wenye tamaa na ambao wanaleta maafa kwa jamii nzima."

Katika salamu za Kristmas, Papa Fransis pia aliongezea kwa kueleza ya kuwa nchi kama DRC Kongo, Nigeria, Sudani ya Kusini na Syria zimekuwa na migogoro ambayo imekuwa  inatakiwa iishe haraka " lakini kutokana na kukosa imani kwa wahusika  watu wamekuwa wakipoteza maisha  kila siku kitu ambacho ni kinyume na maadili a kiutu."

Papa Fransis ametimiza miezi tisa sasa tangu kutawazwa rasmi kuwa mkuu wa kanisa katoliki lenye waumini zaidi ya 1.2 billion na amekuwa akipinga vitendo vya kuvuruga amani vinavyo tokea duniani na  amekuwa akiwaagiza viongozi kwa kushirikiana na wananchi  kuhakikisha amani inakuwepo kwa kila mtu na kila jitihada zifanyike ili watu masikini wasaidiwe kuinua maisha yao.

Umoja wa Mataifa kichwa kuuma kwa Sudani ya Kusini.

New York, Marekani - 25/12.2013. Kamati ya usalama ya umoja wa mataifa imekubali kuongeza zaidi ya wanajeshi wake nchi Sudani ya Kusini kufuatia vita vinavyoenedelea katika ya wanajeshi wanao muunga mkono rais  wa sasa wa nchi hiyo Salva Kiir na mpizani wake na ambaye alikuwa makamu wa Riek Machar.

Toby Lanzer akithibitisha uamuzi huo wa UN alisema "Wanajeshi, 12.000 watakuwepo nchi Sudani ya Kusini  na  polisi 1,323 ili kuweza kulinda na kurudisha amani nchini Sudan, kwani wanajeshi na askari UN waliokuwepo hapo mwanzo walionekana kuzidiwa nguvu kutokana na vita vinavyo endelea hadi sasa nchini humo."

Kwa mujibu wa shirika la kimataifa la  kutete haki za binadamu limesema kuwa zaidi ya watu 1000 wamesha poteza maisha yao kutokana na vita hivyo na hadi sasa kuna makaburi yamegunduliwa yamezikwa watu wengi  jambo ambalo huenda likaleta mstuko mkubwa kwa jamii ya kimataifa.

Tangu kuanza vita kati ya wanajeshi wanao muunga mkono makamu wa rais wa Riek Machar na wanajeshi wa serikali ya rais Salva Kiir, maelfu ya Wasudani ya Kusini wamekimbilia katika makazi ya ofisi na maeneo yanayo tumika na umoja wa mataifa nchi humo ili kupata usalama wa masha yao.

Chama cha rais Mohammed Morsi matatani nchini Misri.

Kairo, Misri -25/12/2013. Serikali inayo ungwa mkono  na jeshi nchini Misri imetangaza imetangaza kuwa chama cha washirki na undugu wa Kiislaam ( Muslim Brotherhood)  ni chama cha kigaidi.

Akitangaza uamuzi huo, makamu wa waziri mkuu Hossam Eissa amesema ". chama cha Muslim Brotherhood ni chama cha kigaidi na kuanzia sasa tunakipiga marufuku na mtu yoyote atakaye husika na chama hicho atachukuliwa hatua  na hii  ikiwemo kushiriki katika kukichangia kipesa na kujumika katika maanadamano yatakayo pangwa na chama  hicho"

Chama hicho ambacho ndicho alichokuwa akiongoza rais Mohammed  Morsi aliyetolewa madarakani na jeshi na kushitakiwa kwa makosa  tofauti kinashutumiwa kwa kushiriki katika mashambulizi na kuvuruga amani nchini Misri, jambo ambalo chama hicho kimekanusha kushiriki katika kuchafua amani nchini humo.

Kufuatia kutangazwa kwa Muslim Brotherhood kuwa chama cha kigaidi, jeshi la Misri limepewa nguvu zaidi kutumi ikiwa wanachama cha chama hicho cha Kislaam watavunja sheria hiyo.

Edward Snowdon bado mwiba kwa shirika la ujasusi la Marekani.

Moscow, Urusi - 25/12/2013.Aliyekuwa mfanyakazi wa maswala ya kimtandao katika ofisi za kijasusi za NSA na ambaye alitoa siri za kijasusi za serikali ya Marekani na mshiriki wake  Uingereza hivi karibuni amezidi kupigilia msumari wa moto katika sekta ya ujasusi za washiriki hao.

Edward Snowden raia wa Marekani,  ambaye alikuwa mfanyakazi wa kijasusi katika maswala ya kimtandao na kwa sasa anaishi ukimbizini nchi Urusi amepigilia msumari huo wa moto kwa kusema  vitendo vya serikali kuchunguza watu wake umefikia hali ya kutisha.

"Na hata mtoto ambaye atazaliwa leo atakuwa hakuna kitu chake ambacho akijulikani, kwani serikali kwa kutumi vitu kama runinga, simu na vifaa vingine vya kisayansi ambavyo tunavitumia kila siku katika maisha yetu ndivyo vinatumika katika kuchunguza nyendo zetu za kila siku."

"Napenda kuwakumbusha kuwa kuishi kwa kuchunguzwa na serikali ni kinyume cha sheria, na nijambo ambalo serikali za Marekani na mshiriki wake wamevunja haki zetu za kibinadamu"

Edward Snowden ambaye kwa sasa amefunguliwa kesi nchi Marekani kwa kuiba nyaraka za siri za serikali akiwa kama mfanyakazi wa shirika la kijasusi la NSA nchini Marekani na kuifanya nchi hiyo kuwa na mvutano wa kidiplomasia na washiri wake wakaribu, baada ya  kutoa siri  kuwa Marekani inawachunguza raia na viongozi wa nchi tofauti duniani kinyume cha sheria.

Monday, December 23, 2013

Viongozi wa siasa nchi Nigeria wavutana.

Viongozi wa siasa nchi Nigeria wavutana.

Lagos, Nigeria - 23/12/2013.Mvutano kati ya rais wa sasa wa Nigeria Goodluck Jonathan  na rais mstaafu wa nchi hiyo Olusegun Obasanjo umefikia hatua nyingine baada ya malumbano ya chini kwa chini ambayo yamekuwa yakiendelea kwa muda sasa kati ya viongozi hao.

Mvutano huo umewekwa wazi na  rais Goodluck Jonathan baada ya kuamua kujibu barua iliyotumwa na aliyekuwa rais wa nchi hiyo Olugun Obasanjo kwa kuandika "baba Obasanjo, nasikitika saana kwa kunishutumu mimi na serikali yangu kuwa inafanya kila njia kuwauwa baadhi ya wanasiasa na kuna watu 1000  ambao wanafuatiliwa na wafanyakazi wa usalama ambao wamefundishwa kuuwa wale wote wanao onekana kuenda kinyume na serikali."

"Napenda kuualifu kuwa hayo unayo sema na kuandika siyo kweli, na nimeagiza uchunguzi ufanywe ndani ya serikali na pia mashirika ya kutetea haki za binanadamu niemaagiza yahusishwe katika uchunguzi huu ambao unania ya kuweka ukweli bayana.

Hali ya kutoelewana kwa viongozi hao kulianza baada ya rais mstaafu Obasanjo kumtaka rais Goodluk Jonathan kutogombe tena kiti cha urais, baada ya kupoteza viti 37 katika bunge la wawakilishi  kutoka na  wabunge 37 wa chama cha PDP kukuacha chama hicho na kujiunga na chama cham APC.

Rais Goodluck Jonathan na rais mstaafu Olugun Obasanjo wote ni wanachama wa PDP na wameweza kupata viti vya urais kupita chama cha PDP. 

Kwa mara ya kwanza Walibya wakubwa na mauaji ya kujitolea muhanga.

Tripol, Libya - 23/12/2013. Watu saba wamefariki baada ya muuaji wakujitolea muhanga kujilipua karibu na kizuizi kilichopo km 30 kutoka  jiji la Tripol.

Hii ni mara ya kwanza kwa  mauaji ya kujitolea muahanga  kutokea nchini Libya tangu kuangushwa kwa  utawalawa Muammar Gaddafi 2011.

Habari kutoka idara ya usalama ya nchi zinasema " hali imezidi kuwa siyo nzuri hasa katika swala la kiusalama, na hali ya kiusalama ya miji wa Benghazi na Tripol imekuwa katika hali tete kila kukicha "

Tangu kuangushwa kwa utawala wa Muammar Gaddafi, Libya imekuwa na vikundi tofauti vya kijeshi ambavyo vimegawanyika kutokana na kutoa afikiana baada ya vita vya kuipindua serikali kwa msaada wa Uingereza, Ufaransa na chini ya NATO jambo ambalo limekuwa likiangaliwa kuwa huenda likaleta mzuko wa kuanza vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Libya.

Mgunduzi wa AK-47 afariki dunia.



Moscow, Urusi - 23/12/2013. Mgunduzi wa siraha ya aina ya AK-47 ambayo imekuwa maarufu na kuwa moja ya siraha kipenzi  kimapambano amefariki dunia.

Mikhail Kalashnikov 94, amefariki dunia na kuacha historia ambayo itakuwa akikumbukwa  kwa muda mrefu kwa umairi wake wa kugundua siraha ambayo hadi leo inaleta  changa moto katika matumizi yake sehemu mbali mbali duniani.

Akiongea baada ya kupata habari ya kifo Mikhail Kalashnikov, rais wa Urusi Vladmir Putin alisema " nivigumu kukubali ya kuwa  hatupo naye tena Mikhail Kalashnikov, na tumepoteza mtu muhimu katika jamii nzima ya Kirusi kwani Kalashnikov alikuwa  mzalendo aliye tetea kwa  kupigania nchi yake wakati wa maisha yake yote."Alimalizia rais Putin.

Mikhail Kalashnikov, aligundua siraha ya AK-47  mwaka 1947 baada ya kupona majeraha ya bega ambayo aliyapata wakati akiwa vitani alisema " nilipata hili wazo baada ya kuzinduka kitandani wakati nilipo kuwa nimelazwa hospital kwa matibabu."

Wakati wa uhai wake mara kwa mara Mikhail Kalashnikov, amekuwa akisema yakuwa hajutii ugunduzi wake, kwani ulisaidia kulinda  heshima ya Urusi."

Siraha ya AK-47 imekuwa ikitumika katika kila aina ya mazingira ya kivita na inasifika kwa kutokuwa na matatizo ya aina yoyote katika matumizi kama siraha nyingine,  na kwa miaka 60 sasa imekuwa ni siraha hatari duniani kutokana na umairi wake.

Sunday, December 22, 2013

Mahakama ya Uingereza yatupilia mbali kesi ya mwanasiasa wa Libya.

Mahakama ya Uingereza yatupilia mbali kesi ya mwanasiasa wa Libya.


Tripol, Libya -22/12/2013.  Mahakama  jijini London imetupilia mbali kesi ya mmoja wa kiongozi waliosaidia kuung'oa utawala wa Muammar Gaddafi 2011.

Akitoa hukumu kabla ya kutupilia mbali kesi ya Belhaj imedai Jaji  Simon alisema, " kwa kuangalia mwenendo mzima wa kesi hii, matendo mengi yalitendeka Malasyia, Thailand and  Libya na ambapo ni  nje ya nchi na hivyo hayahusiki na Uingereza."

Akiongeaa baada ya  hukumu kutolewa Belhaj  alisema " Maelezo ninavyo fahamu ni kuwa ikiwa kesi hii itaendelea, wanadai kuwa itawaaibisha Marekani, navilevile itahatarisha usalama wa taifa la Uingereza."

" Lakini hata hivyo kwa kupitia mwanasheria wangu tutapambana hadi tupate ushindi na kwani haki itatendeka mwisho wa siku."

Abdul - Hakim Belhaj,ambaye kwa sasa amekuwa mmoja wa viongozi wa siasa nchi Libya, ambaye amemeushitaki uongozi wa juu wa ofisi ya mambo ya nje wa Uingereza na mkuu wa MI6, Sir Mark Allen  kwa kosa la kumkamata kwa nguvu na kumpeleka  Libya wakati wa utawala wa Gaddafi na kuteswa.

Kesi ya kuwakamata watu kwa nguvu na kuwapekeka katika maeneo ya mateso, zimekuwa zikiiandama serikali ya Uingereza, na hata baadhi ya majaji kudai kuwa sheria ilivujwa na wakuu wa usalama wa Uingereza katika kufanya vitendo hivyo.

Mkwe wa Bin Osama Bin Laden aongezewa mashitaka.

New York,Marekani - 22/12/2013. Mahakama jijini New  York katika kitongoji cha Manhattan, imemuongezea mashitaka mawili zaidi aliyekuwa mkwe wa mkuu wa kundi la Al Qaeda Osama Bin Laden.

Suleiman Abu Ghaith, ameongezewa mashitaka ya  kusaidia kimali na kutoa habari katika kundi la Al Qaeda kuweza kufanya mashambulizi yake nchini  Marekani ya Sept 11 2001.

Suleiman Abu Gaith ambaye ni mzaliwa wa Kuwait alikutwa hapo awali na kosa baada ya kuongea maneno yakuunga mkono mashambulizi ya Sept 11. kwa kusema " tunafuraha kuona wapiganaji wa Mijaidini wameweza kushambulia nchi Marekani kwa uwezo wa Mungu na mapema dunia itashuhudia kushambuliwa kwa miradi ya Marekani na Waizrael."

Mashambuzi ya Sept, 11-2001 nchini Marekani yalisababisha vifo vya watu 3000, na watu kadhaa kuumia na mali nyingi kuharibiwa baada ndege zilizo kuwa zimetekwa na magaidi wa kundi la Al Qaeda kufanya mashambulizi Trade Centre New York, Pentagon na Pennsylvania.

Suleiman Abu Gaith anatarajiwa kufikishwa mahakamani kusikiza kesi zake Februri 3, 2014.

Friday, December 20, 2013

Rais Vladmir Putin aonyesha huruma yake. 
 

Moscow, Urusi -20/12/2013. Rais wa Urusi Vladimir Putin ametoa msamaha kwa aliyekuwa bilionea ambaye alikuwa amefungwa kwa makosa ya rushwa na kukiuka matumizi ya usambazaji wa pesa wa nchi ya Urusi.
 
Mikhail Khodorkovsky, ambaye amekaa jela miaka 10, baada ya kuhukumiwa kwenda jela mwaka 2003 aliachiwa huru leo kutoka katika gereza lililopo katika mji wa Karelia km 1,000 toka jiji la Moscow, baada ya rais Putin kutoa msamaha kutokana na sababu za kibinadamu na kiutu.
 
Akithibitisha kuachiwa na kuwasili Ujerumani, aliyekuwa waziri wa mambo ya nje Hans-Dietrich Genscher amesema " Mikhail Khodorkovsky amewasili katika jiji la Berlin kwakutumia ndege binafsi na mimi ndo nimemchukua toka kiwanja cha ndege."
 
Kuachiwa kwa Khodorkovsky kumekuja baada ya jitihada za Kansela  Waujerumani Angela Markel kukubalika na rais Putini ambapo kila walipo kutana aliomba serikali ya Urusi kumwachia Mikhail Khodorkosky.
 
 
Edward Snowden azidi kuziumbua Marekani na Uingereza.
 
 
London Uingereza - 20/12/2013. Sakata la shirila la kijasusi la Uingereza  na mshirikiwa wake Marekani kugundulika kuwa walikuwa wanachunguza na kusikiliza mazungumzo na mawasiliano ya simu na mtandao yamefichuliwa kwa mara nyingine tena.
 
Magazeti ya The Guardian Uingereza, The New York Time Marekani  na Der Spiegal la Ujerumani yameandika zaidi ya  majina 1000 ya watu wambao walikuwa wakuchunguzwa, kufuatiliwa nyendo zao kimtandao na kusikilizwa simu zao na  mashirika ya kijasusi ya NSA ya Marekani na GCHQ ya Uingereza  kinyume cha sharia za kimataifa.
 
Magazeti hayo yameandika kuwa "NSA na GCHQ wamechunguza nyendo za viongozi umoja wa Ulaya, mashirika ya haki za binadamu, waziri mkuu wa Izrael na pia zaidi ya nchi 60  hasa viongozi wa Afrika na familia zao, na pia  shughuli zinazo endeshwa na Umoja wa Mataifa na viongozi wake."
 
Kutolewa kwa ripoti hizi mpya ambazo chanzo chake ni raia wa Marekani Edward Snowden ambaye alikuwa mfanyakazi wa NSA na  kwa sasa yupo ukimbizini nchini Urusi, kumekuja baada ya ile kashfa ya kuwa mashirika hayo kwa pamoja yalikuwa yanashirikiana kusiliza mazungumzo ya  Kansela wa Ujerumani Angela Markel na kuleta mtafaruku wa kidiplomasia kati ya nchi hizo.
 
 
 Chama tawala Afrika ya Kusini njia panda na washirika wake.
 
Pretoria, Afrika ya Kusini - 20/12/2013. Moja ya chama kikuu  cha wafanyakazi nchini Afrika ya Kusni kimetangaza kutounga mkono chama tawaza cha ANC - (African National Congress) wakati wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika 2014. 
 
NUMSA ambacho ni chama cha wafanyakazi wa viwanda vya vyuma,  ambacho kinawanachama zaidi ya 3,00,000, kimetoa azimio hilo wakati wa mkutano wa wanchama hao uliyofanyika hvi karibuni jijini Johannesburg.
 
Kiongozi wa chama hicho Irvin Jim  alisema  "NUMSA inajitoa katika kuunga mkono ANC, kwani chama cha ANC kimekuwa hakifanyi jitihada ya kupambana na rushwa na kupunguza umasikini na ufukara kwa wanachi wake na pia kukiuka ilani ya chama."
 
NUMSA imekuwa bega kwa bega na ANC tangu mwaka 1994, na hivi miaka ya karibuni imekuwa ikivutana na ANC kwa kudai ya kuwa chama cha ANC hakitekelezi kazi zake vizuri na kuwa kinatizama sana upande wa uchumi huria ambao haunufaishi watu walio wengi nchi Afrika ya Kusni.
 
ANC imekuwa na wakati mgumu katika sera zake kukuza uchumi chini Afrika ya Kusini, kutoka na na msukumo nguvu uchumi wa kuleta mabadiliko kuruhusu kuwepo na uchumi huria, jambo ambalo vyama vingi vya wafanyakazi vimekuwa vikiupinga mfumo huo.
 
 
Jela maisha ukiwa shoga nchini Uganda.
 
 
Kampala, Uganda - 20/12/2013. Bunge la Uganda limepitisha musuada ambao utakuwa wa kifungo cha maisha kwa mashoga wa kiume na wakike katika kura zilizo pigwa bungeni humo leo.
 
Uamuzi wa bunge la Uganda kupigia kura ya ndiyo ya kupitisha adhabu ya kukaa jela maisha, imekuja maada ya adhabu ya awali ya kunyongwa ambayo ilipingwa vikali na wana harakati wa kimataifa wa kutete haki za mashoga.
 
Msemaji wa bunge la Uganda amesema "Ushoga  ulikuwa ni haramu tangu enzi za serikali ya kikoloni nchini Uganda na kama tukiachia tabia hii itatualibia jamii nzima ya Waganda."
 
Sheria ya kuukataza  ushoga nchini Uganda  ilipitishwa kwa mara ya kwanza nchini humo mwaka 2009 ambapo spika wa bunge Rebeka Kadaga alisema "kupitishwa kwa sheria ya kupinga ushoga ni zawadi nzuri ya Krismasi kwa Waganda."
 
Wabunge wa Uganda wamekuwa wakidai yakuwa kanisa la Kievanjilisti la asili ya kuutoka Marekani limekuwa likiunga mkono ushoga na linakampeni ya kuusambaza ushaoga barani Afrika, madai ambayo wakuu wa kanisa hilo kutoka Marekani walikanusha.
 
Hata hivyo musuada huo utakuwa sheria baada ya rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museni kusaini kuwa sheria.
 
 
Baraka Obama aonya kuhusu mapigano nchini Sudani Kusini.
 
Juba, Sudani ya Kusini - 20/12/1213. Rais wa Marekani amezitaka pande zote zinazo pigana nchini Sudani Kusini kusimamisha mapigano haraka iwezekenavyo.
 
Baraka Obama alionya kwa kusema kuwa " Inabidi pande zote zinazo pigana nchi Sudani ya Kusini kucha mara moja vita, kwani vinaweza kuleta maafa makubwa kwa jamii na hatimayake kuwa vita vya wenyewe kwa wenyewe."
 
" Kitendo cha kutumia siraha ili kuweza kupata nguvu za kisiasa ndani ya nchi ni kitendo kibaya, na kila upande lazima wasikilize busara za kimataifa." Alimalizia rais Obama.
 
Wakati amani nchini Sudani ya Kusini imevurugika, mwanajehi wa umoja wa Mataifa kutoka nchi Indi amefariki dunia na mmoja kujeruhiwa, baada ya kushambuliwa ya wapiganaji wanao muunga mkono mpinzani wa serikali ya  ambaye alikuwa makamu wa rais Riek Machar kwa  kushambulia ngome ya makazi ya wafanyakazi wa umoja wa mataifa katika mji wa Bor.
 
Hadi kufikia sasa, zaidi ya watu 500 wamesha potea maisha yao wakiwemo wanajeshi 100, tangu mapambano yalipo anza, baada ya serikali ya rais Salva Kiir kudai ya kuwa imegundua mbinu za kutaka kuipindua serikali, zilizo kuwa zimepangwa na makamu wa rais Riek Machar, ambaye mmpaka sasa ajulikaani mahaali alipo.
 
 
Rwanda kupeleka majeshi yake Afrika ya Kati.
 

Kigali, Rwanda - 20/12/2013.Serikali ya Rwanda imekubali ombi la umoja wa Afrika kupeleka wanajeshi wake katika nchi ya Afrika ya Kati ili kusaidia kurudisha amani.

Akithibitisha hayo, kwa kutukia mtandao wa twiter, waziri wa mambo ya nje wa Rwanda, Louise Mushikiwabo aliandika " Rwanda iliombwa kuchangia wanajeshi nchini Afrika ya Kati, na wanajeshi wa Rwanda wapo katika matayarisho kuwasili jiji Bangui mapema iwezekanavyo"

Uamuzi wa Umoja wa Afrika kuomba msaada kwa jeshi la Rwanda umekuja baada ya ya hali ya amani katika nchi ya Afrika ya Kati kuwa mbaya zaidi, ambapo imefikia kuwa ugomvi wa kidini, kati ya  kundi linalo julikana kama Anti-Balaka la Wakristu kuanza kushabuliana na kundi la  Kiislaam la Seleka.

Kuchafuka kwa amani katika nchi ya Afrika ya Kati, kumesababisha zaidi ya watu 6,00,000 kukimbia makazi yao na huku kati yao 2,00,000 wakiokea jiji Bangui.

Wednesday, December 18, 2013

Angela Markel kuonngoza Ujerumani kwa mara ya tatu.
 
 
Berin, Ujerumani - 18/12/2013. Angela Markel 59, ameapishwa tena kwa mara ya tatu kuwa Kasela wa Ujerumani na kupewa madaraka ya kuiongoza nchi hiyo ambayo ni uti wa mgongo katika jumuiya wa nchi wanachama wa muungano wa Ulaya.
Kuapishwa kwa Angela Markel kumekuja baada  ya kufikia makubaliano ya chama chake cha CDU  na chama chenye mrengo wa kati kushoto cha SPD ambapo kwa pamoja wataunda serikali ya muungano itakayo iongoza Ujerumani.
 
Angel Markel amekuwa kiongozi wa kwanza kushinda uchakuzi nakuwa kansela tangu vita vya pili vya dunia chini ya chama chake cha CDU ( Christian Democratic Union).
 
Kufuatia kuapishwa kwa Angela Markel kuwa  Kansela wa Ujerumani, wanchi wa Ujerumani wanatongezewa kima cha chini cha mshahara  kama ahaadi ambazo zili aidiwa wakati wa kampeni.
 
  
Baada ya mapinduzi kushindwa hali ya hatari yatangazwa chini Sudani Kusini.
 
Juba, Sudani ya Kusini - 18/12/2013. Milio ya risasi imekuwa ikisika katika jiji la Juba na wanajeshi wanao muunga mkono rais wa sasa Sudani ya Kusini Salva Kiir kuvamia makazi ya makamu wa rais wa nchi hiyo ambaye anasadikiwa kuwa kiongozi wa kutaka kupindua serikali ya Kiir.
 
 Hadi kufikia sasa  watu  zaidi ya 500 waliopoteza maisha kutokana na mashabulizi ya kukusudiwa ya kuaangusha serikali ya rais Kiir na watu  wengine zaidi ya 20,000 kukimbilia katika eneo lenye makazi ya  ofisi za Umoja wa matafa nchi Sudani ya Kusini.
 
Kufuatia jaribio la kuipindua serikali, makamu wa rais Riek Machar ameshutumiwa kuwa muhusika mkuu baada ya kufukuzwa kazi na rais Kiir na baadhi ya watu kukamatwa na kupigwa marufuku matembezi ya usiku hadi hapo hali itakapo kuwa shwari.
 
Riek Machar alitangaza kuwa anataka kugombea urais wa wakati wa uchaguzi wa urais wa mwaka 2015, na alitoa kauli ya " nchi aiwezi kutawaliwa na udikteta wa utawala wa mtu mmoja."na bado hajakamtwa wala alipo hapajulikani.
 
Sudani ya Kusini imekuwa na msuguano wa kisiasa wa ndani tangu kupata uhuru wake toka  Sudan 2011.
 
Jela miaka minne na bakora juu.
 
Riyadh, Saudi Arabia - 18/13/2013. Mwanaharakati nchi Saudi Arabia amehukumiwa kupigwa viboko 300 na kifungo cha miaka 4 kwa baada ya kukutwa na hatia ya kupinga sharia zilizo wekwa na serikali ya  ufalme wa nchi hiyo.
 
Omar al Saed 24, ambaye kesi yake ilisikilizwa katika mahakama ya ndani na kukataliwa kuwa na mwanasheria wa kumtete  nabaadaye  kukutwa na kosa la kuikosoa serikali ya  kifalme ya Saudi Arabia kwa kukiuka  haki za binadamu na
 
Saudi Arabi ni moja ya nchi tano ambazo zimekuwa zikishutumiwa na shirika la kutetea haki za binadamu la Amnest International kwa kukiuka haki za binadamu. 
 
 
Urusi yazidi kutanua nguvu za mabawa yake
 
 
Moscow, Urusi - 18/12/2013. Serikali ya Urusi na serikali ya Ukraini  zimekubaliana kibiashara na kiuchumi, baada ya viongozi wa nchi hizo mbili kukutana jiji Moscow.

Rais wa Urusi Vladmir Putin na rais wa UkrainiVictor Yanukovich walikubaliana kushirikiana kwa ukaribu kati ya nchi hizo katika masuala ya kibiashara, kiuchumi na kisiasa, ambapo Urusi ilikubali kushusha bei ya gesi na mafuta kwa nchi ya Ukraini na kutoa kiasi cha $ dola za Kimarekani 15 billion kwa Ukraini ili iliweze kujenga uchumi wa nchi yake.

Akiongezea baada ya makubaliano hayo rais Putini alisema "makubaliano ya leo ni ya hiyari kati ya nchi hizi mbili na Urusi itachangia pia kwa kiasi kikubwa katika masuala ya kiulinzi nchi Ukraini"

Makubaliano hayo yamekuja wakati wanachi wa Ukraini wakiwa wamegawanyika,  baaadhi yao kutaka nchi yao ijihusishe zaidi na nchi za jumuiya ya muunganao wa Ulaya (EU), na wa wengingene wakitaka nchi hiyo kuwa karibu na Urusi, jambo ambalo limesababisha maandamano makubwa katika jiji la Kiev na kwenye baadhi ya mikoa nchini humo.

Kufuatia makubaliano hayo kati ya Urusi na Ukraini, viongozi wa vyama vya upinzani nchi Ukraini wamedai yakuwa kitendo cha rais Yanukovich kukubaliana na Urusi ni kuvunja nia ya nchi hiyo kuwa mwanachama wa nchi za muungano wa umoja wa Ulaya,  ambao baadhi ya Waukraini wanahisi kutawarahisishia kuwa karibu na nchi hizo za umoja wa Ulaya.

Sunday, December 15, 2013

Nelson Rolihlahla Mandela apumzishwa kwenya makao yake ya milele.

Nelson Rolihlahla Mandela apumzishwa kwenya makao yake ya milele.




Qunu, Umthatha,  15/12/2013. Nelson Rolilhalha Mandela - Madiba kiongozi na rais wa kwanza mweusi wa Afrika ya Kusini huru amepumzishwa kwa amani katika makao yake ya milele kwenye kijiji alicho kulia na kucheza wakati wa udogo na ujana wake.

Kijiji cha  Qunu, kijiji ambacho Nelson Mandela amelazwa na  huku  misa ya kumuaga ilifanyika kwa muda wa masaa mawili,wakati ndugu wa karibu, jamaa, machifu wa ukoo wa Nelson Mandela, viongozi tofauti kutoka sehemu mbalimbali dunia, na marafiki zake wakaribu walishuhudia kupumzishwa kwa Madiba.

Nelson Rolihlahla Mandela 95, kabla ya kushushwa kwenye makao yake ya  milele, aliaagwa kwa kupigiwa mizinga 21 ikiwa ni ishara ya kumuaga kama kiongozi na rais wa nchi.


Na kwa sasa Nelson Rolihlalha Mandela - Madiba hatupo naye kimwili, ila kiroho tupo naye na mishumaa 95 iliyo washwa ikiwa ni ishara ya kuwa miaka 95 aliyo ishi bado tupo naye daima, Amin.

Amba Kahle Utata, Umkhulu, Nelson Rolihlahla Mandela - Madiba.


Friday, December 13, 2013

Mazungumzo ya Irani na nyuklia yaingia dosari.

Tehran, Iran 13/12/201. Iran imesimamisha mazungumzo ya kinyuklia na nchi  sita kubwa duniani baada ya  Marekani kuiwekea vikwazo Iran.

"Umuzi wa Marekani kuyaongeza makampuni 19 ya kutoka Iran katika vikwazo vya kibiashara,kumeelezwa na Tehran kama ni ujumbe unao onyesha kuwa  juhudi za mazingumzo ya Iran na mpango wake wa kujadili maendeleo yake ya kinyuklia ni bure." Alisema Abbas Araghchi ambaye ni  makamu wa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Iran.
 
Hata hivyo msemaji wa serikali ya Marekani Jay Carney  amesema kuwa "kitendo cha kuwekewa vikwazo makampuni 19 ya  Iran hakikuvunja mkataba wa Novemba 24"

Mazungumo kati ya nchi sita, China, Uingereza, Fransa, Germani, Urusi na Marekani kuitaka Iran kuachana na mpango wake wa kuendelea kuzalisha  nguvu za kinyuklia ulikuwa umesha fikia katika kipindi cha kukubaliana, baada ya mazungumzo ya Novemba 24, ambapo Iran na nchi sita ziliafikiana kimsingi kufikia makubaliano.

Rufaa ya Victoire Ngabire yakataliwa.

Kigali, Rwanda - 13/12/2013. Maakama ya rufaa jiji Kigali, imetupilia mbali rufaa ya maombi ya aliyekuwa kiongozi wa chama cha upinzani nchini humo Victorie Ngabire.

Kufuatia kukataliwa kwa rufaa hiyo, Victoire Ngabire ataendelea kutumika kifungo cha miaka 15 jela, baada ya kukutwa na hatia na makama jiji Kigali kwa kosa la kuchonganisha makabila, na vilevile kueneza chiki za mauaji ya kimbari yaliyo fanyika  Rwanda 1994.

VictoireNgabire mama mwenye watoto watatu na mume, alikamatwa mwaka mwezi Oktoba 2010, kwa kosa la kudai ya kuwa pia wale "Watutsi walio husika katika kuua wa Hutu nao washitakiwe."

1994, dunia nzima ilishikwa na mstuko, baada ya mauaji ya watu zaidi ya 800,000 kuuwawa, kutokana na visa vya kikabila kati ya  Watutsi na Wahutu, na Wahutu walio wengi waliuwawa.

Victoire Ngabire 45 ambaye alirudi nchi Rwanda kama kiongozi wa chama cha  Nguvu za Muungano wa Demokrasia Unified Democratic Force (UDF) baada ya kukaa nje ya nchi kwa muda wa miaka 16.

Kim Jong Un ammgeuka mjomba wake.

Pyong Yang, Korea ya Kaskazini - 13/12/2013. Mjomba wa kiongozi na aliyekuwa mkuu wa pili katika uongozi wa jeshi na madaraka yote wa Korea ya Kaskazini amenyongwa kwa mujibu wa shirika la habari KCNA la nchi hiyo.

"Jang Song Thaek, ambaye anadaiwa kwa kukutwa na hatia ya kutaka kupindua serikali, kula rushwa na kuvunja miiko ya serikali." Liliripoti shirika hilo la habari la Korea ya Kaskazini KCNA.

Kunyongwa kwa Jang Song Thaek, kumetamfsiliwa kuwa ni moja ya myumbo wa kiungozi, kwani inaaminika kuwa " Jang Sing Thaek ndiye aliye simamia na kumsaidia  kiongozi wa sasa Kim Jong Un hadi kuweza kuwa imara katika uongozi aliyo nao sasa.

Jang Song Thaek, alikuwa ni mtu wa karibu wa kiongozi wa Korea ya Kaskazini marehemu Kim Jong Il ambaye ni baba wa kiongozi wa sasa Kim Jong Un.

M23 na serikali ya DRC Kinshasa wasaini mkataba wa amani.



Kinshasa, DRC - 13/12/2013. Serikali ya DRC imetiliana sahii makubaliano ya kusimamisha mapigano na kundi la waasi M23 linalo pingana na serikali ya Kinshasa.

Mkataba huo wa makubaliano ambao umewekwa sahii jijini Nairobi Kenya, na kukubaliana  yakuwa wale wapiganaji wa M23 wataaungana na  wanajeshi wa jeshi la serikali na vilevile kusalimisha siraha na vifaa vyote vya kivita ambavyo vilikuwa vinatumika na kundi la M23.

Akisisitiza baada ya kutiliana sahii ya amani, msemaji wa serikali ya DRC, Lambert Mende amesema "katika mkataba huu ni kwamba wale wote walio husika katika uvunjaji wa hali za binadamu, na kutakiwa kujibu mashitaka kwa mujibu wa sheria za kimataifa za kulinda haki za binandamu hawata husishwa na wala kupewa msamahaa kama tulivyo kubaliana."

M23, ni kundi la wapiganaji wa kijeshi, ambao wanaaminika wengi wao wanaasili ya Kitutsi,  na wamekuwa napigana na serikali ya Kinshasa, kwa madai ya kuwa  serikali ya DRC haiwatendei haki.

Wednesday, December 11, 2013

Wezi wavunja nyumba ya Askofu wakati yupo kwenye misa ya Nelson Mandela.

Papa Fransis achaguliwa kuwa mtu muhimu wa mwaka 2013.

Vacan City, Vatican - 11/12/2013. Papa Fransis amechaguliwa kuwa mtu muhimu duniani na  gazeti la Time na kuwashinda Edward Snowden na rais wa  Syria Bashar Al Assad.

Akieleza uamuzi wa kumchagua Papa Fransis kuwa mtu muhimu katika msimu wa mwaka 2013, mhariri mkuu Nancy Gibbs amesema "Katika kipindi cha miaka 1200 Papa Fransis ni kiongozi wa kwanza kutoka Amerika kuongoza kanisa kubwa duniani na ameonyesha uwezo wake na hasa katika kubadirisha mwenendo  wa kanisa Katoliki."

Papa Fransis  amekuwa kiongozi wa tatu wa kanisa Katoliki kuteuliwa kwa kufuata nyayo za Papa John XXII mwaka 1962 na Papa John Paul II 1994.


Wezi wavunja nyumba ya Askofu wakati yupo kwenye misa ya Nelson Mandela.
 
Cape Town, Afrika ya Kusini - 11/12/2013. Wezi wamevunja na kuingia kwenye nyumba ya Askofu Mkuu Mstaafu  wa Kanisa la Anglikani  jiji Cape Town.

Tukio hilo limetokea wakati Askofu Desmond Tutu 82 na mkewe walipokuwa wamekwenda jijini Johannesburg kuhuria misa ya kumkumbuka ya marehemu  rais Nelson Mandel ambaye alikuwa rais wa kwanza  mweusi wa Afrika ya Kusini tangu kuangushwa kwa utawala wa ubaguzi wa rang


Mwangalizi na msimamizi wa Askofu Tutu Roger Friedman alisema" nyumba ya Askofu imevunjwa na mpaka sasa hatuwezi kusema ni vitu kiasi gani vimeibiwa "

Hii itakuwa ni mara pili kuvunjwa kwa  nyumba kwani mara ya kwanza ilivunjwa Agosti 7/2013, ambapo wezi waliingia nakuchukua baadhi ya vitu huku Askofu Desmond Tutu akiwa amelala na mkewe ndani.

Askofu Desmond Tutu 82 ni mshindi wa Nobel ya Amani ya mwaka 1984.

Matumizi ya Bangi yahalishwa nchini Uruguay.

Mwili wa Nelson Rolihlahla Mandela kuonyeshwa kwa mara ya mwisho.


Pretoria, Afrika ya Kusini - 11/12/2013.Familia, ndugu na jamaa pia  maelfu ya watu wamajipanga mstari ili kumuaga na kumona kwa mara ya mwisho aliyekuwa rais wa kwanza mweusi waAfrika ya Kusini Nelson Mandela katika jengo  serikali - Union Building lililopo jijini Pretoria.

Mwili wa marehemu Nelson Mandela ulikuwa umewekwa wazi kwa wanchi, wazalendo na watu kutoka mataifa tofauti ili kutoa heshima zao za mwisho. Mwili wa Nelson Mandela utaonyeshwa kwa watu kwa muda wa siku tatu.

Kufuatia kitendo cha watu kuruhusiwa kuona mwili wa  Nelson Mandela kwa mara ya mwisho, watu kadhaa waliishiwa nguvu huku wakilia na wakati huohuo wengine kuzimia.

Mwili wa hayati rais wa kwanza wa Afrika ya Kusini Nelson Mandela utapelekwa kupumzishwa Qunu katika mji wa Umtatha.

Matumizi ya Bangi yahalishwa nchini Uruguay.


Montevideo, Uruguay, - 11/12/2013. Bunge la Senete la Uruguay limepitisha kwa kura nyingi uamuzi wa zao la bangi kuwa halali. Kura ambazo 16 kati ya 29 ziliunga mkono uhalali wa  kulima bangi na kuwa inatumika bila kuwa kosa la jinai nchini humo.

Kufuatia kukubali kwa wabunge wa senete, rais wa Uruguay Jose Mujic atasahini muswaaada huo kuwa sheria.

Mmoja  kati ya wabunge waliopiga kura ya kukubali uhalali za zao la bangi Seneta Roberto Conde amesema " uamuzi wa bunge kupitisha  muswaada huu, ni kwa sababu ambazo hazikuweza kuzuilika.

Bangi ni moja ya zao amblo linatumika na watu wakila lika, na inaeleweka kuwa inamadhara madogo sana katika jamii."

Hata hivyo shirika la kupambana na madawa ya kulevya limepinga vikali kitendo cha bunge kukubali kuruhusu matumizi ya bangi kwa kusema "nikinyume na makubaliano ya mwaka 1961 ambapo Uruguay ni mwanachama."

Uruguay imingia katika  kundi la nchi kama  Netherlands na Spain ambazo sheria za matumizi ya bangi zinruhusu matumizi ya zao hilo kwa matumizi ya mtu binafsi.