Friday, June 29, 2012

Marais wa Somalia wakutana UAE - Dubai.

Mohamed Morsi aapishwa rasmi kuwa rais wa Misri.

Kairo, Misri - 29/06/2012. Aliyekuwa mshindi wa uchaguzi wa Urais nchini Misri atapishwa rasmi kuwa rais wa nchi hiyo kesho Jumamosi.
Rais Mohamed Morsi  akiongea mbele ya watu walio kuja kumsikiliza siku moja kabla ya kuapishwa na kuhaidi ya kuwa ataijenga nchi kwa kufuata misingi ya katiba na kisisitiza ya kuwa "hakuna mwananchi ambaye atakuwa juu ya sheria na sitaogopa mtu isipokuwa Mungu.
"Nitalinda nchi yangu na mkipaka yake na kuhakikisha safari  ya kuwa serikali ya kiraia inafikiwa."
Hotuba ya rais Mohamed Morsi imeonyesha kuwa hali ya jeshi kuchukua madaraka kama ilivyo fikiriwa itakuwa ngumu kwa kiasi kikubwa.

Nchi za jumuiya ya Ulaya zachukua hatua ya mbadala ilikuinua uchumi

Brussels, Ubeligiji - 29/06/2012. Viongozi wa jumuiya ya nchi za Ulaya wamekubaliana kwa pamoja kuinua benki zao kwa kuzipatia fedha ili kusaidi kuinua biashara  na uchumi.
Viongozi hao ambao walichukua karibu usiku mzima nakukubaliana kimsingi ya kuwa ipo haja ya kuinua hali ya mtiririko wa fedha ili kusaidi mwamko wa kiuchumi na kibiashara.
kansela Angela Merkel ambaye nchi yake ilikuwa inaaonekana kama ni kikwazo hapo awali alisema  " Nimeridhika na matokeo ya mkuno huu japo ulichukua muda mferu, lakini matokeo ya mkutano huu ni mazuri kwa nchi zote wanchama wa nchi za jumuiya ya Ulaya."
Makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano huo yameleta matumani makubwa kwa nchi za ispania na Itali nchi ambazo hali zake za kichumi fedha zilikuwa katika hali ya kuyumba.


Kampuni ya Nestle yalaumiwa.

London, Uingereza - 2012. Kampuni inayo shughulikia vyakula ya Nestle imelaumiwa kwa kutofanya uchunguzi mazingira ya kazi ambayo yanahusisha watoto wadogo.
Habari zilizo tolewa hivi karibuni na shirika linalo shughulikia na kusimamia ufanyaji wa kazi na usawa ( Fair  Labor Association - FLA) zimesema, " Nestle hakutilia maanani ni kwa jinsi gani  mazao yanayo uzwa na kuzalishwa na wakulima yana patikana kwa namna gani, kwani kuna ushaidi ya kuwa kuna watoto 1.8 million ambao wanafanyishwa kazi katika uzalishwaji wa mazo ya kampuni ya Nestle,  hasa  mashamba ya kakao yaliyopo Afrika ya Magharibi."
Nestle nikampuni kubwa duniani ambayo inajihusisha  na uzalishaji wa chokoleti duniani
hata hivyo makamu wa rais wa kampuni hiyo Jose Lopez alikanusha kwa kusema " Hatutumi watoto katika uzalishaji na tunapinga kitendo hicho katika nyanja  zetu zote za uzalishaji wa mazao ya Nestle. na huwa tunahakikisha ya kuwa hakuna watoto wanao tumiwa katika uazlishaji hasa katika zao la kakao kama ilivyo ripotiwa. na huu ndiyo msimamo wetu" 

Wafanyazi wa kutoa misaada watekwa nyara nchini Kenya.

Nairobi, Kenya - 29/07/2012. Wafanyakazi wa shrika linalo toa msaada wa kibinadamu wametekwa nyara nchini Kenya katika kambi ya wakimbizi iliyopo Dadaab.
Masemaji wa Polisi nchini Kenya  Philp Ndolo alisema " raia wanne wa kutoka Kanada, Pakistan, Norway na Phillippin walitekwa nyarawakati wakiwa maeneo ya kambi ya wakimbizi ya Dadaab baada ya gari walilikuwa wakisafiria kushambuliwa."
Utekwaji nyara wa wafanyakazi wa mashirika ya kigeni wamekuwa wakifanya kazi za kuhudumia wakimbizi katika eneo hilo kwa mashaka na kusababisha baadhi ya mashika kusimamisha utoaji misaada katika eneo hilo.

Marais wa Somalia wakutana UAE - Dubai.

Dubai, United Arab Emirates - 29/06/2012. Marais wa Somaliland na Somalia wamekutana Dubai kwa mara ya kwanza tangu kuvunjika kwa muungano wa nchi hizo miaka karibuni 20 iliyopita.
Rais Sheikh Sharif Ahmed na Ahmed Silanyo walikutana  kufuatia mkutano wa kwanza  wa wawakilishi wa nchi hizo  uliyofanyika  nchini Uingereza hivi karibuni.
Lengo la kuaza kwa mazungumzo hayo ni kukubaliani nchi hiyo kuwa moja kama Somalia, tangu kujitenga kwa Somaliland 1991, kufuatiqa kuangushwa kwa serikaliaki ya rais Mohmed  Seyyid Bare.
Rais wa Syria ahaidi kutoruhusu nchi nyingine kumwekea msharti.

Damascus, Syria - 29/06/2012. Rais wa Syria amehaidi ya kuwa hataruhusu na kukubali nchi yoyote kuiwekea masharti serikali yake katika harakati za kutaka kuleta amani nchi humo.
rais Bashar al Assad alisema " matatizo yaliopo nchini Syria ni ya wanachiwa Syria na ni ya ndani ya Syria, na  hayahusiani na nchi za kigeni kama nchi hizo zinavyo dai na Wasyria ndiyo watakao maliza  hili suala bila  msukumo au masharti kutoka nchi nyingine."
Bashar al Asssad amefanya mazungumzo hayo kwa mara ya kwanza tangu vurugu na kutokuwepo na amani  nchi Syria kuanza jambo ambalo linaaminika kuipilekea nchi hiyo kuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Thursday, June 28, 2012

Watu 40 wapoteza maisha katika lori baada ya kukusa hewa.

Ururiki yapeleka majeshi yake kwenye mpaka na Syria.


Ankara, Uturuki - 28/06/2012. Serikali ya Uturuki imeamua kuimarisha ulinzi katika mipaka yake na Syria kwa kuamua  kupeleka siraha  na wanajeshi mpakani na nchi hiyo kufuatia kuangushwa kwa ndege yake ya kivita  hivi karibuni na Syria.
Siraha hizo ambazo ni  za kutungulia ndege na za kuzuia mabomu zimlipelekwa kwenye mpaka na Syria baada la  tamko la serikali ya kuwa hawataruhusu tena kitendo hicho kutokea.
Kutokuelewana kati ya Syria na Uturuki kumekuja baada ya serikali ya Uturuki kuwaunga mkono na kuwahifadhi wapinzani waserikali ya Syria ambao kwa sasa wanapambana kivita na serikali ya Syria.

Benki maharufu duniani yapigwa faini.

London, Uingereza - 28/06/2012. Benki ya Barclays nchini Uingereza imepigwa faini kwa makosa ya kukiuka misingi ya mikopo na kupandisha riba.
Benki ya Barclays ilipigwa faini kiasi cha $453millioni dola za Kimarekani  baada ya wachunguzi wa maswala ya masoko fedha na mikopo kugundua ya kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa masharti na maadili ya kibenki.
Hali hii ya  benki ya Barclays kupigwa faini imezidi kuleta msuguano mkubwa nchini Uingereza, kufuatia uamuzi wa serikali uliyo ufanya hapo wali kwa kuzisaidia benki kifedha baada ya benki hizo kuyumba kibiashara. 

China yakamulisha harakati za kianga kwa njia ya kawaida.

Beijing, China - 29/07/2012. Wanaanga watatu wa wa Kichina wamerudi duniani baada ya kumaliza  harakati zao za kisayansi katika anga (orbit)
Wanasayansi hao watatu ambao kati yao alikuwa mwanamke na  walitumia vyombo ambavyo vilikuwa vinaongozwa kwa njia ya kawaida (manual),  walitua duniani bila matatatizo yoyote kwa mujibu wa habari kutoka serikali ya Uchina.
China imewarusha wanaanga hao kufuatia kitendo kama hicho kilicho fanywa na Marekani na Urusi miaka ya sitini.

Watu 40 wapoteza maisha katika lori baada ya kukusa hewa.

Dodoma, Tanzania - 28/06/2012. Polisi nchini Tanzania wamewakuta watu wapatao 40 wamekufaa ndani ya lori lililo kuwa limewabeba.
Watu hao 40 ambao walikuwa raia wa Somalia na Ethiopia walikufa kutokanaa na kukosa hewa ndani ya lori hilo ambalo walikuwa wanasafiria na  halikujulikana lilikuwaa limetokea sehemu gani na watu hawa.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa  Tanzania Isaac Nantanga alisema " kumekuwa na ongezeko la watu kutoka Somalia na Ethiopia ambao wamekuwa wakielekea nchini Afrika ya Kusini kutokana hali zilizopo katika nchi hizo."
Usafirishwaji wa watu katika  malori umekuwa ukitumika sana katika baadhi yaa nchi za Afrika jambo ambalo limekuwa likihatarisha maisha ya watu wanao tumia maroli hayo.

Sunday, June 24, 2012

Misri yapata rais wa kwaza wa kirahiya baada ya miaka zaidi ya 30 kupita.

Mji wa Mombasa washambuliwa kwa mabomu.

Mombasa, Kenya - 24/06/2012. Mmtu mmoja ameuwaa na wengine kujeruhiwa na mabomu mjini Mombasa siku moja baada ya onyo kutolewa na  ofisi za ubalozi wa Marekani. 
Polisi mjini Mombasa imesema " mashambulizi hayo yalitokea saa nne usiku kwa muda wa masaa ya Kenya wakati wakazi wa mji huo wanaangalia mshindano ya kombe la Ulaya kwenye bar moja iliyopo Mombasa mjini."
Onyo la mashambulizi katika mji wa Mombasa, lilitiliwa maanani na kuzifanya serikali za nchi za Magharibi kuwaonya wananchi wao kuwa waangalifu watakapo kuwa katika matembezi ya kitalii katika mji wa Mombasa.

Marekani ya rudisha msaada wa pesa kwa Malawi.

Lilongwe, Malawi - 24/06/2012. Serikali ya Marekani imerudisha msaada waki fedhe ambao ulikuwa imeizuia kwa serikali ya Malawi, baada ya serikali  iliyopo madaraka ya rais  Joyce Banda kurudisha misingi ya kidemokrasi inayo takiwa.
Dola za  Kimarekani million $350 ambazo zilisimamishwa kutolewa na serikali ya Marekani,  baada ya serikali ya marehemu  Bingu wa Mutharika kukataa makubaliano na nchi za Magharibi na hata kufikia kuvunja uhusiano wa kiplomasia na Uingereza nchi ambayo inatoa misaada mkubwa kwa Malawi.
Malawi nchi ambayo ni moja ya nchi zenye uchumi duni duniani, imekuwa na myumbo wa kisiasa kwa muda tangu mabadiriko ya kisiasa ya vyama vingi kuingia nchini humo.


Misri yapata rais wa kwaza wa kirahiya baada ya miaka zaidi ya 30 kupita.

Kairo, Misri - 24/062012. Matokeo ya uchaguzi nchini Misri yametangazwa na mgombea urais kwa kupitia chama cha Kiislaam cha Muslim Brotherhood nchini huo  amatangazwa kuwa mshinda kwa 51% zidi ya mpinzani wake.
Mohamed Mosri  alitangazwa kuwa mshindi na kamati  ya uchaguzi ya  Misri na huku waananchama wa chama cha Muslimu Brotherhood wakishangilia kwenye makutano maaruufu ya Tahrir yaliyopo katikati ya jiji la Kairo.
Akiongea baada ya kutangazwa kuwa mshindi Mohamed Mosri alisema " sina haki bali ninamajukumu makubwa na kama sitawajibika basi haina haja ya kukubali uongozi wangu na nitawatukumia wa Misri wote  kufanya kazi kwa ajili ya nchi ya yangu."
Matokeo ya uchaguzi nchi Misri yametolewa sikuchache mbele baada ya ya siku iliyo tarajiwa matokeo kutolewa Alhkamisi kuarishwa ili hadi leo siku ya Jumapli ilikuweza kupata matokeo sahihi yasiyo na shaka, baada ya pande zote mbili kulalamika juu ya uchuguzi ulivyo endeshwa.

Saturday, June 23, 2012

Marekani yatoa onyo la mashambulizi katika mji wa Mombasa.

Serikali ya Uganda kupiga marufuku wapenzi wa jinsia moja.

Kampala, Uganda - 23/06/2012. Serikali ya Uganda imezifuta ofisi na mashirika yasiyo yanayo husika katika kuunga mkono ushoga na watu wanao pendana kwa jinsia moja.
Waziri Simon Lokodo ambaye ni waziri wa maadili ya jamii alisema "  pendekezo la kuzisimamisha na kuzifuta ofisi hizo  zimekuja baada ya mimi  kuangalia kiundani na bila kuwa na shaka ya kiubinadamu yakuwa  mashirika  haya 38 yanahusika katika kampeni ya kukuza ushoga, jambo ambalo ni kinyume na maadili yetu na kiimani.
Kampeni hya kuponga ushoga nchini Uganda, imekuwa ikikua siku hadi siku, na kuungwa mkono na wakuu wa dini nchini humo.


Marekani yatoa onyo la mashambulizi katika mji wa Mombasa.


Mombasa, Kenya - 23/06/2012. Mji wa Mombasa umeongezewa ulinzi baada ya ofisi za ubalozi wa Marekani kuaagiza  raia wake waliopo katika mji huo kuondoka.
Uamuzi wa Marekani kuaagiza raia wake kuondoka katika mji wa Mombasa, umekuja baada ya kupata habari ya kuwa "bandari iliyopo katika mji huo, inaweza shambuliwa muda wowote."
Nayo serikali ya Ufaransa imewataka wananchi wake kuwa waangalifu kwa kipindi chote watakapo kuwa katika mji huo wa Mombasa.
Hata hivyo maafisa usalama wa Kenya kwa kushirikiana na polisi, wameeomba "kuwepo na utulivu kwani wanafuatilia habari hizo."
Kenya imekuwa ikikimbwa na mashambulizi ya mabomu kwa muda zaidi ya mwaka mmoja, tangu serikali hiyo ilipo amua kupambana na kundi la Al Shabab nchini Somalia, na kundi la Al Shabab kuhaidi kufanya mashambulizi nchi Kenya ikiwa ni njia ya kulipiza kisasi.


Syria yaangusha ndege ya kijeshi ya Uturuki.


Ankara, Uturuki - 23/06/2012. Serikali ya Uturuki imedandege  iliyoangushwa  na jeshi la Syria ni ndege yake ya  kivita.
Kwa mujibu wa habari kutoka jeshi la Syria, zinasema " ndege hiyo ilivuka mpaka na kuingia ndani ya  anga za Syria na jambo ambalo ililazimisha jeshi hilo kuiangusha ndege hiyo."
Nayo serikali ya Uturuki imedai ya kuwa kitendo cha kuingusha ndege yake, sikitendo cha kuchukuliwa juju juju, na bado inafanya uchunguzi ili kujua ukweli kamili, na itafanya uamuzi baada ya uchunguzi kuisha. 

Friday, June 22, 2012

China na Brazil kubadilishana pesa kibiashara.

Rais wa Afghanistan ashutumiwa kwa undugu.

Kabul, Afghanistan - 22/06/2012. Rais wa Afghanistan amekubwa na wakati mgumu, baada ya kujulikana  ya kuwa binamu yake amepewa tenda ya kuchimba mafuta yaliyopo nchini humo.
Rais Hamid Karzai amekumbwa na shutuma hizo, baada ya  ya binamu yake ambaye anaye miliki kampuni ya Rashi na Reteb Popal kupewa tenda ya kuchimba mafuta pamoja na kampuni moja toka Uchina.
Binamu huyo wa rais Karzai, ambaye alishawahi kufungwa nchini Marekani kwa makosa ya kusafirisha na kuuza madawa ya kulevya  miaka ya 1990s, amepatiwa mkataba kuchimba mafuta yaliyopo katika bonde la Amu Darya kwa miaka 25.
Nchi ya Afghanistan inaaminiwa kuwa na madini tofuti yenya thamani, mafuta na gasi yenye kufikia kiasi cha paund za Uingereza  £2trillion.
China na Brazil kubadilishana pesa kibiashara.
Rio de Janeiro, Brazil - 22/06/2012. Serikali za China na Brazil zimekubalia kubadilishana pesa za kupitia banki kuu za nchi hizo.
Uamuzi huo umekuja baada ya viongozi wa nchi hizo hao kukaa na kujadili ni mbinu gani zifanyike ili kudhibiti myumbo wa kifedha kati ya nchi hizo mbili.
Mabadilishano hayo ya fedha ambayo yata ziruhusu nchi hizo mbili kubadilishana kiasi cha 60billion Brazilian reais na 190 China yuan sawasawa na paundi za Uingereza 31billion, jambo ambalo litafanya nchi hizo kuweza kufanya biashara bila vikwazo kati ya nchi hizo.
Wabunge nchi Zimbabwe wakubali kutailiwa. 
Harare, Zimbabwe -22.06/2012. Baadhi ya wabunge nchini Zimbabwe wamekubali kutailiwa ili kuwa mfano mzuri kwa wananchi ikiwa katika harakati za kupambana  ugonjwa wa ukimwi.
 Blessing Chebundo  ambaye ni Mwenyekiti wa bunge la Zimbabwe alisema " nivizuri kwa wabunge kuonyesha mfano, kwani sisi sote tupo katika harakati ya kupambana na ugonjwa wa ukimwi na kama viongozi ni muhimu kuonye mfano bora kwa wananchi."
Kampeni ya kuwataka viongozi wawe mfano bora wa kupambana na ukimwi ilianzishwa na makamu wa waziri mkuu Bi Thokozani Khupe mwaka 2011.
Uamuzi wa wabunge hao kuamua kutailiwa kumekuja baada ya wachunguzi wa maswala ya kiafya kutoa ripoti ya kuwa mtu aliye tailiwa hana hatari ya kuambukiza ugonjwa wa ukimwi kiurahisi.

Uingereza yamnyima viza mkuu wa Olyimpik wa Syria.
Islamabad, Pakinstan - 22/06/2012. Serikali ya Uingereza imekataa kumpa viza mkuu wa  michezo ya Olyimpik wa Syria.
Mowaffak Joumaa ambaye pia ni mkuu wa jeshi, amekataliwa viza ya kuingia nchini Uingereza kwenye michezo ya kimataifa ya Olyimpik itakayo fanyika hivi karibuni.
Habari zilizo patikana zinasema "uamuzi huo ulichukuliwa katika kikao kilicho fanyika kati ya wakuu wa ofisi ya mambo ya nje ya nchi na wizara ya michezo na utamaduni."
Uamuzi huo wa serikali ya Uingereza kumyima viza mkuu huyo wa maswla ya Olyimpik wa  wa Syria utakabidhishwa kwa viongozi wanaosimamia michezo ya Olyimpik siku chache kuanzia sasa.
Swala la Serikali ya Uingereza kumkatalia viza ya kuingia mkuu huyo wa Syria, umekuja kutoka na mvutano wa kidiplomasia uliyopo kati ya nchi hizi mbili.

Wednesday, June 20, 2012

Viongozi wa Somalia kufanya mkuutano wa kuungana.

Viongozi wa Somalia kufanya mkuutano wa kuungana.


London, Uingereza - 20/06/2012. Wakuu wa Somaliland na Somalia wanatarajiwa kufanya mazungumzo nchini Uingereza ili kuweza kuzungumzia jinsi ya kuunganisha nchi hizo.
Mazungumzo hao ambayo wanatarajiwa kufanyaka nchini Uingereza London katika sehemu ambayo haijatajwa yanania ya kuiwezesha Somalia na Somaliland kuwa  Jamuhuri au kuwa nchi moja.
Somalialanda imekuwa na amani tangu kuanguka kwa serikali ya rais Muahmad Siad Barre 1991, huku upande wa Somalia ya Kusini Mogadishu umekumbwa na machafuko ya kutokuwa na amani na vita ambavyo vimeleta  athari kubwa kwa watu na mazingira.

Mkutano wa G20 nchini Mexico wamalizika.

Los Cobos, Mexico - 20/06/2012. Wakuu wa nchi zilizo tajiri na zile  zinazo kua  kiuchumi wamemaliza kikao na kuagiza kukuza uchumi na kuongeza ajira.
Wakuu hao ambao wa mekubaliana kwa pamoja ya kuwa uchumi wa dunia umepata changamoto katika kila nyaja na ipo haja ya kutumia kila mbinu ili kuimalisha hali ya uchumi wa dunia na kuinua maisha ya raia wa kila nchi.
Mkutano huu umekuja wakati myumbo wa uchumi duniani umekuwa ikiwapa vichwa kuuma wakuuwa nchi kila wanapo kutana tangu mwaka 2008 na hadi sasa bado wanajaribu kutafutia jibu sahihi, 
Julian Assange achukua ukimbizi ubalozi wa Ekuado.

London, Uingereza - 20/06/2012. Mwanzilishi wa mtandao wa Wikileaks amekimbilia ubalozi wa Ekuado uliyopo Uingereza na kuomba ukimbizi.
Julian Assange aliomba ukimbizi kweye ubalozi wa Ekuado jana, baada ya rufaa yake ya kutaka kesi inayo mkabili ya ubakaji isikilizwe upya kukataliwa na mahakama  nchini Uingereza.
Vaunghan Smith ambaye ni rafiki wa Julian Assange alisema " Assange anaogopo kwani akirudishwa Sweden kunauwezekano mkubwa akapelekwa Marekani, kwani anatakiwa na nchi hiyo kwa kutoa siri za nchi hiyo."
Julian Assange anakabiliwa na kesi ya ubakaji nchini Sweden, jambo ambalo amekanusha na alikuwa amewekewa dhamana na watu wake wakaribu ambao hata wao wanadai kushutushwa na kitendo hicho cha kuchukua ukimbi katika balozi za Equado zilizopo London  nchi Uingereza.

Hatimaye Ugiriki yapata serikali.

Athens, Ugiriki -20/06/2012. Wananchi wa Ugiriki wapeta serikali baada ya uchaguzi ambao ulitoa mgwanyo wa matokeo ambao ulifanya serikali ya shirikisho kuundwa.
Antonis Samaras 16 aliyekuwa mshidi kupitia chama cha New Democras Part ameapishwa kuwa waziri mkuu wa Ugiriki baada ya kukubaliana kuunga serikali na chama cha Greece's socialist PASOK.
 Waziri Mkuu Antonis Samaras anakabiliwa na kazi ngumu ya kuhakikisha uchumi wa Ugiriki unarudi katika hali ya kawaida na huku kukubali matwakwa  yaliyoamliwa na nchi za muungano wa Ulaya ya kuwa ili Ugiriki ipatiwe pesa za kuinua uchumi, ni lazima ifanye mabadiliko ya miundo uchumi kwa kubana matumizi katika sekta tofauti jambo ambalo baadhi ya wanchi wa Ugiriki wanalipinga.

Monday, June 18, 2012

Mazungumzo juu ya Iran na nyuklia yaanza nchini Urusi

Rwanda yafunga rasmi koti za Gacaca - Gachacha,


Kigali, Rwanda - 18/06/2012. Serikali ya Rwanda imefunga rasmi koti zilizo julikana kama Gachacha baada ya miaka 10 tangu zifunguliwe.
Mahakama hizo ambazo zilianzishwa ikiwa ni njia moja ya kutaka kuweka ukweli wa mauaji ya kikabila yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994.
Rais  Paul Kagame alitangaza rasmi kufungwa kwa mahamaka hizo na kutoa shukurani kwa wale wote walio   saidi katika kutafuta haki kwa Wanyarwanda wote.
Kwa mujibu wa serikari ya Rwanda zaidi ya watu 400,000 walifikishwa katika mahakama hizo ambazo mahakimu wake walikuwa  wameteuliwa na jamii kwa kuzingatia uwezo wao wa kupima mambo ya jamii.


Mazungumzo juu ya Iran na nyuklia yaanza nchini Urusi

Moscow, Iran - 18/06/2012.  Mazungumzo yameanza nchini Urusi ilikuzungumzia suala la kinyuklia la nchi ya Iran.
Mazungumzo hayo yanazikutanisha nchi za Iran, Urusi, Marekani, China, Ufaransa, Uingereza na Ujerumani kufuatia yale yaliyofanyika nchi Irak, ambayo haya kuleta jibu sahihi kuhusu Iran na mpango wake wa kinyuklia.
Catherine Ashton ambaye anawakilisha muungano wa nchi za Ulaya alisema " tutajitahidi kuongea na Iran ili iweze kukubaliana na jumuiya ya kimataifa kuhusu suala lake la kinyuklia."
Mazungumzo ambayo yanafanyika nchini Urusi yanatarajiwa kutoa utata  japo kuwa Iran, imesha tamka hapo awali kabla ya kuanza mazungumzo haya ya "kuwa hakutakuwa na mabadiliko juu ya haki nchi hiyo katika suala la kinyuklia kwani ni haki yake"kwani ni haki ya kila nchi

Sunday, June 17, 2012

Mahakama ya Kimataifa yapata mwanasheria mkuu Mwafrika.

Kamati ya kusimamia usalama na amani nchini Syria yasimamisha kaza zake.


Damascus, Syria - 17/06/2012. Mkuu wa wa kamati iliyo teuliwa na umoja wa mataifa ya kusimamia hali ya kuwepo kwa usalama na kurudisha amani ametangaza kusimamisha huduma zote za kamati hiyo nchini Syria.
Meja Generali Robert Mood akiongea na waandishi wa habari alisema "kamati ya umoja wa mataifa inayosimamia kuletwa kwa usalama nchini Syria imesimamisha kazi zake kufuatia hali ya usalama kwa wafanyakazi wake kuwa katika hali ya hatari."
Wasimamizi wapatao 300 ambao walikuwa na kazi ya kuhakikisha hali ya usalama nchini Syria wamekuwa na wakati mgumu katika kazi zao kufuatia kutokuwepo kwa makubaliano ya kusimamisha mapigano kati ya jeshi la serikali ya Syria na kundi la upinzani jambo ambalo linamefanya kazi zao kuwa ngumu kwa kuhatarisha usalama wao.

Mahakama ya Kimataifa yapata mwanasheria mkuu Mwafrika.

Hague, Uhollanzi - 17/06/2012.  Mahakama ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu iliyopo nchini Uhollanzi imepata mwanasheria mkuu mpya wa mahakama hiyo.
Fatou Bensouda 51, aliapishwa kuwa mwanasheria mkuu wa mahakama hiyo siku ya Ijumaa 15/06/2012 ili kuchukua nafasi iliyo achwa na aliyekuwa mwanasheria mkuu wa mahakama hiyo Luis Moreno Ocampo ambaye ameachia madaraka hayo ambayo alikuwa anayashikilia tangu 2003.
Bi Fatou Bensouda mzaliwa wa Gambia alikuwa msaidizi wa Luis Moreno Ocampo tangu mwaka 2004 na amekuwa Mwafrika wa kwanza kushukuwa madaraka ya juu katika mahakama hiyo ya kimataifa tangu kuanzishwa.

Aung San Suu Kyi apokea zawadi yake ya Nobel.

 Aslo, Norway - 17/06/2012. Mwanaharakati, mwanasiasa na mtetezi wa haki za binadamu kutoka nchini Myanmar amezawadiwa zawadi Nobel ambayo alitunikiwa mwaka 1991.
Aung San Suu Kyi ambaye alikuwa amefungiwa kutoka katika nyumba aliyokuwa akiishi  kwa muda miaka 21 na serikali ya kijeshi ya nchi yake, alipokea zawadi hiyo jiji Aslo, na kutoa shukurani kwa wale tote waliokuwa muunga mkono wakati wa kifungo chake na kwa kuongeza kusema " zawadi hii ni changa moto na isiishie hapa bali iwe ufunguo kwa wale wote ambao wapefungwa na lazima waachiwe huru."
Aung San Suu Kyi, alishindwa kupokea zawadi hii ya Nobel mwaka 1991 kwa kuogopa ya kuwa akiondoka nchini huenda asiruhusiwe kurudi nchini mwake.

Wednesday, June 13, 2012

NATO haina mpango wa kivita kwa nchi ya Syria.

Polisi wawakamata vinara wa vurugu jiji Warsaw.

Warsaw, Poland - 13/06/2012. Mamia wa wapenzi mchezo wa kandanda nchi Poland waliingiwa na mshangao baada ya washabiki kutoka nchi Urusi na Poland kupambana katika mitaa ya jiji la Warsaw.
Mashabiki hao walipambana kabla ya mmpambano kati ya timu ya taifa ya Urusi na Poland kuanza.
Msemaji wa polisi alithibitisha kukamtwa kwa watu 120 na watu zaid ya 10 waliumia vibaya.
Mashabiki hao walipambana kufuatia historia ya nchi hizi mbili, ambapo Urusi ilishawahi kuitawala Poland, jambo ambalo husababisha mvutano mkubwa kati ya nchi hizi mbili.

NATO haina mpango wa kivita kwa nchi ya Syria.

Sydney Australia - 13/06/2012. Katibu mkuu wa shirikisho la ulinzi la nchi za Ulaya na Amerika (NATO) ameagiza kuwepo na suruhusho la kisiasa nchi Syria.
Anders Fogh ambaye yupo ziarani nchi Australia alisema " Swala la Syria linabidi kusuruhishwa kimazungumzo  na NATO haita jiingiza kijeshi katika mgogoro wa Syria."
Katibu Anders Forgh yupo nchini Australia ili kuimarisha ushirikiano na nchi hiyo ambayo ni mshiriki wa NATO.

Jiji la Baghdad la kumbwa na milipuko.

Baghdad, Irak - 13/06/2012. Jiji la Baghdad limekumbwa na milipuko ya mabomu na kuu watu 57.
Mabomu hayo ambayo yalilipuka kwenye eneo linalo fanyika sherehe za hija za waumini wa dini ya Kislam wa Shia wakati walipokuwa wanatoa sadaka za vyakula na bidhaa nyingine.
Kundi linalo shirikiana na kundi la Al Qaeda lilipo nchini Irak limedai kuhusika na mashambulizi hayo

Wednesday, June 6, 2012

Marekani kutafuta mshiriki mpya kiulizi.

Viongozi wa nchi za Pasifiki na Asia ya kati wakutana nchini China.

Shanghai, China - 06/06/2012.  Viongozi wa nchi za Pasifiki na Asia ya Kati wamekutana nchini China ili kuzungumzia maswala ya  ulinzi , usalama na kukuza ushirikiano wa kiuchumi.
Mkutano huo ambao watakuwepo viongozi na  marais wa Urusi, Iran na wengine ulisimamiwa na rais wa China  Hu Jintao ambaye ni rais mwenyeji.
Rais wa China Hu Jintao alisema " tutaendelea kujenga na kulinda eneo letu, japo kutakuwa na nguvu kutoka nje ya maeneo ya yetu,  na tutashinda.
Na tutafanya kila njia amani inapatikana nchi Afghanistan." Aliongezea rais Hu Jintao.
Mkutano huo unao julikana kama Shanghai Cooparation Organization umetimiza miaka 12 tangu kuanziashwa kwa madhumuni ya kuimairisha uhusiano wa karibu wa nchi zilizopo  katika maeneo ya Pasifiki na Asia ya Kati.

Marekani kutafuta mshiriki mpya kiulizi.

New Dheli, India - 06/06/2012. Waziri wa Ulinzi wa Marekani amefanya ziara ya kiserikali nchini India na kuzungumza na viongozi wa India kuhusu maswala ya kiulinzi na usalama kati ya nchi hizo mbili.
Ziara ya Waziri Leon Panetta inachukuliwa " ikiwa ni moja ya sera za kiulinzi za  Marekani ili kupata mshiriki mpya katika eneo la India na Pasifiki, baada ya uhusiano wa Marekani na Pakistani kuonekana kuyumba." alisema George Little ambaye ni mmoja  wa msemaji  wa Pentagon.
India imekuwa nchi ambayo inakuwa kiuchumi na kiulinzi na kuvutia mahusiano na nchi zenye nguvu kijeshi kama Urusi na China  hivi karibuni. 

Al Qaeda yapata pigo.

Washington, Marekani - 06/06/2012. Serikali ya Marekani imethibitisha ya kuwa mmjo wa viongozi wakuu wa kundi la Alqaeda ameuwawa.
Habari zilisema "Abu Yahya al Libi aliuwawa na baada ya ndege ya aina ya drone kushambulia eneo alilo kuwa amejificha.
Kifo cha Libi ni pigo kubwa kwa kundi hilo la Al Qaeda, kwani alikuwa ni mtu anaye panga mipingo ya kundi hilo." Ikulu ya Marekani ilisema."
Kuu wawa kwa viongozi wa kundi la Al Qaeda kumekuwa kukiendelea na kundi hili ndilo linalo husika katika ugaidi.

Malkia Elizabeth atoa shukurani kwa watu wote. 

London, Uingereza - 06/06/2012. Malkia Elizabeth wa Uingereza  ameanda chakula cha mchana na viongozi wa nchi Commowealth ikiwa ni moja ya katika sherehe za kuadhimisha miaka 60 tangu atawazwe kuwa Malikia.
Malkia Elizabeth aliwashukuru watu wote walio kuwa pamoja naye kisala na furaha katika uongozi wake na siku hii ambayo amefikisha miaka 60 ya Umalkia.
Sherehe hiyo ya pamoja kati ya Malkia Elizabeth na viongozi wa Commonwealth itafanyika katika ukumbi wa Marlborough Pall Hall uliyopo katika ya jiji la London ikiwa ni moja ya ishara ya kuwashukuru viongozi hao wa nchi ambazo zilitawaliwa na Mwingereza.
Malkia  Elizabeth wa Uingereza ni kiongozi wa kwanza katika karne ya hii kukaa katika madaraka kwa muda wa miaka 60, na sherehe hizo zilimalizika 05/06/2012, ambapo mamilioni ya Waingereza waliungana na Malkia kusherekea sikuku hiyo.

Monday, June 4, 2012

Wananchi wa Uingereza washerekea pamoja na Malkia kwa kutimiza miaka 60 ya Umalkia.



London, Uingereza - 04/06/2012. Wananchi wa Uingereza wapo wanamesherekea sikuku ya kutimiza miaka 60 ya  utawala wa Malkia Elizabeth tangu atawazwe kuwa Malkia wa Uingereza.
Sikuku hiyo iliyopewa jina Diamond Jubiles, ambayo itachukuwa siku mbili kwa kuanza tarehe 03/06/2012 na kuishia 04/06/2012, ilishangiliwa kwa pamoja na Malkia Elizabeth huku akiwa ndani ya boti iliyokuwa ikipita katika mto mkubwa unao julikana kwa jina la Thames uliyopo jijini London ikiwa ni moja ya njia ya kuadhimisha sherehe ya miaka 60.
Malkia Elizabeth amekuwa mmoja ya  Malkia walio kaa katika kiti cha Umalkia kwa muda mrefu kulinganishana na viongozi wengine wa Kifalme waliopo duniani. 

Kiongozi wa Iran adai Iran inanguvu zaidi kuliko miaka ya nyuma.

 Tehran, Iran - 04/06/2012. Kiongozi mkuu wa Iran ametangaza ya kuwa Iran ina nguvu za kutosha kulinganisha na miaka ya nyuma.
Ayatollah Sayyed Ali Khamenei akiongea katika siku ya kumkumbuka ya kutimiza miaka 23 ya  kiongozi aliye ongoza mapinduzi Ayatollah Sayyed Rouhallah Khomeini kwa kusema " leo Iran inanguvu kulinganisha na miaka ya nyuma iliyopita baada ya mapinduzi na maadui wanaiogopa Iran siyo kwa nguvu za kinyuklia bali kama Iran nchi ya Kiislaam.
"Nguvu ilizo nazo irani ni za kisiasa na ushawishi mkubwa katika kuhamasisha nchi za jumuiya ya kimataifa ili kujijenga zenyewe na Iran haita tengeneza bomu la nyuklia kamwe."
Mazungumzo hayo ya kiongozi huyo mkuu wa Iran yamekuja huku mazungumzo ya kuhusu Iran na mradi wa kinyuklia kuisha hivi karibuni nchini Irak bila kufukia maaafikiano.


Ajali ya ndege yaua watu 153 nchini Nigeria.

Lagos, Nigeria - 04/06/2012. Watu wapatao 153 wamepoteza maisha baada ya ndege iliyo kuwa imewabeba kugonga maghorofa yanayokaliwa na raia katika jiji la Lagos.
Horald Denuren ambaye ni msemaji wa maswala ya anga alisema " ndege ambayo ilikuwa ikitokea Abuja kuja Lagos imeaanguka na kupoteza maisha ya watu  na pia kusababisha uharibifu mkubwa katika eneo iliyo anguka ndege hiyo."
Kufuatia ajali hiyo, rais wa Nigeria ametangaza siku tatu za maombelezi kutoka na vifo vya vilivyo sababishwa  na ajali hiyo ya ndege.
Ajali hiyo ya ndege nchini Nigeria inafuatia ajali ya ndege iliyotokea nchi ya jirani ya Ghana na kuuwa watu kumi baada ya ndege hiyo kutua kwenye kituo cha mabasi kilichopo karibu na uwanja wa ndege.

Rais Bashar al Assada adai nguvu za kutoka nje zinavuruga amani.

Damascus, Syria - 04/06/2012.  Rais wa Syria amehutubia  baraza la bunge jipya wakati hali ya kiusalama inazidi kuzorota  nchi Syria na kuashiria hali ya kuzuka vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Rais Bashar al Assad akihutubia bunge alisema " Syria ipo katika vita vinavyo sababishwa kwa nguvu kutoka nje ya nchi na mauaji yaliyo tokea hivi karibubi huko Haula yamefanywa na watu wenye roho za kinyama na wasio na utu.
"Tunapigana na ugaidi lakini vita vyote vinapangwa na kupiganwa nchi mwetu na damu za Wasyiria kumwagika hata hivyo tutashinda vita zidi ya ugaidi huo."Bashar al Assad aliyasema hayo wakati alipo kuwa akongea na  wabunge waliochaguliwa hivi karibuni.

Saturday, June 2, 2012

Hosni Mubaraka ahukumiwa kukaa jela maisha.

Hosni Mubaraka ahukumiwa kukaa jela maisha.

Kairo, Misri - 02/06/2012. Aliyekuwa rais wa Misri amehukumiwa kukaa jela maisha, baada ya kukutwa na hatia ya kushindwa kusimamisha vurugu zilizo pelekea mauaji ya raia.
Hosni Mubaraka 84 alihukumiwa adhabu hiyo, yeye pamoja na aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Habib al Adli.
Hosni Mubaraka ambaye alitolewa madarakani baada ya mapinduzi ya maandamano yaliyo fanyika Februari  2011 kufuatia mlolongo wa mapinduzi ya kisiasa yaliyoko katika maeneoa ya nchi za Kiarabu.

Putin akanusha ya kuwa Urusi yaisaidia serikali ya Syria.

Berlin, Ujerumani - 02/06/2012. Rais wa Urusi amekanusha  ya kuwa Urusi inaiunga mkono serikali ya Syria.
Rais Vladmir Putin ambaye  amefanya zaiara  nchini Ujerumani na ya nje ya nchi kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa rais wa nchi hiyo.
Akiwa ziarani nchi Ujerumani Putini alisema " Urusi haiungi mkono upande wowote wa matatizo ya Syria, ila tunachounga mkono ni mpango wa Kofi Annan."
Rais Putin aliyasema hayo baada ya waziri wa mambo ya nje wa Marekani Hillary Clinton kudai ya kuwa Urusi inaisadia serikali ya Syria na ndomaana hali inazidi kuwa mbaya nchi humo. 
Putin alikutana na Kansera wa Ujerumani Angela Markel  na kukubaliana kwa pamoja ya kuwa ya kuwa swala la Syria lazima lisuruhishwe kwa kupita mazungumzo na siyo vita..

Ban Ki-moon aagiza Somalia kupatiwa msaada zaidi wa kiusalama.

Instambul, Uturuki - 02/06/2012. Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa ameagiza jumuiya ya kimataifa kuisaidia serikali ya  mpito ya Somalia katika kujenga nchi japo inakabiliwa na wakati mgumu.
Ban Ki-moon alisema "swala la usalama wa Wasomalia lazima lizidishwe nguvu kutoka pande zote za jumuiya ya kimataifa ili Somalia irudi iweze kurudi kuwa nchi ya maendeleo ya mazuri."
Mkutano huo, ambao uliitishwa ili kuangalia ni kwa kiasi gani jumuiya ya kimataifa inaweza kuisaidia Somalia, na hasa katika swala la kuleta amani nchini humo.
Serikali ya mpito ya Somalia imekuwa ikipambana na kundi la Al Shabab, ambalo linapingana naserikali hiyo ya mpito na kusababisha hali ya usalama kuwa tete na wanachi kushindwa kuijenga nchi.