Hali ya afya ya waziri mkuu wa zamani wa Izreal ipo tete.
Jerusalemu, Izrael 01/01/2014. Afya ya aliyekuwa waziri mkuu wa Izrael, Ariel Sharon inazidi kudorola siku hadi siku toka alipofanyiwa upasuaji wa na kuwekewa mirija ya kupitishia chakula mwezi Septemba mwaka jana.
Amir Marom, ambaye ni msemaji wa hospital ya Hashomer alipo lazwa Sharon alisema kuwa " nikweli hali ya Sharon siyo nzuri kiafya na madakitari bado wapo wanafuatilia afya yake kwa ukaribu."
Kwa mijibu wa habari zinasema kuwa hali ya afya ya Ariel Sharoni ilianzakudhoofika mara baada ya viungo vyake vya ndani ya mwili kushindwa kufanya kazi vizuri. Lakini hazikueleza lini matatizo hayo yaliianza.
Waziri mkuu Arel Sharon 85 ambaye ni mwanzilishi wa chama cha Kadima, alilazwa hospital tangu mwaka January 4, 2006, baada ya kupata ugonjwa wa kiharusi, ambao ulimsababishia kutoka katika ulingo wa siasa nchi Izrael.
Balozi wa Palestina auwawa kwa bomu.
Prague, Czecheslovakia - 01/01/2014. Balozi wa Palestina nchini Czecheslovakia, ameuwawa kwa bomu kwenye jengo analo ishi katika jiji la Prague.
Akithibitisha kuwepo na mlipuko wa bomu, msemaji wa polisi Andrea Zoulova amasema "balozi Jamal al Jamal alifariki mara baada ya kufikishwa hospitali"
Na habari kutoka kwa ofisi ya mambo ya nje ya nchi ya Wapalestina imesema " mlipuko wa bomu ulitokea wakati balozi, Jamal al Jamal alipo kuwa akijaribu kufungua kabati iliyokuwa imeletwa kutoka ofisi za zamani za ubalozi huo"
Hata hivyo serikali ya nchi Czechslovakia haija thibitisha kuwa mlipuko huo unahusika na ugaidi.