Sunday, October 25, 2009

Kansellar Angel Markel ateua serikali mpya.

Wapalestina na Waizrael bado kukubaliana kimsingi haki zao Jerusalem Mashariki, Izrael - 25/10/09. Polisi wa Izrael wamevamia msikiti wa Al Aqsa na kupambana na waumini wa Kiislaam wengi wao wa kiwa Wapalestina. Kufuatia kuvamia eneo la msikiti huo wa Al Aqsa, waumini wa dini ya Kiislaam wengi ambao ni Wapelestina walianza kutupa mawe na huku polisi wa Izrael wakitumia mabomu ya kutoa machozi. Kwa mujibu wa shirika la kuktetea haki za binanadamu, limesema ya kuwa kuna baadhi ya watu walikamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi wa polisi. Picha hapo juu anaonekana mmoja wa kijana wa kipalestina akirusha jiwe kuelekea walipo polisi na huku wapiga picha wakiwa kazini kupata picha kamili ya matukio. Jeshi la serikali la kamata miji iliyokuwa chani ya Taliban. Islamabad, Pakistan -25/10/09.Serikali ya Pakistan, imetangaza yakuwa imekamata mji wa Kusini mwa Waziristan ambao umezungukwa na milima. Kwa mujibu wa masemaji wa jeshi, alisema yakuwa waliweza kupambana na kundi la Taliban na mshiriki wake Al-qaed kwa muda wa wiki moja na kufanikiwa kukaribia mji amabo kiongozi wa Taliban, Hakimullah Mehsud. Kufuatia mapambano hayom, maelfu ya watu wamekimbia maeneo yao kwa ili kuokoa maisha yao. Picha hapo juu wanaonekana wanachi wakiwa wanakimbia kuepuka kipigo kutoka kwa mmoja wa wanajeshi ambaye ana jaribu kuwatuliza wakimbizi waliokimbia vita vinavyo endelea nchini Pakistan kupambana na ugaidi nchini humo. Kansellar Angel Markel ateua serikali mpya. Berlin, Ujeruman - 25/10/09. Kansellar Angel Markel, ametangaza serikali mpya itakaoyo iongoza Ujerumani hasa katika kipindi hiki cha kupapamba na kuinua uchumi wa nchini hiyo. Serikali mpya chini ya uongozi wa Bi, Angel Markel imeteua Wolfgang Schauble kuwa waziri wa fedha amabye atakuwa na kibarua kigumu cha kujaribu kuangali maswala ya pesa na kupunguza kodi za mapato kuanzia mwezi januari mwakani. Picha hapo juu, anaonekana Bi, Angel Markel akiongea mbele ya wanachama wa chama chake mapema wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mapema mwaka huu. Baghdad yashutushwa na hali ya milipuko ya mabomu. Baghdad,Irak - 25/10/09. Mabomu yamelipuka karibu na ofisi za serikali ya Irak na kupoteza maisha ya watu 108 na kujeruhi watu wasiopungua 512. Kwa mujibu wa habari , huenda idadi ya watu watakao poteza maisha ikaongezeka kutokana na milipuko hiyo ya mabomu. Serikali ya Irak, imelaaani kitendo hicho na kudai yakuwa ni kitendo cha kulaani wa na jumuia ya kimataifa na lazima kupigana na hali hii kwa hali na mali. Picha hapo juu, unaonekana moshi ukielekea juu, baada ya bomu kulipuka karibu na ofisi za serikali.

Friday, October 23, 2009

Uchumi wa China wapata nafuu.

Uchumi wa China wapata nafuu. Beijing, China 23/10/09. Serikali ya China imetangaza ya kuwa hali ya uchumi wa nchi hiyo umepanda kwa kiasi cha asilimia 8%, kwa muda mfupi tangu dunia kukumbwa na tetemeko la kiuchumi. Kwa mujibu wa serilikali, kupanda kwa hali ya kiuchumi, kumekuja baada ya matumizi ya nje na ndani kuelekea kufanya vizuri kibiashara. Picha hapo juu ni ya bendera ya China, nchi ambayouchumi wake na maendeleo yake ya kiuchumi duniani yamekuwa yakienda vizuri. Wanchi wa Kenya waishitaki Uingereza kwa makosa ya miaaka ya 1950-60s.

London, Uingereza - 23/10/09. Raia wa Kenya watano wameishitaki serikali ya Uingereza kwa kosa la kuwatesa na kuwanyanayasa wakati wa miaka 1950 - 60, wakati wa harakati za kugombea uhuru wa Kenya.
Kufuatia ushahidi uliopo, unaonyesha yakuwa serikali ya Uingereza iliwafunga maelfu ya watu katika kambi na kuwatesa.
Hata hivyo,ofisi ya mambo ya ndani ya Uingereza, haikutaka kuoelezea lolote kutokana na habari hizi.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Kenya, nchi ambayo wananchi wake waliteswa vibaya wakati walipo kuwa wakigombea uhuru.
Picha ya pili ni ya bendera ya Uingereza,nchi ambayo ilikuwa ikitawala Kenya, kabla ya vita vya Mau Mau kuanza.

Monday, October 19, 2009

Mwaka 2009 hakuna kiongozi bora wa Afrika.

Mwaka 2009 hakuna kiongozi bora wa Afrika. London,Uingereza - 19/10/09.Shirika linalo simamiwa na mfanyabiashara mwafrika, Ibrahim Mo, limetangaza mwaka 2009 halitatoa zawadi kwa kiongozi yoyote wa Afrika. Akiongea leo jijini London, Ibrahim Mo, alisema kamati inayo simamia uchaguzi wa viongozi bora wa Afrika, imekosa kiongozi wa Kiafrika ambaye amekamilisha matakwa ya kiongozi kupewa zawadi na shirika hilo. Zawadi hiyo hutolewa kwa viongozi wa Afrika ni kiasi cha dola za Kiamerika Milllion tano na dola laki lakimbili killa mwaka hutolewa kimaisha mpaka hapo mteuliwa watakapo aga dunia. Picha hapo juu anaonekana, Ibrahim Mo, akiongea leo mbele ya wajumbe wa kamati waliokuja kushuhudia ni nani amechaguliwa kuwa kiongozi bora wa Afrika wa mwaka 2009, alitangaza yakuwa mwaka 2009 hakupatikana kiongozi aliye fikisha matakwa ya kuwa kiongozi bora wa Afrika. Mauji nchini Iran yaleta kushutumiana na nchi majirani.

Tehran, Iran - 19/10/09.Rais wa Iran,Mahmoud Ahmadinejad, ameilamu Pakinstan kwa kuhusika na mauaji ya kujitolea muhanga ambayo yamesababisha vifo ya wakuu wa kijeshi wanchi hiyo pamoja na baadhi ya wananchi.
Hata hivyo serikali ya Pakistan, imekanusha madai hayo.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Iran, ambaye ameilaumu Pakistan kwa kuhusika na mauaji nchini Iran.
Hamid Karzai na wagombea wenzake kukwaana tena katika kiti cha urais.
Kabul,Afghanistan - 19/10/09. Kamati inayosimamia uchaguzi nchini Afghanistan ambayo ipo chini ya Umoja wa Mataifa, imetangaza yakuwa uchaguzi uliofanyika nchini humo ulikuwa na ukiukwaji washeria.
Kufuatia ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, upo uwezekano mkubwa wa wananchi wa Afghanistan
kurudia kupiga kura kumchagua rais wa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa katiba ya Afghanistan, mgombea kiti cha urais lazima apatekura nyingi zaidi ya asilimia 50%.
Picha hapo juu, anaonekana Amid Karzai, akihutubia mbele ya mkutano wa umoja wa mataifa wakati akiwa rais wa Afghanistan mwaka jana.

Wednesday, October 14, 2009

China na Urussi kutiliana mkataba wa kibiashara.

Wanajeshi kuongezwa nchini Afghanistan"Waziri mkuu wa Uingereza atangaza".

London, Uingereza - 14/10/09. Waziri mkuu wa Uingereza,Gordon Brown,ametangaza yakuwa serikali ya Uingereza itapeleka wanajeshi wapatao 500, nchini Afghanistan.
Kutangazwa kwa idadi hiyo ya wanajeshi watakao kwenda nchini Afghanistan, kunakuja baada ya habari za kuaminika yakuwa Taliban na washiriki wake kuendelea kukua na kuongeza mapambano na majeshi ya NATO na washiriki wake, hali ambayo ikiachiwa hivi huenda ikawa mbaya zaidi hapo baadaye.
Hata hivyo uamuzi wa serikali ya Uingereza, kupeleka wanajeshi wake nchini Afghanistan,kunakuja wakati wananchi wa Uingereza wanakuwa na wasiwasi kuhusu hali halisi ya vita hivyo, ambavyo toka vimeanza vimekuwa vina toa matokeo tofauti kwa jamii nzima ya Waingereza.
Picha hapo juu, anaonekana, waziri mkuu wa Uingereza , Gordon Brown, akiwa anashikilia kichwa, kwani uamuzi wake unamweka katika njia ya panda.
Picha ya pili, anaonekana, waziri mkuu wa Uingereza, Gordon Brown, akiongea na wanajeshi, mapema alipo kwenda kuwatembelea, ili kuangalia hali halisi.
China na Urussi kutiliana mkataba wa kibiashara.
Beijing, China -14/10/09. Waziri mkuu wa Urussi, Vladamir Putin, na waziri mkuu wa China Wen Jiabao,wametiliana mkataba wa kibiashara kati ya nchi hizi mbili zenye thamani ya 3.5billion.
Mikataba hiyo,kati ya Urussi na China, ulisainiwa mapema wiki hii, kabla ya kuanza kwa mkutano wa nchi za zenye mali ya asili zilizopo katika aneo la Asia.
Kwa mujibu wa wachunguzi wa maendeleo ya jamii, wanasema kushirikiana kwa kwaribu, kati ya nchi hizi mbili, kunazipa muda mgumu sana nchi za Ulaya magharibi na Amerika, kwa kutaleta ushindani mkubwa wa kimazingira.
Picha hapo juu, wanaonekana, kushoto, waziri mkuu wa Urussi, Vladmir Putin, akipongezana na waziri mkuu wa China, Wen Jiabao, kulia, mara baadaya kumaliza kutiliana mikataba ya kibishara na maendeleo ya nchi hizi mbili.
Umoja wa Ulaya, wataka kiongozi wa Guinea ashitakiwe.
Brussel, Ubeligiji - 14/10/09.Muungano wa Umoja wa Ulaya, umetoa wito yakuwa kiongozi wa kijeshi aliopo madarakani chini Guinea, Kaptain, Mussa Kamara, kufikishwa mbele ya sheria ili kukabiliana na mashitaka ya kukiuka haki za kibinadamu, wakati wa kuzuia maandamano,ambayo yaliandaliwa vyama vya upinzani.
Kwa mujibu wa mjumbe wa maendeleo ya umoja wa ulaya,Karel de Gucht, alisema yakuwa mkuu huyo wa jeshi,Kaptain, Mussa Kamara,anahusika na mauaji ya watu wasipungua 150, wakati walipo uwawa, tarehe 28, Semptemba,mwaka huu.
Hata hivyo , kiongozi huyo, wakijeshi alisema yakuwa hahusiki na mauaji ya watu hao.
Picha hapo juu, anaonekana, kiongozi wa Guinea, Kamptain,Mussa Kamara, ambaye ndiye kiongozi wa sasa wa Guinea.
Picha ya pili,wanaonekana wanajeshi wakiwa kazini kupambana na waandamaji katika jiji la Konakri.
Vifo vya watu ni namba isiyo julikana nchini Iraq.
Baghdad, Irak 14/10/09.Wizara inayo shughulikia haki za binadamu, imesema watu wapatao 85,000, wamepoteza maisha yao kati ya mwaka 2004- 2008, kutokana na vita vilivyo pelekea kung'olewa madarakani, aliyekuwa rais wa Irak, hayati , Saddam Hussein.
Kwa mujibu wa habari hizo , ni kwamba idadi ya namba hiyo ya watu waliopoteza maisha, imepatikana, kutokana na kuwepo kwa vyeti vya kuzaliwa na kutolewa vyeti vya vifo.
Akiongezea , wizara hiyo ilisema zaidi ya watu wapatao, 147,195, wamajeruhiwa.
Hata hivyo, wizara iliongezea yakuwa kunaidadi ya vifo vingi na majeruhi ambao hazijulikani, na huenda idadi ikawa kubwa zaidi.
Picha hapo, anaonekana mmoja wa mwanajeshi akimsaidia mwenzake ambaye ameumua vibaya,mara ya baada ya kushambuliwa vibaya katika mapambano.
Picha ya pili, wanaonekana wakina mama wawili, wakiwa wanauguza watoto wao, ambao wameumia kutokana na mapigano yaliyopo nchini Irak.
Picha ya pili, wanaonekana, baadhi ya watu wakiwa wanaelekea msibani, baada ya mmoja wa familia alipo poteza maisha baada ya kushambuliwa na bomu.

Thursday, October 8, 2009

Swala la nyuklia lawa kitendawili.

Swala la nyuklia lawa kitendawili.

Washington, Amerika 08/10/09.Rais wa Amerika, Baraka Obama,amekubali kuiruhusu serikali ya Izrael kuweza kufunga milango yake ya kufanyiwa uvchunguzi wa kinyuklia kwa muda wa miaka 40.
Kutokana na habari zilizo patikana kutoka ndani ya Ikulu ya Amerika, zinasema , rais, Obama ,alikubaliana na waziri mkuu wa Izrael, Binyamin Netanyahu,wakati walipo kutana hivi karibuni, rais Obama, alihaidi kuendeleza ule mswada wa uanaosema "Usiulize na usiseme au kuongea"
Hata hivyo wasemaji wa serikali zote mbili walikataa kuelezea kuhusu swala hilo.
Picha hpo juu, wanaonekana, rais wa Amerika, Baraka Obama, akiwa ameinama huku akimsikiliza, waziri mkuu wa Izrael, Binyamin Netanyahu, wakati walipo kutana hivi karibuni jiji Washington.
Picha ya pili ni ya moja ya kombora la Izrael, lenye uwezo wa kubeba siraha ya kinyuklia likijaribiwa kwenda angani.
Lazima tujifunze kuishi na hali hii, "Asema waziri wa mambo ya nje wa Izrael".
Jerusalem, Izrael - 08/10/09. Mjumbe wa serikali ya Amerika,George Mitchell, ambaye anashughulikia maswala ya kuleta amani, Mashariki ya Kati, kati ya Izrael na Palestina, amekutana na waziri wa mambo yanje wa Izrael leo Avigdor Lieberman.
Katika kikao hicho,waziri wa mambo ya nje wa Izrael, Lieberman, alisema swala la amani kati ya Wapalestina na Waizrael kwa sasa haliwezekani na lazima jamii ijifunze kushi na hali hii.
Akitoa mfano wa wa kiwiwa cha, Syprus,Nagorno - Karabakh na Visiwa vya Falkland, dunia imekubali kuhishi na hali hii, hivyo basi wakati umefika kukubali kuishi kwa kuzoea hali hii.
Picha hapo juu, wanaonekana,waziri wa mambo ya nchi za nje wa Izrael,Vigdor Lieberman akimkaribisha mjumbe wa serikali ya Amerika George Mitchell anaye shugulikia swala la kuteta amani kati ya Wapalestina na Waizrael.
Mwanasayansi wa Iran apotea kimiujiza.
Tehran, Iran - 08/10/09.Kuna habari za kutatanisha yakuwa aliyekuwa mchunguzi na mwana sayansi maswala ya nyuklia ya Iran, Shahram Amir, amekimbia kutoka Iran na aliko elekea hakujulikani.
Hata hivyo kwa mujibu wa serikali ya Iran, inadai yakuwa kupotea kwa mwanasayansi huyo miezi mitatu iliyo pita akitokea kuhij Makka, kulifanywa na serikali ya Saudi Arabia na Amerika.
Hata hivyo serikali ya Amerika imekanusha habari hizo, na kusema haina habari za Shahram Amir mahari alipo.
Picha hapo juu,ni ya bendera ya Iran, nchi ambayo imekuwa na msimamo mkali hasa katika swala la haki yake ya kuwa na utaalamu wa kinyuklia.
Taliban, bado tishio, ijapokuwa kuna ulinzi mkali.
Kabul, Afghanistan - 08/10/09.Jiji la Kabul, limekubwa tena na mstuko wa bomu, ambalo lililipua ofisi za ubalozi wa India.
Kwa mujibu wa mashahidi walioshuhudia tukio hilo, walisema mlipuko huo ulitokea muda wa mbili na nusu hasubuhi kwa muda wa aneo hilo.
Kufuatia mlipuko huo watu wapatao 17 wamepoteza maisha yao na zaidi ya watu 63 kujeruhiwa vibaya.
Kufuatia mlipuko huo, kundi la Taliban, limedai yakuwa ndilo lililohusika na mlipuko huo.
Picha hapo juu, wanaonekana askari wa Aghanistan, wakiangalia kwa makini, ni jinsi gani bomu lilivyo haribu majengo ya ubalozi huo.

Saturday, October 3, 2009

Rio de Jainero, wenyeji wa michezo ya Olyimpik 2016"Kwa mara ya kwanza katika udongo wa Amerika ya Kusini.

Rio de Janeiro, wenyeji wa michezo ya Olyimpik 2016."Kwa mara ya kwanza katika udongo wa Amerika ya Kusini".

Copenhagen, Denmark - 03/10/09.Jiji la Rio de Janeiro, limekabidhiwa rasmi kuwa mwenyeji na mwandaaji wa mashindano ya michezo ya Olyimpiki ya mwaka 2016.
Jiji la Rio de Jainero, litakuwa la kwanza katika historia ya michezo ya Olyimpik, kufanyika katika bara la Amerika ya Kusini.
Jiji la Rio de Janeiro, liliibuka kuwa la kwa mbele ya majiji ya Chikago Amerika, Madrid, Uispania na Tokyo Japan.
Akitangaza mbele ya wajumbe walioudhulia,rais wa IOC International Olyimpic Committee,Jacques Rogger,alisema waaandazi wa michezo ya Olyimpik mwaka 2016, ni Rio de Jainero,ni nderemo na shwange zilitawala kwa wajumbe wa Brazili na nchi Brazili, huku rais wa Brazil, Lula da Silva, akiwa anatokwa na machozi ya furaha, kwani alikuwa akiongoza kampeni ya jiji la Rio de Jainero kuwa mwenyeji wa mashindano hayo ya Olyimpik mwaka 2016.
Picha hapo juu, anaonekana rais wa Brazili, Lula da Silva, akiwa amekumbatia bendera ya Brazili kwa furaha sana mara baada ya Brazil kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa michezo ya Olyimpiki ya mwaka 2016.
Picha ya pili wanaonekana, wakazi wa jiji la Rio de Jainero, wakishangilia kwa furaha,baada ya matokeo kutangazwa ya kuwa jiji lao, ndilo mwenyeji wa michezo ya Olyimpiki ya mwaka 2016.
Iran na jumuia ya kimataifa wafikia muafaka kwa muda.
Geneva,Uswisi - Serikali ya Iran, imekubali kuruhusu shirika linalo shughulikia ukaguzi wa nyuklia duniani, IAEA, kwenda nchini Iran kuchunguza, kiwanda cha pili kilichopo miji wa Qom.
Makubaliano hayo yamekuja baada ya mazungumzo marefu yaliyo fanyika nchini, Uswisi Geneva, kati ya wajumbe wa serikali za Amerika,Uingereza,China, Urussi,Ujerumani na Iran.
Akiongea mbele ya waandishi wa habari, waziri wa mambo ya nchi za nje wa muungano wa Ulaya ,Javier Solana, alisema huu ni mwanzo wa kutatua mgogoro huu.
Hata hivyo kwa upande wa Iran, mjumbe wake Saeed Jalili, alisema, Iran haitakubali kusimamishwa kwa mpango wake wa kuendelea na mitambo ya nyuklia kwa ajili ya matumizi ya kawaida na mitambo haitakuwa yakutengeneza siraha za nyuklia.
Picha hapo juu, anaonekana,mjumbe wa Iran Saeed Jalili, akiongea na waandishi wa habari kuhusu hali halisi ya mazungumzo yaliyo fanyika jijini Ganeva.
Picha ya pilini ya waziri wa mambo ya nchi za nje wa muungano wa Ulaya ,Javier Solana, akiongea na vyombo vya habari baada ya mkutano na serikali ya Iran, kuhusu swala nyuklia.
Viongozi wa Izrael na Palestina, wakubalianopo kuna unafuu kwa jamii zao.
Jerusalem, Izrael - 03/10/09.Serikali ya Izrael imewaachia huru wanawake 19, ambao ilikuwa imeshikilia kwa muda mrefu.
Kwa mujibu wa habari toka kwa wachunguzi wa hali ya kisiasa na usalama wa Izrael na Palestina,wamesema yakuwa kuachiwa kwa wanawake hao, kumekuja baada ya makubaliano ya kuwa video ya askari wa Izrael, Girad Shilit itaonyeshwa kwenye mitandao , runinga na kutangazwa kwenye vyombo vya habari, ili kuonyesha ya kuwa askari huyo ni mzima wa afya.
Kwa kuthibitisha makubaliano hayo, kundi linalo mshikilia, Girad Shilit, lilitoa video ya askali huyo na kuikabidhi kwa wajumbe wa nao husika na kupelekwa kwa wazazi wa, Gerad Shilit, na ndipo picha za video kusambazwa kwenye vyombo vya habari.
Picha hapo juu, ni picha ya Girad Shilit,akisoma gazeti,wakati alipo kuwa akipigwa picha tayari kutumwa kwa familia yake kuonyesha yakuwa yupo mzima wa afya.
Picha ya pili,anaonekana mmoja ya wanawake,ambao walikuwa wameshikiliwa na serikali ya Izrael, akiwa amebeba mtoto huku akimpangusa machozi, mara baada ya kukutana wa ndugu na jamaa.
Ufaransa yapata faida kubwa kwa mauzo ya siraha duniani
Paris, Ufaransa - 03/10/09. Serikali ya Ufaransa imeongeza maouzo yake ya silaha kwa kufikia asilimia 13% tangu mwaka 2000..
Mauzo hayo yametokana kufanya biashara na nchi kama, Brazil,Saud Arabia na Morokko.
Kuongezeka huko kwa mauzo ya silaha kwa asilimia 13%,yamekuja baada ya rais wa Ufaransa, Nikolas Sarkozy, kuipa kipaombele ukuzaji wa viwanda vinavyo tengeneza zana za kijeshi na ulinzi nchini Ufaransa na kuweza kuajili zaidi ya wafanyakazi 50,000.
Kwa mujibu wa machunguzi wa maswala ya kijeshi wanasema , makampuni ya Ufaransa yameweza kupata thamani ya Amerikani dolla $9.7billion, na kuwa juu kwa asilimia 7% katika soko la dunia.
Picha hapo juu, wanaonekana , baadhi ya wataalamu wa nchi za Kiarabu wakiangalia kwa na kuonyeshana ni jinsi gani ndege zilizo mbele yao zinaweza kufanya kazi.