Sunday, February 24, 2008

Iran yaitaka Amerika na washiriki wake waiombe radhi

Nyota ya kabumbu ya zamani ya Uingereza kupata matibabu ya kuepuka kilevi.

London , Uingereza - Nyota ya zamni katika mchezo wa mpira wa miguu nchini Uingereza Poul Gascoine, au kwa jina maarufu Gazza, amewekwa kwenye kituo maalumu cha kutibia watu wenye matatizo ya kilevi.
Gazza ambaye alikuwa chuchu ya mafaniko ya timu ya taifa ya Uingereza miaka ya 80 mwishoni na ya 90,kwa umaili wake wakujua kulisakata kabumbu na kutoa mapande mazuri kwa washambuliji wake wa timu taifa ta Uingereza.
Pichani hapo juu anaonekana Gazza akisoma kikaratsi jinsi gani ya kuwakumbusha vijana wa timu yake la kufanya ili kutorudia makosa wakati alaipo kuwa kocha wa timu Kattering Town.
Picha ya pili anaonekana Gaza katika hali tofauti, siku za mwisho kabla ya kutundika daruga za kabumbu.
Picha ya tatu anaonekana Gazza, alipo kuwa kazini hakuwa na mchezo, mis the ball, get the man, enzi hizo sheria za mpira zilikuwa zinaruhusu kukandamizana uwanjani.
Picha ya nne na ya tano anaonekana Gazza, akili kwa uchungu baada ya timu yake ya taifa kukuso kuendela na mashindano kwa kutolewa na wapinzani wao wakuu Ujerumani wakati wa mashindano ya mataifa ya Ulaya yaliyo fanyaika Uingereza.
Mungu ni chanzo cha mafanikio yangu,Kaka atoa sadaka kombe lake la dhahabu.
Sao Poulo, Brazil - Mchezaji bora wa dunia kwa upande wa soka, Kaka kombe lake la dhahabu kama mchango kwa kanisa ambalo ni muumini wa kanisa hilo.
Kaka amabye ni amabye ni mmoja ya wachezaji walokole, (born again) alisema ya kuwa nalileta kombe hili hapa mbele ya Mungu, kwani mafanikio yangu yote yamekuwa ni baraka za kutoka kwa Mungu kwa kupitia mwana ye mpendwa Yesu Kristu.
Na kombe hili litakaa hapa Kanisani, alimalizia kwa kusema haya mbela ya waumini wasio pungua 5000.
Hivi karibuni Kaka alishinda kwa kuwa kijana, ambaye ameamua yakuto kuwa na msichana mpaka hapo atakapo oa.
Kaka, ambaye jina lake kamili ni Ricardo Izecson dos Santos Leite, amesema ukifika wakati wa kuacha kucheza mpira atapendelea kuwa mchungaji, ili kumtumikia Mungu.
Uturuki yadai ya kuwa Iraq imeshindwa,basi Uturuki itaendelea mpaka wamalize kazi yao.
Ankara, Uturuki - Helikopta moja ya jeshi la Uturuki, ililipuliwa hivi karibuni na kikosi cha askari na kuleta maafa bmakubwa kwa upande wa jeshi la Uturuki.
Mmoja wa wasemaji wa PKK, alisema ya kuwa waliitungua helikopta hiyo muda wa saa za magharibi karibu na mji kimoja uitwacho Chamsku.
Kuthibitisha habari hizi msemaji wa jeshi la Uturuki, alisema ya kuwa kuna helikopta moja ilianguka na hakuna maelezo zaidi yaliyotolewa na msemaji huyo.
Wakati huo huo , serikali ya Iraq imeitaka serikali ya Uturuki, kuyatoa majeshi yake nchini Iraq na karibu namipaka yake kwani mapambano hayo yanahatarisha usalama wa Iraki.
Hata hivyo serikali ya Uturuku ,inadai ya kuwa imeamua kufanya hivyo baada ya serikali ya Iraq kushindwa kuwazuia wapiganaji wa PKK, kshambulia nchini Uturuki.
Picha ya juu anaonaekana, mmoja wa askari wa Kituruki akiwa kataika uwajna wa mapambano.
Na chini pi picha ya inaonyesha baadhi ya wanajeshi waliiopoteaz maisha kwa kupigania nchi yao wakirejeshwa nyumbani.
Angola yaongoza kwa vifo vya watoto wadogo katika nchi za duina ya tatu.
Luanda, Angola - Nchi ya Angola imekuwa moja ya nchi ambayo inaongoza kwa vifo vya watoto wadogo kulinganisha na nchi nyingine zilizopo kusini mwa jangwa la sahara.
Maelezo haya yaliotolewa na shirika moja la kutoa misaada nchini Uingereza.
Angola ambayo inautajiri wa asili kama mafuta na almasi, lakini wananchi walio wengi wanaishi maisha ya hali ya chini kulinganiasha na uchumi uliopo, ilimalizia ripoti hii ya shirika hili.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Angola akiutubia Umoja wa mataifa siku za karibuni alipo hudhulia mkutano wa viongozi wa umoja huo.
Picha ya katikati wanaonekana watoto wa kiangola ambao wanakabiriwa na magonjwa yanayo weza kutibiwa au kuzuiwa ya siwadhulu ikiwa watapewa kinga.
Chini anaonekana mtoto akipewa dawa ya kinga na mmoja ya wahudumu wa dhahanati nchini Angola.
Serikali ya Eritrea ya iwekea ngumu UN kusambaza misaada kiuraisi
UN - Umoja wa mataifa umeilaumu serikali ya Eritrea, kwa kitendo chake cha kuzuia misada kuingizwa nchini Ethiopia kwa kupitia nchini Eritrea.]
Akiongea hay msemaji mmoja wa UN bi Marie Okebe, alisema ya kuwa imekuwa ni vugumu kuingia nchini Ethiopia, kwani serikali ya Eritrea imakuwa ikiwapa wakati mgumu,na baadhi ya wafanyakazi wa Umoja wa mataifa kutishiwa nanguvu za dola na mitutu.
Hata hivyo uhusiano kati ya serikali ya Ethiopia na Eritrea umekuwa wa mashaka kwa kipindi kilefu sasa, hivyo ni vigumu hali kuwa nyepesi , alisema msemaji mmoja wa serikali ya Eritrea.
Pichani anaonekana rais Isaias Afewerki wa Eritrea, akiongea na wahandidhi wa habari siku za karibuni.
Picha chini wanaonekana askari wa Eritrea wakifungua kizuizi tayari kulikagua gari UN lililo beba misaada.
Amani kupatikana nchini Uganda?Mkataba wa Amani utafikiwa tu msemaji wa serikali.
Kampala, Uganda - Serikali ya Uganda na kikoso cha jeshi la upinzani kinacho ongozwa na bwana Joseph Kony,wametiliana sahii ya makubaliano kusimamisha mapigano na kuelekea njia ya kuleta amani nchini Uganda.
Vita hivi kati ya serikali na wapinzani wanaoongozwa na bwana Joseph Kony , vimechukua karibu ya robo karne, vimekuwa vikileta maafa makubwa kwa wananchi wa kaskazini mwa Uganda.
Hata hivyo mmoja wa wasemaji wa serikali alisema ya kuwa mkataba huu ni njia na ishara nzuri ya kuwa amani itapatikana tu.
Picha hapo juu anaoneka rais Yoweri Mseveni , akiwa amepumzika baada ya kazi ngumu za kiofisi.
Picha ya katikati anaonekana rais Yoweri Kaguta Museveni, akihutubia wapiganaji wake enzi hizo alipo kuwa bado yumo ndani ya magwanda ya kijeshi.
Chini ni picha ya bwana Joseph Kony akiongea na waandishi wa habari hapo siku za nyuma.
Amerika na washiriki wake watakiwa watuombe radhi,serikali ya Irani yaagiza.
Teheran, Iran - Rais wa Iran bwana Mahmoud Ahamadinejad, ameitaka serikali ya Amerika na washiriki wake, kuomba msamahaa kwa wananchi wa Iran, kwa kuishutumu serikali ya Iran yakuwa inampango wa kutengeneza mabomu ya nuklia.
Rais Mahmoud Ahamadinejad, aliyasema haya sikuya jumamos ,baada ya ripoti ya shirika linalo shughulikia nguvu za nyuklia (IAEA) kueleza ya kuwa Iran,imekuwa ikionyesha ni jinsi gani nchi hii inavyo fatilia umakini wa kutengeneza umeme unaotokana na nguvu za nyuklia na siyo kutengeneza siraha za nuklia.
Hata hivyo Amerika na washiriki wake bado, wanasisitiza ya kuwa serikali ya Iran lazima iwekewe vikwazo na mbinyo ili kuacha kuendelea na mpango wake wa kuendeleza nguvu za kinuklia.
Picha hapo juu ni rais wa Iran bwana Mahmoud Amadinejad, akiongea hivi karibuni kusissitizia msimamo wa serikali ya Iran kuhusu uhalari wake.
Picha ya katikati anaonekana rais Mahmoud Ahamadinejad,wakati waenzi zile za kuongoza mapinduzi ya Iran, anavyo onekana kwa sasa.
Chini ni sehemu ya mitambo ya kutengeneza nguvu za nuklia,na anaonekana mmoja ya wafanya kazi wa idara fulani akiwa anaangalia kwa makini jinsi gani uzalishaji unavyo kwenda.

Sunday, February 17, 2008

Hatimaye serikali yaomba msamaha

Dhahabu ya muziki wa pop,waadhimisha miaka 25 ya albumu iliyo vunja rekodi ya mauzo.

New York, Amerika - Kinara na nyota wa muziki wa pop na kuruka majoka, Michael Jackson ameadhimisha miaka 25 ya muziki uliotikisa dunia ujulikanao kama Thriller's.
Mwanamuziki huyu,ambaye albamu yake ya Thriller's ilimwingizia faranga(pesa) nyingi na kuvunja rekodi ya mauzo.
Akiongea na kuwashukuru wapenzi wake, kwakutumia mtandao, Michael Jackson, alisema ya kua ni vigumu kuamini ya kuwa tangu siku ile yeye pamoja na msanii na mtunzi bwana Quincy Jones walikaa na kutua albamu ijulikanayo kama Thriller's, na hivi sasa inatimiza miaka 25.
Albamu ya Thriller's, ilitolewa November 1982.
Michael Jackson, amehaidi ya kuwa wapenzi wasife moyo kwani hivi karibuni atatoa muziki, kwa kushirikiana na Kanye West, Akon. Fergie .
Pichani hapo juu anaonekana, Michael Jackson,akiwa amepozi mbele ya jalada la albamu ya Thriller's.
Picha ya pili zinaonekana picha za Michael Jackson, ya kwanza kushoto ni enzi zake baada ya kutoa albamu ya Thrillr's na picha ya upande wa kulia anaonekana Michael Jackson wa sasa.
Picha ya mwisho anaonekana mfalme wa muziki wa pop akiwatumbwiza washabiki wake, miaka ya hivi karibuni.
Baba wa taifa la Kuba, atangaza kujiuzulu uongozi"Ameongoza nchi nusu karne"
Havana, Kuba - Rais wa Kuba bwana Fidel Castro, ametangaza rasmi kuwa hatagombania tena urais wa Kuba, kutokana na afya yake.
Rais Castro ambaye ametawala Kuba kwa muda wa nusu karne, amesema yakuwa hataweza tena kuwa kiongozi wa Kuba kwa kuzingatia umri wake na afya yake kwa ujumla.
Rais Fidel Castro, ambaye amefanyiwa upasuaji wa tumbo, amekuwa hajishuhurishi na kazi za kiserikali tangu afanyiwe upasuaji huu, na alimwachia kiti mdogo wake bwana Raul Castro.
Rais Fidel Castro, ambaye amekoswa ku uwawa mara nyingi, na majasusi wa kila aina zaidi ya mara miasita, kutokana na maelezo ya habari za usalama wa taifa wa Kuba.
Picha hapo juu, wanaoneka Fidel Castro na Che Guevara wakati wa harakati wa kuikomboa Kuba kutoka kwenye utawala wa kizalimu na rushwa wa rais Batista.
Viongozi wa Kuba, ambao wametawala zaidi ya nusu karne, ambao ni ndugu,rais Fidel Castro na mdogo wake Raul Castro.
Hapo anaonekana rais Fidel Castro akihurubia mamia ya wa Kuba enzi hizo kabla ya kufanyiwa upasuaji.
Picha ya mwisho anaonekana rais Fidel Castro, akishangilia kwa kutumia bendera ya Kuba.
Matunda ya uongozi bora, yaaanza kuonekana,Tanzania yapata kitita kutoka kwa US.
Dar es Salam, Tanzania - Serikali ya Amerika imeipatia serikali ya Tanzania kiasi cha 700 million dola, baada ya kumaliza kutiliana mkataba.
Pesa hizo ambazo zitapatikana katika kipindi cha miaka mitano ni moja ya jitihada za serikali ya Amerika, kusaidia bara la Afrika kupambana na umasikini, magonjwa na kuinua uchumi.
Pesa hizi zimetolewa kwa serikali ya Tanzania, wakati rais George Bush alipo tembelea Tanzania hivi karibuni wakati wa kutembelea baadhi ya mataifa ya Afrika.
Pichani hapo juu wanaonekana rais George Bush akipena mkono na rais wa Tanzania, bwana Jakaya Kikwete baada ya kumaliza kutiliana mkataba kati ya serikali hizi mbili.
Picha chini wanaonekana wakina mama, wakicheza ngoma huku wakiwa wamevalia kanga zenye picha ya rais George Bush.
Ndoto ya kumtumbwiza mwanahaki za binadamu ni za kila mtu.
Pretoria, Afrika ya Kusini - Kundi la musiki lijulikanalo kama Spice Girls, wamesema wangependelea kumtubwiza shujaa na mpigania haki za binadamu, mwanamapinduzi, na kiongozi aliyeongoza kupinga ubaguzi wa rangi nchini Afrika ya Kusini, rais wa zamani wa Afrika ya Kusini bwana Nelson Mandela.
Pendekezo hilo lilitolewa na wanamuziki hawa yakuwa itakuwa kama ndoto kwao ya kuwa kutwimbiza siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa bwana Nelson Mandela, atakapo adhimisha miaka 90 ya kuzaliwa siku ya tarehe, 27/ june, mjini London kwenye uwanja wa Hyde Park.
Picha hapo juu anaonekana babu, Mandela akiwa amekula pozi baada ya kazi ngumu wakati wa urais wake.
Chini ni picha ya kundi Spice Girls ambao wanaota usiku na mchana kumtumbwiza baba, babu Nelson Mandela.
Tunaomba msamahaa, hatimayake serikali ya Australia yakubali ya kuwa ilifanya mabaya kwa wazawa.
Sidney,Australia - Serikali ya Australia imeomba msamahaa kwa mara ya kwanza kwa Wakazi wa Asili wa Bara la Australia.
Wakazi hao ambao wanajulikana kama Aboligini, waliobwa msamaha huu na waziri mkuu mpya wa Australia bwana Kevi Rudd.
Waziri mkuu,bwana Kevin Rudd, kwa kuonyesha masikitiko na hudhuni,kwa kitendo hicho, alisema tunaomba msamahaa na tunakili ya kuwa tulikosa.
Waaboligini hawa, waliombwa msamaha huu, baada ya serikali ya Australia kukubali na kuelewa baadhi maafa ambayo waliyaleta tangu wazungu wa kwanza walipo ingia katika bara hili la Australia.
Moja ya maafa yale yaliyo sababishwa na Australia, ni wakati serikali ya Australia, ilipo wateka nyara na kuwachukua kwa nguvu baadhi ya watoto wa jamii ya Akiabolijini na kuwa ingiza katika jamii ya Wazungu.
Kwa kitendo hicho cha serikali ya Australia, kutambua na kukubali maafa ambayo waliyatenda, kimepokelwa kwa furaha na wananchi wa jamii ya Aboligini kwa hisia tofauti.
Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Australia, bwana Kevin Rudd, alipo kuwa bungeni hivi karibuni kuomba msamahaa kwa wana nchi wa jamii ya Aboligini.
Picha ya kati anaonekana mmoja ya wananchi wa jamii ya abolijini, akitambika kukubali msamahaa kuktoka kwa serikali.
Chini ni picha ya baadhi ya wananchi wa jamii ya Aboligini, wakiwa wamefungwa minyororo kwenye shingo tayari kuelekea sehemu ambayo hawaijui kutumikia kifungo.
Urusi ya toa onyo"Siraha za kulinda Urusi zitaelekezwa nchi Ukraini.
Moscow, Urusi -Rais wa Vladamil Putin wa Urusi, amesemaya kuwa upo uwezekano wa nchi yake kuelekeza mitambo na siraha za nyuklia nchini Ukraini,ikiwa Ukraini itajiunga NATO, (Jumuia ya ushirikiano wa kiulinzi ,kijeshi na usalama wa Ulaya ya Mgharibi na Amerika).
Akiongea haya baada ya kumaliza kuongea na kutiliana mkataba wa kujenga mitambo ya mafuta na gas hivi karibuni, na rais wa Ukraini bwana, Yushchenko.
Akiongezea alisisitizia ya kuwa Urusi, Ukraini, Amerika na Ulaya Magharibi zinawajibika kwa ujumla kuangalia usalama na ulinzi.
Putin amabye anamaliza muda wake wa kumaliza wa kuwa rais wa Urusi mwezi wa Mei,amezilaumu NATO na Amerika kuwa zinaleta utata wa usalama na amani kwa upande wa Urusi.
Wakati huu rais Vladamil Putin, amealikwa kwenye mkutano wa jumuia ya NATO, utakao fanyika mwezi wa nne .Kwa mara ya mwisho rais Putin, aliuzuria mkutano huu mwaka 2002. Pichani anaonekana rais wa Ukraini bwana, Viktor Yushchenko na rais Putini walipo kutana hivi karibuni.

Monday, February 11, 2008

Rais avamiwa Ikulu, waasi wa Mashariki wa Timor wataka kuleta machafuko.

Kosa la kaptain wetu, humtokea kila mchezaji, kwani mpira unazunguka"Wachezaji wa Kamerooni"

Younde, Kameroon - Wachezaji watimu ya taifa ya Kameroon, wamesema yakuwa kushindwa kwao kubeba kombe la maifa ya Afrika nchini Ghana, sikwasababu ya kosa la kaptain wao Rigobert Song,bali haikuwa siku yao ya kushinda kombe hilo.
Wakiongea kwa wakati tofauti, wachezaji wa timu ya taifa ya Kameroon, walisema kosa ambalo amefanya Song , humtokea mchezaji yoyote, na kwa wale wanao jua au wamesha wahi kucheza mpira wanajua yakuwa mpira huwa wakati mwingine unafanya mchezaji asifanye alivyo tarajiwa na mpira unazunguka, hivyo ulimzunguka kaptaini wao mara moja na hapo mchezaji wa Misri timu ya taifa ya Misri Zidan, akaupata mpira na kumpasia Boutrika aliyefunga goli lililo wapa ushindi Wamisri.
Hivyo sisi wachezaji wote tupo pamoja nae, bado tutazidi kuichezea Kamerooon mpaka hapo miguu ikikataa, aliongea haya Geremi Ndjitap, huku akipewa sapoti na Samuel Eto'o.Kwani tuna kombe la Afrika nchini Angola ,na badye kombe la dunia nchini Afrika ya Kusini, hivyo kwa sasa tutaanza panga mikakati ya kuweza kucheza vizuri ili tuweze kushindana kwenye mashindano haya ya 2010 nchini Angola na Afrika ya kusini.
Picha hapo juu anaonekana kaptain wa timu ya taifa ya Kamerooni Rigobert Song, akiwa ndani ya jezi ya timu yake ya taifa ya Kameroon, na huku mguu wake wa kushoto ukiwa umefungwa bandaji,hivyo maumivu ya mwili wake yapo ndani ya mapenzi ya nchi yake.
Picha ya pili anaonekana Rigobert Song, akiwa kazini kutetea nchi yake siku ya mwisho ya mishindano ya kombe la Afrika,wakati Kamerooni ilipo cheza na Misri na kufungwa goli moja kwa nungu.
Picha ya chini ni picha ambayo wapenzi wasoka wa Kamerooni hawataisahau, kwani anaonekana kaptain wa timu ya taifa ya Kamerooni Rigobert Song,akigombea mpira na Mohammed Zidan, baada ya mpira kumzunguka Song, na hatimayake Zidan, aliupata mpira na kutoa pasi mwanana kwa Boutrika aliye wanyima ushindi wa kombe la Afrika Wakamerooni kwa kufunga bao la pekee.
Eddy Murphy King of Zamunda, aowa nakuacha kwa kipindi kifupi.
Los Angeles, USA - Mcheza sinema na mwana vitimbwi, Eddy Murphy, ameachana na mkewe ,bi Tracey Edmond, baada ya kufunga ndoa kwa kipindi cha wiki mbili.
Eddy Murphy mwenye umri wa miaka 46 na bi Tracey Edmond mwenye miaka 40, walifunga ndoa kwenye kisiwa cha Bora Bora.
Eddy Murphy mwenye watoto sita, kutoka kwa ndoa ya zamani, amecheza sinema nyingi, na moja ya sinema ambazo zimempa umaharufu ni ile ijulikanayo Coming to America.
Picha juu anaonekana bwana Eddy Murphy akiwa kazini kataika harakati za kucheza sinema, amabzo huwa kivutio kwa wapenzi wa sinema.
Picha ya pili anaonekana bwana Eddy Murphy, akiwa amekula kodo,mbela ya wapenzi wake baaday ya kumaliza kufanya mavitu yakeya sinema.
Picha ya mwisho anaonekana Eddy Murphy, akiwa na aliyekuwa mkewe, bi Tracey Edmond siku zakaribuni kabla ya kufunga ndoa yao iliyodumu wiki mbili tu.
Misri yawa bingwa wa kombe la Afrika,Kamerooni yakosa kombe kwa kosa la beki.
Accra, Ghana - Timu ya taifa ya Misri imeibuka na ubingwa kwa mara ya sita, baada ya kuzaba bao moja kwa nunge timu ya taifa ya Kamerooni.
Bao hilo la ushindi lilifunngwa na mshambuliaji hatari Mohammed Aboutrika, baada ya kupata pasi kutoka kwa Zidan, ambaye aliweza kufaidika kutokana na makosa ya beki mzoefu wa Kamerooni rigobert Song.
Ushindi huu wa the FARAOS, unakuja kwa kujumisha wachezaji wanao cheza ligi ya Misri,na wachezaji wawili wanao cheza nje ya ligi ya Misri ndiyo walioitwa kujiunga na timu hiyo ya taifa.Hii ni mara ya pili kwa the Farao, kuwafunga Simba wa Kamerooni, kwani katika mzunguko wa kwanza wakati wakigombania kuingia awamu ya pili Misri iliifunga Kamerooni goli 4-2.
Pichani anaonekana timu kamptain wa Misri, Ahamed Hassan akinyanyua kombe la ubingwa la mataifa ya Afrika. Misri imeshinda kome hili kwa mara ya sita.
Picha ya chini anaonekana Mohammed Zidan, akishangilia huku amebebwa na mchezaji mwenzake baaday ya kumzidi maarifa beki wa Kamerooni, Rigobert Song na kumpasia Mohammed Aboutrika, ambaye bila makosa alifanya vitu vyake kwa kuona nyavu za mlinda mlango wa Kamerooni Idriss Kameni, nakuwa bao la ushindi.
Chini ni picha ya wachezaji wa Misri wakishangilia baada ya kukabidhiwa Kombe lao.
Mgombea mwenza wa ZANU-PF afutwa uanachama"Huyu ni kibaraka ZANU -PF ya dai"
Harare, Zimbabwe - Chama tawala cha ZANU - PF, kimemfukuza uanachama bwana, Simba Makoni, baada ya kuamua kugombania kiti cha urais kama mgombea wa kujitegemea.
Bwana Makoni. alitangaza hivi karibuni ya kuwa atagombania kiti cha urais wakati wa uchaguzi wa rais mapema mwishoni mwa mwezi wa tatu, na bwana Makoni alishwa wahi kuwa waziri wa faranga wa Zimbabwe, lakini alitolewa kwenye wizara hiyo .
Akiongea na waandishi wa habari,makamu wa chama tawala ZANU-PF, bwana, Joseph Chinotimba, aliseama ya kuwa bwana Makoni,amekuwa kibaraka wa serikali za magharibi, Amerika na Uingereza, nakuwa hataweza kuigawa ZANU-PF,hivyo atashindwa na kuumbuka, baada ya uchaguzi, hivyo nasikitika sana, kwani alikuwa mmoja wa wapiganaji wenzetu wakati wa kumpiga mkoloni, lakini sasa kawa kibaraka wao.
Pichani anaonekana bwana Simba Makoni,enzi zake akiwa kama waziri wa faranga wa Zimbabwe akielekea bungeni kutoa miswada.
Hapo chini ni picha ya bwana Simba Makoni,akiongea na waandishi wa habari baada ya kutangaza kugombea urais kama mgombea wa kujitegemea.
Mahaka ya Hague yapata mshitakiwa mwingine,ashutumiwa na mauaji ya Ituri.
Hague, Holland - Aliyekuwa kiongozi wa jeshi la waasi lijulikanalo kama(DRC)Democratic Republican of Congo bwana Mathieu Ngdjolo amekamatwa na mjini Kinshasa na kuletwa nchini Holland, kujibu mashitaka ya mauaji ya mamia ya watu.Alisema wakili mmoja wa mahakama ya mjini Hague, ICC (International Criminal Court), bwana Luis Moreno Ocampo.
Bwana, Mathieu Ngdjolo anashitakiwa kwa kutoa amri ya kutekateza zaidi ya wana vijiji wapatao 200 mwaka 2003 wakatia aliipo kuwa mkuu wa usalama wa taifa.
Tuhuma hizo ambazo zinamkabili ni mauaji yaliyo tokea maeneo ya Ituri na kijiji cha Bogoro.
Kutokana na watetezi wa haki zabinadamu na kuhudumia watu waliopata matatizo, wanadai zaidi ya watu wapatao 600,000 wamakimbia makazi yao tangu machafuko ya Ituri yaanze mapema kwenye mwaka ya 1999. Pichani kulia ni picha ya bwana Mathieu Ngdjolo,alipo kuwa kazini enzi zake kama afisa usalama wa taifa, miaka ya 2003.
Waasi wadai wageni wasaidia serikali, wasiwasi waongezeka "roho zipo nyengema"
Ndjamena, Chad - Wakimbizi amabo walikimbilia nchni Kameroni, wakati wa majaribu ya kiipindua serikali ya rais Idriss Deby, wamaeanza kurudishwa nyumbani kwao.
Hii ionakuja baada ya wapinzani wa serikali kushindwa kumuondoa madarakani rais Idriss Deby.
Kutokana wa msemaji mmoja wa kuhudunia watu waliokumbwa na maafa, alisema yakuwa, hali bado ya mashaka mjini Ndjamena, ijapokuwa watu wamekuwa wakiambiwa ya kuwa waasi hawatarudi tena kushambulia jiji la Ndjamena.
Japokuwa kunahabari ya kuwa waasi hawa wanajijenga tayari kwa mashambulizi mengine, na wamedai yakuwa wanashikiria miji ya n Momgo na Bitkine iliyopo katikati ya nchi ya Chad.
Hata hivyo waasi wa serikali wamezidi ilaumu serikali ya Ufaransa kwa kuisidia serikali ya rais Idriss Deby.
Pichani wanaonekana wanajeshi wa serikali wakila doria mjini Ndjamena, baada ya kuyarudisha majeshi ya waasi nyuma ya jiji na vitongoji vyake.
Chini wanaonekana wanajeshi wa Ufaransa wakiwa wanalinda maeneo muhimu ya kusaidi huduma za binadamu jijini Ndjamena.
Chni nim picha ya kina mama wakiwa wamekaa bila kujua ni nini kinafuata kataiaka kambi moja ya wakimbizi.
Mtuhumiwa wa septemba 11/2001, afunguliwa mashitaka, akabiliwa na kinyongo.
Washington,USA - Serikali ya Amerika imetangaza na kumfungulia mashitaka, aliye kuwa kiongozi wa ugaidi wa sempemba 11/2001 bwana Khalid Sheikh Mohammed.
Akiongea haya Brigedia,General Thomas Hartmann, alisema ya kuwa bwana, Khalid Sheikh Mohammed, anatuhumiwa kwa kuhusika kutumia ujuzi wa hali juu, kwa kusaidiana wa magaidi wengine wa Alqaeda walitumia ndege kashambulia ,kulipua na kuharibu majengo yajulikanayo kama World Trade Centle mjini New York na majengo mengini njini Washington, ambapo zidi ya
watu wapatao 3000 walipoteza maisha yao.
Hata hivyo inasadikiwa bwana Khalid Sheikh Mohammed, alikiri makosa baada ya kuteswa kwa kutumia mbinu ijulikanayo kama " Water Boarding" ambayo watetezi wa haki za binadamu wanasema ni kinyume na sheria za haki za binadamu na sheria za nchi.
Inaamini ka ikiwa bwana Khalid Sheikh Mohammed akikutwa na hatia, anaweza kuhukumiwa kifo Hapo juu ni njia tofauti au mojawapo ambayo watetezi wa haki za binadamu wanadai yakuwa ni kunyume cha haki zabinadamu kutumia njia hii kupata ushahidi au ukweli kutoka kwa mtuhumiwa. Picha ya chini ni picha ya Khalid Sheikh Mohammed, ambaye anashutumiwa kwa kuhusika na uigaidi na mauaji ya semptemba 2001
Rais avamiwa Ikulu ,Waasi wa Mashariki wa Timor wataka kuleta machafuko.
Dili, Mashariki ya Timor - Rais wa Mashariki ya Tomor, bwana Jose Ramos Horta, amenusurika kuuwawa na risasi, baada ya waasi wa Mashariki ya Tomor kuvamia nyumbani kwakwe siku ya jumatatu 11/02/08 na kumpiga risasi za tumbo.
Mapambano hayo yaliongozwa na mmoja wa wanajeshi waasi wa Mashariki ya Timor, bwana Afredo Reinado ambaye waliuwawa wakati wa kutupiana risasi na walinzi wa rais.
Rais Jose Ramos Horta, alikimbizwa hospitali ya jeshi iliyopo mjini Dili, nabaadaye kupelekwa Australia kwa matibabu zaidi.
Picha juu ni kiongozi wa waasi wa Mashariki ya Timor, bwana Afredo Reinado, ambaye aliyeongoza kujaribu kuleta mapinduzi ya kijeshi.
Picha ya pili anaonekana rais Jose Horta, akiwa katika hali mbaya kukimbiziwa hospitali kwa matibabu.
Hapo juu ni picha ya rais Jose Ramos Horta, akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.